Friday, September 2, 2016

MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KUFUGA WATUMWA

Watu wote wa kale ikiwa ni pamoja na wanazuoni wa siku hiziwanakubali ukweli wa utumwa katika Uislamu na kubainisha hadhi waliyonayo watumwa hao. Wanazuoni wote wa zamani na hata wa siku hizi wanakubaliana na ukweli wa Utumwa katika Uislamu, na kufafanua hali halisi ya hadhi ya watumwa. Nimechagua maoni ya wanazuoni maarufu kuliko wote ili kuonyesha nuru na misimamo yao.
Wakati tunaposema kwamba Uislamu hauamini katika haki za binadamu na wala hautambui uhuru wa wa watu binafsi, watu wengi hubisha.
Tena vita ambavyo Mohammed na wafuasi wake walipigana vilikuwa ni vita vya uvamizi ili kueneza Uislam kwa nguvu, kupora utajiri wa nchi, kutwaa mali za nchi, na kuwateka kinamama na watoto.
Tunakutana na umati wa watu ambao wanaelezea mshtuko wao na kutokubaliana. Kwa sababu ya kuto kuamini huko, vyanzo vyetu vya taarifa vitakuwa wasomi wa Kiislamu.
Msomi wa Al-Azhar wa Misri
Katika kitabu chake “You Ask and Islam Answers”, (Wewe Uliza na Uislamu Ukujibu), Abdul-Latif Mushtahari ambaye ni Mwangalizi Mkuu na Mkurugenzi wa Kuhutubia na Kuongoza katikaChuo Kikuu cha Azhar anasema (uk 51, 52),
“Uislamu haukatazi utumwa ila unashikilia kwa sababu mbili;
Sababu ya kwanza ni vita (Iwe vita ya wenyewe kwa wenyewe au vita na watu wa nje ambapo mateka wanauwawa au kufanywa watumwa) ilimradi tu vita si ya Waislamu wakipambana wenyewe kwa wenyewe- hairuhusiwi kuwafanya watumwa wavunja sheria au wakosaji kama wao ni Waislamu. Ni wale mateka wasio Waislamu tu wanaoweza kuuwawa au kufanywa watumwa.
Sababu ya pili ni watumwa watokanao na udhalilishaji utokanao na kuwaingilia watumwa hao kingono njia ambayo huweza kumpatia mwenye watumwa watumwa wengi zaidi.’’
Habari hii iko wazi kabisa kwamba wafungwa wote wa kivita lazima wauwawe au wafanywe watumwa.
Wanazuoni wa zamani wanakubaliana kabisa na swala hili kama Ibn Timiyya, Ibn Hisham, Malik, nk.Ibn Timiyya anasema,
(Toleo 32, uk 89)
“Mzizi wa mwanzo wa utumwa ni wafungwa wa kivita. Bonasi (zawadi) imekuwa halali katika taifa la Mohammed.”
Kisha (Toleo 31, uk 380) anaonyesha wazi na bila aibu,

“Utumwa ulihalalishwa kwa sababu ya vita yenyewe; hata hivyo si ruhusa kumfanya Mwislam aliye huru kuwa mtumwa. Inaruhusiwa kuwaua makafiri au kuwafanya mateka na ni halali kuwachukua wazaliwa wake kama mateka”
Katika sehemu ya 4 uk 177 , maelezo ya maisha ya Mtume. (Al Road Al-Anf), Ibn Hishamanasema,
“Kutokana na sheria za Kiislamu zinazohusu wafungwa wa kivita, uamuzi umebakia kwa Maimamu wa Kiislamu. Wanao uchaguzi wa kuwaua au kubadilishana mateka wa Kiislamu au kuwafanya watumwa.
Hii inahusiana na wanaume, lakini wanawake na watoto hawaruhusiwi kuuwawa, lakini ni lazima wabadilishwe (kuwakomboa waislamu mateka) au kuwafanya watumwa kuwachukua kama watumwa na wajakazi”
Hii ni kauli ya Ibn Hisham ambaye kwake wasifu wa Waislamu wote na wanafunzi wa Mohammed unapatikana. Kusema kweli maswala haya ambayo Ibn Hisham aliyaweka kwenye kumbukumbu yalizoeleka na kufanyika mfululizo katika vitavyote vya Mohammed vya uvamizi.
Watu wote wa Muhammed (wake zake na Muhammad mwenyewe) waliwamiliki watumwa wengi wa kike na wakiume katika kampeni zake dhidi ya watoto wa Qurayza (kabila la Wayahudi), Muhammad aliwauwa wanaume wote (700-800) katika siku moja. Kisha akawagawanya wanawake na watoto miongoni mwa watu wake.
Akina Khalifa kwa vizazi vingi wamekuwa wakizifuata nyayo za Mohammed na kuwafanya watumwa (kwa mamia na maelfu) wanaume na wanawake waliotekwa vitani. Wengi wao wakiwa Waajemi na watu wa himaya ya Byzantines.
Waislamu wote ambao wamekuwa wakipanga matukio kutoka nyakati hadi nyakati bila kukosa wameziweka katika kumbukumbu kweli hizi zote. Jinsi Waarabu Waislamu walivyovamia Afrika na kuwaua na kuwafanya Waafrika watumwa inafahamika vizuri ni ukweli ulioko katika historia.
Kwenye toleo la 2, sehemu ya 3 uk 13, Malik Ibn Anas alirudia maandishi kama aliyoandika Ibn Hisham ambaye pia alinukuliwa na Ibn Timiyya na Ibn Qayyim Al-Jawziyya katika kitabu chake“Zad al Ma’ad” (sehemu ya 3, uk 486).
Wote hao walifundisha kanuni zilizo sawasawa na kusema maneno ambayo yote ni yale yale.
Swali hili lilitolewa kwa Ibn Timiyya ambaye alikuwa Mufti wa Kiislamu (Toleo 31, uk 376, 377)
“Mwanaume aliyemwoa mjakazi mtumwa akamzalia mtoto , yule mtoto atakuwa huru au atakuwa mtumwa aliyemilikiwa?”
Ibn Timiyya akasema kwa msisitizo,
“Mtoto wa mwanamke huyo ambaye amemzaa kutokana naye atakuwa mali ya Bwana wake kulingana na maimamu wote (wakuu wa shule nne za sheria za kiislamu)
Kwa sababu mtoto hufuata hali ya mama yake kama yuko huru au ni mtumwa. Kama mtoto si wa asili ya Kiarabu basi yeye moja kwa moja ni mtumwa aliyemilikiwa kulingana na wanazuoni.
Lakini wanazuoni walibishana (juu ya hadhi) wao kwa wao kama alikuwa akitokana na Waarabu – kama ilikuwa lazima afanywe mtumwa au la kwasababu wakati Aisha (mkewe Muhammad) alikuwa na mjakazi mtumwa aliyekuwa Mwarabu, Muhammad alimwambia Aisha“mwachilie mjakazi huyu huru kwasababu anatoka katika wana wa Ishmael”
Kisha Ibn Timiyya akaeleza (toleo 31 uk 380) kwamba mshauri wa sheria Abu Hanifa alisema
“Muhammed ni Mwarabu; kwa hiyo haikubaliki kumfanya Mwarabu mtumwa kwasababu ya ubwana wake utokanao na asili yake kwa vile Muhammad anatokea kwao. Hata hivyo mwanazuoni (msomi) mwingine hakukubaliani naye na alisisitiza kwamba Muhammad (katika moja ya kampeni zake) aliwafanya Waarabu watumwa pia.
Hata hivyo ni wazi kwamba kutoka katika desturi za Muhammad aliichukulia asili ya Kiarabu kuwa ndiyo ya hali ya juu zaidi, hasa hasa Wa-Kuraishi lililokuwa kabila lake. Usemi wake maarufu kwamba Khalifa lazima achaguliwe kutoka kabila la Wa-Kuraishi, umekubaliwa na watafsiri wote wa desturi bila kukosa.
Angeweza akawa amemwambia Aisha “mwachie huru kwa sababu ni mwanadamu kama wewe. Haiwezekani hata kama ni mzaliwa wa Ishmaeli au wa Isaac”
Uislamu Unawachochea Waislamu Kuwafuga Watumwa - Hakuna Ukombozi
Wasomi wa Kiislamu wanakiri kweli Uislamu umebakiza kanuni za utumwa, ingawaje baadhi yao wanadai Uislamu unahamasisha ukombozi wa Utumwa. Labda baadhi ya semi za Muhammad na aya chache za Koran zinaonyesha hivyo lakini bado kutoka katika matendo tunayoyaona tunagundua kwamba uhuru wa utumwa ulitokea kwa nadra.
Sababu inafahamika vizuri, si Muhammad wala wakeze au washirika wake waliokuwa mfano mzuri katika mtazamo huu.
Wakati mwingine Muhammad alizungumzia juu ya ustahili wa kumkomboa mtu wakati bado yeye mwenyewe alimiliki dazeni za watumwa na wajakazi-watumwa. Hata hivyo tunapambana na wazo la ajabu lililotamkwa na wakeze na marafiki zake ambapo yeye aliwatia moyo kushikilia watumwa wao.
Katika toleo la 33, uk 61 Ibn Timiyya anasema,
“Yeyote anayesema kama nikifanya hivyo (kitu cha namna hiyo) kila mtumwa ninaye mmiliki atakuwa huru hawajibiki kwa kiapo chake na anaweza kukikomboa kiapo chake kwa namna yeyote na kuwabakiza watumwa wake. (Anaweza kufanya hivyo) kwa kufunga kwa siku chache au kwa kuwalisha baadhi ya watu wenye njaa.”
Kwenye ukurasa huo huo Ibn Timiyya alisisitiza kwamba hiki ndicho marafiki wote wa Muhammad walichosema, (watu kama Ibn Abbas na Ibn Umar) na vile vile wakeze (kama vile Zainab, Aishana Um Salama).
Je, kuwaachia huru watumwa ni jambo baya kwamba kuwepo na uwezekano wa mtu ambaye aliapa kuwaachia huru watumwa wake kukana kiapo chake na kuendelea kuwashikilia?
Ingeweza kusemwa kwamba yeyote anayekula kiapo kuwaachilia wafungwa wake, kama ndivyo na vivyo ikatokea, angelazimika kutimiza kiapo chake na kuwaacha huru watumwa lakini tunaona wakeze Mohammad, washirika wake wakuu na nduguze wanasema kitu fulani tofauti kutokana na ushuhuda wa Ibn Timiyya.
Koran yenyewe (katika sehemu nyingi) inaafiki utumwa na kuwahakikishia Waislamu haki ya kumiliki dazeni za wanaume na wanawake watumwa aidha kwa kuwanunua au kama zawadi itokanayo na vita. Koran inaongea kuhusu umilikaji wa watumwa kama umilikaji wa shingo zao. (sura 58:3, surah Al- Mujadilah).
Watumwa wa Mohammed –Nabii wa Uhuru na Usawa.
Mohammed mwenyewe alimiliki watumwa wengi baada ya kujitangaza mwenyewe kuwa nabii. Nataka hapa nimnukuu Ibn Qayyim-al-Jawziyya ambaye ni mmoja wa wanazuoni wakubwa na waandishi wa Kiislamu.
Katika kitabu chake “Zad al- Maad” (sehemu ya 1, uk 160) anasema:
“Mohammed alikuwa na watumwa wengi wa kike na wa kiume. Alizoea kuwanunua na kuwauza hasa baada ya Mungu kumtia nguvu kwa aya zake, ikiwa ni pamoja na kuhama kwake toka Maka. Aliwahi kumuuza mtumwa mmoja mweusi kwa wawili. Jina lake lilikuwa Jacob al –Mudbir. Manunuzi yake ya watumwa yalikuwa ni zaidi ya wale aliowauza. Alizoea kukodisha na kuazima watumwa wengi lakini aliazima wengi kuliko aliokodisha.”Biashara hii ilikuwa ikifanyika katika soko la watumwa huko Uarabuni., Peninsula na Maka. Mohammed alikuwa na desturi ya kuuza, kununua, kuazima, kukodisha na kubadilisha mtumwa mmoja kwa wawili.
Kwa hiyo alikuwa na idadi iliyoongezeka ya watumwa hasa baada ya kujitangaza kuwa nabii; na baada ya kuhama kwake toka Maka kuepuka kifo mikononi mwa kabila lake mwenyewe la Kuraishi.
Pia watumwa wa Mohammed na wafuasi wake walidumu kuongezeka ikiwa ni matokeo ya wale waliotekwa katika vita sio tu kwa kununua .
Hii ni kuwatahadharisha wale walioupokea Uislamu. Waislamu wa New York, Chicago, Georgia, Detroit, Los Angels ikiwa ni pamoja na Waafrika na waislamu wote wa duniani.
Hata miongoni mwa Waarabu kuna Waislamu ambao hawaufahamu ukweli huu kumhusu Mohammed. Cha kuhuzunisha hii ni sehemu ndogo ya ukweli ambao hawautambui kuhusiana na Mohammed.
Majina ya Watumwa wa Mohammed
A) Watumwa wanaume;
Ibn Qayyim al –Jawziyya siku zote amekuwa akiyategemea maandishi ya maisha binafsi yaliyoandikwa na wanazuoni wake wakuu ambao waliishi enzi hizo za Mtume kwa hiyo anachukuliwa na Waislamu kama mwenye mamlaka; chanzo cha msingi na kiongozi miongoni mwa wanafunzi wa dini ya Kiislamu.
Mwanazuoni huyu anatuambia katika kitabu chake “Zad al –Maad” (sehemu ya 1, uk 114,115 na 116) kama ifuatavyo;
“Haya ni majina ya watumwa wa kiume wa Mohammed; Yakan Abu Sharf, Aflah, Dhakwan, Tahman, Mirwan, Hunayn, Sanad, Fadala Yanamin, Arijasha al –Haji, Mad’am, Karkara, Abu Rafi, Thawban, Ab Kabsha, Salih, Rabah, Yara Nubyan, Fadila, Waqid, Mabur, Abu Waqid, Kasam, Abu Ayb, Abu Muwayhiba, Zayd Ibn, Harithana pia mtumwa mweusi aliyeitwa Mahran ambaye alipewa jina lingine na Mohammed, Safina (meli).
Mtumwa mwenyewe akiihusisha hadithi yake mwenyewe anasema;
“Mtume wa Mungu na washirika wake walienda safari. Mizigo yao ilipokuwa mizito sana kwao kubeba Mohammed aliniambia ‘Tandaza nguo yako’. Waliijaza mizigo yao kwenye nguo yangu kisha wakanitwika mimi’’.
Mtume wa Mungu akaniambia “Beba kwa kuwa wewe ni safina (meli). Hata kama ningekuwa nimebeba mzigo wa kubebwa na punda sita au saba, tulipokuwa safarini, mtu yeyote aliyejihisi dhaifu angetupa nguo zake au ngao yake au upanga wake juu yangu ili nimbebee ambao ni mzigo mzito.
Mtume aliniambia “wewe ni meli” (soma kwa Ibn Qayyim, uk 115-116; al-Hulya toleo 1 uk 369, imenukuliwa kutoka kwa Ahmed 5:222)
Hadithi hii inaonyesha ukatili na haihitaji ufafanuzi wala maelezo zaidi. Matendo maovu Mohammed na washirika wake waliomtendea Mahram ni ya kukithiri. Ibn Qayyim al – Jawziyya si yeye pekee aliyeweka kumbukumbu ya tukio hili na orodha ya majina ya watumwa wa Mohammed.
Tabari pia katika kumbukumbu zake za nyakati, (Toleo la 2 uk 216, 217, 2180) anatupatia maelezo haya.
Hakuna yeyote kati ya viongozi wa Kiislamu wa siku hizi anayeweza kukanusha mambo haya. Hasa kama anakutana na kumbukumbu za Tabari na Ibn Qayyim al – Jawziyya.
Bado kulingana na mtumwa wa Mohammed Zayd Ibn Haritha, Muhammed alimwachia huru na kumtwaa kama mwanae kisha akamwozesha binamu yake (Mohammed) aliyeitwa Zainab.
Baadaye Zayd alimpa talaka mkewe baada ya kugundua kwamba Mohammed alikuwa akimtamani.
Hadithi hii ya kashfa imethibitishwa kwa aya katika Koran na wanazuoni wa Kiislamu wanakubali hili.
B) Watumwa wanawake;
Katika sehemu hii hii ( ya kwanza, uk. 116) Ibn al – Jawziyya sawa na wanazuoni wengine wa kiislamu waandishi wa kumbukumbu za mambo ya nyakati aliorodhesha orodha ya majina ya watumwa wanawake wa Mtume Mohammed.
Ambao ni Salma Um Rafi, Maymuna binti yake Abu Asib, Maimuna binti yake Sa’d. Kadra , Radwa, Razina, Um Damira, Rayhana, Mary Mkufti (mtu wa asili ya Misri) kwa nyongeza watumwa wengine wawili wa kike mmoja alipewa kama zawadi na binamu yake Zaynab, na mwingine alimteka katika vita.
Hadithi ya Mtumwa Chini ya Sheria za Kiislamu zisizo na Haki
Hebu tukague pamoja baadhi ya mambo ya kustaajabisha yaliyokumbatiwa na Muhammad na Uislamu yaliyofungamana na utumwa.
Mtu huru hawezi kuuwawa kwa ajili ya Mtumwa;
Koran ikiwa ni pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanasema kweli kuhusu mtazamo huu. Koran(sura ya Ng’ombe : 178)
Msomaji hahitaji tafsiri ya wanazuoni ili kuelewa maneno haya ya wazi yanayoonyesha mtu huru anaweza kuuwawa tu kwa ajili ya mtu huru. Mtumwa kwa ajili ya mtumwa na mwanamke kwa ajili ya mwanamke.
Bado niliahidi kuchimba kwenye tafsiri ya wafafanuzi wa aya hizi za Koran kutoka kwa miongoni mwa wasomi wa Kiislamu kwa sababu wanaufahamu zaidi kwenye ufafanuzi wao na sio wa kwetu sisi.
Kwenye maoni ya Jalalan (uk 24) tunasoma hivi kufuatana na aya iliyotajwa juu.
“Adhabu ile ile ilitekelezwa kwa waumini iliyo sawa na kosa la jinai kwa sababu ya uuaji wa binadamu, kwa maadili ya maelezo au uhalisi.
Mtu huru atauwawa kwa ajili ya mtu mwingine aliye huru lakini sio kwa watumwa; mwanamke kwa ajili ya mwanamke, lakini Muislamu (hata kama ni mtumwa) asiuwawe badala ya kafiri hata kama kafiri huyo ni mtu huru.
Kuna usawa gani katika hili kuhusiana na utu? Kuelezea aya iliyotajwa hapo mbeleni (aya 2:178)Baydawi anahusianisha kile kilichotokea kwa Mtume Muhammad, Abu Bakr na Umar. Hii imeandikwa katika kitabu chake kiitwacho “Tafsiri ya al – Baydawi” (The Commentary of Al – Baydawi) uk 36 tunasoma hivi;
Shafii na Malik walikataza kumuua mtu huru kama akimchinja mtumwa wake au mtumwa wa mtu mwingine. Hii ni kwa sababu “Ali Ibn Abi – Talib alitaja kwamba mtu alimuua mtumwa wake na Muhammad akamchapa mjeledi tu, hakumwuua.
Ilihusianishwa na mamlaka ya Muhammad pale aliposema Muislamu hawezi kuuwawa kwa ajili ya asiyekuwa Muislamu; au mtu huru kwa mtumwa; pia kwa sababu Abu Bakr na Umar Ibn al – Khatib hakumwuua mtu huru kwa ajili ya mtumwa.
( Hii ilisemwa ) mbele ya washirika wa Mohammed na hakuna aliyetilia shaka wala kuipinga. Hizi ni aya za Koran na hii ni tabia ya Mohammed mwenyewe na pia ya Abu Bakr na Umar baada yake.
Wanasheria wa Kiislamu
Shafii, Malik na Ibn Timiyya walitangaza kanuni zile zile kama katika Koran (2:187).
Imam Shafii anatuambia kwa ufasaha na kwa uamuzi kamili katika sehemu ya kwanza ya kitabu chake. “Alkam al Quran” (Agizo /a Amri za Koran) uk 275.
“Mtu hawezi kuuwawa kwa ajili ya mtumwa au mtu huru kwa mtumwa.”
Kwenye ukurasa huo huo anaongeza,
“Muumini asiuwawe kwa ajili ya asiye muumini, wala mwanaume kwa ajili ya mtumwa wake au mwanamke.
Haki iko wapi! Usawa uko wapi!
Kisha anaongeza,
“Mtu huru asiuwawe kwa ajili ya mtumwa kufuatana na wanazuoni”
Malik Ibn Anas aliwahi ulizwa “Ni nini adhabu ya bwana aliyempiga mtumwa wake hadi akafa?” Akajibu “Hakuna”. (Toleo 6, sehemu 15, uk 164).
Katika toleo la 28, uk 378, Ibn Timiyya pia alisema
“ Tulichokitaja kuhusiana na waumini ambao damu zao zinachukuliwa kuwa sawa inamhusu tu yule muislamu aliye huru”
Sina mashahidi wazuri zaidi kuhusiana na ukweli huu kuliko hawa wanazuoni, Abu Bakr; Umar, Ali na matendo ya Muhammad na wale wote wanazuoni wa Kiislamu walio wakuu na maarufu.
Mtumwa Hamiliki Mali au Pesa
Ibn Hazm anasema katika toleo la 6 sehemu ya 9,
“ Mtumwa haruhusiwi kuandika wosia anapokufa, au kumrithisha yeyote chochote kwa sababu mali yake yote ni mali ya bwana wake”
Sehemu ya 1, uk 180 wa kitabu chake, “Amri za Koran” Shafii pia anasema,
“Aya ya Koran kuwaoa wanawake wanaoonekana kuwa wazuri kwako, wawili au watatu au wanne imekusudiwa kwa mtu aliye huru tu na siyo kwa watumwa kwa sababu anasema ndani yake kwamba mtu anayeweza kufanya kwa haki ni mtu yule anayemiliki pesa na watumwa hawamiliki pesa.”
Anaonyesha pia katika sehemu ya 2, uk 21, “Anayemilikiwa hana pesa” Badala yake, kufuatana na sheria za Kiislamu, Waislamu wote wanapokea sehemu ya zawadi zitokanazo na vita kasoro watumwa na wanawake. Ibn Anas anasema (Juzuu 2, sehemu 3 uk 33, 34). “Watumwa na wanawake hawana sehemu yoyote katika zawadi zitokanazo na vita”
Hii ndivyo ilivyo hata kama wangekuwa wanapigana pamoja na Waislamu wengine. Katika sehemu ya 3 ya “Wasifu wa Kinabii” (Prophetic Biography) (uk. 386) Ibn Kathir anasema,
“Watumwa hawapati chochote kutokana na zawadi za vita, kwamba zawadi hizo ni fedha au wanawake.”
Ushuhuda wa Mtumwa haukubaliki.
Katika Juzuu ya 35, uk 409 Ibn Timiyya anasema,
“Shafii, Malik na Abu Hanifa, ambao ni wanazuoni wa sheria za Kiislamu wanadai kwamba ushuhuda wa mtumwa haukubaliki.”
Kama pia tukifungua kurasa za “Amri za Koran” kilichoandikwa na Shafii (sehemu 2, uk 142) amedhamiria hivi;
“Mashahidi lazima watoke miongoni mwa watu wetu ambao wako huru, sio miongoni mwa watumwa wetu bali kutoka miongoni mwa watu huru tena walio waamini wa dini yetu”
Ushuhuda wa Myahudi au Mkristo haukubaliwi, kama tulivyotaja hapo juu, hata kama haki itazuiliwa kwa kukosekana ushuhuda wao. Hii sio muhimu.
Katika “Sahih” yake (sehemu 3, uk 223) Bukhari anasema;
“Ushuhuda wa mtumwa haukubaliki katika ndoa”
Ni nini maana ya sentensi ya Shafii?
“Shahidi asitoke kati ya watumwa wetu tunaowamiliki”
Je, huyu Shafii haelewi kuwa Mungu ndio mwenye kumiliki watu? Alidiriki vipi kutamka tamko la “watumwa wetu tunaowamiliki”
Hakuna adhabu kwa yeyote anayefanya shitaka la uongo dhidi ya watumwa.
Inafahamika vizuri kwamba kama Muislamu akifanya shitaka la uongo juu ya Muislamu mwingine aliye huru na kumkashifu na kumvunjia heshima yake ataadhibiwa kwa kuchapwa viboko vinane.
Hivi ndivyo ilivyotokea wakati baadhi ya washiriki wa Mohammed na ndugu zake walipomshtakiAisha mke wake, kwamba alizini na mmojawapo wa vijana kwa sababu (Aisha na kijana) walibaki nyuma baada ya msafara kuondoka, halafu baadaye wakafika pamoja asubuhi, yake.
Mohammed aliamuru wale washtaki wachapwe viboko nane kila mmoja. Lakini kama Muislamu akimzushia au kumsingizia mtumwa, hataadhibiwa. Haya ni maoni ya wanazuoni wote.
Kwa mfano (Juzuu 8, sehemu 2, uk 271), Ibn Hazm anadai kwamba haya ni maoni ya Abu Hanifa, Shafii, Malik, Sufyan al – Thawri na sio maoni yake peke yake. Hivi ndivyo Sharawiasemavyo bila aibu;
“Watumwa wanawake ni watu wa kudhalilishwa na kuvunjiwa heshima kwa sababu sio watu wa kuheshimiwa na yeyote (hii ni kusema hawako huru, wanawake wakuheshimiwa ni wake za wanaume ambao wako huru) Haya ni maneno yale yale yaliyo rudiwa rudiwa na Shafii (sehemu 1, uk 307) katika kitabu chake “Alkam ya Koran”.
Kwa hiyo mtumwa mwanamke siyo lazima ajitande hijabu.
Wakati wowote Mohammed alipomchukua mwanamke kama mateka, kama alimvalisha hijabu, Waislamu walikuwa wakisema alimchukua kama mke , lakini kama angemwacha bila kumvalisha hijabu, walikuwa wakisema, “Amemtwaa kama mtumwa” Ndio kusema atakuwa mali ya mkono wake wa kuume”
Mfano mzuri ni tukio la Safiyya Bintiye Hay, aliyechukuliwa kama zawadi ya vita katika vita yaKhaybar. Waandishi wote wa nyakati (ikiwa ni pamoja na maandishi ya wasifu- bila kukosa) wameandika,
“Tunashangaa ni kwa nini imesemekana juu ya wanawake na wasichana kwamba wao ni wa kuondolewa heshima”.
Shafii na Shawari walitamka hili neno kwa neno. Ni muhimu kwetu kurudia kwamba Uislamu unavunja hadhi ya mtu kwa kisingizio kwamba yeye ni mtumwa, kwamba ni mwanamke, au kwamba yeye sio Muislamu.
Mambo yahusuyo jinsia na ndoa na kuhusu watumwa weusi.
1.Mtumwa hawezi kujichagulia.
Hii ilithibitishwa na wanazuoni wote wa Kiislamu kwa mamlaka ya Mohammed katika Juzuu ya 6 sehemu 9 uk. 467, Ibn Hazm alisema,
“Kama mtumwa akioa bila ruhusa ya Bwana wake, ndoa yake haitatambulika na itabidi achapwe kwa sababu amefanya uzinzi. Ni lazima atenganishwe na mkewe. Na huyo mke pia anachukuliwa kuwa mzinzi kwa sababu Mohammed alisema “Mtumwa yeyote anayeoa au kuolewa bila kibali cha Bwana wake ni malaya”
Maandiko yale yale yalinukuliwa na Ibn Qayyim al – Jawziyya (sehemu 5, uk. 117 ya “Zad al –Maad”) ambapo ni pamoja na Ibn Timiyya (Juzuu 32, uk.201)
Malik Ibn Anas anahusianaisha (Juzuu 2, sehemu 4) zaidi ya hapo. Anasema (uk 199,201,206)
“Mtumwa asioe bila kibali cha bwana wake. Kama yeye ni mtumwa wa mabwana wawili, anatakiwa kupata kibali kutoka kwao wote.”
2. Mtumwa wa kiume na mtumwa wa kike wanalazimishwa kuoana.
Malik Ibn Anas anasema dhahiri:;
“Bwana ana haki ya kuwalazimisha
watumwa wa kiume na wa kike kuoana bila ridhaa yao.” (Juzuu 2,uk.155)
Ibn Hazm anasema kwamba Sufyan al Thawri pia, alisema kwamba bwana ana haki ya kumlazimisha mtumwa wake wa kiume au wa kike kuoana bila kujali ridhaa yao (Juzuu 6, sehemu 9, uk 469) Ibn Timiyya ana maoni hayohayo.
Sitashindwa katika mtazamo huu kumtaja Malik Ibn Anas, ambaye baada ya kukabiliana na wanazuoni wengine kwamba bwana ana haki ya kumlazimisha mtumwa wake wa kike au wa kiume kuoa au kuolewa anaongeza,
“Bwana hana haki ya kumlazimisha mtumwa wa kike kuolewa na mtumwa mwenye sura mbaya, mweusi kama yeye ni mzuri na mrembo isipokuwa katika hali ambayo ni ya lazima sana” (nukuu kwa Ibn Hazm, Juzuu 6, sehemu 9,uk 469).
Tunashangaa hapa Malik Ibn Anas alimaanisha nini aliposema , “mtumwa mwenye sura mbaya mweusi?” Je, mtu anathaminishwa kutokana na rangi ya ngozi yake? Unasema hivyo eeh Malik Ibn Anas na wewe ni mmoja kati ya wanasheria wanne wakuu? Au mtu huthaminiwa kwa misingi ya haiba yake, busara yake na moyo wake?
Tuna haki pia ya kushangaa kwa nini Mihram, mtumwa mweusi, alivyofedheheshwa na kuumizwa kimwili na kiakili na Mohammed na washirika wake alipombebeshwa mizigo ya jangwani kwenye joto kali wakati Muhammed akimwambia wewe ni meli kwa hiyo beba. Hivyo likawa jina lake la utani. Je, hawakuwa na dazeni kadhaa za watumwa wengine?
Mohammed hata hivyo alibagua (katika Uislamu) kati ya mbwa mweusi na mbwa mweupe. Bado tunachohusika nacho sisi ni kile nilichokionyesha kuhusu utumwa kwa ujumla; kwamba mabwana zao waliwachukulia kana kwamba wao sio binadamu hawana hisia, wala hamu na vitu wanavyopendelea.
Hebu tuendeleze mjadala wetu ili tuwe na picha halisi kuhusu jinsi Dini ya Kiislamu inavyodhalilisha hadhi ya wanaume na wanawake chini ya kisingizio kwamba wao ni watumwa na sio watu huru.
3. Mwanaume wa Kiarabu asimwoe mwanamke mtumwa ila katika hali ambayo haiepukiki.
Katika Juzuu 31, uk. 383, Ibn Timiyya anasema;
“Hairuhusiwi kwa mwanaume huru wa Kiarabu kumwoa mtumwa anayemilikiwa ila tu pale ambapo haiepukiki, kama vile kushindwa kumwoa mwanamke aliye huru . Kama ikitokea na akafunga ndoa na mtumwa watoto wa mwanamke huyo watakuwa watumwa pia. Kwa sababu wanafuata hali ya mama yao katika utumwa”.
Malik Ibn Anas anaeleza,
“ Hairuhusiwi kwa mwanaume huru kumwoa mke mwingine ambaye ni mtumwa zaidi ya mkewe aliye huru. Katika jambo kama hilo, mkewe aliye huru ana haki ya kumpa talaka. Hali kadhalika kama akimwoa mwanamke huru wakati ameshamwoa mtumwa na kama alishindwa kumwambia hilo, mwanamke huru ana haki ya kumwacha”.(Malik, Juzuu 2, uk 204)”
Sina maoni yeyote juu ya hizi kanuni za kushangaza, ila bado nashangaa ni kwa nini mwanaume huru wa Kiarabu asimwoe mtumwa. Je, yeye siyo mwanaume na huyo mtumwa sio mwanamke? Na kwanini (kama haiepukiki kwamba basi amwoe) ila wazao wake wote wawe watumwa?
Hizi ni sheria za kidhalimu na za kikatili. Ni wazi kwamba Muhammad alishindwa kubadili mila za kikabila za jamii zilizokuwepo kabla ya kuingia kwa Uislamu.
Wengi wa Waarabu waislamu walikuwa na watumwa, washirika wake, wakeze na yeye mwenyewe alimiliki na kujibakizia dazeni kadhaa za watumwa. Aliwanunua zaidi baada ya madai yake ya Unabii na kutangaza ujumbe wake, ujumbe wa usawa, uhuru na haki za binadamu.
Kingetokea nini kama mwanamke huru angeolewa na mtumwa wake?
Angeweza akawepo mwanamke mwenye nia ya wazi ambaye hakubagua kati ya mwanaume huru na mtumwa. Hivyo akaangukia kwenye mapenzi na mtumwa wake ambaye naye alimpenda na wakakusudia kuoana kisheria kabisa.
Je, mtazamo wa Kiislamu katika hali kama hii ni nini?
Kama jambo kama hili likitokea katika jamii ya Kiislamu itakuwa balaa. Hebu tuangalie jinsi Umar Ibn Khattab alivyochukulia hali kama hii katika Juzuu ya 8, sehemu 11, uk 248, 249, Ibn Hazm anafunua;
“Mwanamke aliolewa na mtumwa wake wa kiume. Umar alikusudia kumpiga mawe lakini badala yake aliwatenganisha na kumpeleka yule mtumwa uhamishoni. Akamwambia yule mwanamke si sheria kwako kuolewa na mtumwa wako mwenyewe.
Mwanamke mwingine aliolewa na mtumwa wake mwenyewe , Umar akamchapa mijeledi mwanamke na kuwakataza wanaume wote kumwoa. Wakati mwanamke mwingine aliye huru alikuja kwa Umar na kumwambia “mimi sio mwanamke mrembo na nina mtumwa ambaye nataka kuolewa naye.Umar aliwakataza. Alimchapa viboko yule mtumwa na akaamuru auzwe nchi za kigeni”.
Akamwambia mwanamke,
“si sheria kwako kuolewa na kile kinachomilikiwa na mkono wako wa kulia.Ni wanaume tu wanaoruhusiwa kuoa kile ambacho kinamilikiwa na mikono yao ya kulia.Hata kama ungemwacha awe huru ili akuoe na akawa mtu huru, huo uhuru wa kutokea utumwani hautakuwa na thamani na ndoa haitathaminika”.
Katika shule za Kiislamu za Sudan wanalazimishwa kunywa maji ambayo yamebaki baada ya kuosha ubao/mbao zao chafu zilizoandikwa kwa chaki. Wanaambiwa hii itawasaidia katika kukariri Koran.
Ni pale tu mtoto anapoweza kuisoma Koran yote kwa kichwa ndipo anaweza kuhitimu shule. Hii huweza kuchukua muda hadi miaka tisa. Baadhi yao wale ambao hawako tayari kukariri wataendelea kushikiliwa pale na kamwe hawahitimu.
Waalimu machachari wa Kiislamu wamewekwa tayari kuhakikisha wanang’ang’ania kwenye sheria za Kiislamu na kuwapalilia wale wanafunzi watakaofuata mafundisho ya Kiislamu kwa nidhamu ile isiyo na maswali.
Wanakuwa wameandaliwa tayari kwa Jihad- Vita takatifu. Wakati ni miili yao inayoweza kufungwa, ni nafsi zao hao watoto ambazo hao walimu wa Kiislamu wanazitamani.
Je, kuna maoni yeyote juu ya ukatili huu wa Kalipha wa pili ambae alikuwa baba mkwe wa Mohammed na mmoja kati ya kumi ambao Muhammad aliwaahidi paradiso?
Yeye ni mmoja kati ya wawili ambao Mohammed aliwaomba watu wawafuate kama mfano wakati alipotangaza “Waigeni Abu Bakr na Umar” Bado Umar alikuwa mwonevu na mkatili asiye na moyo mwema ambaye alijaribu kumpiga mawe mwanamke bila sababu ila tu aliolewa na mwanamume aliyekuwa mtumwa wake.
Alimtandika viboko pia mwanamke mwingine na kuwakataza wanaume wasimwoe, na alimpiga na kumtosa ugenini mtumwa. Na wakati mwanamke wa tatu alipotaka kumwachia huru mtumwa wake ili aolewe naye na waishi maisha ya raha mustarehe, hasa baada ya kupoteza tumaini la kuolewa na mwanaume aliye huru, Uislamu na Umar waliingilia kati na kusema “Hapana hii haiwezekani”
Alimchapa viboko yule mtumwa na kumuuza katika nchi ya kigeni. Kutokana na haya akawa mfano wa mtu asiye na huruma, mwenye moyo mgumu na ukandamizaji uliokithiri.
Kwa habari ya jinsia na ndoa Ibn Timiyya anasema;
“Yeyote ammilikie mama anamiliki na watoto wake pia. Kwa kuwa bwana
wa mama kunamfanya awe mwenye watoto hata kama mama huyo alizaa n
a mumewe au walikuwa sio watoto wa ndoa. Kwa hiyo bwana ana haki ya
Kujamihiana na binti wa mjakazi wake ambaye ni mtumwa kwa sababu
Wao ni mali yake alimradi tu hajamiiani na huyo mama tena wakati huo
huo (Juzuu 35 uk 54)”
Thamani ya mtumwa- Gharama yake kwa dinari ni nini?
“Kama mtumwa anayemilikiwa akimvamia mtu yeyote na kuharibu mali yake,
Uovu wake utafungiwa shingoni mwake, bwana wake ataambiwa waweza kulipa
Faini ya uharibifu uliofanya na mtumwa wako au umtoe ahukumiwe kifo. Bwana
Wake anatakiwa achague moja kati ya hayo mawili; aidha thamani ya mtumwa
Na bei yake au uharibifu aliosababisha mtumwa wake” (Vol 32, uk202, Ibn
Timiyya )
Je, hivi ndivyo thamani ya mtu inavyohesabiwa? Uharibiwa ukiwa na jumla ya dinari 600 na gharama ya mtumwa kwa makisio ya bwana wake haizidi dinari 400 kwa sababu alikuwa mgonjwa na dhaifu, bwana wake katika jambo kama hili angelimtosa ili auwawe.
Tumeangalia alama sita zinazohusiana na hadhi ya mtumwa katika dini ya Kiislamu. Kwa hakika alama mojawapo kama tukifikiri, inatosha kufafanua ukweli.
Inatufunulia jinsi heshima ya mtu inavyosiginwa katika zoezi zima la utumwa kutoka mwanzo kabisa tumetaja kanuni za utumwa kama zilivyodhihirika katika dini hii na tumeorodhesha majina ya watumwa wa Muhammad ambae ni bwana wa watumwa na Mtume wa Mungu.
Nafasi ya Ukristo – Mafundisho ya Injili
Ukristo uko wazi sana kuhusiana na jambo hili. Kutoka mwanzo kabisa tumetumia kanuni za msingi kabisa katika masomo na utafiti huu. Tukiita; ulinganifu lazima kila wakati uwepo kati ya Injili na Koran.
Ukristo kama dini na mafundisho na Uislamu kama dini, ili tuone ipi kati ya hizo mbili inafunua mawazo ya Mungu aliye wa kweli aliye hai. Pia ulinganifu unatakiwa kati ya Mohammed maisha yake, na misemo yake kwa upande mmoja na Kristo, maisha yake na mafundisho yake kwa upande mwingine.
Kama tungetakiwa tutafute (kwa mfano), baadhi ya wazungu au wamarekani walioruhusu nafsi zao kumiliki watumwa tusingeweza kulaumu Ukristo kwa sababu ni lazima tugundue kwamba Injili inafundisha kitu kingine tofauti. Tunaona kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakumiliki watumwa.
Tunalaumu Uislamu kuhusiana na hili kwa sababu Mohammed mwenyewe alimiliki watumwa wa kike na kiume kwa dazani kadhaa. Marafiki zake wote, wakeze na waislamu wengi wa wakati wake na hata wa baadae walimiliki watumwa. Koran inatia moyo jambo hili liendelee na wanazuoni hawakanushi jambo hili.
Tunalaumu mawazo ya Kiislamu na tabia ya Mohammed kuhusiana na jambo hili na mambo mengine yaliyonukuliwa katika vyanzo muhimu vya kuamimika vya Uislamu.
Katika somo lolote hatutang’ang’ania kwenye tabia ya baadhi ya Wakristo au baadhi ya Waislamu lakini badala yake tutajaribu kupima mwenendo wa mawazo ya Kiislmu (au mawazo ya Kikristo) kuelekea mada iliyopo kwenye mjadala.
Watu wengine kwa mfano wanaamini kwamba mtu kama Khomeini kazidi kiasi kwa sababu ya Uislamu, dini ya uvumilivu, upendo na yenye kumaanisha. Sivyo kabisa Uislamu ni kinyume na madai haya kabisa.
Je, hatuoni kama dini hii inafedhehesha na kutesa wanawake na wasio Waislamu ikiwa ni pamoja na kufanya vita ya mashambulizi na kuwatia moyo Waislamu kuwauwa wanaoiasi dini? Je, Mohammed ambaye aliamuru mwanamke aliyemtukana auwawe, aweze kuwa nabii mwenye uvumilivu?
Je, si kwamba Rushdie (kufuatana na sheria za Kiislamu na za Mohammed sio sheria za Umoja wa Mataifa) anastahili kifo kwa kuishambulia Koran, Mohammed na wakeze?
Komeini kamwe hakuwa mfurukutwa; alikuwa kila wakati ni mwanafunzi wa kweli wa Mohammed. Alikusudia kuzitia nguvu sheria na kupigana na mataifa ambayo hayaendi sambamba na wao – kama vile Irak (hata japo Uislamu ni dini yao ya taifa )
Sasa agano jipya linasema nini kuhusiana na watumwa? Tukifungua kwenye kurasa za agano jipya tunasoma mistari hii;
“Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu
mume wala mtu mke, maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo
Yesu”. (Gal 3:28)
Kristo alikuwa kila wakati akiwaonya wanafunzi wake na wote waliomwamini kutojiita mabwana. Aliwaambia;
“Bali ninyi msiitwe rabi (bwana), maana mwalimu (bwana) wenu ni mmoja
nanyi nyote ni ndugu”
“Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Na yeyote atakayejikweza,
atadhiliwa (atanyenyekeshwa) na yeyote atakayejidhili atakwezwa”
Kwa haya maneno ya mwisho Kristo aligeuza viwango vyote dhaifu vya kibinadamu.
“Aliye mkubwa kati yenu atakuwa mtumishi wenu” Ni jinsi gani yalivyo mazito na yenye kina kirefu haya maneno ya ajabu!
Ukweli huu ulifundishwa kwa uwazi katika Agano jipya kwa uongozi wa Roho Mtakatifu. Ilitokea kwamba alikuwepo mtumwa aliyeitwa Onesmo ambaye alikimbia toka kwa bwana wake, Filemoni.
Onesmo alikutana na mtume Paulo kule Rumi na akageuka kuwa mkristo. Paulo akamtuma kurudi kwa Filemoni akiwa na barua ya kuvutia sana ambayo imeandikwa katika Agano jipya na katika hiyo tunasoma maneno haya yang’aayo;
“Ninamtuma arudi kwako wewe kwa hiyo mpokee, ambaye ni moyo wangu hasa.
mpokee---- sio tena kama mtumwa bali----- kama ndugu mpendwa,-----katika
mwili na katika Bwana” (sura 1 )
Paulo, Petro na mitume wengineo hawakuwa na mamlaka ya kukomesha utumwa ndani ya himaya ya Kirumi. Paulo hakuwa mmoja kati ya magavana wa Kirumi; bali mkimbizi na mtu aliyeteswa.
Baadae yeye na wanafunzi wengine wengi waliuwawa katika mikono ya warumi yeye pamoja na maelfu ya kaka zao wengine wakristo. Muhammed na wafuasi wake walikuwa watawala na wangeweza kukomesha utumwa badala yake waliubakiza na kuendelea kuwaweka watumwa wao.
Katika waraka mwingine Paulo anawaagiza Wakristo, “kuwapa watumwa iliyo haki na adili.” (Kol. 4:1).
Kifungu kinasisitiza maneno haya mawili – undugu na haki – kwa sababu hakuna mtumwa wala mtu huru bali wote ni wa moja katika Kristo.
Historia ya Misri inahusianisha hadithi ya mtu aliyekuwa jasiri ambaye alisimama mbele ya watawala wake wakatili ambao waliwatesa watu na kushangaa kwa maumivu makali, “Kwanini mnawafanya watu watumwa, watu ambao mama zao waliwazaa wakiwa watu huru?”
Huyu mtu shujaa hakufahamu kama alikuwa anazungumza na umati wa watu kupitia vizazi vingi, kwamba ni watu wa Magharibi mkatili wa Ulaya na Marekani au ni mtume wa Kiislamu mwenyewe ambaye alishindwa kuwaachia huru watumwa kwa sababu yeye binafsi alikuwa nao dazani kadhaa.
Viongozi wa kidini wa Kikristo kama vile John Wesley kwa ujasiri aliushutumu utumwa kule ulaya na akatuma ujumbe mzito kwa watawala wa Ulaya na Marekani. Waliongoza vuguvugu la watumwa kudai uhuru wao wakati wa siku za Abraham Lincolin.
Sasa kuna kundi linaloongezeka la watu weusi ambao wanashika nafasi kadha wa kadha za heshima na wanaheshimika ndani ya Marekani. Wanafundisha katika vyuo na vyuo vikuu.
Wanakalia viti kwenye mahakama za nchi hata mahakama kuu. Wamechaguliwa kwa uhuru na serikali za mitaa, wilaya, mikoa, Taifa, na nafasi kwenye serikali ya shirikisho. Wanashika nafasi kubwa katika jeshi. Wanajijengea bahati zao wenyewe ambazo wanafanya kama wapendavyo. Wanaoa kwa uhuru na kutunza familia zao bila hofu.
Utata wa kununua watumwa ndani ya Sudan.
Juni 2000
Nimefanyia kazi sheria ambayo sasa niko kinyume nayo. Nimeshawakomboa watumwa kumi na mbili mwaka 1998 kule kusini mwa Sudan katika kijiji cha Turalei. Na nilitoa fungu la hela kwa ajili ya ukombozi wa wengine wakati wa safari yangu nyingine ya Novemba mwaka huo huo.
Nafahamu wanavyojisikia – furaha, ya hali ya juu isiyoelezeka – ambayo inatokea katika kifungo.
Kwahiyo najua kile kilichowahamasisha madarasa ya kiwango cha tano wa Colorado na Oregon na miji mikuu na majimbo kote nchini ili kufanya kazi za kuosha magari na kuuza madoli ili kukusanya hela na kinachowafanya baba na mama waliostaafu wa Minesota kutuma dola zao haba kwa mashirika ya kimataifa yanayotoa misaada na huduma kwa kuwafungua watumwa wa Sudan.
Utumwa ni baa na mateso makubwa. Ni chukizo la kinafsi lililodumu sana kwa vile lingetakiwa liwe limeshatoweka kutoka katika dunia.
Na chochote mmoja wetu anachoweza kufanya ili kukomesha na sisi hatuna budi tukifanye na tukifanye kwa nguvu zetu zote.
Swali langu adhuhuri ya leo kwa kifupi ni hili;
“Wakati tunapojihusisha na zoezi zima la kuwakomboa watumwa – je, tunauondosha utumwa-------- au tunautia moyo uendelee?”
Na hapa ni muhimu sana tujibu swali hilo sio tu kwa kuwasiliana na wale walengwa lakini kwa kutathimini hali halisi kwa sababu wale walengwa halisi kamwe hawatoshi.
Nilisema nafahamu inamaanisha nini kuwakomboa watumwa. Ninafahamu pia mashaka yanayokuja baadaye, hofu za usiku wa manane kwamba watu tuliowakomboa hawakuwa watumwa kamwe hilo ni jambo la kwanza.
Ninafahamu jinsi ilivyo ngumu kupambanua yule unayemhoji ni kweli yuko vile anavyodai yuko. Au lile kundi la watoto tunalodhania kulikomboa walinusurika kutoka katika mwendo wa kuhuzunisha wa Kifo wa maili 500 kukatiza hari za jangwani na naweza kufikiria jinsi ilivyo na ushawishi katika vijiji vingine kuweka sehemu za kujifanya ni za kukombolea watumwa; vikisukumwa na malipo yatakayotolewa.
Kwa sababu ukweli mzito ni huu, kwa wakati huu huu, kule kusini mwa Sudan sheria za kuwakomboa watumwa zinaendeleza soko la kuuza binadamu.
Sawa tu kama vile kuzungumza juu ya soko la bidhaa kama matumbo ya nguruwe au bei ya mafuta yasiyosafishwa, tunajua kwamba binadamu huuzwa kwa $35 hadi $100 kwa kichwa, kutegemeana na hali ya soko la ndani, sawa na usawa wa kundi lililokombolewa.
Na wakati tulipowakomboa watumwa wengine bila mashaka yoyote, sasa tunatengeneza hali bora zaidi ya kuchukua watumwa na hali bora zaidi ya watumwa wakujifanya ili kupata hela katika nchi ambayo $100 ni sawa na malipo ya mtu kwa siku 100.
Ugunduzi huu umesababisha shirika langu likasitisha zoezi la kuwakomboa watumwa.
Na kuliambia kila kundi lililochangamfu kule Sudan kuangalia kwa makini zoezi lile linalodumisha na kuendeleza uovu uleule tunaokusudia kuukomesha.
Nafahamu kile ninachokipendekeza ni dawa isiyofurahisha na ya kikatili. Lakini naamini tunajua ndio sheria iliyofunguliwa kwetu. Kwa sababu ndiyo sheria tunayoitendea kazi sasa hivi. Namaanisha nini? Shuhudia mlolongo mrefu wa zoezi la ustawi uliofuatwa na Wamisionari na mashirika ya misaada wakati tunapowatuma watu wetu wenyewe kule Sudan au sehemu nyingine duniani.
Mfumo ambao Wamisionari na wafanyakazi wa msaada waliotakiwa kuweka sahihi, mfumo ambao labda baadhi yetu tulio katika chumba hiki tumetia sahihi unakiri kwamba kama tumechukuliwa mateka hakuna fidia itakayolipwa. Kwanini?
Kwasababu fidia – kulipa fedha kwa ajili ya uhuru – kutajenga mazingira ya utekaji nyara, na hicho ni kigezo tunachojua hatuwezi kuishi nacho.
Biashara ya utumwa haina tofauti kwa kiwango kile tunachotaka kuamini kwamba ukombozi wa watumwa ni njia ya kuukomesha utumwa Sudan. Lazima tukutane na ukweli kwamba pamoja na makusudio mazuri sana, hatutakomesha utumwa; lakini vinginevyo kuuchochea na kupanua biashara ya utumwa.
Kwa vile kila mtumwa tunayemkomboa tunachochea, wafanyabiashara ya utumwa wengine kumi na ishirini na kuongeza wengine kwa kuwaleta kutokana na uvamizi utakaofuata. Na hilo ni jambo ambalo hakuna mmoja wetu angetaka.
Umoja wa mataifa unatakiwa kuacha mara moja zoezi la kuijulisha serikali ya Khartoum kuhusu wakati na sehemu za tahadhari ambapo chakula cha msaada kinatolewa. Kuna ushahidi wa uhakika – ushahidi wa hali ya juu – kwamba taarifa zinaruhusu kikosi cha jeshi la Sudan kuingilia usafirishaji wa hivi vyakula, kuleta uharibifu katika vijiji vile vile tunavyomaanisha kuvisaidia.
Ni matumaini yangu kwamba tunaweza kufanya kazi pamoja kutafuta njia mbadala kutia nguvu njia zile tunazoweza kuzitumia kuwasaidia watu wasio na hatia wa kusini mwa Sudan – kuwanyakua sio tu katika utumwa, njaa na magonjwa bali pia kutoka katika uwepo ule unaowanyang’anya tumaini lao. Aksanteni.
Hadithi ya Wanawake katika Uislamu
Wengine wanakosea na kuamini kwamba Uislamu unaheshimu wanawake na kuwapa hadhi ya juu kwa sababu rahisi tu kwamba hawajasoma aya za Koran, na maneno ya Mohammed na wanazuoni wote wa Kiislamu kuhusu wanawake.
Kwa hiyo wanathamini madai yote ya Wamisionari wa Kiislamu kuhusiana na jambo hili. Tunawapa pole wale wote waliosilimu na kuwa Waislamu kwani wamedanganywa kwa sababu hakuna mtu yeyote angetegemea dini ambayo inadai kuwa ya Mungu (wakati huo huo ) kuwafanyia wanawake mambo yaliyokosa adili namna hiyo.
Kwa upande mwingine tunawakuta, wengine wanaofikiri (hata miongoni mwa Waarabu waislamu) na ambao wamegundua kwamba wanawake hawachukuliwi sawa na wanaume katika Uislamu, ingawaje ni wa chache tu wanaoweza kudai hivyo hadharani.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW