Thursday, April 7, 2016

YESU KRISTO ALIKUJA KWA MATAIFA YOTE


Nawasalimu kwa jina la YESU KRISTO WA NAZARETI aliye hai na ndiye aliye Mwana wa MUNGU wa pekee na mpaka sasa hajatokea kama yeye na hatatokea mwingine zaidi yake.
Katika Ujumbe huu, ningependa tujikumbushe kidogo kazi ambayo tulipewa na Yesu Kristo ya kuhubiri Injili kwa mataifa yote.
MAANA YA INJILI:
Injili ikiwa na maana ya Habari Njema kama ilivyo fundishwa na Yesu Kristo, ndio Neno tulilopewa sisi Wafuasi wa Yesu kulitanganza kwa Mataifa yote.
Hebu tuendelee kusoma yale ambayo Yesu aliwaagiza wafuasi Wake wa kweli, ambao waliamini kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu, ni Masiya.
Kueneza injili ni kazi ya wakristo wote ulimwenguni.
Imeandikwa:
Mathayo 28:19-20 "basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho mtakatifu na kuwafundisha kuyashika yote niliyo waamuru ninyi na tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari."
Habari njema nilazima ihubiriwe kote kabla ya kurudi kwa Yesu. Imeandikwa Mathayo 24:14 "Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote hapo ndipo ule mwisho utakapokuja."
Tumeitwa tuwe mabalozi wa Yesu imeandikwa:
2 Wakorintho 5:20 "Basi tuwajumbe kwa ajili ya Kristo kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu."
Kueneza injili nikuzungumza kwaniaba yake Mungu na kuutangaza ukweli wake imeandikwa Marko 16:15 na Yohana 13:35 "Akawaambia enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe... hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mikiwa na upendo ninyi kwa ninyi."
Injili ni zaidi ya kuhubiri na ushuhuda imeandikwa Isaya 60:1 "Ondoka ukaangaze kwakuwa nuru yako imekujia na utukufu wa Bwana umekuzunguka. Imeandikwa Isaya 61:1 " Roho ya Bwana Mungu I juu yangu kwa sababu Bwana amenitia mafuta ni wahubiri wanyenyekevu habari njema amenituma ili kuwanganga waliovunjika moyo kuwatangazia mateka uhuru wao na hao walio fungwa habari ya kufunguliwa kwao."
Yesu anamalizia mahubiri Yake yote kwa mfano. Bila shaka ni mfano wenye kuonyesha mahusiano kati ya wokovu na utii.
“Basi, kila asikiaye hayo maneno yangu na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa” (Mathayo 7:24-27).
Mfano wa mwisho wa Yesu si “njia ya kufanikiwa maishani” kama wengine wanavyotumia. Mada siyo jinsi ya kufanikiwa kifedha wakati mambo ni magumu, kwa kuziamini ahadi za Yesu. Hili ni hitimisho la yote ambayo Bwana Yesu alisema katika Mahubiri Yake pale Mlimani. Wale wanaotenda aliyosema ni wenye hekima nao watadumu; hawana haja ya kuogopa ghadhabu au hasira ya Mungu. Wale wasiomtii Yeye ni wapumbavu na watateseka kweli, na kupata “adhabu ya kuangamia milele” (2Wathes. 1:9).
Yesu aliwaambia wanafunzi Wake hivi: “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi … na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi …” (Mathayo 28:19-20 – Maneno mepesi kutilia mkazo).
NDUGU ZANGUNI:
Tumepewa kazi na Yesu Kristo ya kuihubiri Injili kwa Mataifa yote. Hii kazi ya kuhubiri Injil ni ya Wakristo wote, haijalishi wewe ni Meneja, Mwalimu, Mwanafunzi, Mchungaji, Polisi, Fundi, Dereva, na nk. Yesu amepewa Mamlaka yote Mbiguni na Duniani. Ushindi ni wetu katika jina lake lililo zaidi ya majina yote.
Mashetani yote yanatetemeka wanapo sikia Jina la Yesu.
Misukule yote inaachia na watu wanakuwa huru wanapo sikia Jina la Yesu.
Walio fungwa na Nguvu za Giza wanakuwa Huru katika Jina la Yesu.
Walio potea katika dhambi wanawekwa Huru kupitia Jina la Yesu.
Wagonjwa wanapona katika Jina la Yesu.
Jina la Yesu lina Mamlaka yote, duniani na Mbinguni.
Twendeni na tufanye kazi ya Bwana katika Mataifa yote.
Yesu ni yule yule, Jana, Leo na Hata Milele.
Mungu awabariki sana,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 7, 2016

