Wednesday, August 10, 2016

MAPEPO NI NINI? [SEHEMU YA TATU]

Somo: MAPEPO
Mada ndogo: “Mtu anawezaje kupata mapepo?”
Lengo kuu: kuzijua mbinu zamapepo na kujilinda nazo
Lengo mahsusi: kudumu katika maombi ya vita kuzipinga roho za kipepo.
Kama tulivyokwisha kuona kuwa pepo ni roho wachafu wasio na mwili wala umbo wenye uwezo wa kuingia ndani ya kiumbe hai na kuchukua umbo na sura ya kiumbe huyo,pamoja na namna mwanadamu anavyoweza kujikuta katika uhusiano na pepo kupitia ibada za sanamu, sadaka, kuyafuga n.k. hapa tutaendelea kujifunza juu ya habari hizi ambazo kila mtu ni vema akizijua.
Wakati mwingine, mtu huweza kujikuta katika hali ya kuvamiwa bila yeye kujua. Ndugu yangu mpendwa, kuvamiwa na pepo si mpaka uugue au ujisikie kuwa dhaifu, pepo huweza kuharibu vitu vyako pole pole, mtu aliyevamiwa na pepo, anaweza kumvuruga awe na hasira tu, asifanikiwe katika shughuli zake tofauti kama vile biashara, masomo, kazi ya ajira, ufugaji,kilimo n.k.
Mtu aliyefungwa kwa namna hii, huambiwa kuwa nyota yake imechukuliwa, na hapa ndipo waganga wa kienyeji na waaguzi husema kuwa umetupiwa mikosi au mizimu imekasirika na kupaswa kutaaswa kwa kuogeshwa dawa, kuchanjwa au kunyweshwa; hatua hii ni hatari sana, kwa humfanya mwanadamu aingie mikataba mingine na mapepo, na hii huwa ni njia ya moja kwa moja, baada ya kipindi fulani, ile hali ya zamani hujirudia na kulazimika kwenda kwa mganga tena ili kukupatia dawa kali zaidi, bila kujiujua unakuwa unafanya mikataba migumu zaidi na kuzidi kuangamia; utakuta mtu anapewa miiko mikubwa mikubwa ambayo haitekelezeki na mwisho wake mtu huyu anakuwa mtumwa na miiko ya kipepo na anapoivunja basi humwangamiza kabisa.
Mpendwa, dawa iko kwa Yesu, jisalimishe leo uwe huru. Yeye pekee ndiye anayeweza kukuweka huru, ndiye anayeweza kuisafisha nyota yako, ndiye anayeweza kukuinua, njoo kwake leo, usikubali kudanganywa,Yesu ndiye yote ndani ya yote. Haleluya.
Zifuatazo ni njia kuu tano za mtu kupatwa na mapepo;-

JE, UNAFAHAMU KUWA MAKAFIRI NDIO WANAOSEMA DINI MBELE YA MWENYEZI MUNGU NI UISLAM?



LAANA MBAYA YA KAFIRI NI KUMZULIA UONGO MWENYEZI MUNGU KUWA ANAYO DINI
KAFIRI SIO TUSI BALI NI SIFA AU JINA TUU LENYE MAANA YA MPINGA IMANI AU DINI AU KUMZULIA MWENYEZI MUNGU UONGO, AU ANAE ENDA KINYUME NA AMRI ZA MWENYEZI MUNGU ZILIZO KUWEPO KABLA YA QURAN.
SHALOM SHALOM
Ndugu msomaji,
Hakuna siri katika hili jambo la kumzulia UONGO Mwenyezi Mungu kuwa anayo dini. Waislam wamekuwa mstari wa mbele kuuliza hivi: NI IPI DINI YA KWELI YA MWENYEZI MUNGU? Mtafutaji ukweli mara nyingi anafikia mahali ambapo anatatizika pale anapotambua kuwa kila dini, Imani, dhehebu, ideolojia na falsafa yoyote inadai kuwa ndiyo njia ya pekee iliyo sahihi kwa mwanadamu. Kwa hakika, zote zinawahimiza watu kufanya mambo mema na mazuri. Hivyo, ipi ndiyo iliyo sahihi? Haiwezekani zote kuwa sahihi kwa vile kila moja inadai kwamba zile nyengine hazipo sawa. Kwa hivyo, vipi mtafutaji haki na ukweli ataweza kuchagua njia ya sawa.
Kafiri anasema moyoni mwake, ‘‘Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislam.’’ Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa, hakuna atendaye mema.
Njia sahihi ya kumtafuta Mungu lazima itoke kwa Mungu. [[Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu. 1 Petro 3:18]] Na ndio maana Yesu alisema kuwa yeye ni Njia Kweli na Uzima. Mungu hana dini na hakuwai mwambia Adam awe na dini. Hakuna huu ushahid katika Taurat. Zaidi ya hapo hakuna ushahid wowote ule katika Zaburi au Injili kuwa Mungu aliwaamrisha watu wafuate dini yake, la hasha, ila tunasoma kuwa Yesu alikuja kutengeza njia ya kwenda kwa Baba yake. [[Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. Yohana 10:10]]
ALLAH ANASEMA DINI MBELE YA MWENYEZI MUNGU NI UISLAM, AU SIO?

JE, IBADA ZA WAFU NI ZA KIBIBLIA?


Ukweli hakuna Andiko lolote lenye pumzi ya Mungu mahali popote linasomeka kuwakumbuka marehemu, iwe kwa dakika moja au kwa dakika mbili. Lakini lipo Andiko linasomeka, "wafu hawana Ijara tena katika nchi ya walio hai". Kwa hiyo kwa mujibu wa andiko hilo, hata misa za wafu HAZIRUHUSIWI, ikimaanisha arobaini za marehemu wote hazina nafasi ndani ya Neno la Mungu.
WAFU/MFU NI NANI?
Utangulizi:-Neno wafu ndani ya Biblia limetumika likiwa na Maana zaidi ya moja, Linaweza kutumika kama
i. Ni hali ya Roho kutengana na mwili yaani Kifo cha mwili.(Luka 8:55, Muhubiri 9:5)
ii. Ni hali ya Mtu kutengana na Mungu au kuvunja uhusiano mwema na Mungu (Kutenda dhambi) yaani Kifo cha Kiroho (Ayubu 21:25)
Kifo cha kiroho. Kuna aina tatu ya wafu katika eneo hili ambayo mtu anaweza kufa kiroho lakini bado anaendelea kuwa hai kimwili. Huyu anaweza akatubu na kufufuka katika wafu akawa hai tena .Pia mtu anaweza kufa kiroho na kimwili maana yake Roho imekufa na mwili umekufa hana nafasi ya kutubu tena. (Ufunuo 20:5). Kifo hiki ni kibaya zaidi na kinatisha. Ambacho Bwana Yesu alisema msiwaogope wawezao kuuwa mwili bali Mungu mwenye uwezo wa kuuwa mwili na Roho, (Soma Matayo 10:28). Kifo cha tatu ni Mtu kufa kimwili lakini bado anaendelea kuishi Kiroho. Hapa Yesu alisema mtu akiniamini mimi na kutimiza neno langu ataishi hata kama akifa.

TUMIA MAMLAKA ULIYOPEWA NA MUNGU


Mungu ametupa mamlaka ya kipekee sisi wanadamu katika ulimwengu huu sema tu ni kwamba tunashindwa kutumia hiyo mamlaka. Ukisoma katika Mwanzo 1:27-30 Biblia inasema Mungu akamuumba mwanadamu kwa mfano wake na pia akampa mamlaka ya kutawala samaki wa baharini na ndege wa angani na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu nchi, vyote hivi mwanadamu alipewa kuvitawala na Mungu. Swali la kujiuuliza ni kwamba je inakuwaje mwanadamu wa leo anakuwa hana uwezo wa kuvitawala vitu hivyo?
Tunaweza kuona kuwa baada ya anguko la Adam mwanadamu amekuwa akishindwa kuvitwala viumbe vyote na vyote vilivyomo duniani na hii imekuwa ni kifungo kikubwa kwa wanadamu hadi leo hii kwa maana toka Adamu afukuzwe katika bustani ya Eden watu wamekuwa wakihangaika huku na kule bila kujua nini cha kufanya sababu shetani amekamata fahamu zetu ili tusiweze kukumbuka na kutumia mamlaka hii tuliyopewa na Bwana. Lakini Mungu kwa upendo wake na huruma zake na kwa Neema yake ya pekee alimtoa mwana wake Yesu Kristo ili kutupatanisha naye kutuwezesha kutumia ile mamlaka ya kutawala dunia kama ilivyokuwa kusudi lake hapo awali la kumuumba mwanadamu.
Jambo la msingi na la kipekee ni kupokewa Neema hii tuliyopewa bure ya kumkubali Yesu kuwa ni Bwana na Mwokozi ndani ya maisha yatu ili tuweze kutumia tena yale mamlaka. Ukisoma ktk kitabu cha TITO 2:11-12 utaona kuwa Biblia inatuambia kuwa Neema ya Mungu imefunuliwa kwetu nayo inatufundisha kuukataa ubaya .... hii Neema iliyofunuliwa ndio wokovu wenyewe ambao unatuwezesha sisi wanadamu kukiri kuwa Yesu ni Bwana, kwani yeye alifanyika chombo cha kuweza kutubebea ile laana aliyoipata Adam baada ya anguko. Soma Isaya 53:4-5 .... kwa kupigwa kwake sisi tumpona. Hivyo basi Bwana wetu Yesu ameturejeshea ujasiri na nguvu na uweza wa kutumia ile mamlaka ambayo tunatakiwa kuwa nayo kwani kwa kuliita jina lake tu magonjwa, pepo, na nguvu zote za giza zinakimbia. Hakutakuwa tena na maonevu yaletwayo na yule mwovu shetani katika maisha yetu hofu, kuyumba katika kipato, biashara, ndoa, watoto hata katika ulimwengu wa kiroho kwani utakuwa tayari unajua ni jinsi gani unaweza kupigana vita na ukaweza kuvishinda hakuna kitakachoweza kukudhuru kwani uweza unao mikononi mwako tayari ni jinsi gani tu unaweza kutumia na ni silaha zipi utumie ili uweze kushinda.

MAPEPO NI NINI [SEHEMU YA NNE]


Somo: MAPEPO
Mada Ndogo: Dalili 10 za mtu mwenye mapepo.
Lengo kuu: kuyajua mapepo na kazi zake.
Lengo Mahsusi: Kila mtu kuweza kumpinga pepo na kazi zake zote kwa Jina la Yesu.
Bwana Yesu asifiwe sana,
Ndugu mpendwa, katika sehemu tatu zilizotangulia, tumejifunza maana, asili/ chanzo cha ,mapepo. Natumai umebarikiwa sana.
Haleluya! Ndugu mpendwa, napenda kukukarisha katika mwendelezo wa mafundisho yetu juu ya mapepo, ambapo kwasasa tutaangalia kwa kina tabia/dalili za mtu aliyevamiwa na mapepo.
Ni muhimu sana kujua hili. Tabibu mzuri, ni yule anaetibu ugonjwa anaoufahamu, hivyo ni muhimu sana, kujifunza habari hizi,ili kuweza kukabiliana na kila hali kwa usahihi wake.
Pamoja na dalili nyingine ambazo sitazitaja; kwapamoja tuzichunguze hizi zifuatazo:-
(a) Kuwa na nguvu nyingi. Kwa hali isiyo ya kawaida, mgonjwa aliyedhoofu na pengine kulala kwa muda mrefu akiwa hajiwezi, huweza kuwa na nguvu nyingi sana na za ajabu. (Luka 8:28, Marko 5:3&4, Luka 8:29, Matendo 9:15&16). Mtu huyu, huweza kuwa mkali sana, mgomvi na wakati mwingine huweza kuwa na uvutano kama umeme/shoti. Hujiamini sana na hukasirika zaidi anapowaona wanamaombi.
(b) Kujaa ujasili na kujiamini kupita kiasi. Mtu aliyevamiwa na pepo wachafu, hujiamini na kujiona shujaa; tukio hili hulenga kumchosha mwili, kuwaumiza wanaomuuguza na yeye mwenyewe. Anaweza kujiangusha bila sababu,kujiuma meno, kutafuna baadhi ya sehemu zake za mwili,kujipiga,kujiuma meno,kujikatakata n.k. (Mathayo 17:15, Marko 5:5). Pia,mapepom hutumia njia hii ili watu wamwogope washindwe namna ya kumsaidia mtu wa namna hii kwa kuhofia usalama wao, na kubaki kumwonea huruma tu.
(c) Huonesha maumivu hata anapojiumiza mwenyewe ila haachi kujiumiza. Hili hutokana na kuwa yeye hajitawali,bali hutawaliwa na kuongozwa na pepo wabaya. Huumizwa sana ndani kwa ndani,ila hulazimika kuendelea kufanya kile kitu kinachomuumiza. Mfano, kujikatakata,kujiangusha, kurukaruka n.k. (Marko9:20-22).

KIJIJI KIZIMA HUKO UFILIPINO CHA OKOKA NA KUWA WAKRISTO



Habari kutoka "Christian Aid Mission" zinasema kuwa Kijiji cha Mindanao chenye Kabila la Manobo kilicho Kaskazini ya Filipino kimegeuka na kuwa Kanisa.
Baada ya kuangalia sinema ya Passion of Christ, wanakijiji wa Mindanao walimpokea Yesu na kuwa Wakristo.
Mavuno ni mengi sana na Yesu anaendelea kuokoa vijiji kwa vijiji.

MWANA MUZIKI SNOOP DOGG HIVI KARIBUNI KUPITIA VIDEO KATIKA MITANDAO AMESEMA AFADHALI AWE NA YESU KRISTO KULIKO DHAHABU NA UISLAM ....................


Baada ya kuuchoka Uislam na kuona hauna tija, Mwanamuziki wa Rap Snoop Dogg ameamua kusema yaliyo kwenye moyo wake kuwa afahdali awe na Yesu.
Hii ni habari njema na pigo kubwa kwa Waislam ambao walikuwa wakisema kuwa Snoop amesilimu.
Kwa habari kamili ingia hapa:
Rapper Snoop Dogg recently surprised fans by sharing a video on social media in which he sings the famed Gospel song, "I'd Rather Have Jesus."
"I'd rather have Jesus than silver and gold," Snoop, real name Cordozar Calvin Broadus, Jr, repeatedly sings in the video which he posted on his Instagram account (@snoopdogg) on Sunday. "Silver [and] gold. @dashradio Cadillac music Sunday gospel mix," he captioned the video.
Premiere notes that the song was made famous during Billy Graham's evangelistic rallies by worship leader George Beverly Shae, and includes the lyrics "I'd rather have Jesus than worldly applause/I'd rather be faithful to His dear cause/I'd rather have Jesus than worldwide fame/I'd rather be true to His holy name."
While some fans expressed astonishment at the move, others were thrilled to see the rapper praising the Lord.
"Praise Him, Snoop!" wrote one fan.
"Fire refines silver & gold; but the good Lord refines the hearts of man," wrote another.
"Right on Snoop!! I start every day off with Jesus. Now I got you on my prayer list. God bless brother!" added another fan.
Others suggested the "Gin and Juice" singer may be experiencing a change of heart.

JE, UNAFAHAMU KUWA WEWE UNAYE PINGA UUNGU WA YESU NI KAFIRI?

JE, UNAFAHAMU KUWA WANAO PINGA WOKOVU KUPITIA YESU KRISTO NI MAKAFIRI?
Ndugu msomaji,
Utawasikia wakisema, Uislam ndio dini ya haki na ya Mwenyezi Mungu. Wanaendelea kusema kuwa, hakuna kuokoka hapa dunia bali Akhera. Hii ndio sifa ya Kafiri, anapinga WOKOVU KUPITIA YESU KRISTO. ZAIDI YA HAPO WANAPINGA UUNGU WA YESU.
KAFIRI SIO TUSI BALI NI WASIFA WA MTU ANAYE PINGA UPENDO WA YEHOVA. KAFIRI NI MTU YEYOTE YULE, AU KIUMBE CHECHOTE KILE KINACHO PINGA UPENDO WA MUNGU KWA BINADAMU WA KUJA KUMUOKOA KATIKA DHAMBI.
NENO KAFIR LINAMAANISHA ASIYE AMINI. Waislamu hawaanini kuwa Yesu Kristo ni Mungu. Waislamu hawaamini kuwa Yesu Kristo anaweza kuponya dhambi za mwanadamu. Waislamu hawaamini kuwa Yesu Kristo yu hai. Hivyo waislamu ni makafiri.
NENO Kāfir INAMAANISHA MTU AMBAYE ANAJIFICHA AU ANAFICHA MABAYA. Waislamu wanaficha ajenda zao kutumia TAQIYYA NA KITMAN. Na kumbuka pia Quran inaruhusu waislamu kudanganya. Wanadanganya kuwa Yesu sio Mwokozi wa Ulimwengu.
UKIMSIKIA MTU ANASEMA MUNGU ATAWEZAJE KUJA DUNIANI KATIKA MWILI, BASI HUYO NI KAFIRI MAANA ANAFIKIRIA MUNGU HANA UWEZO WA KUFANYA ATAKALO NA ANAMLINGANISHA MUNGU NA BINADAMU.
JE, YESU NI NANI KWAKO?

JE, UNAZIFAHAMU KAFARA ZA KIMASHETANI?


Utangulizi:
Kwa akili zawatu zilivyo, wakisikia neno kafala wanakimbilia kwenye waganga wa kienyeji, lakini neno hili kafara kwenye Biblia ndio linaitwa dhabihu kwenye Biblia, kuna maadiko kadhaa yanayo taja kafara kwenye Biblia kama ifuatavyo :- Mambo ya Walawi 2 :2, 9, 16; Mambo ya Walawi 10:13, 14, maandiko haya yanataja neno kafara kwenye Biblia na limeonekana mara nyingi, hii ni kukuonyesha kuwa neno kafala lipo kwenye Biblia na lina maana sahihi, kwahiyo Kafara ni Sadaka inayotolewa kwa ajili ya kupokea jambo fulani kutoka ulimwengu wa roho aidha kwa Mungu au kwa Shetani.
Maana ya Kafara:
KAFARA NI SADAKA INAYOTOLEWA KWA AJILI YA KUPOKEA JAMBO FULANI KUTOKA ULIMWENGU WA ROHO, AIDHA KWA MUNGU AU SHETANI.
KUWA MAKINI NA KAFARA ZILIZOTOLEWA KWA MASHETANI
Kumbe shetani anaweza kutolewa kafaraza aina mbalimbali inaweza kuwa ya vinywaji, uji, nafaka, harufu, watoto au watu wazima; na ni muhimu kuwa makini sana na kuhudhuria sherehe ambazo si za ki Mungu kwasababu waweza kujikuta unashiriki kwenye sadaka hiyo. Kuna watu ambao matatizo yao yamewaanza baada ya kushiriki chakula cha kafara jambo hili Biblia imekataza kwasababu ya madhara yake.
Ufunuo 5:8; 8:3 hapa Biblia inataja Sadaka ya harufu, na ndio maana ukienda kwenye maduka mengi utakuta wameweka vitu vinaitwa ubani; Hii ni Sadaka au Kafala ya kuteketezwa kwa majini, Isaya 43:23; Yeremia 6:20; 17:26, Ubani na Udi ni Sadaka ya kuteketezwa, kimsingi; ile harufu ndiyo inayoifanya iitwe Sadaka ya kuteketezwa, kwahiyo mtu unayemuona anachoma ubani ni anakuwa anatoa kafara ya ubani. Nehemia 13:9. Sadaka za unga na Sadaka za ubani. Kimsingi watu tuliookolewa hatutoi sadaka za ubani kwasababu Biblia inasema maombi ya watakatifu ndio sadaka ya harufu kwa Mungu, Yohana 19:39.

MAPEPO NI NINI? [SEHEMU YA TANO]


Somo:MAPEPO
Mada Ndogo: Njia 8 za kuyashinda mapepo.
Bwana Yesu asifiwe sana,
Ndugu mpendwa, katika sehemu Nne zilizotangulia, tumejifunza maana,asili/ chanzo cha mapepo na dalili kuu za mtu alievamiwa na mapepo. Natumai umebarikiwa sana. Haleluya! Ndugu mpendwa, napenda kukukaribisha katika mwendelezo wa mafundisho yetu juu ya mapepo,ambapo kwasasa tutaangalia kwa kina mbinu/njia za kumshinda pepo.
Ndugu yangu mpendwa, kanisa la leo, liko katika mapambano makubwa sana. Upinzani mkubwa unatoka kwa ibilisi alie shetani, mwenye sifa kuu ya uharibifu.
Hatahivyo, Mungu ameliweka kanisa kwa wakati huu wa mashambulizi kwaajili ya kuukomboa ulimwengu. Amelifanya kanisa kama asikari wa mwamvuli ambaye hushushwa katikati ya eneo ambalo bado liko mikononi mwa adui, ila ikikusudiwa kupambana na hata kushinda. Kwa mantiki hiyo, si hoja tena juu ya kushinda kwa kanisa, bali daima linashinda na litaendelea kushinda.
Katika mwendelezo wa somo letu, leo tutaziangalia njia/uwezo wa kuyashinda mapepo.
Kwanza; Yesu alitoa mamlaka kwa kanisa juu ya mapepo (Marko 16:17). Uweza huu wa ajabu, Mungu ameutoa kwa watu wote wanaomwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wao (Yohana 17:20-23). Ujue, watu wengine wanateseka kwa kuwa hawajui, yule aliye ndani yao. Biblia inasema, aliyeko ndani ya aliyeokoka ni mkubwa mno, maana yake ni kuwa, anayashinda mapepo. Usikubali kuteswa na mapepo, kemea kwa jina la Yesu, lililo jina kuu kupita majina Yote, nawe utakuwa huru.
Pili; Mapepo huamriwa kwa jina la Yesu tu (Marko 16:17). Jina maagano na ahadi ni jina la Yesu tu. Usitumie jina lingine lolote lililo nje ya jina la Yesu. Ni jina la Yesu pekee huweza kuponya,kuokoa na kuhuisha, hata mapepo yanajua hivyo. Kutumia majina mengine ni sawa na kukosea anwani wakati wa kutuma barua, ni kweli barua itaenda ila usitegemee kupokea majibu uliyotarajia kwa kuwa barua haitaenda kwa mlengwa.
Tatu; Yafukuize kwa kutumia mamlaka uliyonayo kama ilivyoelezwa katika hoja ya kwanza. Usiyabembeleze. Tumia amri. Watu wengine hutumia majadiliano, huyafanyia sherehe, huyafukizia uvumba,udi na hata kuyachezea muziki wa asili. Ndugu yangu, waswahili wanasema” ukifanya urafiki na mkia wa fisi,utakufirisi” usikubali kukaa meza moja na mapepo, shetani habembelezwi, yatimue kwa mamlaka ya Jina la Yesu (Mathayo 12:28,Luka 11:20).

TRENDING NOW