Saturday, January 30, 2016

SHETANI ATEREMSHA AYA ZAKE KWENYE KURUANI NA KUKIRI KUWA ALLAH NDIE MOLA WAKE MLEZI

1. Shetani akiri kuwa Allah ni Mola wake Mlezi.
2. Asema Allah ndie aliye mfundisha kutenda dhambi.
3. Asema na yeye atafanya maovu aliyofundishwa na Allah kwa Binadamu
4. Tabia za Shetani na Allah zafanana

SOMA:
Surah Al Hijr 39. Shetani akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
[Sûrah al-A`râf: 16-17], [Sûrah al-Isrâ’: 62] ,
Ndugu zanguni, huu ni MSIBA mwingine Mkubwa sana kwa Dini ya Jibril. Leo tunajifunza kutoka aya ambayo Jibril aliiteremsha kwa Muhammad. Aya hii katika Surat Al Hijir inakiri kuwa ALLAH NI MOLA MLEZI WA SHETANI.
Sasa Kama Allah ndie Mlezi wa Shetani, na sie wote tunafahamu kuwa Shetani kazi yake ni kufanya Maovu, Kuua watu, na kuendeleza ubaya hapa dunia, JE, inamaanisha hayo yote Shetani kajifunza kwa Allah?
Shetani anaendelea kusema kuwa, NI ALLAH ndie aliye mtia makosani, Je, inamaana kuwa MALEZI ya Allah ndio yaliyo mfunza ubaya na dhambi Shetani?
Shetani anaendelea kusema na kukiri kwa Allah kuwa, NUKUU "basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote" ATAWAPOTEZA WATU WOTE, Swali: Kwanini Allah alikaa kimya wakati Shetani anajitamba kufanya mabaya kwa viumbe visivyo na hatia? Au ni kwasababu yeye Allah ndie aliye mfuza ubaya Shetani, ndio maana alishindwa kumkanya au mwonya Shetani?
Ndugu zanguni, sidhani kuna Muislam atakaye weza bisha na au ipinga hii aya amabayo ipo wazi kabisa kuwa, ALLAH NI MOLA MLEZI WA SHETANI na ALLAH NDIE ALIYE MFUZA UBAYA SHETANI. Huu ni MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM.
Waislam, ningependa mtujibu sio kwa jazba bali kwa aya, KWANINI ALLAH AHAKUKATAA KUITWA MOLA MLEZI WA SHETANI?
Max Shimba Ministries Org

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW