Saturday, April 26, 2014

JAMANI EEEE ALLAH AMEFIRISIKA SASA ANANUNUA WATU?

KUMBE ALLAH NI MFANYA BIASHARA..............

Suratut Tawba 111. Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu - wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na Qur'ani. Na nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa

UKIONA ALLAH ANANUNUA WATU, BASI ELEWA KUWA YESU ANABATIZA KWA MALUNDO.

Hakika hakuna Mbingu wataingia watu walio nunuliwa na Allah.

Friday, April 25, 2014

MUHAMMAD SIO MTUME KWASABABU HAKUWAI ONGEA NA MUNGU


Leo ningependa tujikumbushe mambo machache ambayo labda hatukuyatilia maanani. Mitume wote na manabii wote wa Biblia waliwai ongea na Mungu. Lakini, Mtume wa Allah "Muhammad" hakuwai ongea na Mungu HATA MARA MOJA. Je, utume wake tutauamini vipi maana hakuwai ongea na aliye mtuma?

Lakini Mitume wote wa Biblia waliongea na Mungu.
1. Musa anoangea na Mungu: Kutoka 3:1-21
2. Elia anaongea na Mungu: 1 Wafalme 19- Soma yote
3. Paulo anaongea na Mungu: Matendo ya Mitume 18:9
Hiyo ni mifano michache kutoka Biblia.

Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu?

KUMBE ALLAH ANAYE MSAIDIZI

UTATA NDANI YA KURAN KUHUSU UTAMBULISHO WA ALLAH!!
KUMBE ALLAH ANAYE MSAIDIZI


Je, Allah anaye Msaidizi, mbona anatumia wingi katika kujieleza?
Hebu rejea kwenye Kuran kwanza:


Suratul Anbiyaa 91. Na mwanamke aliye linda uke wake, na TUKAmpulizia katika roho YETU, na TUKAmfanya yeye na mwanawe kuwa ni Ishara kwa walimwengu
.
Ndugu zanguni, Allah ameanza vituko vyake hapa. Katika Koran Allah anadai kuwa hana msaidizi Suratul Baqarah: aya 106 ― 107 Lakini katika aya tuliyo isoma hapo mwanzoni - Suratul Anbiyaa 91 tumeona kuwa Allah anatumia wingi alipo kuwa akielezea jinsi alivyo mpa ujauzito Maryam. 

ALLAH ANAMUUMBA ISA BIN MARYAM KWA KUTIMIA WINGI
Kuran imejaa utata, hebu soma hapa Suratul Attahriim 12. Na Mariamu binti wa Imrani, aliye linda ubikira wake, na TUKAmpulizia humo kutoka ROHO YETU, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa wat'iifu. 


HAPA: Allaha anasema kwa undani zaidi TUKAmpulizia ROHO YETU. Hivi huyu Allah ni kweli alikuwa Mungu au ni madai ya Muhammad na rafiki yake Jibril? Mbona alisema kuwa yeye hana msaidizi wala Mwana? Kivipi Allah anatumia wingi katika kumuumba Isa Bin Maryam? 

Aya zaidi kuhusu Maryam na kupata ujauzito za Isa: Suratul Anbiyaa 91.


Endelea hapa tena: 

ALLAH ANAMUUMBA BINADAMU KWA KUTUMIA WINGI:
Suratul Hijr 26. Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
HAPA tumesoma kuwa Allah anamuumba Binadamu kwa kutumia wingi" Nukuu: Na TULIMUUMBA MTU" 


Endele hapa tena

ALLAH ANAUMBA MAJINI KWA KUTUMIA WINGI:
Suratul Hijr 27. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.


Allah anaendelea kutumia wingi katika uumbaji. Sasa anasema kuwa "TULIWAUMBA MAJINI" Allah anaendelea kutumia wingi katika uumbaji.


Je, unafikiri kuwa labda Allah alijisahau au fanya makosa pale alipo sema kuwa yeye hama msaidizi. 

Wadhalimu wa dini ya Kiislam wamekuwa mstari wa mbele kusema kuwa, eti Wakristu wana miungu mingi na wao wana Mungu Mmoja tu naye ni Allah. Leo tumejifunza kuwa, Allah hayupo peke yake maana sasa anatumia wingi katika kazi zake ikiwa pamoja na ya uumbaji wa Binadamu na Majini.

Nukuu zingine ambazo ALLAH anatumia wingi: S. 3:44, S. 3:145, S. 17:1, S. 6:114, S. 19:40-42, 50-53, 56-74 Arberry, S. 2:252-253 , S. 3:108 Y. Ali; cf. S. 45:6, S. 37:161-166 Pickthall, S. 37:170-182 Y. Ali, S. 23:12-14 Arberry, S. 19:16-2, S. 66:12 Pickthall, S. 15:26-29 Pickthall.

Ndugu zanguni nimeweka ushaidi wa kutosha kutoka Quran yao kuhusu wingi ambao Allah amekuwa anautumia kila mara kwenye Quran yake.

Je, Allah anaye Msaidizi? Je, Allah anaye Mwana ambaye na yeye ana wadhifa wa KiAllah? Kwanini Allah anatumia wingi huku tukifahamu kuwa Allah hafananishwi wala hana msaidizi?

Hakika kuna shaka kubwa kubwa kwenye Quran ya Allah ambayo sasa inasema kwa kutumia wingi. 

Biblia inasema kuwa Mungu anaye Mwana na anaitwa Yesu, zaidi ya hapo Biblia inatuambia kuwa kuna Mungu Roho Mtakatifu na hao wote ni WAMOJA katika Roho. 

Karibuni kwa Mungu wa Biblia ambaye amesema kiuwazi kuwa yeye ni Baba na ana Mwana ambaye na yeye ni Mungu. Kumbuka hawa ni wamoja kwa kupitia Mungu Roho Mtakatifu.

Katika Huduma yake.

Max Shimba Ministries Org.
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

Saturday, April 19, 2014

Eti Biblia inataja mashehe, kwa hiyo inaunga mkono Uislamu!




Wahubiri wa ‘injili’ wa Kiislamu wanaendelea kuhaha kuhalalisha quran kupitia Biblia. Nasema ‘kuhaha’ kwa sababu hakika kabisa wana juhudi kubwa mno lakini inasikitisha kwa sababu hakuna hata siku moja waliyowahi kusema jambo lenye ukweli kibiblia linalounga mkono quran kama wasemavyo wao – Mungu ni shahidi yangu. Mara waseme Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia; mara waseme Yesu aliposema kuwa ataletwa Msaidizi basi alimaanisha Muhammad, n.k. Ni kituko kimoja baada ya kingine. Na wanayemdanganya ni wao wenyewe pamoja na Wakristo wachache wasiojua Biblia.


Kwa msingi huohuo, wanasema eti Biblia imewataja mashehe; na kwa hiyo kwao huo ni ushahidi kuwa uislamu ulikuwapo tangu zamani.

Acha ninukuu hoja ya mmoja wao kama ilivyo, kuhusiana na suala hili, kisha kama kawaida, utaona jinsi hoja hiyo inavyosambaratika mbele za nuru ya Kristo, yaani neno lake.

Wednesday, April 16, 2014

YESU ALIISHI KABLA YA DUNIA KUUMBWA


Yohana 17:5 Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. 

Katika aya hapo juu tunasoma kuwa Yesu aliishi kabla ya kuumbwa ulimwengu. 

Kumbe basi Yesu si Nabii tuu, kama wanavyo dai Waislam kuwa eti, Yesu ni Nabii tu na si zaidi ya hapo. Kumbe Yesu ni zaidi ya Nabii, maana aliishi kabla ya kuzaliwa. 

Ndugu zanguni, nani aliye ishi kabla ya Uumbaji? Hata Koran inakiri kuwa, kabla ya kuumbwa kwa vitu vyote, alikuwepo Mungu. YESU ANASEMA KUWA, ALIISHI KABLA YA UUMBAJI. (Yohana 17:5).

Kumbe basi, Yesu ni Mungu maana alikuwepo wakati wa uumbaji. Wakolosai 1: 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. 

Tumesoma katika Wakolosai kuwa katika Yesu kila kitu kiliumbwa na tunasoma kuwa Yesu alikuwapo kabla ya kuumbwa kwa vitu vyote, kama ilivyo semwa katika Yohana 17:5.

Yohana 1: 3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Katika hii aya nayo inatuambia kuwa, katika Yesu vyote vilifanyika.

Ndugu zanguni, ni nani huyu mwenye mamlaka haya kama sie Mungu? Iweje Yesu aishi kabla ya kuumbwa Dunia? Iweje kila kitu kiliumbwa kupitia Yesu? 

Biblia inatuambia kuwa Mungu ndie muumbaji wa kila kitu. Biblia hiyo hiyo imetuambia kuwa kupitia Yesu, kila kitu kiliumbwa. Kumbe basi Yesu ni Mungu muumbaji. 

Leo tumejifunza kwa ufupi tu kuwa, YESU ALIISHI KABLA YA KUUMBWA DUNIA.

Katika huduma yake,

Max Shimba Ministries

JINA LA YESU LINAMAMLAKA YA KURUDISHA MALI ZAKO ZOTE




Ndugu Msomaji: Leo ningependa tujikumbushe jambo Fulani kuhusu maisha yetu ya kila siku.

Hebu kwanza tusome neno la Mungu kama lilivyo andikwa katika Isaya:

Isaya 42:22‘Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.’

Inawezekana kabisa labda huelewi kuwa, shida zako zote zimesemwa katika hii aya hapo juu. Labda hufahamu kuwa wewe ni tajiri na Shetani amekuwa akikuibia mali zako. Labda hufahamu kuwa wewe ni Msomi na ulitakiwa uwe na Madigirii kadhaa. Labda hufahamu kuwa wewe ni Kiongozi Fulani ambae ameibiwa uongozi wake, “nyota yako”.

Leo ningependa ufahamu kuwa Shetani ni Mwizi na anaweza kukuibia wewe unae soma huu ujumbe. Ningependa ujiulize, hivi, Je, huyu Shetani alikuibiaje wakati wewe ni mtoto wa Mungu na umeokoka?

Katika Injili kutokana na Yohana 10:10 inasema kuwa: Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.

Mpendwa katika Bwana. Ningependa ufahamu kuwa, hiyo ndio kazi kuu ya Shetani katika Maisha ya Mkristo. Shetani amekuja kukuibia mali zako, labda amekuja kukuibia amani yako ya wewe na familia yako. Labda amekuja kukuharibia watoto wako. Ndugu msomaji, jibu tunalo na tumekuwa nalo kila siku, lakini tumeshindwa kulitumia. Isaya anasema kwenye aya hiyo hiyo kuwa “wala hapana asemaye, rudisha”

Je, wewe umesha wai mwambia Shetani arudishe mali zako? Labda kwasababu hukuwai ziona na aliziiba kabla ya wewe kuzishika, haimaanishi kuwa wewe sio tajiri. Baba yetu aliye Mbinguni ni Tajiri Mkuu, hivyo elewa kuwa, wewe kama motto wake ni Tajiri vile vile. Hebu jisifie kidogo kuwa, wewe ni motto wa tajiri. Sema hivyo na anza kukiri kuwa wewe ni tajiri na sio maskini.

Biblia inasema katika Isaya 42:18 kuwa, tutoke kwenye upofu, tumebaki kuridhika na hali mbaya tuliyonayo tukiona amani tu! Kumbe tuko vipofu! Hatuoni uhalisia.

Leo ningependa ufungue macho yako ya Kiroho na uelewe kuwa, Mungu anakupenda na anataka utoke kwenye upofu. Mungu anataka usiridhike na kidogo ulicho nacho. Mungu anataka usikubali kuwa hali mbaya ni ya kwako. Leo nakuomba ufumbue macho yako na umwambie Shetani rudisha mali zangu zote ulizo ziiba katika jina la Yesu. Mwambie Shetani akurudishie fedha zako zote alizo ziiba ukiwa na ufahamu na au bila ya ufahamu. Mpendwa katika Bwana. Mungu wetu ni Upendo na anatupenda ndio maana alimtoa Mwana wake wa pekee ali aje na afe kwa ajili ya matatizo yetu yote. Matatizo ya Kifedha, matatizo ya magonjwa. Matatizo ya kifamilia. Kikazi, kishule. Kila aina ya matatizo Yesu aliyamaliza pale Msalabani. Ndio maana Yesu alisema kabla ya kukata roho kuwa “IMEKWISHA”.

Sasa anza kumwabia Shetani kuwa ameshindwa kwa Jina la Yesu. Mwambie kuwa leo unafahamu kuwa wewe ni mtoto wa Mungu na umebarikiwa na Mungu aliye juu. Mwabie Shetani kuwa kuanzia leo, hana mamlaka na mali zako zote. Mwambie kuwa kuanzia leo, hana mamlaka na familia yako katika Jina la Yesu. Mwambie kuwa Ushindi ni wako katika Jina la Yesu. Mkumbushe Shetani kuwa aliye ndani yako ni Mkuu kuliko yeye aliye nje. Mwambie kuwa Damu ya Yesu imekuzingira na mteketeza na msambaratishe kwa kutumia Damu ya Yesu. Vunja uovu wake wote alio ufanya katika maisha yao. Vunja uchawi wote alio ufanya katika maisha yako kwa kutumia Damu ya Mwana Kondoo katika Jina la Yesu. Vunja hila zote alizo zifanya kwako kwa kutumia Damu ya Yesu. Vunja kila aina ya uovu, wizi, uchawi, uongo alio ufanya kwako kwa kutumia Damu ya Yesu.

Mambo yanaweza kufichwa machoni pako usiyaone, na inakuwa hasara kubwa sana lakini kama ungeona, ungetengeneza. Tunatakiwa tutambue majira ya kujiliwa kwetu. Haya ndio yale majira Yesu anataka kurudisha heshima ya jina lake, majira ambayo Yesu anataka kufanya falme za dunia ziwe zake.

Isaya anasema unaona mambo mengi lakini huyatii moyoni, kwanini inakuwa hivyo ndo linapokuja swala la Isaya 42:22 kwamba huyu mtu anakuwa ameibiwa moyo, macho ndo mana anaona lakini hatii moyoni nk.

Akina Daudi walivyorudi na kukuta mji wao umechomwa moto na kila kitu kimeibiwa hadi wakeze. Wanaume wakaanza kulia hadi wakaishiwa nguvu lakini haikuwa suluhisho! Daudi akaona hili jambo suluhisho si kulia bali ni kuingia mbele za BWANA, kutafuta suluhisho, hata wewe ndugu yangu haijalishi una tatizo kiasi gani, wazazi , ndugu , marafiki , bunge na vyote hapa duniani haviwezi kukusaidia, muige Daudi kwa kumwangalia Yesu maana yeye ndiye mwenye funguo za mauti na kuzimu. Daudi akaruhusiwa na BWANA aende na atarudisha vyote ndipo Daudi alipowaongoza wenzie na kwenda na hakika walirudisha vyote.

1Sam 30:1 ‘Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka. ………………. Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka……… Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote. Basi Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye……. Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia.

18 Daudi akawapokonya wote waliokuwa wamechukuliwa na Waamaleki; naye Daudi akawaokoa wakeze wawili.
19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote. ….’

Leo tunaenda kulifuatilia jeshi la shetani na kurudisha vyote, kwa msaada wa BWANA itawezekana.2 Samw 22:30 ‘Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi; Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
31 Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia..’.

Yoh 5:28 ‘..msistaajabie maneno haya kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 Nao watatoka; ..’
yaani haijalishi shetani aliwapataje pataje, iwe kiuhalali au vinginevyo, mimi najua neno moja tu ‘NAO WATATOKA’

Isaya 49:24 ‘ Je! Aliye hodari aweza kunyang'anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka? 25 Naam, Bwana asema hivi, Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye jabari wataokoka;……’

Isaya 14:17 ‘ Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? ’

SASA FANYA MAOMBI HAYA HAPA CHINI NA AMINI KUWA USHINDI NI WAKO

PASAKA NI NINI NA MAANA YAKE


Pasaka ni sikuku iliyoamriwa na Mungu tangu siku za kale kwa wayahudi kuifanya katika mwezi wa Abibu au Nisani katika “kalenda ya kiebrania” yaani mwezi wa 3 au 4 katika kalenda ya kirumi, kwa lengo la kumbuka njisi Mungu alivyowakomboa kutoka utumwani Misri; Twasoma: “Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka BWANA, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku BWANA; Mungu wako. Nawe umchinjie pasaka BWANA, Mungu wako katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua BWANA apakalishe jina lake.” (Kumbukumbu 16:1-2) Soma pia: (Kutoka 12:14) Kama tulivyoona katika pasaka wayahudi waliamriwa kuchinja mnyama mmoja katika kundi, lakini tunapoendela kusoma tunaona jinsia Mungu alivyoamuru mnyama huyo aokwe na kuliwa; Twasoma:

“Usimle pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate kukumbuka siku uliyotoa nchi ya Misri, siku zote za maisha yako. Wala isionekane kwako chachu muda wa siku saba katika mipaka yako yote; wala katika hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni, kisilale cho chote usiku kucha hata asubuhi. Usimchinje pasaka ndani ya malango yako yote akupayo BWANA, Mungu wako; ila mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinjia pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri.” (Kumbukumbu 16:3-6); Soma pia: (Kut 12:3-13) Katika mwezi huo wa abibu ambao Mungu aliufanya kuwa mwezi wa kwanza kwako, Wayahudi walifanya karamu ya Pasaka kuwa kumbukumbu la jinsi Mungu alivyowaokoa kutoka Misri (Kutoka 12:1-51; Walawi. 23:5).

Pasaka maana yake ni "kupita Juu", maana Mungu alipita juu ya nyumba zao asiwaangamize wazaliwa wao wa kwanza; Twasoma: “Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazo kuwapo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu nitakapoipiga nchi ya Misri.” (Kutoka 12:13); Soma pia:(Kutoka 12:27)

JE WAKRISTO TUNA PASAKA LEO?
Ni kweli wakristo tuna pasaka leo, walakini si katika utaratibu ule Uliotumika katika siku za waisraeli, kama tulivyoshuudia maandiko yaneleza wazi ya kuwa sikukuu hizo zilikomeshwa; Basi hebu tuone utaratibu wa Pasaka ya wakristo leo ni upi;

Zingatia: Kama tulivyoona hapo juu, waisraeli waliokolewa na damu ya mnyama walio ipaka katika miimo na miisho ya milango yao na ndipo malaika wa Bwana alipotambua na kupita juu; Soma tena: (Kutoka 12:13, 27); lakini wakristo tunaambiwa pasaka wetu ni Yesu mwenyewe aliyetuokoa kwa damu yake; Twasoma:

“Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!” (Yohana 1:29); Soma pia: (Yohana 1:36) “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa milioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.” (1 Petro 1-18-19) “Basi jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mapate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;” (1 Wakoritho 5:7) Basi kama tulivyoona Neno la Mungu linatuthibitishia ya kuwa kwa sasa wakristo tunaokolewa na damu ya Yesu ambaye ndiye Pasaka wetu na si kwa damu ya mnyama aliyekuwa Pasaka wa kale. Basi kiwa hivyo ndivyo, ni dhahiri hata utratibu wa kusherehekea pasaka kwa wakristo ni tofauti, Basi hebu tuone wakristo tunasherehekeaje pasaka yetu leo.

Yesu alipokuwa akila Pasaka ya mwisho pamoja na wanafunzi wake, aligeuza Pasaka. Aliwaambia kwamba, kuanza siku ile, watakapokula mikate wangekumbuka mwili wake uliotolewa kwa ajili yao badala ya kukumbuka kuokolewa kutoka utumwani nchini Misri; Twasoma: “Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega akawapa wanafunzi wake, akisema, Twaeni mle; huu ndio mwili wangu Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki; kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.” (Mathayo 26:26-28) “Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa ninyi, ya kuwa usiku ule aliotolewa alitwaa mkate, na ye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu. Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kwa kila mywapo, kwa ukumbusho wangu. Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.” (1 Wakorintho 11:23-26).

JE WANAOSHEREHEKEA PASAKA YA KALE WAMEPOTEA?
Ni kweli karibu ulimwengu mzima unasherehekea pasaka kama walivyokuwa wakisherehekea wayahidi nyakati zile, wakidhani ndivyo ilivyo agizwa, basi na tuzingatie maneno yafuatayo; Twasoma: “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti” (Mithali 14:12) “Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa. Waacheni hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.” (Mathayo 15:13-14) “Si kila aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.” (Mathayo 7:21-23) “Basi ndugu, mambo hayo nimeyafanya kuwa mfano wa mimi na Apolo kwa ajili yenu ili kwamba kwa mfano wetu mpate kujifunza kutokupita yale yaliyoandikwa; ili mmoja wenu asijivune kwa ajili ya huyu, kinyume cha mwenziwe.” (1 Wakorintho 4:6) Basi kama tulivyoona, upotofu uliopo katika sikukuu hii ya pasaka na jinsi Mungu anavyo tuonya kuwa makini na mafundisho ya uongo, ni dhahiri tunawajibu wa kujifunza neno la Mungu kwa bidii ili tupate kujua yaliyo mapenzi yake tukayafanye; Soma: (Yakobo 1:22-25)

Monday, March 24, 2014

ASALIMISHA MANYANGA YA UCHAWI BAADA YA KUTEKWA KANISA LA UFUFUO NA UZIMA

Ni maajabu makubwa ambayo Mungu anaendelea kufanya kupitia huduma ya Ufufuo na Uzima mkoani Arusha chini ya Mch. Frank Andrew; ambapo wiki hii kumetokea na jambo ambalo liliwaacha katika mshangao watu wengi walioudhuria ibada kanisani hapo.
Tukio hilo la aina yake lilimjumuisha dada aitwaye kwa jina la Lightness ambaye alisalimisha mambo yake ya uchawi ambayo kwa hayo alitesa maisha ya watu wengi. Mikoba hiyo ni pamoja na vyungu, ungo, shanga, pete, makombe na maji ya maiti.
Mapema wiki hii, mchawi mwingine alikamatwa usiku wa saa sita akiwa anawanga hali ya uchi wa mnyama; Mchawi huyo aliyefahamika kwa jina la Saidi alidai kukamatwa na nguvu za Mungu kutokana na watu waliokuwa mkesha usiku wa siku hiyo.
Pichani ni Lightness na manyanga yake baada ya kuchomwa moto yote. Mungu ni mkuu na njia za kutoka mautini zina yeye.
imeandaliwa na Information Ministry

Saturday, March 22, 2014

NANI ALIKUWA MUISLAM WA KWANZA?

UTATA MKUBWA KATIKA KORAN
NANI ALIKUWA MUISLAM WA KWANZA?

Ndugu zanguni:
Leo ningependa tuangalie kiundani kidogo kuhusu, “nani alikuwa Muislam wa Kwanza” kutokana na Koran iliyo teremshwa na Allah.
Kwa mujibu wa vifungu kadhaa katika Quran, Muhammad ni Muislamu kwanza :
Quran 6: 14. Sema: Je, nimchukue rafiki mlinzi asiye kuwa Mwenyezi Mungu, ambaye ndiye Muumba mbingu na ardhi, naye ndiye anaye lisha wala halishwi? Sema: Mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza wa wenye kusilimu. Na wala kabisa usiwe miongoni wa washirikina. 161. Sema: Kwa hakika mimi Mola wangu Mlezi ameniongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka, Dini iliyo sawa kabisa, ambayo ndiyo mila ya Ibrahim aliye kuwa mwongofu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina. 162. Sema: Hakika Sala yangu, na ibada zangu, na uhai wangu, na kufa kwangu, ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote. 163. Hana mshirika wake. Na hayo ndiyo niliyo amrishwa, na mimi ni wa kwanza wa Waislamu. (Wa ' Ana ' Awwalu Al- Muslimin ). S. 6:161-163

Sema (Ewe Muhammad): Hakika Mimi nimeamrishwa nimuabudu Mwenyezi Mungu, kwa kumsafishia Dini Yeye ( tu ). Na nimeamrishwa niwe wa kwanza wa wale ambao ni Waislamu ( kujisalimisha kwake ). S. 39:11-12 Pickthall
Sura hizo hapo juu na aya hizo ulizo zisoma zinapingana vibaya sana na sura zingine katika Koran hiyo hiyo ambazo ziliteremshwa na Allah huyo huyo na kusema Manabii walio tangulia kabla ya Muhammad ndio walikuwa Waislam wa Kwanza.  
Kuran inadai kwamba Adam, Ibrahim, Nuhu, mababu, makabila kumi na mawili ya Israeli, Musa, Yesu nk, hao wote walikuwa waumini wa Allah na walikuwa Waislam, kumbuka hao wote waliishi kabla ya Muhammad ambaye anadai kuwa yeye ni Muislam wa Kwanza:

S. 02:30 , 34-35 , 37
30. Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua. 34. Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipo kuwa Iblis, alikataa na akajivuna na akawa katika makafiri. 35. Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale walio dhulumu. 37. Kisha Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi alimkubalia toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu. S. 02:30 , 34-35 , 37

163. Hakika Sisi tumekuletea wahyi wewe kama tulivyo wapelekea wahyi Nuhu na Manabii walio kuwa baada yake. Na tulimpelekea wahyi Ibrahim na Ismail na Is-haka na Yaakub na wajukuu zake, na Isa na Ayub na Yunus na Harun na Suleiman, na Daud tukampa Zaburi. S. 4:163

84. Na tukamtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaakub. Kila mmoja wao tulimwongoa. Na Nuhu tulimwongoa kabla. Na katika kizazi chake tulimwongoa Daud na Suleiman na Ayyub na Yusuf na Musa na Harun. Na hivi ndivyo tunavyo walipa wafanyao wema: S. 6:84

127. Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ile Nyumba wakaomba: Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi.  128. Ewe Mola Mlezi wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.  129. Ewe Mola Mlezi wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima. 130. Na nani atajitenga na mila ya Ibrahim isipo kuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini Sisi tulimteuwa yeye katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema 131. Na Mola wake Mlezi alipo mwambia: Silimu, Nyenyekea! Alinena: Nimesilimu, nimenyenyekea kwa Mola wa walimwengu wote.  132. Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu.  133. Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake. S. 2:127-133 Shakir

JEHANAMU IPO NA INASUBIRI WATENDA DHAMBI

Huko motoni Jehanum kukoje? Mwanangu, kunatisha, nashindwa hata nikueleze vipi unielewe. Moto wa milele, hatukuwekewa wanadamu bali shetani na malaika zake (MATHAYO 25:41). Kama utakwenda huko baada ya kusoma “note” hii, itakuwa ni kwa sababu ya kiburi chako tu, na kushupaza shingo yako na kukataa kulitendea kazi Neno hili (MITHALI 29:1). Moto wa Jehanum siyo mahali pa mchezo kama walimu wa uongo wanavyofundisha. Walimu hawa huwafariji watu na kusema eti mtu ataunguzwa na moto na kutoweshwa na kupotea na kuangamizwa kabisa na ndiyo mwisho wake. Wanatumia maandiko kama MATHAYO 10:28 (kuangamizwa) na YOHANA 3:16 (Kupotea). Kuangamia katika maandiko hakumaanishi kumalizika kabisa, bali kukabiliwa na mauti (ESTA 4:16). Mauti ya watu walioko motoni, ni mauti ya milele, kama tutakavyoona hivi punde. Kondoo akipotea, haimaanishi hayupo kabisa ila ametengwa na mchungaji (ISAYA 57:1-3).
Biblia inaeleza waziwazi kwamba mtu anapokufa, sekunde ileile ya kufa kwake anakabiliwa na hukumu. Tunasoma katika WAEBRANIA 9:27, ”Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”. Watu wanapofundisha kinyume na kweli ya Neno la Mungu, hufundisha kwamba mtu anapokufa analala tu, na hakuna lolote la hukumu mara moja wakitumia maandiko yafuatayo na kuyatafsiri visivyo – MATHAYO 27:52; 1 WAKORINTHO 15:20; YOHANA 11:11-14 n.k; na pia wanasema wafu hawajui lolote kwa kutumia maandiko kama MHUBIRI 9:5. Ilivyo ni kwamba, kinachobaki kaburini ni mwili tu. Roho ya mtu huondoka na kuingia katika mwili mwingine, unaoitwa mwili wa roho. Miili tuliyo nayo wanadamu kabla ya kufa inaitwa miili ya asili. Tunasoma katika 1 WAKORINTHO 15:40, 44, “Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani,……Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko”.
"Na miale ya moto huwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari njema ya Bwana ya Yesu. Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu" - (2 Wathesalonike 1:8,9).

Moto wa Jehanum ni mkali sana kuliko moto wowote tunaoufahamu duniani. Moto wa gesi wa kuunganishia vyuma, unaotokana na kuwashwa mchanganyiko wa gesi ya “Oxygen”, na “Acetylene”, unaonekana kwa hapa duniani kwamba ni mkali. Moto huu, siyo chochote, ukilinganishwa na moto wa Jehanum. Katika karakana au viwanda vya vifaa vya vyuma, chuma huyeyushwa na kuwa uji katika matanuru ya moto mkali unaofikia nyuzi joto 2,000 hadi 3,000 na zaidi. Moto huu unaoyeyusha vyuma na ukali wake, huo si chochote! (Kumbuka kwamba maji yaliyochemka sana hufikia nyuzi joto 100 tu!) Moto ulio katikati ya jua linalotuangaza, unafikia nyuzi joto milioni kumi (10,000,000°C). Moto wa jua nao, si chochote ukilinganishwa na moto wa Jehanum! Ukali wa moto wa Jehanum, unatisha (WAEBRANIA 10:26-27). Siyo hilo tu, moto wa duniani una rangi mbalimbali, njano,bluu,mwekundu n.k. Moto wa Jehanum ni tofauti kabisa; Ni moto wa rangi nyeusi, unaosababisha giza na kumfanya mtu aliye motoni, awaone wenzake wachache tu wa karibu naye, hivyo hamna faraja ya kusema “tuko wengi!” Moto huu mweusi, ndiyo maana unaitwa “giza la nje” (MATHAYO 8:11-12, MATHAYO 22:13; MATHAYO 25:30; YUDA 1:6). Siyo hilo tu. Moto huu wa Jehanum, una meno! Hivyo una uwezo wa kuwala na kuwatafuna walioko motoni (KUMBUKUMBU 32: 22; WAEBRANIA 10: 26-27). Hata hivyo, pamoja na moto huu kumtafuna mtu, bado una sifa ya kumhifadhi mtu huyo na kumfanya asimalizike, kama jinsi chumvi ilivyo na uwezo wa kuizua nyama kuharibika. Hivyo moto unamtafuna mtu wakati wote, lakini haishi na wala moto wenyewe hauzimiki. Ndiyo maana unaitwa moto wa milele (MARKO 9: 43-49; MATHAYO 25:41).

Watu walioko motoni, hutamani mtu mmoja kati yao atoke motoni aje duniani, awashuhudie ndugu zao, ili waache dhambi, na kukwepa mateso yao, lakini huambiwa kwamba ndugu zao wanapaswa kuyasikia maneno ya manabii walioko duniani, maana hata akitumwa mtu kutoka motoni na kueleza mateso ya huko, watasema ni mwongo, hajaenda motoni. Tunasoma haya katika LUKA 16:27-31, ”Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie,wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, wanao Musa na manabii, wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu. Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa (hawatashawishika) hata mtu akifufuka katika wafu”.

Mpendwa msomaji, ikiwa mama yako mzazi alifariki akiwa hajaokoka, ujue yuko motoni, na anakuambia, “Usinifuate huku mwanangu”. Ikiwa baba yako mzazi alifariki akiwa dhambini, anateseka motoni, na hataki umfuate huko aliko! Ndugu, marafiki na jamaa zako walioko huko wanakukumbuka sana, na hawapendi ujiunge nao huko, bali wanataka utubu na kuokoka mateso hayo ya moto. Walioko huko motoni, wakimwona yeyote mwingine kutoka duniani, ambaye alikuwa na nafasi ya kusikia habari kama hizi na akazipuuza, kisha akawafuata huko motoni, humwambia, “Je wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi! ” (ISAYA 14: 10).

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction ...

TRENDING NOW