Wednesday, March 29, 2017

ALLAH KAFANYA MAKOSA MAKUBWA YA KIHISTORIA KUHUSU YUSUFU NA BABA YAKE YAKOBO

Image may contain: 3 people, beard and text
Ndugu msomaji,
Leo tutaangalia kwa undani sana MAKOSA MAKUBWA YA ALLAH kuhusu Yusufu mtoto wa Yakobo.
Allah anasema kuwa, Yusufu alipo kuwa Misri na kufuatwa na ndugu zake, eti, wazazi wake wote walienda Misri. Je, haya madai ya Allah ni ya kweli? Hebu kwanza tusome ushahid hapa chini:
TUANZE NA QURAN:
Surat Yusuf aya ya 99. Na walipo ingia kwa Yusuf aliwakumbatia wazazi wake na akasema: Ingieni Misri, Inshallah, mmo katika amani.
100. Na akawapandisha wazazi wake kwenye kiti cha enzi. Na wote wakaporomoka kumsujudia. Na akasema: Ewe baba yangu! Hii ndiyo tafsiri ya ile ndoto yangu ya zamani. Na Mwenyezi Mungu ameijaalia iwe kweli. Na Mwenyezi Mungu amenifanyia wema kunitoa gerezani, na kukuleteni kutoka jangwani baada ya Shet'ani kuchochea baina yangu na ndugu zangu. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mpole kwa alitakalo. Bila ya shaka Yeye ni Mjuzi Mwenye hikima.
ALLAH ANASEMA KUWA YUSUFU aliwakumbatia WAZAZI WAKE NA AKASEMA INGIENI MISRI kama alivyo shahidiwa kwenye Surat Yusufu aya ya 99 hapo juu, jee, hayo madai ya Allah ni ya kweli?
HEBU SASA TUANZE kupangua madai/hoja ya Allah moja baada ya nyngine kwa kutumia Taurat iliyo kuja kabla ya Quran.
BIBLIA INASEMA:
Mwanzo Mlango wa 35 :16 Wakasafiri kutoka Betheli, hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrathi, Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa, na utungu wake ulikuwa mzito.
17 Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine.
18 Ikawa hapo katika kutoa roho yake, maana alikufa, akamwita jina lake Benoni, lakini babaye alimwita Benyamini.
19 Akafa Raheli, akazikwa katika njia ya Efrathi, ndio Bethlehemu.
20 Yakobo akasimamisha nguzo juu ya kaburi lake, ndiyo nguzo ya kaburi la Raheli hata leo.
BIBLIA IMETUTHIBITISHIA KUWA Raheli mama yake Yusufu alifariki wakati wa kuzaliwa kwa mdogo wake Benyamini na alizikwa njia ya Efrathi. Ushahidi huu ndio tumeusoma katika Mwanzo 35 aya ya 19.
Sasa maswali ya kujiuliza hapa, ni kwanini ALLAH ANASEMA KUWA YUSUFU ALIWAKARIBISHA wazazi wake na sio Mzazi wake, maana aliye kuwa hai ni Baba yake tu?
Wahadhiri wa Kiislam nilipo ongea nao wakadai kuwa eti, ni kweli mama yake mzazi wa kibaologia ambaye ni Raheli alifarikia lakini Benyamini alilelewa na Mama yake Mkubwa aitwaye Leah. Haya madai yapo vile vile katika (Abdullah Yusuf Ali, The Holy Qur'an, Saudi edition, fn. 1777). Je, tunaweza kuyakubali haya madai kama ni kamilifu na kuvunja hoja yangu ya UTATA wa Allah kuhusu WAZAZI WA YUSUFU walio ingia Misri?
Ngoja niongeze na hoja zaidi kutoka Waislam kabla ya mimi kujibu hayo madai yao ya Benyamini kutunzwa na LEAH hivyo basi Yusufu alipo sema kwa WAZAZI WAKE INGENI MISRI alikuwa sahihi.
Kufuatana na ushahidi wa Biblia [Mwanzo 35:16-20], inafahamika kuwa mama yake Yusufu alifariki wakati anamzaa Benyamini. Hivyo, ngoja tu hisi/KUBALI kuwa labda Quran na Allah walimaanisha ni LEAH ambaye aliitwa kama MZAZI WA Yusufu, kwasababu LEAH alikuwa mmoja ya wake wa Yakobo, na hivyo basi, Leah ndie aliye mlea Benyamini baada ya mama yake kufariki wakati akimzaa. Haya madai yanaweza kuwa sahihi kwa tamaduni za Kiarabu kuwa mzazi mwenza ana haki ya kutunza mtoto wa mumewe "mother" to a foster-mother. (Muhammad Asad, The Message of the Qur'an, p. 352, fn. 96; bold emphasis mine)
Ingawa tamaduni za Kiarabu kwenye hiki kisa hazina mshiko kwasababu Yakobo hakuwa Muarabu hata kama Leah alifanya hivyo na kumtunza Benyamini na Yusufu kumuita Leah Mama yake.
Zaidi ya hapo, hayo madai ya Waislam hayana nguvu tena kwasababu Biblia sio tu ilituambia kuhusu kifo cha Raheli, bali ilituambia vilevile kuhusu kifo cha Leah kabla ya Yakobo na familia yake kwenda Misri.
Mwanzo 46: 5 Yakobo akaondoka kutoka Beer-sheba; wana wa Israeli wakamchukua baba yao na watoto wao wadogo, na WAKE ZAO katika magari aliyoyapeleka Farao ili kumchukua.
6 Wakatwaa na wanyama wao, na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani, wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
7 Wanawe, na wana wa wanawe, pamoja naye, binti zake na binti za wanawe, na uzao wake wote, aliwaleta pamoja naye mpaka Misri.
Unapo soma aya hapo juu, utagundua kuwa Biblia imesema kuhusu WAKE ZA WATOTO WA YAKOBO lakini haikusema kuhusu mke wake Yakobo aitwaye LEAH.
Ukiendelea kusoma aya zinazo fuatia utagundua kuwa Wote walio kwenda Misri wametajwa na hakuna jina la Raheli au Leah katika hizo aya. Lakini tunasoma majina ya wake za watoto wa Yakobo. Tafadhali soma Mwanzo 46 aya ya 8 mpaka 25.
SASA BASI, Yakobo alipo karibia kifo, aliwaambia wanawe wapi anataka azikwe Mwanzo Mlango wa 49: 29 Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;
30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.
31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;
32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi.
Katika aya ya 31 inathibitisha kuwa Yakobo alimzika Lea KANANI. Huu ni ushahidi zaidi kuwa Lea alizikwa KANANI na sio Misri, hivyo basi haiwezekani Lea kwenda Misri na apokewe na Yusufu kama amabvyo Quran inadai. Je, unwezaje kumwanini ALLAH AMBAYE ANAFANYA MAKOSA MAKUBWA NAMNA HII KUHUSU TUKIO LA MUHIMU KAMA HILI?
HITIMISHO:
1. Mama yake Yusufu alikufa muda mrefu hata kabla ya Yufuku kwenda Misri.
2. Lea vile vilealifariki muda mrefu hata kabla ya mumewe Yakobo kwenda Misri.
3. Hakukuwa na mke hata mmoja ambaye alikwenda na Yakobo Misri.
4. Allah alipo sema kuwa WAZAZI WA YUSUFU WALIENDA MISRI, hapo ni MAKOSA MAKUBWA SANA AMBAYO yanatufanya tuushuki uungu wa Allah.
Zaidi ya hapo, Quran huwa inasema kuwa baba na mama yako ni wazazi wako wa kibaologia na sio wa kambo, haya madai yalisemwa na Yusuf Ali .
Ndugu msomaji,
Kwa mara nyingine tena tunaona utata mkubwa sana katika Quran ambayo Waislam wanadai kuwa haina shaka ndani yake.
Je, baada ya kusoma hiki kisa na kuona shaka na utata ndani ya Quran, utaweza endelea kuiamini kuwa hicho kitabu ni thabiti na cha Mungu Mkuu?
Ndugu msomaji, mii sipo hapa kubishana bali kukuonyesha kuwa Quran sio kitabu cha Mungu na kimejaa shaka. Amua leo kumfuata Yesu aliye hai ambaye hana makosa wala utata ndani yake na ni MWOKOZI WA MAISHA YAKO.
MUNGU AKUBARIKI SANA NA KARIBU KWA YESU.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 21, 2016

MASHEHE NA USTAADH WASALI KANISA LA UFUFUO NA UZIMA

Image may contain: 1 person, standing
Naona Madhabu ya Ufufuo na Uzima leo imepokea Ustaadhi..😝😝😝. Sijui Shekhe?
Mambo yanazidi Kunoga!
JUMAPILI 26/03/2017
Jumapili ya leo Ufufuo na Uzima wamekuwa na ugeni wa kutembelewa na Mashehe kwa sababu Ufufuo na Uzima ni rafiki wa waislam. “Anasema Shekhe dini ya uislam haizuii mtu kuwa na rafiki asiye Muislam” ameendelea kusema Ugomvi wa kidini ni uchoyo, kila tunalofanya tufanye kwa kuhakikisha watu wanaishi kwa Amani na furaha. Pia amesema ifike mahali Serikaliyetu itumie watu kama Askofu Gwajima kuitangaza Tanzania na vivutio vilivyopo Tanzania na isiwe kuwasakama na kuwasumbua.
@Bishop
Mungu akiwaita watu kuwa makuhani ni kwa makusudi yake na kila kuhani anaitwa kwa saa yake na wakati wake, kila mtu ana wito wake.Image may contain: 2 people, people on stage and people standing

Image may contain: 3 people, people standing
Image may contain: 3 people, child

UNAWAFAHAMU MALAIKA WAKUU SABA WA MUNGU "ARCHANGELS OF GOD? (SEHEMU YA TATU)

Image may contain: 2 people, text
MALAIKA MKUU GABRIEL
Neno "Malaika Mkuu" linatokana na neno la Kiyunani Archangelos, lenye maana ya Mkuu wa Malaika (chief angel), kwa tafsiri ya Krania rav-mal'ákh, linatokana na neno la Kiyunani archein, linalomaanisha kuwa wa kwanza katika cheo au nguvu (to be first in rank or power); na neno angelos linalokaanisha mjumbe (messenger), au muwakilishi wa balozi (envoy).
Neno hili limetumika mara mbili tu katika Agano Jipya katika 1 Wathesalonike 4:16 na katika Yuda 1:9. Ni malaika Wakuu Gabrieli na Mikaeli tu ambao wametajwa kwa majina katika Agano Jipya.
Katika desturi nyingi za kikristo, Malaika Gabrieli anatambuliwa kuwa ni Malaika mkuu, lakini hakuna maandiko ya moja kwa moja yanayoonyesha jambo hili. Ni vema kutambua ya kwamba, neno "Malaika mkuu" linaonekana kutumika tu kwa umoja, na si katika wingi, na pia hutumika tu kumtaja malaika Mikaeli kuwa ndiye Malaika Mkuu.
Malaika waliumbwa katika Roho na ni Roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi Wokovu (Ebrania 1:14). Mungu aliwaumba Wana wake wa Kiroho kabla ya Uumbaji wa nchi (Ayubu 38:4-7). Kuna zaidi ya malaika milioni 100 (Angalia Daniel 7:9-10; Mathayo 26:53; Lk 2:13; Ebrania 12:22; Ufunua 5:11). Malaika wameumbwa katika hali ya mmoja mmoja (individuals) ambao wana uhuru wa kuchagua, ambao ndiyo unahitajika katika kukua kwa tabia.
MAANA YA NENO GABRIEL
Neno au jina “Gabriel” asili yake ni lugha ya kiebrania na maana ni “Mjumbe wa Mungu” katika Biblia jina hili Gabriel limetajwa mara “nne” (4) (Tazama Danieli 8:16 na 9:21, Luka 1:19 na 1:26) kuhusu malaika Gabriel mara nyingi Biblia inaonyesha kuwa Mungu anamtuma ili alete habari njema zinazohusu wokovu wa wanadamu na hutoa maneno ya kuwafariji wale aliowatokea akisema “usiogope”katika Biblia limetajwa mara (366) aidha tunaposoma Biblia tunaona pia malaika huyu anaitwa malaika wa Bwana (The angel of the Lord) Neno hili katika biblia limetajwa mara (65) katika aya zipatazo (61) iwapo sehemu hizo zote zinahusika na malaika Gabriel basi malaika huyo atakuwa ametajwa mara nyingi.
MALAIKA GABRIEL ALIYETUMWA NA MUNGU YEHOVA ANASEMA HIVI…
Malaika akajibu akamwambia Mimi ni Gabriel, nisimamaye mbele za Mungu, nimetumwa niseme nawe na kukupasha habari hizi njema (Tazama Luka 1:19)
Kwa mujibu wa aya hii malaika Gabriel anaeleza kuwa husimama mbele za Mungu hivyo ni wazi kuwa cheo chake ni mjumbe asimamaye mbele ya Mungu.
MALAIKA GABRIEL WA MUNGU YEHOVA ALIFUNDISHA HIVI..
Luka 1:26-35 Nanukuu aya ya 35 tu:
Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako na nguvu zake aliye juu zitakufunika kama kivuli. Kwa sababu hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu “Mwana wa Mungu”
MAFUNDISHO YAO KUHUSU ROHO MTAKATIFU KUPITIA MALAIKA GABRIEL
Luka 1:34-35 “Malaika Gabriel anamwambia Mariam hivi…
34. Mariam akamwambia malaika litakuaje neno hili maana sijui mume? 35. Malaika akajibu akamwambia Roho Mtakatifu atakujilia juu yako na nguvu zake aliye juu zitakufunika kama kivuli- Roho Mtakatifu ni Mungu (Matendo 5:3-4) Na wala siyo malaika ndio maana malaika alisema atakujilia.
MALAIKA GABRIEL ANAPOWATOKEA WATU ANAFANYA HIVI…
Luka 1:19 Alijitambulisha Kwa kusema, “Mimi ni Gabriel.”
Daniel 8:15-16 Au muhusika ambaye alimtokea hujulishwa kwanza
Daniel 8:17-21, Luka 1:13, 30…
Gabriel anamsadia mtu pale anapopatwa na hofu na anasema usiogope. Tabia za malaika Gabriel ni huruma na kumfahamisha mtu kwa upole.
Katika tukio la lingine ni wakati Danieli alipokuwa akiomba na Gabrieli akarushwa upesi akanigusa….. akaongea nami, aliendelea kutabiri wakati wa kuja kwa mara ya kwanza kwa Masihi Yesu Kristo (Daniel 9: 21-27).
Kwa hiyo Wayahudi walikuwa wakitazamia sana wakati wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulipokaribia ; kuonekana dhahiri kwa Grabriel tena kulizidishia matazamio kwanza kwa Zakaria kuhani aliyekuwa zamu hekaluni na kisha kwa Mariamu aliyekuwa ameposwa na Yusufu. Kwa Zakaria , malaika akamwambia "mimi ni Gabrieli nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa niseme nawe" (Luka 1:19).
Tunaona kuwa Malaika anao uwezo wa kusimama mbele ya uso wa BWANA, jambo ambalo wanadamu hawawezi, hivyo Malaika hutumwa kufanya yote yaliyo mapenzi ya Mungu. Hapa ujumbe wake ilikuwa kutangaza muujiza wa kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji.
Miezi sita baadaye, Gabrieli alimtokea Mariamu; ambaye alikuwa ni wa ukoo wa Mfalme Daudi.Maombi yake Mariamu; malaika alisema, uliyepewa neema na Mungu,nawe utakuwa mama wa Masihi anayetarajiwa. Gabriel alimwambia kuwa atapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na mtoto wake ataitwa Yesu, Mwokozi, naye atakuwa Mwana wa Mungu na atakalia kiti cha enzi cha Daudi (Luka 1: 26-33).
Malaika Mkuu Gabriel:
• Alitafsiri maono ya Danieli (Dan. 8:16, 26; 9:20-27)
• Alitangaza juu ya kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji (Lk. 1:11-20)
• Alitangaza kuzaliwa kwa Yesu (Lk. 1:26-38).
Katika kitabu cha Henoko kinataja majina ya Malaika wakuu sita:
Mikaeli (Mkuu wa sehemu mhimu sana ya wanadamu) Gabriel (Mkuu wa Bustani na wa Makerubi), Urieli Malaika Mkuu wa dunia na watu wakali) na Raphaeli (Malaika Mkuu wa Roho za wanadamu), Ragueli (ambaye analipiza kisasi juu ya dunia na mwangaza) na Saragaeli (Malaika Mkuu wa watoto wa wanadamu, ambao Roho zao wametenda dhambi).
Kitabu cha Henoko, sura ya 20, R.H Charles, 2002).
Malaika hawa pia wanaitwa Malaika Walinzi.
Malaika katika Agano Jipya:
Tunaona ya kwamba Malaika walimhudumia Yesu wakati alipokuwa katika nchi (duniani) (Mathayo 4:11, Luka 22:43). Malaika alimtokea Yusufu na kumwarifu habari za kuzaliwa kwake Yesu (Mathayo. 1:20, Luka 1:26-38). Malaika walikuwepo katika ufufuo wa Yesu (Mathayo 28:2-8; Yahana 20:12). Na walizungumzia wakati wa kupaa kwakeYesu Kristo (Matendo 1:9-11). Malaika wanatoa huduma za Kiroho kwa watu wa Mungu (Ebrania 1:14; Mathayo. 18:10; Matendo 5:19; 8:26; 10:3; 12:7; 27:23). Malaika hufurahi mwenye dhambi anapotubu (Luka 15:10).
Katika Agano Jipya, Kristo kama mwanadamu bado alitenda kama mtu aliye mdhihirisha na kumfunua Mungu. Na alitenda kwa ukamilifu akifuata asili ya Mungu na tabia ya Mungu. Kama Mpatanishi kati ya Mungu na Wanadamu, kumwona Yesu ni sawa na kumwona Mungu, na kusikia na kumtii Yesu ni kumsikia na kutii Mungu (Eloah). Maneno aliyozungumza hayakuwa maneno yake mwenyewe bali maneno ya Mungu yaliyotoka kwa Mungu. (Yahana 14:8-10)
Usikose SEHEMU YA NNE INAYO HUSU Archangel Selaphiel.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

HUYU MUHAMMAD ANAHUDUMU CHINI YA UKUHANI UPI?

Image may contain: one or more people and text
……………..
Tangu Mungu alipoanzisha Agano na Israeli pale Sinai (Agano la Kale), daima amekuwa anawasiliana na wanadamu kupitia MAKUHANI. Kunakuwa na KUHANI MKUU na makuhani walio chini yake.
……………
Kati ya kabila 12 za Israeli, aliiteua kabila ya Lawi wawe ndio makuhani.
Kumb 10:8 Na wakati huo Bwana aliitenga kabila ya Lawi … wasimame mbele ya Bwana kwa kumtumikia, na kuwabarikia watu kwa jina lake, hata hivi leo.
……….
Hesabu 1:50 lakini uwaweke Walawi wawe juu ya maskani ya ushahidi, na juu ya vyombo vyake vyote, na juu ya vitu vyake vyote
……….
Kuhani Mkuu alikuwa Haruni.
…………
Yesu alipokuja, alianzisha Agano Jipya na sheria zake mpya. Imeandikwa:
Waebrania 7: 15-17 ametokea KUHANI MWINGINE MITHILI YA MELKIZEDEKI; asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, bali kwa nguvu za uzima usio na ukomo; maana ameshuhudiwa kwamba, WEWE U KUHANI MILELE KWA MFANO WA MELKIZEDEKI.
…………..
Yesu ni kuhani kwa mfano wa Melkizedeki na sio kwa mfano wa Lawi.
…………
Hivi sasa hakuna Kuhani Mkuu zaidi ya Yesu. ---- WEWE U KUHANI MILELE KWA MFANO WA MELKIZEDEKI.
…………….
Watumishi wote wa Mungu leo ni makuhani CHINI YA KUHANI MKUU YESU. --- 1 Pt 2:9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu
……………..
MASWALI
1. Muhamamad alikuwa kuhani?
2. Kama ni ndio, alikuwa chini ya Lawi au chini ya Yesu?
3. Kama sio, uhalali wake ulitoka kwa Mungu gani?
4. Ndugu waisalmu, kuhani wenu ni nani?
…………….
Abiria chunga maisha!!!
Hakuna kama Yesu.
Imeletwa kwenu na Jimmy John

THE LARGEST MOSQUE IN EUROPE WAS BURNING DOWN TODAY IN SOUTH LONDON

Image result for THE LARGEST MOSQUE IN EUROPE WAS BURNING DOWN TODAY IN SOUTH LONDON
Ablaze: Pictured is the Baitul Futuh in Morden, South London, which is the largest in western Europe
Seventy firefighters in south London are battling an enormous blaze which engulfed western Europe’s largest mosque.
Ten fire engines were dispatched to deal with the fire at the Baitful Futuh mosque in Morden, which started burning around midday.
A man has been taken to hospital for smoke inhalation, but community leaders have said they do not believe anybody else was affected. The cause of the blaze is not yet known.
Before: The Baitul Futuh can be seen here in a file photo from 2003. One man caught up in the blaze is is hospital with smoke inhalation
Shocked onlookers gathered opposite the mosque, watching a dark plume of smoke billowing out of the building’s roof before they were ushered behind a police cordon. The fire was reported by a member of the public just after midday.
The enormous building sits on a 5.2acre site and can hold 10,500 people. At the time of the fire, however, only a handful of worshippers were inside, and were quickly evacuated. Nobody was at prayer when the fire broke out.
The huge effort to control the fire involved the police, ambulance services and the large fire brigade presence. The firefighting operation shut down the A24 and traffic was tailed back for miles as a result.
As of 6pm, the London Fire Brigade said they had contained the fire to administrative buildings and halls around the main mosque, which was not directly affected by the fire – though it was engulfed by smoke. Shortly afterwards they declared the fire ‘under control’.
http://jagrukbharat.com/14334/largest-mosque-europe-burning-today-south-london

QURAN INASEMA WAISLAM WAMEBEBA MIZIGO YA DHAMBI








1. MIZIGO YA DHAMBI ZAO NI MIBAYA MNO "QURAN 16:25"
2. SHETANI AKIRI KUWA YEYE NDIE ALIYE IKETIA NJIA YA UISLAM
Ndugu msomaji,
Waislam wamekuwa wakisema kuwa, mtu mwengine hawezi kukubebea mizigo yako, lakini, hayo madai yanapingwa na aya kadhaa za Quran.
Nasi tulipousikia uwongofu tuliuamini; basi anayemwamini Mola wake hataogopa kupunjwa wala kutwikwa (kubebeshwa) dhambi (za mtu mwengine).” (Qurani 72:13)
Quran inasema kuwa, anaye mwamini Mwenyei Mungu, hawezi kuogopa kubebeshwa dhambi za mtu mwengine.
Je, kuna watu wanaweza kubeba dhambi za Mtu mwengine?
Soma Quran Surat An Nahl(16) aya ya 25. Kuna watu wanawapoteza wengine Ili wabebe mizigo ya madhambi Siku ya Kiyama, na sehemu ya mizigo ya wale wanao wapoteza bila ya kujua. Angalia, ni mibaya mno hiyo mizigo wanayo ibeba!
Allah kupitia Quran anawaambia Waislam wote kuwa, hiyo mizigo ya dhambi wanayo beba, NI MIBAYA MNO, na wamepotezwa ili waibebe wenyewe mpaka siku ya kiyama.
SASA, kama kubeba Mizigo siku ya kiyama mbaya mno, je, tuipeleke wapi hiyo mizigo, SASA SOMA Zaburi 55: 22 Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.
BIBLIA INAWAJIBU WAISLAM KUWA, MTWIKE BWANA MZIGO WAKO. Ndio maana Wakristo wote tumegundua hili, ENDELEA KUSOMA Yohana 13:13 INASEA: Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.
Yesu anasema kuwa, NINYI MNANIITA MWALIMU NA BWANA, NANYI MWANENA VEMA. Endelea KUSOMA Yeremia 10:10 Bali Bwana ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.
YEREMIA 10:10 INAWAJIBU WAISLAM KUWA, HUYO BWANA NDIE MUNGU WA KWELI. SASA, Waislam wanashanga kivipi Yesu awe Mungu na Yesu huyo huyo afe Msalabani, ENDELEA KUSOMA
Quran 55:29 INAENDELA KUKUJIBU 29. Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
QURAN inakujibu kwa ufasaha kuwa KILA KITU KILICHOPO MBINGUNI NA ARDHINI VINAMWOMBA YESU. Haya Mwislamu unaendelea kushangaa, Sasa angalia nini kilitendeka na au tokea Msalabani
SOMA: 1 Petro 3: 18 - 19 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, 19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;
Neno la Mungu linasema kuwa MWILI WAKE NDIO ULIUWAWA BALI ROHO YAKE AKAHUISHWA. Sasa hakuna kushangaa tena maana tufahamu ulio uwawa ni Mwili wake to bali Roho yake haikuuwawa.
Maandiko yanasema kuwa MUNGU NI ROHO, sasa aliye UWAWA NI MWILI TU BALI ROHO YAKE AKAHUISHWA
1 Timotheo 6:15-16 15 ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana; 16 ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina
Kumbe basi Yesu aliungama maungamo mazuri mazuri SOMA aya ya 13 katika 1 Timotheo 6: Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, Ushaihid zaidi soma Luka 18: 31.
LAKINI ndugu zetu Waislam wanasema kuwa MSALABA NI ALAMA YA SHETANI, HEBU TUANZE NA QURAN 7:16 16. Akasema: Kwa kuwa umenihukumia upotofu, basi nitawavizia katika Njia yako Iliyo Nyooka.
SHETANI ANAMWAMBIA ALLAH KUWA, Kwa kuwa umenihukumia upotofu, BASI NITAWAVIZIA KATIKA NJIA YAKO ILIYO NYOOKA.
SHETANI AMEAPA KUWA ATAKETI KATIKA NJIA YA ALLAH ILIYO NYOOKA.
SASA HII NJIA YA ALLAH ILIYO NYOOKA AMBAYO SHETANI ameapa atakaa kwenye hiyo njia, ni ipi?
QURAN 6: 126. Na hii Dini ya Uislam, ndiyo Njia ya Mola wako Mlezi ILIYO NYOOKA. Tumezipambanua Aya kwa watu wanao kumbuka.
KUMBE SHETANI AMEKETI KWENYE NJIA ILIYO NYOOKA AMBAYO NI DINI YA UISLAMU, QURAN 7:16.
Kwasababu Shetani kaketi huko kwenye njia iliyo nyooka, ndio maana Shetani ana dini, au unabisha?
MUHAMMAD AMSILIMISHA SHETANI
Kitabu Asili ya Majini Ukurasa wa 20 INASEMA: Ni bahati mbaya kwamba Adam na Hawa hawakufanya jitihada za kumwezesha Shetani na wanawe kuomba Msamaha kwa Mwenyezi Mungu, NI MTUME MUHAMMAD TU NDIE ALIYE MSILIMISHA SHETANI AKAWA MUISLAMU.
Haya sio maajabu, maana tumesoma hapo kwenye Quran Surat Al Anaam kuwa Shetani anakaa kwenye NJIA ILIYO NYOOKA YA ALLAH. Na Njia iliyo nyooka ni UISLAMU Quran 6 aya ya 126 Na hii Dini ya Uislam, ndiyo Njia ya Mola wako Mlezi Iliyo nyooka. Tumezipambanua Aya kwa watu wanao kumbuka.
Ndugu zanguni, kwa mara nyingie tumejifuza kuwa Shetani ndie kiongozi wa dini ya Uislam. Shetani ndie yupo kwenye NJIA ILIYO NYOOKA NA AMEKETI HAPO. ZAIDI YA HAPO, SHETANI AMESILIMISHWA NA MUHAMMAD kama tulivyo soma katika Kitabu cha Asili ya Mini Ukurasa wa 20.
Huu ni Msiba Mwengine katika dini ya Allah ambayo sasa tumejifunza kuwa Shetani anakaa kwenye Njia Iliyo nyooka na alisilimu na kuwa Muislam.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 13, 2016

YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUUMBWA KWA VITU VYOTE DUNIANI NA MBINGUNI


Wakolosai 1:17 “Naye amekuwako kabla ya vitu vyote; na vitu vyote hushikamana katika yeye”.

Yesu Kristo alikuwako kabla ya Ibrahimu kuwako (Yohana 8:52-58).

Watu walioambiwa maneno hayo na Yesu mwenyewe waliokota mawe ili kumpiga Yesu wakisema kuwa anakufuru. Hawa ni watu wa tabia ya mwilini wanaotumia akili kupambanua mambo ya Mungu (mambo ya kiroho huwezi kuyatambua kwa akili maana Mungu ni Roho. (Yohana 4:24).Yohana 17:5,24.Waebrania 7:3.
Yesu ni Alfa na Omega, wakwanza nawa mwisho kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu yeye alikuwako (Ufunuo 22:13).

Shalom
Dr. Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu.

KUMBE JINA LA ALLAH HALINA MAMLAKA KAMA JINA LA YESU


1. KWANINI JINA LA ALLAH HALINA UWEZO WA KUPONYA MAGONJWA?
2. ALLAH ASHINDWA KUMPONYA MUHAMMAD
3. MAOMBI YA JIBRIL YAGONGA MWAMBA
4. LAKINI JINA LA YESU LINAPONYA MAGONJWA YOTE
5. JE, UMESHA WAI ONA KUNA MKUTANO WA UPONYAJI KATIKA USILAM?
Ndugu msomaji,
Uponyaji ni nini?
Ni tendo la kiimani la kupokea uzima katika roho au mwili kwa njia ya kuombewa,kuwekewa mikono au kulisikia neno sahihi la Kristo Yesu. Tendo hili la kiimani humletea mwamini uzima wa kiroho na afya ya kimwili pale ilipopunguka,kumbuka~wengi walipoponywa udhaifu wa miili yao,waliponywa pia na roho zao.
Hivyobasi, kwanini Allah alipo mtuma Jibril kwenda kumuombea uponyaji Mtume wake Muhammad kwa ugonjwa uliosababishwa na kula sumu, maombi yao hayakufanya kazi?
Hivyo basi, uponyaji haufanywi na mtu awaye yoyote yule isipokuwa Mungu. Hata madaktari bingwa wao hawaponyi bali hutoa tiba tu, mwenye kuponya ni Mungu. Watumishi wa Mungu pekee ndio hufanyika kama daraja au chombo cha kuleta uponyaji ulioachiliwa na Bwana kwa muhusika mwenye kuhitaji.
HEBU SASA TUMSOME ALLAH NA JIBRIL KATIKA JARIBIO LAO LA KUMPONYA MUHAMMAD:
Ibn Sa'd Ukurasa wa 265
Aisha, Mke wa Mtume Muhammad alikuwa akisema, "Wakati Nabii wa Allah alipo kuwa anaumwa, Jibril alikuwa anamwombea Muhammad kwa Allah kwa kusema haya "Katika Jina la Allah ambalo litakuponya kutoka kila magonjwa na maumivu na kutoka kila wenye ubaya nawe na kila wanakuombea ubaya, utapona..
Je, jina la Allah liliweza kumponya Muhammad? Hebu tusome Sahih hadith kama ilivyo letwa na Al Bukhari:
MAJIBU YA MUHAMMAD BAADA YA KUOMBEWA UPONYAJI NA ALLAH/JIBRIL:
Bukhari's Hadith 5.713:
Imesemwa na 'Aisha:
Mtume Muhammad wakati alipo kuwa anaumwa na kuchukuliwa na kifo alikuwa akisema, O Aisha, bado nasikia maumivu makali sana kutokana na chakula nilicho kula kilicho kuwa na Sumu kule Khaibar, na wakati huu nasikia kama nyongo yangu inakatwa kutokana na ile Sumu niliyo kula.
Hivi Mungu anaweza kuomba na ashindwe? Mbona Allah na Jibril maombi yao ya uponyaji kwa Muhammad hayakufanya kazi?
SASA TUMSOME YESU WA KWENYE BIBLIA, JE ALIWEZA KUPONYA WATU?
“ Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.” Mathayo 8:14-15
Biblia haituambii kwamba Bwana Yesu alimwombea huyu mama,bali tunachoweza kuona ni kwamba Bwana Yesu alimgusa mkono,homa ikamwacha. Mguso tu wa mtu wa Mungu ni dawa tosha,hata kama hakuomba sababu upako ungalimo ndani yake. Maana hata wakina Petro waliweza kuponya wagonjwa kwa kivuli chake tu,sababu ya upako. (Matendo 5:15)
UMUHIMU WA KUWEKA IMANI YAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO
“Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali , saa tisa. Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu. Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka. Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi. Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao. Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, simama uende. Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu. Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda …” (Matendo ya Mitume 3:1 – 8)
Ukifuatilia historia ya kilema huyu aliyeponywa utaona ya kuwa alikuwa hivyo tangu kuzaliwa, na alipopona alikuwa na umri uliopita miaka arobaini (Matendo ya Mitume 4:22).
Siri ya muujiza huu ilikuwa ni nini? Je! kilema huyu alipona kwa uweza wa Petro na Yohana au kwa uweza wa jina la Yesu Kristo?
Nauliza maswali haya kwa kuwa watu wengi wakimwona mtu anatumiwa na Mungu katika uponyaji wanaweka imani katika mtu huyo badala ya kuweka imani katika jina la Yesu Kristo.
Na ndivyo ilivyokuwa wakati kilema huyu alipopona, watu waliokuwa hekaluni waliwashangaa wakina Petro na Yohana kama vile kilema huyo alipona kwa uwezo wao. Petro alipoona hali hiyo, aliamua kuwaeleza watu hao ukweli ulivyo; alisema hivi;
“Basi (Yule aliyekuwa kilema) alipokuwa akiwashika Petro na Yohana, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana. Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kama kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi au kwa utauwa (utakatifu) wetu sisi?” (Matendo ya Mitume 3:11 – 12).
Petro alikuwa anafanya jambo muhimu hapa kwa kusaidia kubadilisha mawazo ya watu ya kufikiria kuwa uwezo uliomponya kilema ulikuwa ni wa Petro na Yohana ambayo haikuwa si kweli. Kama uwezo huu haukuwa wao, muujiza huu siri yake ni nini? Petro aliendelea kusema hivi;
“Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu ….. Na kwa IMANI KATIKA JINA LAKE, JINA LAKE LIMEMTIA NGUVU mtu huyu
mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele zenu ninyi nyote” (Matendo ya Mitume 3:13 – 16).
Hebu tafakari maneno haya ya Petro; “Na kwa IMANI KATIKA JINA LAKE JINA LAKE LIMEMTIA NGUVU MTU HUYU….” Wakina Petro na Yohana waliweka imani yao katika jina la Yesu Kristo. Walikuwa na uhakika mioyoni mwao kuwa siri ya miujiza imo katika jina la Yesu Kristo – ndiyo maana walipomkuta huyo kilema walimwamuru asimame kwa jina hilo!
Weka imani yako katika jina la Yesu Kristo ukitaka kuona ishara na miujiza ya Yesu Kristo maishani mwako na kwa wale unaowahudumia pia. Wakijua hili wanafunzi wa kwanza wa Yesu Kristo walipokatazwa “wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu” na Anasi kuhani mkuu, waliomba wakasema; “…Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ISHARA NA MAAJABU vifanyike kwa JINA LA MTUMISHI WAKO MTAKATIFU YESU” (Matendo ya Mitume 4:18,29 – 31)
Ni muhimu kuwaeleza na kuwakumbusha watu umuhimu wa kuweka imani zao katika jina la Yesu Kristo wakitaka kuona mkono wa Bwana ukiponya, ukifanya ishara na miujiza.
Ndugu msomaji, kwanini upoteze muda wako kwa waganga wa kienyeji au wapiga ndumba? Hebu liite Jina la Yesu aliye hai, maana anataka kukuponya magonjwa yako yote.
Kama unasumbuliwa na ugonjwa wowote ule, tafadhali wasiliana nasi kwa kupitia maxshimbaminsitries@gmail.com au tupigie simu (347) 770-4886. Haijalishi ni ugonjwa gani, wewe wasiliana nasi, na hakika Jina la Yesu litakuponya.
Max Shimba Ministries 2015

YESU NI MUNGU MUUMBAJI

Image may contain: text
Sifa ya kuumba niya Mungu peke-yake (Yohana 1:3,14) “vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika. Naye Neno alifanyika mwili; nasi tukauona utukufu wake kama utukufu wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli”.
Yesu anaitwa Neno la Mungu (Ufunuo 19:13) “Kwahiyo Neno ni Mungu “(Yohana 1:1).. na huyo ndiye aliyevifanya kuwako vitu vyote. Aliyeshuka kutoka juu na kufanyika mwili ni Yesu pekee aliyezaliwa na bikira Mariamu bila mbegu ya kiume kama inavyotokea kwa wanadamu wengine.
Katika yeye (Yesu) vitu vyote viliumbwa (Wakolosai 1:13-16) vinavyoonekana na visivyoonekana; vya Mbinguni na vya duniani.
Maandiko yako wazi kabisa, na kwa mtu mwenye Roho wa Mungu anaelewa kwa urahisi kuwa Yesu ni Mungu.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

UNAWAFAHAMU MALAIKA WAKUU SABA WA MUNGU "ARCHANGELS OF GOD? (SEHEMU YA NNE)



SELAPHIEL:

Maana ya Selaphiel ni "Maombi ya Mungu" au "mtu anaye omba kwa Mungu".


Hili jina linaweza pia kuandikwa kama Zerachiel, Selapheal, Salathiel, Selathiel, Sealteal, Seraphiel, Sarakiel, Sariel, Suriel, Suriyel, na Saraqael.


Malaika Mkuu "Archangel Selaphiel" anajulikana kama Malaika wa Maombi. Ni Malaika anaye wasaidia na au wahamasisha watu waombe kwa Mungu. Yaani yeye anakusaidia wewe kupunguza mawazo yako wakati unaomba ili uweze kuomba huku ukiwa unamwazia Muumba wako. [He helps people connect to God through prayer, giving them the focus they need to block out distractions and concentrate on praying].

Malaika Mkuu Selaphiel ametajwa katika Kitabu cha Ufunuo 8 aya ya 3 na 4: Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi. 4 Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika. Vile vile ametajwa kimajina katika kitabu cha Orthodox (3 Ezdras 5:16) na kwenye kitabu aya ya [31:6 cha the apocryphal Jewish and Christian text The Conflict of Adam and Eve].

Wakati wowote unapo jisikia kuomba kuhusu kitu Fulani, basi elewa kuwa Mungu anaweza kuwa ametuma ujumbe kwako kwa kupitia Malaika Mkuu Selaphiel, ambaye anapenda kuhamasisha watu ili waombe.

Zaburi 11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote. 12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

Somo hili la Malaika ingawa halifundishwi sana Kanisani, ni la muhimu sana maana hawa Malaika wanahusika sana na maisha yetu ya kila siku. Hebu angalia nini hutokea wakati mmoja wetu anapo okoka. Luka 15: 10 Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.


Najua wengi wenu mtasema wapi Yesu alitumia Malaika.

Mathayo 26: 52 Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga. 53 Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?

Umeona hapo. Hata Yesu anasema kuwa angeweza kumwambia Baba yake amtumie zaidi ya Majeshi kumi na wawili ya Malaika. Sasa, kama Yesu anaweza tumia Malaika katika vita hii, je wewe ulisha mwambia Baba aliye Mbinguni akutumie majeshi ya mailaka katika vita vyako? Kumbe ndio maana unakuta Mkristo anaomba kila siku lakini hapati jibu. Ni vyema kama Mkristo sasa uanze kujua jinsi Ufalme wa Mbinguni unavyo fanya kazi na tuachane na “church doctrines” mafundisho ya kikanisa ambayo yameshindwa kukusaidia tokea ulipo okoka.

Hata Shetani alimkumbusha Yesu kuwa angeweza kuomba Malaika waje kumwokoa, ingawa ilkuwa ni mtego.

Soma Mathayo 4: 5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, 6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

Wana wa Kiroho wa Mungu pia wanatofautiana katika ngazi na katika uwezo wa utendaji, (Ezekiel 1:9,11; Daniel 10:13; 12:1; Efeso 1:21; Kolosai 1:16; 1 Thesalonike 4:16; Yuda 1:9). Malaika wamepewa uwezo na nguvu ya utendaji (2 Thesalonike1:7); “wanaitwa wenye nguvu na uwezo mwingi” (Zaburi 103:20). Ni “Watakatifu” (Luka 9:26), ni “Wateule” (1 Timotheo 5:21). Hawasitahili kuabudiwa au kusujudiwa (Kol 2:18; Ufunuo 19:10).
Malaika wengine wana mabawa na wengine wanafanana kama sanamu wakiwa na sura za nyuso mbili, ambapo uso mwingine unaweza kuwa ni uso unaofanana na nyuso za wanyama na uso mwingine unaofanana na wanadamu. (Ezekiel 1:4-14; Isaya 6:1-3) wanaweza kubadilika katika maumbile yao na kufanana na maumbile ya kibinadamu wanapoonekana kwa wanadamu (Ebrania 13:2). Wakati wote wana miili ya kung’aa na wanavaa mavazi meupe (Matendo 1:9-11; 22:6-9; 2 Samuel 22:13).
Wanadamu hawaruhusiwi kumwona Mungu, kwa hiyo Malaika wanawasaidia wanadamu katika kumjua Mungu Mmoja wa kweli, (Eloah).

Je, unawafahamu Maseraphi na Makerubi na kazi zao? Usikose sehemu ya Tano kuhusu Malaika Mkuu Michaeli na kazi zake.

Shalom,



Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW