Saturday, August 8, 2015

ALLAH ATEREMSHA UCHAWI NA KUWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA

Naam,

Huu ni Msiba Mkubwa sana katika taifa la Mtume Muhammad. Mara nyingi Wakristo wamekuwa wanajiuliza, hivi, uchawi ulitokea wapi na mwanzo wake ni nani?

Leo Quran inakujibu kuwa Uchawi uliteremshwa na Allah na wachawi nambari moja ni Waislam. Nafahamu unafikiri kuwa Max Shimba anawasingizia Waislam au sio?

Hapa inafaa tufahamishane kuwa ushirikina ni jambo ovu linamtia mtu motoni. Kwenda kwa wachawi, wapiga ramli ni katika ukafiri na ushirikina.

Hebu soma Ushahid huu wa Quran: 

SURAT TAHA: 73. Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi. 

Kwenye Surat Taha ayat 73  kama ilivyo teremshwa Makka kwa Muhammad na kutafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani  inasema kuwa ALLAH ANAWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA UCHAWI. Huu ni msiba ndugu zangu. Swali la kujiuliza, hivi, tokea lini Mungu akawa mchawi? Hivi huu uchawi ulio teremshwa na Allah unafaida gani kwa Wislamu?

Hebu tuingalie tafsir ya pili ya Surat Taha aya 73 kama ilivyo tafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin inasema: 73. Kwani hakika sisi ni wenye kusimama juu ya Imani kumuamini Mola wetu Mlezi wa Haki, ili atufutie madhambi yetu yaliyo pita, na atusamehe huku kushughulikia uchawi ulio tulazimisha tujifunze na tuufanye! Na Mola wetu Mlezi ni Mbora wa malipo kuliko wewe, akit'iiwa; na ufalme wake na uwezo wake kulipa unadumu zaidi kuliko wako. 

1. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kujifunza Uchawi
2. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kuufanya Uchawi.

Ndugu msomaji, leo sina mengi ya kusema maana umesoma wenyewe kutoka Quran kuwa Allah aliteremsha uchawi na kawalazimisha Waislam wajifunze na kuufanya uchawi. Nawashauri Wakristo wenye marafiki wa Kiislam wawe makini, maana huyo rafiki yako anaweza kuwa ndiye anaye-kuroga kwasababu kalazimishwa na Allah kufanya hivyo.

MTUME MUHAMMAD ANATUMIA NDUMBA
Muhammad alitumia ndumba [nguvu za kimazingaombwe] dhidi ya jicho ovu na wanyama jamii ya mjusi wenye sumu Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3525 uk.48.

Hivi wapi tunasoma katika Taurat au Zaburi au Injir kuwa Mitume na Manabii wa kwenye Biblia walitumia NDUMBA?

Hivi Allah hana uwezo wa kutibu jicho ovu au Sumu mpaka atumie NDUMBA?

Mungu awarehemu na kuwasamehe ndugu zetu wote wanao fanya Uchawi. Maana Biblia inasema kuwa WACHAWI WOTE WATAINGIA JEHANNAM. 1 Samweli 15 : 23 .......... dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.

Ndugu msomaji, mpokee Yesu aliye hai na upate uzima wa milele. Dini haita kusaidia kitu, maana sasa unaelewa kuwa, ni dini ambayo inakufanya uwe mchawi na kuachana na upendo wa Mungu.

Katika huduma yake,
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2015

YESU NI MUNGU KUTOKANA NA QURAN (SEHEMU YA PILI)


Ndugu msomaji,

Je Yesu anazo sifa za kipekee za Mungu kutokana na Quran? Hebu tuanze utafiti wetu kwa kusoma Quran na tujionee wenyewe kama kweli Yesu ni Mungu au la.

Moja ya sifa au adhama ya Mungu kutokana na Quran: ni Al-Warith, ikimaanisha MRITHI WA VYOTE. Hii sifa ya Al Warith ni moja ya Majina 99 ya Allah wa Quran.

Je, Yesu anayo hiyo sifa ya MRITHI WA VYOTE "Al Warith"? Haya tusome kwanza Quran na tuone kama Allah anayo hii sifa ya Al Warith.

Surat Maryam 40. Hebu jamani! Nawajue watu kuwa hakika Mwenyezi Mungu ndiye mrithi wa kuurithi ulimwengu wote na kila kiliomo ndani yake. Na hisabu yao wote ni juu ya Mwenyezi Mungu. 

Allah anasema kuwa yeye ni Mrithi wa vyote kwenye Quran iliyo andikwa miaka mia 632 AD baada ya Yesu. Ikimaanisha kuwa Yesu ndie aliye kuwa wa kwanza kukiri haya maneno kuwa yeye ni mrithi wa yote kutokana na ushahid wa Biblia iliyo tangulia kabla ya Quran.

Sasa tuangalie kama kweli Yesu anayo hii sifa ya MRITHI WA VYOTE ambayo ni adhama ya Mungu pekee kutokana na Koran iliyo andikwa miaka 632 baada ya Yesu.

Biblia takatifi inasema yafuatayo kuhusu Yesu Kristo:
Waebrania 1 aya 2 inasema: lakini katika siku hizi za mwisho
amesema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye
amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, ambaye
kwa Yeye aliuumba ulimwengu. 

Katika aya hii tunasoma kuwa Yesu anaitwa “MRITHI WA VITU VYOTE” ambayo ni adhama/sifa ya Mwenyezi Mungu kama ilivyo shaidiwa na Koran Surah ya 19 na aya 40. Hivyo basi , Allah na Koran wamekiri kuwa Yesu ni Mungu kwasababu Biblia imetuthibitishia kuwa Yesu ni MRITHI WA VITU VYOTE miaka 632 kabla ya kuandikwa kwa Quran na uthibitisho huu upo kwenye kitabu cha Waebrania 1 aya ya 2.

Ndugu zanguni, huu ni ushahid tosha kuwa Yesu ni Mungu, maana leo tumejifunza kuwa Yesu alisema na kuitwa MRITHI WA VYOTE MIAKA 632 kabla ya Kuandikwa kwa Quran. Sasa kati ya Biblia iliyo kuja kabla ya Quran na Quran iliyo kuja baada ya Biblia, wewe utafuata kitabu kipi?  Watafiti wa mambo mbali mbali huwa wanatumia data za awali katika kuhakiki jambo. Na data tuliyo nayo kuhusu Mrithi wa vyote ambayo ni ya awali ipo kwenye Biblia na inasema kuwa MRITHI WA VYOTE NI YESU.

Hakuna ubishi hapa kuhusu URITHI WA VYOTE ambao ni wa Yesu, Maana yeye ndie Mwana wa Mungu na alithibitishwa kuwa Mrithi wa vitu vyote miaka 632 kabla ya Quran. 
Leo nimejibu hoja ya Waislam kuwa, Je, Yesu ni Mungu? Koran pamoja na Allah wanasema kuwa Yesu ni Mungu kwa kuwa Yesu anazo adhama zote na/au sifa zote za Mungu na moja ya sifa hizo ni AL-WARITH.

Katika huduma yake,

Max Shimba

Copyright © Max Shimba Ministries 2015

Friday, August 7, 2015

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA KWANZA)


Ndugu msomaji,
Mwezi huu nitaweka mada kadhaa zitakazo fundisha kuwa, Isa wa Quran na Yesu wa Biblia ni wawili na tofauti:

MAANA YA JINA ISANi jambo la kawaida sana jina au majina kuwa na maana. Mfano majina haya ya kiarabu yana maana hizi: Muhammad, linamaanisha mwenye kushukuriwa, Abdalla ni Mtumwa wa Allah; Abu-Bakar maana yake ni Baba wa bikira; Abu Huraira ni baba wa Mapaka. Aidha majina ya Kiebrania nayo pie yana maana. Malaki ni mtumishi au Mjumbe wa Yehova, Isaya ni Wokovu wa Yehova; Ezekiel inamaanisha Mungu hutia nguvu, Daniel – Mungu ni hakimu wangu.

JINA LA ISA MAANA YAKE NINI?Katika Qurani yenye jumla ya juzuu 30; Surah 114; aya 6236; maneno yenye kutamkia 76,440; herufi 322,373; jina Isa linatamkwa lisa au Aysi limetajwa mara 25. Isa pia ameitwa masihi mara 93. Lakini tunaposoma Qurani iliofarsiriwa/tafsiriwa na Imam Baidawi Vol 1 Ukurasa 160 ameeleza kuwa Isa jina la Kiarabu maana yake ni Wekundu unaozidiana na weupe. Hii ndio maana ya Jina la Isa wa Quran. Je, Yesu wa Biblia maana yake nini?

JINA LA YESU MAANA YAKE NINI?JINA Yesu linatokana na lugha ya Kiebrania ‘Yehoshua’ katika lugha ya Kigiriki wanasema ‘lesous’ inatamka ‘Yesous’ yaani Yesu. Katika lugha ya Kiarabu wanasema ‘Yasu’, kwa kiingereza ni “Jesus” maana yake ‘Bwana anaokoa au Bwana ni Mwokozi’ Isaya 43:6, 10-11.
Katika Biblia ambayo ina jumla ya Sura 1189; aya 31,102; vitabu 66 – Agano la kale vitabu 39 na agano Jipya vitabu 27; Neno Mwokozi kwa Kiingereza wanasema ‘Saviour’ limetajwa mara 55. Ikumbukwe kwamba katika agano jiypa jina Yesu au Yehoshua (kwa Kiebrania) limetajwa mara 1275 katika aya zipatazo 1226.

Zingatia pia kuwa agano jipya lina jumla ya aya 7930 na sura 260 hivyo hapa tunaona jina Yesu maana yake ni Mwokozi na jina Isa ni wekundu uliozidiana na weupe. Kwa kuwa maana ya haya majina tofauti bila shaka Isa sio Bwana Yesu.

Leo tumejifunza kwa kifupi tu kuwa, Jina la ISA lenye maana ya Wekundu unao zidiana na weupe ni TOFAUTI KABISA NA Jina la Yesu lenye maana ya MWOKOZI katika Biblia. Zaidi ya hapo, tafsir ya Jina la Yesu kwa Kiarabu ni Yasu na sio Isa kama ambavyo Waislam wanadai katika vitabu vyao.
Mungu awabariki sana na tuendele kujifunza Neno lake bila ya kuchoka.
Katika huduma Yake,

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA PILI)



Je, kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni sawa na Isa?
Taarifa za Malaika kabla ya kuzaliwa kwao, kadiri ya Qurani na Biblia.
Jibrili alivyomtokea Mama wa Isa == Gabrieli alivyomtokea mama wa Yesu:
WAISLAM-JIBRIL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa Msikitini Qurani 19:16-17
WAKRISTO-GABRIEL Alienda kwa Mariamu aliyekuwa nyumbani kwake - Lk 1:26-28
WAISLAM-Mariamu Mama wa Isa haijulikani aliishi kijiji kipi wala mji gani wala hata nchi haijulikani. Isitoshe Quran inasema kuwa Jibril ndiye aliyemletea utume Muhammad asiwapelekee Mayahudi (hana kosa) Sura 2:97
WAKRISTO-Lakini Mariamu Mama yake Yesu alitokewa na Malaika Gabriel akiwa katika kijiji cha Nazareti mji wa Galilaya nchi ya Israeli (Lk 1:26) Mariamu Mama wa Yesu ni Myahudi.
WAISLAM-Jibrili hakutoa salamu kwa Mariamu mama wa Isa ila alijimithilisha kwa umbo la binadamu aliye kamili - Sura 19-17
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alimsalimia Mariamu Mama wa Yesu – Luka 1:28
WAISLAM-Jibril alimwambia Mariamu kwamba mimi ni mjumbe wa mola wako ili nikupe mwana mtakatifu - Sura 19-19
WAKRISTO-Lakini malaika Gabrieli alimwambia mama wa Yesu kuwa utachukua mimba – Luka1: 31
WAISLAM-Jibrili alisema kwa Mariamu kuwa ili tumfanye mtoto muujiza kwa wanadamu – Sura 19: 21. Isitoshe Jibrili hakutaja jina la mwana kwa Mariamu. Bali alisema ili nikupe mwana mtakatifu.
WAKRISTO-Malaika Gabrieli alisema kwa Mariamu mama ya Yesu kuwa mtoto jina lake utamwita Yesu (Luka 1:31; 2:21) Gabrieli hakusema kuwa atampa mwana Mariamu. Bali alisema, Roho mtakatifu atakujilia juu yako, yaani motto atazaliwa kwa uwezo wa Mungu.

TOFAUTI YA KUZALIWA KWA ISA NA YESUIsa bin Mariam Yesu Kristo

WAISLAM-Isa alizaliwa katika shina la Mtemde – 19:23

WAKRISTO-Yesu kazaliwa katika hori la kulishia ng’ombe. Luka 2:7

WAISLAM-Kuzaliwa kwa Isa haijulikani mimba ya mama yake ilichukua muda gani maana malaika Jibrili alisema nikupe mwana mtakatifu mara akachukua mimba na kuzaa. (19: 22-23)

WAKRISTO-Lakini Mariamu Mama wa Yesu siku zake za kuzaa zilitimia. (Luka 2:6-7)

WAISLAM-Qurani haionyeshi kama Isa alitabiriwa na manabii kuwa atazaliwa

WAKRISTO-Lakini Biblia inatuthibitishia kuwa Manabii walitabiri kuzaliwa kwa Yesu, (Isaya 7: 14; 9:6) utabiri huu ulitolewa na Nabii Isaya miaka 750 kabla ya Yesu kuja kuzaliwa nao ulitimia (Mathayo 1:18-23)

WAISLAM-Isa haijulikani alizaliwa katika kijiji gani wala mji, wala nchi aliyozaliwa Qurani haikueleza.

WAKRISTO-Biblia inatujulisha kuwa Yesu alizaliwa Bethelehemu ya Uyahudi katika Mji wa Daudi umbali wa maili 5 toka kusini mwa Yerusalemu nchi ya Israeli (Lk 2:8-16). Kuzaliwa kwake mahali hapo pia ni kutimiza unabii uliotolewa na nabii Mika miaka 750-686 kabla ya kristo kuja wakati wa wafalme hawa wakitawala – Jotham, Ahaz na Hezekia wafalme wa Yuda. Yesu mwenyewe alizaliwa kama mwaka wa 4 wakati wa Mfalme Herode.

WAISLAM-Isa aliongea na watu akiwa mototo mchanga, na kusema kuwa yeye ni mja wa Mungu amepewa kitabu na amefanywa Nabii (Sura 19:30-33)

WAKRISTO-Yesu hakuongea na mtu akiwa mtoto mchanga. Alianza kuwauliza maswali na kutoa majibu akiwa na wazee Hekaluni akiwa na miaka 12. (Luka 2: 42-49)

Hivyo tunaona kwamba tuna tofauti nyingi tu kati ya Bwana Yesu na Isa. Swali kwako mfuatiliaji je, Isa bin Maryamu ndiye Bwana Yesu Mwokozi? Tafakari.

Mungu awabariki sana na tuendelee kujifunza tofauti za Isa wa Quran na Yesu wa Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA TATU)

Je, Isa bin Mariamu ni mwana wa Mungu?
Kama kuna jambo ambalo Allah mungu anayeabudiwa na Waislamu analitataa sana kupitia Quran basi jambo hilo si lingine bali ni YESU KUWA MWANA WA MUGU. Allah ansema hivi.

Sura 6:101 – Yeye ndiye muumba wa mbingu na ardhi, inamkinikaje awe na mwana, hali hana mke? Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu.

Quran 9:30 – Na Mayahudi wanasema ‘uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu’ na ‘wakristo wanasema Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu’ haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasina kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale walilkufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa?

Hili ni agizo la kutisha kwamba Wakristo na Wayahudi tuangamizwe kwa kuwa tunaamini Mungu ana Mwana, au wana, lakini Wakristo tunaoamini hivyo kwa sababu Mungu wetu:-
- Yehova alifundisha kuhusu Bwana Yesu hivi:
Kutoka 4:22…Israeli ni Mwanangu Mimi……
Mathayo 17:5……Huyu ni Mwanangu Mpendwa wangu….

Malaika wa Mungu alisem hivi.Luka 1:30-31, 35 – Malaika akamwambia usiogope Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kuvuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.

Hivyo basi Isa wa kwenye Quran siyo Mwana wa Mungu lakini Yesu wa kwenye Biblia ni Mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.

Leo tumejifunza tena kuwa, katika Quran Allah kakiri kuwa yeye hana Mwana, lakini kwenye Biblia Yehovah anasema kuwa Yesu ni Mwana wake.

Mungu awabariki sana na fahamu kuwa Isa wa kwenye Quran sio Yesu wa kwenye Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

ISA WA QURAN SIO YESU WA BIBLIA (UTHIBITISHO WA NNE)



Je, Mama wa Isa ndiye wa Yesu Kristo?
Hapo awali tumeona kuwa mama wa Isa anaitwa Maryamu, Surah 3:45 na pia mama wa Yesu anaitwa Mariamu Mathayo 1: 18-21, Marko 6: 3-4 lakini kufanana kwa majina hakuwezi kamwe kumaanisha kuwa ni mtu mmoja, kwani walio na jina hilo ni wengi. Biblia inatufundisha hivi.

Yohana 19:25 – Na penye Msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama, Mamaye, na ubu la mamaye Mariamu wa Klopa na Mariamu Magdalena.

Hapa tunaona Mariamu watatu. Ili kutambua tofauti baina ya Mariamu mama wa Isa na mama wa Yesu, lazima tulinganishe ujumbe wa Qurani na Biblia. Qurani inasimulia kuhusu baba na kaka wa Mariamu mama wa Isa hivi.

Suratul 66:12 – Na Maryamu mtoto wa Imrani aliyejihifadhi nafsi yake na tukampuliza humo roho yetu, (inayotokana na sisi) na akayasadikisha maneno ya mola wake, na vitabu vyake; na alikuwa miongoni mwa wanyenyekevu (wakubwa).
Surah 19:28 – Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati.

Hapa tunaona kuwa Maryamu mama wa Isa, baba yake ni Imrani na kaka yake aliitwa Haruni. Tusomapo Biblia inatueleza kuwa Amrani aliwazaa hawa:-
Hesabu 26:59 – Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi, ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni, na Musa, na Miriamu umbu lao.
Pia soma 1 Nyakati 6: 1-3 na Kutoka 6:20.

Huyo Amrani aliishi miaka mingi kabla ya Yesu na tena ametokana na kizazi cha Lawi mtoto wa watu wa mzee Yakobo. Mwanzo 29:34; Kutoka2:1-10
Ikiwa Mariamu wa Qurani baba yake ni Imrani basi atakuwa ameishi miaka 1500 kabla mama yake Yesu wa Biblia hajazaliwa!

Je, Mariamu mama wa Yesu ametokana na kizazi gani?Tunaposoma Biblia tunaona kwamba Yesu anaitwa mwana wa Daudi Mathayo 1:1; Marko 10:47 na Luka 1:27, 32, ndiyo maana pia Yesu anaitwa Simba wa Yuda Ufunuo 5:5. Hivyo basi ukoo aliyetoka Yusufu na Mariamu wa Yesu ni mmoja.

Hivyo basi Maryam wa Quran ambaye aliishi miaka 1500 kabla ya Mariam wa Biblia hakuwa mama yake Yesu. Zaidi ya hapo, Maryam wa Quran ni daya ya Musa na Haruni ambao waliishi Misri.
Leo tumeendelea kujifunza kuwa Maryam wa Quran sio na ni tofauti na Mariam wa kwenye Biblia.
Mungu awabariki sana na tuendelee kujifunza tofauti katika ya Isa wa Quran na Yesu wa Biblia.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

Thursday, August 6, 2015

QURAN SIO MANENO YA ALLAH WALA MUNGU


Ndugu msomaji,

Huu ni MSIBA mkubwa sana kwa Waislam wote duniani. Waislam wamekuwa na tabia ya kusema kuwa, eti Quran yote ni maneno ya Allah. Unapo wauliza, huyo Allah aliwezaje ongea na Muhammad, wanabakia kimya na kuanza kukutukana. Zaidi ya hapo, leo nitawawekea ushahid tosha kuwa Quran sio maneno ya Allah.

Haya ungana nani kwa ushahidi:

SHETANI ANASEMA KWENYE QURAN
Surah Al Hijr 39. Shetani akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,

Kwenye Surat Al Hijr, tumesoma kuwa Shetani ndie anazungumza katika hiyo aya ya 39. Kumbe basi, Shetani ni msemaji ndani ya Qurani.


HAPA TUNASOMA KUWA ZAKARIA NA YEYE NI MZUNGUMZAJI KATIKA QURAN
Surat Maryam: Zakaria Akasema: Mola wangu Mlezi! Mafupa yangu yamedhoofika, na kichwa kinameremeta kwa mvi; wala, Mola wangu Mlezi, sikuwa mwenye bahati mbaya kwa kukuomba Wewe.

Waislam, hivi Quran ni maneno ya nani? 

Endelea kupata darasa hapa:

MARYAM NA YEYE NI MSEMAJI KATIKA QURAN
Surat Maryam aya 18: Maryamu akasema: Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamngu.

Waislam, mbona na Maryam anasema kwenye Quran? Au siku hizi Maryam amekuwa Allah? Huu ni Msiba mkubwa sana kwa Waislam.

MALAIKA NAO WANASEMA KWENYE QURAN
Surat Maryam aya 21: Malaika akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.

Ndugu msomaji, kwanini Waislam wanapenda kusema uongo namna hii, eti Quran yote ni Maneno ya Allah? Mbona tunasoma viumbe wengine wakisema ndani ya Quran? 


ISSA BIN MARYAM NA YEYE ANASEMA KWENYE QURAN
Surat Maryam  aya 36: Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.

Issa na yeye alisema kwenye Quran. Lakini Muhammad yeye hakuwai sema chochote kile kwenye Quruani wala kuzaliwa kwake hakukutajwa kwenye Quran. Huu ni Msiba mkubwa sana kwa WAISLAM.

SWALI LANGU KWA WAISLAM NI DOGO SANA:

1. NI NANI MSEMAJI KATIKA QURAN?
2. QURANI NI MANENO YA NANI?

Mkiweza nijibu kwa aya na bila shari, leo hii nitasilimu na kuwa Muislam.

Waislam huwa wanasema kama huamni kuwa Quran ni maneno ya Mungu, basi teremsha aya kama za Quran, huku tukifahamu kuwa kuna aya nyingi ambazo wasemaji wake ni wengine na sio Allah.

Sasa, huu utata tunawaachia waislam waje hapa kutujibu bila ya kuweweseka.

QURAN NI MANENO YA NANI?



Karibu sana kwa Yesu aliye hai ambaye ndie NENO LA UZIMA.

Max Shimba

Max Shimba Ministries

Wednesday, August 5, 2015

MATOLEO 20 TOFAUTI YA QURAN ::::::::20 VERSIONS OF QURAN::::::::::

MATOLEO 20 TOFAUTI YA QURAN
20 VERSIONS OF QURAN

Click to ViewClick to View
Je, Kati ya haya Matolea 20 (Ishirini) ya Quran, toleo lipi ni la kweli?

Ndugu msomaji,

Leo nitaweka ukweli kuhusu Quran ambayo ina Matoleo 20 na kati ya hayo Ishirini (20) Matoleo 7 (Saba) yametajwa katika Hadith Mwaminifu za Muhammad.

Hapa chini ni Wasomaji Saba (7) ambao wote wana Matoleo Mawili mawili. Hawa Wasomaji saba wanapatikana hapa: 
Nafi (from Medina; d.169/785)
Ibn Kathir (from Mecca; d.119/737)
Abu `Amr al-'Ala' (from Damascus; d.53/770)
Ibn `Amir (from Basra; d.118/736)
Hamzah (from Kufah; d.156/772)
al-Qisa'i (from Kufah; d.189/804)
Abu Bakr `Asim (from Kufah; d.158/778)


WASOMAJI SABA NA MATOLEO YAO YA QURAN

1. Msomaji : Nafi` 
MATOLEO YAKE
Warsh
Qalun

2. Msomaji: Ibn Kathir
MATOLEO YAKE
al-Bazzi
Qunbul

3. Msomaji: Abu `Amr al-'Ala'
MATOLEO YAKE
Al-Duri
al-Suri


4. Msomaji: Ibn `Amir
MATOLEO YAKE
Hisham
Ibn Dhakwan


5. Msomaji: Hamzah
MATOLEO YAKE
Khalaf
Khallad


6. Msomaji: al-Qisa'i
MATOLEO YAKE
al-Duri
Abu'l-Harith


7. Msomaji: Abu Bakr `Asim
MATOLEO YAKE
Hafs
Ibn `Ayyash


HAWA NI WASOMAJI WENGI WATATU NA MATOLEA YAO MAWILI KILA MMOJA
"The Three" readers

1. Msomaji: Abu Ja`far
MATOLEO YAKE
Ibn Wardan
Ibn Jamaz

2. Msomaji: Ya`qub al-Hashimi
MATOLEO YAKE
Ruways
Rawh

3. Msomaji: Khalaf al-Bazzar
MATOLEO YAKE
Ishaq
Idris al-Haddad

Wadhalimu wa dini ya Kiislamu wanakiri kuwa kuna WASOMAJI wengi zaidi, lakini wanasema kuwa hawa walio tajwa hapo juu ndio thabit na sahihi. Kumbe basi kuna VERSIONS ISHIRINI ZA QURAN !!!!!!

SASA MASWALI YAKUJIULIZA NI HAYA:
1. Kati ya hao wasomaji wakurani, ni yupi yupo sahihi?
2. Kama Allah ndie aliteremsha Quran kwa Muhammad, kivipi awe na wasomaji wengine na kumsahahu Muhammad mtume wake kipenzi?


Ndugu msomaji, leo tumejifunza kuwa katika Uislam kuna siri nyingi sana ambazo zimefichwa na wanaona aibu kusme aukweli kuwa QURAN INA VERSIONS 20. HUU NI MSIBA KWA ALLAH NA MTUME WAKE MUHAMMAD.


Mungu awabariki sana na kuendelea kuwafungua macho.

Katika huduma yake

Max Shimba Ministries Org.

Kutoka Kwenye Uislamu Hadi Kwenye Ukristo



Jina langu ni Tahir na hii ni safari yangu kutoka kwenye Uislamu hadi kwenye Ukristo.

Mara baada ya kufika Marekani nikitokea Palestina miaka 14 iliyopita, nilimwoa msichana mzuri wa Kikristo. Msichana huyu alijaribu kuwa Mwislamu ili kunifurahisha mimi, lakini kadiri alivyojitahidi kufanya hivyo, ndivyo nilivyozidi kuwa mbali naye. Tulizaa mtoto mmoja, lakini ndoa yetu haikudumu maana ni vigumu sana kupenda wakati moyo wako umejaa chuki. Chuki ndicho kitu ambacho nilifundishwa wakati wa kukua kwangu kule Palestina – chuki dhidi ya Wayahudi, Wakristo na hata dunia nzima. Ukiwa kama Mpalestina, unafundishwa tangu ziku ya kwanza kwamba dunia yote ndiyo inayohusika na mateso yetu, na hasa Wayahudi na Wakristo.

Baada ya kuachana, baadaye mke wangu huyo wa zamani alikuja kuniambia kuwa amembatiza mwanangu. Nilikasirika mno kiasi kwamba nilienda kuingia moja kwa moja kanisani, nikamtukana mchungaji aliyefanya ubatizo ule, na nikamwambia kuwa angeenda jehanamu kwa sababu ya kitendo kile. Sikutaka kabisa mwanangu akue akiwa Mkristo!. Matokeo yake nilipigwa marufuku na mahakama kumtembelea mwanangu maana mke wangu alihofia kuwa ningeweza kuja kumteka mwanangu na kumpeleka Palestina. Hivi sasa sipati nafasi ya kumuona mara kwa mara. 

Uzoefu wangu wa pili kuhusiana makanisa ulikuwa ni chuoni wakati mimi na rafiki yangu wa kike wa Kiarabu tulianza kujadiliana juu ya uwezekano wa kuwa Wakristo kwa kuwa tu tuliona ni dini isiyo na masharti magumu. Tulijua kuwa kile tulichokuwa tunakifanya ni kibaya na adhabu ya kuuacha Uislamu ni kupigwa mawe, lakini tulikuwa tunahitaji itikadi itakayohalalisha maisha yetu ya dhambi. Kutokana na ukaribisho tuliopata kutoka kwa msichana mmoja Mkristo wa Kiarabu kutoka pale chuoni, tulienda kutembelea kanisa lake Jumapili moja. Ibada ilikuwa imejaa furaha, jambo ambalo sikuwahi kuliona kwenye Uislamu. Baada ya ibada, tulipatiwa Biblia na kitabu kinachohusu Uungu wa Yesu Kristo. Miezi michache baadaye wakati wa mkesha wa Krismasi, tulitafuta kanisa ambako baadhi ya marafiki zetu wa Kiarabu walio Wakristo kutoka chuoni kwetu walituambia habari zake. Lakini tulishangaa kukuta limefungwa.

Nilikuwa na rafiki yangu aitwaye Khalil, ambaye tulikuwa tunazungumza pamoja juu ya maisha na hali ya dunia. Wakati mwingine tulikuwa tukijiuliza maswali kuhusu Uislamu na kushangaa kwa nini mambo ni hovyo sana kwenye nchi za Kiislamu. Tulikuwa tukijiuliza iwapo dini hii, ambayo hata hatukuifuata kikamilifu, ilikuwa ni dini ya kweli. Lakini maswali yetu hayakutufanya tufanye uamuzi wa mara moja. 

Nilioa tena. Safari hii ilikuwa ni ndoa ya kupangwa. Nilioana na msichana mmoja kutoka Palestina. Hii ilitokea baada ya familia yangu kunikatalia katakata kumuoa msichana wangu wa chuoni wakidai kuwa hakuwa safi kiasi cha kutosha kwa ajili yao. Nilimleta mke wangu mpya hadi Marekani, lakini nilikuta ni vigumu sana kumpenda maana hata sikuwa namfahamu vizuri. Kwa hiyo, nilikuwa nafurahi kwa sababu kazi yangu ilikuwa inanifanya niende mji hadi mji. Hiyo iliniwezesha kufanya mambo yangu ambayo hata hakuna haja ya kuyasema (ikiwa ni pamoja na kuwa na msichana kwenye kila mji.

Kisha Septemba 11, 2001, ilitokea.  Majengo pacha ya ghorofa yalipoanguka [kule Marekani baada ya kulipuliwa na ndege zilizobamizwa humo], heshima kidogo iliyokuwa imesallia kwangu juu ya Uislamu nayo iliporomoka yote. Suala hili lilinisukuma kabisa kwenye kuanza kuitafuta Kweli.

Niliachishwa kazi kutokana na hali ngumu ya uchumi iliyosababishwa na tukio la 9 -11. Wakati nikiwa kwenye mtandao wa intaneti kila siku kutafuta kazi, “kwa namna fulani”, kila mara nilijikuta nikiangukia kwenye mitandao ya majadiliano ya Kikristo. Na hata siku moja niliweza kupata Biblia ya Kiarabu kwenye mtandao.

Usiku mmoja wakati wa majira ya baridi nilijikuta nikisoma Injili ya Yohana. Sikuwa nikiiamini Biblia hata kidogo, maana nilikuwa nimefundishwa maisha yangu yote kuwa Biblia ni kitabu ambacho kimebadilishwa na wanadamu.

Lakini nilipoanza kusoma, nilishangaa. Nilianza kusoma juu ya Yesu na maisha yake mazuri, safi, yasiyo na dhambi, matakatifu, ya kushangaza, na ya kimiujiza, na sikuweza kuiweka Biblia ile chini. Nakumbuka nilisoma Injili ile yote mwanzo hadi mwisho. Nilipomaliza kusoma, ilikuwa tayari ni alfajiri! Nilikuwa nalia sana kiasi kwamba niliogopa kwamba ningemuamsha mke wangu. Sikutaka anione nikilia ili asije akaniuliza ni kwa nini ninalia.

Siku chache baadaye, nilifungua kompyuta yangu, na kwa sababu nisiyoijua, nikawa natafuta makanisa ya Kiarabu yaliyo kwenye eneo lile. Hatimaye nilipiga simu kwenye kanisa mojawapo. Upande wa pili, simu ilipokelewa na aliyepokea akaniambia kuwa baba yake alikuwa ndiye mchungaji, lakini alishakufa. Alinipatia namba nyingine ya kupiga – kwa mtu aliyeitwa Farooq. Huyu bwana ndiye mchungaji wangu hadi sasa na ni mtu ambaye Bwana amemchagua awe wa kunifikisha kwake. Tulijadiliana mambo mengi ya ndani kama vile tabia na haiba ya Muhammad, maisha yake, wake zake wengi aliooa na vita alivyopigana. Farooq alinipatia kitabu alichoandika ambacho kinalinganisha Uislamu na Ukristo, kikiwa na rejea kutoka kwenye Quran na Biblia.

Nilipoanza kusoma kitabu cha Farooq, nilipatwa na mshtuko pamoja na mshangao. Nilizitafuta rejea zote za Biblia na za Quran – zote zilikuwa sahihi – na sikuamini macho yangu! Nilitambua kuwa kumbe nilikuwa nimedanganyika maisha yangu yote! Jambo kubwa lililonivuta lilikuwa ni tofauti ya jinsi dini hizi mbili zinavyowatendea wanawake.  

Sikumbuki siku hasa ambayo Farooq aliniongoza kuomba sala ya kumpokea Bwana na Mwokozi, lakini ilikuwa ni kwenye mapema mwaka 2002. Ninaikumbuka fika siku niliyobatizwa. Ilikuwa ni siku ya ajabu sana na pia iliniogopesha! Na hivi sasa nimeshakuwa mtu tofauti sana tangu nilipomkubali Kristo.  Niko huru! Nimeshatambua kuwa hakuna kamwe ulinganifu kati ya Ukristo na Uislamu. Pale ambapo mwanzoni nilikuwa nina sheria na taratibu nyingi za kufuata kutoka kwenye Quran na Hadithi, hivi sasa nina uhusiano na Mungu. Ni tofauti kabisa. Uislamu unategemea kulazimisha, lakini Ukristo unaleta amani na upendo mwingi sana. Hivi sasa mimi ni mtu tofauti kabisa. Nimejitoa kikamilifu kwa mke wangu na ninaendelea kujifunza kumpenda. Hivi sasa, badala ya kwenda kwenye starehe, ninasoma Biblia. Ninahudhuria kanisani na kwenye masomo ya Biblia kila ninapoweza. Na sina chuki tena dhidi ya Wayahudi.

Nimekuwa nikimweleza karibu kila mtu ninayekutana naye huu ushuhuda wangu na imani yangu. Nilishawaeleza familia yangu, wafanyakazi wenzangu, na hata watu tu wa mtaani. Familia yangu hawakufurahia sana, hususani mke wangu ambaye bado hataki kukubali kwamba nimeshabadili dini. Anadhani kuwa iko siku fahamu zangu zitanirudia hivyo nitarudi kwenye Uislamu. Familia yangu, kwa upande mwingine, walijaribu kunirudisha kwenye Uislamu kwa njia ya hoja na mijadala juu ya Uislamu na Ukristo, baadaye wakaamua kunipuuza. Lakini hatimaye wakafika mahali pa kukubaliana na hali yangu kutokana na uhusiano mzuri na wa upendo tulio nao. Kama tungekuwa bado tunaishi Palestina, nina uhakika kuwa wangeshanikataa au hata kutishia maisha yangu.

Tuesday, August 4, 2015

UISLAM NI DINI YA MAKAFIRI

Ndugu msomaji,

Hakuna ubishi katika hili, kuwa Dini inayo thibitisha kuwa wao ni Makafiri ni ya Uislam. 

Nini Maana ya Kafiri?

Neno Kafir limetoka katika neno "Kafara" likiwa lina maanisha kupinga Mungu, kuficha , kukataa au kufuru . Kwa hiyo, kaafir ni Mtu au Kiumbe au Roho au Malaika au miungu anaye kufuru, anakataa au anakanusha.

USHAHIDI WAKUPINGA MUNGU KATIKA UISLAM
Shahada: LA ILAHA ILLALLAH Muhammadur Rasulullah, Quran 3:18 na soma hapa pia (Sahih Al-Bukhari, Volume 4, Book 56, Number 725)

Hakuna Mungu ila Allah na Muhammad ni Mtume wa Allah. Hii ni Shahada wanayo sema Waislam au mtu anaye taka kuwa Muislam.

Hii Shahada katika Surat Ali Imran inasema kuwa Hakuna Mungu ila Allah. Huu ni mtego ambao Ibilisi anautumia kwa hwa Waislam na wanakanusha kuwepo na au uwepo wa Mungu. Zaidi ya hapo, Waislam wanakanusha na au ficha ukweli kuwa Yesu ni Mungu.

Hivyobasi, kufuatana na ushahid yakinifu hapo juu wa SHAHADA ya LA ILAHA ILLALLAH Muhammadur Rasulullah, leo tumejifunza kuwa Allah wa Waislam na Mtume wake na Waislam wote wanapinga uwepo wa Mungu na kufanikiwa kuwa MAKAFIRI kutokana na maana ya KAFIR katika Uislam.

Ngoja niweke maana ya hiyo SHAHADA neno kwa neno:

Maneno hayo manne "lâ ilâha illâ allâh" yana maanisha hivi:
:
lâ = HAKUNA,  no, not, none, neither
ilâha = MUNGU, a god, deity, object of worship
illâ = ISIPOKUWA but, except (illâ is a contraction of in-lâ, literally if not)
allâh = ALLAH, allâh

Kama tulivyo soma hapo juu maana ya hayo maneno Manne. Utangundua kuwa Neno ILAHA maana yake ni MUNGU na Neno ALLAH halina Tafsir na kubakia ALLAH (Thibitisha kupitia Al Tafsir Kitengo cha Tafsir cha Serikali ya Saudi Arabia/ http://www.altafsir.com/). 

Huo ndio mtego wenyewe. Kumbuka Allah hana wa kufananishwa na au linganishwa. Hivyo Kumfananisha Allah na Mungu wa Buddah, au Mungu wa Rasta Fari au na Mungu wa Wabantu ni KUKUFUR. Allah yeye kasema hana wa kufananishwa wala linganishwa. Kumbe basi Allah sio Mungu. 

Allah Anasema:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ وَهُوَ السَّمِيعُ البَصِيرُ
"Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona."
Ash-Shuuraa – 11
Hivyo basi, Allah ni Kafir. Muhammad ni Kafir na Waisla wote ni Makafir maana wote wanapinga Uwepo wa Mungu kwa kusema Shahada.

Tusome Biblia na tuone inasemaje kuhusu mtu anaye sema hakuna Mungu:

Biblia inasema: Zaburi 14: 1; Mpumbavu asema moyoni mwake hakuna Mungu wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo hakuna atendaye mema.

Jibu mmesha pata kuhusu mtu yeyote yule (na/au kiumbe chechote kile) anayesema hakuna Mungu.

Leo tumejifunza kutoka Uislam kuwa, MAKAFIR ni WAISLAM na sio Wakristo wanakubali Mungu.

Mungu awabariki sana,

Karibu kwa Yesu aliye hai na Mungu Mkuu,

Mungu awabariki sana,

Katika Huduma Yake,

Max Shimba Ministries Org.

MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

TRENDING NOW