Tuesday, April 5, 2016

SHOGA MAARUFU WA KIISLAMU DAR AOKOKA, NA KUACHANA NA USHOGA NI ANTI ASU (OTHUMAN HAMIS) SASA ANAITWA AMOSI


Ndugu wasomaji,
Kwanza nitaanza na kuweka aya na hadith kutoka Uislam:
*************************************************************
BALAA: KUMBE WANAUME WA KIISLAM WAMERUHUSIWA KUINGILIANA KIMWILI.
Surah An Nisaai 21. Na mtachukuaje na ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti?
HUU SI NDIO ULIBERIA HUU. WAISLAM WANAINGILIANA WAO KWA WAO. HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.
SASA NA WAKE ZAO WAMEJIFUNZA KWA WAUME WAO JINSI YA KUINGILIANA WAO KWA WAO.
Sasa soma hadith zinazo sema Muhammad alifanya hii tabia mbaya.
SIFA ZA NABII MUHAMMAD (PBUH). ANYONYA ULIMI WA MWANAUME MWENZAKE
Hadith Idadi 16,245: "maneno ya Washami," Hadith ya Mu'awiya Ibn Abu Sufyan": "Nilimwona Nabii wa Allah(saw) - akimnyonya ulimi na kulamba mdomo wa Al-Hassan Mwana wa Ali, Mwenyezi Mungu amrehemu, maana hakuna mtu atakaye teswa kwa Moto wa Jehannam baada ya kunyonywa ulimi na kulambwa midomo na Nabii wa Allah.
Mnaona tabia chafu ya Nabii wa Allah?
Eti akikula denda na kukulamba midomo basi wewe huto kwenda Jehannam.
Pia alisema, "Siku baadaye tuliomba muuguzi kwa ajili yake (Ali) lakini alikataa, basi tukamwita Nabii Muhammad - SAW -.ambaye alimnyonya ulimi "Ali" kwa kinywa chahe mpaka akalala. Hivi ndivyo Allah alivyo taka Ali afanyiwe na Nabii wake.
************************************************************
Tamaa ya kua na mke na kuitwa baba, ndiyo imemfanya shoga maarufu jijini Dar es Salaam anaye julikana kwa jina la Othuman Hamis au Anti Asu kuamua kuvua gwanda la kua `mototo si riziki’ na kuvaa gwanda jingine la `kidume cha mbegu’.
Anti Asu ambaye pia ameamua kuokoka na kukiri hadharani kwamba hataurejea kamwe ushoga, inaelezwa kwamba kwa sasa anatafuta mke wa kumzalia watoto na ambaye atampa mapenzi ya dhati.
Imedaiwa kwamba, hivi karibuni Othuman alijisalimisha katika kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), lililopo Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam ambako alitubu dhambi zake. Sani liliamua kuingia mzigoni kufuatilia `ishu’ hiyo ambapo lilifanikiwa kumnasa Othuman akiwa katika saluni moja ya kike iitwayo Emmy’s iliyopo Magomeni Mapipa jijini anakofanya kazi. Alipoulizwa kuhusiana na taarifa za kuukana ushoga, kijana huyo alithibitisha ni kweli ameacha tabia hizo na kwa sasa ameokoka baada ya kubadili dini kutoka kwenye uislamu na kwenda kwenye ukristo akiitwa Amos. ``Nimeokoka kiukweli kabisa. Sitaki tena kuusikia ushoga. Nimemkaribisha mungu katika maisha yangu. Najutia dhambi zangu na namuomba yeye (Mungu) anisimamie na kunilinda ili nisiweze kuanguka tena,’’ alisema Anti Asu ambaye anaonekana ni mwanaume halisi. Amesema kwamba, ameamua kuanza maisha mapya na kwamba anaishi katika kanisa la TAG Magomeni ambako amekuwa akikesha kwa maombi.
``Mimi nilikua shoga namba moja Tanzania baada ya marehemu Anti Kessy. Hakuna alieyekua ananifikia.Nimevunja ndoa zaidi ya 30 na nimetembea na wanaume hata zaidi ya 200. Nimeishi kinyumba na wanaume zaidi ya 10. Nimebwakwa na kufanya kila aina ya ufilauni. Nani ambaye alikua ananifikia mimi? Shoga gani ajitokeze hapa. Lakini sasa nimeachana na yote haya baada ya kubaini nilikua naitwa na Mungu. Nimeludi kwake na ninahisi amani moyoni mwangu,’’ amesema.
Ameongeza kwamba kwa sasa anajiandaa kuoa kwani alipima kama ana maambukizi ya maradhi ya Ukimwi na majibu yameonyesha kwamba yupo salama.`` Nashukuru kwamba hata jogoo anawika.’’ Aliongeza kwamba sababu nyingine nyingine iliyosababisha aokoke ni kutoka na na kuugua sana tangu alipokumbwa na tukio la kubakwa na wanaume zaidi ya 10. Mchungaji Kiongozi wa kanisa la TAG Magomeni Mikumi Dunstan kanemba amethibitisha kuokoka kwa Anti Asu na kusema kwamba yeye ndiye aliyemuombea na kumkaribisha rasmi kanisani hapo. ``NI kweli Amosi (Anti Asu) tunaye hapa.Ibada ya Jumapili iliyopita tulimuombea hadharani na alidondoka chini. Hii ni ishara kwamba alikua na mapepo yanayomsumbua. Kanisa limempa hifadhi ya kuishi hapawakati tunamjenga kiroho. Pia tunamhudumia kwa mavazi na mahitaji mengine,’’ alisema Kanemba. Aliongeza kwamba uamuzi aliofanya kijana huyo ni wa msingi na kuwataka watu wengine ndani ya jamii wenye matatizo kama hayo kufika kanisani hapo kupata msaada wa maombi. ``kwa yoyote anayehitaji kumsaidia zaidi kimwili basi asisite kufika hapa kanisani. Tunaamini kuwa kuokoka kwake kutasaidia sana kuwafanya vijana wengine wenye tabia hiyo kuokoka pia au kuacha’’ alisema Kanemba.
Moja ya habari za zamani za anti asu ambaye sasa anaitwa Amosi baada ya kuokoka.
UKIWA MUISLAMU MATAKO TAKO YANAKUWA NI SEHEMU YA SHETANI KUJIBURUDISHA KWA MICHEZO YAKE.
Kasema Mtume (s.a.w) “Anamwijia mmoja wenu shetani katika sala, basi anapuliza (anampuliza) katika matako yake, basi yule mtu inamwijia fikiria ya kuwa umemtoka upepo (kajamba) nae haukumtoka, basi akiona hali hiyo asiondoke kwenye sala mpaka asikie sauti ya kumtoka huo upepo au anuse harufu yake”. (KITABU CHA MKWELI MWAMIU, JUZUU YA 1 -2 HADITHI NA. 74, UK 42)
Sasa hiyo adha ya kupulizwa matako na shetani kwa kila unaposali nani anaitaka? Yaani kila ukienda kusali basi shetani yeye yupo matakoni tu, najiuliza hivi shetani ambaye ni muislamu hakuona sehemu nyingine mpaka akomae na matako tu? Kina mama Wa Kiislamu zindukeni, maana Wanaume wao wameshazoea, ndiyo maana hawataki ninyi mwende msikitini ili mpulizwe pamoja nao, hivyo sisi Wakristo tunaojitambua, kwa tendo hilo la kupulizwa matakoni na shetani hatuutaki uislamu.
By permission.
For Max Shimba Ministries Org.

