Saturday, May 20, 2017

ZANZIBAR: ATAKAYEKULA MCHANA WA RAMADHAN KUKIONA CHA MOTO

Image may contain: one or more people, shoes and outdoor

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) imetoa onyo kwa wananchi watakaokula hadharani katika kipindi cha mchana wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma, Khamis Juma Maalim wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua serikali inatoa tahadhari gani kwa watu watakaobainika kula mchana wakati wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.


Alisema utamaduni wa wananchi wa Zanzibar ni kuheshimu kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa makundi yote ikiwemo wa dini tofauti. Alifahamisha kwamba utamaduni huo upo hata kabla ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964 wa dini tofauti kuheshimu dini za watu wengine.


Alisema kazi ya kutoa elimu kuhusu ujio wa mwezi mtukufu wa Ramadhani imeanza kutolewa na Ofisi ya mufti ambayo ndiyo yenye jukumu la kushughulikia masuala ya mambo ya dini ya Kiislamu.


Alisema kazi kama hiyo imeanza kutolewa na maimamu wakuu wa misikiti mbalimbali Unguja na Pemba ikiwemo katika sala za Ijumaa ambazo hukusanya idadi kubwa ya Waislamu kwa wakati mmoja.


Alikiri kuwepo vijana wengi wanaoacha kufunga katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na kula hovyo pamoja na kuvuta sigara. Maalim alisema zipo taarifa kwamba hoteli nyingi hufanya kazi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo wateja wake wakubwa ni vijana wa Kiislamu. Waislamu nchini wanatazamiwa kuanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wiki ijayo ambapo ibada ya funga ni moja ya nguzo tano za dini ya Kiislamu

Friday, May 19, 2017

MUNGU ANAKUPIGANIA, MAADUI ZAKO WAMESHINDWA KWA JINA LA YESU

Image may contain: 1 person, text
Wana wa Israel waliteseka kwa miaka mingi katika nchi ya utumwani Misri. Walimlilia Mungu kwa muda mrefu, na wakati wa Bwana ulipofika Mungu akashuka na kuwaokoa.
Kutoka 3:7-9 
“BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.”
Baada ya Bwana kuwatoa misri bado farao aliwafuatilia, lakini muda wa Bwana kuokoa ukifika hakuna awezaye kuzuia. Bwana aliteketeza jeshi lote la wamisri baharini na kuwaokoa watoto wake.
Kutoka 14:13-15, 25
“Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele. Akayaondoa magurudumu ya magari yao, hata yakaenda kwa uzito; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa BWANA anawapigania, kinyume cha Wamisri.”
Bwana atakupigania kinyume na adui zako wawe ni magonjwa, kukataliwa, kukosa kazi, kukosa mtoto n.k. Simama katika imani ukauone wokovu wa Bwana.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

MUNGU NI KIMBILIO NA NGUVU YAKO WAKATI WA MATESO

Image may contain: one or more people, cloud, sky, text, outdoor and nature
Napenda nikutie moyo wewe mzazi ambaye unauguza mtoto au ndugu na hasa wale ambao watoto/ndugu wao wana magonjwa ya kuwafanya wateseke kwa muda mrefu. Hakuna kitu kigumu kama kumuona mtoto/ndugu wako anateseka nawe huna cha kufanya. Kuna watoto/ndugu wanateseka na kansa, vidonda vya kuungua, ajali, na magonjwa mengine mbalimbali. Wazazi hawa wanahitaji maombi yetu sana sana, kibinadamu wanaumia sana na kuchoka sana.
Mungu awatie nguvu, Mungu awakumbuke, Mungu awaponye watoto/ndugu wenu na pia Mungu awape nguvu na neema ya kukabiliana na jambo hilo. Mungu yupo upande wako usikate tamaa, endelea kusimama katika nafasi yako kama mzazi bila kukata tamaa, sisi tunakuombea. Ni njema na inapendeza ukiweza kumtembelea mzazi wa aina hii, mfariji na pia msaidie gharama za matibabu kadiri unavyoweza, hakika wanahitaji sana faraja na maombi na msaada pale inapobidi.
Zaburi 46:1-2, 11
“Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.”
Ezra 10:4
“Inuka; maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitende.”
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

UAMINIFU KATIKA NDOA

Image may contain: 3 people, people smiling, text
Uaminifu katika ndoa ni jambo la kila mmoja, sio la mke peke yake. Inashangaza sana kuona watu wakisema kuwa mwanaume hawezi kukaa bila kutoka nje sababu ndivyo walivyo. Kweli?? Hivi biblia kuna mahali inasema kuwa mwanaume ni kiumbe dhaifu? Nini tofauti kati ya mwanadamu na mnyama kama mwanadamu unasema ulishindwa kujizuia eti ni shetani. Yaani unakuta mwanaume katembea nje ya ndoa tena mara nyingine hadi kupata mtoto akiulizwa anajitetea mara ni shetani, mara nilipitiwa mara mke wangu ndio kasababisha sababu ya hili na lile.
Halafu utakuta analazimisha mkewe amsamehe na haoni kwa nini ashindwe kumsamehe na kila mtu anamshangaa mkewe kwanini amsamehi wakati wanaume ndivyo walivyo na hata kumlaumu mke kuwa ndio sababu. Wakati mke akitoka nje ya ndoa hakuna anayetaka kusikia sababu yoyote tena hao wanawake wanaomlaumu mume akitoka nje ya ndoa ndio wanakuwa wa kwanza kumlaumu na kila mtu anamwambia mume muache huyu mwanamke hakufai. Hivi watu wanapoapa kuwa waaminifu mume huapa kuwa nitakuwa muaminifu kama mke akifanya hili na lile? Hivi wanaume hamuoni kuwa mnajidhalilisha kusema kuwa ulishidwa kujizuia? Ina maana hauna tofauti na jogoo anayemkimbiza kuku na kumaliza haja zake pale anaposikia hamu? Mtu utafute namba ya simu, muwasiliane, mkubaliane, utoke ulipo hadi gest upange foleni reception, upande ghorofani chumbani, uvue nguo bado tu unajitetea hukudhamiria, kweli? Huyo shetani alikufunga kamba?
Usidhani mkeo hapati vishawishi, tena inawezekana vikubwa kukushinda lakini aliahidi uaminifu kutoka moyoni sababu anakupenda na kumheshimu Mungu. Hakuna sababu yoyote inayoweza ku justify mwanandoa kwenda nje ya ndoa. Kila mmoja aheshimu viapo vya ndoa na kumuogopa Mungu. Hii ndiyo silaha pekee ya ndoa.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

TABIA ZITAKAZOKIMBIZA WACHUMBA

Image may contain: 2 people, people smiling, text
Wasichana wengi wanalalamika mimi sijaolewa, akija mtu kunichumbia baada ya muda mfupi anakata mawasiliano, hakuna anayetaka kunichumbia n.k. Ni kweli kuna wakati na kusudi kwa kila jambo lakini pia mara nyingine matendo yetu yanaweza kusababisha kupata na kukosa vitu fulani. Kuna tabia ambazo hufukuza na kukimbiza wakaka wanapotaka au wanapokuchumbia. Angalia kama unazo ufanye jitihada la sivyo unaweza mlaumu Mungu bure:
1. Mizaha mingi
Kuna mtu alisema ukipewa karama ya kuongea omba Mungu akupe na hekima, ni kweli kabisa. Haipendezi mtu kuwa unaongea hadi unapililiza na kuwafanya watu kujisikia vibaya. Maongezi yaliyojaa mizaha ya kupililiza kweli utamkimbiza potential husband. Kuwa na staha kwenye maongezi yako.
2. Kupenda kukosoa hadharani
Watu wanaokuzunguka wanakujua vizuri, ukiwa mtu wa kuwakosoa wengine hadharani hakika utaogopwa. Mtu anaongea katika lundo la watu akakosea kidogo wewe unamkosoa mbele za watu hiyo haifai, au mtu kavaa kakosea kupangilia wewe unamkosoa mbele za watu.
3. Kushurutisha
Ndio kwanza mmeanza mahusiano wewe unataka kujua tarehe ya harusi, unampangia marafiki zake na mahali pa kwenda, unapanga hadi makochi ya sebuleni kwenu yatakuwaje. Yani wewe ndiyo unakuwa na ratiba yake, usiende huku, nenda kule, njoo hapa, haaaa huyo atakuvumilia kwa muda tu. Akimpata kwenye kumheshimu hapo utaona anakata mawasiliano taratibu maana hakuna mwanaume anayetaka kushurutishwa.
4. Kuomba hela mara kwa mara
Leo hela ya saluni, kesho mtaji umekata, mara ada ya mdogo wako hajakaa sawa mama anaumwa dah.. sikatai kusaidiana ila usiwe ndio kila siku unataka kusaidiwa tena fedha. Unambeep akipiga unamwambia akutumie salio au Mpesa akituma unabeep tena akipiga unamwambia asante nimepata. Nakwambia hata kama anakupenda vipi ataazimia kukuacha kwa siri kama Yusufu.
Jichunguze na uchukue hatua, usije kumlaumu shetani kwa kosa lako mwenyewe..
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

MUME KUMPENDA MKE NI AGIZO

Waefeso 5:25, 28-29
“Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa”
Mume kumpenda mke ni agizo. Agizo hili halibadiliki mke akiwa mkorofi, sio mtii au vyovyote vile. Biblia inamuagiza mume ampende mke kama kristo alivyolipenda kanisa. Huu ni upendo mkubwa sana, japokuwa kanisa lilikengeuka mbali naye bado upendo wa Kristo haukubadilika. Kumpenda mwanamke kama mwili wako mwenyewe, kumjali na kumtunza.
Ni rahisi sana kwa mwanamke kuonyesha utii pale anapoonyeshwa upendo. Wanaume wengi huonyesha upendo wakiwa wanachumbia ila wakishaoa tu wanajisahau na kusahau kama mke anahitaji upendo ili aweze kutimiliza majukumu yake kama mke vizuri kwa furaha. Upendo unaanzia kumjali hisia zake, kumtunza kimahitaji na kumtia moyo, kumsifia na kumuonyesha unamthamini.
Mwanamke anahitaji kujua unampenda kwa wewe kumweleza hivyo kuwa unampenda na kumtendea matendo ya upendo. Wanawake wengi hukosa hamu ya faragha na waume zao kwasababu huona kama wanapendwa kwa ajili hiyo tu. Mume siku nzima anamkaripia mkewe, hamsikilizi wala kumjali na usiku anaonyesha kuwa anamhitaji saana, huo sio upendo ambao mke anahitaji toka kwa mume wake.
Mume anapoonyesha kumsikikiza na kujali ushauri wa mkewe na kushauriana naye kabla hajafanya jambo lolote mke anaona anapendwa sana na yeye atazidisha upendo na heshima kwa mumewe. Mpende mkeo ili aweze kukuheshimu kwa furaha na sio kwa kujilazimisha. Kumpenda mke ni kujipenda mwenyewe. Mara moja moja mtoe out bila watoto na umueleze unavyompenda, zawadi sio lazima siku ya sherehe au kitu kikubwa, hata chocolate(unanunua kwa ajili yake na sio watoto), mke atahisi kupendwa sana.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Thursday, May 18, 2017

PANDA KWA MACHOZI UTAVUNA KWA FURAHA

Image may contain: one or more people, text and outdoor
Zaburi 126:5-6
“Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”
Kupanda siku zote ni kazi ngumu. Kwanza ni lazima uamke asubuhi na mapema, ubebe mbegu na jembe, utembee kwenye baridi kuelekea shamba ambalo limejaa matope maana watu hawapandi wakati wa kiangazi, uiname shambani siku nzima au siku kadhaa ukipanda mbegu zako. Sio zoezi la kufurahia au kuchekelea lakini ni la muhimu sana kama unataka kuvuna.
Siku ya kuvuna ni siku ya furaha, siku ya kuhesabu utajiri, siku ya kuhesabu matunda ya jasho, siku ambayo taabu ya kupanda inazaa matunda, pamoja na kwamba utachoka lakini unakuwa umejaa furaha maana sasa mavuno umeyapata. Lakini huwezi kuvuna bila kupanda, lazima upande ili utazamie kuvuna. Usione wengine wanapanda ukavuta shuka halafu ukasubiri nawe ukavune.
Leo nakutia moyo wewe uliye kwenye hatua ya kupanda, Usikate tamaa jua ipo siku utavuna kwa kelele za furaha. Unaweza kuwa unapanda kwenye elimu, biashara, ujasiriamali, ufugaji kazini kwako, uwekezaji, ujenzi, huduma n.k. wewe endelea kupanda kwa bidii, panda mbegu nyingi kadiri uwezavyo wala usiwe mvivu. Mbegu siku zote ni chache na mavuno ni mara 100, hivyo panda, panda, panda. Na wewe unayesubiri kuvuna wakati hutaki kupanda kwa machozi tambua kuwa hakuna kuvuna bila kupanda. Ukitaka siku ya mavuno nawe ushangilie chukua mbegu shika njia nenda shambani ukapande.
Mbarikiwe.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

MUNGU HATAKUACHA, USIKATE TAMAA

Image may contain: cloud, sky, mountain, text, outdoor and nature
Unapopitia magumu na mambo ya kukatisha tamaa wakati mwingine unaona kama Mungu amekuacha. Yesu alipokuwa msalabani alipitia hali hiyo, na Ayubu katika majaribu magumu alipitia pia hali ya kukata tamaa na kuona kuwa Mungu amemuacha.
Mathayo 27:46
“Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Ayubu 13:24
“Mbona umeuficha uso wako, Na kunihesabu kuwa ni adui yako?”
Maumivu makubwa ya moyo lazima yataleta simanzi na kukata tamaa. Lakini hatupaswi kwenda huku na kule kuuliza kwa watu kwanini tunapitia hayo bali tumwendee Mungu, muulize yeye maswali yote na hakika atakuonyesha ni kwanini ameruhusu upitie hayo. Baada ya majaribu magumu Mungu alimuinua Yesu na kumfanya juu ya vyote, na baada ya Ayubu kushinda Mungu alimzidishia mara dufu ya yale aliyoyapoteza.
Unapokuwa huelewi, usitafute jibu kwa wanadamu bali kwa Mungu na ameahidi hatakuacha wala kukupungukia.
Ebrania 13:5b
“kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.”
USIKATE TAMAA, MUNGU HATAKUACHA.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Wednesday, May 17, 2017

Imam hated Christians until Jesus raised him from the dead

Imam leads Friday prayers at Faisal mosque
He not only hated Christians, he directed his followers at the mosque to attack them. But after he died and was being prepared for burial, he stunned his family by returning to life with a new message of salvation.
Munaf Ali*, 45, was an influential imam as well as scholar and preacher of Islam in a Middle Eastern country.
One day a team from Bibles4Mideast approached the imam and they entered into a vigorous discussion about the authority of Jesus and the Bible. Munaf denied the divinity of Jesus Christ and the credibility of the Bible.
Pastor Paul offered him a copy of the New Testament but he refused to receive it. Visibly upset, the imam cursed the pastor and his team.
That night the imam incited a mob to attack the place where Pastor Paul and his team had been staying with shouts of “Allahu Akbar.”
But the Holy Spirit directed them to leave that location a few hours earlier, narrowly escaping the attackers before they arrived, according to Bibles4Mideast.
A few days later, following Friday prayers, Munaf was returning home when he suddenly felt dizzy, fell to the ground, lost consciousness and died.
After his physical body expired, he was aware of demons coming for his soul.
“Get lost, you cursed demons of Allah. You have no right to take my soul!” the imam asserted.
“No. It’s our right to take your life,” one of the demons replied. “And you will be with us,” as he forcefully grabbed the imam and began to depart.
But suddenly, Jesus Christ appeared before the imam with a large retinue of angels and the demons quickly fled in terror.
Then Jesus spoke to his heart: Listen, my son. First Adam disobeyed God and sinned against Him under Satan’s influence.
I am the second Adam, the Word of God and the Messiah Jesus, Son of the Most High. I was born of the virgin Mary, as a sinless Son of Man to redeem Adam and all of his descendants including you from sin and death.
 I was crucified and died as a ransom for all your sins to make you a child of God and citizen of heaven.
 I was raised from the dead and opened the gates of heaven to bring you back to eternal glory. Have faith in me and be my witness. I give your life back, for I have the authority of giving life.
When Munaf’s soul returned to his body, his sons and other family members were trying to lay his body on a table for washing and preparation for burial. Many other people were also in the room.
His family and friends were astonished and some began to shriek when Munaf opened his eyes and sat up on the washing table. Many were frightened and backed away, as if they saw a ghost.
“I was dead and demons tried to take my soul but Messiah Jesus came and gave my life back,” he began haltingly, and then proceeded to describe his experience.
Some believed his report, but others refused to believe and began to ridicule him. One said Munaf must have hit his head and lost his senses. “He speaks meaningless words,” a man said.
“He is possessed by an evil spirit,” someone charged.
Munaf became a bold witness for Jesus Christ, telling his family and anyone who visited him about his remarkable experience. His immediate family believed what he said about Jesus and accepted Him as their Savior and Lord.
As a result of his witness, he was dismissed from the mosque and told to see a psychiatrist. The community began to persecute them.
A short time later, facing serious threats, Munaf and his family left their home and their native country.
Pastor Paul asks for prayers for Munaf and his family, that God would protect them and provide for them as they minister in the region.
*name changed for security reasons
If you want to know more about following Jesus, go here

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU SOMO LA 7

Image may contain: food
MATUNDA YA ROHO MTAKATIFU NI YAPI?
Matunda ya Roho Mtakatifu ni matokeo ya kuwepo kwa Roho Mtakatifu katika maisha ya Mkristo. Biblia inaeleza wazi kwamba kila mtu hupokea Roho Mtakatifu wakati yeye anaamini katika Yesu Kristo (Warumi 8:9, 1 Wakorintho 12:13; Waefeso 1:13-14).
Wagalatia 5:22-23 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi juu ya mambo hayo hakuna sharia.” Matunda ya Roho Mtakatifu ni matokeo ya kuwepo kwa Roho Mtakatifu katika maisha ya Mkristo.
UPENDO:
Kwa nini upendo ni wa kwanza na sehemu muhimu ya tunda la Roho Mtakatifu?
Upendo wa Mungu hubadili Maisha yetu. Tunabadilishwa tunapoelewa upendo wake. Tuna kuwa na uwezo wa kupenda mara tunapopokea upendo wake. Mungu mwenye upendo hutuandaa kuwapenda wengine, hata adui zetu.
Vipengele vingine vya tunda la Roho Mtakatifu sharti vizingirwe na upendo wa Mungu ili vilete mantiki.
FURAHA:
Je; ni nini sababu ya furaha aletayo Roho?
Kuuelewa na kuukubali upendo wa Mungu kwetu, Kafara yake, Rehema yake, Msamaha wake, Ahadi na baraka zake. Hicho huleta furaha idumuyo, haidhuru hali zetu.
Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.” (Warumi 14:17)
AMANI:
Je; Amani aletayo Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa namna gani?
Amani hiyo ni matokeo ya kuwekwa huru dhidi ya dhambi zetu kwa imani katika Yesu kristo.
Amani hiyo hutufanya tuwe wenye amani na kutusukuma Zaidi kuwa na amani na kila mtu (Warumi 12:18).
“Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.” (Warumi 5:1)
UVUMILIVU:
Je; uvumilivu pamoja ukiwa na tunda la Roho mtakatifu hutofautianaje na uvumilivu bila tunda la Roho Mtakatifu?
“Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.” (14:12)
WEMA:
Je; tunawezaje kuuonja wema wa Bwana?
Neno wema limetumika mara 10 katika Biblia. Mara 8 kati ya hizo huzungumza namna mungu anavyotutendea (2 Samuel 22:36; Zaburi 18:35; War. 2:4; War. 11:22; Efeso 2:7; Kolosai 3:12; Tito 3:4; 1P. 2:3) na mara zingine 2 huzungumza kuhusu tunda la Roho ndani yetu (2 Korintho 6:6; Wagalatia 5:22).
Namna njema ambayo kwayo Roho hutuongoza kuwatendea wengine huakisi namna ambavyo Mungu ametutendea sisi kwa kuonesha wema wake.
“ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.” (1 Petro 2:3)
FADHILI:
Je; unawezaje kueleza maana ya fadhili?
Fadhili ni upendo katika vitendo.
Tunaonyesha fadhili tunapopenda tunafanya kazi kwa faida ya wengine. Fadhili ni “kufanya kilicho sahihi, liwalo na liwe.”
Hii ni sehemu ya vitendo ya tunda la Roho.
“Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.” (Luka 6:35)
UAMINIFU:
Kwa nini uaminifu ni muhimu katika Maisha ya ukristo?
Mungu ni mwaminifu kwa asili. Hawezi kuvunja ahadi zake (2 Timotheo 2:13).
Yesu ni “shahidi aliye mwaminifu” (Ufunuo 1:5). Tunaakisi tabia ya Yesu kama tukiwa waaminifu kwa agano letu na Mungu na waaminifu katika mahusiano yetu na wengine kwa kazi ya Roho.
Mkristo wa kweli daima ni mwaminifu.
“Umtumaini Bwana ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.” (Zaburi 37:3)
UPOLE:
Je; Kuna tofauti gani kati ya upole na uoga au soni?
Muoga au mwenye aibu aweza kuonekana kama mpole, lakini anaweza kuwa mwenye kujivuna au jeuri.
Kiburi si sehemu ya upole. Yesu alituambia: “mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo” (Mathayo 11:29).
Kuiamini nguvu ya Roho wa Mungu ambayo hutenda kazi ndani yetu hutufanya tuwe wapole, wanyenyekevu na wavumilivu.
KUWA NA KIASI:
Je; ni katika maeneo gani ya Maisha napaswa kuboresha kiwango changu cha kiasi?
Kiasi ni kuwa na uwezo kamilifu wa kujizuia dhidi ya mambo mabaya na kutumia mambo mazuri kwa uzania sahihi.
Kiasi huhusisha si tu vyakula na vinywaji. Lazima iguse kila Nyanja ya Maisha yetu.
Hilo ni tunda la Roho. Kwa nguvu zake, tunaweza kulionyesha tunda lake kila mahali, katika kila nyanja ya Maisha yetu : upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, kiasi.
“Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.” (Mithali 16:32)
Maisha ya Kikristo ni vita vya mwili ulio wa dhambi dhidi ya asili mpya iliotolewa na Kristo (2 Wakorintho 5:17). Kama binadamu viumbe tulioanguka, sisi bado tumenazwa katika mwili wa dhambi na kwamba tunathami mambo ya dhambi (Warumi 7:14-25). Kama Wakristo, tuna Roho Mtakatifu kuzalisha matunda yake ndani yetu na nguvu za Roho Mtakatifu zinapatikana kwa kushinda matendo ya mwili (2 Wakorintho 5:17; Wafilipi 4:13).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Jesus is God and gives eternal life

 

TRENDING NOW