Tuesday, May 3, 2016

ALLAH WA WAISLAM SIO YEHOVA - MUNGU ALIYE UMBA KILA KITU


Ndugu msomaji,

Leo tutajifunza tofauti kati ya Allah wa Waislam na YEHOVA MUNGU ALIYE UMBA KILA KITU.

Qr. 15 au surat Hijr 30-39,
Basi Malaika wote pamoja walimsujududia, Isipokuwa Ibilisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu. (Mwenyezi Mungu) akasema: ewe Ibilisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?

Akasema: Hiwi mimi nimsujudiemtu uliyemuumba kwa udongo unaotoa sauti! Unaotokana na matope yenye sura.

Mwenyezi Mungu akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! Na hakika juu yako ipo laana mpaka siku ya malipo.
Akasema (Ibilisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula, mpaka siku maalum.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapo duniani na nitawapoteza wote.
Qr. 51 au Surat Adh-Dhaariyat 56 (sur aya upepo),
Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu

ALLAH NI MDOGO KINYUME NA YEHOVA MUMGU MKUU

Qr.92 au surat Al-Layl 1-3,
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
Naapa kwa usiku unapofunika! Na mchana unapodhihiri! Na kwa aliyeumba dume na jike! Kuapa kwa Mungu kuhusu viumbe

Qr. 91 au surat Ash-Shams 1-7 (sura ya Jua)
Naapa kwa jua na kwa mwangaza wake. Na kwa mwezi unapoliandama. Na kwa mchana unapolidhihirisha. Na kwa usiku unapolifunika. Na kwa mbingu na kwa Aliyezijenga. Na kwa ardhi na Aliyeitandaza. Na kwa nafsi (roho) na Aliyeitengeneza.

Qr. 92 au surat Al-Layl 1-3 (Usiku),
Naapa kwa usiku ufunikapo (kila kitu). Na kwa mchana uangazapo. Na kwa aliyeumba kiume na kike.

Hapa tunaona Allah Mungu anayeabudiwa na Waislamu anaapa kwa mbingu na kwa aliyezinjenga, kwa ardhi na aliyeitandaza. Je, huyo mtandazi wa ardhi na mjengaji wa mbingu ni nani? Qurani inaendelea kuhadithia hivi…

Qr. 45 au surat AL- Jathiyah 22 (kiyama/ kupiga magoti), Na mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi kwa haki…
Qr. 44 au surat Ad-Dukhan 7-8 (sura ya moshi)

Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, ikiwa mnayo yakini (basi yakinisheni haya) Hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye anahuisha na kufisha. Mola wetu na ni mola wa wazee wenu (wote) wa mwanzo (na mola wa kila kitu)

Hapa tunaona kuwa Allah kupitia Qurani anasema kuwa mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi na tena anasema hakuna aabudiwaye ila yeye.

Mjengaji wa mbingu na mtandazaji wa ardhi anajieleza hivi ……
Isaya 44:24

BWANA, mkombozi wako yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi, “Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote, nizitandaye mbingu peke yangu, niienezaye nchi. Ni nani aliye pamoja nami?”
Mungu wetu Yehova anasema mimi ninafanya vitu vyote.
(Soma Isaya 45:6-7, 11-12, Yeremia 27:5) Bila shaka Yehova ndiye muumbaji wa vitu vyote
JE Mungu Yehova aliapia vitu alivyoviumba kama Allah?

Isaya 45:22-23
Niangalieni MIMI mkaokolewe, Enyi ncha zote za dunia. Maana MIMI ni Mungu hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba, mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.

Waebrania 6:13-16
Kwa maana Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, Kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake. Akisema “Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza, Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo kwa kuyathibitisha.

Hapa tunaona Mungu wetu Yehova haapi kwa mtu wala vitu alivyoviumba kama Allah anavyoapa, bali Yehova anasema “Naapa kwa nafsi yangu”.Waweza pia kusoma jinsi Yehova alivyoapa kwa nafsi yake katika aya hizi;
Isaya 14:24 na Mwanzo 22:16

Hapa anayeapa ni Allah,
Hivi mtu anayeapa kwa mwingine anakuwa Mungu au mwanadamu?

Je, nani aliyeumba hapo?
Maana Allah anaapa katika aliyeumba, na kuumba ni moja kati ya sifa zake Yehova Mungu kumbe Allah hakuumba chohote!


ALLAH NI MUONGO!

Tukiyachunguza maandiko matukufu ya kiislamu yaani Quran na maandiko matakatifu yaani Biblia tutawapata hao wanaume wawili kuwa na utofauti wa mbali sana.

Tukianza na Quran hizi hapa kweli za wazi kabisa:
Allah wa quran anamkana na kumkataa Yesu Kristo kama si mwana wa Mungu yaani Yehova,
Qr. 19 au surat Maryam 35
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanau, Yeye ametakasika! Anapolihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
Qr. 112 au suratAl-Ikhlas 1-4 (sur aya utakaso)
Sema: Yeye ni Mwenyenzi Mungu mmoja (tu) Mwenyenzi Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyake vyote kwa kumuabudu na kumuomba na kumtegemea) Hakuzaa wala hakuzaliwa Wala hana anayefanana naye hata mmoja.
Kadiri ya aya hii Allah asema kuwa mungu hakuzaa wala hakuzaliwa wala hana mfano wa mtu au watu Yehova anasema hivi kuhusu mtu au watu……

Kila wanapoingizwa watu wajinga katika wavu wa huyo Mpinga-Kristoanayeitwa kwa jina ALLAH haya ndiyo maneno ya kukiri kumwabudu na kumtumikia:

Kwa kiarabu:
Ashihadu Allah ilaha inla ilah
Washihadu ana Muhamad rasuruhlah
Kwa kiswahili:
Nashuhudia kwamba hakuna Mungu isipokuwa Allah,
Na nashuhudia kwamba Muhammad (amani na rehema ziwe juu yake) nimtumishi wake na mjumbe

Biblia inasemaje ?
1Yohane 2:22-26,
Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. Kila amkanayeMwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.

Na hii ndiyo ahadi aliyoyuahidia, yaani, uzima wa milele.
Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.

Wakolosai 1:13-15,
Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana,mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

Yohane 3:16-17,
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoaMwanawe pekee, ili kila mtu amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Kwa maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.


Bila shaka Biblia Takatifu inamweka wazi ALLAH wa kila muislamu kama mwongo na Anti-Kristo ambaye waislamu wanamwita Dadjal bila ya wengi wao kujuwa kama ndiye wanaomwabudu

Sunday, May 1, 2016

KWANINI ALLAH HAWEZI KUWA NA MWANA BILA YA MKE?



Ndugu msomaji,
Leo nitawaeleza kwa kutumia aya kwanini Allah wa Waislam hana uwezo wa kuwa na Mwana bila ya kufanya tendo la ndoa, nikimaanisha kuwa na mke.
Hebu kwanza tuanze kusoma aya yake kutoka Surat AL An A'am iliyo teremk Makka:
Surat Al An A'am ayat 101. Yeye ndiye Muumbaji wa mbingu na ardhi bila ya ruwaza. Itakuwaje awe na mwana naye hakuwa na mke? Naye ndiye aliye umba kila kitu. Naye ni Mwenye kujua kila kitu.
Allah anaye dai kuumba kila kitu na kudai kuwa ni mjuzi wa kila kitu anatutaarifu katika Surat Al An A'am kuwa hawezi kuwa na mwana bila ya kufanya tendo la ndao kwa Mkewe Allat. Huu ni msiba mkubwa sana, maana iweje Mungu mwenye uwezo wa kufanya atakalo sasa anashindwa kuwa na mwana mpaka afanye tendo la ndoa?
Kama kweli Allah aliumba kila kitu, mbona Miti inaweza kuongezeka bila ya tendo la ndoa? http://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK9980/
Mbona Seli zako zinazaana au ongezeka bila ya kuwa na Seli Jike na Seli Dume. Wote tunafahamu hii "Mitosis" na stages zake Nne ambazo ni "Prophase" "Metaphase" "Anaphase" na "Telophase". Sasa Allah yeye anadai ndie aliye umba Seli za zetu tena zinazaliana bila ya kuwa an Seli Dume na Seli Jike, lakini cha kushangaza, Allah yeye hawezi kuwa na Mwana bila ya Mke, je, tunawezaje muamini huyu Allah mwenye udhaifu namna hii? https://ghr.nlm.nih.gov/primer/howgeneswork/cellsdivide
Sasa, tumsome Maryamu, je aliweza kuwa na Mwana bila ya kuwa na Mume?
Maajabu ya dunia, Maryamu anauwezo wa kuwa na Mwana bila ya Mume, lakini Allah hana uwezo wa kuwa na Mwana bila ya Mke. Hakika haya ni maajabu makubwa sana, ingawa Allah atadai eti alimpa yeye huo uwezo.
Kama ni kweli, je , kwanini Allah alishindwa kujipa huo uwezo yeye mwenyewe na aweze kuwa na Mwana bila ya tendo la ndoa?
Hebu tuanze kwa kusoma Surat I'mran iliyo teremka Madina:
Surat I’mran 45. Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).
Surat Im'mran 47. Maryamu akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Mungu akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa. http://www.quranitukufu.net/003.html
Maryam anamuuliza Allah, iweje niweze kuwa na Mwana bila ya Mume, Allah anadai kuwa, eti Mwenyezi Mungu hufanya apendalo, kwa kuliambia jambo, kuwa na LIKAWA. Sasa, kama huu uwezo wote ni wa Allah, kwanini anashindw akuutumia kwake yeye mwenyewe na kusema kuwa na Isa Akawa bila ya kuwa na Mama wala Baba?
Hakika Allah ni dhaif na kamwe hakuumba kitu chechote kile. Uthibitisho ni huu hapa, Quran 92 1. Naapa kwa usiku ufunikapo, 2 kwa mchana uingiapo, 3. na kwa aliye umba kiume na kike..
Hivi mtu anaye apa kwa mwengine anakuwa Mungu au binadamu? Je, nani kaumba hapo. Maana Allah anaapa kwa aliye umba, na kuumba ni sifa ya Mungu. Kumbe Allah hakuumba.
Kumbe ndio maana Allah alikiri kuwa, yeye hawezi kuwa na Mwana bila ya kuwa na Mke. Waswahili wanasema kuwa njia ya mwongo ni fupi. Leo tumesha mgundua Allah anaye apa kwa Aliye umba kiume na kike.
Kama Allah ndie aliye umba kila kitu,
1. Kwanini hawezi kuwa na Mwana bila ya Mke?
2. Kwanini Maryamu aliweza kuwa na Mwana bila Ya Mume?
3. Kwanini Allah anashindwa kutumia uwezo wake anao dai kumpa Maryamu aliye weza kuwa na Mwana bila ya Mume, kwa kupata Mwana bila ya MKE?
Hapa kuna maswali mengi sana ya kujiuliza kuhusu huyu Allah ambaye anaonyesha udhaifu mkubwa sana baada ya kushindwa kupata Mwana bila ya Mme.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
May 1, 2016

Saturday, April 30, 2016

MAJINA YA MUNGU WA BIBLIA


MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El‐Shaddai. Ni neno lenye majina mawili ndani yake. ‘El’ maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana itokanayo na neno ‘Shad’ yaani Titi (Ziwa) la mama anyonyeshaye.
Kutokana na ukweli kwamba, titi/ziwa la mama anyonyeshaye, linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa ya mama yake, humpa mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna vitamini, protini, wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto anachohitaji. Maziwa ya mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo, Waisraeli wanapomwita Mungu El‐Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama ziwa linavyo mtosheleza mtoto, vivyo hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’ kwetu. Halleluyah!
Hivyo, kila jina la Mungu, linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi anasema
“Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” (Zab 29:1‐ 2) Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina lake, kwakuwa lapendeza.(Zaburi 135:3).
Na Bwana Yesu alitufundisha kuanza sala namna hii;
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako tukutuzwe, hakafu Ufalme
wako uje hapa duniani.
Kwahiyo, unaweza pia kumsifu Bwana kwa majina yake. Majina ya Mungu, hueleza aidha sifa za Mungu au tabia za Mungu au Matendo makuu ya Mungu. Yafuatayo hapa chini, ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya Kiebrania, yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.
MAJINA YA MUNGU NA UKUU WAKE.
MUNGU akubariki sana na msingi wa somo letu uko katika Zaburi 83:18 inayosema ''Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.''
1: JEHOVAH ADONAI =MUNGU Mwenye Enzi Yote (Mwanzo 15:2-8 )
2: JEHOVAH EL – SHADAI =MUNGU Ututoshalezae MUNGU Mwenyenzi (Mwanzo 17:1)
3: JEHOAH EL-OHEENU =BWANA MUNGU Wetu (Zaburi 99:5,8,9)
4: JEHOVAH EL- GIBBOR= MUNGU Mwenye Nguvu ( Isaya 9:6-9)
5: JEHOVAH EL-OLAM =MUNGU wa Milele (Mwanzo 21:23)
6: JEHOVAH EL-OHEEKA= BWANA MUNGU Wako (Kutoka 20:2,5,7)
7: JEHOVAH EL-ELYON= MUNGU Aliye Juu Sana (Mwanzo 14:18)
8: JEHOVAH EL-OHIM =Muumbaji wa Milele (Mwanzo 1:1)
9: JEHOVAH SABAOTH =BWANA wa Majeshi (1 Samweli 1:3)
10: JEHOVAH TSIDKEMU= BWANA ni Haki Yetu (Yeremia 23:6)
11: JEHOVAH RAPHA= MUNGU Nikuponyae (Mwanzo 15:26)
12: JEHOVAH MEKADDISHKEM =BWANA Niwatakasae (Kutoka 31:13)
13: JEHOVAH ROHI =BWANA Mchungaji Wangu( Zaburi 23:1)
14: JEHOVAH JIREH= MUNGU Atupaye /Atoaye (Mwanzo 22:14)
15: JEHOVAH HOSEENU= BWANA Aliyetuumba (Zaburi 95:6)
16: JEHOVAH NISSI= BWANA ni Bendera(Beramu) yangu (Kutoka 17:15)
17: JEHOVAH SHALOM =BWANA ni Amani Yangu (Waamuzi 6:24)
18: JEHOVAH SHAMMAH= BWANA Yupo Hapa (Ezekiel 48:35).
MUNGU akubariki sana na kama hujaokoka yaani hujampokea BWANA YESU awe ni BWANA na MWOKOZI wa maisha yako ndugu hakikisha unampokea leo maana wokovu ni sasa.
Namna za kumshukuru, kumsifu, na kumwabudu Mungu wetu.
Kwahiyo, katika maisha yetu sisi, kama waumini, tunatakiwa kumpa Mungu wetu ibada, (kumshukuru, kumsifu na kumwabudu) kwasababu ya mambo yote hayo niliyoyataja. Tunatakiwa kumtukuza Mungu kwasababu ya sifa zake,
na kwasababu ya tabia zake, na matendo yake na fadhili zake na ahadi zake kwetu.
Sasa basi, hapa chini, nimekuwekea njia kuu tatu ambazo unaweza kumsifu na kumtukuza Mungu kwazo. Utengapo muda wa kwenda mbele za Mungu, unaweza kutuia njiia kuu zifuatazo; Kumtukuza Mungu kwa,
1. Kumwimbia nyimbo za kumsifu na kuwabudu
2. Kumweleza au kusimulia kwa maneno
3. Kumtolea Mungu sadaka na dhabihu
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 30, 2016

ALLAH SIO JINA LA MUNGU (SEHEMU YA PILI)


Ndugu msomaji,
Katika mada iliyo pita, tumethibitisha kuwa Mungu wa kwenye Biblia ana jina/majina na Allah wa kwenye Quran naye ana majina 99 kama ilivyo shahidiwa kwenye vitabu vyake angalia link hii:http://www.islamicity.com/mosque/99names.htm .
ZAIDI YA HAPO, NIMETHIBITISHA KUWA ALLAH SIO JINA BALI NI WADHIFA TU KAMA ILIVYO "RAIS" "MFALME" nk. Hayo maneno "Rais", "Mfalme" sio majina bali hao wenye huo wadhifa wanayo majina yao na ndio maana huwa tunasema Rais "fulani" kasema hivi au Mfalme fulani kasema hivi na vile, Lazima tuweke jina la huyo Rais au Mfalme katika maelezo yako.
Kwenye hii mada tunaendelea kumuuliza Allah mswali na kuwauliza Waislam maswali kuhusu huyu Allah mwenye jina lisilo tambulika na au halipo kwenye Taurat, Zaburi, na Injili.
SASA TUANZE MADA YETU:
Waislam hupenda kuanza kusema maneno haya katika hotuba zao: Nukuu: "KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU"
Hayo maneno yanatuambia kuwa "Mwenyezi Mungu" anaye tamkwa na Waislam ana Jina, kama sio "majina".
Swali la kwanza: Kwa ndugu zetu Waislam ni hili hapa. "Mnaweza tuambia hilo jina la Mwenye Mungu ambaye ni mwingi wa Rehema na mwenye kurehemu ni lipi" Tafadhali tujibuni kwa kutumia aya.
Swali la pili kwa Waislam:
Kama "Allah" ni jina la Mwenyezi Mungu wa Waislam, tunaomba mtupe aya kutoka Quran yenu ambayo Mwenyezi Mungu ambaye ni mwingi wa rehema na mwenye kurehemu anasema kuwa "ALLAH" ni jina langu.
Ndugu Waislam, hakuna haja ya kuchukia wala kutuletea lugha chafu kama ilivyo utamaduni wenu baada ya kusoma maswali yetu mawili ya kwanza ambayo yameenda shule. Kitu cha muhimu ni nyie Waislam mtuletee aya ili tufahamu JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEM ambaye mnamtaka kila mnapo anza khutbah zenu Msikitini.
LAKINI KILA NINAPO ISOMA BIBLIA, MUNGU WA KWENYE BIBLIA ANAJITAMBULISHA KWA MAJINA YAKE KITU AMBACHO NI TOFAUTI NA ALLAH WA KWENYE QURAN AMBAYE MPAKA HII LEO HATUJUI JINA LAKE NI NANI.
Kutoka 3: 13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini? 14Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO; akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenituma kwenu.
Nilipo endelea kuisoma Biblia Takatifu ambayo imekamilika, Mungu alimwabia Musa katika Kutoka 6:2, 3Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao. https://www.wordproject.org/bibles/sw/02/6.htm#0
Ndugu msomaji, hata wewe ambaye ni binadamu unalo jina au majina, lakini kitu cha kushangaza Allah ambaye mwenye Majina 99 tofauti kabisa na Mungu wa Musa na Ibrahim na Daudi na Yesu, yeye ameweka "aina za nomino" na kudai hayo ni majina yake. Huu ni msiba mkubwa sana kwa Waislam.
Kusoma juu ya majina tofauti tofauti ya Mungu kunaweza kutusaidia katika kutambua jinsi Mungu alivyo. Baadhi ya Majina yenyewe ni kama yafuatayo:
Elohim – Mwenye nguvu, mtakatifu (Mwanzo 1:1)
Adonai – Bwana, ikiashiria uhusiano wa mtumishi na bwana wake (Kutoka 4: 10, 13)
El Elyon – Aliyetukuka, mwenye nguvu kupita wote (Mwanzo 14:20)
El Roi – Mwenye nguvu kupita wote na aonaye (Mwanzo 16:13)
El Shaddai – Mwenyezi Mungu (Mwanzo 17: 1)
El Olam – Mungu wa milele (Isaya 40:28)
Yahweh – BWANA “NDIMI”, yenye maana ya Mungu wa milele adumuye kwa uwezo wake mwenyewe (Kutoka 3:13, 14).
Unaona raha iliyo katika Ukristo? Mungu wetu anajitambulisha kwa Majina yake ambayo yanaamanisha na au yatatufundihsa jinsi Mungu alivyo.
Sasa nategemea kuwa umeanza kuelewa kuwa Allah sio jina la Mungu bali ni kitu kingine kabisa na wala hana Uhusiano wowote ule na Mwenyezi Mungu ambaye ni Yehova, Mimi Niko Ambaye Niko wa kwenye Biblia.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 30, 2016

Friday, April 29, 2016

ALLAH SIO JINA LA MUNGU


Ndugu msomaji,
Waislam wamekuwa wakidanganya kila siku kuwa eti Mungu anaitwa Allah. Sasa leo nataka tujadili kwa amani na upendo hapa kuhusu huyu ALLAH.
Allah sio jina bali wadhifa tu. Ndio maana Allah AMEKIRI KUWA YEYE ana majina 99, ANGALIA HAPA KWA USHAHID http://www.islamicity.com/mosque/99names.htm.
Kati ya hayo majina 99 hakuna jina la Yehova, JAHAWEH, MIMI NIKO nk ingawa Waislam kila kukicha wanadai eti Mungu wa Musa ni huyo Allah au Mungu wa Daudi ni huyo Allah. Ili kuthibitisha ninacho sema, Mungu wa kwenye Biblia kasema hivi kwenye Yeremia.
Mungu mwenyewe alisema: “Watajua kwamba jina langu ni Yehova.” (Yeremia 16:21)
Sasa, wote tunafahamu kuwa Biblia ilikuja miaka 650 kabla ya Quran na kwenye hiyo Biblia Mungu alisema kuwa yeye jina lake ni "MIMI NIKO", "YEHOVA" n.k. LAKINI CHA AJABU, Allah HAKUSEMA KUWA YEYE NI "MIMI NIKO" AU "YEHOVA" kwenye hayo majina yake 99.
Je, Allah ni nani huyu, maana teyari anapinga na YEHOVA wa kwenye Yeremia 16 aya 21 na AMEKATAA kuyatumia hayo majina ya Mungu wa kwenye Biblia?
Zaidi ya hapo, wapi Mungu anasema kwenye Taurat kuwa jina lake ni Allah?
Wapi Mungu anasema kwenye Zaburi kuwa Jina lake ni Allah?
Wapi Mungu anasema kwenye Injili kuwa Jina lake ni Allah?
Haya ni maswali rahisi sana kwa Waislam na hayahitaji jazba katika kuyajibu zaidi ya wao watuletee aya kutoka Taurat au Zaburi au Injili kuwa Mungu anasema kuwa yeye jina lake ni Allah.
Wakishindwa tuletea basi watuletee aya kutoka Quran ambayo Allah anasema kuwa yeye jina lake ni Yehova au Yahawe au Mimi Niko.
Leo ningependa tujadili kwa kutumia aya na kwa upendo.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 29, 2016

Thursday, April 28, 2016

ALLAH KWA KIEBRANIA MAANA YAKE NI LAANA “CURSE”

Ndugu msomaji,
Je, hili limetokea kwa bahati mbaya?
Isaya 24: 6 Ndiyo sababu laana [“alah”] imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu.
Huu uvumbuzi ulieleweka baada ya kuangalia neno la Kiebrania la “LAANA –CURSE”- linatamkwa kwa Keibrania “alah” sawa sawa na Allah wa kwenye Quran. Nilifanya uchunguzi zaidi kuhusu na kulinganisha neno la Kiebrania “ALAH” na la Kiarabu Allah; yote yapo sawa, isipokuwa tofauti ndogo ya ongezeko la “L” kama ifuatavyo:
אלה , alah (“curse = laana” in Hebrew) na الله , Allah (“mungu katika Kiislamu”), wakati:
א = aleph (Heb) ni sawa sawa na ا = alif (Arab), au “A” katika Kiingereza
ל = lamed (Heb) ni sawa sawa na ل = lam (Kiarabu), au “L” katika Kiingereza; “Allah” ina “L” mbili katika Kiarabu na kiislamu
ה = heh (Heb) ni sawa na ه = ha (Kiarabu), au “H” katika Kiingereza
Inashangaza sana neno la Kiebrania la “laana” na neno la Kiarabu la “Allah” sio tu yanatamkwa vilevile bali yana maana ileile.
Kuna wazo linaitwa “the law of first occurrence” (labda lipo zaidi kama sharia Fulani) ambapo unapo weza kuona neno Fulani huwa linaweza kukusaidia katika na au kivipi neno la Mungu lina maanisha.
Katika kuchunguza “curse –laana” (אלה , alah), neno hilo limeonekana katika Hesabu 5 ya ‘the adultery test’, Njia ya Mosaiki ya kuangalia ukweli kuhusu mume au mke kama una kosa au la.
Kuna mwanzo wa neno “curse-laana” katika Kiebrania (arar); lilitumika kwa mara ya kwanza katika bustani ya Edeni Mwanzo Mlango wa 3 aya ya 14 na 15:
Mwanzo 3: 4 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umeLAANIWA wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; 15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.
KWA MARA YA KWANZA “laana” ilitumiwa kwa Nyoka ambaye ni Shetani; labda tuangalie kwa makini, kama ALLAH inamaanisha LAANA katika Kiebrania, naamini sio kosa tukiendelea kumhusisha Allah wa Waislam katika hili neno LAANA.
Strong’s Concordance namba 422 nayo inakiri kuwa neno la Kiebrania lenye maana ya laana ni ALAH. http://biblehub.com/hebrew/422.htm

Wednesday, April 27, 2016

JE, KUUA AU KUJIUA NI DHAMBI?


Ndugu msomaji,
Nimepata maswali kadhaa kwenye private messaging kuhusu kuua au kujiua.
Watu wanataka kufahamu kuwa, je, mtu akijiua atakwenda wapi?
KOSA LA KUUA AU KUJIUA
Kulingana na Biblia, kujiua si kigezo cha kukufanya uingie mbinguni bali ni kigezo cha kukuingiza Jehannam. Mtu asiyeokoka akijiua huwa amejipeleka moja kwa moja katika ziwa la moto. Mtu huyu atapelekwa huko kwa kukataa kwake wokovu kupitia Yesu, Biblia inasema kuwa USIUWE, Biblia inasema katika Yohana 10:10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Katika Yohana 10 aya 10 tumesoma kuwa Yesu amekuja ili wewe uwe na uzima.
Biblia inataja watu wanne waliojiua: Sauli (samueli wa kwanza 31:4), Ahithofeli (samueli wa pili 17:23), Zimri (wafalme wa kwanza 16:18), na Yuda (Mathayo 27:5). Kila mmoja wao alikuwa mwovu na mwenye dhambi. Biblia inachukulia kujiua sawa na kuua – na hivyo ndivyo ilivyo – kujiua mwenyewe. Mungu ndiye ni aamue lini na vipi mtu afe. Kuchukua jukumu hilo mkononi mwako kibiblia ni kufuru kwa Mungu.
KUUHESHIMU UHAI
Mungu alionaje kuuawa kwa Abeli?
Mungu anataka tuuheshimu uhai wetu wenyewe na wa wengine. Kwa mfano, katika siku za Adamu na Hawa, mwana wao Kaini alimkasirikia sana Abeli, ndugu yake mdogo. Mungu alimwonya Kaini kwamba hasira yake ingeweza kumfanya atende dhambi nzito. Kaini alipuuza onyo hilo. ‘Alimshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.’ (Mwanzo 4:3-8) Mungu alimwadhibu Kaini kwa kumuua ndugu yake.—Mwanzo 4:9-11.
Katika Sheria ya Musa, Mungu alikaziaje maoni yanayofaa kuhusu uhai?
Maelfu ya miaka baadaye, Mungu aliwapa watu wa Israeli sheria zilizowasaidia kumtumikia kwa njia inayompendeza. Kwa sababu sheria hizo zilitolewa kupitia nabii Musa, nyakati nyingine zinaitwa Sheria ya Musa. Mojawapo ya sheria hizo inasema: “Usiue.” (Kumbukumbu la Torati 5:17) Hilo liliwaonyesha Waisraeli kwamba Mungu anathamini uhai wa wanadamu na kwamba wanadamu wanapaswa kuuthamini uhai wa wengine.
Je, Biblia inasemaje juu ya Mkristo akijiua?
Kwa kawaida watu hawapendi kufa, lakini watu fulani huhatarisha uhai wao ili kujifurahisha. Kwa mfano, watu wengi huvuta sigara, hutafuna miraa, au kutumia dawa za kulevya ili kujisisimua. Vitu hivyo huudhuru mwili na mara nyingi husababisha kifo. Mtu mwenye mazoea ya kutumia vitu hivyo hauoni uhai kuwa mtakatifu. Mazoea hayo ni machafu machoni pa Mungu. (Waroma 6:19; 12:1; 2 Wakorintho 7:1) Ili kumtumikia Mungu kwa njia inayompendeza, lazima tuache mazoea hayo. Ingawa huenda ikawa vigumu sana kuacha mazoea hayo, Yehova anaweza kutupa msaada tunaohitaji. Naye huthamini tunapojitahidi kuuona uhai wetu kuwa zawadi yenye thamani kutoka kwake.
Hii si kwamba kujiua ni dhambi ndogo machoni pa Mungu. Kulingana na Biblia kujiua ni kuua na kila mara ni kosa.
KUHESHIMU DAMU
Mungu ameonyeshaje kwamba kuna uhusiano kati ya uhai na damu?
Baada ya Kaini kumuua Abeli ndugu yake, Mungu alimwambia Kaini: “Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.” (Mwanzo 4:10) Mungu alipotaja damu ya Abeli, alikuwa akizungumzia uhai wa Abeli. Kaini alikuwa amekomesha uhai wa Abeli, na sasa ilikuwa lazima Kaini aadhibiwe. Ilikuwa kana kwamba damu ya Abeli, au uhai wake, ulikuwa ukimlilia Mungu ili haki itekelezwe. Uhusiano kati ya uhai na damu ulionyeshwa tena baada ya Mafuriko ya siku ya Noa. Kabla ya Mafuriko hayo, wanadamu walikuwa wakila matunda, mboga, nafaka, na kokwa tu. Baada ya Mafuriko, Mungu alimwambia Noa na wanawe: “Kila mnyama anayetembea ambaye yuko hai anaweza kuwa chakula chenu. Kama nilivyowapa mimea ya majani, nawapeni hao wote.” Hata hivyo, Mungu alitoa amri hii: “Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake [au, uhai wake]—damu yake—msile.” (Mwanzo 1:29; 9:3, 4) Ni wazi kwamba Yehova anahusianisha uhai na damu ya kiumbe.
MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA
Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu. —Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11.
Ni kosa kutoa mimba kwa sababu uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa ni wenye thamani machoni pa Mungu.—Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3.
Tunaonyesha kwamba tunaheshimu uhai kwa kutouhatarisha na kutokula damu. —Kumbukumbu la Torati 5:17; Matendo 15:28, 29.
Wewe umemwamini Bwana Yesu Kristo? Angalia vile Yohana 3:36 inasema, una MAISHA YA MILELE! Sio “inawezekana” ama “natumaini hivyo” – LAKINI UNAO WOKOVU – UMEOKOKA!
Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake." Yohana 3:36
Rafiki, kama umeomba maombi haya na umempokea Yesu Kristo – UMEOKOKA! Umefanya yale Mungu anasema ufanye – NA MUNGU HAWEZI KUSEMA UONGO! Katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, ASIYEWEZA KUSEMA UONGO aliuahidi tangu milele. Tito 1:2
Tunapaswa kumshukuru Mungu sana kwa sababu ya kutupa zawadi ya uhai kwa upendo! Je, hilo halipaswi kutuchochea kuwaambia wengine kuhusu pendeleo la kupata uzima wa milele kwa msingi wa imani katika dhabihu ya Yesu? Ikiwa tunathamini uhai wa wanadamu wenzetu kama Mungu anavyouthamini, tutachochewa kuwahubiria kwa hamu na bidii. (Ezekieli 3:17-21) Tukitimiza jukumu hilo kwa bidii, tutaweza kusema kama mtume Paulo alivyosema: “Mimi ni safi kutokana na damu ya watu wote, kwa maana sikuepuka kuwaambia ninyi mashauri yote ya Mungu.” (Matendo 20:26, 27) Kuwahubiria watu kumhusu Mungu na makusudi yake ni njia bora ya kuonyesha kwamba tunathamini sana uhai na damu.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 27, 2016

USHUHUDA MKUBWA WA KHALIL MUISLAM MWENYE SIASA KALI AMBAYE SASA NI MKRISTO









Khalil alianza kuikariri Kurani alipokuwa bado mdogo sana na akaendelea na hali hiyo aliyoiita kuwa ni upendo kwenye neno la Mungu. Kwa kadri alivyoendelea kukua, akaanza kusoma vitabu vya kiislamu hasa vile vilivyofafanua Kurani. Alipoendelea kuisoma Kurani na alichanganua walio Waislamu kufuatana na mafundisho hayo kutoka kwa wale wasio Waislamu. Hatimaye aliafiki hata wazazi wake kuwa makafiri. Vitu vidogo vidogo kama vile mwanamke kutokuvaa hijabu kungemfanya mtu kutokuwa Mwislamu wa kweli kulingana na vile alivyoelewa Kurani. Kama mwanaume asingezifuga ndevu zake hata zikakua angeeleweka kuwa yeye pia si Mwislamu. Alizingatia kuwa Wakristo ni maadui zake wakubwa, na hivyo akaanza kujihusisha na mashambulizi dhidi ya Wakristo na kanisa kwa jumla. Kikundi hicho kilijitoa kuipindua serikali ya Misri na kuunda serikali ya kiislamu yenye msimamo mkali. Walimwandikisha kuwa mpiganavita hata kumpandisha cheo na kumchagua kuwa kiongozi wa mahali pale. Kikundi chake kilijihusisha na utekaji nyara kwa mwandishi mashuhuri wa kiislamu asiye na msimamo mkali aliyethubutu kuukosoa kikundi cha Uislamu.
Hatimaye mamlaka ilimtia mbaroni Khalil na wenzake wengi wa kikundi chake. Huko gerezani alikaa miaka miwili, alipata mateso yenye maumivu makali, na mara alipoachiwa huru, alienda Yemen pamoja na wenzake washika dini sana. Kutoka kwenye kituo hiki waliendelea na mipango yao ya kupindua serikali ya Misri kwa silaha.
Hata hivyo mipango yao iligundulika na mamlaka ya eneo lile. Wengi wao walikamatwa tena. Hata hivyo njia ya mapinduzi ya jeshi haijaachwa kamwe. Waliporudi tena Misri walihitaji kukanusha shughuli zao za awali. Siku moja wakiwa Kairo walisoma makala gazetini juu ya kukamatwa kwa Wakristo! Khalil na kikundi chake waliamua kwamba sasa “imepitwa na wakati” kufanya kazi kutetea Uislamu. Hata hivyo katika uchache wao, waliamua kuwa, mapambano yao sasa yangechukua sura mpya kwa kutumia akili. Utafiti ufanywe wa kuandika kitabu kwa kuthibitisha kuwa Mohammad ndiye nabii wa kweli wa Mungu, na kwamba Biblia ya Wakristo na ya Wayahudi ni maandiko yaliyobatilishwa! Khalil alichaguliwa na shehe wake aliyekuwa Kiongozi wa kikundi chake cha kiislamu, ili kufanya utafiti na baada ya hapo aandike kitabu. Kwanza alikataa katakata, kisha aliazimu kuifanya hii kazi, ambayo baadaye aliielezea kuwa katika kazi zote alizowahi kuzifanya maishani mwake kazi hii ilikuwa ni “kazi iliyojaa maudhi!”
Khalil alipomaliza kusoma Biblia, na kulinganisha bayana maneno aliyosoma katika vitabu mbalimbali vya kiislamu, alishangaa sana alipogundua Biblia ilikuwa haina makosa na haijabatilishwa. Badala yake alishangaa juu ya mafundisho ya Biblia yaliyohusu msamaha na upendo usio na kosa, ulioonekana katika maisha na maneno ya Yesu. Alishangazwa hasa aliposoma kuwa Yesu mwenyewe aliwaonya wafuasi wake juu ya mateso na jinsi ilivyotokea miaka elfu mbili baadaye, vilevile ambavyo Yesu mwenyewe alikuwa amesema ingelitokea. Kusoma kwake kulimsaidia kuelewa kwa nini Wakristo wa Misri hawakuwa wakilipiza kisasi kabisa dhidi ya Waislamu na kwa nini kusamehe na kusahau kwao ilikuwa rahisi. Jinsi ambavyo alichukia kuisoma Biblia, ndivyo alivyojisikia kuupenda ujumbe na mafundisho yake.
Hata hivyo alikuwa na kazi ya kufanya, na aliendelea na uamuzi wa kutoka ndani kuthibitisha kuwa Yesu si Mungu, na hakuwahi kusulibiwa. Aliposoma Kurani kwa nia au lengo lake hili, alikusanya sifa na majina ya Mungu jinsi zilivyotajwa katika Kurani. Kisha akatafiti zaidi juu ya sifa za Yesu katika Kurani. Kulingana na Kurani, Mungu ndiye mwumbaji, mponyaji, mfadhili, mmoja pekee anayeweza kufufa wafu, mmoja pekee anayetenda miujiza, mmoja pekee atoaye hukumu ya haki na mambo kama hayo. Kwa mshangao Khalil aligundua kwamba huu ni mtazamo ule ule ambao Kurani inamtaja Yesu (Isa) ikimthibitishia kwamba, Yesu na Mungu ndiye ni yuleyule mmoja.
Khalil alipatwa na mashaka maishani mwake kiasi kwamba aliweza kujisikia mnyonge sana. Aliupenda sana Uislamu na kuamini kuwa njia pekee ya kumfikia Mungu ilikuwa ni kupitia Mohammad. Lakini ikiwa Yesu na Mungu ni yuleyule mmoja, sasa Mohammad ndiyo yupi na ni njia ipi ya kwendea mbinguni? Siku moja shehe wake bila ya kumtaarifu ujio wake aliamua kumtembelea nyumbani kwake, na hapo ndipo alipogundua kuwa utafito wote ambao Khalil alikuwa ameufanya ni kuhusu Uungu wa Yesu! Yaani kuwa Kurani si neno la Mungu n.k. Kwa kifupi ni kwamba hakukiamini kile alichokisoma kwa Khalil.
Akamtahadharisha Khalil kuwa angeliweza kumwua endapo angemwambia Mwislamu yeyote kile alichokiandika. Pia akasema kuwa kuanzia pale alianza kumhesabu kuwa ni kafiri!
Hata hivyo, Khalil, hakuweza kuacha msimamo kwamba Ukristo ulikuwa ndiyo njia sahihi. Ili ajifunze zaidi aliamua kujiunga na kanisa. Na kwa vile alivyojulikana kuwa ni mtu mwenye tabia mbaya, mwenye msimamo mkali wa kiislamu, hakuna hata mmoja aliyemwamini. Kila mtu alikataa kukutana naye, hata na wachungaji! Jambo hilo lilimsikitisha sana, na hata akafikiri kwamba pengine aliamua kimakosa, pengine imani ya kikristo haikuwa ndiyo njia pekee ya kufika mbinguni. Hata hivyo sauti ndani yake ilimwambia kwamba asiwaangalie watu.
Siku moja alipokuwa akijaribu kupiga simu kwenye mgahawa, vitu vyake alivyokuwa navyo pale viliibiwa. Begi lake lililokuwa limebeba karatasi zake zote alizokuwa amefanya utafiti, Biblia yake na kitambulisho chake. Alishikwa na hofu kwa sababu mambo yote aliyokuwa ameyaandika yangeonekana ni maeneo ya kumkufuru Mungu. Alikimbilia nyumbani, akiwa amejaa mahangaiko na hofu. Aliporudi chumbani mwake, alianza kutubu kwa yale yote aliyokwisha kuyafanya na hata alifikiri kuwa Mungu alikuwa akimwadhibu kwa kuthubutu kufikiri kwamba Mohammad hakuwa ametumwa na Mungu na kwamba hata Kurani yenyewe haikuwa neno la Mungu. Alitubu, akatawadha au kunawa kulingana na sheria za kiislamu, kisha akachukua zulia lake ili aombe, lakini hata hakuweza kupiga magoti yake, wala hata kufungua mdomo wake kusema japo neno moja toka kwenye Kurani. Alikaa chini na kusema: “Mungu unajua kabisa kwamba ninakupenda, na ninajua kabisa kwamba unanitaka mimi nipite katika njia iliyo sahihi. Mungu nashindwa kuendelea kukupinga. Yale yote niliyoyafanya nilikuwa ninajaribu kukupendeza wewe. Tafadhali sana ninaomba unitoe nje ya giza hili nilimo.” Usiku ule Khalil alilala usingizi mnono ambao kwa miaka mingi hakuwa amelala hivyo. Katika ndoto alimwona mtu aliyemjia na kumwambia kwamba ni yeye ambaye Khalil amekuwa akimtafuta. Hata hivyo Khalil hakujua mtu huyo alikuwa ni nani. Mtu yule alimwambia kuwa, aangalie kwenye kitabu, yaani Biblia. Khalil alisema kuwa Biblia na karatasi zote zimepotea, ndipo mtu yule alimjibu na kumwambia: “Kitabu hakiwezi kupotea kamwe. Amka na ufungue kabati na utaiona, na zile karatasi zako zingine zitarudishwa kwako mwishoni mwa wiki.”
Khalil aliamka toka usingizini akafungua kabati yake. Biblia yake ileile ilionekana ndani ya kabati kwenye shelfu. Kwa kujua kuwa amemwona Yesu aliharakisha na kwenda chumbani kwa mama yake, akamwamsha, kisha akamwomba msamaha, kwa jinsi alivyokuwa mkali na alivyozoea kuitendea familia kwa miaka yote iliyopita. Kutafuta suluhu hakuishia hapa kwa familia yake tu, bali mara kulipopambazuka siku ileile tu asubuhi, Khalil alienda mitaani akiwasalimu marafiki na watu wengine. Hata aliweza kuwatafuta wafanyabiashara Wakristo wale ambao aliwahi kuwaibia, au hata kuwatendea vibaya, hao wote aliwaomba msamaha pia.
Miezi iliyofuata Khalil aliendelea kuimarika katika imani yake mpya. Polepole alianza kupata mazoea na matumaini na Wakristo waliokaa pale. Na alianza kushirikiana kanisani. Alibatizwa na akaendelea kusimama imara aliposhambuliwa kimwili na kutishiwa maisha yake. Maana alijisikia kana kwamba hakukuwa na bei yoyote kubwa ambayo ingeliweza kulipa kwa Yeye Yule aliyetoa kila kitu kwa ajili yake.
 VIDEO: SEHEMU YA PILI:
https://www.youtube.com/watch?v=GKwcJuf3jJ4&spfreload=5

Tuesday, April 26, 2016

KUMBE ALLAH HAJATAKASIKA


ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUKIRI KUWA YEYE NA UISLAM HAWAJATAKASIKA
Bila ya kupoteza muda tuanze kwa kusoma SURAT AL-AH'ZAB
(Imeteremka Madina). Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani , alie fanya tarjuma hii ni Mzalendo wa Zanzibar, aliezaliwa 13 January 1919, akapata mafunzo ya dini kwa baba yake Sheikh Muhsin bin Ali na kwa wanazuoni wengineo wa Afrika ya Mashariki. Pia Sheikh Ali amesoma ilimu ya zaraa katika Chuo Kikuu cha Makerere (Makerere University) huko Uganda.
MAANA YA KUJITAKASA
a. Ni kujiweka wakfu kwa ajili ya Mungu
b. Ni kuamua kwa dhati kabisa kuchukua hatua ya kuacha kutenda dhambi, kuishi katika dhambi na pia kuchukua hatua ya kuondoa kila aina ya dhambi uliyo nayo.
ALLAH ANAOMBA MUMTAKASE ASUBUHI NA JIONI. JE, ALLAH ALICHAFUKA LINI MPAKA AOMBE KUTAKAWASA?
((Enyi mlioamini! Mdhukuruni Allaah kwa wingi wa kumdhukuru)) ((Na mtakaseni asubuhi na jioni)) ((Yeye na Malaika Wake ndio Wanakurehemuni ili kukutoeni gizani mwende kwenye nuru. Naye ni Mwenye kuwarehemu Waumini)) ((Maamkiano yao siku ya kukutana Naye yatakuwa: Salama! Na Amewaandalia malipo ya ukarimu)) [Al-Ahzaab: 42-44]
Al-Ahzaab 33: 41-42,
41. Enyi mlio amini! Mdhukuruni Mwenyezi Mungu kwa wingi wa kumdhukuru.
42. Na mtakaseni asubuhi na jioni. http://www.quranitukufu.net/033.html
Jamani eeeh, Allah wa dini ya Uislam anaomba kutakwaswa, sasa huyu Allah alichafuka lini?
Ndugu Waislam, mnaweza tuambia ni uchafu gani mnao taka kuutakasa?
SWALI: ALLAH ALICHAFUKA LINI?
ALLAH ANAMUOMBA MUHAMMAD AMSAFISHIE DINI. KUMBE DINI YA ALLAH INATAKIWA KUSAFISHWA
Sema (Ewe Muhammad): Hakika Mimi nimeamrishwa nimuabudu Mwenyezi Mungu, kwa kumsafishia Dini Yeye ( tu ). Na nimeamrishwa niwe wa kwanza wa wale ambao ni Waislamu ( kujisalimisha kwake ). S. 39:11-12 Pickthall http://www.quranitukufu.net/039.html
Huu ni msiba mwingine kwa Allah, sasa kwenye Surah ya 39 aya 11-12 Allah anamwomba Muhammad amsafishie dini ya Uislam, sasa tuwaulize Waislam. KWANI UISLAM ULICHAFUKA LINI MPAKA ALLAH AMUOMBE MUHAMMAD KUMSAFISHIA DINI?
Waislam, tuleteeni aya ambayo inathibitisha kuwa Muhammad aliisafisha dini ya Allah?
Waislam, kwanini Allah alimuomba Muhammad kuisafisha dini?
Kwanini Allah alishindwa kuisafisha dini yake?
Kwanini ALLAH ALIOMBA KUTAKASWA?
SASA TUSOME BIBLIA TAKATIFU:
Hesabu 8"17-18 '' Kwa kuwa wazaliwa wa kwanza wote katika wana wa Israeli ni wangu, wa wanadamu na wa wanyama; siku hiyo niliyowapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri niliwatakasa kwa ajili yangu mwenyewe. Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote walio katika wana wa Israeli.''
KATIKA BIBLIA, HESABU 8 17-18 tunasoma kuwa Mungu ndie anaye watakasa watu kinyume na Allah wa Quran anaye omba kutakaswa na watu wenye dhambi. Ndugu msomaji, huu ni MSIBA MKUBWA SANA KWA DINI YA MUHAMMAD YENYE ALLAH ANAYE OMBA ATAKASWE NA WATENDA DHAMBI.
Je, WAISLAM, mnaweza tuambia njia ambayo mnatumia kumtakasa Allah?
2 Nyakati 29:15-17 ''Wakawakusanya ndugu zao, wakajitakasa, wakaingia, kama alivyoamuru mfalme kwa maneno ya BWANA, ili waisafishe nyumba ya BWANA. Nao makuhani wakaingia nyumbani mwa BWANA, katika mahali pa ndani, ili waisafishe, wakatoa uchafu wote waliouona hekaluni mwa BWANA, wakautupa nje uani mwa nyumba ya BWANA. Walawi wakautwaa, ili wauchukue nje mpaka kijito cha Kidroni. Basi wakaanza kutakasa siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, hata siku ya nane ya mwezi wakafika katika ukumbi wa BWANA; wakaitakasa nyumba ya BWANA katika muda wa siku nane; wakamaliza siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza.''
Umesoma kwenye Nyakati kuwa anaye takiwa kufanyiwa utakaso ni binadamu na sio MUNGU, Lakini kwenye Quran ya Waislam, tumesoma kuwa Allah anaomba kutakaswa Al-Ahzaab 33: 42. Na mtakaseni asubuhi na jioni.
JE, ALLAH ALICHAFUKA LINI? TENA ANATAKA KUTAKASWA ASUBUHI NA JIONI.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 23, 2016

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW