Saturday, May 17, 2014

YESU WA BIBLIA SIO ISSA WA KURUAN

YESU WA WAKRISTO SIO ISSA WA WAISLAM
****************************************************************************************
JE, ISA BIN MARYAM NI JINA SAHIHI LA YESU WA BIBLIA?
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika Kiarabu. Je, Isa ni jina la Yesu wa Biblia?
Jibu sahihi la kihistoria na la wataalam wa kutafsiri litatupa ukweli halisi wa Jina la Yesu na kwanini alipewa Jina hilo katika " sherehe ya kumtaja " (Luka 2:21). Jina ambalo aliitwa na Mama yake, Baba yake wa Kambo, Ndugu zake na jamaa wengine, majirani zake , marafiki zake na wanafunzi wake wakati wa maisha yake duniani. Hakuna kutokuelewana kuhusu ukweli kwamba jina la Yeshua halikuwa la Kiarabu bali la Kiyahudi na Yesu/Yeshua mwenyewe aliishi katika Israeli, na alizaliwa katika familia ya Wayahudi wacha Mungu.

Jina la Yesu bila ya shaka yeyote ile ni la Kiyahudi. (Maana yake ni “kweli”). Tafsir ya jina la Yeshua Kiebrania katika Kiingereza itakuwa ni Jesus. Jina la Yesu halikuchaguliwa kiholela na wazazi wake, lakini yeye alipata jina lake moja kwa moja kutoka kwa Mungu (Mathayo 1:21 , Luka 1:31) kwa sababu ya maana ya jina lake na nani alilileta, basi leo hii tunaelewa madhumuni ya Yesu kuzaliwa na kuja hapa duniani (Mathayo 1:21 ).

Katika utamaduni na jadi ya Kiarabu. Jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislam. Na hata leo, jina la Yasu linatumiwa na zaidi ya 99.99% ya Wakristo wote wa Kiarabu. Tembea katika kanisa lolote la Kiarabu huto sikia wanatumia jina la Isa, Sikiliza matangazo ya Wakristo wa Kiarabu katika Radio na Televisheni (za Kiarabu) huto sikiwa Mkristo anatumia jina la Isa, bali wanatumia jina la Yasu. Matangazo yote ya Kikristo katika Uarabu wanatumia jina la Yasu. Kamwe huto ona jina la Isa kama lilivyo kwenye Koran ya Waislamu.

Katika jadi ya Kiarabu na utoaji wa tafsiri wa jina, jina sahihi la Kiebrania (Yeshua) ni Yasu katika Kiarabu. Kila uchaguzi wa tafsiri ya jina la kigeni katika lugha tofauti ni uvumbuzi wa binadamu.
Kiisimu ipo wazi jinsi jina la Yeshua Kiebrania lilivyo tafsiriwa na kuwa Yesu Kiswahili na Jesus Kiingereza:

Yeshua '(Kiebrania) -> Ιησους (Kiyunani) -> Yesu (Kilatini) -> Jesus (Kiingereza) -> Yesu (Kiswahili).

Tuesday, May 13, 2014

UKANAJI MUNGU NI NINI?

“Ukanaji Mungu wazi,” pia waitwa “theolojia wazi” na uwazi wa Mungu,” ni jaribio la kuelezea ufahamu kuhusu Mungu kulingana chuguo huru la mwanadamu. Pingamizi la ukanaji Mungu wazi hasa ni huu: wanadamu wako huru kabisa; ikiwa Mungu alijua hatima, wanadamu hakika hawangekuwa huru. Kwa hivyo, Mungu kabisa hajui kila kitu kuhusu kesho. Ukanaji Mungu wazi washikilia kuwa kesho haijulikani. Kwa hivyo Mungu anajua kila kitu ambacho kinaweza julikana, lakini hajui kesho.


Ukanaji Mungu wazi waweka imani yao katika misingi ya kurasa za maandiko ambazo zaelezea Mungu “anabadilisha mawazo yake” au “kushangaa” au “kuonekana kupata hekima” (Mwanzo 6:6; 22:12; Kutoka 32:14; Yona 3:10). Kwa mwangaza wa maandiko mengine mengi ambayo yaelezea ufahamu wa Mungu wa kesho, maandiko haya lazima yaeleweke kama Mungu anajielezea kwa njia ambazo hatuwezi kuzielewa. Mungu anajua vile hatua zetu na maamuzi yatakuwa, lakini “Anabadilisha mawazo yake” kulingana na hatua yake ikitegemea hatua yetu. Chukizo la Mungu katika unyonge wa mwanadamu haimanishi kwamba hakujua kuwa hayo yatatokea.

Kwa hitalafiano na ukanaji wa Mungu wa wazi, Zaburi 139:4,16 yasema, “Maana hamna neno ulimini mwangu usilolijua kabisa, BWANA. Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.” Mungu angewezaje kutabiri mambo tatanishi katika Agano La Kale kuhusu Yesu Kristo kama hajui siku za usoni? Ni namna gani Mungu kwa njia yo yote ile anaweza kuruhusu wokovu wetu wa milele kama hajui chenye kesho imetubebea?

Mwisho, ukanaji Mungu wa wazi unaanguka kwa vile unajaribu kuelezea yenye hayawezi kuelezeka- uhusiano kati ya ufahamu wa Mungu na penzi huru la mwanadamu. Vile aina ya Kikalvinisti yakaenda kupita kiwango yalivyoanguka ya kuwa yakataa uwepo wa Mungu kila mahali na uwezo wake. Mungu lazima yaeleweke kupitia kwa imani, kwa maana “bila imani ni vigumu kumpendeza Mungu” (Waebrania 11:6a). ukanaji Mungu wa wazi kwa hivyo si wa kiroho. Ni njia nyingine ya mwanadamu aliye na hatima kujaribu kuelewa Mungu asiye na mwisho. Ukanaji Mungu wazi lazima ukataliwe na wafuasi wa Kristo. Huku ikiwa ukanaji wa Mungu wa wazi ni elezo la uhusiano kati ya ufahamu wa Mungu kabla ya uumbaji na penzi huru la mwanadamu, sio elezo la kibibilia.

Monday, May 12, 2014

USHAIDI WA BIBLIA NA KURUAN (SEHEMU YA PILI)


Ndugu wasomaji: Leo ningependa tujifunze sifa za Mungu kupitia Biblia na Kuruani kama ushaidi zaidi wa Umungu wa Yesu.

Hapa chini nitaziweka sifa na au adhama za Mungu na tutaziangalia kama hizo zote zipo kwa Yesu Kristo.

1 Mungu ni wa milele
2 Mungu ndiye muumbaji,
3 Mungu yupo mahali popote,
4 Mungu ndiye anaye samehe dhambi za watu,
5 Mungu anajuwa na kufahamu yote hata yaliyomo mioyoni mwetu,
6 Mungu ni Nuru ya Mbinguni na Duniani
7 Mungu ndiye anaye watuma Mitume na Manabibii!
8 Mungu anauwezo wa kujidhihilisha (kuonekana) na tena mngu ni wa sili (kuto onekana)

JE, YESU WA KWENYE BIBLIA ANAZO HIZO SIFA?

1 MUNGU NI WA MILELE
Quran 2:255, Sifa ya milele ni ya Mungu pekee Je Yesu hiyo sifa unayo?
Waebrania 13:8 Yesu Kristo ni yeye yule jana na leo na hata milele,
Sifa ya Umilele teyari Yesu amesha inyakuwa.

2 MUNGU NDIE MUUMBAJI
Je, hii sifa ya Uumbaji Yesu wa Biblia anayo?
Quran 5: 110. Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!

Friday, May 9, 2014

KWA NINI NAKATAA KUWA MWISLAMU?

Katika ulimwengu wa leo kuna njia nyingi za kutumaini. Furaha ya milele na Mbinguni vina hubiriwa kila mahali. Hata hivyo kuna dini nyingi tofauti, filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo (furaha ya milele) vinatofautiana. Na kila mmoja katika tofauti hizo za dini na filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo; anaamini ya kuwa amesimama katika ukweli.
Katika Surat Maryam, Kuruan inasema kuwa (19) 71.72. Inasema, wala hapana yoyote ila mwenye kuifikia jehanamu, maana ni wajibu wa Mola wako umekwisha kuhukumiwa, nasi tutawaokoa wale wamchao na kuwaacha madharimu hali wamepiga magoti.
Kuruan inakiri kuwan kila bin-adam amekwisha hukumiwa kuingia Jehannam kwa maana huo ndio wajibu wa Allah kuwaingiza watu Jihannam. Allah anaendelea kusema kuwa, yeye atawaokoa Waislam baada kuingia Jehanam. Je, haya madai ni kweli?
Quran 40: 60. Na Mola wenu Mlezi anasema: Niombeni nitakuitikieni. Kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu Mimi wataingia Jahannamu wadhalilike.
Katika Surat Ghaafir inakiri kuwa Alla anaendelea kusema kuwa Waislam wote wataingia Jehannam. Mimi kama Mkristo siwezi kuipenda dini hii ambayo teyari mungu wake amesha toa hukumu ya kwenda Jehannam kwa wote wanao ufuata Uislam.
Zaidi ya hapo, katika Surat Maryam, Allah ameshindwa kutueleza ni kivipi atawatoa watu Jehannam, bali ameweka madai tu kuwa atakuja huko na kuwatoa Waislam.
Bukhari :: Kitabu 6 :: Juzuu 60 :: Hadith 371
Imeletwa kwenu na Anas:
Nabii wa Allah alisema: Watu watatupwa katika Jihannam, na Jihannam itasema. "Je, hakuna watu zaidi wa kuingia huku Jehannam?" (50.30) Mpaka Allah atakapo weka Mguu wake Jehannam, na Jihannam itasema, Inatosha, inatosha (qat! qat!)

YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA!

Katika ulimwengu wa leo kuna njia nyingi za kutumaini. Furaha ya milele na Mbinguni vina hubiriwa kila mahali. Hata hivyo kuna dini nyingi tofauti, filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo (furaha ya milele) vinatofautiana. Na kila mmoja katika tofauti hizo za dini na filosophia na mawazo juu ya tumaini hilo; anaamini ya kuwa amesimama katika ukweli.

Na maisha ya mwanadamu yamefikia mawazo ya hali ya juu. Wengi wetu wanapenda kuishi katika dunia hii kwa muda mrefu iwezekanavyo. Baadhi yao wanategemeo la kuishi milele katika dunia hii.

Lakini kuna njia moja tu ya kumuingiza mtu katika furaha ya kweli ya milele. Kuna ukweli mmoja tu, umfanyao mtu kuwa huru. Kuna namna moja ya maisha itakayomfikisha mtu katika uzima wa milele. Yesu Kristo Mwana wa Mungu, ndiyo “Njia, na Kweli na Uzima.” Kumbuka Yesu mwenyewe alisema, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima; mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya Mimi,” Yoh. 14:6. 

Na Yesu Kristo ni “Njia na Kweli na Uzima.” Kwa sababu Yeye alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. Wote wametenda dhambi kwa kuiasi Sheria ya Mungu (Rum 3:23; 1 Yoh 3:4). “Na mshahara wa dhambi ni mauti,” Rum 6:23. Hii ndiyo mauti ya pili au Jehanamu (Ufu. 21:8; Mat. 10:28). Kwa sababu ya dhambi zetu tulistahili adhabu ya milele katika Jehanamu, lakini kwa sababu ya upendo mkuu wa Mungu na rehema zake alimtoa mwanawe Yesu Kristo akafa msalabani akalipa deni letu la dhambi zetu (Yoh. 3:16-17; Rum. 5:5-10; 6:17-23).

Tuesday, May 6, 2014

JE, NI HAKI KWA MKRISTO KUSALI(KUOMBA) JUMAPILI?

JE, KUNA USHAIDI WOWOTE ULE NDANI YA BIBLIA UNAO MRUHUSU MKRISTO KUSALI(KUOMBA) JUMAPILI?

Tafadhali ungama nami katika somo hili fupi ambalo lina leta utata mwingi sana kwa waaminio katika Kristo na hata wale wanao mfuta Allah.
Sasa rejea na soma hii aya hapa chini:
WALIKUTANA SIKU YA KWANZA YA JUMA:
Matendo 20: 7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.
Siku ya kwanza ya Wiki ni Jumapili na hii ni siku ambayo walio mwamini Yesu walikusanyika na kuabudu. Huu ni ushaidi wa kuonekana kwa macho ambao Wakristo wanaabudu Jumapili hivi leo na walifanya hivyo katika Karne ya kwanza.
1 Wakorintho Mlango 16 1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo. 2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;
Katika Wakorintho hapo juu tunasoma kuwa Watakatifu walikutana siku ya kwanza ya Juma ambayo ni Jumapili.
Ingawa kutokana na Warumi 14:1-12, tumewekwa huru kutokana na laana ya Sheria, hivyo basi, kusali si lazima iwe Jumamosi au Jumapili. Mungu hana utegemezi wa siku tena bali unaweza kusali siku yeyote ile na Mungu akakusikia na si lazima uwe kwenye Jengo ambalo tunaliita "Kanisa".
Biblia inaendelea kusema kuwa, tupo huru katika Kristo Warumi 6:14. Ndio maana tuanenda Kanisani katikati ya wiki na tunasali Mungu.
Zaidi ya hapo, kutokana na kuesabu masaa kwa kutumia kalenda ya Warumi, Siku huwa inaanza saa 6 za usiku, ndio maana Mwaka huwa unaanza Saa hiyohiyo ya 6 usiku. Hivyo basi kutokana na ushaidi wa aya hizi (Luka 11:5; Matendo ya Mitume 16:25; 20:7; 27:27) ni ushaidi tosha kuwa, Wakristo wa Kwanza walisali Jumapili na wali hesabu siku kuanzia saa 6 Usiku.
Katika agano la Kale tunasoma: Nehemia 8: 2 Naye Ezra, kuhani, akaileta torati mbele ya kusanyiko, la wanaume na wanawake, na wote walioweza kusikia na kufahamu, siku ya kwanza na mwezi wa saba.
Hapo tumesoma kuwa Kuhani alisoma Torati meble ya mkusanyiko katika Siku ya Kwanza.
SIKU ZOKE NI SAWA NA UNA HAKI YA KUABUDU:
Sasa soma aya hizi hapa chini kwa ufasaha:
Warumi 14.5 Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. 6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.
Nduguzangu, kutokana na Warumi 14, tumewekwa huru kuchagua siku ya kuabudu, na nini tule au tusile, hivyo hivyo ni kuadhimisha kwa Bwana. Hivyo basi, hakuna kosa lolote lile mtu anapo sali Jumamosi au Jumapili au Jumatatu, au siku yeyote ile ya wiki. Mungu wetu yupo kila siku na siku zote alizumba yeye.
WALIKUTANA KILA SIKU HEKALUNI NA KUSALI:
Matendo ya Mitume 2: 46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,
Unaona hiyo aya hapo juu inavyo sema? Je, Jumatatu imekosekana kwenye hiyo aya, vipi kuhusu Jumanne? Ndio maana nilisema sisi tumewekwa huru kutokana laana ya sheria na sasa tupo huru kuabudu Mungu siku yeyote ile. Mungu si wa Jumamosi tu au Jumapili tu au Ijumaa tu. Mungu ni wa kila siku.
KWANINI UNAPENDA MAFUNZO AMBAYO NI DHAIFU?:
Wagalatia 4:8 Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu. 9 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? 10 Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka.
Mtume Paulo anatukumbusha kuwa, mafunzo ambao tulikuwa tunayafuata kabla ya kukombolewa na Yesu yalikuwa dhaifu. Sasa tumejazwa na Roho Mtakatifu ambaye ndie Mwalimu wetu Mkuu.Basi tushikamane naye na tujifunze kutoka kwake.
Ni mategemeo yangu kuwa, somo hili litatufungua macho na tunasoma Biblia zaidi na kumwomba Roho wa Mtakatifu atufundishe yote.
Katika huduma yake,
Max Shimba Ministries Org.
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

Monday, May 5, 2014

NINI MAANA YA BIBLIA?

Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vilivyo andikikwa na watu 40 katika lugha tatu kuu, na katika mabara Matatu, takribani miaka 1600 kabla na baada ya kuzaliwa Yesu. Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu na kisicho kuwa na makosa yeyote yale.

Biblia inabeba mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na Mashairi(Zaburi), Historia (Mwanzo), Sheria (Taurat) na unabii. Biblia ndio kitabu kinacho tumiwa na Wakristo na ndio muongozo wa Wakristo katika kumtafuta Mungu. Zaidi ya hapo, Biblia hutumiwa kama njia ya Binadamu kuishi hapa Duniani.

Kimsingi, Biblia inaeleza asili ya mtu katika bustani ya Edeni pamoja na kuanguka kwake katika dhambi na nje ya ushirika na Mungu. Kisha inaeleza jinsi Mungu alivyo waita watu wake maalum kwa mwenyewe, Israeli. Mungu katika Biblia aliahidi Masihi atakuja kwa Israel ili aje kuokoa na kurejesha uhusiano wa mwanadamu na Mungu. Yesu alizaliwa na Bikira, alikufa juu ya msalaba, na kulipwa kwa dhambi, huu unabii upo katika Agano la Kale na kutimizwa katika Agano Jipya. (Yohana 5:39).

Zaidi ya hapo, Biblia inatufundisha kusamehewa dhambi kupo katika Yesu pekee. Matendo ya Mitume 4: 12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Wengine wanasema kuwa Biblia ni kitabu zaidi za vitabu vyote vilivyo wai kuandikwa hapa duniani. Huu ushaidi unaweza kuwa ni kwasabau Biblia imetabiri mengi na mabo yote ambayo imetabiri yaliweza kuhakikisha na Wana Historia na Wanasanyi tulio nao hapa duniani.

Hivyo basi, Biblia ni kitabu kinacho beba maneno ya Mungu ambayo ndio msingu mkuu wa Ukristo.

Agano la Kale kilichoandikwa na manabii kama vile Musa, Daudi, Isaya , nk

Vitabu vya sheria - 5 vitabu:
Mwanzo, Kutoka, Walawi, Hesabu , Kumbukumbu
Vitabu vya Historia - vitabu 12 :
Yoshua, Waamuzi , Ruthu, Samweli , Pili Samuel , Wafalme , Pili Wafalme, Mambo ya Nyakati , Pili Mambo ya Nyakati, Ezra , Nehemia, Esta.
Mashairi - 5 vitabu:
Ayubu, Zaburi , Mithali, Mhubiri , Wimbo wa Sulemani
Kinabii - 17 vitabu:
Manabii kubwa - Isaya, Yeremia , Maombolezo, Ezekieli , Danieli;
Manabii Wadogo - Hosea, Yoeli, Amosi, Obadia, Yona, Mika , Nahumu, Habakuki , Sefania , Hagai, Zekaria , Malaki

Vitabu vya Agano Jipya vimeandikwa na wale ambao walimjua Yesu au walikuwa chini ya uongozi wa wale ambao walifanya kazi nae

Vitabu vya Historia - 5 vitabu:
Mathayo, Marko, Luka, Yohana, Matendo
Paulo Nyaraka - 13 vitabu:
Warumi, 1 Wakorintho, 2 Wakorintho , Wagalatia, Waefeso , Wafilipi, Wakolosai , 1 Wathesalonike, 2 Wathesalonike . 1 Timotheo, 2 Timotheo, Tito, Philemon
Mashirika yasiyo ya Paulo Nyaraka - 9 vitabu:
Waebrania, Yakobo, 1 Petro , 2 Petro, 1 Yohana, 2 Yohana , 3 Yohana, Yuda , Ufunuo
Kumbuka: Baadhi ya waandishi sifa Waebrania Paulo.

Katika Ezekiel 23:1-4 inasema, " neno la Bwana likanijia tena kusema, 2 " Mwana wa Mtu , kulikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja; . 3 na wao ukahaba katika Misri Walicheza kahaba katika ujana wao; huko vifua vyao walikuwa taabu , na kuna karibu yao bikira alikuwa kubebwa 4 " majina yao , mkubwa aliitwa Ohola na Oholiba dada yake wakawa Mine, wakazaa wana na binti na kama kwa wao. . . majina, Samaria ni Ohola, na Yerusalemu ni Oholiba. "

Katika Huduma yake,

Max Shimba Ministries Org
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

Thursday, May 1, 2014

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU


SOMO LA 1

ROHO MTAKATIFU,MTOA UTAKATIFU
Katika somo la kwanza katika mfululizo wa masomo haya yanayohusu Roho Mtakatifu,Tulijifunza kwamba Roho Mtakatifu,ni mtakatifu,hivyo anakuwepo na kudumu mahali palipo na utakatifu tu.Tukiwana maisha ya uchafu,yaani dhambi;humfanya Roho Mtakatifu akose makao kwetu,na hivyo hawezi kuwepo kwetu.Kama alikuwepo mwanzo kwetu,huondoka (1Samweli 16:14;
Zaburi 51:4,10-11).Sasa swali linakuja,tunawezaje kuwa watakatifu katika maisha yetu ili Roho Mtakatifu afanye makao
kwetu?Jibu ni kwamba,Roho Mtakatifu ,ndiye huyohuyo anayetoa utakatifu tunaouhitaji.Sasa tunamwangalia Roho
Mtakatifu kama Mtoa Utakatifu,kwa kutafakari kazi yake hiyo katika vipengere vitano:-
1. ROHO MTAKATIFU,ROHO ATUPAYE KUZALIWA MARA YA PILI
2. ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO
3. ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU WALIOZIMIA KIROHO
4. ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO
5. ROHO MTAKATIFU, ROHO ATUPAYE TUNDA LA ROHO

1. ROHO MTAKATIFU,ROHO ATUPAYE KUZALIWA MARA YA PILI
Hatupaswi kamwe kudanganyika kwamba utakatifu siyo duniani ni mbinguni,Maandiko yanaeleza waziwazi kwamba watakatifu walioko duniani ndiyo anaopendezwa nao Mungu(Zaburi 16:3). Hatupaswi pia kudanganyika kwamba tunaweza kufanya dhambi hapa duniani,halafu tukasalimika baada ya kufa,kutokana na misa ya wafu n.k(1Wakorintho 6:9-10;Waefeso 5:5-7;Wagalatia 6:7 ;Waebrania 9:27;IYohana 5:16;Kumbukumbu 10:17) la maana hapa ni kufahamu ni jinsi gani tunavyoweza kuwa na ushindi dhidi ya dhambi hapa duniani,na kuokoka kutupwa motoni,maana bila shaka tunatakiwa kuokoka tukiwa hapahapa duniani (Luka 19:8-10);Tito 3:3-4)Tunawezaje kuwa na ushindi dhidi ya dhambi?Ni kwa kuzaliwa mara ya pili,kwa Roho Mtakatifu(Yohana 3:3-10;Tito 3:3-5)Yesu Kristo,alijaribiwa sawasawa na sisi lakini hakutenda dhambi(Waebrania 4:14-15)Ni nini siri ya ushindi wake huo?Ni kwa sababu alizaliwa kwa Roho Mtakatifu,yaani alizaliwa tofauti na kawaida ya kimwili ya mume na mke.Sisi nasi tunapotubu dhambi
zetu kwa kumaanisha kuziacha,tunapata rehema hii kwa imani tu(Mithali 28:13)Tunazaliwa mara ya pili katika ulimwengu wa roho,na hivyo kuwa na uwezo wa kushinda dhambi kwa muujiza mkubwa.Katika hali ya kawaida ya jinsi tulivyozaliwa kimwili,kamwe hatuwezi kushinda dhambi.Ni mpaka tufanyike viumbe vipya kwa Roho Mtakatifu.Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kuzaliwa mara ya pili,naye atafanya.

2. ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO
Kurudi nyuma na kuacha wokovu kunaitwa pia kufa kiroho(Ufunuo 3:1;Waefeso 2:1).Kwa kila aliyerudi nyuma na kuacha wokovu,hii ni saa ya kuamka usingizini na kuanza upya(Warumi 13:11-12).Lakini,je,inawezekana kuanza upya tena katika hali hii?Ndiyo,kwa msaada wa Roho Mtakatifu.Hii ni kazi yake nyingine .Roho Mtakatifu ndiye aliyemfufua Yesu,alipokufa(Warumi 13:11). Kwa jinsi hiyo hiyo,Roho Mtakatifu anaweza kutufufua kiroho
na kutupa uhai tena wa kiroho(Waefeso 2:1,4-6).Mwambie Roho Mtakatifu kwamba unataka kufufuliwa kiroho, naye atafanya.

3. ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU
Kabla ya kufa kiroho,hutangulia kuzimia kiroho.Shetani hutupeleka hatua kwa hatua,kama upepo katika tairi unavyotolewa kidogo kidogo kutokana na pancha ndogo.Tukizimia kiroho,upendo wa kwanza unatoweka. Ingawa bado hatujafikia hali ya kufanya dhambi za uzinzi,uasherati,ulevi n.k kama mataifa,hata hivyo,mambo ya rohoni yanakuwa hayana mvuto kwetu kama mwanzo.Kuomba,kushuhudia,kuhudhuria ibada n.k,yanakuwa
mzigo kwetu.Tunaanza kuvutwa zaidi na mambo ya dunia.Katika hali hii tunahitaji nguvu mpya,uzima mpya (Isaya 40:28-31). Anayefanya kazi hii pia ni Roho Mtakatifu,Roho wa uzima (Warumi 8:2). Pepo wa udhaifu wanatolewa kwa Roho wa Mungu (Mathayo12:28), na vivyo hivyo udhaifu wetu kiroho unatolewa na Roho wa Mungu.Je umezimia kiroho,Mwambie Roho Mtakatifu akuzindue,naye atafanya.

4. ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO
Baada ya kuokolewa,tunahitaji pia kutakaswa.Bila utakaso,tutajikuta bado hatuna ushindi dhidi ya dhambi za ndani katika mawazo,na moyoni,ingawa tayari tuna ushindi dhidi ya dhambi za kutenda. Dhambi za ndani ,ni kama hasira, wivu ,chuki, masengenyo, kugombania ukubwa,kiburi,majivuno,kutokusamehe,kinyongo,
kupenda udunia n.k.Hivi vinaweza vikaonekana kwa watu waliookoka ambao hawajatakaswa: Mawazo yasiyo ya ki Mungu (Mathayo 16:21-23),kugombania ukubwa (Luka 22:24-26;Mathayo 20:20-22,25-28; Marko 9:30-37),hasira (Mathayo 20:24) wivu, fitina, ugomvi (Marko 9:38-39;Luka 9:49-50; 1Wakorintho 3:3-5), faraka na matengano(1Wakorintho1:10-13),umimi(Mathayo 28:6-13), kutokusamehe (Mathayo 18:21-35), chuki,kushindwa kuvumilia maudhi,kushtakiana wapendwa mahakamani (Luka 9:51-56; 1Wakorintho 6:1-8); Warumi 7:15 n.k .Mambo haya huondolewa kwa utakaso.

Monday, April 28, 2014

Ni Nani Walikuwa Waandishi Wa Qur,aan Tukufu Wakati Wa Mtume Saw?



KORAN HAIKUTEREMSHWA KUTOKA KWA ALLAH

Je, ungependa kuwafahamu waandishi wa Koran?
Katika somo letu la leo, tutajifunza kuhusu waandishi wa Koran. Je, ni kweli Koran ilishushwa? Je, kuna ushaidi wa kutosha wa kusaidia madai ya kuteremshwa kwa Koran?
Unaposema kuwa Allah ndie mwandishi wa Qur'ani, ni uongo mkubwa sana  na wengi wameukubali huu uongo na udanganyifu kwamba eti Koran ilishushwa wakatia inafahamika kuwa iliandikwa miaka 1400AD.
Mtu mwenye fikra anaweza kusema bila ya wasiwasi kuwa Qur'ani iliandikwa na watu kadhaa ambao wanajulikana kimajina. Waandishi Mashuhuri zaidi miongoni mwao ni hawa hapa:
Imrul Qays-mshairi: wa kale wa Arabia ambaye alifariki miaka michache kabla ya kuzaliwa Muhammad
Zayd b. Amr b. Naufal:-'lililopotoka' wa wakati wake ambaye alihubiri na kupandwa Hanifism
Labid:-mshairi mwingine
Hasan b. Thabit:-mshairi rasmi wa Muhammad
Salman: – Mshauri wa Kiajemi wa Muhammad
Bahira:-Nestoraian Mkristo mtawa wa Kanisa huko Syria
Jabr:-Jirani wa Kikristo wa Muhammad
Ibn Qumta:-Mtumwa wa Kikristo
Khadija:-Mke wa kwanza wa Muhammad
Binamu Waraqa:- Ndugu ya Khadija
Ubay b. Katibu Ka'ab;-Muhammad na Mwandishi wake
Muhammad: – Mwenyewe
Hapa chini, nitaandika historia fupi ya baadhi ya waandishi wa Koran. Nitaanza na Bahira ambaye alikuwa ni Mtawa wa Kikrito.
Bahira
        Bahira alikuwa Mtawa wa Kikristo wa Nestorian aliyeishi katika Sham (Syria). Jina lake la Kikristo lilikuwa Sergio Georgius. Inaaminika kwamba alifukuzwa kutoka utawa baada ya makosa.
Katika mji wa Makkah, alikutana na Muhammad, akawa karibu sana na yeye na kukaa pamoja naye. Yeye alikuwa na mazungumzo ya siri na Muhammad, ambayo yeye hakika alimwambia Muhammad  mambo mengi ya Ukristo. Aya kadhaa katika Qur'an zinazozungumzia Ukristo zilitoka kwa huyu Mtawa Bahira.
Mfano, aya zote za ndani ya Kuran zinazozungumzia kitabu cha Zaburi zilihaririwa na huyu Mtawa Bahira:
4.163 Hakika Sisi tumekuletea wahyi wewe kama tulivyo wapelekea wahyi Nuhu na Manabii walio kuwa baada yake. Na tulimpelekea wahyi Ibrahim na Ismail na Is-haka na Yaakub na wajukuu zake, na Isa na Ayub na Yunus na Harun na Suleiman, na Daud tukampa Zaburi.
17: 55. Na Mola wako Mlezi anawajua vilivyo waliomo mbinguni na katika ardhi. Na hakika tumewafadhilisha baadhi ya Manabii kuliko wengine; na Daudi tulimpa Zaburi. 
21:105. Na hakika tulikwisha andika katika Zaburi baada ya Kumbukumbu, ya kwamba nchi watairithi waja wangu walio wema. 
2:113. Na Mayahudi husema: Wakristo hawana lao jambo. Na Wakristo husema: Mayahudi hawana lao jambo. Na ilhali wote wanasoma Kitabu hicho hicho (Biblia). Na kadhaalika walisema wale wasio jua kitu mfano wa kauli yao hii. Basi Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyo kuwa wakikhitilafiana. 

2: 139. Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu. 
3: 23. Huwaoni wale walio pewa sehemu ya Kitabu? Wanaitwa kukiendea Kitabu cha Mwenyezi Mungu ili kiwahukumu baina yao; kisha baadhi yao wanageuka wanakikataa. 
*** Quran haina chochote cha zaidi au bora kuliko vitabu vingine. Qur'an, imeandikwa kwa kuibia, kugezea, kupora, kudanganya na / au kupotosha kutoka BIBLIA, kuhalalisha kwamba Watu wa Kitabu wamwamini au kutumia kama mwongozo. ***
Jabr:
Kamusi ya Uislamu (Hughes Kamusi ya Uislamu, p.223) inasema kwamba Jabir alikuwa mmoja wa Ahlu-l-Kitab (Watu wa Kitabu) na alikuwa amesoma vizuri vitabu vya Taurati na Injil (Injili), na hivyo, Muhammad akamtumia sana Jabr katika uandishi wa Quran. Jabr ndiye aliye kuwa anamsomea Taurat na Injil Muhammad kila alipo pita nyumbani kwake. Muhammad alijifunza kutoka kwa Jabr na kuweka Sura katika Quran yenye mahusiano na Wakristo na Wayahudi. Mistari yote inayo mhusu Daudi na Sulemani ilitengenezwa na huyu Jabr. Baadhi ya aya hizo:
Daudi akamuuwa Jaluti ... 2:251
Zaburi alipewa Daudi ... 4:163
Allah ni mbaguzi ; anapendelea baadhi ya Mitume kwa wengine; aliwapa Zaburi Daudi ... 17:55
Allah alishuhudia hukumu ya Daudi na Sulemani ... 21:78
Allah kampa Sulemani uelewo sahihi ; Yeye alifanya milima na ndege kumtumikia Daudi ... 21:79
Allah kamfundisha Daudi ujuzi wa kufanya vita ... 21:80
Kabla ya Qur'an , Mwenyezi ujumbe katika Zaburi ya Daudi ... 21:105
Allahu kampa maarifa ya Daudi na Sulemani ... 27:15
Baba wa Sulemani alikuwa ni Daudi. Sulemani alikuwa mrithi wa Daudi; Suleiman kueleweka hotuba ya ndege wanyama, na mimea ... 27:16
Sulemani alikuwa na mamlaka juu ya majini ; majini na ndege kupigana katika jeshi la Sulemani ... 27:17
Allah kaweka milima chini ya amri ya Daudi; akamfundisha jinsi ya kufanya silaha kutoka chuma ... 34:10-11
Allah alikuwa na kaweka milima , ndege kwa ajili ya huduma ya Daudi na majaliwa yake kwa hekima na mantiki ... 38:18-20
Allah kusamehe dhambi ya Daudi ... 38:25
Allah alimteua Daudi kuwa mtawala juu ya nchi na akampa mamlaka ya kutoa hukumu ya haki na sheria za Mungu na kwa maoni yake binafsi ... 38:26
*** Bila shaka, hadithi/aya zote hapo juu si kutoka BIBLIA lakini walikuwa wamekopia/wamigizia/wameangalizia na kupotosha mafundisho ya baadaye ya Wayahudi na Wakristo ***
Ibn Qumta
       Ibn Qumta alikuwa mtumwa wa Kikristo ambaye aliishi katika mji wa Makkah . Muhammad alijifunza kuhusu injili apocryphal ya Ukristo (kama vile : Injili ya Utoto na Injili ya Barnabas ) kutoka kwake. Sura nzima juu ya Maria na kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Sura 19) kiliandikwa na mtumwa huyu wa Kikristo.
       Vyanzo kutoka Wakidi , Alphonso Mingana , katika insha yake , Maambukizi ya Koran, Chimbuko la Koran, p.103 , anaandika:
' Mwanahistoria wa kale zaidi, Wakidi , ina sentensi zifuatazo ambazo zilipendekeza na ' Abdallah b. Sad b. Abi Sarh , na mtumwa Mkristo, bin Qumta , walikuwa na kitu cha kufanya katika Koran.
Na bin Abi Sarh akarudi na kusema kwa Makureshi : "Ilikuwa tu Mtumwa wa Kikristo ambaye alikuwa akimfundisha yeye ( Muhammad ); Nilikuwa na kazi ya kuandika na kubadili chochote alichoa taka Mtume Muhammad. " '
       Tafadhali kumbuka kwamba Abdallah b. Sad b Abi Sarh alikuwa mwandishi mwaminifu wa Muhammad. Wakati Muhammad anahamia Madina Abdallah na yeye alimfuata. Kila Muhammad alipo kuwa katika maono Abdallah ndiye aliye kuwa mwandishi wa hayo maono. Wakati Abdallah alipendekeza baadhi ya mabadiliko ya Muhammad lisping, Muhammad alikubali kirahisi. Mfano ni wakati Muhammad alikuwa anasema hii aya 23:12-14 .
23.12 Na sisi tulimuumba Mtu kutoka Udongo;
23.13 Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti
23. Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.!
Hii hapa ni orodha fupi ya baadhi ya aya katika Qur'an ambazo Muhammad alinakili/ ilibia kutoka vitabu au nakala za Wakristo, Wayahudi, Waarmenia, Wahindu na Majusi (Wazoroastro):
Tayammum ( 04:43 ): Kunakiliwa kutoka kwenye maandiko ya Kiyahudi Talmud.
Kinga ya maisha ndani ya ndege (2:260 , 3:49 , 5:110): Kunakiliwa kutoka vitabu Coptic .
Houris , Azazil (44:54 ): kujifunza kutoka kwa wageni katika Makkah.
Harut amd Marut (2:102 ): Kutoka Muarmeni -vitabu Harut na Marut ni katika udhibiti wa upepo na mvua.
Kiti cha enzi ya Mwenyezi Mungu juu ya maji (11:07 ): Kutoka mapokeo ya Wayahudi
Malik, mtawala wa Jahannamu (43:77): Kutoka Wayahudi. [ Moleki - Mambo ya Walawi 18.21 ; 20.2/3/4/5 , nk]
7 Mbinguni (2:29, 41:12) : Iliyopitishwa kutoka katika maandiko Sanskrit ya Wahindu.
Mariamu kujifungua chini ya shina la mti ( 19:23 ): Kunakiliwa kutoka Injili ya Utoto , apocryphal Mkristo Injili
Mtoto Yesu kuzungumza ( 3:46 , 19:30-31 , 19:33 ): Kunakiliwa kutoka Injili ya Utoto .
Maelezo ya peponi na Kuzimu (kuna aya nyingi - tazama sehemu ya Salman, Kiajemi: Kunakiliwa kutoka Majusi ( Wazoroastro ) na Wahindu.
Yesu si kuuawa , Mwenyezi Mungu akainua Yesu ( 3:55 , 4:157-158 ): Kunakiliwa kutoka Injili ya Barnabas
Hadithi ya Yusufu (Sura 12): Kunakiliwa kutoka Midrash, maandiko ya Kiyahudi.
Hadithi ya Sulemani na Sheba ( 21:78-82 , 27:17-19 , 27:22-23 ): Kunakiliwa kutoka Haggada , Maandiko Wayahudi. [ Wafalme mimi 10.1 ]
Qur'ani ya awali ni agizo katika Mbinguni ( 43:4 , 85:21-22 ): Talmud anasema kuwa Torati ni kibao katika ulinzi wa Mbinguni.
Malaika wa kifo - Azrail au Azazil , Malaku'l Maut ( 6:61 , 7:37, 32:11 ): Iliyopitishwa kutoka Wayahudi na mchawi maandiko ( Zoroastrian ).
WAPAGANI WANASEMA QURAN NI SAWA NA HADITHI ZA KALE
Hapa ni ushahidi wa baadhi ya mistari ya kuchaguliwa kutoka Quran kutuambia kwamba wapagani walikuwa na ufahamu kwamba Muhammad alikuwa anawaambia hadithi ya kale walizokuwa wamesikia kabla ya-Muhammad:
Wasioamini walisema kuwa Quran ni kama hadithi za watu wa kale wa Kipagani ... 08:31
Wasioamini walisema kwamba Aya za Muhammad zilinakiliwa kutoka hadithi za kale ... 16:24
Wapagani wengi walishasiikia hadithi za ufufuo kutoka katika hadithi zamani za Kipagani... 23:83
Makafiri walisema kuwa 'Qur'ani ni hadithi za kale ambazo walisikia kabla ya Muhammad' ... 25:5
Wasioamini walisisitiza kwamba Qur'ani ni hadithi kutoka vitabu vya kale ... 27:68
Wakasema makafiri Quran imejaa visa vya watu wa kale ... 46:17
Wasioamini wanaliziita na kuzifananisha aya za Muhammad na hadithi za kale ... 68:15
HITIMISHO
       'Quran' si maandishi ya Mwenyezi Mungu. Mungu mwenye Hekima hawezi kuandika Kitabu chenye Makosa, Utata, kujirudiarudia , makosa ya kimaandiko kama yalivyo jaa kwenye Qur'an yenye muongozo potofu kwa Mwanadamu.
       Anomalies zote, utata , MAKOSA YA KIMAANDIKO, upayukaji , KUJIRUDIARUDIA , makosa ya kisarufi na kilugha, Makosa ya Kihistoria, TABIA YA KUPENDEKEZA MAUAJI, HATEMONGERING , WARMONGERING , UBAGUZI , ubaguzi wa rangi na sifa nyingine za mapepo ya Quran kutakufanya kwa urahisi uelewe kuwa Koran si Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtakatifu aliye jaa huruma na rehema angeweza kuandika kitabu cha kishetani kama Qur'an kwa Muhammad .
       Inafahamika na wenye Hekima kuwa Muhammad ambaye anadai eti kapewa Koran ni uongo wa wazi kabisa na ndio maana Muhammad akasema alipewa maono na Allah ili kuwafunga Mdomo wale wote ambao wanatia shaka katika Kitabu chake.
       Qur'an Nzima ni Maandishi ya Muhammad na imejaa matakwa na fikra zake.
                                       Alter ego
       Katika hali halisi, Muhammad, Jibril na Allah ni Mtu mmoja.
Muhammad
       Ilikuwa ni Muhammad ndiye aliye anzisha Uislam na baadaye baadhi ya wafuasi wake ambao, 'Kwa jina la Allah' walitengeneza Qur'ani kwa kurekebisha , kurekebisha na kuibia kutoka maandiko mbalimbali na mila ya watu wengine wa wakati huo.
       Wafuasi wake waliendelea kutangaza huu udanganyifu wa Muhammad na kuusambaza katika fahamu za binadamu, ili kupata matakwa yao ya  kisiasa yenye nia ya kutawala peninsula ya Arabia na baadaye, nchi nyingine za amani.
Koran si Kitabu cha Mungu bali ni maandishi ya Muhammad na marafiki zake.
Katika huduma yake.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

Copyright © Max Shimba Ministries 2013

Saturday, April 26, 2014

UTATA WA ALLAH KATIKA KUSAMEHE WATU DHAMBI

Je, Allah anao uwezo wa Kusamehe watu dhambi?
Ndugu zanguni,
Leo ningependa tumuangalie Allah wa dini ya Uislam ambaye wanasema ndie Mungu wao. Je, huyu Allah anayo mamlaka ya kusamehe dhambi zote?
Ungana nami katika some letu la leo na tuone utata mkubwa sana uliopo ndani ya dini ya Uislam.
Tuanze na Surat Azzumar aya 53 na 54 ambazo zinadai na kusema kuwa, Allah anasamehe dhambi zote, hebu tusome kwanza:
Surat Azzumar 53. Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. 54. Na rejeeni kwa Mola wenu Mlezi, na silimuni kwake, kabla ya kukujieni adhabu. Kisha hapo hamtanusuriwa.
Katika aya hizo hapo juu, tumesoma kuwa Allah anasamehe dhambi zote na labda tukubaliane naye kwasasa kwa ajili ya kujifunza Utata na Mashaka yalio ndani ya kitaa'b cha Allah.
SASA TUANAGALIE VIFUNGU VINGINE AMBAVYO ALLAH ANASEMA KUWA, HANA UWEZO WA KUSAMEHE DHAMBI
Sasa rejea katika Surat Al I'mran: 86.Mwenyezi Mungu atawaongoaje watu walio kufuru baada ya kuamini kwao, na wakashuhudia ya kuwa Mtume huyu ni wa haki, na zikawafikia hoja zilizo wazi? Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu. 87. Hao malipo yao ni kuwa ipo juu yao laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika na ya watu wote. 88. Humo watadumu. Hawatapunguziwa adhabu wala hawatapewa nafasi. 89. Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu. 90. Hakika wale walio kufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, toba yao haitakubaliwa, na hao ndio walio potea. 91. Hakika wale walio kufuru, na wakafa hali ni makafiri haitakubaliwa kutoka kwa yeyote wao fidia ya dhahabu ya kujaza dunia nzima lau wangeli itoa. Hao watapata adhabu chungu, wala hawatakuwa na wa kuwanusuru.
Kifungu cha hapo juu kinatoa habari inayo changanya na kuweka shaka kubwa sana: Swali la kwanza nauliza kwa kejeli, "Je, Allah atawaongoaje watu ambao ..." na alisema jibu kwamba Allah hawaongoi watu hao. Kinyume chake ni kwamba, kwa mujibu wa aya hizi laana ya Allah itakaa kwa wale walio amini, ambao walikuwa Waislamu, lakini baadae waligeuka na kufuata imani zingine. Na Allah anasema kuwa wao waliongezwa na watakuwa huko kwenye laana na hata waongoa "kukaa humo," "makao yao ni humo milele" (mstari 88), ambayo kulingana na baadhi ya wafasiri wa Kiislamu inahusu makafiri na Waislam walio mpokea Yesu kuwa watadumu katika Jahannamu :
Hebu tusome tafsir nyingine ya Surat Al I'mran 88. Laana hiyo haitowabanduka, wala hawatapunguziwa adhabu, wala hawapewi muhula.
Hii aya inatuambia kuwa, hao Makafir hata wakiomba msamaha na kuamua kumfuata Allah, yeye hato wasamehe maana Allah alisha fanya maamuzi kuwa Makafir hata wakubali kumfuata Allah hato wasamehe. Lakini Waislam wao wana nafasi nyingine maana laana kwao inaweza kuwabanduka na Allah atawapunguzia adhabu na muhula wao wa kukaa Jehannam utatolewa.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW