Tuesday, November 24, 2015

MAMBO SITA YANAYO SABABISHA MAELFU YA WATU WA AINA MBALIMBALI KUINGIA KWENYE VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA


1. Wapo waliopata watoto kwa njia za ushirikina
2. Kukubari huduma za kishirikina
3. Kuzindika nyumba
4. Matumizi ya hirizi na baadhi ya vifaa vya ushirikina
5. kuhuzuria au kuishi maeneo yenye utawala wa kipepo
6. Wengine majina yao yamewaingiza kwenye vifungo

Kwa kurithi watoto wengi wanao zaliwa kwenye familia ambazo kuna mambo ya uchawi au wanaabudu mizimu na kufanya mambo ya matambiko huwa wanatolewa kwa pepo au mizimu wangali bado wadogo kadri wanavyoendelea kukua ndivyo wanavyoendelea kuona kama mambo yanayo fanyika ni sahemu halali kwa maisha yao. Nakumbuka safari moja tukiwa kilimanjaro tulifanya huduma na kijana mmoja wa kidato cha pili aliyekuwa amefungwa na nguvu za giza , na tukiwa tunafanya nae maombi alitapika vitu fulani vyeupe vya kushangaza sana. Baada ya kufunguliwa na Bwana Yesu na yale mapepo kumuachia tukapata nafasi ya kukaa nae na kuzungumza nae, alitueleza kuwa yeye ni mtoto wa kwanza kuzaliwa kwenye familia yao na kuwa amekuwa akipelekwa kwenye makaburi na kufanya matambiko na wazazi wake kuanzia akiwa mdogo na akaeleza kuwa alikuwa akilishwa vyakula kama nyama za aina fulani kila alipofika makaburini kwa tambiko, sasa hii ina maana kama Bwana Yesu asinge mfungua angeendelea kuishi maisha ya ushirikina chini ya utawala wa nguvu za giza.namna watoto wanavyoingizwa kwenye vifungowazazi wengi wasio amini huwaingiza watoto wao kwenye vifungo vya ushirikina bila ya wao kujua. watoto wengi wakizaliwa hupelekwa kuchanjwa chale, kwa waganga wa kienyeji au wengine hupelekwa kwa Bibi zao kwa ajili ya mambo fulani ya kimira kama kuzika kitovu, kwa taratibu za kimila, kupewa jina chini ya taratibu za kiganga, zipo sara mtoto anaombewa kwa babu zake waliokufa wakati mwingine hizi sara hufanyika makaburini ‘mfano wa sara inayoombwa { mtoto wenu amekuja, mumkumbuke, mumsaidie, tunawakabidhi ni wa kwenu, maneno mengi sana yanatamkwa mara nyngi nkuwa kwa kiluga bila hata ya wao kujua ni nini wanafanya katika ulimwengu wa roho, kumbe katika ulimwengu wa roho yule mtoto anakabidhiwa chini ya falme na mamlaka za giza} Na ndio sababu ukisoma Kumb 18 :10 utakuta anasema Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au Binti yake kati ya moto’ ukiendelea mbele kidogo utakuta anasema ‘wala asionekane mtu aombae wafu sasa u mstari 12a utakuta anasema ‘kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana’Wakati fulani tukiwa na huduma mkoa wa Tanga nilipata nafasi ya kupita mitaani watu wanako ishi asilimia kubwa ya watoto nilio waona walikuwa wamevishwa Hirizi, na vitambaa vyeusi mikononi, shingoni,kwenye miguu wengine walikuwa wamevishwa shanga viunoni, japo hii aina maana mambo haya yako huko tu isipokuwa niliguswa sana nikiwa huko cha kushangaza leo hii hata wakristo wengi wamevalisha watoto wao hivyo vitu, wengine ukiwauliza hata yeye mzazi hajui kwa nini kamvalisha mtoto hicho kitambaa cheusi wengine ukiwauliza atakuambia Bibi yake alimvalisha.

Kwa kushiriki mambo ya uchawi na ushirikina wapo wakristo wengi leo hii ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakijihusisha na mambo ya uchawi na ushirikina bila ya wao kujua mfano kuchangia tambiko, kuhudhuria ibada za wafu, kula nyama za kusongolewa, kunyoa nywele kwa ajili ya aliyekufa, kunywa dawa za kimila, kwenye misiba mingi ambayo watu huamini mambo ya ushirikina huwa wanakunywa Dawa wanafamilia au ukoo mara baada ya mazishi au msiba kuisha . lakini

Biblia imesema wazi kabisa kuwa ‘msishiriki ibada zao’ na ukisoma katika Kumb 14 :1 utakuta anasema ‘msifanye upaa kwa ajili ya aliye kufa.’ Sasa ni muhimu ukafahamu kuwa haya ni moja ya mambo yanayoingiza maelfu ya watu kwenye vifungo

1. Wapo waliopata watoto kwa njia za ushirikina


Wapo wanawake ambao baada ya kutafuta watoto kwa mda mrefu bila mafanikio wakaamua kutafuta kwa njia za ushirikina, wengine walilishwa madawa ya kienyeji ili apate mimba, wengine walilazimika kufanya tendo la ndoa na waganga wa kienyeji, wengine walienda kulala juu ya makaburi, na mambo mengine mengi hakuna hata muda wa kutosha kuelezea kila kitu, kitu nataka ufahamu ni hiki kuwa huyo mtoto aliyepatikana kwa namna ya uchawi na ushirikina ni lazima tu awe chini ya utawala wa Nguvu za giza {kwenye vifungo} {maana agano la kupatikana kwake lilifanyioka wakati wa kutungwa mimba} yaani mimba ilipokuwa inatafutwa. Na mara zote mtoto wa namna hii kuwa na tabia za tofauti huwa na uwezo wa kuona vitu vya tofauti, maana roho za giza zina hati miliki juu yake,

2. Kukubari huduma za kishirikina
Wapo watu ambao walipoibiwa tu wakashauliwa kwenda kuagua kitu ambacho ni chukizo mbele za Bwana Kumb 18:10b ‘Wala asionekane mtu atazamae bao,,,,’ ukiendelea mbele kidogo utakuta
anasema ‘wala mwenye kubashiri, wala mshihiri, Wala mtu alogae kwa kupiga ufundo shida ni hii kuwa wapo wakristo wengi sana leo wanao muhuzunisha Bwana kwa kushiriki au kukubariana na huduma za kishirikina na wakati huo huo wanamuabudu Mungu, wakristo wengi leo wamependa mambo ya Unajimu kwa mfano Unajimu wa Nyota, matumizi ya vitu mbalimbali kama karata, kubashiria bahati kupiga ramli, kutegua tego,

3. Kuzindika nyumba
Wapo watu wengi leo walio danganywa kuwa kuna kuweka ulinzi kwenye nyumba zao Hivyo wakaruhusu waganga kuja kuchimbia vitu Fulani kwenye Nyumba zao na matokeo yake huwa inakuwa ni kupuputika kwa familia ikiwa ni pamoja na kukaribisha magonjwa na mikosi kwenye familia, ikiwa ni pamoja na vilio visivyoisha, maana mnaikabidhi ardi yenu chini ya utawala wa nguvu za giza, sasa kwenye kitabu changu cha kwanza kijulikanacho kama {PAMBAMBANA DHIDI YA NGUVU ZA GIZA}nilipokuwa natoa utangulizi wa masomo haya nilitoa ushuhuda jinsi tulivyo fanya huduma ya kufukua mazindiko kwenye familia Fulani maana familia iligeuka maali pa maombolezo, mtoto wa kwanza na wa pili walikufa katika hali ya kutatanisha mtoto wa tatu akawa yuko taabani, ukimtazama mama yake hajiwezi kwa ugonjwa ndipo mzee mwenye nyumba akakumbuka agano la ardi yake na mapepo, nakumbuka

Tulipomaliza kufukua mahali palipo chimbiwa tulikuta vitu vya ajabu kweli,lakini ninachotaka ujue ni kuwa mara baada ya kufukua vitu vilivyo chimbiwa zaidi ya miaka kumi iliyopita tulivichoma moto, na familia yote wakaamua kumpa Bwana maisha kuanzia pale, yule mgonjwa waliyekuwa wakitegemea angekufa mda wowote na kukamilisha idadi ya watoto watatu kufa maana alikuwa mahututi, alipokea uzima toka kwa Bwana Yesu, mpaka leo hii nikienda kwenye ule mkoa namkuta akiimba kwaya ya vijana kanisani kwao. mateso na vilio vikaondoka.kitu nilitamani uone ni hiki kuwa Bwana asipoulinda mji yeye alindae akesha bure,

USICHANGANYE NGUVU ZA MUNGU NA SHETANI NI HATARI
acha kumchanganya Mungu kabisa, maana utakufa. ukiamua kumtegemea Bwana Yesu, mtegemee yeye kwa asilimia mia moja na si vinginevyo maana wapo wanaopenda kuchanganya nguvu za Mungu na za Ibilisi kumbuka hilo ni kosa kubwa na Nyuma yake kuna laana na mauti utaishia kufa kifo kibaya na aibu yako itajulikana..maana ukisoma Kumbukumbu la torati 28:4 -13 utaona Mungu akitoa Baraka ikiwa watu watamtegemea na kumuamini yeye peke yake, anaanza na kuzungumza habari za uzao wa tombo lako utakavyobarikiwa, anazungunza habari za adui zako kupigwa na kuanguka mbele yako, na jinsi ambavyo kila utakalo lifanya litabarikiwa, ameeleza mambo mengi sana ambayo anatamani yafanyike Baraka kwenye maisha yako, endapo utatii na kufuata maagizo yake, Lakini ukisoma ule mstari wa 14 anasema "msipogeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia." Sasa lile neno msipogeuka kwa tafsiri nyingine msiponiacha na kufuata mambo ya ushirikina{miungu mingine} maana ni rahisi sana kudanganywa kuwa uko msaada kwenye uchawi, na mambo ya ushirikina lakini nataka ujue wazi leo hii kuwa, huko ni kijitafutia laana na mauti yako mwenyewe. Maana hakuna kitu Mungu anapingana nacho kama sisi kumchanganya yeye na miungu mingine.
Na ndio sababu ukisoma ule mtari wa 15 anasema ‘lakini itakuwa usipotaka kuisikiliza ile sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata’. Ukiendelea mbele kidogo anaelezea hizo laana mstari wa 16 utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. litalaaniwa kapu lako na chombo cha kukandia {kapu lako : {kwa tafsiri nyingine utalaaniwa uchumi wako}anaendelea ‘BWANA atakuletea laana na mashaka, na kukemewa katika yote utakayotia mkono wako kufanya, hata uangamie na kupotea upesi’ {kumbuka sio mapepo, ila Bwana atafanya } na ndio sababu kuna wakati shida yako inaweza ikaombewa na kila mtumishi na isipatiwe ufumbuzi isipokuwa ni mpaka Mungu atakapokuja kumpa mtumishi mwingine neno la maarifa juu ya dhambi yako na kwamba uondoke kwenye maagano ya ushirikina uliko ndipo uvumbuzi wa shida yako utakapotokea, na ndio sababu ni bora uwe na uadui na shetani Mungu atakusaidia, kuliko ukawa na uadui na Mungu hii ni hatari kubwa maana hatakuwepo wa kukusaidia.
Ukisoma ule mstsri wa 28 anasema ‘BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu na kwa bumbuazi la moyoni utakwenda kwa kupapasa papasa mchana,kama apapasavyo kipofu gizani wala hufanikiwi katika njia zako ; nawe siku zote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.’ Sasa ukiendelea mbele kidogo utaona jinsi ambavyo utachumbia mke na mtu mwingine atalala nae {watamchukuwa} na mambo mengine mengi ambayo yatakupata tu kwa sababu umeabudu miungu mingine. Na kama hayo mambo hayajakupata wewe hata ikiwa yamekupata kwa sehemu, basi uwe na uhakika watoto wako watarithi mateso ya dhambi yako. Maana Mungu hupatiliza maovu, alihaidi kupatiliza maovu ya Baba kwa mwana, ukisoma { Kutoka 20 :4 anasema ‘usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu kilicho juu mbinguni, wala kilicho majini chini ya Dunia ; Usivisujudie wala kuvitumikia kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu ; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,’
Sasa Mungu ameshasema kuwa wana watapatilizwa maovu ya Baba zao tu kwa sababu Baba zao waliabudu miungu mingine. Ili kuepuka mambo haya yote usimchanganye Mungu maana kuna watu leo wanaenda makanisani na bado wanairizi, bado wanashiriki mambo ya giza, bado wanashiriki mambo ya jadi na mila, hivyo basi ni muhimu sana ukawa na maamuzi ya kumtumikia Mungu peke yake na si vinginevyo

Mambo yanayotokea nyumba inapokuwa imezindikwa
Nyumba ikizikilicndikwa maana yake imekabidhiwa kwa pepo kwa tafsiri nyingine watoto wanakuwa wamekabidhiwa pia maana ni sehemu ya familia, miradi inakuwa imekabidhiwa pia biashara, ndoa, pamoja na kazi, hii ni hatari sana, na watu wengi sana wanaoishi kwenye Nyumba za kupanga zilizozindikwa huwa wanapata shida sana ya mapambano na roho za giza mara kwa mara wachache huwa wanapewa macho ya rohoni kujua kuwa ziko falme mbili zinapambana mahali hapo.Biblia inaposema katika {Yoshua 1:3 } kila mahali zitakapo kanyaga nyayo za miguu yenu nimewapa,

haina maana ufike tu hotelini au nyumba ya wageni na kulala tu, au uamie tu kwenye Nyumba na kuanza kuishi bila kufanya chochote au uinmgie kwenye basi na kustare kama abiria wengine hiyo naifananisha na imani pasipo matendo maana kwa tafsiri halisi wewe mtoto wa Mungu kupewa kila mahali nyayo za miguu yako zinapokanyaga ni kupateka mahali hapo na kuvuinja falme zingine zilizokuwa zinatawala na kuupanda ufalme wa Mungu na ndio sababu Mungu alimwambia Yeremia kitu alichotakiwa kufanya ukisoma Yeremia 1:10 anasema ‘Angalia nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme’ kwa tafsiri nyingine nimekupa mataifa nimekupa na falme utawale ukiendelea pale mbele utakuta anasema ili….. sasa neno ili linatafsiliwa kama sababu, sasa ni sababu ipi ya M ungu kumuweka Yeremia juu ya mataifa na juu ya falme utakuta Mungu alikuwa na lengo la kungoa, na kubomoa, na kuharibu kazi za ibilisi alafu aujenge na kuupanda ufalme wa kwake. Hivyo basi mambo haya ambayo mungu aliyatarajia yalitegemea sana uelewa wa Yeremia kwa habari ya yeye kuwekwa juu ya mataifa na juu ya falme.

4. Matumizi ya hirizi na baadhi ya vifaa vya ushirikina
Maelfu ya watu leo wameingia kwenye vifungo kwa sababu walikubari kupokea hirizi na wengi wao wanazitumia kwa siri wakifikili kuna ulinzi na usalama kumbe ni kujiingiza kwenye mikataba ya nguvu za giza,wako wengine ambao wameziweka kwenye Magari yao, wengine kwenye vitanda vyao, wengine wameshonea kwenye nguo zao, ilimradi tuu isionekane, ni muhimu kufahamu kuwa Mungu wetu yu kinyume cha Irizi ukisoma Ezekiel 13:20 anasema ‘ Basi Bwana Mungu asema hivi mimi ni kinyume cha Irizi zenu…….’ Sasa ukianzia pale mwanzo kidogo utakuta anatoa ole, kwa wanawake wanao shona irizi.. na utaona jinsi ambavyo matumizi ya irizi ni kwa ajiri ya kuondoa Roho za watu kishirikina. Na ndio sababu Biblia ikasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maana yake ni kuwa hawana ufahamu,juu ya mambo wanayoyafanya na ndio sababu maelfu ya watu wameingia au wameingizwa kwenye vifungo vya ibilisi wakidhani wanatafuta ulinzi,usalama,amani,furaha,maisha mema, na matokeo yake kuwa vilio na majuto.

Je kuhusu shanga bangili na mikufu

Ni kweli kabisa kuwa wapo watu wengi leo wanaopenda kutumia vitu vya ulembo kama Shanga, maana zipo zinazotengenezwa kwa mfumo wa kuvaa hata wanaume pia, mfano ni zile za mikononi, na wapo wanawake wanaopenda kuvaa zile za kiunoni, mikufu, bangiri, pete, mapambo ya ndani kama vinyago na vibuyu, ni muhimu sana kuwa makini hapa maana kwenye ulimwengu huu wa utandawazi kila kitu huonekana kuwa ni cha muhimu na chenye thamani kwa Binadam.
Ni katika ulimwengu huu tunaoishi tunapotakiwa kuwa makini sana na kila chaguo la jambo tunalotaka kufanya kama wacha Mungu, na si tu kufanya kwa sababu wengine wamefanya, tunahitaji kuwa na macho ya rohoni hasa tunapofanya maamuzi ya maisha na mambo ambayo tungetamani yaambatane na maisha yetu, kuna kitu kiaitwa macho ya rohoni tunahitaji kuwa na macho ya rohoni ili kuepukana na vitu amabavyo miili yetu inaweza ikavutiwa navyo pasipo ufahamu wa mambo ya rohoni ikawa ndio tunapelekwa kwenye vifungo

Biblia inaposema katika {Kor 3 :15} kuwa ‘na amani ya kristo iamue mioyoni mwenu….’ Maana yake ni hii kuwa anayeleta amani ya kristo mioyoni mwetu ni roho mtakatifu peke yake , sasa kwa nini akasema amani inayotakiwa iamue mioyoni mwenu ni ya kristo hii ina maana zipo amani nyingine zinazoweza zikaamua moyoni mwako na matokeo yake zikasababisha mambo magumu sana kwenye maisha yako, ikiwa ni pamoja na milango kwa adui,
Sasa ni muhimu kutambua kuwa ni wajibu wa Roho mtakatifu kuamua kwa niaba yetu, kwani ndie kiongozi wetu, msaidizi na mwalimu wetu. lakini asipopewa nafasi kwenye maisha yetu hukaa pembeni akihuzunika kwani hawezi kukulazimisha kufanya jambo, ‘Efeso 4:30 wala msimuhuzunishe yule Roho mtakatifu wa Mungu,ambaye kwa yeye mlitiwa mihuri hata siku ya ukombozi’ na sehemu nyingine ya Biblia inaonyesha jinsi ambavyo Roho hututamani kiasi cha kuona wivu yaani huwa anatamani kama angeamua kwa niaba yetu, angefanya kila kitu kwa niaba yetu, sasa kwa sababu maisha yetu hayana nafasi ya Roho mtakatifu kufanya kwa niaba yetu ndio sababu tunashindwa kuyafahamu mambo ya rohoni, na mipango ya Adui iliyo katika siri kubwa kuharibu maisha Yetu. na ndio sababu pia ukisoma Rumi 8 :26a anasema ‘kadharika Roho nae hutusaidia udhaifu wetu, miili yetu ina madhaifu mengi sana, mfano tamaa, tunatamani kila kitu hata bila kujiuliza maswali wakati mwingine, wala kutafuta maana ya hicho kitu ni nini, hata kuna baadhi ya vitu tumejiingiza kwavyo tu kwa sababu labda ukifanya ndio unaonekana wa kisasa zaidi, sio vibaya kuonekana wa kisasa isipokuwa swali la kujiuliza ni je ninaliolifanya au ninalotaka kulifanya linampa Mungu utukufu ? na je Adui hawezi akapata nafasi kwa njia hii ? korosai 3 :17 ‘Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu’ maana yake ni hii kila unalolitamka kinywani mwako au muonekano wako au unalolitenda, limtangaze kristo, limdhihilishe kristo, limfanye kristo apate utukufu. Kitu ambacho si rahisi kama Roho mtakatifu ajapata nafasi ya kwanza kwenye maisha yako,

Sasa ukiunganisha na mapungufu tuliyo nayo inampa ibilisi milango ya uvamizi kwenye maisha
yetu

Yapo mambo mengi ambayo kwa hayo tunakuwa tumejiingiza kwenye vifungo bila ya sisi kujua ukielewa kitu cha namna hii hautaacha kumpa Roho mtakatifu nafasi ya kwanza katika kuamua mambo yako na kuhakikisha kuwa inayoamua ndani yako ni amani ya kristo.

mambo mengine yanayokupa ulazima wa kuhakikisha anayeamua moyoni mwako ni ni Roho mtakatifu
kujua fikra za ibilisi 2korinto 2 :11 ‘shetani asije akapata kutushinda kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake’ fikra zake ni mipango yake ya uharibifu juu ya maisha yako sasa ili asikushinde ni lazima uzijue kwanza fikra zake, mbinu zake za uharibifu,na jinsi anavyotaka kukuingiza kwenye vifungo upo msemo wa kiswahili usemao { kumjua adui ni nusu ya kumshinda} sasa basi ile tu kujua kuwa kwa kufanya hili nitakuwa nimempa ibilisi nafasi na hivyo kutokufanya ni kumshida Adui teyariUshuhudanikiwa nafanya huduma hii ya kufunguliwa katika mkoa fulani yupo binti ambae alikuwa amepagawa na Roho za giza, sasa Baada ya kufunguliwa na bwana yesu nilipata nafasi ya kuzungumza naye na kutaka kujua iyo shida ilianzaje, alieleza kuwa siku moja ya jumamosi alipewa rifti na watu asiowajua lakini walidai kuelekea alikokuwa akielekea yeye,Anasema akiwa kwenye gari alipewa Biskuti na hakuona haja ya kukataa, kwa sababu ilikuwa ni biskuti tu, anasema walipo mshusha tu alipotakiwa kushuka gafra akasikia kutapika na alipotapika zilikuwa ni nywele za binadamu, alic`hanganyikiwa hakuelewa nini. Na kuanzia hapoalianza kujisikia vibaya mwilini na vitu vya ajabua vikaanza kutokea kwenye maisha yake,Anasema kuna wakati akawa anajikuta anatamani tu kukaa uchi, bila nguo watu wote wakiondoka ndania anafunga milango yote anavua nguo zote, alinieleza mambo mengi sana ya ajabu, kitu nilitaka uone ni hiki kuwa milango ya adui ilikuwa ni kwenye ile Taxi na zile biskuti, sasa sisemi usipande taxi wala usipokee vitu isipokuwa Roho mtakatiifu aamue kwa niaba yako,Shida ni hii kuwa kama Roho wa Mungu hachukui nafasi ya kwanza kwenye maisha yako hutaweza kabisa kuzijua fikra za Ibilisi kwenye maisha yako na hatimae kujikuta uko katikati ya vifungo vya adui.

Miitego ya ibilisi Zaburi 91 colonthree emoticon ‘Maana yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji na katika tauni iharibuyo’ ndugu unayefuatilia mafundisho haya ni muhimu ukatambua kuwa kuna mitego mingi sana ya ibilisi kila siku kwenye maisha yetu, mitego ambayo unatakiwa kuitegua kwa neno la Mungu ,maombi na kwa kuongozwa na Roho mtakatifu katika kila unalolifanya.na ndio sababu Biblia ikasema msimpe ibilisi nafasi maana yake ni kuwa jambo lolote utalolifanya bila msaada wa Roho mtakatifu linaweza likampa ibilisi mlango wa kukuingiza kwenye vifungo maana anatutafuta usiku na mchana Biblia inaonyesha wazi kabisa kuwa anawashitaki wateule wa Mungu mchana na usiku, na pia ni kama Simba aungurumae anawatafuta wateule awameze, Hebu fikiria kama katika kila masaa 24 kwenye kila sekunde inayopita kuna mtego wa ibilisi unakutafuta, wewe unajipangaje au umejipangaje.Na mitego yote ya ibilisi ina lengo la kuwaingiza watu kwenye vifungo vya nguvu za giza na kuwabana mahali ambapo watendelea kunyanyasika,.na hii ndio sababu unatakiwa kujifunza kuwa mtu wa rohoni maana Roho wa Bwana atakuongoza katika kila unalolifanya, na kukuepusha na mitego ya ibilisi.na kukupa macho ya rohoni kujua nini upokee na nini usipokee, nini ufanye na nini usifanye, wapi uende wapi usiende, je kuna ulazima wa kushiriki hayo mazungumzo au hakuna ulazima, je ununue iyo bidhaa ya mamna iyo au usinunue, je ununue leo au kesho, je uupokee huo ushauri au usiupokee, je uvae iyo nguo kwenye hicho kikao au uvae nyingine, hii itakusaidia sana kutoishi maisha ya kawaida na kuepukana na mitego ya ibilisi.Na ndio sababu Biblia ikasema katika 1korinto 2 :15 ‘Lakini mtu wa Rohoni huyatambua yote, wala yeye atambuliwi na mtu’ mtu wa rohoni ni nani ni Yule aliyempokea Bwana Yesu na anayeongozwa na Roho mtakatifu, hivyo roho mtakatifu kumpa nafasi ya kujua mambo mbalimabali yanayoendelea katika ulimwengu wa Roho, Amosi 3:7 Hakika bwana hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake, manabii siri zake, hii ina maana Mungu kuna vitu hata ruhusu kwako mpaka amekujulisha na Mungu anapokujulisha kama icho kitu ni kibaya maana yake anataka ukipinge, au ukikatae, au ukiepuke, hivyo basi kama kuna mtego wa ibilisi mbele yako au mkakati wa adui, wa kukuingiza kwenye dhambi, au vifungo, Mungu anakuapa kujua. Na unapewa kuyafahamu Mambo ambayo wengine hawayajui wala hawawezi kuyatambua na ndio sababu Biblia ikasema mtu wa rohoni huyatambua yote, kwa vipi ? kwa msada wa Roho mtakatifu {ni muhimu kuelewa kuwa hatuwezi kuyajua mambo yanayoendelea katika ulimwengu wa Roho mpaka tumekuwa katika Roho}

Ukisoma Daniel 2 ;18 anasema ‘Ndipo Danieli akafunuliwa siri hiyo katika njozi ya usiku. Basi Danieli akamuhimidi Mungu wa mbinguni’

Sasa ukianza nyuma kidogo na hii habari utagundua ilikuwa ni shida iliyompata Mfalme nebukadreza, na vile ambavyo hakuna mtu mwingine angeliweza kujua jambo lolote isipokuwa ni yule tu wa rohoni, kwa sababu Danieli alikuwa ni mtu wa rohoni Bwana alisema nae rohoni jambo ambalo wenye hekima, na wachawi wote walishindwa kuliletea uvumbuzi, lakini kijana mmoja wa Rohoni aitae Danieli, akawa ana jibu na kusababisha amani kwa nchi nzima.

Ndugu msomaji isikutishe hii kuitwa mtu wa Rohoni au la, Biblia imesema wazi kabisa ‘Rumi 8 :14 kwa kuwa wote wanaongozwa na Roho wa Mungu hao ndio wana wa Mungu’ hivyo basi kama umeokoka Roho mtakatifu yuko ndani yako, maana huwa anashuka kwa ajili ya kuwaongoza maelfu ya watu wanaoingia kwenye orodha ya kuitwa wana wa Mungu, maana ndie anayetakiwa kumfundisha na kumuongoza kila anae ingia katika maisha mapya sasa shida ni kuwa watu wengi huwa tuna muhuzunisha, na wakati mwingine tunamzimisha kabisa.

Ingekuwa kama tungejua jinsi tunavyotafutwa na ibilisi usiku na mchana na hatuwezi kuona kwa sababu tunaishi mwilini na kuwa Roho mtakatifu anatakiwa kuona kwa niaba yetu kama ni balaa atuepushe, kama ni mauti atuepushe,na kuwa kama kuna jambo lolote atuajulishe kitu cha kufanya. Tungeyatambua hayo tungeudumisha uhusiano wetu na Roho mtakatifu.

maana kadri utavyoendelea kuudumisha uhusiano wako na Roho mtakatifu kwa maombi, na kwa kulisoma neno, ikiwa ni pamoja na akujiepusha na uovu unampa roho mtakatifu nafasi ya kuyafungua macho yako ya Rohoni,na masikio yako ya Rohoni hivyo basi ukianza kusikia na kuona Rohoni hakuna namna adui anaweza akakupata,

Maana kuna wakati mwingine utaambiwa usipande iyo Gari, au usichukue iyo nguo. Au usitumie iyo zawadi, au usinunue icho kinyago, au usinunue huo mdoli, au usile icho chakula,

Nakumbuka tukiwa tunafanya huduma ya ukombozi mahali fulani Dada mmoja alikuwa amevamiwa na nguvu za giza tu kwa sababu alilithi gauni la shangazi yake kumbe baada ya shangazi mtu kufariki Roho za giza zikabaki kwenye Nguo zake tulipokuwa tukiamuru zile roho za giza zimtoke zilipiga kelele na kusema tunataka gauni letu la marehemu, amechukuwa gauni letu, kwa kweli sikuelewa sana, isipokuwa mara baada ya kumaliza ile huduma nilipata nafasi ya kuzungumza nae na kumuuliza endapo kuna kitu chochote amekirithi ni cha marehemu ndipo aliponijulisha kuwa ni kweli kuna gauni la Shangazi alipokufa nikalichukuwa huwa ninalivaa ila kuanzia nilipoanza kulivaa kuna vitu niliona vimebadilika sana mwilini mwangu.

Kitu ninachotaka uwe mwangalifu ni hiki kuwa kuna wakati utatakiwa kuombea hata nguo kabla ya kuivaa, lakini anayetakiwa kukumbusha na kukuambia kama uombee au la, si mwingine isipokuwa ni roho mtakatifu. Na ndio sababu ukisoma katika Zekaria 3 :4 anasema ‘Nae huyo akajibu akawaambia wale waliosimama mbele yake akisema mvueni nguo hizi zenye uchafu, kisha akamwambia yeye tazama nimekuondolea uovu wako nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi,,,,,,,,’ kitu nilitaka uone ni jinsi amabavyo unaweza ukabeba matatizo,uovu,uchafu, shida tu kwa sababu ya mavazi, na ndio maana baada ya huyu ndugu kutolewa yale mavazi yake machafu uovu wake uliondolewa hii ina maana uovu ulikuwa kwenye mavazi. Na kumbuka ndugu mmoja aliniuliza swali sasa utajuaje hili vazi lina nguvu za giza na hili halina,
Ndugu msomaji ndio maana tunasisitiza uhusiano wa mtu binafsi na Roho mtakatifu maana si kweli kwamba mavazi yote yana mapepo isipokuwa kunawakati utakutana na mtego wa namna hiyo na kama hautakuwa na macho ya rohoni itakuwa rahisi sana kwa wewe kutekwa na ibilisi.

5. Kuhuzuria au kuishi maeneo yenye utawala wa kipepo
Ndugu msomaji wapo watu ambao huchukulia mambo haya kirahisi wapo watu amabao hupenda kuhuzuria maeneo ya matambiko hata kama wao wameokoka, wengine hawaoni shida huhudhuria vikao vya sadaka kwa miungu wengine huudhuria siku ambapo zile nyama zinaliwa ambabazo ni batili, wengine hudiliki hata kunywa zile dawa ambazo wao jadi na mila, wanaziita kinga ya ukoo, wengine huwa wanadai wanawasindikiza wengine kumbuka kadri unavyoendelea kuhudhuria kwenye hayo maeneo ndivyo unavyoendelea kufungua mirango kwa Adui hutajua ni saa ngapi mapepo yalikuvaa, maana ulinzi wa Mungu huondoka na kwa sababu yeye ni Mungu mwenye wivu ukijiingiza kwenye miungu mingine ulinzi wke unakuacha na laana yake inaambatana nawe, na Biblia inaonya , Kumbu 4 : 23 jihadhalini nafsi zenu msije mkalisahau agano la BWANA, Mungu wenu alilofanya nanyi mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu chochote, ulichokatazwa na BWANA, Mungu wenu, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ni moto ulao Mungu mwenye wivu.’ Sasa ukiufuatilia huu mstari utakuta anasema jihadhalini nafsi zenu. Msije mkaanza kuabudu miungu maana washirikina wengi leo hawajui ni lini walianza kuamini hivyo vitu wanavyo amini pia hofu ya Mungu imewatoka na ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa hiki ndicho kilichozaa huu mstari bandia wa biblia {jisaidie nami nitakusaidia} watu kutaka kuhalalisha kumchanganya Mungu na shetani,kuchanganya mambo ya ushirikina na Mungu. {hatari} kumbuka Mungu ni moto ulao na ni mwenye wivu.

6. Wengine majina yao yamewaingiza kwenye vifungo
Ndugu msomaji wa mafundisho haya ukifuatilia leo majina mengi sana amabayo watu wanayo kwa asilimia kubwa yamekuwa yakiendana na maisha yao, sababu ni hii kuwa jina lina sehemu kwenye maisha ya mtu, ukifuatilia malaika Gablieli wakati anamwambia Yusufu sababu za kumuita mtoto jina Yesu utagundua kuwa aliitwa Yesu kwa sababu ndie aliyekuja kuwaokoa wanadamu na dhambi zao kwa iyo jina Yesu ndani yake kulikuwa na ukombozi wa dhambi za watu, hebu soma
"basi alipokuwa akisafiri tazama malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto akisema ‘Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu naye atamzaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu MAANA YEYE NDIE atakaye waokoa watu wake na dhambi zao." Sasa lile neno maana tunaweza tuka sema kwa sababu, fikilia kama Yusufu angeamua kumuuliza malaika kwa nini mtoto aitwe Yesu? Na tusimuite jina jingine, Malaika angemjibu kwa sababu ndie atakayewaokoa watu na dhambi zao. Hivyo unaweza ukaona kuwa ndani ya jina la Yesu kulikuwa na ukombozi, na ndio maana leo tukilitaja kuna mambo ya tofauti yanatokea, pia zipo sababu nyingi zinazowafanya watu waape watoto majina wanayo wapa

Yapo majina kama Taabu, Shida, Majuto, kibaya, Cha usiku, Mbutolwe hili ni la kilugha maana yake kwenye matatizo, yapo mengi yanayofanana na haya sasa sisemi majina kama haya ni mabaya isipokuwa natamani wewe unaye muamini Mungu upate uwanja mapana wa maarifa, maana asilimia kubwa ya watu waliopewa majina haya majina yao yanaendana na maisha yao, maana Jina linanafasi kwenye maisha ya mtu. Hivyo basi jina linaweza likafungua mlango kwa roho za giza kumiliki maisha ya mtu. Hebu tuangalie mfano mwingine ukisoma Mwanzo 35:16-18 anasema "wakasafiri kutoka betheli hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrasi Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa na utungu wake ulikuwa mzito ikawa alipokuwa anashikwa na utungu mzalisha akamwambia usiogope maana sasa utamzaa mwanamume mwingine ikawa hapo katika kutoa Roho yake maana alikufa akamwita jina lake Beloni lakini lakini Baba yake akamwita benjamini" sasa unaweza ukaona mazingira jina lilivyo tolewa, jina lilitolewa mama akiwa anakufa na unaweza ukajiuliza swali kwa nini Yakobo alipofika akambadilisha mtoto jina? Jina a la kwanza halikutolewa kwenye mazingira ya baraka isipokuwa mazingira magumu yaliyojaa uchungu. Lakini pamoja na hayo yapo majina ambayowatoto walipewa na waganga wa kienyeji, watu wa mira, wazee wa jadi, majina mengine yalitolewa kwenye matambiko ibada za kuwaombea watoto kwa wafu majina haya huambatana moja kwa moja na roho za giza.

Jifunze kutangua maneno mabaya ya watu kwenye maisha yako. Mtu anapokuambia utakufa palepale mwambie sifu, utafeli sifeli, jifunze kutangua laana za maneno kila wakati maana maneno ya mshirikina au mchawi yanaenda kutengeneza kitu katiaka ulimwengu wa roho ambacho uanaweza ukakitangua hapohapo anapokisema.

Mungu awabariki sana

Max Shimba Ministries

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW