Tuesday, May 3, 2016

ALLAH WA WAISLAM SIO YEHOVA - MUNGU ALIYE UMBA KILA KITU


Ndugu msomaji,

Leo tutajifunza tofauti kati ya Allah wa Waislam na YEHOVA MUNGU ALIYE UMBA KILA KITU.

Qr. 15 au surat Hijr 30-39,
Basi Malaika wote pamoja walimsujududia, Isipokuwa Ibilisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu. (Mwenyezi Mungu) akasema: ewe Ibilisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?

Akasema: Hiwi mimi nimsujudiemtu uliyemuumba kwa udongo unaotoa sauti! Unaotokana na matope yenye sura.

Mwenyezi Mungu akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! Na hakika juu yako ipo laana mpaka siku ya malipo.
Akasema (Ibilisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula, mpaka siku maalum.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapo duniani na nitawapoteza wote.
Qr. 51 au Surat Adh-Dhaariyat 56 (sur aya upepo),
Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu

ALLAH NI MDOGO KINYUME NA YEHOVA MUMGU MKUU

Qr.92 au surat Al-Layl 1-3,
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
Naapa kwa usiku unapofunika! Na mchana unapodhihiri! Na kwa aliyeumba dume na jike! Kuapa kwa Mungu kuhusu viumbe

Qr. 91 au surat Ash-Shams 1-7 (sura ya Jua)
Naapa kwa jua na kwa mwangaza wake. Na kwa mwezi unapoliandama. Na kwa mchana unapolidhihirisha. Na kwa usiku unapolifunika. Na kwa mbingu na kwa Aliyezijenga. Na kwa ardhi na Aliyeitandaza. Na kwa nafsi (roho) na Aliyeitengeneza.

Qr. 92 au surat Al-Layl 1-3 (Usiku),
Naapa kwa usiku ufunikapo (kila kitu). Na kwa mchana uangazapo. Na kwa aliyeumba kiume na kike.

Hapa tunaona Allah Mungu anayeabudiwa na Waislamu anaapa kwa mbingu na kwa aliyezinjenga, kwa ardhi na aliyeitandaza. Je, huyo mtandazi wa ardhi na mjengaji wa mbingu ni nani? Qurani inaendelea kuhadithia hivi…

Qr. 45 au surat AL- Jathiyah 22 (kiyama/ kupiga magoti), Na mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi kwa haki…
Qr. 44 au surat Ad-Dukhan 7-8 (sura ya moshi)

Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, ikiwa mnayo yakini (basi yakinisheni haya) Hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye anahuisha na kufisha. Mola wetu na ni mola wa wazee wenu (wote) wa mwanzo (na mola wa kila kitu)

Hapa tunaona kuwa Allah kupitia Qurani anasema kuwa mwenyenzi Mungu ameziumba mbingu na ardhi na tena anasema hakuna aabudiwaye ila yeye.

Mjengaji wa mbingu na mtandazaji wa ardhi anajieleza hivi ……
Isaya 44:24

BWANA, mkombozi wako yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi, “Mimi ni BWANA, nifanyaye vitu vyote, nizitandaye mbingu peke yangu, niienezaye nchi. Ni nani aliye pamoja nami?”
Mungu wetu Yehova anasema mimi ninafanya vitu vyote.
(Soma Isaya 45:6-7, 11-12, Yeremia 27:5) Bila shaka Yehova ndiye muumbaji wa vitu vyote
JE Mungu Yehova aliapia vitu alivyoviumba kama Allah?

Isaya 45:22-23
Niangalieni MIMI mkaokolewe, Enyi ncha zote za dunia. Maana MIMI ni Mungu hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba, mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.

Waebrania 6:13-16
Kwa maana Mungu alipompa Ibrahimu ahadi, Kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake. Akisema “Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza, Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo kwa kuyathibitisha.

Hapa tunaona Mungu wetu Yehova haapi kwa mtu wala vitu alivyoviumba kama Allah anavyoapa, bali Yehova anasema “Naapa kwa nafsi yangu”.Waweza pia kusoma jinsi Yehova alivyoapa kwa nafsi yake katika aya hizi;
Isaya 14:24 na Mwanzo 22:16

Hapa anayeapa ni Allah,
Hivi mtu anayeapa kwa mwingine anakuwa Mungu au mwanadamu?

Je, nani aliyeumba hapo?
Maana Allah anaapa katika aliyeumba, na kuumba ni moja kati ya sifa zake Yehova Mungu kumbe Allah hakuumba chohote!


ALLAH NI MUONGO!

Tukiyachunguza maandiko matukufu ya kiislamu yaani Quran na maandiko matakatifu yaani Biblia tutawapata hao wanaume wawili kuwa na utofauti wa mbali sana.

Tukianza na Quran hizi hapa kweli za wazi kabisa:
Allah wa quran anamkana na kumkataa Yesu Kristo kama si mwana wa Mungu yaani Yehova,
Qr. 19 au surat Maryam 35
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanau, Yeye ametakasika! Anapolihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
Qr. 112 au suratAl-Ikhlas 1-4 (sur aya utakaso)
Sema: Yeye ni Mwenyenzi Mungu mmoja (tu) Mwenyenzi Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyake vyote kwa kumuabudu na kumuomba na kumtegemea) Hakuzaa wala hakuzaliwa Wala hana anayefanana naye hata mmoja.
Kadiri ya aya hii Allah asema kuwa mungu hakuzaa wala hakuzaliwa wala hana mfano wa mtu au watu Yehova anasema hivi kuhusu mtu au watu……

Kila wanapoingizwa watu wajinga katika wavu wa huyo Mpinga-Kristoanayeitwa kwa jina ALLAH haya ndiyo maneno ya kukiri kumwabudu na kumtumikia:

Kwa kiarabu:
Ashihadu Allah ilaha inla ilah
Washihadu ana Muhamad rasuruhlah
Kwa kiswahili:
Nashuhudia kwamba hakuna Mungu isipokuwa Allah,
Na nashuhudia kwamba Muhammad (amani na rehema ziwe juu yake) nimtumishi wake na mjumbe

Biblia inasemaje ?
1Yohane 2:22-26,
Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. Kila amkanayeMwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.

Na hii ndiyo ahadi aliyoyuahidia, yaani, uzima wa milele.
Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.

Wakolosai 1:13-15,
Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; Naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana,mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

Yohane 3:16-17,
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoaMwanawe pekee, ili kila mtu amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Kwa maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.


Bila shaka Biblia Takatifu inamweka wazi ALLAH wa kila muislamu kama mwongo na Anti-Kristo ambaye waislamu wanamwita Dadjal bila ya wengi wao kujuwa kama ndiye wanaomwabudu

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW