Tuesday, April 5, 2016

MCHAWI AJISALIMISHA KANISANI TAG MAGOMENI

Mchungaji Kanemba akiangalia vifaa vya kishirikina vya kijana huyo.
Haya ndio yaliyotokea Jumapili katika Kanisa la TAG Magomeni Mikumi kituoni jijini Dar es salaam. Katika mwendelezo wa ushuhudiaji wa shabaha ambapo kijana aliyekuwa akitumikishwa na shetani katika mambo ya kichawi kuamua kuokoka na kukabidhi sanduku lake lenye vifaa vya kichawi ili vichomwe moto.

Kijana huyu ambaye ni dereva wa bodaboda na ni mkazi wa Magomeni Mapipa aliamua kwa hiari yake kuokoka wakati wa ibada kuu ya jumapili kanisani hapo alipokwenda kuabudu ambapo baada ya ibada alikwenda kwa mazungumzo ofisini kwa Mchungaji Kanemba akiwa yeye na mama yake ambako aliomba alete vitu vyake vya kichawi ili vichomwe moto  jambo ambalo lilitekelezwa.

Tukio hilo lilipelekea kilio kikuu kwa mama yake mzazi maana hakuwa akijua kuwa mwanaye huyo alikuwa anajishughulisha na mambo ya kichawi, kijana alieleza matumizi ya vifaa hivyo vya kichawi; ikiwemo na mvuto ki-biashara, mvuto wa ki-mapenzi na hata kuwadhulu wabaya wake jambo ambalo liliwaacha watu waliokuwa wakishuhudia tukio hilo kwa mshangao na wengine wakimtukuza Mungu.

Mchungaji Kanemba alimwombea rehema za Mungu kijana huyo na kuongoza shughuli nzima ya kuteketeza uchawi kwa moto wa petroli na kisha kumshauri kijana jinsi ya kuishi maisha ya wokovu, ambapo kijana huyo na mama yake wamekuwa washarika wa kanisa hilo wakimtukuza Mungu kwa matendo makuu aliyowatendea.

Mchungaji Kanemba akizungumza na kijana huyo ofisini kwake.
Mchungaji Kanemba akatoka kujionea mambo yote.
Vifaa vya kichawi ndani ya sanduku.
Mchungaji Kanemba akiangalia daftari lenye maelezo mbalimbali ndani yake. 

Mchungaji Kanemba akionyesha yaliyokuwamo ndani ya sanduku hilo.

Kijana akimweleza mchungaji Kanemba jinsi alivyokuwa akitumia vifaa hivyo.
Mama wa kijana akilia baada ya kugundua aliyokuwa akifanya kijana wake.
Vitu vikiteketezwa.
Mchungaji Kanemba akimfanyia maombi kijana huyo. Picha na habari kwa hisani ya Martmalecela.blogspot.com.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2013/10/mchawi-ajisalimisha-kanisani-tag.html#sthash.k3eFL7IH.dpuf

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW