Thursday, September 19, 2013

Shekhe Zaheed Ampokea Yesu Kristo




Zaheed alizaliwa kwenye familia ya Kiislamu. Baba yake na kaka zake wote walikuwa viongozi wa dini ya Kiislamu. Zaheed naye alifuata mkondo uleule.


Mara baada ya kuhitimu masomo ya dini na kukabidhiwa msikiti, chuki yake na kutokuwa na uvumilivu dhidi ya Wakristo kulianza kujionyesha waziwazi.


Zaheed anasema, “Nilikuwa nawakusanya vijana kwenye msikiti wangu na kuwachochea dhidi ya Wakristo. Niliwaambia kuwa Wakristo ni makafiri. Niliwaambia waende wakawapige Wakristo kwa fimbo na kwa nondo. Niliwaambia kuwa Allah anafurahi wakifanya hivyo. Tulikuwa tukichoma moto Biblia tunazozikusanya.”



Zaheed anaendelea kusema, “Lakini siku moja, nilijisikia tu nichukue Biblia moja niende nayo nyumbani. Nilikuwa naisoma ili niweze kutafuta mambo yanayotatanisha ili niweze kuyatumia dhidi ya imani ya Kikristo. Ghafla, nuru kubwa iliangaza kwenye chumba changu. Halafu nikasikia sauti ikiita jina langu. Nuru ile ilikuwa kali sana. Iliangaza chumba kizima. Ile sauti ikauliza, ‘Zaheed, kwa nini unanitesa?’ Niliogopa. Sikujua cha kufanya. Nilidhani ninaota. Kwa hiyo nikauliza, ‘Wewe ni nani?’ Kisha nikasikia, ‘Mimi ni njia, na kweli, na uzima.’”

Juhudi za Kupinga Ukristo za Mwanaharakati wa Kundi la Ahmadiah Kutoka Pakistani Zamfanya Aachane na Uislamu



Nusrat Aman alikuwa ni mwanaharakati wa kiislamu wa kundi la Ahmadiah kule Pakistani. Siku moja aliamua kuingia kanisani ili akamwulize mchungaji ni kwa nini hasa hataki kuwa mwislamu ilhali unabii wote umeshatimizwa ndani ya Muhammad? Nusrat aliishia kupata aibu, hasira na hatimaye wokovu …!


Je, ilikuwaje? Endelea kusoma ushuhuda wake wenye kichwa kisemacho "Kwa nini niliamua kuwa Mkristo?" ambao unafungua macho na mioyo kwa kuwa ni watu wengi walio katika kundi alimokuwa Nasrat hapo zamani.


*****************

Kwa nini niliamua kuwa Mkristo?

Na Nusrat Aman
Nilizaliwa katika familia halisi wa Kiislamu nchini Pakistani mwaka 1958. Nilisoma katika shule ya kimishenari ya Kiislamu na chuo kilichosimamiwa na Ahmadiah Movement in Islam, Pakistani. Wakati wa masomo yangu katika shule ya kimisionari na chuo cha Kiislamu vyenye mwamko mkubwa sana kuhusu Uislamu, nilijenga shauku kubwa ya kujifunza dini ya Kiislamu. Kwa hiyo, nilijiunga na Ahmadiah Movement, kundi ambalo lilitangazwa na Serikali ya Pakistani mwaka 1974 kuwa ni dini ya kizushi isiyo Kiislamu.

Mimi nilikuja kujua neno, "Kristo au Masihi" kwa mara ya kwanza katika maandiko ya Ahmadiah Movement yanayopinga Ukristo. Mwasisi wa harakati za Ahmadiah, Mirza Ghulam Ahmad alidai kuwa yeye ndiye "Masih Maud" (yaani Masihi aliyeahidiwa). Mimi nilikuwa na furaha sana na shauku ya kuhubiri mafundisho ya Ahmadiah Movement ambayo yalikuwa ni mapya na ya kuvutia sana kwangu. Nilikuwa nakumbuka aya zote kwenye Biblia zinazoongelea kuhusu ujio wa pili wa Kristo katika Biblia na Quran lakini bila kuwa na ufahamu wa kina kuhusiana na aya hizo.

Kosa nililofanya, likaniokoa

Ndoto Yamfanya Al-Haji Mohammed Ampokee Yesu



Al-Haji Mohammed Ahmed alikulia kwenye familia ya Kiislamu. Anaitwa al-Haji kwa sababu alishaenda Makka kuhiji.


Mohammed anasema:”Maishani mwangu mwote nilikuwa Mwislamu thabiti sana. Katika familia yangu, lengo letu kuu lilikuwa kujenga misikiti na kueneza Uislamu kila mahali.” 


Akiwa kiongozi kwenye msikiti, Mohammed alihamasiaha vikundi vya waumini vilivyoenda mitaani kusaka Wakristo waliokuwa wakienda kanisani. Kisha waliwapiga na kuchoma moto Biblia. Mohammed hata alimshambulia Mkristo mmoja kwa kisu. Hayo ndiyo yalikuwa maisha ya Mohammed.


Kisha usiku mmoja aliota ndoto ya ajabu. Mohammed anasema, “Wakati nikiwa nimelala, ilikuja sauti ya namna fulani kutoka mbinguni. Ikasema, ‘Mohammed, Mohammed, toka humo na unifuate.’”

Kwa Nini Niliacha Uislamu na Kumpokea Yesu?




Mutee'a Al-Fadi alikuwa ni Mwislamu mwenye msimamo mkali wa Wahabbi ambao alisomea kule Saudi Arabia. Lakini baada ya kukutana na upendo wa Yesu, moyo wake uligeuka kabisa na akaanza kuitafuta kweli iliko. Hatimaye alitambua kuwa Yesu ndiye Njia, Kweli na Uzima. Ufuatao ndio ushuhuda wake:



****************

Mimi nilikuwa Muislamu wa Wahabbi ambaye nilizaliwa na kulelewa kama Mwislamu nchini Saudi Arabia. Katika maisha yangu yote nilikuwa mfuasi mwaminifu wa Kiislamu ambaye nilifuata na kuishi mafundisho ya Uislamu katika kila eneo la maisha yangu. Mafundisho haya yalikuwa ni pamoja na imani:

  • kwamba Uislamu ndio dini ya mwisho duniani; 
  • kwamba ndiyo dini pekee inayokubalika kwa Mungu; 
  • kwamba ndiyo njia ya kwenda Mbinguni; 
  • kwamba wale wasioukubali Uislamu wanakwenda jehanamu na kwamba matendo na ibada zao hazitawaokoa hadi watakapomkubali Allah kama Mungu wao na Muhammad kama mtume wake; 
  •  kwamba wokovu kwa Mwislamu ni kwa njia ya matendo mema na hauna uhakika isipokuwa kwa wale walio tayari kufa kwa jina la Allah; 
  • kwamba Waislamu ni watu bora kuliko wengine; 
  • kwamba watu wote wasio Waislamu ni makafiri, ikiwa ni pamoja na Wakristo; 
  • kwamba Kristo alikuwa ni mwanadamu tu na nabii aliyetumwa na Allah; 
  • kwamba yeye si Mungu au Mwana wa Mungu; 
  • kwamba hakuwahi kusulubiwa, kufa msalabani au kufufuka kutoka kwa wafu; 
  • kwamba Yesu alipaishwa Mbinguni ili kuokolewa dhidi ya waliotaka kumuua na 
  • kwamba Yesu atakuja tena siku za mwisho ili kuujenga upya Uislamu kama dini ya kweli ya Allah, kuharibu msalaba, kumuua mpinga-Kristo, na kuwafanya Wakristo wawe Waislamu.

Lakini jambo lenye nguvu zaidi ambalo nilijifunza katika makuzi yangu ni kuwa na CHUKI dhidi ya wale wote wasiomwabudu Allah; wasiomfuata Muhammad; wasioamini Uislamu – ikiwa ni pamoja na Wakristo na Wayahudi. Kwa lugha rahisi ni kwamba, nilikuwa adui wa Kristo.

Katika umri wa miaka 12, nilikuwa nimeshakariri nusu ya Qur’an. Lengo langu lilikuwa kukariri kitabu chote; maana huwa tunafundishwa kwamba kukariri Qur’an kunasaidia kufunika baadhi ya dhambi zako na kuboresha matendo yako mema Siku ya Hukumu; pia kunakupandisha daraja mbinguni.

Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia? - Sehemu ya I



 Marehemu Ahmed Deedat

Waislamu wanashikilia kwamba Muhammad alitabiriwa kwenye Biblia. Andiko lao kuu wanalotumia kutetea hoja hii ni Kumbukumbu la Torati 18:18. Andiko hilo linasema:

Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


Haya ni maneno ambayo aliambiwa Musa na Yehova.


Mmojawapo wa watu ambao walijaribu sana kuonyesha kuwa andiko hili lilimhusu Muhammad, alikuwa ni mwanaharakati wa Kiislamu, marehemu Ahmed Deedat wa Afrika Kusini.



Unaposoma au kusikiliza sababu wanazotoa ili kuthibitisha madai yao hayo, kwa kweli ni sababu zenye nguvu sana (kwa mtu ambaye haelewi Biblia); ingawaje hazina uzito hata chembe ukijua Biblia inasema nini katika ujumla wake na ni nini makusudi na malengo ya Mungu kwa uzao mzima wa Adamu.


Siku moja Ahmed Deedat alimkaba mchungaji mmoja kwa maswali kuhusu mstari huu wa Kumbukumbu 18:18 kiasi kwamba, kwa maneno yake, Deedat anasema kuwa mchungaji yule alikosa cha kusema.

Deedat alimpomsomea mstari huo, alimwuliza, “Unabii huu unamhusu nani?”

“Unamhusu Yesu,” mchungaji alijibu.

“Unajua,” alisema Deedat, “Maneno ya msingi kabisa kwenye unabii huu ni ‘mfano wako’. Sasa, ni kwa vipi Yesu ni mfano wa Musa?”

“Musa alikuwa Myahudi na Yesu alikuwa Myahudi. Pili, Musa alikuwa nabii na Yesu alikuwa nabii,” alijibu mchungaji.

Deedat anaendelea kusema, “Kama hizi ndizo sababu mbili pekee zinazotuwezesha kumtambua mhusika wa unabii huu wa Kumbukumbu 18:18, basi unabii huu unaweza kumhusu yeyote kati ya wafuatao baada ya Musa: Sulemani, Isaya, Ezekieli, Danieli, Hosea, Yoeli, Malaki, Yohana Mbatizaji, n.k. maana hawa wote nao walikuwa Wayahudi na pia manabii. Kwa nini basi useme kuwa unabii huu unamhusu Yesu na si hawa wengine?”

Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia? – Sehemu ya II




Katika makala yaliyopita tuliona hoja za ndugu wa Kiislamu wanavyojaribu kwa juhudi nyingi kuonyesha kwamba Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia.

Katika makala hayo niliahidi kuwa nitaeleza jinsi ambavyo hoja zao hazina ukweli wowote. Licha ya kwamba Mungu wanayemwamini amewahakikishia kwamba Muhammad ametajwa kwenye Biblia, ukweli ni kwamba hajatajwa hata kidogo!

Katika sehemu ya kwanza ya mfululizo huu, nilimalizia kwa kunukuu kile ambacho Yehova, Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, anasema juu ya Neno lake. Hebu tuangalie tena baadhi ya maneno hayo. Imeandikwa:

Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho,tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.

Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. (1 Wakorintho 2:12-15).

Tatizo mojawapo kubwa ninaloliona mara nyingi kwenye Uislamu na Waislamu ni kutazama mambo kwa jinsi ya mwili. Hapo ndipo penye shida kubwa yanapokuja masuala ya rohoni.

Je, Mtume Muham-mad Yuko Wapi Hivi Leo?




Mungu hutufunulia mambo mbalimbali kupitia watumishi wake mbalimbali ili kutujulisha yale yaliyopo na hata yajayo; katika ulimwengu huu na pia ule ujao. Wapo watu wengi ambao Mungu amewatumia kutufahamisha juu ya mbingu na hata juu ya kuzimu.

Bo Ra Choi ni mchungaji kutoka Korea ya Kusini. Mchungaji huyu amekuwa akionyeshwa maono mbalimbali na Mungu kuhusu mambo ya ulimwengu wa roho. Mojawapo ya maono aliyoonyeshwa yanamhusu Muhammad, mtume wa Uislamu.

Je, Muhammad yuko wapi hivi leo? Katika video hii, mchungaji Bo Ra Choi anafikisha kwetu ujumbe kwa namna ambavyo alisikizishwa Muhammad akisema kule aliko sasa.

Kwa maana nyingine, ananukuu moja kwa moja maneno ya Muhammad ili kwamba iwe ni kama vile tunamsikia Muhammad akizungumza.

Tafadhali zikiliza kwa makini video hii, kisha utaupata ujumbe wa Mungu anaouleta kwetu kupitia mtumishi wake, Mchungaji Bo Ra Choi.

Toufik Alikuwa Mwislamu Lakini Alimwita Yesu, Leo Ameokolewa na Hajawahi Kujuta


Ufuatao ni ushuhuda wa Toufik, ambaye alikuwa ni Mwislamu lakini alikutana na injili ya Bwana Yesu na kubadili welekeo ambao hajaujutia; na hata anapoelezea neema hii ya wokovu wa Yesu aliyoipata, machozi yanamtoka. Pia machozi yanamtoka zaidi anapowafikiria ndugu zake Waislamu ambao wanapambana kwa jitihada nyingi wakijaribu kumpendeza Mungu kwa njia ya matendo yao ya kidini. Toufik analia anapotambua kuwa yote hiyo wanayofanya ni kazi bure kwa kuwa hawajagundua ziri ambayo na yeye, miaka mingi iliyopita, alikuwa hakuijua.


......................

Nilikulia kwenye familia ya Kiislamu ambayo ilikuwa inatii imani ya Uislamu. Nilipokuwa na miaka mitano nilienda shuleni. Na wakati huohuo nilihudhuria msikitini na kufundishwa kuhusu Uislamu.

Nilipokuwa nikimtafakari Allah, sikumuona kama Mungu mzuri, Muumba anayependa viumbe wake. Nilimuona kama Mungu mkubwa sana ambaye wakati wowote alikuwa tayari kuniharibu.

Hata mimi mwenyewe sikujiona kama mtu anayekwenda mbinguni. Nilipotazama matendo yangu mazuri na yale mabaya, sikuona uwezekano wa mimi kupona.

Nilijiuliza maswali mengi: Hali yangu ya kiroho ikoje? Mungu yuko wapi sasa? Hivi mimi anaponiangalia ananionaje hasa? Anawaza nini juu yangu? Hivi ndio nimetengwa kabisa naye kutokana na dhambi zote nilizofanya? Je, kuna njia ya kumrejea? Nawezaje kurejea tena kwake?

Yesu Aongea na Binti wa Kiislamu; Binti Aokoka




Sharoni hakuwa Mkristo bali alikuwa ni binti wa Kiislamu. Na wala hakuwa amewahi kujifunza habari za Yesu na Ukristo. Lakini Bwana Yesu mwenyewe alimfuata na kujidhihirisha kwake. Je, ilikuwaje, na nini kilitokea baada ya hapo? Tafadhali fuatilia ushuhuda huu wenye nguvu na unaodhihirisha upendo na uweza na uungu wa Bwana Yesu.

……………………………….

Jina langu ni Sharoni Sabina Natrajan. Kwa sehemu kubwa ya maisha yangu nilikulia Bombay. Familia yangu si Wakristo. Kwa hiyo sikuwahi kupata mafundisho yoyote ya Kikristo. Natokea kwenye familia ambayo inathamini sana elimu, na kila mtu ana elimu ya kutosha. Upande wa mama yangu, anatokea kwenye ukoo wa Zaminda. Na hata nyakati zile, wavulana na wasichana walikuwa na elimu kubwa.

Baba yangu ni injinia ambaye amesoma kwenye chuo kinachoheshimika sana, na anashikilia cheo kikubwa kwenye makampuni ya kimataifa hapo Bombay.

Sisi ni familia ndogo tu yenye mimi, dada yangu, baba na mama. Tangu nikiwa mdogo, nilikuwa ni mtu ninayependa masuala sanaa (creative arts). Nilisomea na kuhitimu katika sanaa za maonyesho na pia uchoraji. Kwa hiyo, maisha yangu yote ya utotoni yalikuwa yamejikita kwenye mambo haya.

Wazazi wangu walikuwa na upendo sana na nilipata kila nilichohitaji. Sikupungukiwa na chochote maishani mwangu.

Baba yangu alipenda sana nisomee uinjinia, licha ya kuwa wakati nikiwa sekondari ya juu nilikuwa tayari nikifanya sanaa za maonyesho kote nchini – kucheza ngoma, maigizo,n.k. Sasa, kwa kuwa alitaka niwe injinia, nilituma maombi na kupata nafasi kwenye chuo kizuri sana. Uinjinia haukuwahi kuwa jambo la moyoni mwangu, lakini nilifanya hivyo ili tu kuwafurahisha wazazi wangu. Kwa hiyo, nilienda Puna kusomea uinjinia lakini wakati huohuo nilikuwa nikifanya sanaa za maonyesho.

Mungu Amwonyesha Nabeel Njia ya Kweli Kati ya Uislamu na Ukristo - Sehemu ya 2




Katika sehemu ya kwanza ya ushuhuda huu wa Nabeel, aliyekuwa Mwislamu kisha akakutana na Bwana Yesu na kupokea wokovu, tuliona jinsi ambavyo alimwomba Mungu ampe maono yatakayomwonyesha imani ya kweli. Alionyeshwa misalaba kwenye maono lakini yeye akasema labda ni macho yake tu yamemchezea mchezo. Kwa hiyo, alimwomba tena Mungu kwamba, kama yale maono yalitoka kwake, basi ayathibitishe kwa ndoto. Je, Mungu alifanya nini? Tafadhali endelea kusoma sehemu hii ya pili.


…………………………………

Mungu alinipatia ndoto ile kwa uwazi sana kiasi kwamba sikuwa na ulazima wa kuitafsiri. Lakini ilikuwa wazi hata zaidi kuliko nilivyotarajia. Saa chache baadaye niliwasiliana na David na kumwambia kuwa nimeota hivi na hivi.

David aliniambia, “Sina ulazima wa kutoa maoni yangu juu ya hilo. Kila kitu kiko kwenye Biblia.”

Nikasema, “Unasemaje?”

Akasema, “Nenda kwenye Luka 13.”

Nilienda kwenye Luka 13 mstari wa 22 hadi 29. Niliposoma nikakuta kumeandikwa kuhusu kuingia kwenye Ufalme wa Mungu, na Kristo akasema kwamba, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza. Jitahidini kuingia kupitia mlango mwembamba. Na watu watakuwa wamesimama kwenye mlango huo wakibisha hodi.

Na hicho hasa ndicho kilichotokea kwenye ndoto yangu. Nilikuwa kwenye huo mlango ambao ulikuwa haujafungwa bado. Fursa ya mimi kuingia humo kwenye kushiriki sherehe ile ilikuwa bado ipo. Nilichotakiwa tu kufanya ni kukubali mwito.

BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds

  BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds. The targets included a Radwan Force training facility used for weapons drills ...

TRENDING NOW