Monday, March 18, 2019

WADADA WA KISOMALI WANAENDELEA KUUKUBALI UKRISTO NA KUMKANA MUHAMMAD

Image may contain: 1 person, text and closeup


Maisha ya Maonyesho na Ubatili
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? 
(Yeremia 17:9).
Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. (Wagalatia 6:4).
Katika somo lililopita nililoliita Nia ya Ndani ya Moyo niligusia kuhusu umuhimu wa kuwa makini na nia zetu pale tunapomwendea Mungu, maana Mungu anajali sana hizo nia ambazo ndizo zinazoamua endapo atayakubali maombi yetu au tutaishia kupata hasara.
Katika somo hili namwomba Mungu anisaidie kufafanua kwa uwazi zaidi kile ambacho hasa kinaweza kuwa kinaendelea ndani ya mioyo yetu, ambacho ndicho anachokiona Mungu wetu pale anapotutazama.
Katika nyakati za Biblia kulikuwa na dhambi ambazo, labda niziite kuwa ni “za jumuiya.” Dhambi za namna hii zingeweza kutendwa na mtu mmoja lakini athari zake zikaangukia familia au hata taifa zima – ingawaje wengine wanakuwa hata hawakushiriki au hawakujua kwamba mkosaji halisi alikuwa anatenda dhambi hiyo.
Kwa mfano, Mfalme Daudi alipofanya kosa la kuwahesabu Israeli, alisababisha vifo kwa watu ambao hawakuhusika na kosa lake. Imeandikwa: Basi Bwana akawaletea Israeli tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu toka Dani mpaka Beer-sheba sabini elfu (2 Samweli 24:15).
Pia, tunasoma kuhusu wana wa Israeli kwa ujumla kuhesabika kuwa wametenda dhambi kutokana na kosa la mtu mmoja, yaani Akani. Matokeo yake walishindwa kwenye vita na kakabila kadogo sana ka Ai.
Imeandikwa: Lakini wana wa Israeli walifanya dhambi katika kitu kilichowekwa wakfu; maana Akani, mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila ya Yuda, alitwaa baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu; hasira ya Bwana ikawaka juu ya wana wa Israeli. (Joshua 7:1).
Mbali na hivyo, kosa la Akani pia lilisababisha kuangamia kwa familia yake yote. Imeandikwa: Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na lile joho, na ile kabari ya dhahabu, na wanawe, na binti zake, na ng'ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori. Yoshua akasema, Mbona umetufadhaisha hivi? Bwana atakufadhaisha wewe leo. Ndipo Israeli wote wakampiga kwa mawe, kisha wakawateketeza kwa moto, na kuwapiga kwa mawe. (Yoshua 7:24-25).
Lakini ilifika mahali ambapo Bwana akasema: Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama. … Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi. Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi. (Yeremia 31:27, 29-30).
Na tena, ingawaje tunatakiwa kabisa kubebeana mizigo, kwa maana ya kusaidiana kwa upendo ili kuleta furaha, amani, uponyaji, n.k., lakini inapokuja kwenye hatima ya suala la dhambi na athari zake kwa yule azitendaye, imeandikwa: … kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5).
Ndugu zangu, ninachotaka kusema hapa ni kwamba, Mungu anatupima kibinafsi katika kila jambo tunalojihusisha nalo hapa duniani. Kama ambavyo unaona kwamba ukinunua muda wa maongezi kwenye simu, hauwezi kamwe kuidanganya mitambo ili kwamba eti uongee hata kwa nusu sekunde na usikatwe pesa. Haiwezeani! Ukibonyeza tu, hata kama ingekuwa ni usiku wa manane, lazima mtambo utatambua na pesa yako itakatwa mara moja kulingana na kiwango cha upigaji simu wako!
Hiyo ni teknolojia ya kibinadamu. Mungu ni zaidi! Hakuna sekunde yoyote katika maisha yetu inayompita. Hakuna!! Na kila kitu kinawekwa kumbukumbu mbinguni – kiwe ni tendo linaloonekana kwa nje au ni wazo lililojificha moyoni!! Ndiyo maana imeandikwa kwamba Mungu atazihukumu siri za wanadamu (Warumi 2:16).
Je, ni kwa nini unafanya yale unayoyafanya?
Hakuna mwanadamu anayejua kile kinachoendelea moyoni mwako. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? (1 Wakorintho 2:11). Roho yako, au wewe mwenyewe (pamoja na Bwana) ndio mnaojua kile kinachoendelea ndani ya moyo wako. Na kwangu vivyo hivyo! Na kwa mwingine vilevile!
Sasa, kwa nini unafanya yale unayoyafanya? Nia yako ni nini?
Katika mambo ya kawaida kabisa ya kila siku maishani mwetu ni lazima kujiuliza swali hili: Kwa nini ninafanya hivi? Makusudi yangu ni nini?
Kwa nini unataka nguo ya gharama kubwa wakati ziko za gharama ndogo za ubora uleule?
Kwa nini unataka uwe na magari kumi?
Kwa nini unataka kumiliki maduka matano?
Kwa nini unachubua ngozi yako?
Kwa nini umebadili rangi ya nywele zako?
Kwa nini umechora ‘tattoo’ kwenye mwili wako?
Kwa nini unavaa mavazi yanayoacha wazi sehemu za mwili wako ambazo hazitakiwi kuachwa wazi?
Kwa nini umevaa mlegezo?
Kwa nini ulitoa mchango mkubwa sana kwenye harusi ya yule ndugu?
Kwa nini umevaa nyusi za bandia?
Kwa nini ukiwa kanisani unaonyesha sura ya unyenyekevu lakini ukiwa nje haufanyi hivyo?
Simu yako ni ya gharama. Kwa nini unapenda kuitoatoa mbele za watu hata kama haupigi au haujapigiwa?
Kwa nini umevaa cheni na unafungua vifungo vya shati lako?
Kwa nini umevaa nguo inayoacha maziwa nje?
Kwa nini ulimsaidia yule mtu aliyeomba msaada?
Mengi ya mambo haya ni ya kawaida kabisa katika maisha yetu ya kila siku na hayana ubaya hata kidogo!! Hakuna ubaya kuwa na magari kumi, nyumba tano, simu ya shilingi milioni moja, n.k. Hakuna ubaya!
Swali hapa ni moja tu: Moyo wako au moyo wangu unakuwa unanisukumaje mbele za watu? Kwa lugha rahisi, je, ninapenda kujionyesha? Ninaona fahari fulani watu ‘wanaponitambua’? Ninakuwa na shauku kila mtu ajue kuwa mimi ni wa kiwango cha juu? Je, kila wakati nakuwa naangalia kwa jicho la chati ili kubaini kama kuna watu wananitupia angalau jicho sawasawa na ninavyotamani wafanye?
Ni hakika kabisa hivi ndivyo maisha ya wengi wetu yalivyo. Ni maisha ya maonyesho, maonyesho, maonyesho tu! Ni maisha ya kusaka sifa na umaarufu! Ni maisha bandia! Hatumfikirii Bwana bali tunawafikiria wanadamu. Tunatamani kusifiwa na wanadamu.
Kwa watu wa dunia hii ni sawa kabisa. Lakini je, kwa Mungu nako ni sawa? Kwa wapendwa nako inatakiwa iwe hivyo?
Je, kanisa litatofautishwaje na dunia kama nalo linafanya mambo haya? Je, ni kwa kiasi gani haujanaswa na mtego huu? Ni kwa kiasi gani haujaingia kwenye kapu hili?
Kwa nini unafanya yale unayoyafanya?
Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. (Wagalatia 6:4).
Labda binti au msichana unasema, “Sasa nisipojipodoa na kujipamba nitapataje mume?” Dada yangu, kama Mungu ni Baba yako, basi lia na Yeye. Kibinadamu unaonekana kuna mantiki kabisa. Inaonekana kana kwamba usipojihangaisha kwa namna Fulani, basi utakosa mume. Lakini Bwana anapotutazama anasikitika kwa sababu hayo si maagizo yake. Maagizo yake yanasema: Maana twaenenda kwa imani, si kwa kuona. (2 Wakorintho 5:7). Kwa kuwa: Mwenye haki ataishi kwa imani. (Warumi 1:17).
Jambo moja la msingi sana, si kwa akina dada tu, bali kwa kila mwanadamu, ni kufika mahali pa KUAMUA kuwa, “Mimi nitasimama na Bwana peke yake! Awe amenipa kile ninachokiomba au hakunipa. Basi!!”
Huku ndiko kuyatoa maisha YOTE kwa Bwana. Lakini hii haitufanyi tuache kuomba kwa bidii zote yale ambayo mioyo yetu ina shauku nayo.
Ni hasara sana kuishi maisha ambayo yanataka tu kuwavutia wanadamu na kutaka kusifiwa nao. Hayo ni maisha ya UBATILI mkubwa.
Bwana anatuagiza katika sura ya sita ya Kitabu cha Mathayo:
1 Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.
2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.
3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
5 Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
7 Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
8 Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba. (Mathayo 6:1-8).
Japo hapa Bwana anaongelea zaidi suala la utoaji sadaka na maombi, lakini, kimsingi, yuko kinyume na maisha ya maonyesho mbele za watu. Tukifanya mambo kwa nia ya kuonekana mbele za watu ni kweli kabisa tutafanikiwa katika hilo. Tutasifiwa na kupata umaarufu huu batili wa dunia. Lakini hiyo ndiyo itakuwa thawabu yetu.
Simaanishi kuwa sasa basi uwe mchafumchafu kwa sababu tu eti hauko hapa kuifurahisha dunia bali Bwana! La hasha! Uchafu pia ni dhambi. Ninachomaanisha ni mtu kufanya mambo yake hasa kwa ajili ya Bwana. Ni kufika mahali ambapo kila kitu ninachofanya ni kwa ajili ya kumtukuza Bwana wangu, Yesu Kristo. Kama kwa jambo hilo dunia itanisifu, sawa. Kama haitanisifu, nako sawa pia. Lakini kusifiwa na wanadamu kusiwe ndio sababu ya msingi inayonisukuma kufanya jambo lolote.
Bwana anaagiza: Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. (1 Wakorintho 10:31).
Siamini kamwe kwamba mtu aliyeamua kwa dhati kuyafanya yote kwa utukufu wa Mungu atahangaika na mambo haya. Tunahangaika nayo kwa kuwa tu tumenaswa na ubatili wa dunia.
Ni nani yuko tayari kumwangalia Bwana pekee na kuachana na ulimwengu huu? Ni nani ee Bwana aliye tayari kutafuta kwa bidii sifa kutoka kwako badala ya sifa za wanadamu? Ni nani aliye tayari ee Bwana kujikagua katika KILA wazo, neno na tendo, KILA sekunde ya maisha yake?
Hakika yake Bwana hatuwezi. Hatuwezi kabisa bila neema yako. Tusaidie kuishi maisha matakatifu badala ya kushiriki na kuwa sehemu ya giza la dunia hii. Maana umesema kuwa sisi ni nuru ya ulimwengu. Lakini badala yake tumemezwa na giza; na sasa tunatafuta kila sababu [hata za kimaandiko] za kuhalalisha mambo haya ya giza. Tupe ufunuo wa rohoni ee Roho Mtakatifu ili tujue umuhimu na kuwa na utayari wa kubadilishwa na kupewa mioyo mipya inayoweza kukutii. Ni katika jina la Yesu naomba. Amina.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW