Tuesday, November 24, 2015

JE MTU ALIYEOKOKA ANAWEZA AKAVAMIWA NA ROHO ZA GIZA ?

1. Je, anaweza kuwa chini ya vifungo, wakati Yesu alimaliza yote Msalabani?
Ndugu mpendwa unayefuatilia mafundisho haya, kila mahali ambako Mungu amenipa neema ya kufundisha masomo haya ya ukombozi nimekuwa nikiulizwa hili swali.na inawezekana hata wewe unashauku ya kujua mengi kuhusiana na hili,
Mpendwa unayefuatilia mafundisho haya, ni kweli kabisa kuwa hata mtu aliyeokoka anaweza akavamiwa na roho za giza.
Na zika athiri mambo yake, kama biashara yake, uchumi wake, ndoa yake na hata maisha yake kwa ujumla na bado akawa anaenda kanisani, anaomba, anaimba, na kufanya baadhi ya mambo,
Kumbuka adui mkubwa wa ibilisi ni yule aliyempokea kristo, na ndio maana wakati mwingine kuokoka kumetamkwa kama kutangaza vita, mtu aliyeokoka anafananishwa na mtu ambae yuko vitani na kuwa amezungukwa na maadui kila mahali, na kila adui anatamani kama angelimmaliza yeye maana anasababisha matatizo makubwa kwenye ufalme wa adui bila ya yeye kujua.
Watu wengi kwa sababu ya kutokuyasoma maandiko hudhani ya kwamba kuokoka ni kumaliza kila kitu ikiwa ni pamoja na uhakika wa kufika mbinguni na kumbe kuokoka ni kuanza safari ya maisha mapya katika ulimwengu wa mapambano, na ndio sababu Biblia ikasema katika 2kor 10 :12 kwamba ‘kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke, sasa ukiufuatilia huu mstari utagundua Biblia inatutaka tuwe waangalifu, maana Adui ni kama simba aungurumae anaye tafuta mtu apate kummeza, wakati huo huo ukisoma Yakob 4 :7 utakuta anasema ‘basi mtiini Mungu mpingeni shetani nae atawakimbia’ sasa kwa nini Biblia inakutaka umpinge shetani ndipo nakukimbie, hii ina maana usipompinga atakukimbilia wewe.
Ulinzi wa Mungu unakuwa juu ya mtu, tu pale anapokuwa Hodari katika Bwana huku akiutafuta uweza na nguvu zake, Efeso 6 :10 ‘Hatimae mpate kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake’
Nini maana ya kuwa hodari katika Bwana, huku ni kukaa kwenye maombi, kuwa na neno la Mungu ndani yako, kujifunza kuutafuta uso wa Mungu kwenye maeneo Mbalimbali ya maisha yako, kwa kadiri utakavyokuwa ukiendelea katika hali hii ndivyo utakavyo kuwa ukiuona uweza na nguvu za Mungu kwenye maisha yako ukiendelea mstari wa 11 utakuta anasema ‘vaeni siraha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani’ sasa hii inakupa kujua kuwa unatakiwa kupingana na hila za shetani kila siku maishani mwako na hauwezi ukazipinga tu hivi hivi ni mpaka umevaa siraha zote za Mungu, ikiwa ni pamoja na neno la Mungu kujaa kwa wingi ndani yako, kuwa muombaji, na kweli ya Mungu kuwa kwenye maisha yako,
Hii inaweza kuwa moja ya mirango ya adui kwa mtu aliye okoka
Fitina, kule kumfitini mtu au kumsengenya mtu na hauoni shida kufanya hayo, na kule kushindwa kabisa kumtoa mtu moyoni mwako,kushindwa kuachilia,kusamehe, kuendeleza kinyongo, kuacha uchungu uendelee kujaa ndani yako inaweza ikampa ibilisi mrango na ukavamiwa na roho za giza, maana ukiwa kwenye hali hii huna mda wa kuomba, ila unamda wa kulaumu na kunungunika, ikiwa ni pamoja na kujisemea vibaya au kumsemea mwingine.
Kiburi, kule kujaa kiburi na ukaidi, kutokutaka kusikiliza ushauri, kuwaona wengine wote hawana kitu isipokuwa wewe au fulani, na hivyo kutokunyenyekea, wala kushuka kitu ambacho kimesababisha roho za ukengeufu kwa watu wengi leo{uasi} hii imesababisha mirango kwa nguvu za giza.
Tendo la ndoa kabla ya ndoa, au nje ya ndoa kumbuka mtu anapoamua kutoa nguo zake kwa mtu amabaye si mke wake halali, kwa tafsiri ya rohoni anautoa utukufu wa Mungu, au anauvua, hivyo basi anauvua ulinzi, na kwa sababu hiyo Roho za giza zinakuwa na nafasi kubwa ya kuweza kumvaa mtu huyu
Na ndio sababu watoto wa kuhani heli Hofsini na Finehasi walipofanya uzinzi na wanawake waliokuwa wakitumika malangoni pa hema ya kukutania, utukufu wa Mungu uliondoka, na ulinzi wa Bwana ukaondoka na lile sanduku la agano likatekwa, habari hizi utazipata vizuri samweli wa kwanza na kuanzia sura ya pili, kitu nilitaka uone ni jinsi ambavyo utukufu wa Mungu ukiondoka juu ya mtu na ulinzi wa Mungu ukiondoka kwa sababu ya dhambi uwezekano wa mtu kuvamiwa na aroho za giza unakuwa ni mkubwa zaidi.
Kukata tamaa ile hali ya kujikatia tamaa, kuvunjika moyo, kupoteza kabisa matumaini hata kujisemea maneno ya laana, inafungua mirango kwa roho za giza kuvamia maisha yako. Ndio sababu Biblia ikasema Filip 4 :6 msijisumbue kwa neno lolote ; Bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. sasa kule kulaumu kulalamika, kujilaani haja zako zinajulikana na mapepo na sio Mungu. Iyo ndio inayompa adui nafasi kwenye maisha ya watu wengi leo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW