Wednesday, February 8, 2017

YESU ALIKUWA 100% MUNGU NA 100% MWANADAMU

Image may contain: text
Ndugu msomaji,
Tunaendelea kujifunza kuhusu Uungu wa Yesu. Quran, Allah, Muhammad na Jibril kwa mara nyingine tena wanakiri kuwa Yesu ni Mungu.
Hii ni sifa nyingine ya Mungu pekee na wala si ya mwanadamu.
Quran 40:2-3 Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye kujua. Anaye SAMEHE DHAMBI na anaye pokea toba, Mkali wa kuadhibu, Mwenye ukarimu, hakuna mungu ila Yeye; marejeo ni kwake.
Je, Bwana Yesu alikuwa na sifa hii ya kusamehe dhambi?
Katika tukio moja ambalo Yesu alionesha mamlaka yake ya Uungu kwa kusamehe dhambi na wakuu wa dini walioina hiyo kama kufuru kwani mwenye uwezo wa kusamehe dhambi ni Mungu pekee kwa vile hata wao hawakufahamu mamlaka ya Yesu ni Mungu
Marko.2:5-11 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza), Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.
Hili ni mojawapo ya matendo ya Yesu ***kusamehe dhambi*** aliyotenda kuonesha Uungu wake na mamlaka yake.
Sura ya 4
Ubinadamu wa Yesu na sababu ya kuitwa Mwana wa Mungu toka mamlaka ya Uungu.
Ndugu mpendwa msomaji tutakubaliana kuwa hilo ni moja kati ya maswali nyeti yanayoulizwa na watu wengi wanao hoji na kutafiti mamlaka haswa ya Bwana Yesu.

MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE


MAJINA YA MUNGU WA BIBLIA
MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El‐Shaddai. Ni neno lenye majina mawili ndani yake. ‘El’ maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana itokanayo na neno ‘Shad’ yaani Titi (Ziwa) la mama anyonyeshaye.
Kutokana na ukweli kwamba, titi/ziwa la mama anyonyeshaye, linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa ya mama yake, humpa mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna vitamini, protini, wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto anachohitaji. Maziwa ya mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo, Waisraeli wanapomwita Mungu El‐Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama ziwa linavyo mtosheleza mtoto, vivyo hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’ kwetu. Halleluyah!
Hivyo, kila jina la Mungu, linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi anasema
“Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” (Zab 29:1‐ 2) Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina lake, kwakuwa lapendeza.(Zaburi 135:3).
Na Bwana Yesu alitufundisha kuanza sala namna hii;
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako tukutuzwe, hakafu Ufalme
wako uje hapa duniani.
Kwahiyo, unaweza pia kumsifu Bwana kwa majina yake. Majina ya Mungu, hueleza aidha sifa za Mungu au tabia za Mungu au Matendo makuu ya Mungu. Yafuatayo hapa chini, ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya Kiebrania, yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.
MAJINA YA MUNGU NA UKUU WAKE.
MUNGU akubariki sana na msingi wa somo letu uko katika Zaburi 83:18 inayosema ''Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.''
1: JEHOVAH ADONAI =MUNGU Mwenye Enzi Yote (Mwanzo 15:2-8 )
2: JEHOVAH EL – SHADAI =MUNGU Ututoshalezae MUNGU Mwenyenzi (Mwanzo 17:1)
3: JEHOAH EL-OHEENU =BWANA MUNGU Wetu (Zaburi 99:5,8,9)
4: JEHOVAH EL- GIBBOR= MUNGU Mwenye Nguvu ( Isaya 9:6-9)
5: JEHOVAH EL-OLAM =MUNGU wa Milele (Mwanzo 21:23)
6: JEHOVAH EL-OHEEKA= BWANA MUNGU Wako (Kutoka 20:2,5,7)
7: JEHOVAH EL-ELYON= MUNGU Aliye Juu Sana (Mwanzo 14:18)
8: JEHOVAH EL-OHIM =Muumbaji wa Milele (Mwanzo 1:1)
9: JEHOVAH SABAOTH =BWANA wa Majeshi (1 Samweli 1:3)
10: JEHOVAH TSIDKEMU= BWANA ni Haki Yetu (Yeremia 23:6)
11: JEHOVAH RAPHA= MUNGU Nikuponyae (Mwanzo 15:26)
12: JEHOVAH MEKADDISHKEM =BWANA Niwatakasae (Kutoka 31:13)
13: JEHOVAH ROHI =BWANA Mchungaji Wangu( Zaburi 23:1)
14: JEHOVAH JIREH= MUNGU Atupaye /Atoaye (Mwanzo 22:14)
15: JEHOVAH HOSEENU= BWANA Aliyetuumba (Zaburi 95:6)
16: JEHOVAH NISSI= BWANA ni Bendera(Beramu) yangu (Kutoka 17:15)
17: JEHOVAH SHALOM =BWANA ni Amani Yangu (Waamuzi 6:24)
18: JEHOVAH SHAMMAH= BWANA Yupo Hapa (Ezekiel 48:35).
MUNGU akubariki sana na kama hujaokoka yaani hujampokea BWANA YESU awe ni BWANA na MWOKOZI wa maisha yako ndugu hakikisha unampokea leo maana wokovu ni sasa.

ALLAH SIO JINA LA MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)


Ndugu msomaji,
Waislam wamekuwa wakidanganya kila siku kuwa eti Mungu anaitwa Allah. Sasa leo nataka tujadili kwa amani na upendo hapa kuhusu huyu ALLAH.
Allah sio jina bali wadhifa tu. Ndio maana Allah AMEKIRI KUWA YEYE ana majina 99, ANGALIA HAPA KWA USHAHID http://www.islamicity.com/mosque/99names.htm.
Kati ya hayo majina 99 hakuna jina la Yehova, JAHAWEH, MIMI NIKO nk ingawa Waislam kila kukicha wanadai eti Mungu wa Musa ni huyo Allah au Mungu wa Daudi ni huyo Allah. Ili kuthibitisha ninacho sema, Mungu wa kwenye Biblia kasema hivi kwenye Yeremia.
Mungu mwenyewe alisema: “Watajua kwamba jina langu ni Yehova.” (Yeremia 16:21)
Sasa, wote tunafahamu kuwa Biblia ilikuja miaka 650 kabla ya Quran na kwenye hiyo Biblia Mungu alisema kuwa yeye jina lake ni "MIMI NIKO", "YEHOVA" n.k. LAKINI CHA AJABU, Allah HAKUSEMA KUWA YEYE NI "MIMI NIKO" AU "YEHOVA" kwenye hayo majina yake 99.
Je, Allah ni nani huyu, maana teyari anapinga na YEHOVA wa kwenye Yeremia 16 aya 21 na AMEKATAA kuyatumia hayo majina ya Mungu wa kwenye Biblia?
Zaidi ya hapo, wapi Mungu anasema kwenye Taurat kuwa jina lake ni Allah?
Wapi Mungu anasema kwenye Zaburi kuwa Jina lake ni Allah?
Wapi Mungu anasema kwenye Injili kuwa Jina lake ni Allah?
Haya ni maswali rahisi sana kwa Waislam na hayahitaji jazba katika kuyajibu zaidi ya wao watuletee aya kutoka Taurat au Zaburi au Injili kuwa Mungu anasema kuwa yeye jina lake ni Allah.
Wakishindwa kutuletea aya basi watuletee aya kutoka Quran ambayo Allah anasema kuwa yeye jina lake ni Yehova au Yahawe au Mimi Niko.
Leo ningependa tujadili kwa kutumia aya na kwa upendo.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

ALLAH SIO JINA LA MUNGU (SEHEMU YA PILI)


Ndugu msomaji,

Katika mada iliyo pita, tumethibitisha kuwa Mungu wa kwenye Biblia ana jina/majina, na Allah wa kwenye Quran naye ana majina 99 kama ilivyo shahidiwa kwenye vitabu vyake angalia link hii:http://www.islamicity.com/mosque/99names.htm .

ZAIDI YA HAPO, NIMETHIBITISHA KUWA ALLAH SIO JINA BALI NI WADHIFA TU KAMA ILIVYO "RAIS" "MFALME" nk. Hayo maneno "Rais", "Mfalme" sio majina bali hao wenye huo wadhifa wanayo majina yao na ndio maana huwa tunasema Rais "fulani" kasema hivi au Mfalme fulani kasema hivi na vile, Lazima tuweke jina la huyo Rais au Mfalme katika maelezo yako.

Kwenye hii mada tunaendelea kumuuliza Allah mswali na kuwauliza Waislam maswali kuhusu huyu Allah mwenye jina lisilo tambulika na au halipo kwenye Taurat, Zaburi, na Injili.

SASA TUANZE MADA YETU:
Waislam hupenda kuanza kusema maneno haya katika hotuba zao: Nukuu: "KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU"

Hayo maneno yanatuambia kuwa "Mwenyezi Mungu" anaye tamkwa na Waislam ana Jina, kama sio "majina".

Swali la kwanza: Kwa ndugu zetu Waislam ni hili hapa. "Mnaweza tuambia hilo jina la Mwenye Mungu ambaye ni mwingi wa Rehema na mwenye kurehemu ni lipi" Tafadhali tujibuni kwa kutumia aya.
Swali la pili kwa Waislam:

Kama "Allah" ni jina la Mwenyezi Mungu wa Waislam, tunaomba mtupe aya kutoka Quran yenu ambayo Mwenyezi Mungu ambaye ni mwingi wa rehema na mwenye kurehemu anasema kuwa "ALLAH" ni jina langu.

HATIMAYE MUHAMMAD AKIRI KUWA YESU NI MUNGU.


Nani atakuhukumu walimwengu wote?
Biblia inakujibu kuwa Yesu ndie atakaye hukumu walimwengu wote, ikimaanisha Muhammad, Allah, Waislam wote, Majini yote yatahukumiwa na Yesu.
(Zaburi 58:11 ), ‘Hakika yuko Mungu anayetawala katika dunia“. (Ufunuo 18;8 ) “Kwasababu hiyo, mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti na huzuni na njaa naye atateketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu“. Tene ndiye atakaye ihukumu Dunia yote “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote,bali amempa Mwana (YESU) hukumu yote“.
(Mathayo 25:31-32 ) “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu (YESU) katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote yatakusanyika mbele zake,naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi”.
(Matendo 10:42 ) “Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudiaya kuwa huyu ndiye (Yesu) aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu” ( WARUMI 2:16 ) “Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu,sawasawa na injili yangu,kwa Kristo Yesu“. (2 Timotheo 4:1 ) “Nakuagiza mmbele za Mungu,na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu waliohai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake’.
LAKINI NILIPO VISOMA VITABU VYA KIISLAM Sahih Bukhari....... 95 Hadith ya Abu Huraira (ra0 amesema: Mtume wa Allah (s.a.w) amesema, "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, karibu atatetemka kati yenu Mwana wa Maryam atahukumu kwa uadilifu....
USHAIDI UNASEMA KUWA:
1. Muhammad anaapa kwa Yesu na sio Allah.
2. Muhammad anakiri kuwa Yesu atarudi kutoa hukumu kwa uadilifu.
3. Muhammad anakiri kuwa nafsi yake ipo mikononi Mwa Yesu ambaye ni Mungu wake.

LEO TUMEJIFUZA KWA KUTUMIA VITABU VYA WAISLAM KUWA, HATA MUHAMMAD NABII WA ALLAH AMEKIRI KUWA YESU NI MUNGU WAKE NA ANAMHUKUMU SIKU YA KIYAMA.
Sasa kwanini usimpokee Yesu ambaye atakuhumu maisha yako/ Kumbuka, HAKIMU NI YESU NA SIO ALLAH, AU MUHAMMAD.
Karibu kwa Yesu
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo

ALLAH SIO YEHOVA "YAHUH" ( يهوه ) MWENYEZI MUNGU (SEHEMU YA KWANZA)



Huu ni msiba mwengine kwa Waislam na kwa Muhammad.
Yehova ni Jina la Mungu ambalo kwa Kiingereza anaitwa Jehovah na kwa Kiebrania anaitwa יהוה (YHVH) na kwa Kiarabu anaitwa (yahuh ) au ( يهوه ). ngoja niweke kwa urahisi ili wafuasi wa Muhmmad waelewe;
1. Kiebrania = יהוה (YHVH)
2. Kiingereza = Jehovah
3. Kiswahili = Yehova
4. Kiarabu = yahuh ( يهوه )
Allah katika Surat Bani Israil anasema kuwa yeye anamajina mazuri mazuri na kasema kuwa Allah ni Jina na sio Wasifa. Nilipo chunguza kwa makini katika Majina yake 99, sikuliona jina la Allah katika hayo 99. Ingia hapa na thibitsiha mwenyewe http://www.searchtruth.com/Allah/99Names.php
Lakini cha ajabu Allah anadai katika Surat Bani Israil 110 kuwa "ALLAH" ni jina lake angalia ushahid hapa chini.
Qr. 17 Surat Bani Israil 110 (Wana wa Israil)
Sema; muombeni (Mwenyenzi Mungu) kwa (jina la) Allah au muombeni (kwa jina la) Rahman. Kwa jina lolote mnalomwita (katika haya itafaa). Kwani ana majina mazuri mazuri………
Hivi huyu Allah anamatatizo gani? Maana ameshindwa kutupa jina lake. Sasa anasema kuwa Allah ni Jina lake, na nilipo angalia kwenye yale majina 99, ALLAH HALIPO. Na hata kama tukiliweka, basi ALLAH ATAKUWA NA MAJINA 100 na sio 99. Huu ni msiba mwengine kwa Waislam.
Allah ana majina mangapi, 99 au 100?
SASA TUMSOME MUNGU WA KWENYE BIBLIA:
Mungu anayejulikana
Kutoka 6:2-3,
Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, mimi ni YEHOVA;
Nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.

ALLAH YEYE ANAPENDA WATU WANAO PIGANA KWA AJILI YAKE TU


Surat Assaf 4. Kwa hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanao pigana katika Njia yake kwa safu kama jengo lilio kamatana. Maelezo
Surat An Nisaai 74. Basi nawapigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanao uza uhai wa dunia kwa Akhera. Na anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauliwa au akashinda basi tutakuja mpa ujira mkubwa.
75. Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anaye toka kwako. Maelezo
76. Walio amini wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio kufuru wanapiana katika njia ya upotofu. Basi piganeni na marafiki wa Shet'ani. Hakika hila za Shet'ani ni dhaifu
Hivi Mungu gani huyu anaye penda kuwachinganisha watu?
Hakika Allah ahakuumba ndio maana yeye hapendi watu na amewaitwa WATWANA huku yeye akiwa ni BWANA wao.
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.

KWANINI MUHAMMAD NA ALLAH WANAWACHUKIA WAKRISTO NA WAYAHUDI?

Image may contain: 1 person, text
Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kuhusu chuki iliyo ndani ya Allah na dini yake ya Uislam. Wengi wenu huwa mnadai na au fikiria kuwa Mungu wa Biblia aliye jaa upendo ni huyo huyo wa kwenye Quran ya Jibril. La hasha.
Allah ambaye ndie miungu wa Waislam yeye amejaa chuki na anawataka na kuwaamrisha Waislam wote kufanye chuki iliyo ndani ya Quran.
Hebu anza moja kwa moja kusoma chuki za Allah:
ALLAH ANAWAAMBIA WAISLAM WOTE KUWA: NI MARUFUKU KUWA MARAFIKI NA WAKRISTO:
Surat Al Maida 51. Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu. http://www.quranitukufu.net/005.html
SASA, kama Allah ni Yehovah wa Biblia, mbona hatusomi Mungu wa Biblia akisema muwachukie watu ambao sio wa imani yenu?
SOMA Luka 6:35 Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
35 Bali, wapendeni adui zenu, watendeeni mema. Wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo mtapata zawadi kubwa nanyi mtakuwa wana wa Mungu Aliye Juu. Yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na watu waovu.
MUNGU WA BIBLIA ANSEMA Wapendini adui zenu, ni tofauti kabisa na Allah anaye sema WACHUKIENI WAKRISTO NA WAYAHUDI. Allah wa Quran sio Mungu wa Biblia.
ALLAH ANASEMA KUWA, WAISLAM HAWARUHUSIWI KUWAPENDA WAKRISTO HATA KAMA NI BABA ZAO AU MAMA ZAO AU NDUGU ZAO:

SHEIKH AOKOKA BAADA YA KUOMBEWA NA KUPONA KWA JINA LA YESU.


AKIRI KUWA YESU NI MUNGU MKUU.
More details to follow....................
Image may contain: 1 person, sitting

Image may contain: one or more people and people standing

MASWALI MAGUMU AMBAYO WAISLAM WAMEGOMA KUYAJIBU.

Image may contain: 1 person, text
1. Adamu na Hawa walifukuzwa kwenye Bustani ya Edeni kutokana na dhambi. Sisi pia tulio uzao wao ni wenye dhambi? Suluhisho la tatizo hili ni moja tu kulingana na Biblia – Yesu Kristo alikufa msalabani na kufanyika sadaka au dhabihu ili sisi tusiendelee kuchinja wanyama kila siku kwa ajili ya dhambi zetu kama torati inavyosema, badala yake tuamini TU katika sadaka ya Yesu na kupokea msamaha wa dhambi na wokovu wa Mungu bure.
Waislamu hamumwamini Yesu Kristo kama mwokozi aliyefia dhambi za wanadamu wote. Je, suluhisho la dhambi kwa mwanadamu ni nini? Kwa maana nyingine, ninyi Waislamu mtaponaje na jehanamu ya moto ilhali ni wazi kuwa ninyi, kama ilivyo kwa kila mwanadamu, mna dhambi ambazo ndizo hizohizo zilimtenga Adamu na Mungu?
2. Biblia inasema: Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. (1 Yohana 1:8-9). Kwa hiyo mimi Mkristo nikijikuta nimetenda dhambi nakwenda mwenyewe kwa Bwana Yesu na kumwambia, “Bwana wangu, nimesema uongo, nimeiba, nimetukana, nimetamani, … n.k. naomba unisamehe.” Sisubiri hadi mchungaji au mtu mwingine anikamate kwenye kosa kama polisi wanavyokamata wahalifu.
Ninyi Waislamu mnasema kuwa torati ndiyo njia sahihi ya maisha ya mwanadamu, kwamba mtu akifanya makosa ni lazima aadhibiwe kama vile kupigwa mawe, kuchapwa viboko, kukatwa mikono, n.k.
Swali ni kuwa, kwa nini hatusikii Waislamu wakijipeleka wenyewe kupokea adhabu hizo baada ya kufanya dhambi? Hatujawahi kusikia Mwislamu ameenda kusema, “Jamani nimezini kwa hiyo nimekuja mnipige mawe; Nimeiba, hivyo nimekuja mnikate mkono.” Kwa nini wanaoadhibiwa ni wale TU wanaokamatwa? Mnataka kutuambia kuwa wakosaji ni hao tu? Kama unaamini kuwa mzinzi ni lazima apigwe mawe, si uende ukaombe wakupige mawe baada ya kuzini. Kwa nini hamfanyi hivyo?

Contradictions in the Quran: A Theological and Textual Examination

Contradictions in the Quran: A Theological and Textual Examination By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction Muslims ...

TRENDING NOW