Thursday, March 3, 2016

MUHAMMAD AKIRI KUPATA UTUME KWA KUCHEZEWA NAFSI YAKE NA SHETANI

Ndugu msomaji,
Kwanza ningependa tujifunze maana ya neno Nabii:
Nabii ni mtu gani?
Nabii ni mtu aliyeteuliwa rasmi kwa vigezo vya Kiungu ili kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu, kwa maneno mengine nabii ni msemaji wa siri za Mungu.
Mitume wote na manabii wote wa Biblia waliwai ongea na Mungu. Lakini, Mtume wa Allah "Muhammad" hakuwai ongea na Mungu HATA MARA MOJA. Je, utume wake tutauamini vipi maana hakuwai ongea na aliye mtuma?
Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu aliye Mtuma? Maana ya neno Mtume kwa kifupi: Ni Mtu aliye tumwa.
HEBU TUANGALIE, HUYU MUHAMMAD ALIZALIWAJE NA KUUPATAJE UTUME WAKE?
1. MUHAMMAD ALIKUWA NA SHETANI TANGU KUZALIWA KWAKE,
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa "Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa na shetani tangu alipozaliwa, (Fat'hul Baary Juzuu ya 6 Uk. 389).
Je, kuna ushahid wowote ule kuwa Muhammad alitolewa Shetani ALIYE KUWA NALO TANGU KUZALIWA KWAKE? Kama upo Basi Waislam, tuleteeni tuuone.
2. MUHAMMAD AKIRI KUPINGWA NA KUBANWA MBAVU ZAKE NA KIUMBE AKIWA PANGONI,
Katika kitabu kiitwacho: Maisha Ya Nabii Muhammad s.a.w uk 16-17 kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy, tunasoma kama ifuatavyo;-
Hata siku moja- katika mwezi wa Ramadhani mwezi 17, Jumatatu katika mwaka wa 40 ½ wa umri wake- mtume alimwona mtu kamsimamia mbele yake bila ya kumwona wapi katokea, akamwambia; “soma”. Mtume akamjibu; “Mimi sijui kusoma kwani sijapata kujifundisha kusoma.” Akaja akamkamata akambana, akamwambia tena; “soma,” Mtume akamjibu jawabu yake ileile. Hata mara ya tau akamwambia; “soma- Iqraa Bismi Rabbik.” Akamsomea sura hiyo ya 96 mpaka kati yake. Kisha mtume akaisoma kama alivyosomewa. Hii ndiyo sura ya kwanza kushuka katika Qur’an, ingawa haijawekwa mwanzo.
Mara, yule mtu (Malaika) akaondoka machoni mwake- asimwone kenda wapi. Na mtume naye akarejea kwake-khofu imemshika. Alipofika nyumbani, Bibi Kadhija alidhani ana homa, akamfunika maguo gubigubi na akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka. Hata homa ilipomwachia alimweleza Bibi Kadhija yote yaliyomtokea; na Bibi Kadhija akamtuliza moyo wake, akamyakinishia ya kuwa hapana lolote baya litakalomzukia. Mara bibi huyu akaondoka akenda kwa jamaa yake – Bwana Waraqa bin Naufal- akampa habari yote iliyompata mumewe. Naye akamwamrisha amwite. Na mtume akenda akamweleza habari yake yote. Bwana Waraqa akamwambia; “ Huyo ndiye Jibril aliyemshukia Nabii Musa na Nabii Isa. Basi jibashirie kuwa wewe ni mtume wa umma huu, nami natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako; Inshaallah nitakuwa mkono wako wa kulia” Wakarejea kwao na khofu yote imemtoka”.
Alipokuwa pangoni alichezewa na Shetani: Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya
3. MUHAMMAD AKIRI KUCHEZEWA NAFSI YAKE NA SHETANI
“Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na Shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.
Katika tukio hili lililompata Muhammad akiwa pangoni , ndipo Waislamu wote ulimwenguni wanapolieleza kuwa hapo ndipo Muhammad s.a.w alipoletewa wahyi (ufunuo) na kupewa unabii na utume. Lakini unapotafakari juu ya ujumbe huo utaona kuwa hata yeye mwenyewe hajui nini kilichokuwa kimemtokea kule pangoni. Ndiyo maana tunasoma kuwa alipofika nyumbani kwake mkewe Bi. Khadija alimfunika nguo mumewe akidhani ana homa. Muhammad alimweleza mkewe kilichomtokea kuwa ni “Shetani” hakumsema malaika yeyote kama Waislamu wanavyotaka kutuaminisha leo. Kwa sababu kama angekuwa ni malaika kama tunavyosoma ndani ya Biblia ,asingesita kujitambulisha kwa Muhammad kuwa yeye ni nani.
KUFUATANA KITABU CHA MAISHA YA NABII MUHAMMAD, tunajifunza kuwa Muhammad kwa mara ya kwanza kabisa alipata utume wake pangoni baada ya NAFSI YAKE KUCHEZEWA NA MASHETANI.
Wahyi (ufunuo) uliokuja kwa Muhammad alisikia makengele, uso kuwa mwekundu, jasho kumtoka. Katika Bukhar, Hadithi na 2, Juzuu na 1,Al-Lu’lu Kitabu cha 3.Uk. Na.874 Hadithi na 1505 “Hadithi ya Aisha r.a mama wa waumini amesema, kuwa Al Harith ibn Hisham r.a alimuuliza mtume wa Allah s.a.w ‘ Ewe mtume wa Allah hivi wahyi (ufunuo) hukujia vipi?’ Mtume wa Allah s.a.w akajibu, “ Wakati mwingine hunijia kama mlio wa kengele, na aina hiyo ndiyo ngumu zaidi kwangu, inaondolewa hali hiyo kwangu wakati tayari nimeshapata wahyi. Na nyakati nyengine malaika anakuja kwangu akiwa katika mfano wa mtu, kwa hiyo ananieleza na ninayazingatia aliyoyasema.” Aisha r.a alisema , Na hakika nilimwona unamshukia wahyi siku ya baridi kali na ilipomuondoka hali hiyo, paji lake la uso lilichuruzika jasho.”
Muhammad akiwa Medina aliulizwa na Wayahudi ikiwa ufunuo wake umetoka kwa Mungu wa Kweli kwa kumtaka atoe sifa za manabii. Akijibu swali hilo alisema:
Mkweli Mwaminifu Juzuu 3-4 Uk.63.Hadithi Na. 880. “Kasema Mtume (s.a.w):- (Mambo) mane ya sheria za mitume (Kuwa na) na haya,na kujipaka mafuta mazuri,na kuowa (wake),na kupiga mswaki.
Hizi si sifa za Ki-Mungu kwa nabii na mtume bali ni za kibinadamu tu.
4. QURAN INASEMA KUWA, NABII LAZIMA AFANYE MIUJIZA; MUHAMAMD AKIRI KUWA YEYE NI MTUME BANDIA NA HAKUFANYA MIUJIZA
Qur’an nayo inathibitisha kuwa manabii na mitume ni lazima wafanye miujiza.
Qurani 40:78 Suratul Al-Muumini [Waumini] inasomeka “Na kwa yakini tumewatuma mitume kabla yako wengime katika wao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia na haikuwa kwa mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu”
Muhammad hakupewa kufanya muujiza wowote ili kuthibitisha madai ya unabii na utume wake.
Qur’an 29:50 Suratul Al-Ankabuut (Buibui). “Na walisema “Mbona hakuteremshiwa miujiza kutoka kwa Mola wake? Sema miujiza iko kwa Mwenyezi Mungu tu (akitaka atakuteremshieni na kama hataki basi),nami hakika ni mwonyaji mbainishaji (dhahiri tu).” (Taz. Qur,an 6:35-37 13:7,)
MASWALI:
(i). Kama Jibril ndie alitumwa na Allah, na huyo Allah ni Mungu, kwanini Muhammad alisema kuwa nafsi yake imechezewa na MASHETANI baada ya kukutana na Jibril?
(ii). Kama Jibril alitoka kwa Allah, kwanini Muhammad alipo toka pangoni alisema kuwa Jibril AMEMZUGA AKILI YAKE?
(iii) Je, wapi katika Injili au Taurat au Zaburi tunasoma kuwa Manabii na Mitume katika Biblia walipata kwa njia ya homa na kukiri kuchezewa na mashetani kama Muhammad wa kwenye Quran?
(iv) Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu aliye Mtuma? Maana ya neno Mtume kwa kifupi: Ni Mtu aliye tumwa.
3. KUROGWA KWAKE MUHAMMAD
Zaidi ya hayo tunaona Muhammad alirogwa. Kurogwa ni hali ya mtu kuathirika na nguvu za giza yaani uchawi. Je nabii au mtume wa Mwenyezi Mungu wa Kweli anaweza kurogwa?
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo na kupiga makelele. (Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
Hii ni uthibitisho mwingine mzito unaoonesha kuwa utume wa Muhammad una utata.
MASWALI:
(a) Hivi, kuna Mtume au Nabii yeyote yule ambaye alikiri kurogwa kama Muhammad?
(b) Hivi Allah alikuwa wapi wakati Muhammad anarogwa? [Ingawa Quran inakiri kuwa aliye teremsha uchawi/urogi ni Allah]
(c) Wapi tunasoma kuwa Muhammad aliombewa na kutoa huo uchawi/urogi aliofanyiwa na Labiid bin Al'answan?
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MTU ALIYECHEWA NA MASHETANI KAMA HUYU?
Ndugu msomaji,
Muhammad hakuwa Mtume wa Mungu na wala hana sifa za KITUME.
1. Muhammad hakuwai ongea na Allah aliye mtuma.
2. Muhammad alikuwa na Shetani tokea kuzaliwa kwake.
3. Muhammad alikiri kuchezewa na Shetani wakati wa kusimikwa utume wake Pangoni.
4. Muhammad alikiri kuwa Shetani amechezea akili na nafsi yake.
5. Muhammad alikiri kuwa alirogwa na Labiid bin Al'answan.
SASA WAISLAM, NIONYESHENI, wapi kwenye Taurat, au Zaburi au Injili kama kuna Mtume aliye na sifa za ajabu kama za Muhammad.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAPINGA WOKOVU KWA KUMKIRI YESU KRISTO

i. Wanadai kuwa kuna Nafasi ya Pili Kuokolewa.
ii. Wanadai kuwa si nia ya Mungu kuwaokoa watu sasa.
iii. Wanadai kuwa Mavuno ya Injili yamekwisha.
Ndugu msomaji,
NINI MAANA YA KUOKOKA?
KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya;
Kunusurika, kusalimika, kupona, kukombolewa, kufunguliwa au kutoka katika janga au hatari fulani. Ambavyo jamii yetu maneno haya tunayatumia sana,
NINI MAANA YA WOKOVU?
Watu wengi neno hili wamelitafsiri vile wa pendavyo au waonavyo sasa Swali hili acha lijibiwe na maandiko matakatifu, na maneno haya yasibadilishwe kwamba ni wakati gani wa kuokoka kitendo kikishamalizika cha kukiri kifuatacho ni uwokovu kwa mjibu wa neno, fuatilia hapa chini, “Kwasababu ukimkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa mtu hukiri hata KUPATA WOKOVU”. (Warumi 10:9-10.)
LAKINI, MASHAHIDI WA YEHOVA WANASEMA KUWA ILE FIDIA ALIYOTOA YESU KWA WANADAMU WOTE HAITHIBITISHI UZIMA WA MILELE WALA HAIWEZI KUKUOKOA:
Kitabu chao cha “Studies in the Scriptures” Vol. 1, uk. 150, cha Mashahidi wa Yehova kinasema, “Ile ‘fidia kwa watu wote’ aliyoitoa yule ‘mwanadamu Kristo Yesu’ haitoi wala kuthibitisha uzima wa milele wala baraka kwa mtu ye yote; bali inamthibitishia kila mtu nafasi nyingine au jaribu la kupata uzima wa milele.”
MASHAHIDI WA YEHOVA WANADAI KUWA KUNA NAFASI YA PILI YA KUOKOLEWA
Katika uk. 143, wanasema, “Nafasi ya pili itakuwa bora kuliko nafasi ya kwanza kwa sababu ya mazoezi yaliyopatikana katika matokeo ya jaribu la kwanza.” Tena, katika uk. 130, 131 wamesema: “Wote walihukumiwa mauti kwa sababu ya kuasi kwake Adamu, na wote watafurahia (katika maisha hayo au yanayokuja) na nafasi kamili kupata uzima wa milele kwa masharti mema ya Agano Jipya.”
LAKINI, MAFUNDISHO YA BIBLIA YANASEMA NINI KUHUSU WOKOVU?
HAKUNA NAFASI YA PILI KUOKOLEWA KAMA WANVYODAI MASHAHIDI WA YEHOVA!!!!!
Soma Waebrania. 9:27, “Kufa mara moja na baada ya kufa hukumu.”
Luka. 9:59-60, “Akamwambia Waache wafu wawazike wafu wao.”
Matendo. 13:44-46 “Kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele.” Je, alisema hapa kwamba wata pata nafasi ya pili! Hata siku moja!
Waebrania. 10:26, “......haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.”
Kwa hiyo tumeona kwa urahisi kwamba Biblia inatufundisha kwamba tutaishi na tutakufa mara moja tu na bada ya kufa hukumu!!
Lini unatakiwa ufanye uamuzi huu muhimu?
Hebu MUNGU na aseme nawe kupitia maneno yake ambayo ni amina na kweli anasema:
Warumi 13:11 Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
2Wakorintho 6:2 "Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa"
Biblia inaonya kuwa "tazama, wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa" yaani wakati huu unaposoma hapa ndio wakati wako wa kutubu na kumgeukia Mungu kwa njia ya kristo kama bado haujafanya hivyo kwani huu ni uamuzi ambao kila mwanadamu lazima aufanye.Mungu ana kalenda yenye miaka mingi lakini kwenye swala la kuukiri wokovu wa kristo wakati ni sasa..Ninakuomba umpe kristo maisha yako,ili hata kama ukifa muda wowote akupokee na uishi naye milele.
MASHAHIDI WA YEHOVA WANAENDELEA KUFUNDISHA KUWA SI NIA YA MUNGU KUWAOKOA WATU KATIKA KIPINDI CHA INJILI BALI ULIMWENGU UTAOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA UTAWALA WA MIAKA 1000.
Mafundisho ya Biblia yanasema nini kuhusu Wokovu:
Yesu mwenyewe alifundisha katika Marko. 16:15-16, kwamba tuhubiri Injili ili watu waokolewe. Na tangu siku ya Pentekoste wakovu umehubiriwa, Matendo. 2:38, 40; 13:26, 47. Pia Paulo alisema, “LEO NI SIKU YA WOKOVU”, katika 2 WaKorintho. 6:2; Wafilipi. 2:12. Na katika Waebrania. 2:3-4, mwandishi anatuambia kwa urahisi kama tunakataa wokovu hatuwezi kukwepa adhabu!!! Kwa hiyo ina maana tunaweza kukosa wokovu leo!
Na tunakosa kwa kutotii injili, katika kipindi cha Injili.
LAKINI, MASHAHIDI WA YEHOVA WANADAI KUWA, “MAVUNO” YA INJILI YAMEKWISHA.
Katika kitabu chao, “Studies in the Scriptures,” Vol 2, uk. 245, Mashahidi walisema: “Miaka arobaini ya mavuno ya kipindi cha Injili itakoma Oktoba 1914, na vivyo hivyo, upenduzi wa Ukristo, kama unavyoitwa, lazima tutegemee kuuona mara.” Hivyo wanasema kuwa hakuna mtu awezaye kuokolewa baada ya Oktoba 1914, BK. Tena, Ukristo (maana yake madhebehu yote isipokuwa kanisa lao) utapinduliwa mara baada ya mwake ule.
BIBLIA INAWAJIBU MASHAHIDI WA YEHOVA KUWA:
Mwaka 1914 umekwisha kupita zamani; mbona madhehebu bado yapo? Isitoshe, ikiwa mavuno ya kipindi cha Injili yalikwisha mwaka 1914, basi Mashahidi wenyewe walio hai leo wamechelewa!
Imekuwaje wao kudai kuwa wamejua tareje na majira hali Yesu amesema hakuna ajuaye mambo hayo?
(Marko. 13:32; Matendo. 1:7).
WOKOVU NI HAPA DUNIANI
Usikubali uongo wowote wokovu ni hapa duniani na baada ya kufa ni hukumu na hukumu hii itategemea uliishije hapa duniani.” Na Kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, baada ya kufa hukumu, Waebrania 9:27”
“Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo Watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliofanya mabaya kwa ufufuo wa hukumu Yohana 5:28-29”
Kwa hiyo maisha yetu ya hapa duniani ndiyo yatakayoamua hukumu yetu itakavyokuwa.
Mungu amezibitisha mwenyewe kuwa kuna Watakatifu Duniani.”Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, Nao ndio nliopendezwa nao, Zaburi 16:3”
Kataa uongo wowote tunaokoka hapa duniani na tunaishi Maisha ya utakatifu yanayompendeza Mungu.
SALA YA TOBA
Inawezekana kabisa ya kuwa wewe unayesoma ujumbe huu hujaokoka - yaani hujampokea Yesu Kristo ndani ya moyo wako kama Bwana na Mwokozi wako. Lakini sasa umeona umuhimu wa kumpokea Yesu Kristo katika maisha yako.
Naamini Roho Mtakatifu ameweka fursa hii mikononi mwako kwa mpango maalum wa Mungu ili ufike mahali pa kutubu na kuokoka. Inawezekana kabisa, pia ya kuwa hujawahi kuambiwa juu ya umuhimu wa wewe kuokoka. Lakini napenda kukuambia ya kuwa ni mpango wa Mungu uokoke. Soma Wakolosai 1:13,14 na Yohana 1:12-14 na 1 Timotheo 2:3-6 na Warumi 1:16,17 na Yohana 3:7. Ni vigumu kuona baraka za Damu ya Yesu bila ya kuokoka.
Kwa hiyo kama unataka kuokoka - tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa sauti sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)
“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu. Ninatubu kweli. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho wako – uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina.
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zimesamehewa na kusahauliwa na Mungu sawasawa na alivyoandika katika neno lake. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka
Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
1.Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7)
2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11)
3.Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17)
4.Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6)
5.Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25)
Ukipenda unaweza kuniandikia kwa anwani hii hapa chini juu ya uamuzi uliofikia leo wa kuokoka, ili tumshukuru Mungu pamoja, na tuzidi kukuombea; na pia, tukutumie maandiko mengine ya kukusaidia: maxshimbaministries@gmail.com.
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Tuesday, March 1, 2016

MUHAMMAD AKIRI KUWA ALLAH NI MUNGU WA KIPAGANI

Je, Wakristo na Waislam, wanaabudu Mungu mmoja?
Je, Allah ni Mungu wa Kipagani?
Ndugu wasomaji, kwa mara nyingine tena, Nabii wa Allah amekiri kuwa Wakristo na Waislam hawaabudu Mungu mmoja na Allah ni mungu wa Kipagani.
Katika hiki kijarida tunaangalia ushahidi mbalimbali kuwa, Allah sio Mungu wa Adam, Musa na Mitume wote walio tajwa kwenye Biblia Takatifu.
Kutokana na Surat Al Kafirun iliyoteremka Makka, Nabii Muhammad anakiri kwa mdomo wake kuwa Wakristo na Wayahudi hawaabudu Mungu mbaye anaabudiwa na Waislamu.
Sura 109 1. Sema: Enyi makafiri! 2. Siabudu mnacho kiabudu;
3. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. 4. Wala sitaabudu mnacho abudu. 5. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu. 6. Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Surah hii inamatatizo mengi sana ambayo ypo wazi kuwa, madai ya Wiaslam ya Mungu wa Wakrist na Mungu wao ni mmoja, ni batili na hayana ushahid.
TATIZO LA KWANZA: Hivi, hii Surah inamzungumzia nani?
(a) Watu wa Kitabu (Wayahudi, Wakristo na labda Wasebia)?
(b) Makafir wa Makkah?
Quran hapa imeshindwa kutueleza kuwa, Muhammad alikuwa anaongelea ummah upi.
TATIZO LA PILI: Hata kama ni moja ya dai la (a) au (b) hapo juu, hii Surah ya 109 imejaa utata na kupinga aya mbaimbali za Quran ambazo zinadai kuwa Wakristo, Wayahudi na wengine wote wanaabudu Mungu mmoja ambaye anaabudiwa na Waislamu.
Surat Al Baqara 62. Hakika Walio amini, na Mayahudi na Wakristo, na Wasabai; yeyote atakaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akatenda mema basi watapata malipwa yao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
2: 139. Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu
Surah 3: 64. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.
KWENYE Surat Al Ankabut 46. Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake.
Kwenye hiyo aya hapo juu, Muhammad anadai kuwa Mungu wa Wakristo, Wayahudi na Waislam ni mmoja.
Hivyo basi, kwenye ushahidi tulio sona unaonyesha kuwa kikundi cha (b) nacho kinaabud Mungu wa Waislam ingawa vilevile kinaabudu miungu mingine na mbalimbali.
Surah 29: 61. Na ukiwauliza; Nani aliye umba mbingu na ardhi na akafanya jua na mwezi kuti'ii amri yake? Bila ya shaka, watasema: Mwenyezi Mungu. Wapi basi wanako geuzwa? ***
62. Mwenyezi Mungu humkunjulia, na humdhikishia, riziki amtakaye katika waja wake. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. ***
63. Na ukiwauliza: Ni nani anaye teremsha maji kutoka mbinguni, na akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake? Bila ya shaka watasema: Ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdu Lillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Bali wengi katika wao hawafahamu. ***
Surat An Nahl 35. Na washirikina wanasema: Mwenyezi Mungu angeli taka tusingeli abudu chochote badala yake, sisi wala baba zetu, wala tusingeli harimisha chochote bila ya Yeye. Kama hivyo walifanya walio kuwa kabla yao. Basi lipo lolote juu ya Mitume isipo kuwa kubalighisha kwa uwazi? ***
Wapagani tulio wasoma hapo juu, walikuwa wanarudia na au sema maneno ambayo Allah aliyasema kwa Muhammad.
Surat Al Ana’am 107. Na lau Mwenyezi Mungu angeli penda, wasingeli shiriki. Na Sisi hatukukufanya wewe uwe mtunzaji wao. Wala wewe si mlinzi juu yao. ***
Mwisho basi:
Surat Azzumar 3. Hakika Dini Safi ni ya Mwenyezi Mungu tu. Na wale wanao wafanya wenginewe kuwa ni walinzi wakisema: Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu - Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika wanayo khitalifiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamwongoi aliye mwongo kafiri. ***
Katika aya hapo juu, tumejifunza kuwa mungu wa Wapagani ni Allah, na hao miungu wao wengine walikuwa ni wasaidizi katika kumwabudu Allah. Hivyo basi, Allah, ndie aliye kuwa MUNGU WA MKUU WA KIPAGANI.
Kuna aya moja katika Quran ambayo inawasema watu ambao wanamwamini Allah kama muumba wa vitu vyote:
Surah Luqman (31:25). Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu. Wewe sema: Alhamdulillahi! Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu. Lakini wengi wao hawajui kama hii aya inazungumzia kundi la A au B, au yote mawili, hii aya ipo wazi kuwa, Muhamamd alijua ni kuwa anamwamini Allah wa Magani wa Mekkah.
Ngoja niweke kwa kifupi hiyo aya:
1. Wakristo na Wayahudi wanadaiwa kumwabudu Allah.
2. Wapagani na waislam vilevile nao wanamwabudu Allah, ingawa walikuwa na miungu wengine.
Kama hii ndio dai letu, ni kivipi Surah 109 idai kuwa Makafiri hawamwabudu mungu wa Muhammad na hawaabudu anacho abudu Muhammad?
Kusema kuwa hii aya inahusu waabudu “idols” ni Wapagani peke yao, ni uongo kwasababu zifuatazo:
1. Waislam wanafahamuje kuwa hii aya iliteremshwa kwa ajili ya Wapagani peke yao?
2. Hata kama hii aya ilikuwa inawaongelea Wapagani peke yao, je, Quran si inasema kuwa Wapagani walijua kuwa wanamwabudu Allah, na hivyobasi walikuwa wanaabudu alicho kuwa anaabudu Muhammad.
Ni kweli kuwa Muhammad hakuabudu miungu wao wote, lakini ukweli unabakia palepale kuwa wote Muhammad na Wapagani waliabudu mungu wa Kipagani aitwaye Allah kama ilivyo semwa kwenye sura 109:3.
Kwa mfano, Quran inadai kuwa Muhammad aabudu ambacho Wapagani waliabudu isipokuwa Allah:
Surat Yunus (10: 104). Sema: Enyi watu! Ikiwa nyinyi mnayo shaka katika Dini yangu, basi mimi siwaabudu mnao waabudu nyinyi badala ya Mwenyezi Mungu. Lakini mimi namuabudu Mwenyezi Mungu anaye kufisheni. Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waumini.
Surat Ghafir (40:66). Sema: Mimi nimekatazwa kuwaabudu hao mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu, zilipo nijia hoja zilizo dhaahiri kutokana na Mola wangu Mlezi. Na nimeamrishwa nisilimu kwa Mola wa walimwengu wote.
Hizo aya hapo juu zinasema kuwa, Wapagani walikuwa wanamwabudu Allah, pamoja na miungu wengine wa kipagani.
Hivyo basi, leo tumejifunza kwa undani kabisha kuwa Muhammad alikuwa anamwabudu Allah ambaye ni mungu wa kipagani. Jina la Baba yake Muhammad ni Abdallah, likimaanisha slave of allah. Inafahamika kuwa Muhammad ndie muislam wa kwanza, au sio. Kama hayo madai ni kweli, je, baba yake Muhammad alilipata wapi jina la Abdallah kama si yule Allah mungu wa kipagani?
Hakika Allah aabudiwe na Wapagani ni yule yule ambaye aliabudiwa na Muhammad.
Katika Hudma yake
Max Shimba Ministries
@February 9, 2015

MUHAMMAD AKIRI KUWA DHAMBI ZAKE HAZIKUSAMEHEWA

Katika kitabu chake " mwisho mstari wa mbele "anaandika Reza Safa F inasema katika hadith ambapo mke wa Muhammad Khadija kumtaka kusamehe dhambi yake, Muhammad alimjibu kuwa hakuwa na uhakika wa kusamehewa dhambi zake mwenyewe! Angewezaje kusamehe dhambi yake?
YESU HAKUWA NA DHAMBI NA WALA HAKUWAI FANYA DHAMBI
Lakini kwa upande mwingine, Biblia na Quran vinasema kwamba Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, hakuwa na dhambi na wala hakutenda dhambi:
Waebrania 4:15 Kwa maana huyu kuhani wetu mkuu si kuhani ambaye hawezi kutuhurumia katika udhaifu wetu, bali ni kuhani ambaye kwa kila hali amejaribiwa kama sisi, lakini pasipo kutenda dhambi.
Yesu anaweza kuokoa na kusamehe dhambi kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa bila dhambi, na zaidi ya hapo, Yesu ni Mungu! Alikufa kwa ajili ya watu wote ili kuwaokoa. Kwa kifo chake msalabani alichukua dhambi zetu!
Muhammad hawezi kujiokoa na kusamehe kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa mwenye dhambi kubwa kiasi cha kuomba msamaha mara mia kwa siku.
Sasa ndugu msomaji, hivi ni sahihi kumfuata Mtume ambaye alikuwa mtenda dhambi na hisia mbaya kwenye nyoyo yake?
Karibu kwa Yesu aliye hai. Yeye anamamlaka ya kusamehe dhambi na kukuokoa.
Hakika Yesu ni Mungu.
Kwa maana huyu kuhani wetu mkuu si kuhani ambaye hawezi kutuhurumia katika udhaifu wetu, bali ni kuhani ambaye kwa kila hali amejaribiwa kama sisi, lakini pasipo kutenda dhambi.
MUHAMMAD ALIKUWA NA DHAMBI KUBWA KIASI CHA KUOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU
Leo ni leo asemaye kesho ni mungo. Ndugu zanguni, kila ninapo usoma Uislam, nazidi kupata shaka kubwa kubwa, maana hakuna jema kabisa katika hii dini ya Muhammad na Jibri. Hivi mtu anye omba msamaha mara mia kwa siku, unafikiri ametenda dhambi gani kiasi cha kuogopa namna hii?
MUHAMMAD AOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU:Katika "Sahih Muslim, Kitabu 35, 6522 Idadi" inasema kwamba Mtume Muhammad alikuwa mwenye dhambi kubwa sana kiasi cha kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu mara mia kila siku. "Nukuu"
"Al-Agharr al-Muzani, ambaye alikuwa mmoja wa (Mtume) wenzake taarifa kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani ilikuwa juu yake) alisema: Kuna (wakati mwingine) aina ya kivuli juu ya moyo wangu, na mimi kutafuta msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu mara mia kwa siku. "
Kumbuka kwamba utamaduni si tu anasema kwamba Muhammad alikuwa mwenye dhambi kubwa, lakini kwamba alijisikia kivuli, hisia mbaya, juu ya moyo wake. Katika kesi hii kwa Muhammad, itakuwa vigumu kwa sababu Qur'an inasema kuwa yeye ni kipaji katika maisha yake na vitendo:
Sasa, kivipi Muhammad alikuwa na kivuli ndani ya nyoyo yake?
Hii chuki aliipataje wakati yeye alikuwa anapokea wahyi kutoka kwa Allah?
Je, inawezekana kuwa hiyo wahyi ndio ilikuwa chuki iliyo jaa ndani ya nyoyo yake?
68: 4
Maisha yako na matendo yako ni `aa [mfano]. (Mohammed Knut Bernstöm, Qur'an)
Watu wote wamefanya dhambi
Biblia inasema kwamba watu wote wamefanya dhambi. Hii ni pamoja na Mtume Muhammad alikuwa mwenye dhambi kama watu wengine wote, lakini Muhammad yeye alikiri kuwa dhambi zake hazikusamehewa ingawa aliomba msamaha mara mia kwa siku.
Ndugu msomaji, kwanini tumfuate na sikiliza Muhammad aliye kiri kuwa dhambi zake hazikusamehewa?
Kwanini Allah alishindwa kumsamehe Muhammad dhambi zake?
Je, Allah anauwezo wa kusamehe dhambi?
Muhammad ndio mtume pekee aliye kufa na dhambi na Mshahara wa dhambi ni mauti ya Jehannam. Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwa sababu mwenye dhambi, amehukumiwa kufa.“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti”(Warumi 6:23). Hii ina maana kutengwa na Mungu katika Jehanum milele.“Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu” (Waebrania 9:27).
Hivyo basi, kwanini ufe na dhambi kama Muhammad na utengwe na Mungu katika Jehannam?
Rafiki yangu:Ninakuuliza swali muhimu maishani mwako. Furaha yako ya milele au huzuni yako ya milele inategemea jibu Ia swali hili. Swali ni hili:Je, umeokolewa? Si swali la jinsi ulivyo mwema, wala si swali la kama u mshiriki wa kanisa, bali:Je, umeokolewa? Una uhakika kwamba utaenda mbinguni utakapokufa?
Hakikisha kwamba umeokoka. Ukipoteza nafsi yako utapoteza mbingu na utapoteza vyote. Tafadhali, mruhusu Mungu akuokoe sasa hivi.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

UTATA MKUBWA KUHUSU KUTEREMSHWA KWA QURAN

Ndugu msomaji,
Leo tutaangalia UTATA kuhusu kuteremshwa kwa Quran. Allah na Muhammad kwa mara nyingine tena, wameshindwa kutuhakikishia kuhusu lini Quran iliteremshwa?
Hapa chini kuna aya kadhaa ambazo zinaendelea kutuonyesha shaka kubwa kubwa iliyo ndani ya Quran.
ALLAH ANASEMA KUWA, QURAN ILITEREMSHWA MWEZI WA RAMADHANISurat Al Baqara 185. Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi. Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.
Lakini nilipo soma aya kutoka Surat Addukhan, Allah alibadilika na kusema kuwa:
QURAN ILITEREMSHWA USIKU MMOJASurat Addukhan 3. Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji. 4. Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima
Nilipo endelea kuisoma Quran kwa makini katika Surat Al Furgan, Allah akabadilika tena na kusema kuwa:
QURAN ILITEREMSHWA KIDOGO KIDOGOSurat Al Furgan
32. Na wakasema walio kufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur'ani kwa jumla moja? Hayo ni hivyo ili tuuthibitishe moyo wako, na ndio tumeisoma kwa mafungu.
Ndugu zanguni, hivi ni kweli huyu Allah aliteremsha Quran?
Hivi ni kweli kuwa Allah ni mjuzi wa yote?
Hivi, kwanini Allah anashindwa kukumbuka, ni lini aliiteremsha Quran?
Hivi, hata huyo Muhammad, kwanini anashindwa kumkumbsha Allah wake kuhusu kuteresmhwa kwa Quran?
Mbona hata Jibril na yeye ameshindwa kumkumbusha Allah kuhusu lini aliteresmhwa Quran.
WAISLAM, naomba mnijibu kwa aya na bila ya matusi, KURAN ILITERESMHWA LINI?
Watakabahu,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Sunday, February 28, 2016

KWANINI MASHAHIDI WA YEHOVA WANAPOTOSHA KWA MAKUSUDI KUHUSU UUNGU WA YESU?

Mashahid wa Yehova wanadai kuwa:
1. Yesu alikuwa Malaika aliyeumbwa.
2. Yesu hakuwa Mungu na mwanadamu wakati ule – “God incarnate”.
Mashahidi wa Yehova wanasema kuwa Yesu hakuchanganya au kushiriki tabia za kiungu na za kimwili alipokuwa duniani. Wanadai alipokuwa duniani alikuwa mwanadamu mkamilifu tu, ikimaanisha, hakuwa na adhama ya Uungu. Na tangu kufufuliwa, yeye ni nafsi kamili ya kiroho tu.
3. Yesu alishindwa kuwakomboa wanadamu.
4. Mwili wa Yesu haukufufuliwa.
5. Mwanadamu Yesu amekufa kwa hiyo haishi tena.
6. Kabla ya kufa Yesu alikuwa mwanadamu tu, bali baada ya kufufuliwa alikuwa na hali ya kiungu (malaika).
7. Yesu si mpatanishi wetu.
Je, madai ya hawa Mashahidi wa Yehova ni ya kweli?

LAKINI BIBLIA INATUFUNDISHA NINI KUHUSU YESU?
Biblia inakataa na kuvunja hoja zote dhaifu za Mashahidi wa Yehova kama ifuatavyo:
1. Yesu si malaika kama wanavyo dai hawa Mashahidi wa Yehova. Soma-Waebrania 1:1-8. Yeye ni bora. Pia soma Yohana 1:1-3; 8:58; Ufunuo 1:8; 21:6; 22:13 – Yesu hakuumbwa bali yeye mwenyewe ni mwumbaji aliye wa milele.
WAEBRANIA MLANGO WA 1: 1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu; 4 amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao. 5 Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana? 6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu. 7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto. 8 Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio. 10 Na tena, Wewe, Bwana, hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako; 11 Hizo zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa kama nguo,
1. Aya ya 2: Inakiri kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu.
2. Aya ya 3: Inakiri kuwa Yesu alimaliza deni la dhambi na yupo upande wa Kuume wa Ukuu huko juu.
3. Aya ya 4: Yesu ni Mmbora kupita mailaka, hivyo basi hawezi kuwa ni Malaika Mikaeli kama wanvyo dai Mashahdi wa Yehova.
4. Aya ya 5: Mungu Baba anakataa kuita Malaika Mwanae.
5. Aya ya 6: Malaika wote wanamsujudia Yesu, pamoja na Mikaeli na Gabrieli.
6. Aya ya 7: Inakiri kuwa Yesu ndie aliye umba Malaika.
7. Aya ya 8: Yesu ndie mwenye Kiti cha Enzi, zaidi ya hapo Yesu anaitwa Mungu na Baba yake.
8. Aya ya 9: Yesu kwa mara nyingine tena anaitwa Mungu na Baba yake.
9. Aya ya 10: Yesu anaitwa Bwana na kukiri kuwa yeye ndie aliye weka Misingi ya Nchi na Mbingu. Ni kazi ya mikono ya Yesu.
10. Aya ya 11: Yesu ni wa milele.
2. Isaya alitabiri kwamba Mungu angeishi kimwili-Isaya 7:14; Mathayo 1:23. Mariamu pia alikuwa na mimba kupitia uwezo wa Roho Mtakatifu, mwili wa Yesu alitoka kwa Mariamu lakini Roho kwa Mungu. Kwa hiyo Yesu alikuwa asili zote mbili--kimwili na kiroho, Mathayo 1:18-20. Katika Filipi 2:6-7 tunaona kwamba Yesu alifanyiwa kuwa mfano wa Mwanadamu, Filipi 2:6-7; Waebrania 2:16. Pia tunaweza kusoma katika Ynoha 1:1-2, 14; 16:28; 1 Timotheo 3:16. Pia tunaweza kumwona Petro alikiri katika Mathayo 16:18, Yesu ni nani? Na kama kuna mtu ambaye anatufundisha ya kuwa Yesu hatokani na Mungu, mwambie asome 1 Yohana 4:3 na 2 Yohana 7.
Isaya Mlango 7: 14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.
Aya inakiri kuwa Yesu ni Imanueli.
3. Mashahidi wa Yehova wanasema Yesu si mkombozi wetu. Tusome Yohana. 1:29; Mathayo. 10:28; Rum. 5:11; Waebrania 10:3-14.
Yohana 1: 29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Sasa Je, Nani ni mwongo hapa, Mungu au Mashahidi?
4. Wanadai mwili wa Yesu haukufufuliwa. Yesu alisema kwamba atafufuka, Yohana 2:19-22 [Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha] na pia alionyesha mwili wake (uliofufuliwa) kwa Tomaso, Yohana 20:24-28.
5. Wanadai mwanadamu Kristo alikufa asiwe hai tena. Lakini Biblia inasema katika Zaburi 16:10, hapa Daudi alitabiriwa kuwa Yesu atafufuka. Na Petro alidai kwamba Kristo alifufuka, Matendo ya Mitume 2:30-31, wakati alipokuwa anahubiri siku ya Pentikoste alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu. Na katika Matendo ya Mitume 1:1-3, Yesu alithilibitisha sana kwamba alikuwa hai.
6. Pia Mashahidi wanadai Yesu hakuwa na hali ya kimungu isipokuwa baada ya kufufuliwa. Katika Yoh.
1:1-3; 17:5 tunaona Yesu alikuwa Mungu tangu mwanzo. Katika Flp. 2:6, Yesu alikuwa sawa na Mungu, na Kristo na Mungu ni kitu kimoja, Yohana. 14:11; 17:21.
Kwa hiyo wanasema kuwa Kristo aliyekufa na yule aliyefufuliwa sio mtu yule yule, wale ni watu wawili tofauti. Lakini Biblia inasema ni yule yule kabla ya kufufuka na baada ya kufufuliwa, Matendo ya Mitume 1:11; Waefeso. 4:10; Waebrania 10:12.
7. Mwisho wanadai Yesu siye mpatanishi wetu. Tusoma gazeti lao, “Watch Tower” Toleo 15/9/1909, uk. 283. “Katika toleo lao la 1906, ukarasa wa 26, walisema, ‘Bwana wetu Yesu, kati ya Baba na nyumba ya waaminio, katika kipindi cha Injili.’ Usemi huu si kweli. Hakuna maandishi yanayosema hivyo. Ni sehemu ya mwisho ya kipindi cha giza, ambao tunafurahi kuufuta kutoka machaoni mwetu.”
Mashahidi ni waalimu gani? Wanaobadili mafundisho yao? Nani anaweza kuamini wameongozwa na Mungu ikiwa wanasema wenyewe kuwa wamekosa katika kufundisha kwao? Lakini, ukweli ni kwamba Yesu ndiye mpatanishi wetu, 1 Timotheo 2:5; Waebrania. 9:15; 1 Yohana 2:1.
YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Mashahidi wa Yehova ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yeremia 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Hebu tusome Wafilipi 2: 5-11 INASEMA:
5 Tuweni na nia ile ile aliyokuwa nayo Kristo Yesu. 6 Yeye ingawa alikuwa sawa na Mungu, hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho, 7 bali alijifanya si kitu, akajifanya sawa na mtumwa, akazaliwa katika umbo la mwanadamu. 8 Naye akiwa na umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza hata mauti, naam, mauti ya msalaba! 9 Kwa hiyo, Mungu alimtukuza sana na kumpa Jina lililo kuu kuliko kila jina, 10ili kwa Jina la Yesu, kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, vya duniani na vya chini ya nchi 11 na kila ulimi ukiri ya kwamba YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.
NENO la "Kuwa sawa na Mungu" kwa Kigiriki ni MORPHE-: Iikimaanisha Yesu alikuwa na adhama zote za Kimungu na Mungu. Hivyo basi katika ushaidi huu wa katika kitabu cha Wafilipi tunasoma kuwa Yesu hakuwa mtu wa kawaida bali alikuwa ni Mungu pamoja nasi yaani Imanueli.
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Saturday, February 27, 2016

MAFUNDISHO POTOFU YA MASHAHIDI WA YEHOVA KUHUSU UTATU WA MUNGU

Ndugu msomaji,
Katika somo hili, nitajibu hoja ya Mashahidi wa Yehova kuhusu kupinga kwao Utatu Mtakatifu wa Mungu.
Taasisi ya Mashahidi wa Yehova wanafundisha kuwa kuna nafsi moja tu katika Uungu naye ni Baba tu. Ikimaanisha kuwa, wanapinga Uungu wa Yesu na wanapinga Uungu wa Roho Mtakatifu.
Mafundisho ya Biblia:
1. Je! Yesu ni yule Mungu mmoja?
Musa alisema: “Sikiliza, Ee Israeli: Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja,” Kumbukumbu ya Torati 6:4
Lakini katika Injili kutokana na Yohana Yesu anasema yafuatayo: Yesu alisema: “Mimi na Baba tu umoja,” Yohana. 10:30.
Mtume Paula alisema, “Maana katika yeye (Yesu) unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili,” Wakolosai 2:9.
Sasa Mashahidi wa Yehova wanafundisha kuwa kuna nafsi moja na ni Yehova.
Lakini hapa kwenye Wakolasai 2: 9 tumeona nini? Tumeona kwamba wako wawili sasa [kuna Mungu Baba na kuna Yesu ambaye kuna utimilifu wote wa Mungu]. Lakini JE, kuna wawili tu? La hasha! Mafundisho ya Biblia yaliyo wazi sana yanasema.
Soma: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”
Tazama, neno la Mungu lasema kuwa WAKO WATATU MBINGUNI, na nafsi hizi tatu hufanya Uungu ule mmoja. Na maana ya kusema hayo ni sawasawa na maana yake aliposema kuwa duniani kuna “Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja.” mst. 9. Na tunaelewa kwamba roho, maji na damu sio kitu kimoja kiasili. La, bali umoja wao ni ushuhuda wanaotoa kuhusu Yesu. Vivyo hivyo, Baba, Neno, na Roho Mtakatifu ni nafsi tofauti tatu wanaomshuhudia Yesu kuwa Mwana wa Mungu. Kuna Mungu mmoja tu, walakini ana nafsi zake tatu. Yesu aliposema, “Mimi na Baba tu umoja,” hakuwa na maana kuwa Yeye mwenyewe ndiye Baba.
Tena tuangalie 2 Wakorintho. 13:14, maneno hayo ya Biblia yaonyesha kuwa Uungu ni wa nafsi tatu. Sasa tuchunguze kwenye Biblia maana ya “Umoja” walio nao Baba na Mwana.
Waefeso 5:29-32, “Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitndea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili moja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi na nena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.”
Mst. 30 - “Tu viungo vya mwili wake”.
Mst. 31 - “Hao wawili watakuwa mwili moja.”
Tazama:
1) Kanisa ni mwili ule mmoja wa Kristo. Sasa maana ya maneno hayo ya Waefeso. 5 ni kwamba kanisa ni mtu mmoja tu. Je, Petro, Paulo, Apollo, Barnaba, Timotheo, Tito na Yohana wote walikuwa mtu mmoja tu? La, mtume mwenyewe alisema kuwa ni Viungo vya mwili ule mmoja. Kanisa ni watu mbalimbali tofauti wanaounganishwa washiriki umoja wa kiroho. Wanashirikiana katika baraka na kazi za Yesu. Vivyo hivyo, Yesu na Baba wa umoja, hata ingawa ni wawili.
2) Pia mistari hii inasema mume na mkeo ni mwili mmoja tu! Je, kweli hawa wawili ni mwili mmoja?
Hapana. Lakini wale wawili ni umoja katika kazi na baraka za ndoa? Vivyo hivyo Yesu, Baba na Roho ni mmoja; hata ingawa ni watatu.
Yohana 17:20-21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako: hao nao wawe ndani yetu.”
Je, umoja ambao Yesu alituombea ni kwamba Wakristo wote wawe mtu mmoja tu? Si anaongea habari ya umoja wa matendo, imani, na maneno yetu? Kama vile Yesu na Baba wanao umoja katika kutuumba na kutuletea wokovu, vivyo hivyo Wakristo wawe na lengo moja na juhudi moja. Tuone mfano mwengine wa umoja katika Biblia. 2 Samweli 7:23, “Tena ni taifa lipi duniani lililo kama watu wako, kama Israeli...?”
Waisraeli walikuwa watu wengi na makabila mengi lakini wanaitwa kuwa ni taifa moja tu! Vivyo hivyo, Uungu ni mmoja, lakini una nafsi tatu.
2. Matatizo ya kusema kuna nafsi moja tu.
Yohana 17:1-5, Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza dunia, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa nifanye. Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.”
Sasa kama Mungu ni nafsi moja tu, na Mungu alikuja ulimwenguni katika mwili na aliitwa Yesu. Sasa huyo Yesu (Kama nafsi pekee) alikuwa ana ongea na nani hapa? Mbona alisema, Wakujue wewe, Mungu wa pekee, na Yesu Kristo uliyemtuma. Akiwa yeye (Yesu) alikuwa nafsi pekee sasa nani alitumwa huyu?
Kwa hiyo tumeona Baba na Mwana ni nafsi mbili tofauti. Na wana umoja katika kazi zao na asili yao ya Uungu.
Soma Yohana 14:9-10, “Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.”
Sasa wakati Yesu alisema “Siyasemi kwa shauri langu”. Sasa ameyasema kwa shauri la nani? Akiwa ninafsi pekee, ni nani aliyempa maneno ayaseme? Yesu tena alisema, “Mimi ni ndani ya Baba na Baba yu ndani yangu.” Sasa hakusema Yeye ni Baba! Lakini alisema Baba yu ndani yake! Kwa hiyo 1 + 1=2!
Kumbe!
Yohana 14:26, “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”
Tazama 1+1+1=3. Wako Watatu! Roho Mtakatifu atakayepelekwa na Baba kwa jina
la Yesu! Pia angalia mistari hii:
1 Wakorinth 11:3; 1 Wakorintho 15:24-28; 1 Timotheo 2:5; Marko 13:32; Mathayo 27:46; Luka 23:46-47.
HIVYOBASI, TUMEJIFUNZA kuwa kumbe wako Watatu, tena hao watatu wapo Mbinguni: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”
Baada ya kusoma huu ujumbe, sasa jiulize maswali yafuatayo:
MASWALI YAKINIFU:
Je, Yesu na Baba ni UMOJA – Yohana Mlango wa 10 aya ya 30?
Je, UMOJA maana yake ni MMOJA?
Je, Yesu ni UKAMILIFU WA KIMWILI WA MUNGU – Wakolosai 2”9?
Je, UNAKUBALINA NA: 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.”?
Namaliza kwa kusema kuwa, hoja ya Mashahid wa Yehova kupinga UTATU MTAKATIFU wa Mungu ni dhaifu, maana 1 Yohana 5:8, “Kwa maana WAKO WATATU washuhudiao mbinguni, BABA, na NENO, na ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja
Ni maombi yangu Mungu ayafungue macho ya Mashahidi wa Yehova kwa ukweli wa injili na mafundisho ya kweli ya neno la Mungu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Friday, February 26, 2016

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFUNDISHA KUWA HAKUNA JEHANNAM

(i) Wanafundisha kuwa, kifo ndio mwisho wa maisha yako
(ii) Wanafundisha kuwa, hakuna Jehannam.
Ndugu msomaji,
Mashahidi wandai kwamba hakuna Jehannam. Wanasema mwovu anapokufa, basi anapotea moja kwa moja tu! Wanadondoa Mhubiri 3:20-21; 12:7.
Je, haya madai ya Mashahid wa Yehova ni ya kweli?
Je, ni kweli kuwa hakuna maisha baada ya kifo, yaani wewe ukifa ndio unapotea moja kwa moja?
Biblia Yasema Nini kuhusu jambo hili?
1. Ni kweli mwili wa mtu hurudi mavumbini anapokufa, Mwanzo 3:19. Lakini mwanadamu si mtu tu -MWILI NA NYAMA PEKEE!
Mwanadamu ni nafsi ya roho pia, maana tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, (Mwanzo 1:26) naye Mungu hana mwili bali ni roho (Yohana 4:24; Luka 24:39). Miili ya wanadamu wote itarudi mavumbini hata wakiwa wema au waovu. Lakini roho za mwanadamu ndizo zitakazoishi milele ama pamoja na Mungu ama katika Jehannam.
WEWE NI MFANO WA MUNGU
Mwanzo 1: 26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
MUNGU NI ROHO, KUMBE BASI WEWE NI ROHO!
Yohana 4: 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Kumbebasi wewe ni roho na sio mwili na nyama.
2. Kifo Cha Roho-Kifo maana yake ni utengano. Ukitenga roho na mwili basi mwili umekufa, Yakobo 2:26. INASEMA: Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Vivyo hivyo, ukitenga roho na Mungu aliye uhai wetu, basi roho nayo imekufa. (Mungu hakumwambia Adamu uongo aliposema “Siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika” Mwanzo 2:17. Adamu hakufa kimwili siku ile bali alikufa kiroho maana alitengwa na Mungu, na kufukuzwa katika bustani.
Kifo cha roho hakina maana kwamba roho haitakuwapo tena. Roho ni ya milele. Roho ya mwovu inapotengwa na Mungu, basi tunaweza kusema imekufa hata ingawa ili roho bado ipo, 1 Timotheo 5:6 6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.
Waefeso 2:5; Warumi 8:10. Walakini, mtu akifa katika dhambi zake, basi roho ya mwovu yule itakuwa katika hali ya mateso daima mbali na Mungu, 2 Thesalonike1:7-9; Mathayo 25:41-46. Hii ndiyo inayoitwa MAUTI YA PILI na ndiyo kifo cha kiroho, Ufunuo 21:8; 20:14-15.
3. Ikiwa hakuna mahali pa mateso panapoitwa Jehannam, mbona Yesu hakujua? Maana Yesu ametuonya mara nyingi kuhusu Jehannam, Mathayo 10:28; Luka 12:5; Mathayo 5: 22, 29-30; 23:33.
Yohana 10: 28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
4. Mhubiri 3:20-21; 12:7 haisema kwamba hakuna Jehanum. Mistari hii inaonyesha kwamba mwili unarudi mavumbini mtu anapokufa. Lakini, miili yetu haitakaa mavumbini daima. La! bali Yesu atakapokuja, wafu wote watafufuliwa, Yohana 5:28-29; Ufunuo 20:12-15. Si vigumu kwa Mungu kufufua miili yetu kutoka
mavumbini, Ezekiel 37:1-13. Isitoshe, mara tutakapofufuliwa miili yetu itabadilishwa kama apendavyo Mungu maana nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, 1 Wakorintho. 15:50-54.
5. Mashahidi wanasema kwamba hakuna adhabu ya milele, Soma Daniel 12:2; Mt. 25:46; Yonana 5:28-29; Ufunuo 20:10.
JEHANNAM:
Jehanamu, kama vile mbinguni, si mahali patajwapo kwa utisho tu bali ni mahali dhahiri. Hapa ni mahali ambapo wasiohaki watakutana na ghadhabu isiyokoma ya Mungu. Watavumilia mateso ya kihisia, kiakili, na kimwili wakiwa katika akili zao timamu huku wakijihisi kuaibika na kujuta kwa matendo yao maovu.
Jehanamu inaelezewa kama shimo la giza (Luka 8:31, Ufunuo wa Yohana 9:1), na Ziwa la Moto, liwakalo na kiberiti ambapo watakao kuwemo watateswa usiku na mchana milele na milele (Ufunuo 20:10). Huko kutakuwa na kulia na kusaga meno, ikiashiria machungu makali na hasira (Mathayo 13:42). Hapa ni mahali ambapo mdudu hatakufa wala makaa kuzimika (Marko 9:48). Mungu hafurahishwi na kufa kwa mtu muovu, lakini hutaka wazighairi njia zao mbaya ili waishi (Ezekiel 33:11). Lakini hatatulazimisha kumkubali; tukiamua kumkataa yeye. Hana budi kutupatia tulilolichagua – kuishi mbali naye.
Je unaamini kuwa kunayo maisha baada ya kifo?
Ni nini hufanyika baada ya kufa?
Je, unaamini kuwa hakuna Jehannam kama Mashahid wa Yehova?
Je, unaamini kuwa ukisha kufa wewe ndio umeishia hapo/unapotea moja kwa moja kama ambavyo Mashahid wa Yehova wanavyo kiri?
Mungu awabariki sana,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wake.
Max Shimba Ministries Org
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

Thursday, February 25, 2016

MALAIKA GABRIEL WA BIBLIA NI TOFAUTI NA JIBRIL WA KWENYE QURAN


Ndugu msomaji,
Tokea kuanzishwa Kwa dini ya uislam, waislamu duniani wanaamini na kuifundisha jamii kuwa malaika aitwae ‘Gabriel’ Kama maandiko matakatifu ya Biblia yanavyofundisha ndiye malaika ‘Jibril’ Kama Quran inavyosimulia.
Swali la muhimu je ni kweli kuwa malaika “Gabriel” ndiye “Jibril” nakusihi fuatilia somo hili ili kujua ukweli….
HOJA ZA WAISLAMU ZA KUAMINI KUWA MALAIKA GABRIEL NDIYE JIBRIL
Waislam wanalinganisha kwa kusoma aya za Quran na Biblia na kusema kuwa malaika Gabriel ndiye Jibril wanasoma aya hizi….
QURAN 19:16-17 SURAT MARYAM
16. Na mtaje Mariamu kitabuni (humu) alipojitenga na jamaa zake (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) 17. Na akaweka pazia kujikinga nao.Tukampelekea muhuisha sharia yetu (jibril) - akajimithilisha kwake kwa sura ya Binadamu aliye kamili.
LUKA 1:26-28
26. Mwezi wa sita, malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. 27. Kwa mwana mwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu 28 Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa Neema, Bwana yu pamoja nawe.
“Mbali na kusoma aya hizi, pia wanaendelea kusoma kitabu cha maisha ya nabii Muhammad kilichotungwa na aliyekuwa kadhi mkuu wa Kenya marehemu sheikh Abdallah Saleh Al-Farsy katika ule ukurasa wa 17 kifungu (A) kuna maneno haya...
NAMNA YA KULETWA WAHYI…
Waislamu wanaitikadi kuwa Quran ni maneno ya Mwenyezi Mungu na vilevile Taurat ya nabii Musa na injili ya nabii Isa, na Zaburi ya nabii Daudi. Vyote pia ni vitabu vyenye maneno ya mwenyezi Mungu. Lakini Mungu haonekani Kwa macho wala hayupo mahali mahsusi. Basi vipi hao mitume wamepata maneno haya? Jawabu yake ni hii wao huyapata ima kwa Jibril malaika mkubwa kuliko malaika wote wa Mwenyezi Mungu.
QU-RAN 53:2-6 SURATUL NAJM (NYOTA)
2. Kwamba mtu wenu huyu Nabii Muhamad (hakupotea Kwa ujinga) na wala hakukosa (na hali ya kuwa anajua) 3. Wala hasemi Kwa matamanio (ya nafsi yake) 4. Hayakuwa haya (anayosema) ila ni wahyi (ufunuo) uliofunuliwa (kwake) 5. Amemfundisha (malaika) mwenye nguvu Sana 6. Mwenye uweza na yeye (huyu jibril) akalingana sawa sawa.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW