Saturday, July 2, 2016

SINAGOGI SIO MSIKITI (SEHEMU YA PILI)


Kama tulivyosema Neno SInagogi linatokana na Kigiriki συναγωγή Sinagoge likimaanisha "mkutano"; ni tafsiri ya Kiebrania בית כנסת beit knesset yaani "nyumba ya mkutano".
Wayahudi hutumia pia neno la Kiyiddish "shul" (=shule) kutajia Sinagogi.
Katika lugha ya Kiebrania neno “ beit ” linamaana “ nyumba” ndio maana hata ukisoma Bethsaida “ Nyumba ya mvuvi” au bethsania-Nyumba ya masikini. Bethlehemu, nyumba ya mkate. (Soma injili imetajwa sana majina haya )
Katika Israeli ya Kale (kabla ya maangamizi ya Yerusalemu mwaka 587 KK) inaonekana hakukuwa na Sinagogi: walau halitajwi kabisa katika Agano la Kale.
Inaonekana ya kwamba masinagogi yalianzishwa baada ya hekalu ya Yerusalemu kubomolewa pamoja na kuanza uhamisho wa Wayahudi kwenda nchi mbalimbali.
Tangu kuharibiwa kwa Hekalu la Pili mwaka 70 Wayahudi wana masinagogi tu kufanyia ibada.
Neno hilo limetumiwa katika maana hiyo ya mukutano kwenye Septuajinti, yaani, tafsiri ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania. Lakini, baada ya muda neno hilo lilitumiwa kurejelea jengo ambapo watu walikutana kuabudu. Kufikia karne ya kwanza W.K., karibu kila mji ambao Yesu alitembelea ulikuwa na Sinagogi; Majiji yalikuwa na Masinagogi kadhaa; Jiji la Yerusalemu lilikuwa na Masinagogi mengi.
Ukumbi wa sala huwa na sehemu zifuatazo:
• Sanduku la Torati ni kabati au sanduku ambako hati za kuviringisha zenye mwandiko wa Biblia ya Kiebrania hutunzwa;
• Taa inayoendelea kuwaka muda wote;
• Meza ya msomaji ambako hati za torati hufunguliwa na kusomwa;
• Mimbari ya mafundisho;
• Kinara cha menorah chenye mishumaa 7 au 9.
Karibu na sanduku hilo, kulikuwa na viti vya mbele vilivyopangwa kuelekea kutaniko, navyo vilikaliwa na maofisa-wasimamizi wa sinagogi pamoja na wageni wowote waheshimiwa. (Mathayo 23:5, 6)
Hii ni tofauti ni Misikiti ya kiislamu isiyokuwa na Viti
Karibu na eneo la katikati la Sinagogi palikuwa na jukwaa lililokuwa na kinara na kiti cha msemaji . Kwenye upande wa mbele, wa kushoto, na wa kulia wa jukwaa hilo, kulikuwa na viti vya washiriki wa kutaniko .
• Kwa kawaida, gharama za kuendesha shughuli za Sinagogi zililipiwa na kutaniko. Michango ya hiari iliyotolewa na wote, matajiri kwa maskini, ilitumiwa kurekebisha na kudumisha jengo hilo
Bwana Yesu alipenda sana kufundisha kwenye hekalu na katika masinagogi walimokusanyika wayahudi.
“Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na katika hekalu, ambapo Wayahudi wote hukusanyika.”—Yohana 18:20.
Hekalu katika Jerusalemu ( hekalu katika Uyahudi )
Kulikuwa na Mahekalu mawili yaliyojengwa katika nyakati tofauti tofauti na watu tofauti tofauti ndani ya Yerusalemu.
Hekalu la kwanza lilijengwa na mtoto wa mfalme Daudi, Mfalme Suleimani. Lilijengwa mnamo mwaka 957 KK.
Hekalu hili likabomolewa na mfalme Nebukadreza II mnamo 586 KK.
Hekalu la pili,
Lilijengwa 536 KK -515KK baada ya uhamisho wa Babeli.
Uhamisho wa Babeli ni kipindi ambacho Wayahudi walilazimishwa kuishi Babuloni. ( kwa lugha nyingine ni kwamba Wayahudi walilazimishwa kuishi Babeli,ambayo kwa sasa tunaweza kusema walipelekwa Iraq, sababu magofu ya Babeli yapo katika mji wa kisasa wa Al-Hillah, kando ya mto flati kama 90km kusini mwa Baghdadi)
Hekalu hili la pili linajulikana pia kwa jina la hekalu la Herode mkuu kwa sababu herode alihusika pia katika upanuzi na kuliwekea nakshi katika Hekalu hili. Wataalamu wa mambo ya kale wanasema kwamba liliwekewa wakfu na Yuda Mmakabayo.
Hekalu hili la pili likabomolewa na Warumi mwaka wa 70. Tangu hapo halikujengwa hekalu la tatu, bali Wayahudi waliendelea kukusanyika katika mikutano yaani Sinagogi na sio katika Hekalu tena mpaka leo hii.
Tangu hapo halijajengwa tena, hivi kwamba sadaka zinazodaiwa na Torati hadi sasa haziwezi kutolewa kwa muda wa miaka 2000 hivi.
TOFAUTI KATI YA HEKALU NA SINAGOGI NI KAMA IFUATAVYO.
~ Hekalu huwa ni jengo kubwa lenye sehemu mbali mbali za ibada,wakati Sinagogi huwa ni mkutano tu wa watu katika jengo lisilokuwa na mgawanyo mkubwa.
~ Hekalu lina sehemu ya patakatifu pa patakatifu, Sinagogi halina sehemu hiyo.
~Hekalu lilikuwa kuanzia agano la kale mpaka agano jipya mfano kuanzia kitabu cha 1 Samweli 1:9, mpaka Ufunuo 21:22- Wakati Sinagogi lenyewe halitajwi katika agano la kale bali agano jipya tu.
Swali:
MBONA BIBLIA INASEMA KUWA SINAGOGI NI MSIKITI WA WAYAHUDI?
UFAHAMU
Katika tafsiri ya Biblia Union Version yapo maneno kadha wa kadha yenye asili ya lugha ya Kiarabu na Kiswahili cha kimvita hii ina tokana na mfasili (Mmisionary) wa kwanza aliye tafsiri Biblia kumshirikisha mzee (Shekhe) ili aweze kusaidiana naye katika kazi hiyo iliyo onekana kuwa ngumu kwake kutokana na kutojua vizuri Kiswahili hivyo ndiyo maana utakuta maneno mengi yenye asili ya Kiarabu ndani ya Biblia (Tazama Mifano). Mashekhe kwa maana ya wazee, Kadhi kwa maana ya hakimu, Iddi kwa maana ya Sikukuu, kutawadha kwa maana ya kunawa miguu na kadhalika
Pamoja na hayo alipo tafsiri neno hili Sinagogi kuwa ni msikiti haku tafsiri kwa kuzingatia utalaamu wa lugha bali alifananisha mambo Fulani Fulani yanayo tendeka katika majengo hayo mawili yaani Sinagogi na Msikiti na ndipo akafasiri kuwa Sinagogi ni Msikiti wa Wayahudi kwa kulinganisha baadhi ya matendo yanayo fanana baina ya majengo hayo mawili.
Ni sawasawa na leo mtu kumwambia babu yake kuwa Computer ni Runinga ya kisasa wala kamwe hana maana ya Computer ni TV ila amechukua anachokifahamu mhusika ili kumweleza kitu au jambo Fulani. Hivi na sawa na mjaluo wa ugenya kusilimu kisha akirudi huku nyarigunga kavaa Kanzu yake akiulizwa vipi kulikoni? Anasema “Siku hizi mimi naenda ile Kanisa ya Waislamu” .
Hieleweke pia lugha yeyote ile iliyohai uzidi kuimalika . Ndivyo ilivyo na Kiswahili pia. mathalani leo tunayo maneno mengi yamezalishwa ambayo kimsingi miaka michache hayakuwepo kwenye kiswahili
Aina ya tafsiri iliyotumika kitaaluma
Kwa kadri ya taaluma ya Kiutafsiri mtafsiri huyo wa Biblia ametumia moja kati ya aina kuu mbili za kiutafsiri ambapo aina ya kwanza ni ile ya tafsiri “Shabihifu” na ya pili ni tafsiri “Maanifu”.
Hivyo kimsingi katika kutoa maana hiyo ya Sinagogi- Msikiti wa Wayahudi, msaidizi huyu katika utafsiri wa Biblia alionekana kukosa namna ya kulieleza neno hilo sinagogi na ndipo akaadhimu kutoa tafsiri hiyo ambayo kitaaluma siyo tafsiri “Maanifu” (haiendani na asili ya neno katika lugha husika) bali alitumia tafsiri “Shabihifu” inayozingatia mambo machache yanayofanana baina ya vitu viwili ndiyo maana alisema ni Msikiti wa Wayahudi hivyo kamwe hakusema kuwa ni Msikiti wa Waislam maana alitambua kuwa katika wakati huo bado uislam haukuwa umeanzishwa.
Lakini pia nimeelezea kuwa mtu anaweza akamwelezea mzazi wake kuhusu kumputa kuwa ni Runinga ya siku hizi, hii aina maana kuwa computer ni TV ila unafananisha anachokijua mhusika ili japo kumweleza.
Hivyo basi kwa kuwa wenyeji wa pwani walikuwa wana ufahamu wa misikiti, basi mfasiri akaamua kutumia kauli hii.
Ebu fikiria kwa Kiswahili mara nyingi huwa twafasiri neno Pharmacy kwa maana ya Duka la dawa!!! Lakini je ni sawa?
HEBU SASA TUANGALIE MAANA NA MAJINA YA MAJENGO YA IBADA ILI TUONE UKWELI WA NENO HILI SINAGOGI KATIKA UTAALAMU WA WA LUGHA
Je Sinagogi laweza kuwa ni Msikiti katika uasili wa lugha?
Qur-an Surat 22:40
Andiko hili linataja majina ya majengo mbalimbali ya ibada ikiwemo na Sinagogi ingawa halikuwekwa kwenye tafsiri ya Qur-an ya Kiswahili ila tutalichunguza kwa watafsiri wengine wa Qur-an hususani tafsiri ya kingereza iliyotolewa na Mwanazuoni wa Kislam ndugu Yusufu Ally.
Qur-an ya sura ya 22 :40 katika tafsiri ya kiingereza inaeleza yafuatayo
Those who have been expelled from their homes unjustly but only because they say our Lord is Allah for had it not been that Allah checks one by means of another have been pulled down Monasteries Churches Sinagogues and Mosques …….
Tafsiri ya aya hiyo katika Kiswahili
Wale ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki, ila kwa kuwa wanasema: Mola wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu! Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hawakingi watu kwa watu, basi hapana shaka zingeli vunjwa nymba za wat'awa, na Makanisa, na Masinagogi, na misikiti, ambamo ndani yake jina la Mwenyezi Mungu linatajwa kwa wingi. Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anaye msaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu. Al barwani Ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki ila kwasababu wanasema mola wetu ni Mwenyezi Mungu, na kama Mwenyezi Mungu asingeliwakinga watu baadhi yao kwa wengine bila shaka yangelivunjwa Mahekalu, Makanisa, Masinagogi na Misikiti…………. Al farsy
Katika sehemu hii tafsiri hiyo ya Qur-an iliyotolewa kwa lugha ya kingereza inataja wazi kuwepo kwa majengo mawili kati ya manne ambayo kwahakika ndiyo yanayosumbua watu wengi hata hivyo Qur-an inaonekana tena kwa uwazi ikiyatofautisha majengo hayo ambayo ni Masinagogi na Misikiti. Hilo linaonekana siyo tu katika tafsiri bali hata katika maandishi ya lugha ya Kiarabu.
Fuatilia majina ya majengo hayo katika matamshi ya kiarabu na maana zake hapo chini.
BILASHAKA YANGELIVUNJWA
KISWAHILI KIARABU
1) Mahekalu Swawamiyu
1. Hekalu Swawaamiu
2. Kanisa Biyaun
3. Msikiti Masjid
4. Sinagogi Swalawaatun
Katika ushahidi huu yametajwa majengo manne lakini mwishoni tunakuta majengo mawili na jengo la kwanza linaitwa “Swalawatuni” yaani Sinagogi na la pili “Masjid” yaani “Msikiti” hivyo haya ni majengo yaliyotofauti kabisa maana Sinagogi ingekuwa ni msikiti lisinge itwa Swalawatuni kwa kiarabu bali lingeitwa Masjid hivyo hii inadhihilisha kuwa katika maana halisi ya lugha sinagogi kamwe haliwezi kuwa ni msikiti hivyo ni kama nilivyoeleza mwanzo kuwa neno Sinagogi lilimaanisha kikutanisho au kukutanika.
ENDELEA SEHEMU YA TATU
Edited by Max Shimba
Narrated by Mwalimu Chaka wa Musa

KWANINI MUHAMMAD ALIRUHUSU KUNYWA MIKOJO YA NGAMIA?


Ndugu msomaji,
Huu ni MSIBA mkubwa sana kwa Waislam na Mtume wa Muhammad. Leo, Muhamamd kawa Daktari na kudai kuwa eti, MKOJO WA NGAMIA NI DAWA.
Soma:
Kwa mujibu wa Muhammad, watu waliteswa kwenye makaburi yao kwa sababu ya kujichafua na mkojo [wao wenyewe]. Bukhari juzuu ya1 kitabu cha 4 sura ya57 na.215 uk.141; Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 4 sura ya 57 na.217 uk.142.
Hata hivyo Muhammad aliwaamuru baadhi ya watu kumfuata mchungaji wake na kunywa maziwa na mikojo ya ngamia. Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 sura ya 6 na.589, 590 uk.398, 399 na juzuu ya 7 kitabu cha 71 sura ya 29 na.623 uk.418.
Muhammad pia alisema kuwa mkojo wa ngamia ni dawa nzuri. Ibn-i-Majah juzuu ya 5 kitabu cha 31 na.3503 uk.38.
Baadhi ya Waislam waliambiwa kunywa mkojo wa ngamia, waliishia kuwa waasi na kumuua mchungaji. Muhammad aliamuru wakatwe miguu na mikono yao na macho yao yachomwe. Sunan Nasa’i juzuu ya 1 na.308-309 uk.255-256. Tazama pia Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 52 sura ya 152 na.261 uk.162.
Hivi huyu kweli alikuwa Mtume wa Mungu? Mbona hatusomi hata sehemu moja kuwa Muhamamd alitumia neno la Allah kutibu watu?
Mbona Allah anatumia Mikojo kutibu watu, kwani Allah hana uwezo wa kuponya kwa jina lake?
Mbona Muhammad na Allah hawakuponya watu kwa jina la ALLAH?
Kwanini Muhammad alipo kula nyama yenye sumu hakunywa MIKOJO ya Mgamia ili kujitibu?
Kumbe kunywa mikojo ya ngamia ilikuwa ni sehemu ya NDUMBA ya Muhammad.
Kumbe Mikojo ya Ngamia inawafanya watu wawe vichaa.
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.
Soma kituko kingine cha Muhammad.
Muhammad na Maji Safi
Udhibiti wa afya kwa kuondoa maji machafu na takataka (Sanitation): Watu walipomuliza kuhusu kunywa maji ya kwenye kisima chenye nguo za hedhi, mbwa waliokufa, na vitu vyenye kunuka, Muhammad alisema kuwa maji ni safi kabisa na huwa hayachafuliwi na kitu chochote. Abu Dawud juzuu ya 1 sura ya 35 na.66-67 uk.16-17.
Muhammad alikuwa Nabii wa uongo na sio Mungu.
Waislam nawakaribisha kwa Yesu Mungu Mkuu.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

KUMBE QURAN IMEJAA SHAKA NA HAIPO WAZIWAZI

Je, madai ya kuwa Quran imekalika na ipo waziwazi ni ya kweli?
Allah ateremsha aya na kudai kuwa, Quran haijakamilika na haipo waziwazi.
Allah asema kuwa aya zingine ndani ya Quran hakuna ajua maana yake isipokuwa Allah.
Ndugu wasomaji;
Leo tutaangalia utata ulio jaa ndani ya Quran ambayo wanadhuoni wengi hudai kuwa imenyooka, huku Allah akiwapinga na kuteremsha aya ambayo inasema kuwa Quran haijanyooka na haipo waziwazi.
Kwanza tuanze kwa kuangalia aya ambayo inasema kuwa Quran ipo wazi na aya zake zimepambanuliwa ni uongofu kwa walio ongoka.
Surat HUD (11:1). Alif Lam Ra. Hiki ni Kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi, kisha zikapambanuliwa, kilicho toka kwa Mwenye Hikima na Mwenye Khabari
Surat Al Anaam (6:114). Je, nimtafute hakimu ghairi ya Mwenyezi Mungu, naye ndiye aliye kuteremshieni Kitabu kilicho elezwa waziwazi? Na hao tulio wapa Kitabu wanajua ya kwamba kimeteremshwa na Mola wako Mlezi kwa Haki. Basi usiwe katika wanao tia shaka.
Surat An nah’k (16:89). Na (waonye) siku tutakapo wainua mashahidi katika kila umma wakiwashuhudia kwa yanayo tokana na wao, na tutakuleta wewe uwe shahidi juu ya hao. Na tumekuteremshia Kitabu hiki kinacho bainisha kila kitu, na ni uwongofu, na rehema, na bishara kwa Waislamu
Surah tulizo ziweka hapo juu, zinasema na kudai kuwa Quran imepambanuliwa na ni kitabu kilizo elezwa waziwazi. Ikimaanisha kuwa, unapoisoma Quran, hautapata maswali au kusoma utata katika aya zilizo teremshwa na Allah.
LAKINI HAYO MADAI, YANAPINGANA NA UTATA KATIKA AYA IFUATAYO INAYO DAI KUWA, NDANI YA KURAN KUNA AYA AMBAZO ALLAH PEKE YAKE NDIE ANAZO ZIFAHAMU
Hebu tuisome hiyo aya:
Surat Al Imra (3:7) Yeye ndiye aliye kuteremshia Kitabu hichi. Ndani yake zimo Aya muhkam, zenye maana wazi. Hizo ndizo msingi wa Kitabu hichi. Na ziko nyengine za mifano. Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zile za mifano kwa kutafuta fitna, na kutafuta maana yake; na wala hapana ajuaye maana yake ila Mwenyezi Mungu. Na wale wenye msingi madhubuti katika ilimu husema: Sisi tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu Mlezi. Lakini hawakumbuki hayo isipo kuwa wenye akili.
Ndugu zanguni, huu ni msiba mwingine katika Uislam, Allah katika Surat Al Imra iliyoteremka Madina anasema kuwa:
i. Ndani ya Quran kuna Aya mukham, zenye maana wazi,
ii. Zipo aya zenye mifano ambazo wanao zifuata hutafuta fitna na kutafuta maana yake,
iii. Zipo aya ambao hapana ajuaye maana yake ila Allah.
Ndugu zanguni, hii Surat 3 aya 7 inapingana na Surat HUD 11:1, Surat Al Anaam (6:114), na Surat An nah’k (16:89) zinazo dai kuwa aya za kuran zipo waziwazi na zimepambanuliwa.
Sasa, Waislam wafuate kipi?
Je, Waislam wanaamini kipi katika hii Quran inayo jipinga yenyewe na ambayo haipo waziwazi?
Mbona Allah anajipinga mwenyewe katika hizo aya hapo juu?
Au tatizo lilikuwa ni Muhammad ambaye alikuwa hajui kusoma wala kuandika na alishindwa kukariri maelekezo ya Jibril?
ZAIDI YA HAPO, kwanini Allah aliteremsha aya ambazo hakuna azijuaye ila yeye Allah?
Hizo aya zinamsaidia vipi Mwislamu?
Waislam wanapata faida gain wanapo zisoma hizo aya huku ikifahamika kuwa ajuaye maana zake ni Allah peke yake?
MWSIHO, ningependa kufahamu, hawa Waislam wanaelewaje kuwa aya walizo zisoma ndivyo walitakiwa walelewa huku ikifahamika Allah ameweka mtego kwa kusema kuwa, kuna aya ndani ya Quran ambazo ni Allah pekee anaye zifahamu.
Kumbe ndio maana Waislam wana pigana wenyewe kwa wenyewe kama ISIS, Sunni vs Shia, nakadhalika.
Kumbe ndio maana Quran inausaidizi wa Sahih Hadith na Suna za Muhammad.
Huu ni msiba mwingine katika dini ya Allah.
Kwanini Allah aliteremsha aya ambazo anazifahamu yeye mwenye?
Karibuni kwa Yesu aliye hai ambaye ametuletea Roho Mtakatifu kama Kiongozi wetu.
Yohana 16: 3 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. 14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari. 15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.
YOHANA 16: 26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
1 YOHANA 2: 27 Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.
Ndugu wasomaji, Yesu amesha weka kwa uwazi kuwa, ukimfuate yeye, basi utapokwa kipawa cha Roho Mtakatifu na yeye huyo Roho Mtakatifu ataishi ndani yetu na atatufundisha yote.
Karibuni kwa Yesu.
Mungu awabariki sana
Max Shimba Ministries Org

ALLAH ATEREMSHA AYA NA KUSEMA MAJINI NI MAISLAM NA YANAMWABUDU YEYE


MAJINI KATIKA DINI YA KIISLAM ( Q 72:1-14 )
1. QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
2. ALLAH AYARUHUSU MAJINI KUZAA NA WAISLAMU
3. QURAN INAKIRI KUWA MAJINI NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
4. MAJINI YANAMWABUDU ALLAH
5. KILA MUISLAM AMEPAGAWA NA MAJINI KATIKA MWILI WAKE
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu Majini au Mashetani katika Uislam.
JINI NI NINI?
Katika lugha ya kiarabu, neno Jini linamaanisha kitu kilichofichwa au kisichoonekana QURAN 1:71 Neno hili hutumiwa na Waarabu kwa ajili ya kutaja jina fulani. Kwa Waarabu, Jini anayevaa sura ya kike humwita Jinivya, hivyo majini Ghul/Ghilan, nao hujifunua kwa sura ya kike.
Katika imani ya Kiislamu, wao huamni kwamba Majini hutofautiana na Mashetani. Majini waliosilimu wao huitwa majini mazuri na hawa wakiwa katika hali kujionyesha kwa wanadamu, hao huitwa AJINU na wale walioacha kusilimu mwaka 610 AD (Baada ya Kristo) katika safari ya mtume Muhamad alipotoka Taif , wao wanaitwa Mashetani . Hivyo, wao wanapokuwa katika hali ya kutoonekana huitwa ALBAHATWA lakini pia Majini wote wanapokuwa katika hali ya kutoonekana waweza kuitwa ALBAHATWA, yaani PEPO.
QURAN INASEMA KUWA MAJINI YANAZALIANA NA KUFA KAMA BINADAMU
Muislamu huamini kwamba kuna majini ya kike na kiume. Lakini pia , huamini kuwa Majini huoana na kuzaliana QURAN 55:56 na kuwa Majini huzaa sana kuliko binadamu na kwamba, Jini mmoja anaweza kuzaa watoto 300, na kuwa Jini huzaa watoto 3 hadi 4 kwa mkupuo. Somo QURAN 55:26-28 na kuwa Majini wanaweza kuishi miaka 400-1,000 kisha wanaweza kufa. Tofauti yao na binadamu ni kwamba wao wanaishi miaka mingi kuliko binadamu. Lakini pia, huamini kuwa wapo Majini wanaokula, wanaomeza, wanaokunywa, ila tofauti yao na wanadamu ni kwamba wao hula kwa kutumia mkono wa kushoto.
ALLAH AYARUHUSU MAJINI KUZAA NA WAISLAMU
Pia hiamini kuwa Majini wana uwezo wa kuzaa na Wanadamu. Soma QURAN 17:64. Waislamu huamini kwamba mtu anauwezo wa kuoa au kuolewa na Jini bila kujua, na mwanadamu anauwezo wa kumuua Jini. Soma QURAN 57:14-15
SURATULJINN
Ndani ya QURAN pia imo sura inayoitwa Suratuljinn (QURAN 72). Sura hiyo huitwa hivyo kwa sababu ni sura ya Majini (Mapepo).
Kwa nini wanatajwa Majini katika imani ya Kiislamu?
QURAN INAKIRI KUWA MAJINI NI MAISLAM NA YALISILIMU PALE QURAN ILIPO TEREMSHWA KWA MUHAMMAD.
KUMBE MAJINI YANAIGOPA TAURAT, INJIL NA ZABURI.
Majini wanatajwa sana katika dini ya Kiislamu kwa kuwa ni Waislam kwa kusilimu, kwa kuiamini Quran tukufu aliyopewa Muhammad.
Majini walisilimu na kuwa Waislamu mwaka 610 AD(Baada ya Yesu) SOMA 72:1-14 QURAN. Hivyo basi, unapotumia neon jinni maana yake unatumia lugha ya Kiarabu ukimaanisha Pepo mchafu. Ni kama Spoon/kijiko, vyote ni kitu kimoja. Ndani ya Quran, neon “PEPO” limetumika kama Paradiso, mbinguni. Lakini pia, tunapata neon jingine liitwalo AKHERA ila neno hilo halimaanishi PARADISO, bali kwa lugha ya Kiarabu neno hili “AKHERA” lina maana ya KUZIMU.
Lakini pia ukiangalia ndani ya SURALJINN ( QURAN 72:1-2, 8-9, 12 ) Mapepo hawa wanajieleza waziwazi kabisa kuwa mwanzo waliishi Mbinguni, walipogeuka kwa kuasi, walitegwa na Mungu. Linganisha na maandiko haya katika Biblia ( UFUNUO WA YOHANA 12:7-9; YUDA 1:6-8; UFUNUO 20:10; UFUNUO 21:8 ). Kwa mujibu wa dini ya Kiislamu, hawa majini ( Mapepo ) waliotegwa na Mungu Mbinguni wakiwa Malaika huko na kutupwa Duniani baada ya kuasi huko, sasa, wakati wa mtume Muhamad katika safari yake ya kurudi Taif mwaka 620 AD (baada ya Yesu) wapo walioamini na kuona kuwa Quran ni ya ajabu ya kuwatangazia neema ya kuabudu. Katika vol 8-9, husema , wanapojaribu kwenda Mbinguni ( walikotoka zamani ), hukuta ile Mbingu imezungushiwa vimondo vya moto. Hivyo, hudai kuwa mbingu yao iko Akhera, yaani Kuzimu, maana Mbingu ya juu ina moto na hawana uwezo wa kwenda huko. SOMA (QURAN 72:9), Mbingu ina utisho wa moto ila Akhera ( kuzimu ) hakuna shida kwao.
MAJINI YANAMWABUDU ALLAH
Hivyo basi, kulingana na jinsi Allah asemavyo ndani ya Quran kuwa nimeumba binadamu na majini ili muniabudu ( QURAN 57:58 ; 51:56) na kuwa , mbinguni mwao Majini wanaabudu (Majini waliosilimu mwaka 620 AD) ,SOMA QURAN 72:14, ambao ni wema wanaosafiri na kurithi uzima wa milele upatikanao Akhera ( Kuzimu ). Lengo kubwa la Shetani na Majini ni kufanya urafiki na wanadamu wengi ili kwa wingi huo apate watu wengi wa kwenda nao JEHANAMU ( QURAN 6:128 ). Jambo la muhimu kujua hapa ni kwamba moto wa milele hakuwekewa Mwanadamu bali ni Shetani na malaika zake wote ( Majini au mapepo ). Hawa, hawana nafasi tena ya kuungama au kutubu.
Yesu Kristo anayetambuliwa na Waislam kama Mtume tu WANAE MWITA ISSA, hakuwa na urafiki wowote na Shetani wala Mapepo ( Majini ). Aliyaamuru Majini kutoka ndani ya watu waliokuwa wakiteswa nayo ( MATHAYO 8:29: MARKO 5 N,K )
Wakati Yesu anaondoka hapa duniani, alichukuliwa na wingu na kupaa kuelekea juu. Mbinguni ni juu kama Quran inavyothibitisha. Yesu aliweza kupaa na kuingia Mbinguni lakini Majini ( Mapepo ) walioslimu wakijaribu tu, wanakutana na moto mkali. Tumeona kuwa Majini ambao ni Waislamu kwa kusilimu, wanaishi AKHERA yaani Kuzimu. Je, Waislamu wengine unadhani wataishia wapi milele? Katika imani ya Kiislam huamini kuwa, Muislam akifa anakuwa na Majini wawili wa Kumlinda humo Kaburini.
KILA MUISLAM ANA JINI KATIKA MWILI WAKE
Majini wamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote, hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea. Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam. Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo. Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo. Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muhamad kwa muda wa siku 40 akiwa Mabondeni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.
USHAURI WANGU KWA WA WAKRISTO:
Ushauri wangu wa bure kwa Mkristo ni huu, USIMUACHE KAMWE KRISTO NA KUINGIA KATIKA IMANI ZA MASHETANI (1TIMOTHEO 4:1-2 ).
Majini au Mashetani ni kitui kimoja na wala hakuna tofauti yao. Wote hao Mashetani/Majini yalimpinga Mungu na kutupwa duniani. Biblia inasema kuwa Hakuna Msamaha kwa Majini maana wao walisha hukumiwa na wanacho subiri ni kutupwa Jehannam.
Shetani bado ni “mfalme wa nguvu za anga” (Waefeso 2:2). Hii inamaanisha kwamba Shetani na Malaika wengine walioasi wanaweza kushawishi mia zetu na mawazo yetu kupitia miziki, runinga, mijadala, nk. Tumeambiwa kujihadhari katika mawazo na nia zetu (2Wakorintho 10:3-5). 2Wakorintho 4:4 inatuambia kuwa mungu wa dunia hii amepofusha mawazo ya watu ili wasiamini.
Shetani ndiye yuko nyuma ya dini zote za uongo na dini za dunia. Shetani atafanya na kila kitu katika uwezo wake ili ampinge Mungu na wale wote wanaomfuata. Ingawa hatima ya Shetani imewekwa muhuri kuwa tanuru la moto milele (Ufunuo Wa Yohana 20:10).
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

SINAGOGI SIO MSIKITI (SEHEMU YA TATU)


Ndugu msomaji
KIGEZO CHA YESU KUINGIA KATIKA SINAGOGI SIYO KIGEZO SAHIHI CHA KUFUNDISHA LA KUWA YESU NI MUISLAM.
Hebu fuatilia fungu hili la Biblia
MATENDO YA MITUME 17:1
Akiisha kupita kati ya amfipoli na Aporonia akafika Thesalonike ambapo palikuwa na Sinagogi la Wayahudi na Paulo akaingia mle walimo akahojiana nao kwa maandiko Sabato tatu.
Endapo umefuatilia fungu hilo kwa makini unaweza kujiuliza swali lifuatalo ………….
Ikiwa kuingia tu kwenye Sinagogi kulimaanisha Yesu ni Muislam je Paulo naye kwa tendo hilo lakuingia humo alikuwa Muislam?
Jambo la kushangaza hata wale wanaotoa fundisho hili humkataa Paulo kwa kadri ya imani yao na huku wakijivisha kitanzi kwa madai hayo kuwa mtu huwa muislam kwa kuingia katika Sinagogi.
Alichofanya Yesu katika Sinagogi hakiwiani na Misikiti ya Waislam
Luka 4:16 – 17 Yesu apewa chuo cha Nabii Isaya je Waislam leo hii wanachuo cha Nabii Isaya Msikitini? (La Hasha ) hii inaonyesha utofauti mkubwa uliopo baina ya Masinagogi na Msikiti ingawa ni vitu vichache tu vianavyolingana baina ya majengo hayo mawili.
Pamoja na hayo chuo hicho Nabii Isaya humtaja Yesu kama Mungu mwenye nguvu Isaya 9:6-10 tendo ambalo linapingwa na Umma wa Kiislam hivi leo hivyo kamwe Sinagogi na Misikiti si Majengo yanayowiana katika tafsiri na pia hata katika matendo kadhaa makuu ya kiimani pamoja na kufanana kwa machache kama yale yahusuyo mavazi n.k.
KUMFANYA YESU NI MUISLAM NI MAKOSA
Yesu alipaa kwenda mbinguni mwaka wa 33 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhamadi mwaka 570 (BK) ambaye ndiye muanzilshi wa Uislam.
Yesu hakufuata kamwe nguzo tano za Uislam na hata hivyo bado hapakuwa na nguzo hizo kwa kuwa muasisi wa imani ya Uislam yaani Muhamadi (SAW) hakuwepo.
Hebu sasa tuchunguze nguzo hizo tano za uislam na kisha upime mwenyewe endapo Yesu alizitekeleza hizo ili kuwepo na usahihi kwa wanaofundisha na kudai kuwa Yesu alikuwa Muislam.
NGUZO (5) ZA UISLAM
1) Shahadat - kushahadia- hili ni tendo la kukili kuwa Mungu ni mmoja na Muhammad ni Mtume wake.
2) Ikhamu Swalat - Kusimamisha swala- hili ni tendo la kufuata utaratibu wa kusali swala mara tano kwa siku.
3) Ita-U Zhakhati - Kutoa zaka- kutoa mali kwaajili ya Masikini.
4) Swaum Shar Ramadhani - Kufunga – hili ni tendo la kufunga kwa kuangalia mwezi linalochukua muda wa siku 29, 30
5) Hijat ila Baitu Llah - Kuhiji Maka- hili ni tendo la ibada yakwenda mji wa Makka linalo ambatana na matukio mbalimbali kama vile kupiga mawe Shetani na kuheshimu jiwe
Jeusi n.k
Je Yesu alifanya hayo ili aitwe Muislam?
Yesu kamwe hakuwa Muislam (Yasuu Laysa Muslimuna).
Barikiwani; Maswali yanakaribishwa
Na Mwalimu Chaka
Edited by Max Shimba
Amended and narrated by Max Shimba
Barikiwa sana ndugu msomaji baada ya kujifunza kuwa Sinagigi sio Msikiti.
Max Shimba Ministries Org

JIBRIL WA QURAN SIO GABRIEL WA KWENYE BIBLIA


Ndugu msomaji,
Tokea kuanzishwa Kwa dini ya Uislam, Waislamu duniani wanaamini na kuifundisha jamii kuwa Malaika aitwae ‘Gabriel’ Kama maandiko Matakatifu ya Biblia yanavyofundisha ndiye Malaika ‘Jibril’ Kama Quran inavyosimulia.
Swali la muhimu je ni kweli kuwa Malaika “Gabriel” ndiye “Jibril” nakusihi fuatilia somo hili ili kujua ukweli….
HOJA ZA WAISLAMU ZA KUAMINI KUWA MALAIKA GABRIEL NDIYE JIBRIL
Waislam wanalinganisha kwa kusoma aya za Quran na Biblia na kusema kuwa Malaika Gabriel ndiye Jibril wanasoma aya hizi….
QURAN 19:16-17 SURAT MARYAM
16. Na mtaje Mariamu kitabuni (humu) alipojitenga na jamaa zake (akenda) mahali upande wa Mashariki (wa Msikiti) 17. Na akaweka pazia kujikinga nao.Tukampelekea muhuisha sharia yetu (jibril) - akajimithilisha kwake kwa sura ya Binadamu aliye kamili.
LUKA 1:26-28
26. Mwezi wa sita, Malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. 27. Kwa mwana mwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu 28 Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa Neema, Bwana yu pamoja nawe.
“Mbali na kusoma aya hizi, pia wanaendelea kusoma kitabu cha maisha ya nabii Muhammad kilichotungwa na aliyekuwa kadhi mkuu wa Kenya marehemu sheikh Abdallah Saleh Al-Farsy katika ule ukurasa wa 17 kifungu (A) kuna maneno haya...
NAMNA YA KULETWA WAHYI…
Waislamu wanaitikadi kuwa Quran ni maneno ya Mwenyezi Mungu na vilevile Taurat ya nabii Musa na injili ya nabii Isa, na Zaburi ya nabii Daudi. Vyote pia ni vitabu vyenye maneno ya mwenyezi Mungu. Lakini Mungu haonekani Kwa macho wala hayupo mahali mahsusi. Basi vipi hao mitume wamepata maneno haya? Jawabu yake ni hii wao huyapata ima kwa Jibril Malaika Mkubwa kuliko Malaika wote wa Mwenyezi Mungu.
QU-RAN 53:2-6 SURATUL NAJM (NYOTA)
2. Kwamba mtu wenu huyu Nabii Muhamad (hakupotea Kwa ujinga) na wala hakukosa (na hali ya kuwa anajua) 3. Wala hasemi Kwa matamanio (ya nafsi yake) 4. Hayakuwa haya (anayosema) ila ni wahyi (ufunuo) uliofunuliwa (kwake) 5. Amemfundisha (malaika) mwenye nguvu Sana 6. Mwenye uweza na yeye (huyu jibril) akalingana sawa sawa.
Waislamu kwa kusoma aya hizi, wanaamini Malaika Gabriel ndiye Jibril lakini aya hizi zinaonyesha tofauti kwani malaika Jibrili alipelekwa na Allah ambaye sio Yehova aende kwa Mariamu ambaye alikua Msikitini na Quran haikutaja mji wala nchi aliyoenda jibril, lakini tunaona Biblia inafundisha kuwa, malaika Gabriel aliingia nyumbani kwa Mariamu na tena biblia inatufundisha kuwa ufunuo wa unabii uliletwa kwa muongozo wa Roho Mtakatifu (2 Petro 1:20-21) na wala si malaika jibril kama Qurani inavyosimulia.
JE, MALAIKA NI VIUMBE WA NAMNA GANI?
WAEBRANIA 1:13-14.
13. Je, yuko malaika aliyemwambia wakati wowote uketi mkono wangu wa kuume hata nitakapo waweka adui zako chini ya nyayo zako? 14. Je, hao wote si “roho”watumikao walitumwa kuwahudumu wale watakao urithi wokovu?
Ni wazi tunaona kuwa malaika ni vyumbe ambao ni nafsi ya roho ambao wanauwezo wa kuwajia watu kwa umbo la wanadamu eg (Mwanzo 18:1-19:12) kama tunavyoona walipomwendea Ibrahim na lutu.Malaika alimwendea Musa katika sura ya kijiti kinacho waka bila kuteketea (kutoka 3:1-5)
JE, MALAIKA WOTE NI WEMA NA HAWAMKOSEI MUNGU?
Tukisoma Quran tunaona Allah anayeabudiwa na Waislamu anasimulia Malaika kuwa ni viumbe wenye sifa hii.

ALLAH ATEREMSHA MATOLEO ISHIRINI 20 TOFAUTI YA QURAN


JE TOLEO LIPI NI SAHIH?
Je, Kati ya haya Matoleo 20 (Ishirini) ya Quran, toleo lipi ni la kweli?
Ndugu msomaji,
Leo nitaweka ukweli kuhusu Quran ambayo ina Matoleo 20 na kati ya hayo Ishirini (20) Matoleo 7 (Saba) yametajwa katika Hadith Mwaminifu za Muhammad.
Hapa chini ni Wasomaji Saba (7) ambao wote wana Matoleo Mawili mawili. Hawa Wasomaji saba wanapatikana hapa:
Nafi (from Medina; d.169/785)
Ibn Kathir (from Mecca; d.119/737)
Abu `Amr al-'Ala' (from Damascus; d.53/770)
Ibn `Amir (from Basra; d.118/736)
Hamzah (from Kufah; d.156/772)
al-Qisa'i (from Kufah; d.189/804)
Abu Bakr `Asim (from Kufah; d.158/778)
WASOMAJI SABA NA MATOLEO YAO YA QURAN
1. Msomaji : Nafi`
MATOLEO YAKE
Warsh
Qalun
2. Msomaji: Ibn Kathir
MATOLEO YAKE
al-Bazzi
Qunbul
3. Msomaji: Abu `Amr al-'Ala'
MATOLEO YAKE
Al-Duri
al-Suri
4. Msomaji: Ibn `Amir
MATOLEO YAKE
Hisham
Ibn Dhakwan
5. Msomaji: Hamzah
MATOLEO YAKE
Khalaf
Khallad
6. Msomaji: al-Qisa'i
MATOLEO YAKE
al-Duri
Abu'l-Harith
7. Msomaji: Abu Bakr `Asim
MATOLEO YAKE
Hafs
Ibn `Ayyash
HAWA NI WASOMAJI WENGI WATATU NA MATOLEO YAO MAWILI KILA MMOJA
"The Three" readers
1. Msomaji: Abu Ja`far
MATOLEO YAKE
Ibn Wardan
Ibn Jamaz
2. Msomaji: Ya`qub al-Hashimi
MATOLEO YAKE
Ruways
Rawh
3. Msomaji: Khalaf al-Bazzar
MATOLEO YAKE
Ishaq
Idris al-Haddad
Wadhalimu wa dini ya Kiislamu wanakiri kuwa kuna WASOMAJI wengi zaidi, lakini wanasema kuwa hawa walio tajwa hapo juu ndio thabit na sahihi. Kumbe basi kuna VERSIONS ISHIRINI ZA QURAN !!!!!!
SASA MASWALI YAKUJIULIZA NI HAYA:
1. Kati ya hao wasomaji wakurani, ni yupi yupo sahihi?
2. Kama Allah ndie aliteremsha Quran kwa Muhammad, kivipi awe na wasomaji wengine na kumsahahu Muhammad mtume wake kipenzi?
Ndugu msomaji, leo tumejifunza kuwa katika Uislam kuna siri nyingi sana ambazo zimefichwa na wanaona aibu kusme aukweli kuwa QURAN INA VERSIONS 20. HUU NI MSIBA KWA ALLAH NA MTUME WAKE MUHAMMAD.
Mungu awabariki sana na kuendelea kuwafungua macho.
Katika huduma yake
Max Shimba Ministries Org.

KWANINI MUHAMMAD ALIRUHUSU UCHOMWAJI WA QURAN


NI NANI ALIYECHOMA QURAN? NI NANI ANAYEENDELEZA UCHOMAJI WA QURAN?**********************************************************
Sasa inefahamika kuwa aliyekuwa wa kwanza kuchoma kitabu kinacho daiwa ni cha "haki, kikamilifu na kisichokuwa na dosari" kiitwaacho "QURAN TUKUFU" ni yule yule aliyeandika Quran.
Caliph Uthman aliandika Quran na kuchoma aya ambazo hakupendezwa nazo!
(Sahih Bukhari 6:61:510)
CALIPH UTHMAN ALIANDIKA QURAN NA KUCHOMA AYA AMBAZO HAKUPENDEZWA NAZO!-(Sahih Bukhari 6:61:510)
Caliph Uthman hakuchoma tu aya za Quran bali aya zingine alizifuta kwa maksudi. (Bukhari 6:61:527).
HAPA MASWALI NYETI YANAIBUKA;
**************************
Je, ni aya gani hizo alizozichoma?
Je, aliakuwa anaandika Quran kwa manufaa ya nani?
Je, aliandika Quran kwa mamlaka ya nani?
Je, mwenye mamlaka hayo hakumwongoza aandike Qurani mufti bila dosari kama wanavyodai waumini wa kiislamu kuwa kuran haina dosari?
SWALI:-KWANINI BASI WAISLAMU WALALAMIKE KUWA QURAN YAO INACHOMWA?
JIBU:-WAO NDIO WALIOANZISHA UCHOMAJI NA HADI SASA HAO NDIO WANAOENDELEZA UCHOMAJI WA KURAN.
Kumbe Quran inachomeka.
Kumbe Quran haikuteremshwa.
Kumbe Quran iliandikwa na viumbe dhaifu.
Max Shimba Ministries Org

MAHAKAMA YA KADHI HAIPO KWENYE QURAN

Ndugu wasomaji.
Leo ningependa kusema kuwa, dai la Waislam wa Tanzania la Mahakama ya Kadhi halina msingi wala usaidizi wa Quran.
Kwa wanao ifahamu Quran, watakubaliana na mimi kuwa HAKUNA AYA HATA MOJA ambayo Allah alisema na au Waamrisha Waislam waende kwenye Mahakama ya Kadhi.
Narudia tena hakuna aya.
SASA NDUGU WAISLAM:
1. Who appoints Chief Kadhi and Kadhis?
- Nani anawachagua wamchifu wa kadhi na ipo wapi aya inayo sema hivyo?
2. What are the qualification for appointment to the office of a Kadhi (including a Chief Kadhi)?
- Zitaje sifa zinamfanya mtu apewe hiyo kazi ya uchifu nk Leteni aya kutoka Quran.
3. Since the Kadhis are not trained lawyers who understand the Evidence Act and the Civil Procedure Act, how and/or what will they use to administer their Courts?
- Kwasababu wanao ongoza hizo Mahakama sio Mawakali walio somea na hakuna aya kutoka Quran inayo wapa uongozi huo, je, hoa viongozi watatumia nini kuweka haki katika hizo mahakama?
4. Muslims are mainly of two sects in Tanzania - the Sunni and Shia. Majority of the Muslims in Tanzania are Sunni Muslims but there is a significant population of Shia Muslims too and consideration ought to be given to the appointment of Kadhis of the Shia Sect to cater the interest of the Shia Muslims. Will they have two different Courts? For Sunni and Shia?
- Kuna madhebu makubwa mawili ya Waislam, Suni na Shia. Wengi wao wa Tanzania ni Suni, ingawa kuna Shia wengi vile vile, Je, watakapo chagua hao viongozi wa kadhi, watachaguaje maana Suni na Shia hawakai kiti kimoja? Je, watakuwa na mahakama mbili tofauti?
5. How will Muslim Women be protected since: Muslim law regards women as less than men in matters of both marriage and divorce, as well as devolution of property: Holy Quran Surah 2:228-232, and Surah 65:1-7 (only a man may divorce his wife even if he is required to provide for her); a man may beat his wife, even if lightly, the evidence of two women, is equal to evidence of one man (Surah 2:282). The application of such beliefs of faith are contrary to the Constitution.
- Je, ni kivipi Mwanamke wa kiislam analindwa maana Allah alisha sema kuwa Mwanamke yeye ni nisu ya Mwanaume(Surah 2:282) katika maswala ya mirathi? Zaidi ya hapo Quran inampa haki Mume tu kutoa talaka na mke anaachwa bila ya haki yeyote ile Quran Surah 2:228-232, and Surah 65:1-7? Je, ikiwa mke anataka kutoka talaka, atatumia aya zipi za Quran?
Sheria za taifa la Tanzania zinapingana na hii Kadhi, je, Waislam watafuata sheria za nchi au watafuata sheria za kadhi na kuvunja sheria za nchi?
Islamic "Kadhi" courtsis illegal and discriminatory.
Mahakama ya Kadhi inapinga sheria za nchi.
Waislam, kwanini mnamsaidia Allah kwa kuanzisha Mahakama ya Kadhi?
Hakika ni dhambi kubwa kumzulia uongo Allah na kumsaidia Allah ambae kasema hana msaidizi na ni muweza wa yote.
Karibu katika Ukristo ambao utawaweka huru kutoka vifungo vya sheria.
“Kwa maana Mungu alimfanya Yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi TUPATE KUFANYWA HAKI YA MUNGU katika Yeye.” (Wakor.5:21). Mstari wa maana sana na mwenye uzito! Na tena imeandikwa, “Kwa maana kama vile kwa kutokutii yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi WATAFANYWA WENYE HAKI.” (Warumi 5:19). Huu ni ukweli wa Mungu – kutokana na dhambi ya Adamu tulifanywa wenye dhambi. Kwa kuzaliwa kwetu kwa kwanza tulipata tabia ya mwenye dhambi, na sawasawa na tabia hiyo tunafanya dhambi. Sasa, VIVYO HIVYO kupitia utii na mateso ya Yesu Kristo msalabani TUMEFANYA WENYE HAKI! Kwa kuzaliwa kwa pili tunapata Roho ya Mungu na maisha ya Yesu ndani yetu na sawasawa na Uzima huo tumewekwa huru mbali na dhambi ili “tusitumikie dhambi tena.”
Yesu amevunja ile nguvu za dhambi katika maisha yetu. “Kwa sababu sheria ya ROHO WA UZIMA ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.” (Warumi 8:2). Sheria ya nje haina uwezo kuibadilisha hali ya kiroho yako au tabia yako. Kwa mfano, na tuweke sheria kwa ajili ya nyoka, na sheria hiyo inasema “uwe mwanakondoo!” Sasa, nyoka anaweza kujitahidi sana awe mwanakondoo; anaweza kujaribu kufanya hivi na hivi; anaweza kusali na kwenda kanisani, lakini anabaki nyoka! Hakuna mabadiliko! Kwa hiyo Yesu alisema, “Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa; ili kila mtu aaminiye AWE NA UZIMA WA MILELE KATIKA YEYE.”
Karibuni kwa Yesu na atakuweka huru kutoka Mahakama ya Kadhi na Sharia za Uislam.
Max Shimba Ministries Org
© Max Shimba Ministries 2013

KWANINI ALLAH NA MUHAMMAD WANAMCHUKIA ISA BIN MARYAM?


Ndugu msomaji,
Labda hukuwai jiuliza jambo hili, KWANINI ALLAH ALISEMA ISA BIN MARYAM SI CHOCHOTE?
KWANINI ALLAH HAKUWAI SEMA KWA MANABII WENGINE KUWA WAO SI CHOCHOTE, BALI ALIMDHIHAKI KWA CHUKI MBAYA ISA BIN MARYAM?
Hebu tusome kwanza aya kutoka Suratul Al Maidah:
Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume. Wamekwisha pita Mitume kabla yake. Na mama yake ni mwanamke mkweli. Wote wawili walikuwa wakila chakula. Angalia jinsi tunavyo wabainishia Aya, kisha angalia vipi wanavyo geuzwa.http://www.quranitukufu.net/005.html
Eti, Isa Bin Maryam si chochote na anageuzwa. Hivi kuna aya gani zingine kwenye Quran zinaita mitume wengine si chochote na wanageuzwa?
Hivi kwanini Allah na Muhammad wanamchukia Isa Bin Maryam namna hii? Huyu Isa bin Maryam aliwafanya nini Allah na Muhammad kiasi cha kusema eti "WAMEKWISHA PITA MITUME KABLA YAKE". Kwani Isa Bin Maryam alikuwa anashindana na Allah na mtume wake Muhammad, mpaka kusema eti wamekwisha pita mitume kabla yake? Nani hajui hilo kuwa kulikuwa na mitume kabla ya Isa bin Maryam? Mbona Allah hakusema maneno haya machafu na ya dhihaka kwa Muhammad?
Eti, Isa na Mama yake walikuwa wanakula chakula!! Hivi wapi Isa na Mama yake walisema hawali chakula? Allah mbona unaonyesha kupaniki namna hii?
Angalia jinsi Allah anavyo endeleza chuki zake kwa Isa Bin Maryam, MARA ASEMA KAZALIWA CHINI YA MTENDE, MARA ASEME ISA KAUBWA KWA KUSEMA KUWA NA ISA AKAWA.
UTATA WA KWANZA: ISA KAZALIWA CHINI YA MTENDE
Tofauti ya kuzaliwa Isa ni hii
- Isa alizaliwa katika shina la mtende, Qr, 19:23 Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa! http://www.quranitukufu.net/019.html
Umesoma mwenyewe kuwa Isa anazaliwa chini ya Mtende. SASA ONA MAAJABU YA ALLAH HAPA CHINI.
UTATA WA PILI: ISA BIN MARYAM KAUMBWA
Qr. 3 au surat Imran 59
“Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa”http://www.quranitukufu.net/003.html
Ngugu msomaji, Isa bin Maryam haijulikani alikujaje maana Allah anaweka UTATA mkubwa sana. Mara asema kazaliwa na Maryam, mara asema kaumbwa kwa kusema kuwa na Isa akawa, hivi Isa Bin Maryam alimkosea nini Allah mpaka afanywe namna hii? Allah, kwanini unamchukia Isa Bin Maryam namna hii?
Allah anaendelea kusema kuwa eti, Isa atakapo kuja tena ataoa na kuzaa watoto. Hii nayo ni chuki kubwa kubwa kutoka kwa Allah.
Soma:
ISA BIN MARYAM ATAKAPORUDI, ATAOA NA KUZAA WATOTO
Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk.1159 na Sahih Muslim, vol. 1 uk 92 wanadai kwamba Isa atakaporudi ataishi miaka arobaini (40), muda ambao atakuwa ameoa na kuzaa watoto, na atafanya ibada ya hija.
Hivi kwanini Allah anapenda kulazimisha mambo? Kama Isa Bin Maryam alitaka kuwa na Mke, si angeoa alipo kuja mara ya kwanza? Lakini Allah na Muhammad wanatuambia uongo eti Isa anakuja Kuoa, hivi, kwani kuoa ni lazima?
Ndugu msomaji, nategemea unaziona chuki kubwa kubwa za Allah kwa Isa Bin Maryam, ETI ISA BIN MARYAM SI CHOCHOTE, kama vile Isa Bin Maryam alikuwa anajigamba kwa Allah kuwa yeye ni zaidi? Hivi Allah kwanini unamchukia Isa bin Maryam?
Labda kwasababu Isa bin Maryam aliumba ndege kutoka UDONGO na Muhammad hakuwai fanya muujiza hata chembe moja.
Labda kwasababu Isa bin Maryam alizaliwa bila ya Baba na Allah hana uwezo wala ubavu wa kuwa na Mwana bila ya MKEWE Allat.
Zipo sababu nyingi tunaweza zitumia kama ushahidi wa Allah na Muhammad kumuonea WIVU Isa Bin Maryam.
Swali kwa Allah na Waislam: Kwanini Allah alisema " Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume"? Kwani Allah alifikiria Isa ni nani? Allah si anadai alimuumba yeye, mbona inaonekana kama vile Allah anajibizana na mtu? Allah, hivi Isa Bin Maryam ni nani kwako? Maana inaonekana kuwa umepaniki na humjui Isa Bin Maryam.
HIVI KWANI ISA BIN MARYAM ALIJIITA NANI? Mpaka uanze kutoa maneno makali na dhihaka namna hii ambayo hukuwai sema kwa Mtume mwengine?
Eti, Isa Bin Maryam si chochote, hivi, Isa bin Maryam alisema yeye ni nani mpaka uanze kujihami namna hii NA KUSEMA "ISA SI CHOCHOTE"?
Eti, Isa na Mama yake wanakula chakula: Kwani ISA NA MAMA YAKE walisema hawali chakula?
Allah, kwanini unamchukia Isa Bin Maryam namna hii?
Sina la ziada zaidi ya kuwaonea huruma Waislam wanao fuata Allah na marehemu Muhammad wenye chuki kubwa kubwa tena kwa viumbe anavyo wana dai kuwa vimeumbwa na Allah.
Poleni sana Waislam kwa msiba huu.
Katika huduma Yake,
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 8, 2016

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW