Thursday, July 30, 2015

JE, ISA BIN MARYAM NDIYE YESU KRISTO?



 Utangulizi

SHALOM TENA,

Kwa mara nyingine twamshukuru Yehova Mungu kwa kutupa neema hii tena ili tuweze kukufikishia ujumbe huu wa Biblia na kweli zake.

Kwa muda wa miaka mingi sana pia duniani pote imekuwa ni kawaida kuwasikia waislamu wakifundisha watu wao na kuwadanganya bila ya wao kujuwa ao wengine wakiwa wanakijuwa wanachokifanya kuwa ISA bin Maryam’ Kama Qurani inavyofundisha ndiye “YESU KRISTO”.

Mafundisho haya hivi sasa yanaendeshwa kwa kulinganisha aya za Biblia na Qurani. Ma sheihk, ma Imam na wahubiri wengi wa dini ya kiislamu wanaendesha mihadhara kwa uwingi duniani. Wahadhiri hao pia hutumia mbinu zingine mbali-mbali kama majarida na kurekodi kanda za audio na video, ambazo zimesababisha baadhi ya wakristo nusu au wakristo wajinga waamini kuwa Isa Bin Maryamu ndiye Yesu Kristo. Swali la msingi kwa wakristo wote;Je, ni kweli Isa bin Maryam ndiye Yesu Kristo?

Nakusihi kwa jina lake Bwana wetu Yesu Kristo kufuatilia somo hili kwa umakini wote kama tulivyokuahidi katika lile somo ambalo lilitangulia wiki jana.

SEHEMU KUU ZA SOMO HILI

1. Madai yanayotumika na waislamu kusema Isa ndiye Yesu

2. Je, mama wa Isa ndiye wa Yesu?
3. Maana ya jina Isa
4. Maana ya jina Yesu
5. Je, kuzaliwa kwa Yesu ni sawa na Isa?
6. Je, Isa bin Mariamu ni mwana wa Mungu?
7. Je, mamlaka ya Isa na Yesu ni sawa?
8. Ikiwa Yesu ndiye Isa je, Isa.
9. Ujue umuhimu wa kumwamini Bwana Yesu

1.  Kisingizio N0.1
Waislamu husema Isa ndiye Yesu
Qr.3 au surat I’mran 45
(Kumbukeni) waliposem malaika. ‘Ewe Maryamu Mwenyezi Mungu anakupa habari njema za (kumzaa moto bila mume bali hali kwa kutamka) Neno tu litokalo kwake (la kumwambia zaa ukazaa pasina kuingiliwa) jina lake ni Masihi Isa mwana Maryamu, mwenye hishima kaitka dunia na ahera na miongoni mwa waliopelekwa mbele na Mwenyezi Mungu.
Marko 6:3-4, Huyo si Yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake. Yesu akawaambia ‘Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake na nyumbani mwake.
Hapa Waislamu wanasema kana vile Qurani inavyofundisha jina la mama wa Isa ni Mariamu kadhalika Biblia inafundisha jina la mamake Yesu ni Mariamu. Hivyo wanasema kuwa Yesu ndiye Isa.
Soma pia Mathayo 1: 18-21 na Yohana 2:1.
2. Kisingizio N0.2
Isa ni Mtume wa Allah kwa Waisraeli
Qr. 4 au surat An-Nisaai 171
Enyi watu wa kitabu misipindukie mipaka katika dini yenu, wala msiseme juu ya Mwenyezi Mungu ila yaliyo kweli. Masihi Isa bin Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu…
Hapa tunaona kuwa Qurani imemtaja Isa kuwa ni ntume, je, mtume kwa akina nani? Endelea kusoma aya hizi katika Qurani:
Qr.  61 au surat Ass’af 6
Na Isa bin Maryamu aliposema: enyi wana wa Israili! Mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu kaitka Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakeayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad…
Soma pia katika Qr. 3 au surat Al I’mran 49:
Ayah ii inathibitisha kuwa Isa ni mtume kwa Waisraeli. Je, Yesu ni mtume kwa akina nani? Waislamu wanaoendesha mihadhra pia husoma aya hizi za Biblia.
Waebrania 3:1Kwa hiyo ndugu watakatifu wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtakafarini sana mtume na kuhani mkuu wa maungamo yetu Yesu.
Mathayo 15:24Akajibu, akasema, ‘Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Kwa hivyo kama Qurani inavyofundisha kuwa Isa mwana wa Maryamu ni mtume kwa Waisreali ndivyo Biblia inafundisha kuwa Yesu ni mtume kwa waisraeli hivyo basi Isa ndiye Yesu. Hapa ndipo wahadhiri wa dini ya Uislamu wanavyoifundisha na kuwashika mateka na jamii za wakristo-nusu. Je, madai haya ni sahihi? Biblia itatusaidia kujibu huko mbele.
3. Kisingizio N0.3
Isa bin Maryamu alifanya miujiza
Qr. 5 au surat Al Maida 110
Na pale Mwenyezi Mungu atakaposema, Ewe Isa mwana wa Maryamu kumbuka neema yangu juu yako na juu ya mama yako. Nilipokutia nguvu kwa Roho takatifu (Jibrili), ukazumgumza na watu katika utoto (wako) na katika utuuzima (wako). Na nilipokufundisha kuandika na hikima na Torati na Injili na ulipotengeneza kwa undongo sura za ndege kwa idhini yangu, na ulipo waponesha vipofu na wenye ukoma kwa idhini yangu, na ulipowafufua (baadhi ya) wafu (makaburi mwao) kwa idhini yangu, na nilipokuzuilia wana wa Israeli (wasikudhuru) ulipowafikia kwa joha zilizo wazi; wale walio kufuru miongoni mwao wakasema: Haya si chochote ila ni uchawi dhahiri
Waislamu wanasem huu ni ushahidi wakutosha kwani Allah anasema Isa alifanya miujuza mingi hii.
Isa aliponyesha vipovu ndiye Yesu aliponyesha vipovu Mk 10:46-52, aliyewafufua wafu makaburi ndiye Yesu aliyewafufua pia huu upande, Mk 5:21-43 na aliyewaponyesha wenye ukoma ndiye…Yesu aliponya Ukima  Luka17:1
Walimu wa kiislamu hao wanasema kama vile Qurani invyosimulia kuwa Isa amefanya miujiza mingi, ndiyo Biblia inavyofundisha hivyo Yesu ndiye Isa, isitoshe wanasema hivi pia:
Isa ibin Maryamu ni Nabii, Quran suratul 4:171, kadhalika Biblia inafundisha kuwa Yesu ni Nabii, Yohana 6:14Yohan 7:40Luka 13:3324:19Marko 6:4, na Mathayo 13:57.
Kulingana na watafiti wa Biblia imeelezwa kuwa imerikodiwa kwamba Yesu ni Nabii mara 12. Vile vile wahadhiri wa Kiislamu wanafundisha ya kwamba Isa ni Neno la Kiarabu, katika kiingreza Jesus na kwa Kiswahili ni Yesu. Kupitia ushawishi huu wamara kwa mara baadhi ya Wakristo wameshawishika kuamini kuwa Isa ndiye Yesu. Lakini, lazima tuzichunguze hizi hoja moja kwa moja ili tujue ukweli.

          4. TUFANYE UCHUNGUZI PAMOJA
 
1. Je, Mama wa Isa ndiye yule wa Yesu Kristo?

VIOJA VYA UISLAM KUHUSU KIFO NA KUFUFUKA WAKATI WA KIYAMA

1. Eti Binadamu asili yake ni MBEGU YA "Ajabu Dhanab"
2. Eti Siku ya Kiyama Allah atanyeshea Mvua Ajab Dhanad na itafufuka tena.

Ndugu Msomaji, ebu jiunge nami leo na jifunze kuhusu Sayansi dhaif ya Allah na Muhammad.


MTU ANAPOKUFA, ZILE ASILI TATU KILA MOJA INARUDI MAHALA PAKE PA ASILI
Kwa kifo, udongo ambao kwao ndio mwili ulijengeka, unarudi mahala pake pa asili napo ni ardhini.
Mwenyezi Mungu anasema:
"Kwa hakika tunajua kiasi cha kila kinachopunguzwa na ardhi katika miili yao (wakati wanapooza huko makaburini) Na kwetu kiko kitabu kinachohifadhi (kila kitu)".
Qaf -4

AJABU DHANAB- ETI BINADAMU NDIO KATOKEA HAPO
Kinachobaki katika mwili wa mwanadamu ni kitu kidogo kinachoitwa "Ajabu dhanab" (kilichoingia pamoja na mbegu). Hii ni sehemu ambayo ndani yake mtu aliumbiwa, na kitu hiki asili yake kilikuwa katika uti wa mgongo wa Baba yetu Adamu(AS), kwa vile kitu hiki ni kidogo sana (Hakiwezi kuonekana ila kwa kutumia microscope zenye nguvu sana), ndiyo maana uti wa mgongo wa Baba yetu Adamu(AS) uliweza kuzibeba asili hizi zote za wanawe.
Na sehemu hii iitwayo "Ajabu dhanab" haiozi wala haivurugiki.
Mtume(SAW) amesema:-
<<Mwili wote wa mwanaadamu unaoza isipokuwa "Ajabu dhanab", kutokana nayo ameumbwa na kutokana nayo atakusanywa tena >>.
Bukhari – Muslim – An Nasai, Malik katika Muwata a na Abu Daud.

Ama Roho itarudi mahali anapopataka Mwenyezi Mungu (katika Barzakh) mpaka Siku ya Kiama.

SIKU YA KUFUFULIWA ZILE SEHEMU TATU ZINAKUSANYIKA TENA
Unapofika wakati wa kufufuliwa, Mwenyezi Mungu atateremsha mvua na kuifanya ile mbegu isiyooza "AJABU DHANAB”, imee tena.

Mtume (SAW) amesema:-
<<Kisha inateremshwa mvua na watamea kama imeavyo mboga, na hapana katika mwili wa mwanadamu kisicholiwa na ardhi isipokuwa fupa moja nalo ni "Ajabu dhanab" ndani yake humo watakusanywa viumbe Siku ya Kiama>>.
(Bukhari, Muslim, Imam Malik, Abu Daud na AnNasaiy)

Yaliyofanana na haya yanatokea duniani kila siku. Panapotokea ukame, tunaona miti ikianguka na kufa (na kutoweka). Hauonekani mti wowote wala mmea. Lakini Mwenyezi Mungu amejaalia ndani ya ardhi au ndani ya mawe kuwemo mbegu, na mbegu hizo hazionekani kwa macho, isipokuwa mvua inaponyesha ndipo hupasuka na kuchipua miti na mimea mbali mbali.

Mwenyezi Mungu anasema:-
"Hukitoa kilicho hai katika kilichokufa na hukitoa kilicho kufa katika kilicho hai na huihuisha ardhi baada ya kufa kwake na hivyo ndivyo mtakavyofufuliwa".
(Al - Rum - 19).
Mtu mmoja alimuuliza Mtume (SAW):-
"Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, namna gani MwenyeziMungu atawarudisha tena viumbe, na nini dalili yake?” 

 Mtume (SAW) akamjibu;
"Uliwahi kupita bondeni kijijini kwenu wakati wa ukame (miti yote ikiwa imekufa), kisha ukapita tena wakati miti (imeota tena na) imejaa na ardhi ikageuka (na kuwa) rangi ya kijani?
Akasema:- "Naam".
Mtume(SAW) akamjibu:
"Basi hiyo ndiyo dalili ya Mwenyezi Mungu katika kuumba kwake na hivyo ndivyo atakavyowafufuwa wafu".
(Imam Ahmad )

(Siku ya Kiama), Pale Ajab dhanab itakapochipua na kutoka ndani ya ardhi na mwili ukarudi tena, ndipo zitakapokuja roho na kuingia kila moja katika mwili wake.
Ndio sababu Mwenyezi Mungu akasema:
"Na nafsi zitakapounganishwa (na viwiliwili vyake)."
(At - Takwiyr - 7)
Na hivi ndivyo watakavyorudi viumbe mara ya pili kama walivyoanzishwa hapo mwanzo.

Mwenyezi Mungu anasema:-
"Kama tulivyoanza umbo la awali tutalirudisha tena, ni ahadi ilio juu yetu, bila shaka sisi ni wenye kufanya (tusemavyo).”
(Al - Anbiyaa -104).

Ndugu msomaji, hivi ni kweli Allah wa hii dini ya Kiislam aliumba? Mbona hii imani imejaa shaka na utata kila kona?

Leo Allah kesha jisahau na kusema kuwa eti wewe umetoka katika Ajabu Dhanab na sio tena vumbi.

UHAKIKA WA UFUFUO WA WAFU KWA WAKRISTO

Wednesday, July 29, 2015

YESU YUPO NA ANAKUJUA HATA JINA LAKO

Yesu ni wa kweli, anajua jina lako na kila kitu kinacho kuhusu, pia anakupenda. Hayuko mbali nawe, yuko karibu nawe, anataka ujue kuwa yupo, anaishi, na anataka kukusaidia ikiwa utapenda. Na kama utapenda kumfahamu, unaweza kumfahamu. Ikiwa utahitaji msaada, atakusaidia, kama utaongea nae atakusilikiza, naye ataongea nawe pia.

Yesu ndiye aliyekufanya usome maandishi haya, kwa sababu ametuambia tukuandikie, na amehakikisha kuwa yamekufikia. Anajua kila kitu kinachokuhusu tangu mwanzo wa maisha yako hadi sasa hivi, amejumuika nawe katika huzuni, madhaifu na hata matatizo yako, atakusaidia mara tu utakapo muhitaji. Hakutaka uwe peke yako, mara nyingi ametaka umjue yeye. Ndiyo maana amekufanya kuwa rafiki kwa makusudi hayo. Mwamini yesu, kwani kwa Yesu urafiki ni mzuri tena wa kweli, isitoshe ni wa upendo ule wa ndani. Hatokuacha kamwe, unachotakiwa kufanya ni kumwamini na uongee nae yeye Yesu, naye atakujibu, atakusaidia, na ndipo utakapomfahamu Yesu. Anakutazama sasa unaposoma maandishi haya na amejaa upendo juu yako.

Imeandikwa kuwa, Yesu alikuja duniani, akafa, akatoa uhai wake kwa ajili yetu. Hii inaonyesha kuwa kifo kilikuwa ni cha lazima, ili kulipa deni la dhambi zetu. Kwa nini alichagua kulipa deni la dhambi kwa njia ya kifo? Ni kwa sababu anakupenda sana!

KAFARA: BABA KAMA MTOTO
Hakuna mtu mwingine katika historia ya dunia hii bali Yesu tu. Hakuwa mdhambi, dhambi ilikuwa kwa wengine. Dhambi zote zinakuja zenyewe kwa namna moja ama nyingine alionekana mnyenyekevu. Baba wa mbinguni alituumba ili tupendane sisi kwa sisi, na pia tumpemde yeye, lakini dhambi imekuwa kinyume na upendo huo na imechukua nafasi kubwa katika maisha yetu, hata kusababisha kifo. Hata hivyo, kifo ndio kimekuwa malipo makuu ya dhambi. Dhambi inatembea kutoka kwa mtu mmoja. Kwenda kwa mwingine, nchi moja kwenda nyingine, na inaleta maumivu kwa kila mtu, na ndiyo maana inawatenganisha wanadamu wote na Mungu, na inawapeleka kuzimu. Mungu hatokubali dhambi iingie Mbinguni, na mbingu ziwe kama dunia ilivyo hivi sasa, imejaa maovu na kujiona zaidi. Kwa miaka mingi Mungu aliruhusu wanyama wafe. Kwa njia hiyo wanadamu walikuwa na mahusiano ya karibu zaidi na Mungu wao mpendwa na waliongea nae. Aliwapenda na kuongea nao pia, kwa mfano, Abrahamu, Ayubu, Adamu na wengine wengi. Mungu anataka uhusiano huo leo kwako, lakini hutaki kujitolea kafara wanyama ili kuwa nae.

HEKIMA ZA MWANADAMU
Mwanadamu amejaribu kuwa na ukaribu na Mungu kwa kupitia njia mbali mbali, lakini si kwa njia ile ambayo Mungu alitegemea kutoka kwao. Kaini mtoto wa Adamu alitoa kafara ya mazao yake badala ya mnyama. Hata hivyo, Mungu hakupokea kafara ya Kaini kwa sababu haikuwa na thamani sawa na dhambi iliyokuwa ndani yake. Haijarishi Kaini alikuwa na mawazo mazuri au mabaya juu ya Mungu, bali kafar yake haikuwa na thamani ya kulipa deni la dhambi.

Ukweli ni kwamba watu bado hawajajua dhambi. Kwetu dhambi imekuwa ni neno la kidini. Wengi hawajajua kwa nini jambo lifanyike kwa ajili ya dhambi. Lakini Mungu ameona ni jinsi imekuwa ya kuume na ya kipekee tena yenye nguvu. Na jinsi ambavyo inaleta shida na masumbufu ndani yetu. Huko mbinguni kama siyo dhambi, tungeweza kuonana na Yesu uso kwa uso, tungekuwa huru kutoka dhambini na kuwa huru wenye nguvu zaidi na zaidi, pia tungekuwa mahali ambapo kila mtu awaye binadamu, au
malaika, au kiroho, angependa kuwepo. Wote tungependana na Mungu angeishi maisha ya upendo kwa wengine na siyo ya kibinafsi.

HEKIMA ZA MUNGU

Tuesday, July 28, 2015

Why Do Muslims Face The East When Praying?

Everyone looking towards the east, west, north and south may be looking towards the same direction but not the same geographical location.  

If the objective is to face Ka'aba, then everyone's east cannot be towards Ka'aba. For some it may be south east, North West etc.

Everyone on the same latitude as Ka'aba would be facing Ka'aba technically if they face east or west. Time would decrease as you head west from Ka'aba and fall again on the same line as you approach the eastern flank of Ka'aba.

For those on higher or lower longitude as Ka'aba, they can look east or west all they like and would not be facing (looking towards) Ka'aba.

Facing EAST ====>>                                                   <<==== Facing WEST
------------------------------------------
Now questions: (please see direction of arrows above)
#1. If a muslim in North America faces the direction of Mecca, is he or she facing EAST or WEST
#2. If another Muslim in Australia faces the direction of Mecca, is he or she facing WEST or EAST
#3. What about yet another Muslim in South Africa facing the direction of Mecca, is he or she facing NORTH, SOUTH, or EAST


Abu-DawudBook 1, Number  0010 
Narrated Ma'qil ibn AbuMa'qil al-Asadi: The Apostle of Allah (peace_be_upon_him) has
forbidden us to face the two qiblahs at the time of urination or excretion.

Abu-DawudBook 1, Number  0013
Narrated Jabir ibn Abdullah: The Prophet of Allah (peace_be_upon_him) forbade us to face
the qiblah at the time of making water. (that is, "urinating" - my note)
Then I saw him facing it (qiblah) urinating or easing himself one year before his death.

What are we to understand from these two records in your holy books??  Thank you.

Thursday, July 23, 2015

SABABU KUMI (10) KWANINI NAMPENDA YESU

1. YESU NI MCHUNGAJI MWEMA
Yohana 10: 10Mwivi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi imekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele. 11‘‘Mimi ndimi Mchungaji Mwema. Mchungaji Mwema huutoa uhai Wake kwa ajili ya kondoo.

Yesu ninae mpenda ni mwenye Mikono Wazi na yupo tayari kutupokea sote. Sote tumefanya makosa, lakini habari njema ya Ukombozi ni kuhusu Upendo wa Mungu kwetu sisi ambao tunaupata kutoka na kupitia Yesu Kristo ambaye ni Bwana na Mwokozi wa Maisha yangu. Karibu kwa Mchungaji Mwema ambaye ni Yesu Kristo aliye kufa Msalabani kwa ajili ya dhambi zako.

2. YESU ALIKUJA KUWASAIDIA WALIO LEMEWA NA MIZIGO AU MATATIZO YAO
Matayo 11: 28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.’’

Ukristo sio kuhusu kufanya sheria bali ni kupokea jibu ambalo Yesu alisha kujibu pale Msalabani. Hii ndio Raha ya kuwa na Yesu. Yesu alisha maliza matatizo yako yote pale Msalabani, alisha maliza au ponya Magonjwa yako yote. Ndio Maana Yesu anasema kwako kuwa, NJOONI NINYI NYOTE MLIO LEMEWA NA MIZIGO. Kitu ambacho unatakiwa kufanya ni kuja kwa Yesu, halafu yeye atakupa Majibu yako yote. Sasa njoo kwa Yesu na upokee majibu ya matatizo yako.

3. YESU AMEKUSAMEHE -UPENDO WA MUNGU
Zaburi 103: 2 Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA, wala usisahau wema wake, 3 akusamehe dhambi zako zote na kuponya magonjwa yako yote, Kumfahamu Yesu ni kujua kuwa Yesu alisha maliza kazi zote pale Msalabani, ikiwa pamoja na kukusamehe dhambi zako zote. Sasa basi, najua unasema kuwa labda ulifanya vitu vibaya hapo nyuma na unashindwa elewa kivipi Yesu atakusamehe dhambi zako. Ndugu msomaji, Yesu hajali nini umefanya hapo nyuma, Yesu anacho taka kutoka kwako ni kuwa, umkabidhi matatizo yako yoke na yeye alisha maliza kazi pale Msalabani. Sasa basi, mwambie Yesu kuwa wewe ni mwenye dhambi na omba msamaha na amini kuwa amesha kusikia na kukujibu/samehe. Yesu ni Mungu na Mungu wetu ni Upendo.

4. YESU NI UHURU
Warumi 8: 1. Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho. 2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti. 3 Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, Yeye aliihukumu dhambi katika mwili, 4ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.

Kuna Uhuru Mkubwa sana unapo kuwa ndani ya Yesu Kristo. Unapo mkabidhi Yesu maisha yako na kuwamchia yeye ayaendesha, basi unakuwa huru kabisa. Yesu ni Mungu, na yeye anampango mzuri sana kwa maisha yako. Hivyo basi, nakusihi uache kuwa mungu wa maisha yako na Mkabidhi Yesu maisha yako ili akuonyeshe nini cha kufanya. Anza maisha ya Kiroho na Yesu ambaye ndie muumba wako. (2 Wakorintho 5:19) Dhambi haina mamlaka juu yangu kwa sababu mimi sasa naishi chini ya neema. (Warumi 6:14) Neema ni msingi wangu na ukombozi katika Kristo. Neema ya Mungu sio leseni ya dhambi, ni nafasi ya kufanikiwa.

5. YESU NI HAKI YANGU
Warumi 5: 1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wokovu ni zawadi ya haki. (Warumi 5:17) Katika Ufalme wa Mungu, hakuna kufanya kazi ili kupata haki yako, bali haki yako ni zawaidi kutoka kwa Mungu. Dini zingine zinafundisha kuwa, wewe ufanye kazi na Mungu ndio nakupa haki yako, Katika UKRISTO, tunapokea zawadi ya Wokovu. Hivyo basi, elewa kuwa Yesu alisha kulipia kwa kupitia damu ya Msalaba. Nakukaribisha kwa Yesu aliye hai ambaye ni Mungu na amekupa haki ya kuwa Mwana wa Mungu kwa kupitia damu yake.

6. YESU NI FURAHA YANGU

Wednesday, July 22, 2015

YESU NI MUNGU AMBAYE ANAPONYA MAGONJWA YOTE

Yesu alisema kwamba ishara moja itakayofuatana na waaminio ni kwamba wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapona (ona Marko 16:18).
[Yesu] Akawaambia, Enendeni ulimwengu mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini atahukumiwa. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya (Marko 16:15-18).
Mtumishi afanyaye watu kuwa wanafunzi, akiwa anaiga huduma kamilifu ya Kristo, hakika atatumia vipawa vyake kuendeleza huduma ya uponyaji wa Mungu katika eneo lake la ushawishi. Anajua kwamba uponyaji wa Mungu hukuza ufalme wa Mungu kwa njia mbili. Kwanza – miujiza ya uponyaji ni matangazo mazuri sana kwa Injili, kama mtoto yeyote anayesoma Injili au kitabu cha Matendo atakavyoelewa (ingawa watumishi wengi wenye madigirii makubwa wanaonekana hawaelewi). Pili – wanafunzi wenye afya njema hawazuiwi kufanya huduma kwa magonjwa binafsi.
Pia, mtumishi anayefanya wengine kuwa wanafunzi anahitaji kuwa makini kwa wale katika mwili wa Kristo wanaohitaji uponyaji, ila wana shida ya kupokea. Mara nyingi wanahitaji mafundisho ya taratibu na kutiwa moyo kwa upole, hasa kama wamefikia mahali pa kupingana na ujumbe wowote wa uponyaji. Mtumishi anayefanya wengine kuwa wanafunzi anakabiliwa na uchaguzi: anaweza kuepuka kufundisha kuhusu uponyaji wa Mungu moja kwa moja. Akifanya hivyo, hakuna atakayekwazika wala hakuna atakayeponywa. Au, anaweza, kwa upendo sana, kufundisha somo hilo na kudiriki kuwakwaza wengine huku akiwsaidia wengine kupokea uponyaji. Mimi binafsi nimeamua kufanya la pili, nikiamini kwamba ni kufuata mfano wa Yesu.
Uponyaji Pale Msalabani
Mahali pazuri pa kuanza kujifunza kuhusu uponyaji wa Mungu ni katika sura ya hamsini na tatu ya kitabu cha Isaya, ambayo huhesabika kuwa unabii kuhusu Masiya. Kwa njia ya Roho Mtakatifu, Isaya anaeleza vizuri sana juu ya kifo cha Yesu cha kujitoa dhabihu na kazi ambayo angetimiza msalabani.

Tuesday, July 21, 2015

MPINGA KRISTO NI NANI?

1. Biblia inathibitisha kuwa ni Allah na Uislam
2. Quran inakiri kuwa Yesu si Mwana wa Mungu
3. Dini ya Uislam ni ya Mpinga Kristo

Ndugu Msomaji,
Leo nitawathibitishia kwa kutumia Biblia na Quran kuhusu nani ni Mpinga Kristo. Hebu tuanze kwa kusoam neno la Mungu.
WARAKA WA KWANZA WA YOHANA 4:1-6
Wapenzi msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho kwamba zimetokana na Mungu, kwa sababu manabii wa uongo wametokea duniani. Katika hili mwamjua Roho wa Mungu , kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya Mpinga Kristo, ambayo mmeisikia kwa yaja , na sasa imekwisha kuwako duniani, ninyi watoto wadogo mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndanii yenu ni mkuu kuliko yeye aliyeko katika dunia.hao ni wa dunia , kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia. Sisi twatokana na Mungu . yeye amjua Mungu atusikia na yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.

Kwanza: Biblia inatufundisha kuwa Mpinga Kristo ni yule ANAYEKATAA KUWA YESU KRISTO HAJAJA KATIKA MWILI…YANI SIYE MWANA WA MUNGU, Soma (2 Yohana 1:7) na hapa tunawaona Waisilamu ndiyo namba moja wa kukataa hilo, sasa je, ni nani ni Mpinga Kristo kama si nyinyi waislamu? Isitoshe bado mnakazania kuwa YESU SIYE KRISTO Kwa madai kuwa eti huyo Kristo ni wa Paulo, na hapo pia Biblia inatuthibitishia kuwa nyinyi waislamu ndiyo haswa ni Wapinga Kristo…tazama na uthibitishe mwenyewe kwenye (1 Yohana 2:22).

Sisi Wakristo lazima tufahamu kuwa Mpinga Kristo kwa mujibu wa Biblia ni yule anayekataa kuwa YESU KRISTO NI MWANA WA MUNGU ALIYESHUKA KATIKA MWILI ILI KUTUOKOA SISI WANADAMU HAPA DUNIANI…Huu ndiyo msingi wetu sisi Wakristo ambao Waislamu wote duniani wamefundishwa na mungu wao Allah kuupinga kabisa kabisa msingi huu…Sasa lazima tujiulize Mpinga Kristo haswa ni nani? Jibu ni rahisi mno ‘ALLAH NA DINI YAKE YA UISILAMU’.

Pili: Mtu yeyote ambaye hamwamini Bwana Yesu ya kuwa ni Bwana na Mwokozi wa maisha yake huyo tayari ni mpinga Kristo kwa sababu hana ushirika nayeye na wala hamuabudu yeye kabisa. Aliye hivyo huyo anaitwa Mpinga Kristo na ule mwisho Yesu akija kuhukumu ulimwengu hatawachukua hao wasiyo mwabudu yeye, na Nabii huyo Yesu wa Nazareti. Nabii huyu watu wanamjua ni nabii wa Mungu na ndiye atakayekuja kuhukumu ulimwengu siku ile ya kiama. Sasa kama hapa tu sasa hivi unampinga, je jiulize swali nayeye atakukubali uende naye uzimani alipo yeye? Jibu hatakuchukua na ameniambia niuambie ulimwengu wote atakaye sikia na asikie atakayekataa shauri lake. Wote wasiomwabudu yeye 100% ni wapingaji wa kumpinga Yesu Kristo na hao ni wapinga Kristo.

WAABUDU NYOTA, MWEZI, JUA NA SANAMU MWISHO WAO NI JEHANAMU.

KUTOKA 20:1 – 6 MUNGU akanaena maneno haya yote akasema, mimi ni Bwana, MUNGU wako niliyekutoa katika nchi ya Misri katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi. Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilichopo juu mbinguni, wala kilichopo duniani wala kilichopo majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia, kwa kuwa mimi BWANA MUNGU wako ni MUNGU mwenye wivu, nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukizao. Nami nawarehemu maelfu wanipendao, na kuzishika amri zangu. Ndugu msomaji wa makala haya ya Nabii Hebron, na uliyeumbwa na MUNGU tena umefanana na yeye, ni ili umwabudu yeye na kuzishika amri zake peke yake ili upone na ile siku ya mwisho na wewe ukafurahie pamoja na yeye paradiso ila ukienda kinyume na maagizo yake hakika ujijue 100% wewe hauta kwenda mbinguni hata kama unajifariji angalia matendo yako .

Ukisoma kutoka 20: 4 MUNGU anasema usije ukatengeneza sanamu yeyote halafu ukaitumia wakati wa kuomba, sanamu ya aina yeyote iwe ni ya mnyama, au mwanadamu kwa jinsia yeyote kike / kiume, wala kitu chochote kilichopo juu mbinguni (Nitaelezea hapa kidogo ili mpate kufunguka ufahamu na adui ambaye ndiye huyo miungu ya uongo asikupate tena. Biblia inasema na maneno haya ni MUNGU ndiye aliyeyasema na akatoa amri hii, usiabudu hata kitu kilichopo mbinguni). Sasa kuna watu baadhi yao wanaabudu mwezi,nyota, jua , hivi vipo juu ya nchi . Hii ni makosa na unaposhiriki tu , wewe tayari unakuwa unamwabudu MUNGU mwingine ambaye ni mungu wa uongo. MUNGU huyu ni kweli ndiye aliyeziumba hata hizo nyota, jua na mwezi. Na unapoviabudu au kuvisujudia matokeo yake na wewe unakuwa tayari umesha muasi MUNGU aliyekuumba wewe na ukaiacha njia yake ya kweli , ukaifuata ya uongo. Huyu ndiye MUNGU wa Ibrahimu, Isaka, Yakobo, na Eliya na ndiye aliyewaumba Adamu na Hawa pia ndiye Baba yake YESU KRISTO WA NAZARETI , na kwa jina lingine anaitwa Masihi. Akasema pia wala kilichopo chini ya maji kisiabudiwe yani viumbe vyote na hata vilivyopo duniani. Yeye alishajua kuwa haya yatatokea watu watakuja kudanganyika na shetani kama alivyosema ili mzivunje amri zake mpotee na yeye anasema katika kitabu cha Matendo 7:43 .

YESU NDIE ATAKAYE HUKUMU SIKU YA KIYAMA



HAKIKA YESU NI MUNGU
Ndugu msomaji:
Jambo hili si mzaha wala uzushi bali ni kweli; Yesu Kristo anakuja kuhukumu ulimwengu wote. Yesu Kristo ametutamkia kwa kiywa Chake kwa kusema kwamba;
“Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote; ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba.” (Yohana 5:22,23)
Katika hukumu siku ya kiyama hatutegemei kumwona YEHOVA akija kuhukumu ulimwengu, bali, Yesu Kristo ndiye ajaye kuhukumu ulimwengu. Hii itakuwa hivyo ili WATU WOTE WAMHESHIMU Yesu sawa sawa na jinsi ambavyo wanamheshimu YEHOVA. Hapo ndipo viumbe vyote watathibitisha kuwa Yesu ni Mungu. Biblia Takatifu inasema kwamba:
“...kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA...” (Wafilipi 2:10,11)
Hakika Yesu ni Mungu. Najua hapa huwachanganya baadhi ya watu hata wanaweza kuhoji;
Je! Wapo Miungu wangapi? Kwa maana tunasikia habari za Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu? Inawezekanaje tuseme Yupo Mungu mmoja wakati hapo tunaona wapo watatu?
Ni kweli Utatu Mtakatifu wa Mungu umekuwa mgumu sana kueleweka kwa watu wengi kutokana na mafundisho dhaifu waliyoyapokea kutoka kwa viongozi wao wa madhehebu yao na imani zao. Je! Utatu Mtakatifu wa Mungu ni uzushi uliotungwa na wanadamu kwa lengo la kupotosha watu au Biblia Takatifu inatuthibitishia wazi wazi kuhusu Utatu Mtakatifu wa Mungu? Hebu twende katika neno la Mungu tuone jinsi lisemavyo.
Biblia Takatifu inatuambia kwamba:
“Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni: Baba, Neno, na Roho Mtakatifu; na watatu hawa ni umoja.” (1 Yohana 5:8 / 1 John 5:7)
Andiko hilo katika Biblia ya New King James Version inasema “...these three are one.” (1 John 5:7) kwa maana ya kwamba “...WATATU HAWA NI MMOJA.” Hebu tujiulize; je! Huo umoja wao unaowafanya watatu hao (YEHOVA, Yesu, na Roho Mtakatifu) hata wote wawe MMOJA ni upi?
Umoja wao upo katika Uungu. Wote watatu wanaungana kuwa Mungu mmoja kwa maana ya kwamba uumbaji wa vitu vyote umefanywa kwa pamoja na hawa watatu (yaani; YEHOVA, Yesu, pamoja na Roho Mtakatifu).
Tukirejea katika uumbaji; Neno la Mungu linasema kwamba:
“Mungu akasema, Na Tumfanye mtu kwa mfano Wetu, kwa sura Yetu...” (Mwanzo 1:26)
Pindi niliposoma andiko hilo kwa umakini nilijiuliza; Mbona Mungu hakusema;
"...Nimfanye mtu kwa mfano Wangu, kwa sura Yangu..."? Kwa nini Mungu ametumia maneno "...kwa mfano WETU, kwa sura YETU..."? Maneno hayo "...WETU..." na "...YETU..." yanadhihirisha hapo kuna zaidi ya mmoja. Je, ni nani mwingine aliye muumba mwanadamu zaidi ya Mungu?
Wakati nikiwa ninajiuliza maswali mengi, ndipo Roho Mtakatifu akanifundisha kwamba neno "Mungu" ni cheo, na sifa zake ndizo tulizojifunza hapo awali. Mungu hufanya kazi katika ushirika ambao katika Umoja huo ndipo aliumba vitu vyote.

QURAN IMEJAA SHAKA NA MASWALI YA KUTATANISHA



Waislamu wamekuwa na kawaida ya kufanya kila juhudi kuonyesha kwamba Biblia imepotoshwa, ingawaje jambo hilo si kweli hata kidogo.
Na juhudi hizi zote zinafanywa ili kutaka kuonyesha kwamba Quran ni neno la Mungu la kweli ambalo halijapotoshwa hata kidogo. Basi mimi naomba mnisaidie majibu ya maswali haya machache kati ya mengi:
1. Sura 54:19 inasema kuwa mji wa Aad uliharibiwa kwa siku moja na sura 69:6,7 inasema kuwa uliharibiwa kwa 'usiku' sita na siku nane (seven nights and eight days). Hapo kuna mkanganyiko au la?
2. Sura 19:17 inaonyesha kuwa malaika alimtokea Mariamu lakini sura 3:42 inasema walikuwa malaika wengi.
3. Sura 28:40 inasema kuwa farao alizama na kufia kwenye maji lakini sura 10:92 inasema kuwa farao huyo alipona.
4. Sura 18:86 inasema kuwa jua huzama kwenye chemchemi ya maji yenye tope. Unadhani hii ni sahihi. Jua lina joto la zaidi ya nyuzijoto 6000 kwenye uso wake. Lakini maji yakifika nyuzijoto 100 yanageuka mvuke. Je, maji yanayotajwa kwenye sura hii ni maji gani? Unadhani ni Mungu aliyeumba jua na maji ndiye anayesema haya?
5. Sura 15:19 inasema kuwa dunia ni bapa kama meza (flat). Kama Mungu ndiye aliumba dunia na ndiye alileta Quran, anaweza kusema jambo kama hili?
6. Sura 86:6,7 inasema kuwa manii ya mwanamume hutokea kati ya uti wa mgongo na mbavu. Hii ni sayansi ya wapi? Ni kutoka kwa Mungu aliyeumba wa mbingu na nchi na uti wa mgongo na mbavu kweli? Kama haitoki kwa Mungu basi hata kitabu chenyewe nacho hakitoki kwa Mungu, au siyo?
7. Sura 19:27,28 inasema kuwa Mariamu alikuwa ni dada wa Haruni. Lakini tangu Haruni aishi ilipita miaka 1300 ndipo alipozaliwa Mariamu. Ni Mungu gani basi anayeweza kusema maneno kama haya?
8. Sura 28:8 inasema kuwa farao na Hamani waliishi wakati mmoja na mahali pamoja. Lakini historia iko wazi kwamba kuna tofauti ya miaka takribani 1000 kati ya watu hawa. Vilevile, farao aliishi Misri wakati Hamani aliishi Uajemi kwenye ngome iliyoitwa Shushani.
Huu ni Msiba Mkubwa sana katika Uislam
Max Shimba Ministries Org

TRENDING NOW