ASILI YA QURAN NA UISLAM NI SHETANI



Ndugu msomaji,
Leo tutajifunza asili na au mwanzo wa Quran na Uislam ni nini na au nani?
Bila ya kupoteza muda, hebu tuanze kusoma vitabu vya Waislamu.
KAMA MUHAMMAD ALIZALIWA NA SHETANI, AKACHEZEWA NA MASHETANI MNAMFUATA KWA LIPI?
1. KUZALIWA KWAKE MUHAMMAD,
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa "Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa na shetani tangu alipozaliwa, (Fat'hul Baary Juzuu ya 6 Uk. 389).
Katika uthibitisho tulio usoma hapo juu, tumejifunza kuwa Muhammad alizaliwa kwa nguvu za Mashetani na huo mwanzo ni mbaya sana maana hatuna aya au hadith ambayo inasema kuwa, Muhammad alitolewa hayo Mashetani alipopewa unabii na kiumbe cha ajabu ajabu.
Cha kushangaza, Muhammad anapewa unabii na kiumbe cha ajabu ambacho kilimpiga kabali/loba mpaka Muhammad akaweeseka na kuona nyotanyota. Soma uthibitisho hapa chini.
2. MUHAMMAD BAADA YA KUTOKA PANGONI ANIKIRI YAFUATAYO,
Basi Mtume akafanya khofu, akarejea kwa mkewe, akamhadithia, na pale pale homa kubwa kabisa, ikampanda, akataka afunikwe maguo, akawa anatetemeka kwa ngerema, na kuweweseka, na kusema, "Najikhofia nafsi yangu, kuchezewa na mashetani, na kuniharibu akili yangu na kunizuga"(Kitabu cha maisha ya Nabii Muhamaad s.a, uk.17 kilichoandikwa na Sheiky A.Farsy).
Umesoma mwenyewe na kuelewa kuwa kitendo cha Muhammad kupigwa mpaka kuweweseka namna hii hakika hakitoki kwa Mungu wa Adam, Ibrahim, Musa na Mitume wengine wa Biblia. Maana hakuna aya hata moja kwenye Biblia Takatifu inayosema kuwa Manabii wake wapigwa kabali na Malaika, bali tunasoma kuwa Manabii wote wa kwenye Biblia wapiewa Utume na Mungu mwenyewe na sio kiumbe cha ajabu kilicho msimika utume Muhammad usiku tena kwenye pango.
3. KUROGWA KWAKE MUHAMMAD,
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo.
(Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MUHAMMAD ALIYECHEWA NA MASHETANI?
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM, MAANA SASA TUNAFAHAMU KUWA MUHAMMAD SIO TU ALIZALIWA NA MASHETANI BALI ALIONGEZEWA MASHETANI KWA KUROGWA.
Ingawa hakuna aya au hadith inayo sema kuwa Muhammad alitolewa Mashetani, hivyo sio kosa kukiri kuwa Muhammad alikufa akiwa na Mashetani ndani ya nyoyo yake na hivyo mwisho wake ni Jehannam ya moto.
Msiba ukaendelea baadae, sasa na Mwandishi wa Quran na yeye kapagawa na Mashetani.
Jamani, hivi, kwanini Waislam hawasomi vitabu vyao?
KUMBE ALIYEANDIKA QURAN ALIKUWA NA SHETANI?
SOMA:
Mtu wa Awali, aliyejifundisha kusoma na kuandika katika Mji wa Makka alikuwa Bwana Harb bin Umayya-babu yake Bwana Muawiya. Alijifunza kwa watu wa Yaman, na yeye akaja kuwafundisha waliotaka katika mji wa Makka.
Wakati Mtume alipopata utume walikuwako watu 6 tu katika Makka waliokuwa wakijiua kuandika. Wa 4 katika yao waliingia katika Uislamu, wakawa ndiyo waandikaji "Wahyi" (aya za Qur'an), watu hao walikuwa ni Sayyidna Abubakar. Sayydna Umar, Sayyidna Uthman na Sayyidna Ali. (Kitabu cha Maisha ya Nabii Muhammad uk. 8,na Sheiky A.Falsy)
SAYYIDNA ABUBAKAR,
Abubakar, Anasema: "Hakika mimi ninae shetani hunifikia mara kwa mara, basi wakati wowote atakaponifikia muniepuke" (Tabaqatul Kubra, J. 3 Uk. 212)
SASA KAMA "QURAN" KILIANDIKWA NA MTU ALIYEKUWA NA SHETANI, KWA NINI TUSIKUBALI KUWA NI AYA ZA SHETANI?
Ndugu msomaji, nakusihi uwe makini na Uislam maana hakuna jema kule zaidi ya Mashetani kila kona. Kuanzia Muhammad, Quran mpaka Allah wao, wote wamethibitisha kuwa Shetani ndio aliye kwenye nyoyo zao.
Sasa kwanini ufuate Shetani wakati Mungu Mkuu yupo na anakupenda?
YESU NDIO NJIA PKEE YA WOKOVU. ALLAH SIO NJIA. MUHAMMAD SIO NJIA. QURAN SIO NJIA.
Yesu ndiye njia ya pekee ya wokovu kwasababu yeye pekee anaweza kutulipia adhabu ya dhambi zetu (Warumi 6:23). Hakuna dini nyengine yoyote ifundishayo kwa kina au uzito wa dhambi na madhara yake. Hakuna dini nyengine yoyote inayogarimia malipo ya dhambi isipokuwa Yesu pekee. Hakuna “mwanzilishi wa dini” mwengine ambapo Mungu alifanyika kuwa mwanadamu (Yohana1:1, 14) - njia ya pekee ya kuweza kulipa deni. Ilibidi Yesu kuwa Mungu ili aweze kutulipia deni. Ilibidi Yesu afanyike kuwa mwanadamu ili aweze kufa. Wokuvu unapatikana kwa imani ndani ya Yesu Kristo! “Wala hakuna wokovu katika mwengine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya Mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” (Matendo 4:12).
Je, umefanya uamuzi kwa Kristo kwa kile ulicho soma hapa?
Hakikisha unaelewa maana ya wokovu.
1 Yohana 5:13 anatuambia,” Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue yakuwa mna uzima wa milele. Mungu anataka tuelewe maana ya wokovu.Mungu anataka tuwe na ujasiri wa kufahamu kwa kweli kwamba tumeokoka. Kwa ufupi tu,wacha tuviendee vipengele muhimu vya wokovu:
(a) Sote tumefanya dhambi.Sote tumefanya mambo ambayo hayampendezi Mungu (Warumi 3:23).
(b) Kwasababu ya dhambi zetu,tunastahili kuadhibiwa kwa kutengwa milele na Mungu (Warumi 6:23).
(c) Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu (Warumi 5:8; 2 Wakorintho 5:21).Yesu alitufia pahali petu,kwa kuchukua adhabu ambayo sisi tulistahili. Kufufuka kwake kulidhihirisha yakuwa kifo chake Yesu kilitosha kutulipia dhambi zetu.
(d) Mungu hutoa msamaha na wokovu kwa wote wale wamuaminio Yesu – kwa kuamini kifo chake kama malipo ya dhambi zetu (Yohana 3:16; Warumi 5:1; Warumi 8:1).
Hizo ndizo habari za wokovu! Ikiwa umeweka imani yako kwa Yesu kama mwokozi wako, umeokoka! Dhambi zako zote zimesamehewa na Mungu ana ahidi kutokuacha wala kutokutenga (Warumi 8:38;Mathayo 28:20).Kumbuka,wokovu wako uko salama ndani ya Yesu Kristo (Yohana 10:28-29). Ukiwa unamuamini Yesu pekee kama mwokozi wako, unaweza kuwa na uhakika yakuwa utaishi milele na Mungu mbinguni!
Mungu awabariki sana,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 5, 2016

MCHAWI AJISALIMISHA KANISANI TAG MAGOMENI

Mchungaji Kanemba akiangalia vifaa vya kishirikina vya kijana huyo.
Haya ndio yaliyotokea Jumapili katika Kanisa la TAG Magomeni Mikumi kituoni jijini Dar es salaam. Katika mwendelezo wa ushuhudiaji wa shabaha ambapo kijana aliyekuwa akitumikishwa na shetani katika mambo ya kichawi kuamua kuokoka na kukabidhi sanduku lake lenye vifaa vya kichawi ili vichomwe moto.

Kijana huyu ambaye ni dereva wa bodaboda na ni mkazi wa Magomeni Mapipa aliamua kwa hiari yake kuokoka wakati wa ibada kuu ya jumapili kanisani hapo alipokwenda kuabudu ambapo baada ya ibada alikwenda kwa mazungumzo ofisini kwa Mchungaji Kanemba akiwa yeye na mama yake ambako aliomba alete vitu vyake vya kichawi ili vichomwe moto  jambo ambalo lilitekelezwa.

Tukio hilo lilipelekea kilio kikuu kwa mama yake mzazi maana hakuwa akijua kuwa mwanaye huyo alikuwa anajishughulisha na mambo ya kichawi, kijana alieleza matumizi ya vifaa hivyo vya kichawi; ikiwemo na mvuto ki-biashara, mvuto wa ki-mapenzi na hata kuwadhulu wabaya wake jambo ambalo liliwaacha watu waliokuwa wakishuhudia tukio hilo kwa mshangao na wengine wakimtukuza Mungu.

Mchungaji Kanemba alimwombea rehema za Mungu kijana huyo na kuongoza shughuli nzima ya kuteketeza uchawi kwa moto wa petroli na kisha kumshauri kijana jinsi ya kuishi maisha ya wokovu, ambapo kijana huyo na mama yake wamekuwa washarika wa kanisa hilo wakimtukuza Mungu kwa matendo makuu aliyowatendea.

Mchungaji Kanemba akizungumza na kijana huyo ofisini kwake.
Mchungaji Kanemba akatoka kujionea mambo yote.
Vifaa vya kichawi ndani ya sanduku.
Mchungaji Kanemba akiangalia daftari lenye maelezo mbalimbali ndani yake. 

Mchungaji Kanemba akionyesha yaliyokuwamo ndani ya sanduku hilo.

Kijana akimweleza mchungaji Kanemba jinsi alivyokuwa akitumia vifaa hivyo.
Mama wa kijana akilia baada ya kugundua aliyokuwa akifanya kijana wake.
Vitu vikiteketezwa.
Mchungaji Kanemba akimfanyia maombi kijana huyo. Picha na habari kwa hisani ya Martmalecela.blogspot.com.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2013/10/mchawi-ajisalimisha-kanisani-tag.html#sthash.k3eFL7IH.dpuf

Monday, April 4, 2016

KHALIL GAIDI WA KIISLAM AMPOKEA YESU




Huu ni ushuhuda wa kweli kabisa kutoka kwa kijana wa Kimisri ambaye Bwana Yesu mwenyewe alimtoa kutoka kwenye uasi na kumfanya kuwa mtu mpya kabisa anayempenda Bwana Yesu pamoja na wanadamu wenzake wote.


Khalil alianza kukariri Qur’an angali mdogo sana. Baadaye alianza kusoma vitabu vingine vinavyozungumzia Uislamu na tafsiri ya Qur’an. Kulingana na welewa wake juu ya Quran, alifikia mahali ambapo hata wazazi wake aliwaona ni makafiri. Kwake, kama mwanamke aliacha hata kujifunika ushungi, basi anakuwa si Mwislamu tena. Khalil aliwaona Wakristo kuwa ni maadui zake wakubwa na akaanza kujihusisha na mashambulizi dhidi yao pamoja na makanisa. Kundi la Kiislamu ambalo lilikuwa na mipango ya kuangusha serikali isiyo ya kidini ya Misri na kusimika sheria kali za Kiislamu, walimchukua ili awe mmoja wao, kisha wakamfanya kuwa kiongozi wa eneo lake.


Lakini hatimaye, vyombo vya usalama viligundua njama hizo na kumkamata Khalil pamoja na wanakikundi wenzake wengi. Alikaa gerezani miaka miwili. Alipoachiwa, alikimbilia Yemen pamoja na baadhi ya wenzake. Huko waliendelea na mipango yao ya kujiandaa kuangusha utawala wa Misri.


Kule nako mipango yao iligundulika na wengi wao walikamatwa tena. Matokeo yake kikundi kile kiliamua kuachana na mipango yao ya kuangusha utawala kwa njia ya kijeshi. Aliporudi Misri, siku moja alisoma kwenye gazeti juu ya Wakristo waliokamatwa kwa kuwahubiria watu Injili. Khalil na wenzake waliamua kuwa inabidi wafanye jambo kwa ajili ya Uislamu.


Kwa vile sasa walikuwa wachache, waliamua kuwa vita yao wataifanya kwa kutumia elimu, utafiti na kuandika kitabu ambacho kinaonyesha kuwa Mohammad ni Mtume wa kweli wa Mungu; na kwamba Biblia ya Wakristo na Wayahudi ni maandiko ambayo yamepotoshwa kwa kuingizwa mambo ambayo si ya Mungu. Khalil aliteuliwa na Amir, (yaani kiongozi wa Kundi la Kiislamu), ili afanye huo utafiti na kuandika kitabu hicho. Mwanzoni, Khalil alikataa katakata, maana kulingana na maneno yake, mama yake alishawahi kusema kuwa Wakristo hutumia kitabu hicho kulaani watu na kufanyia mambo ya kimazingara; na kwamba mtu anayekisoma kitabu hicho, anapata laana. Hata hivyo, baadaye alikubali; kazi ambayo anasema aliiona kuwa ni mbaya kuliko zote alizowahi kufanya.


Alipomaliza kusoma Biblia na kulinganisha kile alichosoma na kile kilichoko kwenye vitabu vya Kiislamu, Khalil alishangaa sana kuona kuwa Biblia haina mahali ambako haiko sahihi wala mahali ilikoingizwa maneno yasiyo ya Mungu. Badala yake alishangazwa na mafundisho ya Biblia yanayohusu kusamehe na kuwa na upendo usio na masharti. Alishangazwa zaidi aliposoma jinsi Yesu alivyowaonya wafuasi wake kwamba watateswa; na miaka elfu mbili baadaye, hilo lilikuwa linatendeka kama Yesu alivyosema ingekuwa (huku Khalil akiwa ni mmoja wa wanaosababisha mateso hayo kwa wafuasi wa Yesu). Kusoma kwake Biblia kulimwezesha kuelewa kwa nini Wakristo wa Misri hawajawahi kulipiza kisasi kwa Waislamu; na kwa nini mara zote kwao imekuwa rahisi kusamehe na kusahau. Japokuwa alianza akiwa anaichukia kabisa Biblia, alijikuta amependa ujumbe wake na mafundisho yake.


Hata hivyo, jukumu lake alilokabidhiwa lilikuwa bado paleplale likimngoja. Naye aliendelea nalo kwa nguvu kabisa, ili kuthibitisha kwamba Yesu si Mungu na kwamba hakuwahi kusulubiwa. Angali akisoma Qur’an kwa lengo hili, aliandika sifa zote za Mungu kulingana na Quran; kisha akapekua kwenye Qur’an hiyohiyo juu ya sifa za Yesu. Kulingana na Quran, Mungu ni muumbaji, mponyaji, mtoa mahitaji, ndiye pekee anayeweza kufufua wafu, ndiye pekee anayetenda miujiza, ndiye pekee mwenye kuhukumu kwa haki, na kadhalika. Kwa mshangao mkubwa, Khalil aligundua kwamba hizi ndizo sifa zilezile ambazo Qur’an hiyohiyo inampa Yesu (Isa), jambo ambalo lilimthibitishia Khalil kuwa Yesu na Mungu kumbe ni kitu kimoja.


Lakini hapo sasa mashaka yaliingia moyoni mwa Khalil. Maisha yake yakawa ya mateso. Akawa anawaza afuate kipi. Siku zote aliupenda Uislamu na kuamini kuwa ndiyo njia pekee ya kwenda kwa Mungu kupitia Mohammad. Alianza kujiuliza maswali, “Sasa kama Yesu na Mungu ni kitu kimoja, Mohammad ni nani sasa; na njia ya kwenda mbinguni ni ipi?” 


Siku moja, Amir wake alifika kumtembelea nyumbani kwake ili kuona anavyoendelea na utafiti waliokubaliana. Amir aliweza kuona mambo yote ambayo Khalil alikuwa ameandika (uungu wa Yesu, kwamba Qur’an si neno la Mungu, n.k.).  Amir hakuamini macho yake. Alimwambia Khalil kwamba angemuua kama angesema mawazo yake hayo ya kizushi kwa Mwislamu yeyote, na kwamba kuanzia hapo yeye, Khalil, amekuwa ni kafiri!


Khalil, hata hivyo, hakuachana na mawazo aliyoyapata kwamba Ukristo ndiyo njia ya kweli. Huku akiwa na shauku ya kujifunza zaidi, aliamua kwenda kujiunga na kanisa. Kutokana na historia yake ya ukatili na ghasia, hakuna mtu aliyemwamini. Kila mtu alikataa kukutana naye, hata wachungaji nao waligoma. Hapo alikata tamaa na kuwaza kuwa huenda alikosea kuwaza hivyo; labda Ukristo wala si njia ya kwenda mbinguni. Lakini, sauti ndani yake ilimwambia asiwatazame wanadamu.

Siku moja alikuwa anajaribu kupiga simu kwenye kibanda cha simu huku akiwa ameweka begi lake nje ya kibanda. Alipita kibaka na kuiba lile begi. Ndani yake kulikuwa na nyaraka zote za utafiti wake, Biblia na kitambulisho chake. Aliogopa sana kwa sababu kila kitu alichokuwa ameandikwa kingehesabika kuwa ni kufuru; ilhali kuna na kitambulisho chake ndani humo! Alikimbia nyumbani huku akiwa na mawazo mengi sana.


Akiwa chumbani kwake, alianza kutubu kwa yote aliyofanya. Aliwaza kuwa Mungu alikuwa anamwadhibu kwa kuthubutu kuwaza kuwa Mohammad hakutumwa na Mungu na kwamba Qur’an si neno la Mungu. Alitubu, akatawadha, na kuchukua mkeka ili afanye sala. Lakini magoti yalishindwa kukunjika, na wala kinywa chake hakikufunguka kusema hata neno moja la Qur’an. Khalil alikaa chini na kusema, “Mungu unajua kuwa nakupenda, na ninafahamu kuwa unapenda mimi niwe kwenye njia sahihi. Mungu, siwezi kupingana na hilo tena. Kila nilichofanya, nilikuwa najaribu kukupendeza wewe. Tafadhali, nitoe kwenye giza hili.”


Usiku ule, Khalil alilala kwa namna ambayo hakuwahi kulala kwa miaka mingi. Aliota ndoto. Alimwona mwanamume aliyemjia na kumwambia kuwa alikuwa ndiye yule ambaye Khalil amekuwa akimtafuta. Khalil hakujua huyo alikuwa ni nani. Yule mtu alimwambia Khalil aangalie kwenye Kitabu (yaani Biblia). Khalil akasema kuwa Kitabu pamoja na nyaraka zake zote vilipotea. Yule mtu akasema, “Kitabu huwa hakipotei. Inuka ufungue kabati lako, utakikuta humo. Na nyaraka zako zingine utarudishiwa ifikapo mwisho wa wiki.”  


Khalil aliamka kutoka usingizini na kwenda moja kwa moja kufungua kabati. Cha kushangaza, aliikuta Biblia yake palepale, japokuwa iliibwa pamoja na begi lake! Huku akijua kuwa amemwona Yesu, kwa haraka alienda kwenye chumba cha mama yake, akamwamsha, akaanza kumwomba msamaha kutokana na miaka mingi ya ukali na madhila mbalimbali aliyowafanyia familia yake. Hakuishia hapo kutafuta amani na mapatano. Kulipokucha, Khalil aliingia mitaani, akawa anawasalimu marafiki na wageni. Akawatafuta Wakristo wamiliki wa biashara ambao aliwahi kuwaibia, au kuwafanyia ukatili, akawaomba msamaha pia!


Baada ya miezi kadhaa, Khalil alikua katika imani yake mpya; na kidogo kidogo akaanza kuaminiwa na Wakristo wa mahali hapo na akawa ameingia kanisani. Alibatizwa na sasa anaendelea kupambana na mashambulizi ya kimwili na vitisho dhidi ya maisha yake kutoka kwa wale aliokuwa nao zamani. Lakini Khalil anahisi kuwa yuko tayari kulipa gharama yoyote kwa ajili ya Yule ambaye alitoa kila kitu kwa ajili yake, yaani Yesu Kristo.

JE, SABATO NI SI SIKU KATIKA JUMA?


1. Je, Israeli walipokuwa jangwani kwani hawakuwa wakitunza sabato kama siku?
2. Kama basi waliitunza sabato, iweje tena Mungu aseme, ‘Hawataingia rahani mwangu’? 

Ndugu msomaji,

Upo ushahidi wa kutosha katika Biblia unaoonyesha kwamba sabato si siku katika juma. Bwana anapoongelea kuhusu safari ya wana wa Israeli anasema:

Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, nikasema, Siku zote ni watu waliopotoka mioyo hawa ... hawataingia rahani mwangu. (Waebrania 3:10-11).

Pia imeandikwa: Maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote; na hapa napo, Hawataingia rahani mwangu. (Waebrania 4:4-5).

Katika maandiko haya Mungu anasema kwamba, kutokana na kukasirishwa na uasi wa wana wa Israeli kule jangwani, alimua kwamba hawataingia kwenye raha aliyokuwa amewaandalia. Neno rahani hapa, au kwa Kiingereza rest, ndilo hilohilo sabato. Ndiyo maana hapo juu katika Waebrania. 4:4-5, anahusisha siku ya saba na kuingia rahani.

Lakini hebu tujiulize maswali yafuatayo ili tuweze kupiga hatua zaidi.

1. Je, Israeli walipokuwa jangwani kwani hawakuwa wakitunza sabato kama siku?
Jibu ni ndiyo, waliitunza. Biblia inasema: Basi ikawa siku ya sita wakaokota kile chakula sehemu mara dufu, kila mtu pishi mbili; na wazee wote wa mkutano wakaenda na kumwambia Musa. Akawaambia, Ndilo neno alilonena BWANA,Kesho ni starehe takatifu, Sabato takatifu kwa BWANA ... (Kutoka 16:22-23).

2. Kama basi waliitunza sabato, iweje tena Mungu aseme, ‘Hawataingia rahani mwangu’?
Kama ingekuwa ni kumwuliza Mungu, mtu ungesema, “Bwana, unasemaje hawataingia rahani mwako wakati kila siku ya saba wanapumzika?” Hii ni ishara ya wazi kwamba sabato hasa si kupumzika au kutofanya kazi kimwili katika siku ya saba. Sabato ni jambo jingine tofauti na siku ya saba. Iko sabato halisi ambayo siku ya saba na kupumzika kwake vilikuwa ni kivuli chake tu.

Jambo jingine la kujiuliza ni kwamba, japo ni kweli kwamba wale ambao Mungu alisema hawataingia rahani mwake walifia wote jangwani, lakini walikuwapo wengine wengi walioingia, yaani watoto wao. Sasa je, hao walioingia waliipata hiyo raha (sabato)?

Mtu anaweza kujibu, Ndiyo, maana sote tunajua kuwa hata wakati alipokuja Bwana Yesu, alikuwa akifundisha mara nyingi kwenye masinagogi 'siku ya sabato'. Kwa hiyo, mtu anaweza kusema, ‘Ndiyo, waliingia kwenye raha au kwenye sabato.’

Lakini Mungu ambaye ndiye mwenye usemi wa mwisho juu ya mambo yake mwenyewe anasema:

Basi kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao, aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo, kama mtaisikia sauti yake, msifanye migumu mioyo yenu. Maana kama Yoshua angaliwapa raha (yaani sabato), asingaliinena siku nyingine baadaye. Basi imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. (Waebrania. 4:4-9).

Yaani, hawa watu licha ya kwamba kila mwisho wa wiki walikuwa wakipumzika, bado Mungu anasema ‘walikosa kuingia.’ Lakini cha kushangaza zaidi ni kwamba, kumbe hata siku yenyewe ilibadilishwa! Je, umeona hayo maneno ‘aweka tena siku fulani’? Pia hapo mwishoni nako anasema, ‘siku nyingine baadaye’!!

Hebu jiulize, inakuwaje siku nyingine wakati tumesema kwamba hadi Yesu anakuja watu hao walikuwa wakipumzika kila mwisho wa wiki?

Jibu ni wazi kwamba ‘siku nyingine’ hapa haimaanishi siku katika juma – maana hiyo haikuwahi kuachwa! Kwa hiyo, ni wazi kwamba, hii ni ‘siku ya sabato’ tofauti na ile iliyojulikana na kufuatwa tangu siku za Musa!

HOJA YA SABATO KUTOKA KINYWANI MWA MUNGU

Iko hoja kwamba sabato ni amri ya muhimu sana kwa sababu ilitoka moja kwa moja kinywani mwa Mungu tofauti na amri zingine ambazo zililetwa kupitia manabii au mitume.

Hoja hii haina uzito kwa sababu kuu mbili:

1. Biblia kwa ujumla wake ni Neno la Mungu ambalo limetoka kinywani mwake lote. Na maandiko yako wazi kwamba: Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa, apate kutenda kila tendo jema. (2 Timotheo. 3:16-17).

Na kimsingi maandiko haya, ukisoma kwenye Biblia ya Kiingereza, hayasemi “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu”. Badala yake yanasema: All Scripture is God-breathed (NIV); au All scripture is given by inspiration of God (KJV). Hii ina maana kwamba: Maandiko yote yametokana na pumzi ya Mungu.

Kwa hiyo, hakuna mantiki kusema kwamba andiko hili lina maana zaidi kuliko lile kwa kuwa hili alitamka Mungu mwenyewe. Yote yana nguvu ileile; yote yametoka kwa Mungu yuleyule.

2. Sababu ya pili ni kuwa, Bwana Yesu alisema: Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. (Matendo ya Mitume. 10:40).

Maana yake ni kuwa Musa au nabii yeyote hakusema kwa niaba yake au kwa nafsi yake mwenyewe. Maneno waliyoyasema na kuyaandika hayakuwa yao.

Ukimpokea Musa au Paulo na maneno yake, unakuwa umempokea Kristo, na hatimaye Mungu Baba mwenyewe.

Kwa hiyo, si sahihi kudhani kuwa maneno ya Musa au ya Paulo ni yake yeye, na kwamba yana uzito wa chini kuliko yale yaliyotoka kinywani mwa Mungu moja kwa moja kuhusiana na sabato.

Mungu awabariki sana.

By permission: Yesu ni Njia, Injili Timilifu, James John, NKJV, NIV, KJV, Christ Nations and Max Shimba Ministries Org.

Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,

For Max Shimba Ministries Org,

MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED

Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

KWA NINI YESU ALIVUNJA SABATO?


Ndugu msomaji,
Hebu tuangalie mifano kadhaa hapa:
MFANO WA KWANZA
Yesu alipomponya mtu ambaye alikuwa hawezi kwa muda wa miaka 38, alimwambia ‘jitwike godoro lako, uende.’ (Yohana 58). Hii ilikuwa ni siku ya sabato.
Lakini tunaona kwamba Wayahudi walipomwona mtu huyo walimwambia, Leo ni sabato, wala si halali kwako kujitwika godoro. (Yohana 5:10). Bila shaka walisema hivi kwa kuwa walifahamu fika jinsi sabato inavyotakiwa kutunzwa.
Hii ni kusema kwamba, kwa kadiri ya kanuni za utekelezaji wa sabato, hili lilikuwa ni kosa. Sasa, swali ni kwamba, kwa nini Yesu alivunja sabato kwa kumruhusu yule mtu abebe godoro?
MFANO WA PILI
Wayahudi walipomkasirikia Yesu kwa sababu ya kumruhusu yule mtu kubeba godoro siku ya sabato, Bwana Yesu aliwajibu kwamba: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. (Yohana 5:17). Haya ni maneno ya ajabu sana. Wewe uliye Mungu ulituambia kwamba siku ya sabato tusifanye kazi bali tupumzike; tumemwona mtu anafanya kazi ya kubeba godoro, tumekuja kwako, lakini wewe si tu kwamba hukumkemea, bali unasema tena kwamba na wewe unafanya kazi hata sasa (siku ya sabato)!
Kama sabato hasa ni kuacha kufanya kazi, iweje tena Yesu atamke jambo ambalo ni wazi kabisa linavunja sheria aliyoiweka mwenyewe ya kutofanya kazi; yaani aseme kuwa hata sasa yeye anafanya kazi?
MFANO WA TATU
Siku moja Yesu aliingia kwenye sinagogi ambamo mlikuwamo mwanamke mwenye pepo wa udhaifu. Yesu alimponya mama yule.
Hata hivyo, Biblia inasema: Basi mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu amemponya mtu siku ya sabato, akajibu, akawaambia mkutano, Kuna siku sita zifaazo kufanya kazi, basi njoni mponywe katika siku hizo, wala si katika siku ya sabato. (Luka. 13:14).
Maneno haya ya mkuu wa sinagogi yanatuonyesha kwamba, jambo alilofanya Yesu lilikuwa ni kuvunja sabato. Swali ni lilelile, kwa nini Yesu alivunja sabato?
Tunafahamu kuwa maandiko yanasema kwamba kuvunja sabato ni dhambi, tena ambayo iliadhibiwa vikali sana. Na katika mifano hiyo hapo juu, tunaona kwamba Yesu alivunja sabato kwa kufanya mambo ambayo jamii nzima ilikuwa haiyafanyi siku ya sabato. Kwa harakaharaka, mtu anaweza kusema kwamba, Yesu alitenda dhambi.
Lakini wakati huohuo, maandiko yanasema kwamba, katika kuishi kwake kote hapa duniani, Bwana Yesu hakuwahi kutenda dhambi. (Waebrania 4:15).
Swali la kujiuliza hapa ni kwamba, iweje uvunje sabato, jambo ambalo ni dhambi, halafu uhesabiwe kuwa hujatenda dhambi? Pili, iweje wewe ambaye ndiye ulisema watu wapumzike siku ya sabato, ndio uwe wa kufanya kinyume na agizo lako mwenyewe? (Maana Yesu ndiye Mungu aliyeagiza sheria ya sabato ifuatwe). Iweje hapa yeye ndiye awe wa kuivunja?
Hapa jibu ni moja tu. Sabato si siku katika juma! Kama sabato ingekuwa ni siku katika juma, Bwana Yesu angekuwa na hatia ya kuvunja sabato, maana ni wazi kuwa alitenda mambo ambayo ni kinyume na sabato kama siku!
Lakini kwa sababu sabato ina maana tofauti na siku, ndiyo maana aliruhusu mtu yule abebe godoro siku sabato; ndiyo maana hakuwa na tatizo na uponyaji siku ya sabato; ndiyo maana hakuwa na tatizo na wanafunzi kukwanyua masuke mashambani!
MAANA HALISI YA SABATO
Sabato ni kitu gani basi kama si siku katika juma?
Maandiko yanasema: Basi imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana yeye (yaani mwanadamu) aliyeingia katika raha yake (yaani raha ya Mungu) amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. (Waebrania 4:10).
Aha! Kumbe sabato si kupumzisha damu na nyama katika siku mojawapo ya wiki; si kujizuia kukoka moto, kubeba mzigo au kusafiri mwendo mrefu kimwili!
Sabato ni kitendo au hali ya mwanadamu kuacha ‘kazi zake’ kama Mungu alivyoacha zake. Mungu ni mtakatifu, kwa hiyo kazi zake ni takatifu na kamilifu. Mwanadamu ni mpungufu, kwa hiyo kazi zake ni uasi, yaani dhambi. Hizo ndizo anazotakiwa kupumzika kwazo, yaani kuziacha na kumgeukia Mungu.
Ili kuweza kuingia rahani mwa Bwana, yaani kwenye sabato yake, Bwana akasema: Njoni kwangu ninyi nyote wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha. (Matayo 11.28).
Pumziko au raha au sabato hiyo si kupumzisha damu na nyama katika siku fulani ya wiki, bali Bwana anasema: Nanyi mtapata raha (sabato) nafsini mwenu. (Matendo ya Mitume 11:29) – si kwenye miili yenu!
Na pale unapowezeshwa kuacha dhambi na ukamgeukia Bwana na kumfuata maishani mwako, ndipo raha au sabato hiyo inapokuwa ni kwa faida au kwa ajili yako, yaani sabato inakuwa ni kwa ajili ya mwanadamu. Lakini ukishikilia kutunza siku, hapo wewe ni kwa ajili ya siku (sabato) na wala si sabato kwa ajili yako.
Kwa hiyo, sabato si siku bali ni pumziko, raha na starehe ndani ya Kristo katika Roho Mtakatifu. Imeandikwa: Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu. (Warumi 14:17).
HITIMISHO
Tumalizie kwa kujiuliza swali hili. Je, kuabudu siku ya sabato au jumamosi ni vibaya?
Yapo mambo mawili ya kutofautisha hapa. Kuna kushika siku kama siku tu; na kushika siku kama sehemu ya utekelezaji wa sheria.
Ukishika siku kama siku tu, unaweza kumwabudu Mungu katika siku yoyote upendayo maana siku zote ni sawa tu.
Lakini ukishika siku kama sheria, hutaweza kuabudu katika siku yoyote, maana sheria ina siku yake maalumu.
Kuabudu katika siku ya sabato (jumamosi) kama siku tu haina tatizo hata kidogo. Lakini kuabudu katika siku hiyo kama sheria kunaweza kuwa na maswali.
Tumeshaona kwa ushahidi mwingi kwamba, sabato ilikuwa ni kivuli au mfano au taswira ya kitu kingine.
Jambo la msingi ni kuwa, sabato au pumziko halisi ni kuwa ndani ya Yesu, yaani kuokoka. Ukishaingia ndani ya Yesu, haijalishi tena endapo utamwabudu siku ya kwanza, ya pili au ya mwisho ya juma.
Biblia inasema: Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona kuwa siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu. (Warumi 14:5-6).
Tena imeandikwa: Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. (Wakorintho 2:16-17).
Vilevile imeandikwa: Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka. Nawachelea, isiwe labda nimejitaabisha bure kwa ajili yenu. (Wagalatia 4:9-11).
Je, umeokoka?
Kama jibu ni ndiyo na unapenda kumwabudu Bwana wa sabato (pumziko) siku ya jumamosi, basi songa mbele katika hilo, maana siku kama siku haikuongezei wala kukupunguzia chochote.
Je, hujaokoka?
Kama jibu ni ndiyo, nasikitika kusema kwamba kushika kwako siku hakutakusaidia, maana hapo hakuna tofauti na kung’ang’ania mfano au kibao na kuacha jambo lenyewe ambalo hasa ndilo lililolengwa na kibao au mfano huo.
Mtu akiwa mwizi, wizi wake hautoki kwa sababu ameabudu katika siku fulani ya juma. Na mtu mtakatifu, utakatifu wake hauji kutokana na kuabudu katika siku fulani. Utakatifu unatoka kwa Bwana wa sabato, Yesu Kristo mwenyewe.
Umeona mwenyewe hapo juu kwamba Mungu anaita ‘kushika siku’ kuwa ni ‘mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge!’
Achana na mambo ya kimwili maana wakati wake ulishapita! Bwana Yesu alisema wazi: Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. (Yohana. 4:23-24).
Si katika mwili!!
Mungu awabariki sana.
By permission: Yesu ni Njia, Injili Timilifu, James John, NKJV, Christ Nations and Max Shimba Ministries Org.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 4, 2016

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ

Neuroplasticity, Spiritual Formation, and Holistic Redemption in Christ By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute Introduction ...

TRENDING NOW