Imaam Al-Albaaniy:
Je, kusherehekea Maulidi ya Nabiy ni khayr au shari?
Anayejadiliana na Imaam:
Ni khayr.
Imaam Al-Albaaniy:
Sawa. Lakini je, kwani khayr hii Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) walikuwa hawaijui?
Anayejadiliana na Imaam:
Hapana!
Imaam Al-Albaaniy:
Sijaridhika na jibu lako hilo la “hapana,” bali unawajibika kuendelea kusema: “Haiwezekani kwamba ‘khayr’ hii (ya kusherehekea Maulidi), ikiwa ni khayr au vinginevyo, kuwa ifichike na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum), na hali sisi hatuujui Uislamu na Iymaan isipokuwa kutoka kwa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Basi vipi tuijue sisi hiyo ‘khayr’ ambayo yeye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuijua! Haliwezekani hili!
Anayejadiliana na Imaam:
Kusimamisha Maulidi ni kuhuisha kumbukumbu zake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuheshimu.
Imaam Al-Albaaniy:
Falsafa hii tunaijua sisi, tunaisikia kutoka kwa watu wengi na tumeisoma katika vitabu vyao. Lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipowalingania watu, je, aliwalingania katika Uislamu wote au aliwalingania katika Tawhiyd? (kumpwekesha Allaah).
Anayejadiliana na Imaam:
At-Tawhiyd.
Imaam Al-Albaaniy:
Jambo la kwanza alilowalingania ni Tawhiyd. Kisha ikafaridhishwa Swalaah. Kisha Swiyaam (funga ya Ramadhwaan), kisha ikafaradhishwa Hajj, na hivyo ndivyo ilivyokuwa. Basi nawe fuatia katika Sunnah hii ya Shariy’ah hatua kwa hatua.
Tumekubaliana sasa kuwa haiwezekani kwamba kuna ‘khayr’ ambayo hakuijua Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kwani ‘khayr’ zote tumezijua kupitia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na uhakika huu hakuna wawili wanaoupinga wala hakuna kondoo wawili watakaopigana kwa pembe zao juu ya hili, na naitakidi kwamba yeyote atakayetilia shaka hili basi yeye si Muislamu. Na miongoni mwa Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inayounga mkono kauli hii ni kauli yake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
مَا تَرَكْتُ شَيْئًا يُقَرِّبُكُم إلى اللهِ إلَّا وَأَمَرْتُكُم بِهِ
“Sikuacha jambo lolote linalokukurubisheni kwa Allaah isipokuwa nimekuamrisheni kwalo.” [Atw-Twabaraaniy Isnaad yake ni Swahiyh. Rejea Swiffatu-Swalatin-Nabiy (3/942) ya Imaam Al-Albaaniy]
Basi ingelikuwa Maulidi ni ‘khayr’ na ingekuwa ni jambo linalotukurubisha kwa Allaah basi ingebidi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) atuelekeze nayo. Sawa au si sawa?
Mimi sitaki ukubaliane nami bila ya kukinaika kila herufi ninayotamka. Una uhuru kamili useme: “Tafadhali nukta hii sikukinaika nayo!”
Je, basi kuna lolote ambalo hukuridhika nalo nami au uko pamoja nami?
Anayejadiliana na Imaam:
Pamoja na wewe tamaam!
Imaam Al-Albaaniy:
Jazaaka Allaahu khayraa. Kwa hiyo ikiwa (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema:
“Sikuacha jambo linalokukurubisheni kwa Allaah isipokuwa nimekuamrisheni kwalo.”
Sisi tunawaambia wote wanaosema kuwa inafaa kusimamisha Maulidi: Maulidi haya ni ‘khayr’ kwa madai yenu. Basi ima Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuelekeza kusherehekea Maulidi au hakutuelekeza nayo.
Wakijibu kuwa “Ametuelekeza kusherehekea Maulidi,” tunawaambia:
هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٦٤﴾
“Leteni ushahidi wenu wa wazi mkiwa ni wakweli [An-Naml: 64]
Na wala hawatoweza kamwe kuipatia njia (dalili hiyo).
Nasi tumesoma vitabu vya 'Alawiy na vinginevyo visivyokuwa vya 'Alawi kuhusu Maulidi, na wala hawatumii dalili isipokuwa kusema tu kuwa “Maulidi ni bid’ah hasanah, bid’ah hasanah! (uzushi mzuri!).”
Basi wote wanaosherehekea Maulidi au wanaopinga sherehe hii wanakubaliana kwamba Maulidi haya hayakuweko katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala zama za Maswahaba watukufu wala zama za Maimaam Wanachuoni.
Lakini wanaojuzisha sherehe hii ya Maulidi husema: “Kwani kuna nini Maulidi na hali anatajwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumswalia na kadhaalika.”
Sisi tunasema: Ingelikuwa ni ‘khayr’ wangetutangulia kwa hayo (Maulidi).
Wewe unaijua Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
خَيْرُ النَّاسِ قَرْنِي، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ
“Watu bora kabisa ni karne yangu, kisha wanaowafuatia kisha wanawafuatia.”
nayo imo katika Asw-Swahihayn [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na karne ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ndio ambayo wameishi humo Maswahaba, kisha waliowafuatia ambao ni At-Taabi’uwna, kisha ambao wamewafuatia nao ni Atbaa’ut-Taabi’iyna. Na hili pia hakuna kukhitilafiana kwalo.
Je, basi mnadhani kuwa kuna ‘khayr’ yoyote ambayo imewapita, katika yote mawili; elimu na ‘amali? Inawezekana hilo?
Anayejadiliana na Imaam:
Ama kuhusu elimu, ingelikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemwambia yeyote katika zama zake kwamba “dunia inazunguka…”
Imaam Al-Albaaniy:
Samahani! Nakuomba usipindishe maneno. Kwa vile nimekuuliza kuhusu mambo mawili; elimu na ‘amali. Na kwa hakika kupindisha kwako kumeninufaisha kwani mimi ninavyokusudia elimu, huwa nakusudia elimu ya Dini (shariy’ah) si ya utabibu. Mfano naweza kusema kuwa: “Daktari huyu ana ujuzi zaidi kuliko Ibn Siynaa katika zama zake kwa sababu (daktari huyu) ametokea katika karne za baadaye, na amefanya majaribio mengi mno ya uzoefu.” Lakini hii haina maana kuwa anasifika mbele ya Allaah wala haimtangulizi mbele ya karne zilizoshuhudiwa (katika Hadiyth ya juu kuhusu watu bora kabisa). Lakini anasifika katika elimu aliyoisomea na sisi tunazungumzia kuhusu elimu ya shariy’ah, baaraka Allaah fiyka. Basi unapaswa utanabahi kwa haya. Kwa hiyo ninapokuambia: “Je, unadhania kuwa tunaweza kuwa ni wajuzi zaidi?” Nikimaanisha ni elimu ya shariy’ah na si elimu ya majaribio kama jiografia au falaki au kemia au fizikia. Na chukulia mfano zama hizi; mtu amemkufuru Allaah na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) lakini yeye ni mjuzi kabisa katika watu kwa elimu yake katika sayansi hii, je basi hiyo elimu yake itampelekea kuwa karibu na Allaah?
Anayejadiliana na Imaam:
Hapana.
Imaam Al-Albaaniy:
Kwa hiyo sisi hatuzungumzii elimu katika fani hizo, bali tunazungumiza elimu inayotukurubisha kwa Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa). Na hapo nyuma kidogo tumezungumza kuhusu kusherehekea Maulidi. Basi swali linarudi sasa na nataraji kuwa nitapata jibu la wazi bila ya kupindisha tena. Basi nauliza: “Je unaitakidi kwa akili na fahamu uliyopewa kwamba inawezekana sisi katika zama hizi tuwe wajuzi zaidi kuliko Maswahaba na At-Taabi’iyna (Waliofuatia) na Maimaam waliofanya juhudi katika elimu ya shariy-‘ah, na kwamba sisi tuwe ndio wepesi zaidi katika kufanya ya khayr ya kujikuribisha kwa Allaah kuliko hao Salafus-Swaalih (wema waliotangulia)?
Anayejadiliana na Imaam:
Unaposema “elimu ya shariy’ah” je, unakusudia elimu ya kufasiri Qur-aan?
Imaam Al-Albaaniy:
Wao wana elimu zaidi kuliko sisi katika kufasiri Qur-aan, na wana elimu zaidi kuliko sisi katika kufafanua Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na mwisho wana elimu zaidi kuliko sisi katika Shariy’ah nzima ya Kiislamu.
Anayejadiliana na Imaam:
Kuhusu Tafsiyr ya Qur-aan, labda kwa sasa ni zaidi kuliko zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mfano Aayah katika Qur-aan:
وَتَرَى الْجِبَالَ تَحْسَبُهَا جَامِدَةً وَهِيَ تَمُرُّ مَرَّ السَّحَابِ ۚ صُنْعَ اللَّـهِ الَّذِي أَتْقَنَ كُلَّ شَيْءٍ ۚ إِنَّهُ خَبِيرٌ بِمَا تَفْعَلُونَ ﴿٨٨﴾
Na utaona majabali ukiyadhania yametulia thabiti nayo yanapita mpito wa mawingu. Utengenezaji wa Allaah Ambaye Ametengeneza kwa umahiri kila kitu. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana kwa yale myafanyayo. [An-Naml: 88]
Basi ingelikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema katika zama zake kwamba “ardhi inazunguka”, je, hivi ataamini yeyote? Hakuna ambaye angeamini!
Imaam Al-Albaaniy:
Hivyo wewe unatutaka sisi – na nasema haya bila ya kukulaumu – kurekodi dhidi yako kupindisha kwako tena maneno? Ee ndugu yangu! Mimi nauliza kwa ujumla na si sehemu tu ya swali! Sisi tunauliza swali la ujumla. Nani wenye ujuzi zaidi kuhusu Uislamu kwa ujumla?
Anayejadiliana na Imaam:
Bila shaka ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba zake.
Imaam Al-Albaaniy:
Hivi ndivyo tunavyotaka kwako baaraka Allaahu fiyka.
Ama kuhusu Tafsiyr unayoihojia, haina uhusiano na ‘amali, bali ina uhusiano na kutafakari na kufahamu. Kisha tulishazungumza nawe kuhusu Aayah iliyopitia na na tumekuthibitishia kwamba wale wanaonukuu Aayah hii kuwa ni dalili kwamba dunia inazunguka wamekosea kwa sababu Aayaah inakusudia Siku ya Qiyaamah:
يَوْمَ تُبَدَّلُ الْأَرْضُ غَيْرَ الْأَرْضِ وَالسَّمَاوَاتُ ۖ وَبَرَزُوا لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿٤٨﴾
48. Siku ardhi itakapobadilishwa kuwa ardhi nyingine na mbingu pia na (viumbe wote) watahudhuria kwa Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.” [Ibraahiym: 48]
Hata hivyo, sisi hatuko katika maudhui haya.
Nami kwa kukubaliana nawe kimjadala, basi huenda akaweko mtu katika wale waliokuja mwishoni ambaye ana utaalamu wa sayansi au utaalamu wa ki-ulimwengu kuliko Swahaba au Taabi’iy (mwanafunzi wa Swahaba) na kuendelea. Lakini haya hayana uhusiano na ‘amali njema. Kwa sababu mfano leo, makafiri wana utaalamu zaidi ya falaki na aina zake, lakini je, wananufaika nini kwayo? (kuhusiana na Allaah?) Si lolote! Basi sisi hatutaki sasa kutumbukia katika haya. Tunataka kuzungumzia kila jambo litakalotukurubisha kwa Allaah. Basi sisi sasa tunataka tuzungumzie kuhusu Maulidi ya Nabiy Mtukufu.
Na tumeshakubaliana kwamba kama ingelikuwa ni ‘khayr’, basi bila shaka Salafus-Swaalih (wema waliotangulia) na kiongozi wao ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wangekuwa na ujuzi nao zaidi kuliko sisi na wepesi zaidi kuyatenda kuliko sisi. Je, una shaka na hili?
Anayejadiliana na Imaam:
Hapana, hapana hakuna shaka kwa hilo!
Imaam Al-Albaaniy:
Basi usivuke mipaka ukachanganya haya na mambo ya elimu ya majaribio, kwani hayana uhusiano nayo katika kukurubisha kwa Allaah kwa ‘amali njema.
Maulidi hayakuweko zama za Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kukubaliana sote. Kwa maana ‘khayr’ hii haikuweko zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba na At-Taabi’iyn na Maimaam Mujtahidiyn. Vipi basi imefichika ‘khayr’ hii kwao?
Hakuna budi ila tuseme mojawapo kati ya mawili:
Waliijua ‘khayr’ hii kama tunavyoijua sisi; nao ni wajuzi zaidi yetu. Au hawakuijua. Sasa vipi basi sisi tumeijua?
Tukisema: Waliijua ‘khayr’ hii, na hii ni kauli iliyo karibu zaidi na bora zaidi kwa wale wanaosema Maulidi yanajuzu kusherehekewa, basi kwanini hawakuyafanyia kazi? Je, sisi tuko karibu zaidi kwa Allaah (kuliko wao)?
Kwanini asikosee mmoja wao hata mara moja; Swahaba au Taabi’iy au Mwanachuoni miongoni mwao au mfanya ‘ibaadah mno miongoni mwao (kwanini wasikosee) wakaifanyia kazi ‘khayr’ hii?
Je, inaingia akilini mwako kwamba ‘khayr’ hii haikufanywa kamwe na yeyote yule? Nao walikuwa ni mamilioni na ni wajuzi zaidi kuliko sisi na wema zaidi kuliko sisi na wako karibu zaidi na Allaah?
Hivyo wewe unajua kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
لاَ تَسُبُّوا أَصْحَابِي؛ فَإِنَّ أَحَدَكُمْ لَوْ أَنْفَقَ مِثْلَ أُحُدٍ ذَهَبًا مَا أَدْرَكَ مُدَّ أَحَدِهِمْ وَلاَ نَصِيفَهُ
“Msiwatukane Swahaaba wangu. Ninaapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi Mwake, hata mmoja wenu atajitolea katika njia ya Allaah kugawa dhahabu ukubwa wake mfano wa jabali Uhud, basi hatofikia gao lao wala hata nusu ya gao lao.“ [Al-Bukhaariy, Muslim]
Je, unaona upeo wa tofauti baina yetu na wao?
Kwa sababu wao wamefanya Jihaad katika njia ya Allaah (Ta’aalaa) pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na wakapokea elimu ikiwa mbichi safi mpya kutoka kwake moja kwa moja, bila ya kuwa kiungo kirefu baina yetu na baina yake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
Kama alivyoashiria (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) maana hiyo katika Hadiyth Swahiyh:
((مَنْ أَحَبَّ أنْ يَقْرَأَ القرآنَ غَضًّا طَرِيًّا؛ فَلْيَقْرَأْهُ على قراءةِ ابنِ أمِّ عَبْدٍ)) يعني عبد الله بن مسعود
“Anayependa kuisoma Qur-aan mbichi safi mpya basi asome kwa Qiraa cha Ibn Ummi ‘Abd” (Yaani ‘Abdullaah bin Mas’uwd) [As-Silsilah Asw-Swahiyhah (5/379)].
Hawa Salafus-Swaalih (wema waliotangulia) na viongozi wao Maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum), haiwezekani sisi tuwadhanie kuwa hawakujua ‘khayr’ iliyowakurubisha kwa Allaah, na kwamba sisi ndio tuliyoijua ‘khayr’ hiyo! Na kama tukisema kuwa waliijua kama tunavyoijua basi ni mustahili kwetu kufikiria kuwa wameipuuza ‘khayr’ hiyo.
Huenda haya yamekuwekea wazi nukta ninayoizungumzia In Shaa Allaah?
Anayejadiliana na Imaam:
AlhamduliLLaah.
Imaam Al-Albaaniy:
Jazaaka Allaahu khayraa.
Kuna jambo jengine. Kuna Aayah na Hadiyth nyingi zinazobainisha kuwa Uislamu umekamilika. Na nadhani kuwa ukweli huu wewe unautambua na unaamini na hakuna tofauti baina ya ‘Aalim na Twaalibul-‘Ilm (mwanafunzi) na mtu wa kawaida asiye msomi kuhusu kujua uhakika huu. Nao ni, Uislamu umekamilika na si kama dini ya ki-Yahudi au ki-Naswara kila siku kuna mageuzo na mabadiliko.
Na nakukumbusha mfano kauli ya Allaah (Ta'aalaa):
الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمْ الْإِسْلَامَ دِينًا
Leo Nimekukamilishieni Dini yenu na Nimekutimzieni Neema Zangu kwenu na Nimekuridhieni Uislamu kuwa ni Dini yenu)) [Al-Maaidah 5: 3]
Na sasa linakuja swali, nalo ni njia nyingine ya kubainisha kwamba kusherehekea Maulidi si jambo la khayr, hii mbali na yaliyotangulia kwamba ingelikuwa ni ‘khayr’ basi wangelitutangulia wao yaani: Salafus-Swaalih; walio na elimu zaidi yetu na wenye kufanya ‘ibaadah zaidi yetu.
Maulidi haya ya Nabiy ingelikuwa ni ‘khayr’ basi ni katika Uislamu. Tunasema: Je, hivi sisi sote tunaopinga kusimamisha Maulidi na wenye kuyajuzisha, je, sote tunakubaliana kama tulivyokubaliana nukta iliyotangulia kwamba sherehe hii haikuweko zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)? Je, tuko bado katika kukubaliana huku (nukta hii ya pili?) kwamba sherehe hii, kama ni ‘khayr’ basi imo katika Uislamu na ikiwa si ‘khayr’ basi haimo katika Uislamu? Na siku ambayo Aayah hii imeteremshwa:
Leo Nimekukamilishieni Dini yenu…
Siku iliyoteremshwa hakukuwa na sherehe ya Maulidi ya Nabiy. Kwa hiyo je, imo katika Dini katika uoni wako?
Tafadhali uwe mkweli nami. Wala usidhani kuwa mimi ni miongoni mwa Mashaykh wanaonyamazisha wanafunzi, bali hata watu wa kawaida kwa kuwaambia: “Nyamaza! Hujui! Huna elimu!” Hapana wewe uko na uhuru kamili kama kwamba unaongea na mtu kama wewe au chini yako kwa umri na elimu. Ikiwa hukukinaika sema: “Sikukinaika.”
Hivyo sasa, ikiwa Maulidi ni ‘khayr’ basi hayo ni katika Uislamu, na ikiwa si ya khayr basi sio katika Uislamu. Na tukikubalilana kwamba kusherehekea Maulidi hayakuweko pindi ilipoteremshwa Ayaah iliyotangulia, basi ni mantiki kusema kuwa si katika Uislamu.
Na nitathibitisha nnayoyasema kwa aliyoyasema Imaam wa makazi ya hijrah (Madiynah) Imaam Maalik bin Anas ambaye amesema:
“Atakayezusha bid’ah katika Uislamu…” (Tanabahi amesema: “bid’ah moja” wala hakusema bid’ah nyingi!) “…kisha akaiona kuwa ni nzuri basi amedai kuwa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekhini risaalah (ujumbe).”
Na hili ni jambo khatari mno! Nini dalili ee Imaam (Maalik)?
Akasema Imaam Maalik: “Someni mkipenda kauli ya Allaah (Ta’aalaa):
الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمْ الْإِسْلَامَ دِينًا
Leo Nimekukamilishieni Dini yenu na Nimekutimzieni Neema Zangu kwenu na Nimekuridhieni Uislamu kuwa ni Diyn yenu)) [Al-Maaidah (5: 3]
"فمالم يكن يومئذٍ ديناً ؛ فلا يكون اليوم ديناً".
“Basi ambayo hayakuwa ni Dini siku hizo, hayawezi kuwa ni Dini leo.” (mwisho wa maneno yake Imaam Maalik)
Je, alisema lini haya Imaam Maalik? (Alisema) Katika karne ya pili baada ya hijrah ambayo ni mojawapo wa karne zilizoshuhudiwa kuwa ni karne bora. Sasa itakuwaje basi ikiwa ni karne ya kumi na nne (tuliyonayo sasa?)
Maneno haya (ya Imaam Maalik) yanapasa kuandikwa kwa dhahabu, lakini sisi tumeghafilika na kitabu cha Allaah (Ta’aalaa) na Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kauli za Maimaam ambao tunadai kuwa tunawafuata. Mbali kabisa mbali kabisa! Na tofauti baina yetu na wao katika kufuata ni kama tofauti ya Mashariki na Magharibi.
Huyo (Imaam Maalik) ni Imaam wa mji wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipohajiri (Madiynah). Anasema kwa lugha safi sahihi kabisa ya Kiarabu: “Basi ambayo hayakuwa ni Dini siku hizo, hayawezi kuwa ni Dini leo.”
Leo kusherehekea mazazi ya Nabiy ni ya Dini na ingekuwa si hivyo, basi mjadala huu usingejiri baina ya ‘Ulamaa wanaoshikamana na Sunnah na kuihami (Dini) dhidi ya bid’ah. Itakuwaje yawe (Maulidi) katika Dini wakati hayakuweko wakati wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala zama za Maswahaba wala zama za Taabi’iyna (waliofuatia Maswahaba) wala Taabi’iy Taabi’iyna (Waliofuatia baada ya Taabi’iyn)?
Imaam Maalik ni katika Atbaa’ut-Taabi’iyn na ni miongoni mwa waliotajwa katika Hadiyth:
((خَيْرُ النَّاسِ قَرْنِي ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ)) متفق عليه
((Watu bora kabisa ni wa karne yangu, kisha ambao wanafuatia kisha ambao wanafuatia)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Imaam Maalik amesema: “Basi ambayo hayakuwa ni Dini siku hizo, hayawezi kuwa ni Dini leo, na ummah wa mwisho hautatengemaa isipokuwa kwa kile kilichofanya ummah wa kwanza kutengamaa.”
Je, ummah wa mwanzo kabisa ulitengamaa (ulikaa sawa) kwa nini? Kwa kuzusha mapya katika Dini kwa kujikurubisha kwa Allaah (Ta’aalaa) mambo ambayo hakujikurubisha nayo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)?
Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mwenyewe ndiye aliyesema:
ما تَرَكْتُ شيئاً يُقَرِّبُكُمْ إِلَى اللهِ إلى وأَمَرْتُكُمْ به
“Sijaacha lolote litakalokukurubisheni kwa Allaah isipokuwa nimekuamrisheni kwalo.”
Kwanini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakutuamrisha tusherehekee Maulidi yake? Swali hili lina jawabu:
Kuna sherehe ya kusherehekea Maulidi ya Nabiy yaliyowekewa shariy’ah kinyume na hizi sherehe za Maulidi haya (mnayoyafanya) ambayo hayakuamrishwa. Sherehe hii iliyoamrishwa ilikuweko zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kinyume na yaliyokuwa hayakuamrishwa yakiwa na tofauti kubwa kabisa iliyoko baina ya sherehe mbili (hizi).
Tofauti ya kwanza: Ni kwamba sherehe iliyoamrishwa (tutaitaja) ni ‘ibaadah ambayo wamekubaliana Waislamu wote.
Tofauti ya pili: Sherehe iliyoamrishwa inakariri kila wiki mara moja, lakini hiyo yao ambayo haikuamrishwa inatokea mara moja tu kwa mwaka.
Hizi ni tofauti mbili baina ya sherehe mbili hizo. Kwamba ya kwanza ni ‘ibaadah, na inakariri kila wiki mara moja, kinyume na ya pili ambayo si ya kishariy'ah na si ‘ibaadah na wala haikariri kila wiki!
Na mimi sizungumzi kwa matamanio yangu ambayo Allaah Hakuteremshia dalili, bali nakutoleeni dalili kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambayo imehadithiwa katika Swahiyh Muslim (Rahimahu Allaah):
عنْ أَبِي قَتَادَةَ الْأَنْصَارِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سُئِلَ عَنْ صَوْمِ الِاثْنَيْنِ فَقَالَ: ((فِيهِ وُلِدْتُ وَفِيهِ أُنْزِلَ عَلَيَّ)).
Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu Swawm ya Jumatatu akasema: “Nimezaliwa siku hiyo na siku hiyo nimeteremshiwa (Qur-aan).” [Muslim]
Yanamaanisha nini maneno hayo?
Ni kama vile anasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
Utaniulizaje hivyo na hali Allaah Amenitoa siku hiyo kuwa na uhai na nikateremshiwa wahyi humo?
Yaani inawapasa mfunge Swawm siku ya Jumatatu kumshukuru Allaah (Ta’aalaa) kuniumba mimi siku hiyo na kuteremsha Wahyi kwangu siku hiyo.
Na hivyo ni sawa na Swawm ya Mayahudi siku ya ‘Aashuraa. Na huenda ukajua kuwa kabla ya kufaridhishwa Swawm ya Ramadhwaan, Swawm ya siku ya ‘Aashuraa ndio ilikuwa fardhi kwa Waislamu. Na kuna kauli nyengine za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba alipohamia Madiynah aliwakuta Mayahudi wanafunga Swawm siku ya ‘Ashuraa. Akawauliza sababu yake wakamjibu: “Ni siku ambayo Allaah Alimuokoa Muwsaa kutokana na watu wa Fir’awn, hivyo tunafunga Swawm kumshukuru Allaah.” Hapo yeye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:
“Sisi tuna haki zaidi juu ya Muwsaa kuliko nyinyi.”
Basi akafunga Swawm siku hiyo na akaamrisha watu, pia siku hiyo ikawa ni fardhi mpaka Allaah Alipoteremsha kauli Yake:
شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ ۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ۖ ﴿١٨٥﴾
Mwezi wa Ramadhwaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan ili iwe mwongozo kwa watu na hoja bayana za mwongozo na pambanuo (la haki na batili). Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu (mwandamo wa) mwezi na afunge Swiyaam. [Al-Baqarah: 185]
Hapo ikawa Swawm ya ‘Aashuraa ni Sunnah ,na kukafutwa kuwajibika kwake.
Ushahidi wa haya ni kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliungana na Mayahudi kufunga Swawm siku ya ‘Aashuraa kama ni shukurani kwa Allaah (Ta’aalaa) kumuokoa Muwsaa ('Alayhis-Salaam) kutokana na Fir’awn. Hivyo mlango wa shukurani umefunguliwa kwetu kwa kufunga Swawm siku ya Jumatatu kwa sababu ni siku ambayo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amezaliwa na ni siku ambayo ameteremshiwa Wahyi.
Sasa nakuuliza: Je, hawa watu wanaosherehekea mazazi (yasiyokuweko katika shariy’ah) ambayo tunajua kuwa hayana khayr ndani yake - najua kuwa wengi ya watu hao hufunga Swawm Jumatatu kama wanavyofunga Swawm siku ya Alkhamiys - lakini je, Waislamu wengi wanafunga Swawm ya Jumatatu pekee?
Hapana! Hawafungi Swawm Jumatatu, lakini Waislamu wengi wanasherehekea mazazi ya Nabiy mara moja kwa mwaka. Je, hivi si kinyume na usahihi?
Hawa inawathubutikia kauli ya Allaah (Ta’aalaa) kwa Mayahudi:
أَتَسْتَبْدِلُونَ الَّذِي هُوَ أَدْنَىٰ بِالَّذِي هُوَ خَيْرٌ ۚ
“Je mnataka kubadilisha yaliyo duni kwa yaliyo bora? [Al-Baqarah: 61] (Kuchagua yaliyo duni na kuacha yaliyo bora)
Hiyo ndio khayr. Kufunga Swawm iliyokubalika kwa Waislamu wote; nayo ni Swawm ya Jumatatu, na juu ya hivyo Waislamu wengi hawafungi Swawm hiyo!
Kisha kwa ambao wanaifunga Swawm nao ni wachache. Je, wanajua siri ya Swawm hiyo?
Hapana hawajui!
Basi wako wapi Wanachuoni wanaotetea Maulidi?!
Kwanini hawawabainishii watu kuwa Swawm ya Jumatatu ni kusherehekea kulikoamrishwa kuwa ni Maulidi na wakahimiza kuifunga Swawm badala ya kutetea ambayo hayakuamrishwa? Na Amesadikisha Allaah (Ta’aalaa) Anaposema:
“Je mnataka kubadilisha yaliyo duni kwa yaliyo bora?
Na Amesadikisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliposema:
لَتَتَّبِعُنَّ سَنَنَ مَنْ قَبْلَكُمْ؛ شِبْرًا بِشِبْرٍ، وذِرَاعًا بِذِرَاعٍ؛ حَتَّى لَو دَخَلُوا جُحْرَ ضَبٍّ لَدَخَلْتُمُوهُ
“Mtafuata nyendo za wale waliokuja kabla yenu hatua kwa hatua mpaka itafika hadi wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah nyingine iliyo khatari:
حتى لو كان فيهم مَنْ يَأْتِي أُمَّهُ على قارعةِ الطريقِ لَكَانَ فيكم مَنْ يَفْعَلُ ذلك
“...hadi kwamba hata ingekuwa mmoja wao angejamiiana na mama yake katikati ya barabara, angekuweko mtu miongonii mwenu ambaye angefanya hivyo pia” [Al-Haakim ikiwa ni Hasan kama alivyoisahihisha Al-Bazzaar na Al-Albaaniy ameikubali katika Silsilah Asw-Swahiyhah (1348)]
Basi sisi (tunaosherehekea Maulidi) tunafuata mwendo wa Mayahudi, tukabadilisha ambayo ni ya (kuchagua yaliyo) duni kwa (kuacha) yaliyo khayr kama tulivyobadilisha (tukachagua) Maulidi ya Nabiy ambayo yanatokea mwaka mara na hayana dalili kwa (kuacha) ambayo yaliyo khayr nayo ni kusherehekea kila Jumatatu ambayo ni kusherehekea kulikoamrishwa kwa kuifunga Swawm, pamoja na kutanabahi siri yake humo kuwa unafunga Swawm kwa ajili ya kumshukuru Allaah (Ta’aalaa) kwa kumuumba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Akateremsha wahyi humo (siku hiyo).
Na nahitimisha maneno yangu kwa kutaja kauli ya (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
أَبَى اللهُ أنْ يَقْبَلَ توبةَ مبتدعٍ
“Allaah Amekataa kabisa kupokea tawbah ya mwenye kufanya bid’ah.” [Ibn Maajah na Imaam [Imaam Al-Albaaniy amesema ina udhaifu, lakini kuna Hadiyth ambayo ameisahihisha yenye maana kama hiyo iliyokusanywa na Abuu Imaam katika Taariykh Asbahaan (Uk. 259), Atw-Twabaraaniy katika Al-Awsatw (4360) na wengineo].
Na Allaah (Ta’aalaa) Anasema:
يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖوَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ
Ee Rasuli! Balighisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukubalighisha ujumbe Wake. Na Allaah Atakuhifadhi dhidi ya watu. [Al-Maaidah: 67]
Anayejadiliana na Imaam:
Je, kusoma Siyrah ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) si takrima kwake?
Imaam Al-Albaaniy:
Naam (endelea).
Anayejadiliana na Imaam:
Si mna thawabu ya khayr kutoka kwa Allaah?
Imaam Al-Albaaniy:
Yote ni khayr! Lakini hutofaidika chochote kutokana na swali hili. Kwa hiyo nakukatisha kwa swali: Je ,kuna yeyote aliyekuzuia kusoma Siyrah yake?
Kisha sasa nakuuliza swali: Ikiwa ni aina ya ‘ibaadah iliyoamrishwa lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuiwekea muda makhsusi wala hakuiwekea jinsi ya kuitekeleza; je, inajuzu kwetu kuiwekea wakati makhsusi au namna ya kuitekeleza? Je, unalo jibu?
Anayejadiliana na Imaam:
Hapana sina jibu.
Imaam Al-Albaaniy:
Allaah (Ta’aalaa) Anasema:
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ شَرَعُوا لَهُم مِّنَ الدِّينِ مَا لَمْ يَأْذَن بِهِ اللَّـهُ ۚ
Je, wanao washirika waliowaamuru Dini yale ambayo Allaah Hakuyatolea idhini? [Ash-Shuwraa: 21]
Na Anasema pia Allaah (Ta’aalaa):
اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَـٰهًا وَاحِدًا ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٣١﴾
Wamewafanya Wanavyuoni wao mafuqahaa wa dini na Wamonaki wao kuwa ni miungu badala ya Allaah, na (pia wamemfanya) Al-Masiyh mwana wa Maryam (kuwa ni mungu); na hali hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu Ilaah (Allaah) Mmoja (Pekee). Hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye. Utakasifu ni Wake! kutokana na yale yote wanayomshirkisha nayo. [At-Tawbah: 31]
‘Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliposikia Aayah hii na alikuwa kabla ya kusilimu kwake, alipokuwa Mnaswara, ilikuwa ngumu kwake akasema: “Hatukuwa tukiwaabudu.” Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:
أَلْيَسَ يُحَرِّمُونَ مَا أَحَلَّ اللهُ فَتُحَرِّمُونَهُ وَيُحِلُّونَ مَا حَرَّمَ اللهُ فَتُحِلُّونَهُ؟
“Je, kwani hawakuwa wakiharamisha Aliyoyahalalisha Allaah nanyi mkayaharamisha, na wakahalalisha Aliyoyaharamisha Allaah nanyi mkayahalalisha?”
Akasema: Ndio.
Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Basi hiyo ndio kuwaabudu kwao.” [At-Tirmidhiy (3095) na ameipa daraja ya Hasan Imaam Al-Albaaniy]
Na hii inabainisha khatari ya kufanya bid’ah katika Dini ya Allaah (Ta’aalaa):
Mwisho wa Mjadala
************************
Imetolewa kutoka katika moja ya kanda za Imaam Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika Silsilat Al-Hudaa wan-Nuwr Kanda namba (1//94)
Friday, October 22, 2021
MJADALA BAINA IMAAM AL-ALBAANIY NA MSHEREHEKEAJI MAULIDI
ETI MIKOJO YA MTUME MUHAMMAD INAWAKINGA WAISLAM NA MOTO WA JEHANNAM
Mtume (SAW) alikuwa na bakuli la mbao alilokuwa akikojoa na kuliweka chini ya kitanda chake. Usiku mmoja, aliitafuta lakini hakuipata na akaiuliza kwa kusema, bakuli liko wapi? Washiriki wa nyumba hiyo walijibu "Kijakazi wa Umm Salamah Barrah alikunywa". Mtume akajibu, "Hakika amejilinda na moto wa jehanamu kwa ukuta mkubwa".
KUMBE MIKOJO YA MUHAMMAD NI DAWA YA TUMBO
HAKIKA HUU NI UCHAWI
Matba’ah Da’irat al-Ma’arif, Hayder Abad
Imam Jalal al-Din Suyuti anaripoti kutoka kwa Abu Ya’la, Hakim, Dar Qutni, Tabarani na Abu Nu’aym kutoka Umm Ayman Mwenyezi Mungu amridhie, ambaye alisema, ‘Mtume aliamka usiku mmoja na akakojoa kwenye bakuli. Wakati wa usiku huo, niliinuka katika hali ya kiu kwa hivyo nikanywa chochote kilichokuwa kwenye bakuli. Asubuhi nilimwambia kile nilichokuwa nimefanya ambacho alitabasamu na kusema, 'hakika hautawahi kupata maumivu ndani ya tumbo lako' '. Maneno ya Abu Ya’ala ni kama ifuatavyo, ‘hautawahi kusikia maumivu ya tumbo kama ya leo’.
Al-Khasa’is al-Kubra 2:252, Matba’ah Da’irat al-Ma’arif, Hayder Abad
Imam Jalal al-Din Suyuti reports from Abu Ya’la, Hakim, Dar Qutni, Tabarani and Abu Nu’aym from Umm Ayman May Allah be pleased with her, who said, ‘the Prophet got up one night and urinated in a bowl. During that night, I rose in the state of thirst so I drank whatever was in the bowl. In the morning I told Him what I had done to which He smiled and said, ‘surely you will never have pain in your stomach’’. Abu Ya’ala’s wordings are as follows, ‘you will never feel stomach pain as of today’.
الخصاسات الكبرى 2: 252 ، مطبعة دائرة المعارف ، حيدر آباد
وروى الإمام جلال الدين السيوطي عن أبي يعلا والحكيم ودار قطني والطبراني وأبو نعيم عن أم أيمن رضي الله عنها ، قال: قام النبي ليلة وبول في وعاء. خلال تلك الليلة استيقظتُ من العطش فاشربت كل ما في الوعاء. في الصباح أخبرته بما فعلته فابتسم وقال له "بالتأكيد لن تشعر بألم في معدتك". كانت كلمات أبو يعلا كما يلي: "لن تشعر بألم في المعدة أبدًا اعتبارًا من اليوم".
alkhisasat alkubraa 2: 252 , matbaeat dayirat almaearif , haydar abad
warawaa al'iimam jalal aldiyn alsuyutiu ean 'abi yaela walhakim wadar qutni waltabarani wa'abu naeim ean 'umi 'ayman radi allah eanha , qal: qam alnabiu laylat wabul fi waea'. khilal tilk allaylat astyqzt min aleatash fashrabat kula ma fi alwaea'i. fi alsabah 'akhbiratuh bima faealath faibtasam waqal lah "bialtaakid lan tasheur bi'alam fi maedatik". kanat kalimat 'abu yaela kama yali: "lan tasheur bi'alam fi almaeidat abdan aetbaran min alyawmi".
Shalom
Max Shimba Ministries
Tuesday, October 12, 2021
11-YEAR OLD CHRISTIAN GIRL BAFFLES ISLAMIC SCHOLAR WITH ONE SIMPLE QUESTION
Choose you this day whom ye shall serve
An 11-year old Arab Christian girl was listening to an Islamic scholar preach about Allah. When he was done, the little girl approached him and said this – “show me where in the Koran that Allah loves me as the sinner that I am, and I will become a Muslim.” The dumbstruck man was silent for a long time, and then walked away. He had no answer to give her. Why?
“Herein is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son to be the propitiation for our sins.” 1 John 4:10 (KJB)

God will save anyone who calls on Him whether they be Muslim, the Arab Catholic girl in this photo, a Buddhist, Hindu, or even an Atheist. He will even save you.
Because the Allah of the Koran does not love the sinner, or the unrighteous, or the lost, or the struggling, or the backslider. Allah of the Koran displays only a highly-qualified, conditional type of “love”, and it is for Muslims only. The Koran clearly teaches that Allah hates non-Muslims:
QUR’AN 3:31-32—SAY [O MUHAMMAD]: IF YOU LOVE ALLAH, THEN FOLLOW ME, ALLAH WILL LOVE YOU AND FORGIVE YOU YOUR FAULTS, AND ALLAH IS FORGIVING, MERCIFUL. SAY: OBEY ALLAH AND THE APOSTLE; BUT IF THEY TURN BACK, THEN SURELY ALLAH DOES NOT LOVE THE UNBELIEVERS.
QUR’AN 30:43-45—THEN TURN THY FACE STRAIGHT TO THE RIGHT RELIGION BEFORE THERE COME FROM ALLAH THE DAY WHICH CANNOT BE AVERTED; ON THAT DAY THEY SHALL BECOME SEPARATED. WHOEVER DISBELIEVES, HE SHALL BE RESPONSIBLE FOR HIS DISBELIEF, AND WHOEVER DOES GOOD, THEY PREPARE (GOOD) FOR THEIR OWN SOULS, THAT HE MAY REWARD THOSE WHO BELIEVE AND DO GOOD OUT OF HIS GRACE; SURELY HE DOES NOT LOVE THE UNBELIEVERS.
This is a startling contrast to the words of Scripture that shows that God offers His love to any and all who will receive it, as a free gift paid in full with no strings attached:
“The LORD thy God in the midst of thee is mighty; he will save, he will rejoice over thee with joy; he will rest in his love, he will joy over thee with singing.” Zephaniah 3:17
“But God commendeth his love toward us, in that, while we were yet sinners, Christ died for us.” Romans 5:8
“For God so loved the world, that he gave his only begotten Son, that whosoever believeth in him should not perish, but have everlasting life.” John 3:16
The bible teaches that God is not interested in “making you a Christian”, He desires to save you from the penalty of your sins which is an eternity in Hell. God’s salvation is a free gift that only needs to be received to become active. It is the Great Transaction – your sins in exchange for His righteousness and a full and free eternal pardon.
The Allah of the Koran is not the same as the God of the Bible. Allah wants to make you a Muslim, God wants to set you free.
“If the Son therefore shall make you free, ye shall be free indeed.” John 8:36
https://www.nowtheendbegins.com/11-year-old-christian-girl-baffles-islamic-scholar-one-simple-question/
Monday, October 11, 2021
THE SHACKING BUTTOCKS OF THE TRIBE OF DAUS
Sahih Bukhari Hadith No. 7116
Chapter 94 The Book Of Al-Fitan
Book Sahih Bukhari
Hadith No 7116
Baab Fitno Ka Bayan Mein
ENGLISH
ARABIC
URDU
Narrated Abu Huraira: Allah's Apostle said, The Hour will not be established till the buttocks of the women of the tribe of Daus move while going round Dhi-al-Khalasa. Dhi-al-Khalasa was the idol of the Daus tribe which they used to worship in the Pre Islamic Period of ignorance.
Sahih Bukhari 7116
Hadith on Al-Fitan of Sahih Bukhari 7116 is about The Book Of Al-Fitan as written by Imam Muhammad al-Bukhari. The original Hadith is written in Arabic and translated in English and Urdu. The chapter The Book Of Al-Fitan has eighty-nine as total Hadith on this topic.
Monday, October 4, 2021
JE NI SAWA KWA MWANAMKE KUVAA SURUALI?
BWANA YESU asifiwe!
Je, Mwanamke anaweza kuvaa suruali akiwa katika mazingira ya kikazi kama Jeshini au Kama ni Fundi Umeme au Hotelini n.k?
Je, Mwanamke anaweza kuvaa Suruali akiwa kwenye mazingira ya baridi kali la barafu? Au anaweza kuvaa kulingana na tamaduni yanchi zao?
Je, ipo wapi aya ndani ya Biblia isemayo Suruali ni vazi la wanaume?
Nimekutana na swali jana ya kuwa "Je ni halali kwa mwanamke kuvaa suruali?" Nikapewa na andiko katika Kumbukumbu laTorati 22:5 Haya Wapendwa tunasemaje juu ya hili!! Maoni yangu ni haya yafuatayo Kwani Imeandikwa wapi kwamba Suruali ni Vazi la Kiume?
Pia Biblia inataja kuwa kuna mavazi ya kikahaba, (Mwanzo 38:14 ) ukisoma Mithali 7:10 inasema “Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;…mtu yeyote aliyekuwa ameonekana ameyavaa hayo” Kulikuwa na mavazi ya kikuhani pia ambayo yakivaliwa, yanamjulisha Yule ni Kuhani nk. yote hayo mtu alipokuwa akivaa yalikuwa yaashiria kitu Fulani rohoni.
Shalom ndugu zangu mimi nimesoma swali hilo na nimebarikiwa sana na kufurahi sana na mimi pia naomba nichangie kidogo juu ya suala hili nionavyo mimi kuvaa suruali kwa mwanamke sio dhambi ila itakua dhambi tu kama itasababisha wengine kutenda dhambi katika Mathayo 18:7 Biblia inasema ''Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha, maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; LAKINI OLE WAKE MTU YULE ALILETAYE JAMBO LA KUKOSESHA.''
Kwa hiyo ndugu zangu Suruali itakuwa dhambi kama itawashawishi wengine kuingia dhambini maana tukisema tu kuvaa nguo fulani ni dhambi basi mvaaji hatakiwi kuvaa hata kama yuko chumbani na mmewe maana kuvaa nguo hiyo ni dhambi na dhambi zingine ni dhambi hata kwa kusababisha mfano unakuta kijana anaenda kutongozea kijana mwingine kwa binti na ukimuuliza atakwambia kutongoza sio dhambi ila dhambi ni kuzini lakini ukweli hiyo ni dhambi kubwa wote mnajua na hili pia la kuwavalia wengine nusu uchi ni dhambi na kwa habari ya Suruali kuwa ndio vazi la kiume napata tafakari hii.
HOJA YA KUFIKICHA AKILI:
Je, ipo wapi aya ndani ya Biblia isemayo Suruali ni vazi la wanaume?
Biblia iliposema mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanaume haikutaja Suruali. Kwa upande wangu neno Suruali kwenye Biblia lipo katika Danieli 3:21 ikizungumzia habari ya wale vijana watatu, Anania, Azariya na Mishael "Shedrack, Meshach, and Abednego) waliotupwa katika tanuri la moto huku wakiwa wamevaa Suruali zao na joho zao. Hawa walikua wanaume wote hata hivyo hapa haionyeshi kwamba hayo ndio mavazi ya wanaume.
Muhimu na cha kuzingatia ni kwamba Biblia imeagiza wanawake wavae nguo za kujisitri na nguo hizi haijalishi ni sketi au Suruali maana wapo wadada wengine huvaa sketi za kuwachora maungo yao utasema hata heri ya anayevaa suruali. Pia hakuna haja ya kuiga kila mtindo maana kuna baadhi ya mitindo chanzo chake ni kuzimu. Kumbuka pia tunaitwa Wakristo yaani wanaomfuata Kristo. Matendo 11:26, pia tukumbuke kuwa kama tutaupenda sana ulimwengu na mambo yake basi kumpenda MUNGU hakumo ndani yetu hivyo hakuna haja ya kuwaweka majaribuni wenzako na ukiangalia wengi wa wanaovaa nguo ambazo zinalalamikiwa ni wale ambao hawajaolewa na akiolewa anaacha hapo ndio unajua kwamba alikua anavaa zamani kwa sababu fulani ambayo ni dhambi.
Warumi 14 : 2 - Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.
👉� _Wewe ambaye unaitazama suruali kama dhambi kwako ukiivaa, usijaribu kuvaa kwako ni dhambi, umekwisha kujihukumu nafsi, na kila tendo lisilo tokana na imani ni dhambi_ Yule avaaye kwa nia ya vazi, la kujisitiri, kwa nia safi, nia yake haikuwaza uovu, amevaa yeye kama yeye, usimuhumukumu wewe usiye vaa, maana yeye anaimani na dhamiri yake yamshuhudia vema.
Mathayo 5 : 28 - lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Agano la kale dhambi ilikuwa ni matendo, na yalihumumiwa matendo, lakini agano jipya Yesu anahukumu kuanzia nia, yaani mpaka umezini, siku ulio zini, siyo siku ulioanguka, ulizini na kuanguka tangu ulipo anza mchakato wa nitalala na huyu binti, au ulipo kubali kwamba ntakupa👉�👙, sasa wewe unaye vaa Suruali ndani yako umekusudia nini, ndo hukumu inako anzia.
Warumi 8 : 27 - Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.
Mungu anatujua vizuri, kwa kuichunguza Nia ya moyo na kujua, huyu amevaa suruali lakini lengo, ka msukumo awatege watu, aonyeshe umbo lake, nk, nk... Huyu amevaa walaaa hana lolote ndani, kavaa kujisitiri na safari, na kazi hii, sheria ya ofisini nk, na Ameamua kuvaa ya heshima
Lakini wapendwa tusiwe na ufahamu mdogo, wewe waihukumu Suruali kama dhambi, hujui gauni, blause, sketi nayo ni dhambi, ila tu umevaaje, ikoje? Kwani vimini ni Suruali? Vitop ni suruali? Magauni na sketi za mpasuo hatari ni suruali? Je, ni vizuri kwa sababu ni nguo za kike? Kata K, Suruali siyo dhambi kwa sababu imevaliwa na mvulana ni vazi lake? Tusiwe na ufahamu finyu panua fikira.
Kama watoto wa MUNGU tuliozaliwa sio kwa mwili bali kwa ROHO WA MUNGU basi na tuenende kama watakatifu wa MUNGU pasipo lawama.
Natamani niendelee lakini mwisho kabisa Biblia katika Waefeso 5:10 inasema ''MKIHAKIKI NI NINI IMPENDEZAYO BWANA'' .
MUNGU awabariki sana na kila mtu awe ni mwanamke au mwanaume kwa kila tendo lolote afanyalo ahaakiki kama anampendeza MUNGU maana tukitenda kwa kumpendeza MUNGU hatutalalamikiwa .
MUNGU awabariki sana Na nahitaji michango ya watumishi wengine hapa au kwenye page yetu ya facebook itwayo Maisha ya Ushindi FUNGUA HAPA KUTOA MAONI YAKO.
Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani.
ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
Shalom
Friday, October 1, 2021
WOMEN PROSTITUTES BEING REPLACED BY SEX SHEEP AND CAMELS IN KABUL BROTHELS AFTER TALIBAN TAKEOVER
The dozen brothels operating in Kabul before the Taliban victory have been emptied of their sex workers by the Islamists, whom replaced them with sheep and camels designated to be used for sexual activity.
Despite promises from the new Taliban regime to allow Afghan women to continue working and participating in public life, armed insurgents have already closed several “anti-Islamic” businesses in Kabul, including bars and brothels.
Various sources have reported Taliban fighters forcing women out of the various brothels across Kabul and replacing them with sheep and camels in concordance with the sharia, the Islamic law.
According to Margaret Smith, regional director of Human Rights Watch in Afghanistan, this is an important regression for Afghan women, whom she says are “treated worse than animals”.
“Sheep and camels have more rights under the Taliban regime than women. For them, sex for fun is with animals. Women are just walking wombs designed to bear and raise children.”
Ms. Smith fears this could be “just a first step” and that women could gradually be totally kicked out of public life by the new regime.
“They banned women from the world’s oldest profession to replace them with animals. I wouldn’t be surprised if they’d replace female secretaries with monkeys to humiliate them.”

Dozens of Afghan sex workers were kicked out of the various brothels allowed by the previous regime over the last few days, to be replaced by “sex animals” in concordance with the sharia.
During the Taliban rule in the 1990s, dozens of animal brothels were allowed across the country while human prostitution was severely repressed.
The group’s new leadership, seeking international recognition, made several promises concerning human rights, particularly women’s rights.
The treatment of Kabul’s sex workers suggests the Islamist organization is still extremely rigorous in its application of the sharia, despite its public promises.
SAUDI RELIGIOUS POLICE CRACKS DOWN ON MAJOR PORK SMUGGLING RING: 319 ARRESTS, 27 TONS OF BACON SEIZED
Thousands of police officers were mobilized this morning in Saudi Arabia for a massive operation against a large pork smuggling network, arresting 319 suspects and seizing more than 30 tons of pork meat.
More than 4,000 officers of the Saudi police and the Committee for the Promotion of Virtue and the Prevention of Vice acted simultaneously to hit what they describe as “the largest criminal organization in the country.”
According to Minister of Interior spokesman Abdulaziz bin Salam, 319 of the 327 suspects aimed by the operation were arrested, and more than 30,8 metric tons of pork meat were seized.
“The operation was a success. We arrested most of the suspects, seized 27 tons of bacon and 3 tons of pork chops. We stopped this sinful meat from defiling the souls of Saudis.”
Mr. bin Salam says more arrests are to be expected over the next few weeks as the kingdom is ” extremely determined to put an end to pork smuggling”.
“Pork is evil. Corrupting a man’s soul with pork is worse than cutting his head off. We need to end this anti-Islamic trade right now before it corrupts our population.”

Minister of Interior spokesman Abdulaziz bin Salam says the kingdom’s police is dedicated to put a definitive end to pork smuggling “whatever it takes”.
Eating, possessing or selling live pigs or any pork product is strictly prohibited in Saudi Arabia, leading to sentences going from 2 to 25 years of imprisonment as well as corporal punishments like whipping.
More the 1,200 Saudis are arrested every year in pork related charges and 17% of the country’s prison population is imprisoned for eating or selling pork meat.
https://worldnewsdailyreport.com/saudi-religious-police-cracks-down-on-major-pork-smuggling-ring-319-arrests-27-tons-of-bacon-seized/
The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration
The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...
TRENDING NOW
-
Baba umenipa funguo muhimu katika Mathayo 16:19 za kufunga na kufungua. Ninatumia funguo hizo kufunga na kufungua, kuvunja na kubamiza kil...
-
Kuna watu wanapitia mateso mengi sana, wengine wamefungwa katika vifungo bila wao kujijuwa basi chukua muongozo huu utakusaidia au itasaid...
-
Adui anakuja kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari kupambana na maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mun...
-
Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu. Twazidi pia kukushukuru kwa ajili ...
