Tuesday, December 25, 2018

Iraq officially makes Christmas Day a national holiday

Clergymen hold Mass on Christmas Eve for people who returned to Bartella, Iraq, after ISIS militants had been driven out of the town.
(CNN)The Iraqi Cabinet approved a law to mark Christmas Day, December 25, as an official holiday across the country "on the occasion of the birth of Jesus Christ," according to a statement released by the Iraqi government.
The Cabinet voted on an amendment to the national holidays law in the country that Christmas Day is a holiday for all Iraqis, and not only for the Christian community, as it had been for decades.
"Happy Christmas to our Christian citizens, all Iraqis and to all who are celebrating around the world," the Iraqi government said on Twitter.
    Before the US-led invasion of Iraq in 2003, there were about 1.4 million Christians in the country. However, their numbers have dwindled to roughly 300,000 after hundreds of thousands fled the country following violence and attacks by various armed groups over the years.

    Sunday, December 23, 2018

    KWANINI WAKRISTO TUNATUMIA MTI WA KRISMAS? SEHEMU YA KWANZA

    Image may contain: sky, christmas tree and outdoorKWANINI WAKRISTO TUNATUMIA MTI WA KRISMAS?
    JE, NI SAHIHI KIBIBLIA KUTUMIA MTI WA KRISMASI?
    SEHEMU YA KWANZA

