Thursday, April 12, 2018

Neymar’s ‘100% Jesus’ motto was censored in the Ballon d’Or gala

neymar, erased, edited video, fifa, 2016, ballon d

FIFA, the highest institution in the world of football, censored a reference to Jesus by Ballon d’Or candidate Neymar. Neymar was one of the three finalists of the Ballon d’Or ceremony held in Zürich (Switzerland) on January 11, 2016. 

Lionel Messi (also a FC Barcelona player) won the award, the fifth of his career. A video summarising the successful year of the Brazilian FC Barcelona player was played during the gala. Images of the Champions League final celebration were included in it. 

The Spanish team won the match against Juventus (1-3) and Neymar celebrated the trophy wearing a headband with an inscription reading “100% Jesus”. But in the FIFA video, the reference to Neymar’s Christian beliefs disappeared.
See more: http://evangelicalfocus.com/lifetech/1288/Neymars_100_Jesus_was_censored_in_Ballon_dOr_gala

JINSI YA KUFUFUA WAFU KIBIBLIA

Image result for raising the dead
Mathayo 9:24 23 “Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo, akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.”

Mungu wetu ni Mungu wa kurudisha na anaweza kumrudisha mtu aliyetoka nje ya mwili wake. Rudisha vyote na ufufue vitu vyako vilivyokufa kwa jina la Yesu, Amen

Tena imeandikwa katika Yohana 5:25….(Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.). Hili ni agizo alilotoa Bwana Yesu, ya kuwa wafu wataisikia sauti ya Bwana na kufufuka. Kumbe hata wafu wanaweza kuisikia sauti ya Yesu na baada ya hapo wakafufuka.

Sasa tunagalie UTHIBITISHO kadhaa kutoka Biblia.

1. ELIYA ALIMFUFUA MTU
1 Wafalme 17: 21 “Akajinyosha juu ya mtoto mara tatu, akamwomba Bwana, akanena, Ee Bwana, Mungu wangu, nakusihi, roho ya mtoto huyu imrudie ndani yake tena. Bwana akaisikia sauti ya Eliya; na roho ya mtoto ikamrudia, akafufuka.”

3. ELISHA ALIMFUFUA MTU.
2 Wafalme 8:5 “Ikawa, alipokuwa katika kumwambia mfalme jinsi alivyomfufua mtu aliyekufa, tazama, huyo mwanamke aliyemfufulia mwanawe, alimlilia mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, Bwana wangu mfalme, huyu ndiye mwanamke, na huyu ndiye mwanawe, ambaye Elisha alimfufua “

4. MIFUPA YA ELISHA ILIMFUFUA MTU.
1 Wafalme 13: 20 “Elisha akafa, nao wakamzika. Basi vikosi vya Wamoabi wakaingia katika nchi mwanzo wa mwaka. Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu.”

5. YESU ALIMFUFUA BINTI YAIRO
Marko 5: 22 “Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake, akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi. Hata alipokuwa katika kunena, wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema, Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu? Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu. Wala hakumruhusu mtu afuatane naye, ila Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye Yakobo. Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu. Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu. Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana. Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka. Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu.”

6. YESU ALIMFUFUA KIJANA KWENYE LANGO LA NAIM, KIJANA ALIKUWA NDANI YA GENEZA.

Luka 7: 12 “Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye. Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie. Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka. Yule maiti akainuka, akaketi, akaanza kusema. Akampa mama yake.”

7. YESU ALIMFUFUA LAZARO. AMBAYE ALIKAA KABURINI SIKU NNE ALIKUWA AMEKUFA AKAZIKWA AKAANZA KUOZA.

Yohana 11: 25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo? Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni. Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake; akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akisema, Mwalimu yupo anakuita. Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea. Na Yesu alikuwa hajafika ndani ya kijiji; lakini alikuwa akalipo pale pale alipomlaki Martha. Basi wale Wayahudi waliokuwapo na Mariamu nyumbani, wakimfariji, walipomwona jinsi alivyoondoka upesi na kutoka, walimfuata; huku wakidhania ya kuwa anakwenda kaburini ili alie huko. Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake, akasema, Mmemweka wapi? Wakamwambia, Bwana, njoo utazame. Yesu akalia machozi. Basi Wayahudi wakasema, Angalieni jinsi alivyompenda. Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife? Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake. Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma. Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.”

8. PETRO ALIMFUFUA MWANAMKE MJANE DORKASI ALIFUFULIWA NA PETRO ALIYEMKANA YESU MARA TATU.
Matendo ya Mitume 9: 40 “Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi. Akampa mkono, akamwinua; hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai. “

9. PAULO ALIMFUFUA EUTIKU ALIYEDONDOKA GHOROFANI AKIWA ANASINZIA PAULO AKIWA ANAHUBIRI, ALIDONDOKA MPAKA CHINI. (Alikufa kwa ajali akafufuliwa.)

Matendo ya Mitume 20:9 “Kijana mmoja, jina lake Eutiko, alikuwa ameketi dirishani, akalemewa na usingizi sana; hata Paulo alipoendelea sana kuhubiri, akazidiwa na usingizi wake akaanguka toka orofa ya tatu; akainuliwa amekwisha kufa. 10 Paulo akashuka, akamwangukia, akamkumbatia, akasema, Msifanye ghasia, maana uzima wake ungalimo ndani yake. Akapanda juu tena, akamega mkate, akala, akazidi kuongea nao hata alfajiri, ndipo akaenda zake. Wakamleta yule kijana, yu mzima, wakafarijika faraja kubwa sana.”

10. YESU ALIPOKUFA MIILI MINGI ILITOKA MAKABURINI. WATU WENGI WANASEMEMA ZILIKUWA ROHO LAKINI BIBLIA INASEMA NI MIILI MINGI ILIFUFUKA.

Mathayo 27:51 “Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.”

11. YESU ALIFUFUKA KUTOKA KWA WAFU.
Marko 16:6 “Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulibiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka.”

Yohana 21:14 “Hiyo ndiyo mara ya tatu ya Yesu kuonekana na wanafunzi wake baada ya kufufuka katika wafu.”

1 Wakorintho 15:15 “Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.”

1 Wakorintho 15:16 “Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.”

Shalom

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

YESU ALIDHIHIRISHWA KWA MIUJIZA NA AJABU NA ISHARA

Tuanze kusoma aya:
Matendo 2: 22 Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;
Siku hizi kume kuwa na tabia ya watumishi kui\pinga hili andiko. Neno linatukumbusha kuwa, Yesu Kristo alidhihirishwa kwa miujiza, na ajabu na ishara. Je, kuna miujiza na ajabu na ishara kwenye Kanisa lako?
Mpendwa, kama Kanisani kwako hakuna hii miujiza na ishara na ajabu, basi elewa kuna tatizo hapo.
Bwana Yesu kabla ya kuondoka alituambia hivi:
Marko 16: 17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
19 Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu.
Je, mnatoa pepo Kanisani kwenu? Mnazungumza kwa lugha mpya? Naam, bado tuna mwendo mrefu sana, lakini, ukweli unabakia pale pale.
Sasa kama hakuna hii miujiza Kanisani kwenu, je, nyie mna tofauti gani na waislam na wapagani nk?
Mathayo 10: 7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu”
Leo hii watu wanataka waaminiwe kwa maneno matupu bila kufanya matendo. Huwezi kufanya matendo ya Baba yako kama humwamini Baba yako. Yesu alipooza wagonjwa akaturuhusu sisi tukimwamini tunaweza kutenda kama yeye alivyotenda na zaidi ya yale aliyoyafanya.
Waefeso 3:20 “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu”
Kuna nguvu itendayo kazi ndani yetu. Unapompokea Roho Mtakatifu nguvu inaingia ndani yako ambayo hauombi ili uwe nayo sababu tayari ipo ndani yako.
Yesu alifufua wafu, alipooza wagonjwa, alitakasa wenye ukoma, alitoa pepo na sisi tumwaminiye tunafanya kama yeye alivyofanya halafu alisema tutafanya zaidi yake kama tukimwamini.
Shalom
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

Image result for miujiza na ajabu

Saudi firm sacks 1,300 staff after closure of Quran printing press

Related image
At least 1,300 staff were laid off by the Saudi Oger conglomerate this week, after it lost a contract to run what is thought to be the largest Quran printing press in the world.
The once-mighty firm led by Lebanon's billionaire former prime minister Saad Hariri has been hit by a drop in income from its core construction business after the Saudi government delayed or cancelled projects in the face of plummeting oil revenues.
In a letter reportedly sent to all employees on Tuesday but dated 22 September, the firm announced the end of a contract with the Saudi government to run the King Fahad Quran Printing Complex.
The letter, which was shared online, appeared to announce that as a result all employee contracts would be terminated as of 3 September, weeks before the letter was issued.
Thousands of the company’s foreign workers were due to leave the country while still owed several months’ worth of wages this week, sources told news site Arabian Business.
Saudi Oger, whose core business is in the construction industry, currently employs some 6,500 Pakistani nationals.
The Saudi government is organising flights to send the redundant workers from Oger’s printing complex back to Pakistan, with the first group of around 450 reportedly flying back on Wednesday.
More than 30,000 Saudi Oger Ltd construction workers, mostly from India, Pakistan and the Philippines, have gone unpaid for up to nine months, with frequent strikes over salaries.
Local news site the Saudi Gazette said the printing plant staff had also gone months without pay or allowances.
Last month, King Salman announced a $27 million assistance plan for unpaid construction workers in the kingdom, which is highly dependent on migrant labour.
The package helps them with food, medical needs, a trip home, exit visas or, if they want, transfer to another employer in Saudi Arabia.
Other construction companies that are dependent on state contracts have also suffered because of delayed government receipts.
But sources told AFP that the broader economic context is compounded at Saudi Oger by deeper problems including poor management.
The Saudi Gazette said the government has begun the tendering process to find a new operator for the Qur’an printing complex.

Source: Middle East Net

Tuesday, April 10, 2018

ETI, YESU ALIPOKUWA AMEKUFA DUNIA ILIKUWA INAENDESHWA NA NANI?

Image may contain: fire, text and food
Hili ndilo swali la wafuasi wa Muhammad kwa Wakristo na leo nitalijibu hapa.
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO, YAANI YESU KRISTO MUNGU MKUU. TITO 2:13!
Kwanza: Hili swali ni jibu tosha kuwa Allah anaye abudiwa na Waislam sio Mwenyezi Mungu na hana uwezo wa Kimungu. Kabla sijaweka jibu, ngoja nianze na swali kwa Waislamu: HIVI ALLAH ANAENDESHAJE DUNIA WAKATI HAJAWAI FIKA HAPA DUNIANI?
Sifa moja ya Mungu ambayo haipo kwa Allah ni ya kuwa kila mahali kwa wakati mmoja. Hii sifa ya kuwa kila mahali "omnipresent" ni ya Mungu peke yake. Je Yesu alipokufa aliwezaje kuendesha dunia kama wanavyo uliza hawa Waislam wanao mwabudu Allah asiye na uwezo wa kuwa kila mahali?
Yesu anaanza kukujibu kwa kupitia Injili ya Mathayo kama ifuatavyo:
Mathayo 18:20, Inasema: 20 Kwa maana wanapokutana watu wawili au watatu katika jina langu, hapo mimi nipo pamoja nao.”
Sifa ya kuwa kila mahali kwa wakati mmoja ni ya Mungu pekee, lakini Yesu anasema yeye hiyo sifa ni yake na anayo. Umesoma mwenye kwenye Mathayo hapo juu kuwa watu wawili au watatu wakikutana kwa jina lake yeye yupo, Haijalishi mpo nchi gani, yeye yupo. Mkitutana Johannesburg na wengine Capetown na wengine Texas yeye yupo. Hii ndio raha ya Yesu ambaye ni Mungu.
Tuendelee kumsoma Yesu kupitia Zaburi Mlango wa 139
aya 7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? 8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. 9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; 10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.
Tunamsoma Mfalme Daudi hapo juu akikiri kuwa, Mungu yupo kila mahali na huwezi kujificha kutoka kwake. Jambo la kutia aibu, Muislam anauliza, eti Yesu alipo kuwa amekufa nani alikuwa anaongoza dunia? Hivi kweli mtu mwenye akili anawezaje kuuliza swali la kitoto na la kidunia namna hii? Hivi unawezaje kulinganisha uwezo wa Mungu na binadamu ambaye ni dhaifu? Ndio maana huwa nasema Allah hawezi kuwa Mwenyezi Mungu hata mara moja, maana wafuasi wake hawana uelewo wa KIMUNGU kuwa Mungu yupo kila mahali?
SASA nawauliza Waislam: HIVI ALLAH ANAENDESHAJE DUNIA WAKATI HAJAWAI FIKA HAPA DUNIANI? Nijibuni kwa aya na sio matusi.
Leo nimeweka kwa kifupi tu kuwa Yesu yupo kila mahali, haijali wewe upo wapi au nchi gani, ukimwita anaitika na kuja kukusaidia. Ili kumfahamu Yesu zaidi soma kijarida cha http://www.maxshimbaministries.com/…/asilia-mbili-ya-yesu-k… kwa msaada zaidi. Yesu si nabii tu kama ambavyo Waislam nadai, bali ni zaidi ya hapo, maana yeye ni Mungu http://www.maxshimbaministries.com/…/uthibitisho-10-kuwa-ye…
Yesu alipo kuwa amekufa au alipo kuwa nje ya mwili wa kibinadamu bado alikuwa Mungu maana Mungu ni Roho na hafi. Kilicho kufa ni mwili na sio Roho ambaye bado ilikuwa inafanya kazi. Ndio maana Yesu alisema mnapo kuwa wawili au watatu katika jina lake yeye yupo.
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua!
Katika huduma yake Max Shimba Ministries Org.

JE, MKRISTO ANAWEZA KUINGIWA NA PEPO?


Muumini wa Yesu Kristo, ambaye amezaliwa mara ya pili na kuokoka anaweza kuingiwa na pepo?

Tuanze kwa kusoma aya hii:

Mathayo 16: 23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.

Hili ni somo gumu sana, lakini linaweza kuw rahisi sana kama tukifuata aya za Biblia na kutoa "Doctrines" za kanisa.

Petro ambaye alikuwa anatembea na Yesu, aliwezaje kuingiwa na SHETANI?

Zaidi ya hapo, Shetani aliwezaje kukaa ndani ya Petro aliye kuwa kwenye huduma ya Yesu?

Ndugu zanguni, pepo anaweza kuiingia na kuharibu maisha yako. Wakristo huwa wana sema hivi: Wakristo wanaitwa watoto wa Mungu na Roho Mtakatifu yuko ndani mwa kila muumini. Mapepo hayawezi kuingia sehemu ambayo kuna Mungu na Roho Mtakatifu kwa sababu Mungu ni Mkuu kuliko roho zote chafu kwa kuwa ndiye Muumbaji wa vyote wakiwemo malaika.

Hayo naweza kuyaita madai na sio facts:
1. Kama kweli Uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yako hauwezi ruhusu pepo, kuingia ndani yako, IWEJE, wewe huyo huyo unaweza umwa? Je, hapa Roho Mtakatifu ameshindwa kazi au amepungua nguvu?

2. Dai la pili tunasema, pepo hawezi kuingi au kaa sehemu alipo Roho Mtakatifu, Je, IWEJE, basi Petro aingiwe na pepo, huku akiwa na Yesu wakati wote?

Yesu anatoa onyo juu ya roho wachafu katika Mathayo 12:43-45 anaposema, Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kibaya.

Shetani ameshika pabaya sana Wakristo kwa kuwaaminisha kuwa, eti hawawezi kupagawa na pepo au ingiwa na pepo.

Swali la kujiuliza, ni wapi, pepo anakaa ndani ya Mwili?

Hebu tumsome Mtume Paulo katika Warumi 7: 15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.
16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema.
17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.
19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo.
20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.

Mtume Paulo anatufamisha katika aya ya 17, kuwa DHAMBI INAKAA NDANI YANGU, sasa tujiulize, KIVIPI dhambi ikae ndani ya Nabii Paulo huki akiwa na Roho Mtakatifu ndani yake kwa wakati huohuo?

Aya ya 18, inasema ndani yako halikai neno jema, sasa, Roho Mtakatifu anakaa wapi?

Hata wewe unayo soma mada hii na kukataa, kivipi utende dhambi huku ukiwa umejazwa na Roho Mtakatifu?

Nafsi na roho ni sehemu mbili muimu za mwili wa ndani ambazo Bibilia yaamini ni tabia kamili za mwanadamu. Inaweza tatanisha kujaribu kutambua kabisa tofauti ilioko kati ya hayo mambo mawili. Neno “roho” laashiria mwili wa ndani pekee wa mwanadamu.

Wanadamu wako na roho, nafsi na mwili. “… nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.” 1 Wathesalonike 5:23

Ingawa katika maandiko ni waumini wanatambulika kuwa hai kiroho (1 Wakorintho 2:11; Waebrania 4:12; Yakobo 2:26), bali wasio amini wamekufa kiroho ( Waefeso 2:1-5; Wakolosai 2:13). Paulo katika uandishi wake, roho ni kitu cha maana katika maisha ya Mkristo (1 Wakorintho 2:14; 3:1; Waefeso 1:3; 5:19; Wakolosai 1:9; 3:16). Roho ni kitu katika maisha ya mwanadamu ambacho kinampa uwezo wa kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu. Popote neno “roho” limetumika, linaashiria sehemu ya ndani ya mwanadamu ambayo “yakutanika” na Mungu, ambaye Yeya mwenyewe ni Roho (Yohana 4:24).

ROHO NA NAFSI:
Hivi viwili hushindana kila kimoja. Kwa maana kila kimoja chaweza kuwa mkuu wa mwili. (Kwa maana mwamini aweza akaongozwa kwa roho akawa rohoni au akaongozwa na nafsi yake akawa mwilini). Hivyo huu ni uhusiano wa ndani. Dhambi ndio adui wa roho ya mwamini kufanya kazi ya Mungu katika utimilifu, hivyo roho ya mtu isipookoka haiwezi kutenda mambo ya Mungu/kumlingana Mungu bali nafsi ataitawala kuamuru mwili ufuate matendo yake(matendo ya mwilini)

Nafsi ikiisha kupokea taarifa,hufikiri na kufanyia maamuzi lakini ikiwa roho ya mtu ikiwa imepokea Yesu,maamuzi yale ya nafsi yanaweza kubatilishwa na roho pamoja na Roho (Roho wa Bwana uleta maamuzi mengine.

Mwanadamu Ni roho, Ana Nafsi na Anakaa Ndani Ya Mwili.
Ukisoma 1Wathesalonike 5:23 Inatusaidia Kuona Maeneo Yote Matatu Ya UTU Wa MTU;


"Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU na ROHO ZENU na MIILI YENU Mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo"
Hapa Unaona Nafsi, Roho Na Mwili Vimetajwa.

ROHO YAKO
Hii Ndo Sehemu Ya Uhai Wako Ulipo. Hii Ndiyo Iliyo Chanzo Cha Uhai Wako. Hii Ndiyo Wewe Halisi. Ikitoka Kwenye Mwili Wanakuita MAREHEMU..."MWILI WA MAREHEMU FULANI" Hii Ni Kwa Sababu "ROHO NDIYO ITIAYO UZIMA"
Soma Ayubu 32:8, Ayubu 33:4, Mithali 20:27

NAFSI YAKO
Hii Nayo Imebeba Sehemu Kuu Tatu; NIA/ AKILI (Mind), HISIA (Emotions And Feelings) Na UTASHI (Will).
Soma Mathayo 11:28-29, Zaburi 103:1-2, Mithali 23:7a

MWILI WAKO
Ni Nyumba Yako Inayohifadhi Roho Na Nafsi Yako.
Soma Mwanzo 2:7, Mwanzo 3:19b, Wagalatia 5:17-21, 24, 1Thesalonike 4:4.

Utendaji Wako Kama Mtu Unategemea Na "UZIMA ULIONAO ROHONI"

Aliyekombolewa Kwa Damu Ya Yesu [ALIYEOKOKA] na kujaa Neno la Mungu; Huwa anaanza kufanya chochote toka ROHONI- NAFSINI- MWILINI.

Lakini yule ambaye "AMEKUFA ROHONI" Kwa Sababu Ya Dhambi Na Kutokuwa Na Ushirika Na Mungu; Anaishi kinyume chake. Anaishi toka MWILINI- NAFSINI- Na Roho haina kazi maana Imekufa "KIUTENDAJI" Imebakiza tu "UHAI WA KUWA NDANI YA MWILI" Lakini Haina Uwezo Wa KUSHIRIKI MICHAKATO YA KIMAAMUZI NA UTENDAJI!

Mtu ambaye HAJAOKOKA "ALIYEKUFA KIROHO" Anaweza "KUZINI NA KAHABA" Huku "ANAJUA KABISA NI MWATHIRIKA WA VVU", Hajali maana "ANAENDESHWA TOKA MWILINI" Na kwenye NAFSI anachukua tu Uamuzi wa kutenda Hiyo Dhambi.

Mtu ambaye "AMEKUFA KIROHO" anaweza kwenda kumchukua Mme/ Mke Wa Rafiki yake au hata ndugu yake wa damu, japo anajua HAIPENDEZI KWA WANADAMU NA NI DHAMBI KWA MUNGU lakini kwakuwa "ROHO YAKE HAIFANYI KAZI" Bado anajikuta ametenda ingawa anajua ubaya na madhara ya hilo.

NINI KINATOKEA UNAPOOKOKA?

Unapookoka, "MUNGU ANAUMBA ROHO NYINGINE MPYA NDANI YAKO" Maana Ile Ya Kwanza "ILISHAKUFA KWA SABABU YA DHAMBI" Na Hapa Ndipo Ilipo Ile 2Wakorintho Isemayo "HATA IMEKUWA MTU AKIWA NDANI YA YESU KRISTO AMEKUWA KIUMBE KIPYA; YA KALE YAMEPITA, NA TAZAMA! YOTE YAMEKUWA MAPYA"

Unapookoka "ROHO YAKO INAUMBWA UPYA" Ndo Maana "UNAANZA KUICHUKIA DHAMBI" Utajikuta tu "KIU YA DHAMBI IMEONDOKA" Halafu "KIU YA KUMPENDA MUNGU NA KUTAKA KUMPENDEZA MUNGU INARUDI"

NINI HUFUATA BAADA YA KUOKOKA?

Unapookoka, "MUNGU ANAKUUMBA UPYA ROHO YAKO-Yaani anaingia ndani ya Roho Yako na kuisafisha" Lakini nafsi yako inaendelea kuwa Ileile; Utakuwa unakumbuka dhambi zako, matendo yako maovu, maisha yako yasiyompendeza Mungu nakadhalika lakini tofauti Iliyopo ni hii, "ROHO YAKO ITAKUWA HAI KUKUKUMBUSHA KUWA UMEOKOKA" Kukujulisha kuwa "WEWE NI MWANA WA MUNGU SASA" Na Hivyo kukunyima "UJASIRI NA NGUVU YA KUIENDEA DHAMBI KUITENDA KAMA KABLA YA KUOKOKA"

Hii Sehemu ya nafsi yako inaendelea "KUBADILISHWA NA KUJENGWA KUWA SAWA NA MUNGU APENDAVYO KUTEGEMEA JUHUDI YAKO YA KUJIFUNZA NENO LA MUNGU NA KULITENDA"

Hivyo basi, kumbe unapo okoka, ni ROHO YAKO inayo okoka na sio nafsi au mwili wako. Hivyo, Shetani bado anaweza kuinfluence nafsi yako na akakaa huko, lakini roho yako imesha okoka. Ndio maana Mtume Paulo anasema kwenye Warumi 7 kuwa, dhambi inakaa ndani yake, yaani dhambi bado ipo kwenye nafsi yoke na nasfi yoke bado inataka kuendesha mwili wako.

Naamini Mungu amekusaidia kujifunza kitu hapa; Yapitie maandiko yote niliyokuwekea hapa Ili kupanua kiasi na wigo wa NENO ndani yako, usiishie kusoma tu.


Shalom

Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mung Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

TRENDING NOW