Friday, September 2, 2016

JE, MUHAMMAD AMETABIRIWA KWENYE BIBLIA (SEHEMU YA PILI)


Katika makala yaliyopita tuliona hoja za ndugu wa Kiislamu wanavyojaribu kwa juhudi nyingi kuonyesha kwamba Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia.
Katika makala hayo niliahidi kuwa nitaeleza jinsi ambavyo hoja zao hazina ukweli wowote. Licha ya kwamba Mungu wanayemwamini amewahakikishia kwamba Muhammad ametajwa kwenye Biblia, ukweli ni kwamba hajatajwa hata kidogo!
Katika sehemu ya kwanza ya mfululizo huu, nilimalizia kwa kunukuu kile ambacho Yehova, Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, anasema juu ya Neno lake. Hebu tuangalie tena baadhi ya maneno hayo. Imeandikwa:
Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho,tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.
Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. (1 Wakorintho 2:12-15).
Tatizo mojawapo kubwa ninaloliona mara nyingi kwenye Uislamu na Waislamu ni kutazama mambo kwa jinsi ya mwili. Hapo ndipo penye shida kubwa yanapokuja masuala ya rohoni.
Kama uko kwenye safari ya kimaisha katika ulimwengu wa kimwili na unalenga kuishia kwenye ulimwengu wa kiroho (jambo ambalo ndilo linaloendelea kwa wanadamu wote), basi ni lazima utafute maana ya mambo ya ulimwengu wa mwilini kulingana na ulimwengu wa rohoni. Ukiishia tu kutazama mambo katika mwili, una hasara kubwa!!
Ni lazima kutambua kuwa Mungu hatupi ujumbe wake ili tuweze kuwa matajiri, maarufu na wenye vyeo wa hapa duniani. Kama hayo ndiyo malengo yako makuu katika maisha haya, basi wewe una hasara kuliko watu wote. Hayo si mambo ya msingi. Mungu ametuweka duniani kwa makusudi makubwa zaidi ya hayo. Yeye analenga mambo yadumuyo; si mambo ya kupita. Hivyo, kiini hasa cha ujumbe wa Mungu wa kweli ni maisha ya milele yajayo kwenye ulimwengu wa roho.
Sasa, kwa kuwa ndugu zangu hawa, wao wako zaidi katika mambo ya hapa duniani, ya kimwili, haishangazi basi kumwona Ahmed Deedat na wenzake wakiishia kuangalia tabia za kimwili za Musa na kuzilinganisha na tabia za kimwili za Muhammad na kusema kwamba eti, huo ndio uthibitisho kwamba maandiko ya Biblia wanayonukuu yanamzungumzia Muhammad.

UISLAM NI DINI YA KIPAGANI (SEHEMU YA KWANZA)


Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni -
Allah alitokea wapi?
Uislamu unajinadi kwamba Allah ndiye Mungu yuleyule aliyejishughulisha ya Wayahudi tokea nyakati za Ibrahimu katika Agano la Kale. Je, jambo hilo ni kweli?
Uislamu ulianza na Muhammad kwenye miaka 600 baada Kristo. Je, kabla yake imani za Waarabu zilikuwaje? Je, yako mambo yoyote kutoka kwenye imani hizo ambayo yaliingia kwenye Uislamu? Kwa maneno mengine, je, Uislamu hauna upagani ndani yake?
Fuatana nami kwenye makala haya marefu yanayochambua chimbuko la Uislamu ili tuweze kuona iwapo upo uhusiano wowote kati ya Uislamu na upagani uliokuwa ukitawala miongoni mwa jamii za Waarabu kabla ya kutokea kwa Muhammad?
Asili Ya Allah
Jamii za wanadamu KOTE duniani zimekuwa na kawaida ya kujiuliza ni wapi ulimwengu huu umetokea, nini maana ya maisha na wapi watu huenda baada ya kufa. Matokeo yake, kila jamii ilifikia kuamini kuwa kuna aliye na nguvu (au walio na nguvu) kuliko wanadamu wote ambao ndio wanapaswa kuabudiwa na kuombwa msaada pale matatizo yanapotokea.
Hawa wenye nguvu wakajulikana kwa majina mbalimbali kwenye jamii tofauti. Vilevile, kila jamii ilianzisha utaratibu maalum wa kuwasiliana na hawa wenye nguvu, yaani miungu.
Lakini jambo moja ni dhahiri, kwamba UKIACHA JAMII YA WAYAHUDI PEKE YAO, jamii zote za wanadamu zilizobakia duniani – iwe ni Afrika, Ulaya, Asia, n.k. - zimeanzia kwenye ibada za kipagani. Jamii hizi ziliabudu miungu mbalimbali. Na miungu hii iliwakilishwa na vitu kama vile milima, miti mikubwa, jua, mwezi, majoka makubwa, sanamu, wafalme, n.k. Kwa mfano, Warumi walikuwa na miungu kama vile artemi, jupiter, minerva, atlas, n.k. Tazama hapa. Wagiriki walikuwa na miungu kama vile chronos, dionysus, eros, ares, appolo, hermes, poseidon, n.k. Tazama hapa. Wahindi wana miungu kama vile durga, ganesha, garusha, brahma, n.k. Tazama hapa. Imani hizi za kipagani ziliweza hata kukua sana na kuenea maeneo mengi. Kwa mfano, imani ya ubudha ni imani ya kipagani lakini iliweza kuenea sehemu kubwa sana ya Asia – India, Japan, Sri Lanka, Uchina, n.k.
Kwa hiyo, jamii za Kiarabu, kama ilivyo kwa wanadamu wengine, vilevile hazikuwa tofauti. Jamii hizi nazo zilikuwa zina ibada zao za kipagani.

WAKRISTO 27 WAFUKUZWA SAUDI ARABIA KWA KOSA LA KUWA NA BIBLIA


Wakristo 27 wamefukuzwa nchini Saudi Arabia baada ya kukutwa na Biblia nyumbani kwao.
Kabla ya kufukuzwa na kurudishwa kwao, Wakristo hao walihukumiwa kwa kosa la kufanya ibada ambayo sio ya Kiislamu.
Askari wa Kidini wa Saudi Arabia katika eneo la Al-Aziziyah huko Mecca walithibitisha kukamatwa kwa hao Wakristo huku wakiwa katika ibada ambayo si ya Kiislamu.
Saudi Arabia ndio nchi yenye sheria kali za kidini na yenye chuki kubwa kwa Wakristo na Ukristo.

IMAM AKAMATWA KWA KUBAKA MVULANA WA MIAKA KUMI (10) HUKO NIGERIA




Mkuu wa Usalama wa Jimbo la Nasarawa (NSCDC) amemkamata mwalimu wa dini ya Kiislam mwenye umri wa miaka 45 kwa kosa la kubaka mvulana ambaye anadai alikuwa akimfundisha dini huko katika kitongoji cha Lafia.
Imam Shahidu Suleh, ambaye ni Maalim vile vile, amekuwa akimbaka (Almajiri), Okasha Ishaka alisema. Huyo mtoto alisema kuwa, Maalimu alikuwa anambaka kila mara, na alimtishia kumuua, kama angemsema kwenye vyombo vya sheria.

UISLAM NI DINI YA KIPAGANI (SEHEMU YA PILI)


Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni –
Ka’aba
Katika sehemu ya 1 ya makala haya tuliangalia kuhusu asili ya Allah. Katika sehemu hii ya 2 tutaongelea kuhusiana na mji wa Makka na ka'aba, ambayo ni madhabahu kuu ya Uislamu.
Mji wa Makka ndio kitovu cha Uislamu duniani. Kwenye mji huu ndiko iliko Ka’aba, au kama wanavyoamini na kuiita Waislamu Bait – ul- Haram; au Bait – ul- Allah, yaani ‘nyumba ya Allah’ au ‘nyumba ya Mungu’. Na kila Mwislamu kokote duniani anatakiwa kuswali swala 5 kila siku huku akielekeza uso wake Makka iliko hiyo nyumba ya Mungu wao. Vilevile, kila mmoja wao anatakiwa kwenda Makka kuhiji walau mara moja katika maisha yake, maana hija ni moja ya nguzo kuu katika Uislamu. Kwa maana nyingine, Ka’aba ndiyo madhabahu kuu katika Uislamu.
Ka’aba ni nyumba ya umbo la takriban mchemraba ambayo, pamoja na vitu vingine vichache iliyo navyo, kuna kipande cheusi cha jiwe ambacho kimejengewa ukutani kwenye kona mojawapo. Hivyo, Waislamu wanapoenda Makka kuhiji huzunguka Ka’aba na pia kulibusu jiwe hilo, au kuligusa tu, na kama ikishindi kana, basi japo kulinyoshea mkono.
Zamani, Allah anasema, kuwa Muhammad alikuwa akitazama mbinguni wakati anapoomba [nadhani kila mwenye imani juu ya Mungu anaamini kuwa Mungu yuko juu – na huo kusema kweli nadhani ndio mtazamo sahihi kabisa].
Lakini Allah akamwambia mtume wake:
We have certainly seen the turning of your face, [O Muhammad], toward the heaven, and We will surely turn you to a qiblah with which you will be pleased. So turn your face toward al-Masjid al-Haram. And wherever you [believers] are, turn your faces toward it [in prayer]. Indeed, those who have been given the Scripture well know that it is the truth from their Lord. And Allah is not unaware of what they do. (sura Al Baqarah 2:144) – Sahih International Version.
Yaani:

MTUME MUHAMMAD AONEKANA JEHANNAM


Mungu hutufunulia mambo mbalimbali kupitia watumishi wake mbalimbali ili kutujulisha yale yaliyopo na hata yajayo; katika ulimwengu huu na pia ule ujao. Wapo watu wengi ambao Mungu amewatumia kutufahamisha juu ya mbingu na hata juu ya kuzimu.
Bo Ra Choi ni mchungaji kutoka Korea ya Kusini. Mchungaji huyu amekuwa akionyeshwa maono mbalimbali na Mungu kuhusu mambo ya ulimwengu wa roho. Mojawapo ya maono aliyoonyeshwa yanamhusu Muhammad, mtume wa Uislamu.
Je, Muhammad yuko wapi hivi leo? Katika video hii, mchungaji Bo Ra Choi anafikisha kwetu ujumbe kwa namna ambavyo alisikizishwa Muhammad akisema kule aliko sasa.
Kwa maana nyingine, ananukuu moja kwa moja maneno ya Muhammad ili kwamba iwe ni kama vile tunamsikia Muhammad akizungumza.
Tafadhali zikiliza kwa makini video hii, kisha utaupata ujumbe wa Mungu anaouleta kwetu kupitia mtumishi wake, Mchungaji Bo Ra Choi.
........................
Lakini anachosema Muhammad humo ni nini hasa?

Kifuatacho ndicho anachokisema Muhammad humo
kwa kilio kikubwa:
...........................

JE, ASILI YA YESU NI WAPI?


Katika kujibu swali hili Bwana Yesu mwenyewe mara kadhaa aliwaelimisha Wayahudi juu ya ukweli kuhusu asili yake ili kuwasaidia kuondokana na dhana au mtazamo wa kumchukulia kama mtu mwenye asili ya kidunia na badala yake alitaka waone kuwa yeye alikuwako kabla ya kuja duniani kama mwanadamu kwa kusudi la ukombozi wa watu. Soma kwa makini maandiko haya:-
Yohana 8:23
Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu
Yahana 6:62
Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?
Katika maandiko hayo yote mawili, Bwana Yesu kwa uwazi kabisa anaweka bayana juu ya asili yake ya mbinguni kabla ya kufanyika mwanadamu na kuzaliwa na bi’ Mariam, katika andiko lile la kwanza Bwana Yesu anaweka utaofauti wa wazi baina yake na wanadamu wa kawaida kwa kusema ‘Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
Na katika tamko jingine Yesu anawauliza Wayahudi kuwa Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?, kwahivyo Yesu anaonyesha kuwa kabla ya ujio wake duniani kuna mahali (mbinguni) alikokuwako kwanza.
Asili ya Yesu na msingi wa mamlaka yake ya Uungu:
Uelewa juu ya asili ya Yesu linakuwa ni jambo rahisi tu sasa kadri ya msingi mzuri tuloujenga tangu mwanzo wa uchanbuzi wa mada hii na hususani kupitia matamko mbalimbali hata yale ya Yesu mwenyewe yanayotoa picha ya wazi kuwa Yesu hakuwa kamwe na asili ya dunia hii ya ubinadamu licha ya kwamba alizaliwa na Mariam kwakuwa pale alipozaliwa na Mariam haukua ndiyo mwanzo wa kuwepo kwakwe, bali kupitia kuzaliwa na Mariam alikuwa tu akitengenezewa njia ya kufunika mamlaka yake ya kuu ili aweze kumfikia mwanadamu kama tutakavyoona katika kipengele kinachofuata.
Hatahivyo kanuni za msingi zinazofanya Yesu kuwa mwanadamu wa asili ya kawaida hazikufikiwa katika mchakato wa kuzaliwa kwake, hebu tusome kidogo andiko hili’

MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KUFUGA WATUMWA

Watu wote wa kale ikiwa ni pamoja na wanazuoni wa siku hiziwanakubali ukweli wa utumwa katika Uislamu na kubainisha hadhi waliyonayo watumwa hao. Wanazuoni wote wa zamani na hata wa siku hizi wanakubaliana na ukweli wa Utumwa katika Uislamu, na kufafanua hali halisi ya hadhi ya watumwa. Nimechagua maoni ya wanazuoni maarufu kuliko wote ili kuonyesha nuru na misimamo yao.
Wakati tunaposema kwamba Uislamu hauamini katika haki za binadamu na wala hautambui uhuru wa wa watu binafsi, watu wengi hubisha.
Tena vita ambavyo Mohammed na wafuasi wake walipigana vilikuwa ni vita vya uvamizi ili kueneza Uislam kwa nguvu, kupora utajiri wa nchi, kutwaa mali za nchi, na kuwateka kinamama na watoto.
Tunakutana na umati wa watu ambao wanaelezea mshtuko wao na kutokubaliana. Kwa sababu ya kuto kuamini huko, vyanzo vyetu vya taarifa vitakuwa wasomi wa Kiislamu.
Msomi wa Al-Azhar wa Misri
Katika kitabu chake “You Ask and Islam Answers”, (Wewe Uliza na Uislamu Ukujibu), Abdul-Latif Mushtahari ambaye ni Mwangalizi Mkuu na Mkurugenzi wa Kuhutubia na Kuongoza katikaChuo Kikuu cha Azhar anasema (uk 51, 52),
“Uislamu haukatazi utumwa ila unashikilia kwa sababu mbili;
Sababu ya kwanza ni vita (Iwe vita ya wenyewe kwa wenyewe au vita na watu wa nje ambapo mateka wanauwawa au kufanywa watumwa) ilimradi tu vita si ya Waislamu wakipambana wenyewe kwa wenyewe- hairuhusiwi kuwafanya watumwa wavunja sheria au wakosaji kama wao ni Waislamu. Ni wale mateka wasio Waislamu tu wanaoweza kuuwawa au kufanywa watumwa.
Sababu ya pili ni watumwa watokanao na udhalilishaji utokanao na kuwaingilia watumwa hao kingono njia ambayo huweza kumpatia mwenye watumwa watumwa wengi zaidi.’’
Habari hii iko wazi kabisa kwamba wafungwa wote wa kivita lazima wauwawe au wafanywe watumwa.
Wanazuoni wa zamani wanakubaliana kabisa na swala hili kama Ibn Timiyya, Ibn Hisham, Malik, nk.Ibn Timiyya anasema,
(Toleo 32, uk 89)
“Mzizi wa mwanzo wa utumwa ni wafungwa wa kivita. Bonasi (zawadi) imekuwa halali katika taifa la Mohammed.”
Kisha (Toleo 31, uk 380) anaonyesha wazi na bila aibu,

JE, MUHAMMAD ALIKUWA JINI AU MTUME WA MAJINI?


1. Allah ateua Mtume wa Majini Quran 6: 130
2. Kumbe Muhammad ni Jini.
Ndugu zanguni,
Allah anasema katika Quran kuwa, ameteua Mtume kwa kila kiumbe mpaka Majini machafu. Hebu soma aya hapa chini
ALLAH ANASEMA KUWA MAJINI YANA MTUME WAO
Quran 6: 130. Enyi makundi ya majini na watu! Je, hawakukujieni Mitume kutokana na nyinyi wenyewe wakikubainishieni Aya zangu, na wakikuonyeni mkutano wa Siku yenu hii. Nao watasema: Tumeshuhudia juu ya nafsi zetu. Na yaliwadanganya maisha ya dunia. Nao watajishuhudia wenyewe ya kwamba walikuwa makafiri.
Swali lamsingi kwa Allah :
Jina la Mtume wa Majini ambaye ni Jini ni nani?
Kwasababu kila Umma ulipewa kitabu na mtume wake, Je, umma wa Majini walipewa kitabu gani?
Lakini nilipo soma Hadith nikagundua kuwa, Muhammad alikuwa anaongea na Majini na kuyafundisha Quran. Kumbe basi majini ndio yalipewa Quran. Kumbe basi mtume wa Majini ni Muhammad. Kumbe Muhammad alikuwa Jini.
MTUME MUHAMMAD AKUTANA NA MAJINI USIKU
Allah S.W.T. ametuhakikishia wazi kuwa ujumbe aliopewa Mtume S.A.W. ulikuwa kwa Wanadamu na Majini na Mashetani pia. Na katika Qurani na Hadithi za Mtume S.A.W. kuna dalili zilizo wazi zinazoyakinisha kuwa Mtume S.A.W. alikuwa akikutana nao na kuwafundisha dini. Na hata wakati mwingine Majini walikuwa wakitoa majibu mazuri zaidi kuliko Binadamu kwenye masuala ya dini. Na mfano ni wakati waliposomewa Suratir Rahmaan. Hadithi iliyopokelewa na Jaabir bin Abdallah R.A.A. na iliyotolewa na Ttirmidhi kasema, “Wakati ambapo Mtume S.A.W. alipowasomea Majini Suratir Rahmaan, “
لَقَدْ قَرَأْتُهَا ‘‘يعني سُورَةَ الرَّحْمَنِ’’ عَلَى الْجِنِّ …، فَكَانُوا أَحْسَنَ مَرْدُودًا مِنْكُمْ ، كُنْتُ كُلَّمَا أَتَيْتُ عَلَى قَوْلِهِ ]فَبِأَيِّ آلاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ[ قَالُوا: لا بِشَيْءٍ مِنْ نِعَمِكَ رَبَّنَا نُكَذِّبُ ، فَلَكَ الحمد

IMAMU MOHAMMED HUSSAIN NA MWENZAKE WAKAMATWA KWA KUBAKA MWANAMKE MWENYE MATATIZO YA AKILI



Mwanamke mwenye matatizo ya akili (miaka 22) amebakwa na Imamu wa Msikiti wa Meerut aitwaye Mohammed Hussain aliye shirikiana na Abdul Rashid kufanya huo unyama.
Imam Mohammed akiwa na Abdul walionekana wakiwa na huyo mwanamke usiku huku wakimburuza kwa nguvu. Walipo ulizwa na wapita njia, walidai walikuwa wanamsaidia ili asifanyiwe unyama na watu wabaya, lakini hapo baadae walimpeleka karibu na kituo cha mafuta "Petrol Station" na kumbaka.
Baada ya kumbaka, huyo Imam Muhammed na Abdul waliamua kumrudfisha walipo mtoa, ndipo Polisi waliwaona na kuwakamata.
Kwanza Imam Muhammad na Abdul walidai kuwa huyo mwanamke ni dada yao walipo ulizwa na Polisi, lakini huyo mwanamke aliwaomba Polisi wamsadiai ili awe huru kutoka wabakaji. Polisi walipo wauliza tena kuwa nini hasa kinaendelea, ndipo Imamu Muhammad na rafikiye Abdul walikiri kumbaka huyo mwanamke asiye kuwa na akili timamu. Haya yalisemwa na Kharkhoda ambaye ndie Mkuu wa Kituo cha Polisi.

The Prophethood of Muhammad

  The Prophethood of Muhammad: A Critical Theological Evaluation By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute, New York, NY The cla...

TRENDING NOW