    SOMO:-UKWELI KUHUSU MTI WA KRISMAS
    (CHRISTMAS TREE)
    NA
    MAJIBU YA UFAFANUZI KWA WAPINGA CHRISTMAS
    Ili iwe vyepesi kwetu kulielewa vizuri somo hili Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vinne ambavyo ni:-
    1? HISTORIA YA MTI WA KRISMAS NA UCHAMBUZI WAKE.
    2? KWANINI WAKRISTO TUNATUMIA MTI WA KRISMAS?
    3? VITU VIWI VYA KUEPUKWA KATIKA SHEREHE YA KRISMAS.
    4? MAJIBU YA UFAFANUZI KWA WAPINGA KRISMAS.
    Mstari muhimu wa kukumbuka:-
    ISAYA 60:13:-" Utukufu wa Lebanoni utakujia wewe, (miti ya) mberoshi na mtidhari na mteashuri pamoja; ILI KUPAPAMBA MAHALI PANGU PATAKATIFU, Nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.".
    UTANGULIZI
    Katika kipindi kama hichi cha kusherekea sikukuu ya Krismasi. Moja vitu muhimu sana vinavyotumika katika kuipamba na kuitambulisha sherehe hii ni hichi kinachoitwa "Mti wa Krismas" (Christmas tree). Ambao mti huu ni maarufu sana duniani kote katika kuitambulisha Krismas yenyewe. Kila inapofikia majira kama haya ya sikukuu hii, mti huu huwekwa kama pambo muhimu la Krismasi katika makanisa au majumbani mwetu.
    Mti huu wa Krismas una historia yake hata kabla ya kuingizwa kwa sherehe yenyewe ya Krismas hapo kabla.
    Wako watu wengine kwa mafundisho yao potofu ya kutokuiekewa ile KWELI HALISI YA BIBLIA na kutokuwa na ufahamu mzuri wa kupambanua kujua kipi ni kipi kilicho sahihi na ambacho siyo sahihi kukifuata. Watu hao wapotoshaji wa sikukuu hii, wanapoona wakristo hasa tuliookoka kwenye makanisa ya kipendekoste tunautumia huo mti wa Krismas. Kumekuwa na kelele zao nyingi za kutukashifu imani yetu eti kwa kuutumia huo mti wa Krismas eti tunaabudu miungu ya kipagani ~Tamuz na kufuata desturi za kipagani.
    HIII SIYO KWELI HALISI. Bali ni hila za shetani tu za kupindisha pindisha mambo kihistoria ili kututoa katika msingi wa imani yetu ya kweli. HATUNABUDI KUWA NA UFAHAMU MZURI KATIKA KUIELEWA HISTORIA NA KUIPAMBANUA VYEMA kulingana na kipimo cha kweli ya Neno la Mungu (Biblia ).
    WAKOLOSAI 2:4-8:-"Nasema neno hili, MTU ASIJE AKAWADANGANYA KWA MANENO YA KUSHAWISHI. Maana nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho, nikifurahi na kuuona utaratibu wenu na uthabiti wa imani yenu katika Kristo. Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye shina na wenye kujengwa katika yeye; mmefanywa imara kwa imani, kama mlivyofundishwa; mkizidi kutoa shukrani. ANGALIENI MTU ASIWAFANYE MATEKA KWA ELIMU YAKE YA BURE NA MADANGANYO MATUPU, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo."
    WAEFESO 4:14-15:-" ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. LAKINI TUISHIKE KWELI katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.".
    Kumekuwa na kelele nyingi za mafundisho ya upotoshwaji kwa kigezo kupitia dondoo za kihistoria kuhusu sherehe hii ya Krismasi. Neno la Mungu limetuonya hapo TUSIDANGANYIKE BALI TUIFAHAMU ILIYO KWELI NA KUISHIKA.
    N. B:- Wakristo katika imani yetu ya wokovu hatuongozwi na historia kama dira ya imani yetu. BIBLIA NDIO DIRA YETU NA KIPIMO CHETU. Na historia yoyote ile usahihi wake tutaufuata baada ya kuupima kwa misingi ya Neno la Mungu (Biblia ) inasema nini au inatufundisha nini kuhusu jambo husika! ". Sio lazima jambo hilo litajwe moja kwa moja kama lilivyo, bali Biblia imetupa kanuni zilizoko kwenye maandiko za kupima kila jambo kama ni vyema au sio vema kwa Mungu.
    [ 2 PETRO 1:19; ZABURI 119:105; 2TIMOTHEO 3:15-17].
    Ndiomaana tuko hapa leo ili kujifunza neno la Mungu kwa usahihi. Ili Kupitia katika somo hili tupate ufafanuzi na kuelewa kilicho sahihi kwetu wakristo tuliookoka kukifuata.
    Endelea kufuatilia somo hili mpaka mwisho.
    1? KIPENGELE CHA KWANZA.
    HISTORIA YA MTI WA KRISMAS NA UCHAMBUZI WAKE
    ?? ORIGIN OF THE MODERN CHRISTMAS TREE
    (Christmas tree - Wikipedia)
    Modern Christmas trees originated during the�Renaissance�of�early modern Germany. Its 16th-century origins are sometimes associated with Protestant Christian reformer�Martin Luther, who is said to have first added lighted candles to an�evergreen�tree.
    The first recorded Christmas tree can be found on the keystone sculpture of a private home in�Turckheim, Alsace (then part of Germany, today France), dating 1576.
    While today the Christmas tree is a recognized symbol for the holidays, it was once a pagan tradition unassociated with Christmas traditions.
    Other sources have offered a connection between the symbolism of the first documented Christmas trees in Alsace around 1600 and the trees of pre-Christian traditions. For example, according to the�Encyclop�dia Britannica, "The use of�evergreen trees, wreaths, and garlands to symbolize eternal life was a custom of the ancient Egyptians,�Chinese, and�Hebrews. Tree worship was common among the pagan Europeans and survived their conversion to Christianity in the Scandinavian customs of decorating the house and barn with evergreens at the New Year to scare away the devil and of setting up a tree for the birds during Christmas time."
    During the Roman mid-winter festival of Saturnalia, houses were decorated withwreaths�of evergreen plants, along with other antecedent customs now associated with Christmas.
    The�Vikings�and�Saxons worshiped trees.
    In�Poland�there was an old�pagancustom of suspending a branch of fir, spruce or pine called�Pod?a?niczka�from the ceiling. An alternative to this wasmistletoe. The branches were decorated with apples, nuts, cookies, colored paper, stars made of straw, ribbons and colored wafers. Some people believed that the tree had magical powers that were linked with harvesting and success in the next year.
    In the late 18th and early 19th century, these traditions were almost completely replaced by the German custom of decorating the Christmas tree.
    ?? (Christmas tree - Wikipedia)
    ?? UCHAMBUZI WAKE IKO HIVI.
    Kama ulivyosoma hapo juu . Miongoni mwa wapagani wa ulaya kabla ya kuwa wakristo na suala hili la Krismas kuanza. Hapo mwanzoni kabla, wapagani hao walikuwa na desturi ya Ibada ya kuabudu mimea/miti ya kijani na kuipamba, wakaingiza majumbani mwao. Kwa sababu waliamini kwamba miti hiyo ilikuwa na nguvu za kimiujiza za kuweza kuwalinda na roho ovu , katika kuwapa mavuno na kuwafanikisha katika mwaka ujao. Miti hiyo pia ilishirikishwa na masuala ya sikukuu ya miungu (sarturnalia-mungu wa kilimo). Na hata baada ya wapagani hao kuwa wakristo waliendelea kuwa na imani hiyo juu ya miti.
    Kwa sababu miti hiyo ilitumiwa na wapagani. Sasa JE WAKRISTO KUTUMIA TU MITI HIYO NI KOSA?
    Jibu ni hapana! Kwa sababu gani? Ni muhimu kuelewa vizuri Biblia neno la Mungu inaiita miti hiyo kuwa ni "MITI YA BWANA" yeye ndiye aliyeiumba na kuifanya kuwako mimea yote. Biblia inasema katika ISAYA 41:19-20:-"Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja; ili waone, na kujua, wakafikiri, na kufahamu pamoja, ya kuwa mkono wa BWANA ndio uliofanya jambo hilo. Mtakatifu wa Israeli ndiye aliyeliumba."
    ZABURI 104:16:-" Miti ya BWANA nayo imeshiba, Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda".
    Unaweza kuona! Kumbe hiyo miti siyo ya wapagani, ni ya Mungu. Kwahiyo kama miti ni ya Mungu. Sio kosa sisi wakristo kuitumia. INATEGEMEA TU NI MATUMIZI GANI YA HIYO MITI JINSI TUNAVYOITUMIA ! Kuitumia miti yoyote au mimea yoyote kama kifaa kwa ajili ya matumizi ya kumpa yeye Mungu utukufu sio kosa. Ni halali kabisa!
    Kwa mfano juu ya hilo Biblia inasema :- " Msifuni, jua na mwezi; msifuni, nyota zote zenye mwanga. Msifuni, enyi mbingu za mbingu, na maji mlioko juu ya mbingu........Msifuni BWANA kutoka nchi, Enyi nyangumi na vilindi vyote......Milima na vilima vyote, MITI YENYE MATUNDA na mierezi yote. Na vilisifu jina la BWANA, kwa maana aliamuru vikaumbwa..... " [ZABURI 148:1-13]. "Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, Maana VITU VYOTE ni watumishi wako" [ZABURI 119:91].
    Unaweza kuona! Kumbe MITI nayo ni miongoni mwa vitu vinavyopaswa kutumiwa kumwadhimisha yeye BWANA katika kumtumikia na kumsifu (kumpamba).
    Sasa ni muhimu kuelewa vizuri walichokosea wapagani sio kutumia hiyo miti, bali ni MATUMIZI MABAYA ya hiyo miti. Wao kwa ujinga wao kosa kubwa walilolifanya ni "kuiabudu hiyo miti na kuitumaini kama kinga yao badala ya Mungu aliye hai. Waliiweka imani yao kwenye mti badala ya kwa Mungu aliye juu". Ndiyo kosa!
    Neno la Mungu linatuonya tusiwe na miungu mingine ila BWANA na tena hatupaswi kukitumainia chochote kile badala ya kumtumainia Mungu wetu aliye juu.
    HABAKUKI 2:18-20:-" Sanamu ya kuchora yafaa nini, hata yeye aliyeifanya ameichora? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa uongo, yafaa nini, HATA YEYE ALIYEIFANYA AIWEKEE TUMAINI LAKE, na kufanya sanamu zisizoweza kusema? OLE WAKE YEYE AUAMBIAYE MTI, Amka; aliambiaye jiwe lisiloweza kusema, Ondoka! Je! Kitu hicho kitafundisha? Tazama, kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, wala hamna pumzi ndani yake kabisa. Lakini BWANA yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake."
    KUMBUKUMBU 16:21-22:" Usipande MTI UWAO WOWOTE KUWA ASHERA(mungu) kwako kando ya madhabahu utakayofanya ya BWANA, Mungu wako. Wala usisimamishe nguzo; ambayo BWANA, Mungu wako, aichukia."
    Soma pia [KUTOKA 20:3; ISAYA 44:14-19; ZABURI 52:7-8].
    Ifahamike vizuri kuwa sisi wakristo tuliookoka tunapoitumia miti hiyo ya Krismasi hatuitumii kwa malengo yale kama walivyoitumia wao wapagani . Maana yetu ya kuitumia miti hiyo iko tofauti kabisa na jinsi ilivyokuwa ikitumika kwa wapagani. Sisi hatuitukuzi wala kuiabudu miti hiyo, wala tumaini la imani yetu haiko juu ya mti bali kwa BWANA.
    2? KIPENGELE CHA PILI
    KWANINI WAKRISTO TUNATUMIA MTI WA KRISMAS?
    Ni kwa mambo makuu mawili:-
    (1) Sisi tunautumia mti huu KAMA PAMBO TU la sherehe. Na hata ukiingia makanisani wakati wa majira haya ya Christmas, miti hii hupamba kwenye madhabahu, malangoni n.k. nyumbani mwa Mungu wetu.
    Na jambo hili la KUPAMBA KWA MITI liko ki-biblia pia . Tazama neno la Mungu linavyosema:-
    ISAYA 60:13:-" Utukufu wa Lebanoni utakujia wewe, (miti ya) mberoshi na mtidhari na mteashuri pamoja; ILI KUPAPAMBA MAHALI PANGU PATAKATIFU, Nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.".
    Ndani pia ya hekalu la sulemani alilomjengea Mungu kulikuwamo na miti fulani ya mapambo katika kupapendezesha mahali patakatifu
    [2NYAKATI 3:5-6; 1WAFALME 6:14-18].
    Na si hilo tu. Kuhusu hoja ya kuitumia miti nyakati za sikukuu. Bado hata hapo ni jambo linaloungwa mkono ki-biblia. Sio kosa wala sio upagani. Tazama neno la Mungu linachosema kwa mfano katika
    MAMBO YA WALAWI 23:39-41:-" Lakini siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya BWANA muda wa siku saba; siku ya kwanza kutakuwa na kustarehe kabisa, na siku ya nane kutakuwa na kustarehe kabisa. Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya MITI MIZURI, na MAKUTI YA MITENDE, na MATAWI YA MITI MINENE, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za BWANA, Mungu wenu, muda wa siku saba. Nanyi mtaishika kuwa sikukuu kwa BWANA muda wa siku saba katika mwaka; ni amri ya milele katika vizazi vyenu; mtaishika katika mwezi wa saba."
    Kwahiyo watu wanaotaka kujua uhalali wetu ki-biblia wa kutumia miti nyakati hizi za sikukuu, andiko hilo hapo. Kama watatuita sisi wakristo kwa kutumia miti hiyo eti ni upagani. Hao ni wapumbafu wa kawaida! Hawaijui Biblia kwamba Mungu ndio mwanzilishi wa elekezo la kutumia mti wakati wa sikukuu kwa msingi huo huo pia.
    (2) NI ISHARA YA MTI WA UZIMA KUPITIA KWA YESU KRISTO MWOKOZI
    Kwanini mti wa Christmas unahusishwa na tendo la kuzaliwa kwa Yesu? Hili ni tendo hasa la ufunuo wa rohoni zaidi. Lakini mtu ukiwa mwilini huwezi elewa lolote.
    Iko hivi! Baada ya mwanadamu kuanguka dhambini katika bustani ya Edeni . Alihukumiwa adhabu ya kifo. Na baada ya hapo Mungu alimfukuza kutoka katika bustani ya Edeni. Na hakuweza kuruhusiwa tena kula matunda ya mti wa uzima, Mungu alisema wakila hawa wataishi milele. Biblia inasema Mungu akailinda NJIA YA MTI WA UZIMA, ili mwanadamu asije akausogelea [ MWANZO 3:22-24].
    Dhambi ndiyo iliyotutenganisha na mti wa uzima na kufanya tufe milele. Tulipotea kutoka kwenye njia ya mti wa uzima.
    Sasa ni muhimu kuelewa Yesu Kristo alizaliwa ulimwenguni ili awaokoe wenye dhambi. Tena Alikuja kutufuta na kuokoa kile kilichopotea njia [MATHAYO 1:21; LUKA 19:9-10].
    Sasa Yesu Kristo alipozaliwa ulimwenguni, yeye ndiye aliyekuwa ni njia ya huo mti wa uzima [ YOHANA 14:6; MITHALI 3:18].
    Ndiomaana Mti wa Krismas mara nyingi utakuta umepambwa kwa namna fulani ya mfano wa matunda na nyota/taa zenye mwanga. Nyota/taa juu ya mti huo vinamwakilisha Yesu Kristo mwenyewe [MATHAYO 2:1-11; UFUNUO 22:16; YOHANA 8:12]. Kumbuka Yesu Kristo yeye ndiye njia. Sasa mti huo kupambwa kwa nyota/taa, maana yake inamainisha kuwa Yesu Kristo yeye ndiye njia ya huo mti wa uzima.
    Sasa kwa ujumla wake MTI HUO WA KRISMAS unatufundisha mambo makuu mawili kwamba:-
    (i) Yesu Kristo amekuja kuturudisha kwenye mti wa uzima
    (ii) Na sisi tulio ndani ya Yesu yaani tuliookoka, ndio wenye kibali cha kuishi milele kwa kula matunda ya mti ule wa uzima. Haleluya!
    UFUNUO 22:1-5, 14:-".........Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake"
    UFUNUO 2:7:-" Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, NITAMPA KULA MATUNDA YA MTI WA UZIMA, ulio katika bustani ya Mungu ". Haleluya!
    Ndiyo maana mti wa krismas umekuwa ni alama/nembo muhimu kote duniani katika kuitambulisha Krismas. Hii ndiyo maana ya mti huu na makusudi ya sisi wakristo kuuendelea kuutumia mti huo katika makanisa yetu, majumbani mwetu nakadhalika katika majira haya ya sikukuu.
    MUNGU AKUBARIKI.
    Sehemu ya pili itaendeleaa...........!
    ????????????????????
    Ukipenda kuwasiliana nami kwa ushauri , maombezi na mafundisho zaidi ya masomo ya neno la Mungu. Karibu :-
    Mtumishi wa Mungu aliye hai.
    MWL, REV:-ODRICK BRYSON
    SIMU:- 0759 386 988; 0717 591 466
    Email:- Odrick16@gmail.com.
    Whatsapp group.
    "KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA"
    [ 2 WAKORINTO 2:17 ]

    KWANINI WAKRISTO TUNASHEREHEKEA KRISMAS? = SEHEMU YA KWANZA =

    Image may contain: text
    SOMO:-UKWELI KUHUSU SIKUKUU YA KRISMASI
    NA
    SABABU ZA MSINGI KI-BIBLIA ZINAZOTUFANYA WAKRISTO KUSHEREKEA KRISMASI .
    Ili iwe rahisi kwetu kulielewa vizuri somo hili. Tutajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele vinne ambavyo ni:-
    1. MAANA YA NENO KRISMASI
    2. HISTORIA YA KRISMASI NA TAREHE 25/ DESEMBA
    3. MAMBO YA KUYAELEWA NA KUYAZINGATIA KUHUSU HISTORIA YA KRISMASI
    4. SABABU ZA MSINGI KI-BIBLIA ZA KUWAFANYA WAKRISTO TUSHEREKEE KRISMASI
    Mistari muhimu ya kukumbuka :-
    L U K A 2:9-11:-"Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang’aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana."
    Z A B U R I 118:22-24:"Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa BWANA, Nalo ni ajabu machoni petu. Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA, Tutashangilia na kuifurahia."
    Amen!.
    1/ KIPENGELE CHA KWANZA
    MAANA YA NENO KRISMASI
    KRISMASI (pia Noeli) ni sikukuu ambayo Wakristo wengi husheherekea kuzaliwa kwake mwokozi Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita duniani .
    Kwa kawaida husheherekewa tarehe 25 Desemba katika Ukristo wa magharibi na tarehe 6 Januari katika ule ukristo wa mashariki.
    Kuna majina mawili yaliyo ya kawaida kwa Kiswahili kwa ajili ya sikukuu hii
    Neno KRISMASI linatokana na neno la Kiingereza lenye maana ya "Christ`s Mass" yaani misa au ibada ya Kristo.
    Neno Noeli inatokana na neno la Kiingereza "Noel" (au "Nowell") ambalo limepokewa kutoka lugha ya Kifaransa "No�l". Hilo ni ufupisho wa neno la Kilatini "Natalis (dies)", "(siku ya) kuzaliwa".
    N.B:- IBADA NA SHEREHE YA KUZALIWA KWA YESU (KRISMASI) IKO KI-BIBLIA.
    Hili si suala tu ambalo limetungwa na wanadamu fulani. La hasha! Hili ni jambo ambalo lipo ki-biblia kwa kuanzishwa na Mungu mwenyewe.
    Tukio la kwanza la IBADA NA SHEREHE YA KUZALIWA KWA YESU KRISTO lilifanyika tokea Yesu alipozaliwa. Na watu wa kwanza kabisa kusherekea kuzaliwa kwake walikuwa majeshi ya malaika wa Mungu. Na pia wanadamu pia walimsifu Mungu na kumtukuza kwa kuzaliwa kwake mwokozi Yesu Kristo. Kwa hiyo suala la Krismasi liko ki-biblia
    [ LUKA 2:7-14,20, 25-38].
    2/ KIPENGELE CHA PILI
    HISTORIA YA KRISMASI NA TAREHE 25/DESEMBA
    Tarehe halisi kabisa ya kuzaliwa kwake Yesu haijulikani kwa sababu utamaduni wa Wayahudi wa wakati ule haukuwa na sherehe au kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa.
    Lakini baadaye Ukristo ulienea katika Dola la Roma kati ya mataifa yaliyokuwa na kawaida ya kuzingatia siku ya kuzaliwa. Hivyo ilijitokeza hamu ya kusheherekea pia sikukuu ya kuzaliwa kwake mwokozi Kristo. Ndiyo asili ya sikukuu ya Krismasi.
    Tangu mwanzo wa karne ya 3 BK kuna kumbukumbu ya waandishi mbalimbali waliojadili tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
    Habari za kwanza kabisa za makadirio ya tarehe ya kuzaliwa kwake Yesu zinapatikana kutoka Misri mnamo mwaka 200.
    Mwandishi Mkristo Klemens wa Alexandria alilalamikia udadisi wa wataalamu kadhaa wa Misri waliodai kwamba wamekadiria tarehe hiyo katika mwezi Mei, wengine katika Aprili. Alisema pia kuwa kikundi cha Kikristo cha wafuasi wa Basilides huko Misri walisheherekea Epifania pamoja na kuzaliwa kwake Yesu tarehe 6 Januari.
    Labda kadirio la tarehe ya 25 Desemba pia lina asili katika Misri. Kuanzia mwaka 200 (kwa mara ya kwanza katika maandishi ya Sixtus Julius Africanus) tunasikia kwamba wataalamu wa Misri walifikiri tarehe 25 Machi ilikuwa tarehe ya kufa kwake Kristo na pia siku ya utungaji mimba wake. Kwa kuongeza miezi tisa ya mimba inajitokeza 25 Desemba kama tarehe ya kuzaliwa.
    Inaonekana tarehe 25 Desemba ilijitokeza wakati huo. Kuna taarifa ya mwaka 204 kutoka Ipolito wa Roma kwamba tarehe 25 Desemba ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
    KRISMASI NA SIKUKUU YA SOL INVICTUS
    Wataalamu mbalimbali walidai kwamba Kanisa lilipachika sikukuu ya Kristo kwenye tarehe hiyo kwa nia ya kufanya ichukue nafasi ya sikukuu ya jua kama mungu "Sol invictus" (yaani "Jua lisiloshindika").
    Lakini pengine mambo yalikwenda kinyume, yaani kwamba Makaisari walianzisha sikukuu hiyo, halafu wakaipanga tarehe ya Krismasi ili kushindana na Ukristo uliokuwa bado chini ya dhuluma ya serikali yao lakini ulikuwa unazidi kuenea.
    Aliyeingiza sikukuu ya "Kuzaliwa Jua" (Mitra) huko Roma ni Eliogabalus (kaisari kuanzia 218 hadi 222). Baadaye kaisari Aurelianus akaithibitisha rasmi mwaka 273, hatimaye ikahamishiwa tarehe 25 Desemba.
    Wakati wa kaisari Licinius (308-324) sikukuu hiyo ilikuwa ikiadhimishwa bado tarehe 19 Desemba.
    Mwandishi wa kikatoliki MARIO RIGHETTI kwa utii kabisa anakubali kwamba, " ili kuwezesha kukubalika imani kikristo kwa wapagani , Kanisa la Roma (chini ya mfalme Constantinel aliyeongoka na kubatizwa kuwa mkristo), WAKAIGEUZA KUTOKA sikukuu ya kipagani ya kumpa heshima " Invincible sun" Mithra na mshindi wagiza , wakaona ni busara Desemba 25 kuwa ni sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo".
    ( Rejea :- Historia ya mwongozo wa kiliturujia, 1955, vol. 2.P.67).
    Kutoka Roma, uliokuwa mji mkuu wa Dola la Roma, sherehe ya 25 Desemba ilienea kote katika Ukristo.
    Wakristo wengi husheherekea tarehe 25 Desemba (Wakatoliki na sehemu ya Waprotestanti na Waorthodoksi). Kati ya Waorthodoksi kuna tarehe nyingine, hasa 6 Januari kutokana na tofauti katika kalenda."
    Mwisho wa kunukuu
    3/ KIPENGELE CHA TATU
    MAMBO YA KUYAELEWA NA KUYAZINGATIA KUHUSU HISTORIA YA KRISMASI.
    (1) Kama tarehe 25 Desemba hapo mwanzoni ilikuwa ni sikuu ya kipagani . Halafu Wakaibadilisha kutoka katika imani ya kipagani badala yake ili ichukue nafasi ya kusherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
    Jambo hilo ni sahihi kabisa mbele za Mungu.
    Na katika jambo hilo. Ni ROHO MTAKATIFU aliyelitumia kanisa la Roma chini ya mfalme Constantinel kuibadilisha sikukuu ya kipagani iliyokuwepo , badala yake iwe Chrismasi.
    Tendo hilo ni sawa na mtu kumtoa gizani na kumleta kwenye Nuru halisi. Kumtoa katika njia yake upotevu ili kumleta sasa katika njia sahihi ya kweli iliyoonyokaa.
    Hakuna tatizo la tarehe 25 Desemba ilyobadilishwa kutoka kwenye sikukuu ya upangani, ili ije kuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Krismas). Jambo ni sahihi kabisa. Kwa mfano Biblia inasema juu ya hilo katika
    MATENDO 26:16-18:-"BWANA akaniambia, mimi ni Yesu.... Lakini inuka , usimame kwa miguu yako, maana nimekutokeaa kwa sababu hii , nikuwekee wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako; nikikuokoa na watu wako, na watu wa mataifa, AMBAO NAKUTUMA KWAO; UWAFUMBUE MACHO YAO, NA KUWAGEUZA WAIACHE GIZA NA KUILEKEA NURU, waziache na nguvu za shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu Mimi".
    (2) SIKU ZOOTE NI ZA MUNGU NA HAKUNA SIKU YA SHETANI.
    Mtu anayeipinga sherehe ya sikukuu ya krismasi kwa kudai kwamba eti 25 Desemba ilkuwa ni siku ya sikuu ya kipagani. Na hivyo hana haja ya kusherekea Krismasi.
    Mtu wa namna hiyo. Tatizo lake hajui wala kuelewa anachokisema badala yake anajidanganya mwenyewe na kujipotosha. Uelewa wake ni mdogo!
    Ni muhimu kufahamu vizuri . Siku zote ni za Mungu na hakuna siku ya shetani. Inategemea tu na mtu mwenyewe binafsi anaitumia vipi siku hiyo kwa kufanya mambo ya kumpendeza Mungu au mambo ya shetani !! Lakini hakuna siku maalumu ya shetani . Bali Siku zote ni mali ya Mungu mwenyewe. Na anataka tuzitumie siku zote kumsifu, kumwabudu, kumtukuza na kumpendeza yeye .
    Kwa mfano Biblia inasema juu ya hilo katika
    MWANZO 1:14:-" MUNGU AKASEMA, na iwe mianga katika Anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka."
    ZABURI 105:4:-" Mtakeni BWANA na nguvu zake, utafuteni uso wake SIKU ZOTE".
    YOHANA 8:29:-" Naye aliyenipeleka yu pamoja nami: hakuniacha pekee yangu; kwa sababu NAFANYA SIKU ZOOTE yale yampendezayo ".
    MATENDO 2:46-47:-" NA SIKU ZOOTE kwa moyo mmoja walidumu ndani ya Hekalu......... wakimsifu Mungu,, na kuwapendeza watu woote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa".
    Unaweza kuona! Tusimpe siku shetani. SIKU ZOOTE NI ZA MUNGU, maana yeye ndiye aliyezifanya kuwako. . Kilichobaki ni kwa mtu mwenyewe tu binafsi anaitumia vipi hiyo siku kufanya mapenzi ya nani ya Mungu au ya shetani ?!
    Na kwa maana hiyo. Kama tarehe 25 Desemba ilikuwa ni siku ya sikukuu ya wapagani. Hilo lilikuwa ni kivyaoo wenyewe kwa upotofu wa mioyo yao wenyewe walivyoamua kuitumia hiyo kufanya mambo yao ya kipangani. Lakini hilo Bado haimanisha kwamba 25 Desemba basi siku hiyo ni ya wapagani. La hasha !! Itakuwa ni ya kipagani kwetu wakristo iwapo kama tutashiriki mambo yao kipagani kama walivyokuwa wakifanya wao. Lakini siku hii tukiitumia tofauti na jinsi walivyoitumia wao. Hii siyo siku tena ya kipagani, bali ni takatifu kwa Bwana.
    TAREHE 25 DESEMBA kwetu sisi wakristo tuliookoka tunaitumia siku hiyo maalumu kwaajiri ya kumuadhimisha BWANA kwa kukumbuka tukio kubwa mno la kuzaliwa kwake Yesu Kristo mwokozi wa ulimwengu. Biblia inasema hivi katika
    WARUMI 14:4, 6-7:-" Wewe u nani umuhukumuye mtumishi wa mwingine ? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha. YEYE AADHIMISHAYE SIKU , HUIDHIMISHA KWA BWANA; naye alaye hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu ; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu . Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwenu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake."
    Katika siku hii ya tarehe 25 Disemba, tunaitumia kumwadhimisha Bwana, ni siku maalumu na ya kipekee ambayo wakristo tunaitumia kutafakari mambo mengi ya ukuu wa Mungu wetu na upendo wake kwa wanadamu. Tunamshangilia , tunamsifu na kumtukuza, tunamwimbia na kumshukuru Mungu Baba yetu na MWOKOZI wetu Yesu Kristo aliyekuja kutuponya, kutuokoa na kutukomboa wanadamu kutoka kwenye gereza la Ibilisi.
    " Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa, ya kwamba YESU KRISTO ALIKUJA ULIMWENGUNI AWAOKOE WENYE DHAMBI; ambao wa kwanza wao ni Mimi".
    [YOHANA 3:16-17; LUKA 2:28-34; 1TIMOTHEO 1:15-16].
    IKiwa watu wengine wanaweza kukumbuka kusherekea kuzaliwa kwao na wakamshukuru Mungu. Basi ni jambo zuri na bora zaidi kupita yoote kukumbuka kusherekea kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo.
    (3) HATUSHEREKEI TAREHE BALI KUMBUKUMBU YA TUKIO LA KUZALIWA MWOKOZI WETU ULIMWENGUNI.
    Biblia inasema
    YOHANA 21:25:-" kuna na mambo MAMBO MENGINE MENGI aliyoyafanya Yesu; ambayo kama yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa. Lakini hizi zimeandikwa; ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima wa milele kwa jina lake".
    Nini maana yake? Ingawa haijulikani tarehe na mwezi maalumu aliyozaliwa Yesu Kristo au kuandikwa kwenye Biblia. Ndiyo hatuoni! Kwa sababu mbele za Mungu tarehe ya kuzaliwa Yesu sio jambo la msingi, bali lilo la msingi ni TUKIO LA KUZALIWA KWA YESU, ndiomaana Mungu akaliandika. Matukio mengi aliyoyafanya Yesu hayakuandikwa na Mungu, lakini tukio lake hili la kuzaliwa limeandikwa. Hii ni kwa sababu Mungu anataka kutufundisha, tukio hili ni la msingi sana kwetu kulitafakari.
    Kujua tarehe ni ipi hilo sio jambo la msingi kwetu kama ambavyo halikuwa la msingi kwa Mungu . Narudia tena Hoja ya msingi kwetu hapa sio tarehe ngapi mwezi gani , bali HOJA YA MSINGI NI KWAMBA YESU KRISTO AMEZALIWA. Full stop. Kwa sababu lilo la msingi kwetu sio tarehe bali ni kumbukumbu ya tukio lilotendeka la kuzaliwa kwa Yesu Kristo ulimwenguni .
    Narudia tena kusisitiza unielewe vyema. La msingi kwetu hapa wakristo hatureshekei tarehe, bali tunasherekea kumbukumbu ya tukio la kuzaliwa kwake Yesu Kristo.
    Mbali hata na tarehe 25 Desemba, siku zote na wakati woote tungepaswa kusherekea kukumbuka kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo ulimwenguni . Biblia inasema katika
    MATHAYO 28:20:-"Na kufundisha kuyashika yoote niliyowaamuru ninyi; NA TAZAMA , MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, hata ukamilifu wa dahari ".
    Kwa maana hiyo hiyo hata tunaposherekea 25 Desemba kuzaliwa kwake , bado Yesu yupo pamoja nasi.
    4/ KIPENGELE CHA NNE
    SABABU ZA MSINGI KIBIBLIA ZA KUWAFANYA WAKRISTO TUSHEREKEE KRISMASI.
    Ni kwa sababu zifuatazo:-
    (1) Ni taarifa ya agizo la Mungu kwetu kupitia kwa mkono wa malaika.
    Biblia inasema katika LUKA 2:10-14:-" Malaika akamwambia, msiogope; kwa kuwa Mimi nawaletea HABARI NJEMA YA FURAHA KUKUU ITAKAYOKUWAKO KWA WATU WOOTE; Maana Leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwaajili yenu, mwokozi Ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia".
    Unaweza kuona , hata wingi wa jeshi la mbinguni la malaika waliungamana pamoja na wanadamu kufurahia kwa kusherekea kuzaliwa kwake YESU KRISTO.
    ISAYA 9:6-7:-" MAANA KWA AJILI YETU MTOTO AMEZALIWA, tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, mfalme wa Amani......."
    Mtu yoyote ambaye anapinga kusherekea sikukuu za Krismasi. Mtu wa namna hiyo bila shaka anasema kwa kutumiwa na roho ya shetani bila kujitambua.
    (2) Ni Agizo la Biblia kwamba (SIKU YA KRIMASI) tuishangilie na kuifurahia.
    Biblia inasema katika
    ZABURI 118:22-24:-" Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa BWANA, nalo ni la ajabu machoni Petu; SIKU HII NDIYO ALIYOIFANYA BWANA, TUTASHANGILIA NA KUIFURAHIA".
    Jiwe kuu la pembeni anayetajwa hapo ni Yesu Kristo (2 Waefeso 2:20). Na siku inayotajwa hapo ni siku yake ya kuzaliwa ( Christmas).
    Na Biblia inasema tena katika ZABURI 70:4:-" Washangilie, wakufurahie, wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako waseme daima, Atukuzwe Mungu".
    Sasa Yesu Kristo alipozaliwa, yeye ndiye aliyefanyika wokovu wa Mungu wetu [LUKA 2:27-32; 1KOR 1:30]. Na ndiomaana wakristo Leo tunaidhimisha siku hiyo ya Krismas kwa kushangilia na kuifurahia, kwa kuzaliwa kwake mwokozi wetu Yesu Kristo , aliyetupatia wokovu. HALELUYA!!
    (3) Kusherekea Krismasi sio dhambi wala kosa, bali ni mapenzi ya Mungu kwetu.
    Biblia inasema katika
    1 WAKORINTO 10:-" Basi , mlapo , au mnywapo, au MTENDAPO NENO LOLOTE, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu".
    WAKOLOSAI 3:17:-" Na KILA MFANYALO, kwa neno au kwa tendo, FANYENI YOOTE katika jina la Bwana Yesu, mkishukuru Mungu Baba kwa Yeye".
    Ndiomaana Siku ya Krismasi mbali tu na kusherekea inavyostahili. Lakini bado imekuwa ni siku maalumu na ya kipekee ambayo mambo mengi mema yanayafanyika ya kuumpa Mungu sifa, heshima na utukufu na shukrani tele, kwetu sisi wakristo tuliookoka. Na Mungu anaonekana kwa namna ya kipekee siku hii pia akiwaponya, akiwaokoa, akiwagusa na kuwatembelea watu wengi.
    (4) SIKUKUU YA MWANDAMO WA MWEZI NI KIVULI CHA SIKUKUU YA KUZALIWA KWA YESU KRISTO LEO (KRISMAS).
    Nyakati za Agano la kale watu waliagizwa kusherekea sikukuu ya Mwandamo wa mwezi, mara tu mwezi ulipoanza kuandama . Watu walisherekea .
    Biblia inasema Katika ZABURI 81:3-4:-" PIgeni panda mwandamo wa mwezi, wakati wa mbalamwezi, SIKUKUU YETU. Kwa maana nu sheria kwa Israeli, ni hukumu ya Mungu wa Yakobo ".
    Ni muhimu kuelewa Sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi ilikuwa ni picha/mfano/ kivuli cha Yesu Kristo atakayekuja baadaye .
    Biblia inasema katika WAKOLOSAI 2:16-17:-" Basi , mtu asiwahukumu ninyi kwa vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au MWANDAMO WA MWEZI, au sabato ; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo ; bali mwili ni wa Kristo ".
    Sasa Yesu Kristo Leo yeye ndiye anayeitwa ni Nuru halisi ya ulimwengu. Biblia inatuambia katika YOHANA 8:12:-"Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima".
    [ Soma pia YOHANA 1:9-10].
    Sasa YESU KRISTO KAMA NURU HALISI iliyokuja katika ulimwengu. Mara tu Wakati huo Alipozaliwa Yesu Kristo katika ulimwengu huu uliojaa Giza . Ilikuwa ni sawa na kama nuru ndogo iliyochomoza na kuanza kuangaza katika ulimwengu huu uliojaa Giza. Na kwa maana hiyo kama katika Agano la kale walivyosherekea sikukuu ya Mwandamo wa mwezi. Jambo hilo lilikuwa ni kivuli tu cha Sherehe ya sikukuu ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo, tunapoisherekea leo . HALELUYA !!
    (5) Tunasherekea Krismas , kwa sababu Yesu Kristo alikuja ili tuwe na uzima tena tuwe nao tele.
    Biblia inasema YOHANA 10:10:-" Mwivi (shetani) haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; Mimi Yesu nalikuja ili wawe na uzima tena wawe nao tele".
    Kabla ya Yesu Kristo hajaja duniani kwa kuzaliwa kwake. Hapo mwanzoni shetani alituonea , alitutesa na kutuua bila kuwa na msaada wowote ule.
    Lakini kwa kuja kwake Yesu Kristo duniani. Alikuja ili atuponye, atuokoe na kutuweka huru mbali na dhambi na vifungo vya shetani . Na kwa kila allitajaye jina la BWANA anaponywa na kuolokewa.
    MATENDO 10:38:-" Habari za Yesu wa Nazaret, jinsi alivyomtia Mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu; naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na KUPONYA WOOTE WALIOONEWA NA IBILISI; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye ".
    LUKA 9:1-2:-" Akawaita wale Thenashara, AKAWAPA UWEZO NA MAMLAKA juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, NA KUPONYA WAGONJWA".
    [ LUKA 10::17-19 ]
    Kama Yesu asingezaliwa dunia Leo . Maana yake ni kwamba uzima , uponyaji wala wokovu tusingeupata.
    Lakini ashukuruliwe Mungu Baba kwa kuwa kwa kuzaliwa kwake Yesu Kristo ametupa uwezo na mamlaka, tena tumeponywa na kuweka huru mbali na vifungo vyote vya Ibliisi. Neno la Mungu linasema katika
    WAKOLOSAI 1:12-14:-" Mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. Naye alituokoa katika nguvu za Giza , AKATUHAMISHA NA KUTUINGIZA KATIKA UFALME WA MWANA WA PENDO LAKE; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi".
    (6) Tunasherea siku ya Krismas , kwa sababu kwa kuzaliwa kwake Yesu Kristo duniani. Ametufanya sisi mataifa mengine yoote nje na Israeli, ambao hapo mwanzo tulikuwa hatuna tumaini wala MUNGU duniani. Lakini kupitia kuja kwa Yesu Kristo duniani, tumehesabika pamoja na Israel kuwa sehemu ya urithi mmoja wa watoto wa Mungu.
    Maana hapo mwanzo TAIFA LA MUNGU NA WATU WAKE YEHOVA WALIKUWA NI WA ISRAELI TU . Sisi mataifa mengine tulikuwa hatuna tumaini wala Mungu duniani. Maana yake Tulikuwa ni watu wa kufa tu na kwenda Motoni moja kwa moja.
    kama Yesu Kristo asingezaliwa , sisi mataifa mengine nje na Israeli, tungebaki kuwa tumetengwa mbali na uso wa Mungu milele .
    Lakini kwa kuja kwake Yesu Kristo duniani alipozaliwa. Tumepatanishwa sisi na Israel kuwa kitu kimoja , SISI SOTE NI WATOTO WA MUNGU. Hakuna cha myahudi wala myunani. Biblia inasema katika WAEFESO 2:11-21; WAGALATIA 3:26-29; 1 PETRO 2:5-10.
    NB.
    Kwa sababu hiyo . Hizo ndizo sababu kuu za msingi ki-biblia zinazotufanya WAKRISTO TUSHEREKEE CHRISTMAS.
    Kuamua kusherekea Krismasi au kuacha kusherea yote mawili sio dhambi . kwa maana hakuna Andiko linalotukaza kutoshetekea Krismasi wala hakuna sheria ya Andiko linamlolazimisha mtu kusherekea Krismasi.
    Kwahiyo kama utapenda basi sherekea kwa utukufu wa Mungu. Vema. Na kama wewe moyoni mwako kwako haupendi kusherekea Krismasi. Basi acha!
    La msingi tusikwazane, tusinyosheane vidole wala kuhukumiaana kwa jambo hili la Christmas. Kila mmoja atumie Uhuru wa imani yake, maadamu kwa kufanya hivyo hatendi dhambi.
    Biblia inasema katika WARUMI 14:10-13, 19:-" LAKINI WEWE JE! MBONA WANUHUKUMU NDUGU YAKO? Au WEWE JE MBONA WAMDHARAU NDUGU YAKO ? kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu . kwa kuwa imeandikwa , kama niishivyo asema Bwana, kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utamkiri Mungu. Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu. BASI TUSIZIDI KUHUKUMIANA, bali afadhali toeni hukumu, MTU ASITIE KITU CHA KUMKWAZA NDUGU AU CHA KUMWAGUSHA. Basi kama ni hivyo , na tufuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana".
    La msingi tusihukumiane wala kukwazana kwa wewe unayependa kusherekea Christmas na kwa wewe ambaye husherekei. Bado wote tunabakia ni watoto wa Mungu na tunakwenda mbinguni.
    Na la msingi kuliko yote tunaposherekea sikukuu ya Christmas. Ni YESU KRISTO AZALIWE UPYA NDANI YA MIOYO YETU. Tubadilike kitabia , kiusemi, kimavazi , kimwenendo na kufanyika kuwa viumbe vipya machoni pa Mungu wetu.
    2 WAKORINTO 5:17:-" Hata imekuwa , MTU AKIWA NDANI YA KRISTO AMEKUWA KIUMBE KIPYA; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya".
    Na Hakuna maana yoyote ya kusherekea Christmas hii kama bado wewe hujaokoka. MPE YESU MAISHA YAKO NDUGU YANGU , AKUOKOE . Maana neno la Mungu linasema
    MATHAYO 1:21:-" Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, YEYE NDIYE ATAKAYEWAOKOA WATU WAKE NA DHAMBI ZAO".
    Mungu awabariki wote kwa kila asomaje ujumbe wa Neno hili.
    Nakutakia HERI YA KRISMASI NA MWAKA MPYA .
    Ukipenda kuwasiliana nami kwa ushauri , maombezi na mafundisho zaidi ya masomo ya neno la Mungu. Karibu :-
    Mtumishi wa Mungu aliye hai.
    MWL, REV:-ODRICK BRYSON
    SIMU:- 0759 386 988; 0717 591 466
    Email:- Odrick16@gmail.com.
    Whatsapp group.
    "KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA"
    [ 2 WAKORINTO 2:17 ]
    Shalom,
    By permission Rev Odrick Bryson
    Max Shimba Ministries Org,

    Saturday, December 22, 2018

    ROHO MTAKATIFU NI PARAKLETOS IKIMAANISHA NI MSAIDIZI WETU


    Image may contain: text




    Mfariji/ Mshauri / Msaidizi: (Isaya 11: 2; Yohana 14:16; 15:26; 16: 7) Maneno yote matatu ni tafsiri ya Kigiriki parakletos, ambayo tunapata "Paraclete," jina jingine la Roho Mtakatifu. Yesu alipokwenda, wanafunzi wake walikuwa na wasiwasi sana kwa sababu walikuwa wamepoteza uwepo wa ufariji wake. Lakini aliahidi kutuma Roho Mtakatifu kuwatuliza, kuwafariji, na kuongoza wale ambao ni wa Kristo. Roho Mtakaatifu pia "anatoa ushahidi" na roho zetu kwamba sisi ni wa Yeye na kwa hiyo hutuhakikishia wokovu.
    Kabla ya kuondoka, Yesu alimtambulisha Roho Mtakatifu kwa wanafunzi wake. Katika utambulisho huu aliourudia sehemu kadhaa, tunapata kujifunza juu ya umuhimu wa Roho wa Mungu. Huu ni moja ya mistari ambayo Yesu anamtambulisha Roho Mtakatifu kwetu:
    Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. Mkinipenda, mtazishika amri zangu.Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. (Yohana 14:14-17)
    Yesu anaahidi Roho Mtakatifu: Yohana 14:15-31
    Hatua muhimu mwishoni mwa sura ya 14 ni ahadi ya kwamba wanafunzi watapokea Roho Mtakatifu kama Msaidizi wao. Neno 'Msaidizi', katika parakletos ya Kigiriki, lina maana nyingi. Wanasayansi wamejaribu kutambua asili yake katika historia ya dini kwa kusoma maandiko kutoka kwa dini mbalimbali. Mfano unaofanana unaonekana katika fasihi za Kiyahudi, na pia kati ya Wayahudi wa Qumran, na baadaye katika maandiko ya Mandaa. Utafiti wa maandiko haya haujawasaidia sana. Neno hilo ni la zamani, lakini somo ni jipya.
    Hata hivyo, Roho Mtakatifu ni Mchungaji (tazama Ayubu 33:23), Msaidizi (1 Yohana 2: 1), Msaidizi na Msaidizi (hasa katika sehemu tunayozungumzia sasa) kwa Wakristo. Tunapojifunza kutoka kwa sehemu ya sasa, Roho Mtakatifu alikuwa, juu ya yote, alitumwa ili kuwasaidia Wakristo baada ya Yesu hakuwa tena kimwili miongoni mwao. Hivi karibuni Yesu alikuwa amekwenda, lakini kupitia Msaidizi, wale walio wake wanaweza bado kumwona. Tofauti na "watu wa ulimwengu", wafuasi wa Yesu wanaelewa kwamba Baba yuko ndani ya Mwanawe, Mwana ni ndani ya Baba, Yesu ni yeye mwenyewe, na yeye mwenyewe ni ndani ya Yesu - hii inatuchukua sisi juu ya mambo ya kiteolojia. Dunia haijui Msaidizi, wala haitamjua.
    Kipengele kingine kikubwa katika kifungu hiki, kinachoonekana mara kadhaa, hujali utii wa waumini kushika maneno ya Mwalimu wao. Ikiwa tunampenda Yesu, ni kuonekana katika matendo yetu halisi. Tunataka kutii mapenzi ya Bwana ambayo ametuonyesha. Kuna msisitizo mkubwa sana juu ya haya yote katika maandishi ya Yohana na (tazama mfano 1 Yohana 2: 7-11). Upendo wetu kwa Bwana siyo dhana tu, lakini inamaanisha kwamba tunatenda kwa maneno yake. Hatuwezi kumpenda Yesu na, wakati huo huo, tusijali neno lake.
    Katika mistari ya mwisho ya sura hii, giza huanza kuanguka juu ya utukufu. Saa iko karibu, Yesu yuko karibu kusulubiwa. Utii wa Mwana kwa mapenzi ya Baba unaonyeshwa kwa ukweli kwamba Yesu mwenyewe ni wa kweli kwa maneno, ambayo alianza tu kutangaza. Upendo kwa Baba hupimwa kwa vitendo halisi, na hivyo Bwana huweka njia ya msalaba.
    Yafuatayo ni mambo mbalimbai ambayo Biblia inatufundisha kuhusu nafsi ya Roho Mtakatifu.
    Parakletos (mfariji, yeye anayekuwa pamoja nasi - Yohana 14:16, 26; 15:26)
    Hufahamu mawazo ya ndani ya Mungu (1 Korintho 2:10-11)
    Huongea nasi (Matendo 13:2; Ebr 3:7)
    Hutufundisha (Yohana 14:26)
    Kama mzazi, ili kwamba tusiwe yatima (orphanos kwenye Kigiriki - Yohana 14:18)
    Hutuongoza (Yohana 16:13)
    Hutufundisha (Yohana 14:26; 1 Korintho 2:13)
    Huishi ndani yetu (1 Korintho 3:16; 2 Tim 1:14; Rum 8:9, 11; Efeso 2:22)
    Mioyoni mwetu (2 Korintho 1:22; Galatia 4:6)
    Hutuombea (vitu visivyo na uhai haviombi au kuombea - Rumi 8:26-27)
    Anaweza kufanyiwa jeuri (Ebrania 10:29)
    Humshuhudia Kristo (Yohana 15:26)
    Anao ufahamu (Rumi 8:27)
    Anaweweza kuhuzunishwa (Isaya 63:10; Efeso 4:30)
    Hufanya maamuzi (1 Korintho 12:11)
    Hupenda (Rumi 15:30)
    Anaweza kupendezwa na mambo (Matendo 15:28)
    Huchunguza mambo ya ndani ya Mungu (1 Korintho 2:9-10)
    Huugua (na kwa ajili hiyo hutujali - Rumi 8:26)
    Shalom,
    Max Shimba mtumwa wa Yesu kristo Mungu Mkuu. Tit0 2:13

    Thursday, December 20, 2018

    SHETANI NI NANI?


    SHETANI NI NANI?
    JE, SHETANI ALIUMBWA NA MWENYEZI MUNGU KAMA WANAVYO DAI WAISLAM?
    Biblia humwita “mungu wa ulimwengu huu.” Lakini alitoka wapi? Je Mungu alimuumba kama alivyo? Je, yeye ni roho aliyeanguka? Haya hapa ni majibu kutoka katika Neno la Mungu!
    Biblia inamfafanua Shetani kuwa kiumbe halisi ambaye yuko katika makao ya roho. (Ayubu 1:6) Inatueleza kuhusu sifa zake za ukatili kutia ndani matendo yake ya uovu. (Ayubu 1:13-19; 2:7, 8; 2 Timotheo 2:26)
    Asili ya Shetani ni wapi au nini?
    Tangu mwanzo Shetani hakuwa anaitwa Shetani, yaani hapakuapo na kiumbe kilichoumbwa na kuitwa Shetani. Alikuwa ni “mwana wa asubuhi” (Isa.14:12) yeye pamoja na jeshi lingine la mbinguni,waliumbwa wote wakiwa wakamilifu katika njia zao zote ( Ezekieli. 28:14-19). Kulikuwa na amani na umoja Mbinguni. Kisha mambo yakaharibika. Biblia haiko wazi sana juu ya swala hili ni nini hasa kulitokea na kwa namna gani, ila uovu au kutokumtii Mungu kulioneka kwa Lucifa. Mwishowe alifukuzwa kutoka Mbingini, pamoja na jeshi lake lote lililoasi, wakafukuziwa mbali kabisa kutoka mbinguni na kutupwa, na wanazunguka zunguka katika nchi (duniani).
    (Wakolosai 1:15) Mungu aliumba malaika. (Ayubu 38:4-7) Wote walikuwa wakamilifu na waadilifu. Hata hivyo, mmoja kati ya malaika hao aliitwa Lusifa ndie akaja kuwa Shetani.
    Malaika huyo hakuitwa Shetani alipoumbwa. Jina hilo ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu. Ni sawa na kusema, Mungu hakuumba majambazi, bali Majambazi ni sifa ambayo mtu anaipata anapo fanya unyang'anyi kwa kutumia nguvu. Mungu wetu hakuumba uovu.
    Kiumbe huyo wa roho akaanza kukuza hisia za kiburi na za kushindana na Mungu. Alitaka wengine wamwabudu yeye. Yesu alipokuwa hapa duniani, Shetani alimtaka Yesu ‘amfanyie tendo la ibada.’—Mathayo 4:9.
    Shetani alitupwa na malaika wake?
    Ufunuo 12: 7-21 Imeandikwa “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. 9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. 10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya MwanaKondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. 12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
    Ufunuo 12 husema juu ya Shetani na pepo wake wabaya “walitupwa katika nchi” (fu. 13). Kwa hakika sura hii imepachikwa katikati ya kitabu cha Ufunuo, na ni muhtasari mfupi wa historia ya Kanisa la Agano Jipya.
    Fungu la 3 linamwelezea Shetani kama “joka” aliye “kokota theluthi ya nyota za mbinguni na kuziangusha katika nchi” (fu. 4). Kumbuka kwamba “nyota” hizi zilikuwa ni theluthi ya malaika wote waliokuwa chini ya Nyota ya alfajiri kabla hajaasi.
    2 Petro 2:4 hutoa kiashiria kingine juu ya huku “kutupwa chini” kwa Shetani na malaika zake “aliowakokota pamoja” naye. Angalia: “Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa [Shetani hakuwa malaika pekee aliyeasi], bali aliwatupa shimoni.” (Neno la Kigiriki hapa ni tartaros na linamaanisha aidha “gerezani” ama “kizuizini”—hii ni dunia yenyewe.) Pepo hawa wabaya pamoja na Shetani “wanalindwa hata ije hukumu,” wakiisha “kutiwa…katika vifungo vya giza.” Hii inafunua kwamba Mungu aliwatia katika gereza hili la giza pepo wengine wengi walioanguka waungane na “mkuu wa giza.”
    Ufunuo 12:7-9 hueleza, kwa undani, lini Shetani na pepo wake wabaya watatupwa hata nchi kwa mara ya mwisho wasipate tena kibali cha kuingia mbinguni. Mafungu ya 12-14 yanaonyesha kwamba mwitikio wa ibilisi ni hasira kuu. Wakati huu wa kutisha unakuja kwa ulimwengu mzima hapo mbeleni kidogo!
    Shetani anatushawishi vipi?:
    Asili ya shetani ni roho mchafu. sio kitu kinachoweza kuonekana, lakini ni kitu ambacho tunaweza kukifahamu kwa kusoma Biblia. Biblia ilitolewa kama Neno la Mungu. Yesu Kristo alikuja kwetu kama mfano hai wa Neno la Mungu. Ni katika kusoma Biblia tu, ndipo tunaweza kutambua mazuri na mabaya, kujua juu ya utauwa, au kutambua haki na imani ya kweli, na yapi yaliyo ya shetani. Na ni nini yaliyo Mapenzi ya Mungu. Sio jambo tunaloweza kulifahamu tangu kuzaliwa au ambalo tukiwa tunazaliwa tunakuwa tunalifahamu.Wengi kati yetu tunafanya uchaguzi mbaya kwa sababu hatusomi Biblia na kulifuata Neno la Mungu, sawa sawa na Mapenzi ya Mungu.
    Shetani ni roho mchafu na anatushawishi kiroho, njia moja ya kumuona shetani ni katika mawazo yetu, akilini mwetu. Tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu. Shetani sio kitu kilichoandikwa, sio kitu tunachoweza kukiona kwa macho, kukisikia, kugusa, kuonja au kunusa. Mungu ni kama hivyo kwa namna fulani na malaika wote na hata shetani pia.
    Waefeso. 2:2 Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumufuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi.
    Mwisho wa Shetani ni wapi?
    Ufunuo 20:2 Akamshika yule joka, yule joka wa zamani, ambaye ni ibilisi na shetani, akamfunga miaka elfu.
    Shetani atafungwa na hataweza kumshawishi mtu tena mwanadamu yeyote kwa muda miaka elfu moja kisha atafunguliwa tena (Ufunuo 20:7) mwisho wa hiyo miaka elfu moja. Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, shetani atafunguliwa, atoke kifungoni kwake; na kutambua ya kwamba ameshidwa; ni mnyonge hawezi kupata nguvu pasipo Mungu, na kuna vita vingine tena vitakavyotokea dhidi ya Mungu kama shetani atakavyowadanganya nakuwashawishi watu tena kama anavyofanya wakati huu wa sasa
    Shetani anatupwa katika shimo (Isaya 14:15-17). Na wale wanaomwona washangaa na kustajabu ya kwamba huyu ndiye yule aliyeleta matatizo yote ya duniani na huzuni na masikitiko yote. Ghafla anabadilika na kutokuwa tena yule mnyama wa roho chafu ya kutisha na ya kuogofya ambaye hapo mwanzo alikuwa ni wa kuogofya na wa kutisha, aliyeweza kusababisha watu waamini ya kuwa ndivyo alivyo. Yeye ni mhongo aliyouadhibu uumbaji wa Mungu uliyofundishwa kumkili Mungu katika nguvu zake ambaye Yeye ni Mweza.
    Ufunuo 20:10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
    Hata hivyo shetani atatambua ya kuwa Mungu alikuwa ni wa haki wakati wote. Hili neno “shetani” maana yake ni mshitaki. Shetani ataacha kuwa mshitaki, hatakuwa shetani tena. Hatawashitaki tena ndugu, kama alivyowashuhudia kwa uongo. Mashitaka yamekwisha lakini yatakuwepo daima kama kumbukumbu. Adhabu gaini kwa shetani ! Mashitaka yake hayatasahaulika. Yatakumbukwa daima kama aliyemvunjia Mungu heshima, na kwa kuudan ganya ulimwengu. Atapata mateso yake kwa sababu atatambua makosa yake. Msamaha wetu ni muhimu sana katika kurudisha utukufu na heshima yake na katika maisha mema.
    Mwishowe, kila mtu atamtambua Kristo kuwa ni Mfalme na Kuhani Mkuu anayeunganisha dunia yote na kumwakilisha Mungu. Jambo hili litakapokamilika vita kati ya mema na mabaya vitakuwa vimekwisha. Ushawishi wa shetani utakuwa umekwisha. Mauti yamekwisha. Makanisa ya uongo na manabii wa uongo na unabii wa uongo utakuwa umekwisha. Yote yatakuwa yamekwisha; wote watatambua Mpango wa Mungu na watakuwa sehemu ya Familia ya Mungu. Wote watakiri ya kwamba Mungu alijua yote, na anajua yote, na daima atajua yote.
    Shalom,
    Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13
    Image may contain: 1 person, text

    Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ

    Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction ...

    TRENDING NOW