Saturday, June 18, 2016

SHETANI LA ULAFI KATIKA UISLAMU


Ndugu msomaji,
Leo ningependa tujifunze kidogo kuhusu roho ya ulafi ambayo inawasumbuwa ndugu ztu katika Adam. Hebu tusome Biblia kama ushahidi.
Wafilipi 3: 19 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.
Walafi wao wamesha amua kuabudu chakula na mungu wao ni matumbo yao. Mtu mlafi akiona chakula, basi yeye hula kwa haraka haraka na kujaza tumbo lake mpaka anavimbiwa. Ulafi ni dhambi kama ilivyo sema kwevye Wafilipi hapo juu. Ulafi ni kuabudu tumbo.
Mithali 23: 20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Watu wanao kula nyama kwa Pupa mpaka wanavimbiwa na kushindwa kutembea, hao wana roho chafu ya ulafi, na ni dhambi kuabudu chakula au kuwa mtumwa wa chakula au mtumwa wa tumbo lako.
Kuna dini fulani wao wanapo dai kuwa wanafunga siku thelasini, huwa wanabadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha mpaka wanavimbiwa matumbo yao. Hiyo dini ni dini ya walafi na wanatenda dhambi, huku wao wakifikiria kuwa wanafunga kwa Allah wao.
Wagalatia 5: 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Kama Neno la Mungu linavyo sema kuwa, tusiwe na tamaa za mwili, maana mwili wetu ni hekalu la Mungu. Ikimaanisha kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya mwili wetu, na hivyo, ni vyema tuutunze. Ulafu ni roho kutoka kwa Shetani na kula mpaka kuvimbiwa ni dhambi na ni kuabudu chakula na matumbo yetu.
1 Wakorintho 6: 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Basi mpendwa, usiongozwe na tamaa za mwili bali ongozwa na Roho aliye ndani yako.
Leo tumejikumbusha kuwa, Ulafi ni roho kutoka kwa Shetani na ni dhambi.
1. Kwanini Waislam wanakula usku kucha wakati wa mfungo wa Ramadhani?
2. Kwanini Allah amewaruhusu kula usiku kucha na kuwakalisha na njaa mchana kucha, je huko si kubadilisha masaa ya kula?
3. Mbona Yesu wa Biblia alipo funga, yeye hakula Daku?
Hakika kubadilisha masaa ya kula na kula usiku kucha ni ulafi, na ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu.
Max Shimba Ministries

WAISLAM WAMELAZIMISHWA KUFUNGA SWAUMU

Quran 2:183 Enyi mlioamini mmelazimishwa kufunga saumu kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha mungu.
Aya hapo juu inatuambia kuwa, kumbe kufunga kwa ndugu zetu hawa ni kwa kulazimishwa na sio hiyari yao.
1. Wapi tunasoma katika Taurat kuwa Adam alifunga Ramadhani?
2. Wapi tunasoma katika Taurat kuwa Musa alifunga Ramadani?
3. Wapi tunasoma katika Taurat kuwa Ibrahim alifunga Ramadhani?
Ndugu zanguni, hii dini ni ya kujitungia na si kama wanavyo dai kuwa eti iliteremshwa na Allah. Kama kweli Allah ndie aliye iteremsha hii dini kwa Adam, sasa kwanini Adam hakufunga Ramadhani/Swaumu?
Zaidi ya hapo, kwanini katika mfungo hawa ndugu zetu wanakula Usiku kucha/daku? Wapi katika Taurat panasema kuwa watu wale Daku?
Waislam huwa wanatumia aya ambayo inasema kuwa Yesu alifunga, lakini hawasemi kuwa Yesu alifunga kwa siku ngapi na wala hakuna aya ambazo zinasema kuwa Yesu alikula Daku saa nane/kumi za usiku.
Zaidi ya hapo, hatusomi kuwa Yesu alianza kufunga pale alipo uona Mwezi umeandama, la hasha. Wala hatusomi kuwa Yesu alifungulia/maliza kufunga pale Mwezi ulipo andama, la hasha.
Hii tabia ya kuabudu Mwezi ipo kwenye Uislam peke yake.
Maswali kuhusu Mwezi:
1. Hivi kati ya Allah na Mwezi ni nani mwenye Mamlaka ya kuongoza Waislamu?
2. Hivi kwanini Waislam wafuate maamrisho ya Mwezi?
KUMBE MWEZI NDIYE MOLA MLEZI ANAYEABUDIWA NA WAISLAMU!
Q6:77 SURAT AL - AN-A'AM
Alipo uona mwezi unachomoza alisema: Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Ulipotua asema:Kama Mola Mlezi wangu hakuniongoa, nitakuwa katika kaumu walio potea.
HII NDIYO SIRI YA ILE NYOTA NA MWEZI ILIYO JUU YA KILA MSIKITI!
KULA DAKU ASUBUHI:
Kula Daku saa alfajiri ni jibu tosha kuwa, Waislam wamebalisha masaa ya kula na kuamua kula usiku kucha na kukaa na njaa mchana kutwa.
Kumbe basi, hata Wakristo wanao lala usiku na kula asubuhi wao vile vile wanafuga.
Kumbe basi, ndio maana Wazungu wanaita chakula cha asubuhi "BREAKFAST"
Waislam kwanini kula usiku mnaita kufunga?
Wapi Yesu kasema kwenye Injir kuwa watu wafunge Ramadani?
Hakika Ukristo ndio Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Max Shimba
Max Shimba Ministries Org @2015.

MUHAMMAD ALIKUWA ANAPIGA WAKE ZAKE

Ndugu msomaji,
Muhammad alikuwa na tabia ya kuwapiga wake zake, hususan Aisha na Hafsa.
Nabii wa Alah Muhammad alipiga Aisha kifuani na kumsababishia maumivu makali. Sahih Muslim #2127:
SOMA KISA HIKI HAPA CHINI.
Sahih Muslim #2127:
Ilipokuwa zamu yangu kwa Nabii wa Allah kuwa nami usiku, aliingia na kugeuka, akavua joho lake na viatu vyake, na kuviweka karibu na miguu yake, na akajilaza kwenye kitanda mpaka alipo fikiria kuwa na mimi nimelala.
Basi akachukua joho lake taratiibu na kuvaa viatu vyake, na akafungua mlango na kutoka nje na kuufunga taratibu. Aisha akasema, na mimi nikajifunika kichwa changu, na kuvaa hijabu yangu na kujifunga nguo kiunoni mwangu, na baadae nikatoka nje na kumfuta Nabii wa Allah mpaka alipo fika Baqi.
Alisimama pale kwa muda mrefu. Na baadae akanyanyu mikono yake mara tatu, na baadae kurudi, na mimi vile vile nikarudi nyumbani. Alikuwa anatembea kwa haraka haraka, na mimi vile vile nilitembea kwa haraka haraka. Alikimbia, na mimi nikakimbia vile vile. Akaja nyumbani na mimi vile vile nilikwenda nyumbani, ingawa mimi nilkwenda kwa haraka kabla yake. Nilipo ingia tu na kujilaza kitandani, na Nabii wa Allah akaingia nyumbani, akasema: Hii ni nini, O' Aisha, mbona unahema sana? Nikamwambia, hakuna kitu. Akasema, Niambie au una mambo ya siri hautaki kuniambia.
Nikamwabia, Nabii wa Allah, baba na mama yangu wawe fidia kwako, halafu nikamwambia kila kitu bila kumficha kitu. Muhammad akasema, kumbe nilicho kuwa nakiona kwenye giza mbele yangu ilikuwa ni wewe? Nikamjibu, NDIO. Basi Nabii wa Allah, AKANIPIGA KWA NGUVU SANA KWENYE KIFUA CHANGU, na nilipatwa na maumivu makali sana. HALAFU AKASEMA, unafikiri Allah na Nabii wake wamekuonea?
Bukhari volume 8, #828
Amesema Aisha: Abu Bakr alikuja kwangu na akanipiga ngumi kwa nguvu sana na kusema, umewaweka watu kizuizini kwasababu ya mkufu wako. Lakini nilikuwa nimekaa kimya kama vile nimekufa, .......
Jamani, eti huyu ndie Nabii wa Allah. Hana jema zaidi ya kupiga wake zake, kisa, mke mtu kamfuata Baqi. Je, kama Muhmmad alicho kuwa anafanya ni jambo jema, kwanini aliondoka nyumbani kwake kimya kimya?
Kama kweli Muhammad hakwenda kufanya NDUMBA, kwanini alichukia pale alipo ambiwa kuwa Aisha na yeye alikuwa Baqi?
Hivi, kwanini MUHAMMAD ALIKUWA ANAPIGA WAKE ZAKE?
Hakika huyu hakuwa Nabii wa Mungu bali Allah mpinga Mungu.
Leo tumejifunza tena kuwa, kumbe katika Uislam, wanaruhusikwa kuwapiga wake zao. Huu ni MSIBA.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org

KWANINI KWENYE QURAN HAKUNA JINA LA LUSIFA?

ALLAH AMBAYE SIO YEHOVA YAHUH ( يهوه ) HALIJUI JINA LA SHETANI
NDIO MAANA NAENDELEA KUSEMA KUWA ALLAH SIO MWENYEZI MUNGU.
Swali la kwanza la kujiuliza: KWANINI KWENYE QURAN HAKUNA JINA LA LUSIFA?
Ndugu msomaji,
Tunapofikiria juu ya shetani, Je tunakuwa tunafikiria juu ya kitu gani au shetani ni nini? Au ni nani? Je alikuja kutokea wapi? Madhumuni na makusudi yake ni nini? Je, Anatuathiri kwa namna gani? Na ni kwa nini shetani yupo? Je Ana mahusiano gani na Mungu?
NINI MAANA YA SHETANI NA AU SHETANI NI NANI?
Tangu mwanzo Shetani hakuwa anaitwa Shetani, yaani hapakuapo na kiumbe kilichoumbwa na kuitwa Shetani kama ambavyo Quran inadai katika Surat Al Araaf aya ya 11-12.
Lusifa ambalo ndilo jina la Shetani alikuwa ni “mwana wa asubuhi” (Isaya 14:12) yeye pamoja na jeshi lingine la mbinguni,waliumbwa wote wakiwa wakamilifu katika njia zao zote ( Ezekieli. 28:14-19). Kulikuwa na amani na umoja Mbinguni. Kisha mambo yakaharibika. Biblia haiko wazi sana juu ya swala hili ni nini hasa kulitokea na kwa namna gani, ila uovu au kutokumtii Mungu kulioneka kwa Lusifa. Mwishowe alifukuzwa kutoka Mbingini, pamoja na jeshi lake lote lililoasi, wakafukuziwa mbali kabisa kutoka mbinguni na kutupwa, na wanazunguka zunguka katika nchi (duniani).
LAKINI ALLAH ANASEMA HIVI:
Katika Quran Allah anasema alimuumba Shetani kama Shetani tena akiwa na maouvu yake yote:
Surat Al Araaf 11. Na hakika tulikuumbeni, kisha tukakutieni sura, kisha tukawaambia Malaika: Msujudieni Adam. Basi wakasujudu isipo kuwa Iblisi, hakuwa miongoni mwa walio sujudu. 12. Mwenyezi Mungu akasema: Nini kilicho kuzuia kumsujudia nilipo kuamrisha? Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, naye umemuumba kwa udongo.
1. Kwanini kwenye Quran hakuna jina la Lusifa?
2. Kwanini Allah aliogopa kuweka jina la Lusifa kwenye Quran?
Allah anadai kuwa eti alimuumba Shetani kama alivyo dai kwenye Surat Al Araaf 11-12 huku YEHOVA anasema kuwa HAKUMUUMBA SHETANI KAMA SHETANI bali alikuwa LUSIFA "Malaika wa Mungu" Kabla ya kuasi.
SHETANI SIO JINA BALI NI WASIFA/MATOKEO WA KAZI/KITENDO ALICHO FANYA. NDIO MAANA NASEMA ALLAH HALIJUI JINA LA SHETANI MAANA KWENYE QURAN HAKUNA JINA LA LUSIFA.
Allah ambaye anaajiita mjuzi wa kila kitu, kwanini ameshindwa kutuambia jina halisi la huyu ADUI MKUBWA WA BINADAMU aitwaye Lusifa?
Waislam wao wanafikiria kuwa eti Neno Shetani ni jina, la hasha. Shetani sio jina bali ni kama wasifa wa kazi anayo itenda Lusifa.
DARASA FUPI KWA WAISLAM:
Mfano: Neno Polisi sio jina bali ni wasifa wa jina/kazi ya mtu fulani ambaye analo jina lake. Vivyo hivyo NENO Mwalimu sio jina bali ni wasifa wa jina/kazi anayo ifanya mtu fulani, wakati huo huyo neno JAMBAZI sio jina la mtu bali ni wasifa wa jina/kazi anayo ifanya mtu fulani anayeweza itwa Abdallah au Juma au Muhammad. Ndio maana inashangaza tunaposoma katika Quran kuwa eti, SHETANI ni jina huku ikifahamika kuwa SHETANI sio jina bali ni matokeo/kazi/tabia/wasifa wa Lusifa alio upata baada ya kuasi mbinguni.
Quran hiyo hiyo inawaitwa watu wanao fanya mambo mabaya ni MASHETWAIN huku ikifahamika kuwa hao watu wana majina yao halisi kama Abdulah au Saidi. Hivyo basi, hata Ibilisi naye analo jina lake ingawa Allah anaogopa kulitaja kwenye Quran.
NINI KILITOKEA MPAKA KUKAWA NA SHETANI?
Inaonekana Lusifa hakufahamu Mpango wa Mungu, na alifikiri ya kwamba yeye Lusifa angeweza kufanya vizuri zaidi kuliko Mungu. Hii ndiyo ilikuwa dhambi kuu ya Shetani. Kwa kufikiri hivi hakumwabudu wala kumsujudia Mungu, lakini anamwona Mungu kama sawa na yeye (Filipo. 2:6)
Isaya 14:14. Nitapaa kupita vimo vya mawingu. Nitafanana na yeye Aliye Juu.
Isaya. 14:12 Jinsi ulivyoanguka kutoka Mbinguni. Ewe nyota ya alifajiri, mwana wa asubuhi ! Jinsi ulivyokatwa kabisa. Ewe uliyewaangusha mataifa !(KJV imetumika wakati wote)
Kazi zote za Yehova ni kamilifu; yeye siye mwanzilishi wa ukosefu wa uadilifu; kwa hiyo hakumuumba yeyote akiwa mwovu akama Waislam na Quran yao inavyo dai. (Kum. 32:4; Zaburi 5:4) Yule aliyekuja kuwa Shetani hapo mwanzoni alikuwa mwana mkamilifu wa kiroho wa Mungu. Aliposema kwamba Ibilisi “hakusimama imara katika kweli,” Yesu alionyesha kwamba wakati mmoja huyo alikuwa “katika kweli.” (Yohana 8:44)
Lakini, kama walivyo viumbe wote wa Mungu wenye akili, mwana huyo wa kiroho alipewa uhuru wa kuchagua. Alitumia vibaya uhuru wake wa kuchagua, akaruhusu maoni ya kujitafutia umashuhuri yasitawi moyoni mwake, akaanza kutamani ibada iliyokuwa ya Mungu peke yake, na kwa hiyo akamshawishi Adamu na Hawa wamsikilize yeye kuliko kumtii Mungu. Basi kupitia matendo yake, yeye mwenyewe akajifanya Shetani, jina linalomaanisha “mpinzani.”—Yakobo 1:14, 15;
Swali la kujiuliza:
1. Kwanini hakuna jina la Lusifa kwenye Quran?
2. Kwanini Allah analiogopa jina la Lusifa?
3. Kwanini Quran inafundisho tofauti na Taurat, Zaburi na Injili kuhusu mwanzo wa Shetani?
Kama Mwenyezi Mungu analo jina "Yehova". Vivyo hivyo Malaika wanayo majina mfano "Mikaeli" au "Gabrieli". Hata alipo umbwa Binadamu alipewa jina, "Adam na Hawa", kwanini Allah anashindwa kutuambia jina la shetani?
Hayo maswali ni kwa ajili ya kukufumbua macho kuwa Allah sio Yehova "YAHUH" Hivyo basi Allah sio Mwenyezi Mungu aliye muumba Lusifa kama Malaika mkamilifu.
Ni mimi Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo

VIOJA NA VIROJA KATIKA QURAN

Leo nawaletea burdan kutoka kwa Allah.
1. Eti "Sperms" zinatoka katika kifua cha Mwanaume " Soma (Quran 86:5-7).
2. Mfalme Sulemani alikuwa anazungumza na Ndege Soma (Quran 27:16).
3. Sulemani alikuwa anazungumza na Chunguchungu. Soma (Quran 27:18)
4. Allah kaumba Dunia kama Zulia "Carpet" The Qurân 20:53. (Qurân 13:3; 15:19; 18:7; 19:6; 21:30; 35:40; 41:10; 43:10; 50:7; 51:48; 55:10; 78:6; 79:30; 88:20)
5. Eti USIKU UNAOGELEA KATIKA anga. The Qurân talks of the earth in terms as if it were stationary, with the sun and stars moving around the earth (Qurân 2:258; 21:33; 36:40; 52:49; 53:1). "It is he who created the night and the day, and the sun and the moon: all (celestial bodies) swim along, each in it's rounded course" (21:33). We know today that the sun is far bigger than the earth, and is drawing the round earth in it's orbit.
Huyu ndie Allah wa ajabu ajabu. Anapenda sana kulazimisha vitu. Sasa anadai kuwa Solomoni alikuwa anaongea na Ndege, Chunguchungu. Huku Zaburi na Taurat vinakataa huo usanii wa Allah wa kwenye Quran.
ALLAH anadai eti "Sperm" zinatoka kwenye kifua, huku sayansi inapinga huo usanii wa Allah.
Allah anadai kuwa eti USIKI unaogelea katika Anga. Hivi huyu Allah ni kweli aliumba au ni msanii tu?
Sasa Allah anadai eti, Dunia ni kama Zulia "Carpet" huku ikifahamika kuwa dunia haipo kama Zulia. Ndio maana naendelea kusema kuwa Allah sio Mwenyezi Mungu. Allah sio Yehova. Allah sio Yehuh.

MAANA YA KUFUNGA KATIKA UKRISTO

Katika somo letu la "Maana ya kufunga katika Ukristo" tutajifunza maana ya neno "Kufunga na "Swaumu".
Nini maana ya KUFUNGA?
Neno “Kufunga“ linatokana na neno la Kiyunani “Nestevo“, ambalo ni muunganiko "consolidation" or "integral" wa maneno mawili ya Kiyunani “NE“ na “Esthio“. Neno “NE“ ikiwa na maana ya “bila“ au “hapana“, Kiingereza “no“ au “without“.
Neno “ESTHIO“ ikimaanisha “kula chakula au kunywa kinywaji“, Kiingereza “to eat solid food or drink liquid“. Neno “NESTEVO” sasa linaunga maneno hayo mawili ya Kiyunani ”NE” na “ESTHIO”, na lina maana “bila kula chakula au kinywaji chochote kile”. Hivyo maana ya kufunga, ni “bila ya kula chakuna na kinywaji chechote”.
Nini maana ya "SWAUMU"?
Neno Saumu katika lugha ya kiarabu maana yake ni 'Kujizuwia'. Yote sawa ikiwa kujizuwia na kula au kujizuwia na kusema, nk.
Bibi Maryam baada ya kumzaa Nabii Issa (Alayhas Salaam), alisema;
"Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema ya kufunga, kwa hivyo leo sitasema na mtu".
Maryam - 26
Kwa hivyo hapa Bibi Maryam (Alayhas Salaam) ametumia neno 'Sauma' pale aliposema ((Inniy nadhartu lilrahmani 'Sauma')), si kwa maana ya kujizuwia na kula, bali kwa maana ya kujizuwia na kusema.
Anasema Abu Ubaidah (Radhiya Llahu anhu);
"Neno 'Saumu' katika lugha ya kiarabu, maana yake ni 'Kujizuwia na kula au kujizuwia na kusema au na kwenda".
SASA TUNAGALIE, BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU KUFUNGA:
Nyakati za Biblia, watu walifunga kwa sababu mbalimbali zilizokubaliwa na Mungu. Baadhi yao walifunga kwa sababu ya huzuni au toba (1 Samweli 7:4-6), wengine walifunga ili kuomba mwongozo wa Mungu au ili wapate kukubaliwa naye (Waamuzi 20:26-28; Luka 2:36, 37), au ili kukaza fikira walipotafakari.—Mathayo 4:1, 2.
Bibilia inawazilisha kufunga kama kitu ambacho ni kizuri, cha muimu na cha manufaa. Kitabu cha Matendo Ya Mitume kimerekodi kuwa Wakristo walifunga kabla ya kufanya uamuzi wa maana (Matendo Ya Mitume 13:2, 14:23). Kufunga na maombi kila mara zimeambatanishwa pamoja (Luka 2:37; 5:33). Kila mara, angazo la kufunga ni kutokuwa na chakula. Badala ya lengo kuwa, kufunga ni kuyapeleka mawazo yako nche ya vitu vya dunia na kiukamilifu kumtazamia Mungu. Kufunga ni njia mojawapo ya kudhihirishia Mungu na sisi wenyewe kwamba hatutaki mchezo katika uhusiano wetu na yeye. Kufunga kunatuzaidia kupata mtazamo na kufanya upya tegemeo letu kwa Mungu.
Katika matukio kadhaa katika Agano la Kale, kufunga kunahusishwa na maombi ya kuombea. Daudi aliomba na kufunga juu ya mtoto wake mgonjwa (2 Samweli 12:16), akilia kwa bidii mbele za Bwana katika maombezi (vv. 21-22). Esta alimsihi Mordekai na Wayahudi kufunga kwa ajili yake alipokuwa akipanga mbele ya mumewe mfalme (Esta 4:16). Ni wazi, kufunga na kuomba sina uhusiano wa karibu.
Kwa kuchukua macho mbali na vitu vya dunia, tunaweza zaidi kuyaweka mawazo yetu kwa Kristo. Kufunga sio njia ya kumfanya Mungu atende vile tunavyotaka. Kufunga kunatubadilisha, sio kumbadilisha Mungu. Kufunga sio njia ya kuonekana mwokovu sana kuliko wengine. Kufunga kunastahili kufanyika kwa moyo wa unyenyekevu na nia ya furaha.
Mathayo 6:16-18 yasema, “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamna; maana hujiimbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso; ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
1. Katika Ukristo hakuna kula daku wakati wa kufunga.
2. Yesu hakula daku wala futari wakati alipo funga kwa siku Arobaini.
3. Yesu hakujioneysha kwa wanafunzi wake kuwa alikuwa anafunga bali ilikuwa ni siri yake.
4. Hakuna Sheria ya kufunga katika Injili.
5. Hakusomi katika Taurat au Zaburi au Injili kuwa wakati wa Biblia watu wali kula daku na hakuna aya inayo ruhusu kula daku.
FAIDA YA KUFUNGA:
Katika Biblia, tunaona jinsi ambavyo mambo yalivyobadilika baada ya kufunga na kuomba. Angalia mifano michache hapa chini:-
A. Wana wa Israeli walipigwa mfululizo katika vita na wana wa Benyamini. Baada ya kushindwa mfululizo, wakaamua kufunga na kuomba (WAAMUZI 20:20-22, 24-26). Baada ya kufunga na kuomba matokeo yakabadilika, Benyamini wakapigwa sana, na wana wa Israeli wakashinda vita (WAAMUZI 20:34-35, 41-45, 48). Tunaweza kuitia moto miji yote ya Shetani tukiwa wafungaji, na siyo kinyume cha hapo;
B. Ezra hakumtegemea mfalme, bali alifunga, na matokeo ya kufunga yakawa kwamba mkono wa Mungu ulikuwa pamoja naye na yeye na wenzake wakaokolewa na mkono wa adui (EZRA 8:21-28, 31-33). Ikiwa Kanisa linahitaji kuokolewa kutoka katika mkono wa adui, ni lazima liwe na wafungaji.
Mpendwa msomaji, unaona faida ya kufunga? Usifunge kama wale wanao jionyesha kwa kukunja nyuso zao na kusema Swaumu kali bali funga kwa siri maana anaye fahamu kuwa unafunga ni Mungu na yeye anajua ya moyoni mwako.
Mungu akubariki sana,
Ni mimi Max Shimba, Mtumwa wa Yesu Kristo

NDANI YA QURAN HAKUNA AYA INAYOSEMA KUWA BIBLIA SIO MANENO YA MUNGU


Allah anateremsha aya na kukiri kuwa Injil ya Yesu ni Nuru na inasadikisha Taurat.
Surat Al Maida 46. Na tukawafuatishia hao Isa bin Maryamu kuyahakikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyomo ndani yake uwongofu, na NURU NA INAYO SADIKISHA yaliyo kuwa kabla yake katika Taurati, na uwongofu na mawaidha kwa wachamungu.47. Na wahukumu Watu wa Injili kwa yale aliyo teremsha Mwenyezi Mungu ndani yake. Na wasio hukumu kwa yale aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio wapotofu. Maelezo
Katika aya hapo juu, tunajifunza kuwa Injili ni NURU, na Biblia inasema kuwa YESU NI NURU YA ULIMWENGU. Allah anakiri kwa mdomo wake kuwa Injili ni Nuru na HAKUWAI SEMA KUWA Quran ni Nuru. ALLAH AMESHA ANZA KUKIRI KUWA BIBLIA NI NURU na haina shaka ndani yake.
KAMA KUNA MUISLAM ANABISHA, ANILETEE AYA KUTOKA QURAN INAYOSEMA KUWA BIBLIA SIO MANENO YA MUNGU.
Endelea kusoma
ALLAH ANATHIBITISHA KUWA BIBLIA HAINA SHAKA NA NI NENO LA MUNGU.
Surat Al Maida 48. Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia. Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni nyote umma mmoja, lakini ni kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja kuwaambieni yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.
ALLAH katika Surat Al Maida aya ya 48 anaendelea kukiri kuwa KITABU-BIBLIA ni maneno ya Mungu na haina shaka ndani yake.
ALLAH ANAMWAMBIA MUHAMMAD katika Surat Yunus 94 KUWA, KAMA ANA SHAKA NAYE KUWA BIBLIA SIO MANENO YA MUNGU, BASI AWAULIZE WAKRISTO AMBAO WANASOMA "KITABU-BIBLIA".
HAPA ALLAH ANAHAKIKISHA NA KUTHIBITISHA KWA MUHAMMAD KUWA BIBLIA NI MANENO YA MUNGU.
Surat Yunus 94. Na ikiwa unayo shaka katika tuliyo kuteremshia, basi waulize wasomao Kitabu kabla yako. Kwa yakini imekwisha kujia Haki kutoka kwa Mola wako Mlezi. Basi usiwe miongoni mwa wenye shaka
Ndugu msomaji, unaona jinsi Allah anavyo KIRI KUWA BIBLIA NI MANENO YA MUNGU? Sasa kwanini Waislam wanabishana na Allah wao na Mtume wake kipenzi Muhammad kuwa Biblia sio maneo ya Mungu?
KAMA KUNA MUISLAM ANABISHA, ANILETEE AYA KUTOKA QURAN INAYOSEMA KUWA BIBLIA SIO MANENO YA MUNGU.

MUHAMMAD SIO MTUME KWASABABU HAKUWAI ONGEA NA MUNGU

Leo ningependa tujikumbushe mambo machache ambayo labda hatukuyatilia maanani. Mitume wote na manabii wote wa Biblia waliwai ongea na Mungu. Lakini, Mtume wa Allah ambaye sio Yehoah "Muhammad" hakuwai ongea na Mungu HATA MARA MOJA. Je, utume wake tutauamini vipi maana hakuwai ongea na aliye mtuma?
Lakini Mitume wote wa Biblia waliongea na Mungu.
1. Musa anoangea na Mungu: Kutoka 3:1-21
2. Elia anaongea na Mungu: 1 Wafalme 19- Soma yote
3. Yeremia anaongea na Mungu (Yeremia 1:5)
4. Yona anaongea na Mungu (Yona 3:2)
5. MTUME Paulo anaongea na Mungu: Matendo ya Mitume 18:9Wagalatia 1:1 Paulo, mtume, si mtume wa wanadamu aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu
Biblia ipo wazi kabisaa, kuwa Paulo alitumwa na Mungu, wakati Muhammad alitumwa na Jibril ambaye si Mungu. Koran inakiri kuwa Muhammad alikutana na Jibril na hakuwai kukutana na au ongea na Mungu hata mara moja. Lakini tunasoma katika Biblia kuwa, Paulo alipewa utume na Mungu mwenyewee.
Warumi 1:1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, ALIYEITWA KUWA MTUME na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu.
Hiyo ni mifano michache kutoka Biblia.
Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini hakuongea na Mungu aliye Mtuma? Maana ya neno Mtume kwa kifupi: Ni Mtu aliye tumwa.
HEBU TUANGALIE, HUYU MUHAMMAD ALIZALIWAJE?
1.KUZALIWA KWAKE,
Abu Huraira (r.a) amesimulia kuwa "Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa na shetani tangu alipozaliwa, (Fat'hul Baary Juzuu ya 6 Uk. 389).
Je, kuna ushahid wowote ule kuwa Muhammad alitolewa Shetani? Kama upo Basi Waislam, tuleteeni tuuone.
2.BAADA YA KUTOKA PANGONI,
Basi Mtume akafanya khofu, akarejea kwa mkewe, akamhadithia, na pale pale homa kubwa kabisa, ikampanda, akataka afunikwe maguo, akawa anatetemeka kwa ngerema, na kuweweseka, na kusema, "Najikhofia nafsi yangu, kuchezewa na mashetani, na kuniharibu akili yangu na kunizuga"(Kitabu cha maisha ya Nabii Muhamaad s.a,uk.17 kilichoandikwa na Sheiky A.Farsy).
KUFUATANA KITABU CHA MAISHA YA NABII MUHAMMAD, tunajifunza kuwa Muhammad kwa mara ya kwanza kabisa alipata utume wake pangoni baada ya NAFSI YAKE KUCHEZEWA NA MASHETANI.
MASWALI:
(i). Kama Jibril ndie alitumwa na Allah, na huyo Allah ni Mungu, kwanini Muhammad alisema kuwa nafsi yake imechezewa na MASHETANI baada ya kukutana na Jibril?
(ii). Kama Jibril alitoka kwa Allah, kwanini Muhammad alipo toka pangoni alisema kuwa Jibril AMEMZUGA AKILI YAKE?
3.KUROGWA KWAKE,
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo na kupiga makelele. (Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
MASWALI:
(a) Hivi, kuna Mtume au Nabii yeyote yule ambaye alikiri kurogwa?
(b) Hivi Allah alikuwa wapi wakati Muhammad anarogwa?
(c) Wapi tunasoma kuwa Muhammad aliombewa na kutoa huo uchawi/urogi aliofanyiwa na Labiid bin Al'answan?
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MTU ALIYECHEWA NA MASHETANI KAMA HUYU?
Ndugu msomaji,
Muhammad hakuwa Mtume wa Mungu na wala hana sifa za KITUME.
1. Muhammad hakuwai ongea na Allah aliye mtuma.
2. Muhammad alikuwa na Shetani tokea kuzaliwa kwake.
3. Muhammad alikiri kuchezewa na Shetani wakati wa kusimikwa utume wake Pangoni.
4. Muhammad alikiri kuwa Shetani amechezea akili na nafsi yake.
5. Muhammad alikiri kuwa alirogwa na Labiid bin Al'answan.
SASA WAISLAM, NIONYESHENI, wapi kwenye Taurat, au Zaburi au Injili kama kuna Mtume aliye na sifa za ajabu kama za Muhammad.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Max Shimba Ministries Org.

KWANINI ALLAH ANAAPA KWA YEHOVA "YAHUH" ALIYE UMBA KILA KITU?


1. Kumbe Allah sio Yahuh-Yehova.
2. Kumbe Allah hakuumba.
3. Kumbe Yesu ni Mungu.
Ndugu msomaji,
Kwanza tujifunze maana ya kuapa ili tuweze elewa kwanini Allah aliapa kwa Yehova.
Nini maana ya kuapa?
Kuapa, au Kula kiapo, au Kula Yamini, kunamaanisha kumthibitishia, kwa kutumia Jina la Mwenyezi Mungu, kwamba jambo fulani linaloapiwa – na ambalo halina ushahidi wazi wazi- ni kweli na sahihi kama linavyodaiwa na mwenye kula kiapo hicho na hivyo basi ni budi kusadikiwa madai hayo kwani Mdhamini Mkuu ni Mwenyezi Mungu, Mjuzi Pekee wa ukweli au uwongo wa mambo yaliyofichika nyoyoni!
katika Hadithi iliyopokelewe na Abdallah bin `Umar R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “
"إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أو فَلْيَصْمُتْ"
Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kuapa kwa baba zenu, atakaeapa aape kwa Mwenyezi Mungu au anyamaze
Sasa tumsome Allah ambaye sio Yehova "Yahuh", je yeye anaapa kwa nani?
SURAT ASH-SHAMS 1-3
1. Naapa kwa usiku ufunikapo, 2 kwa mchana uingiapo, 3. na kwa aliye umba kiume na kike..
Hivi mtu anaye apa kwa mwengine anakuwa Mungu au binadamu? Je, nani kaumba hapo. Maana Allah anaapa katika aliye umba, na kuumba ni sifa ya Mungu. Kumbe Allah ambaye sie Yehova hakuumba.
Zaidi ya hapo, Allah anaapa kwa usiku. Kumbe usiku una mamlaka zaidi ya Allah. Allah anaapa kwa mchana, kumbe mchana una mamlaka zaidi ya Allah.
Mbona katika SURAT ASH-SHAMS Allah anaapa kwa (1) Usiku (2) Mchana (3) kwa aliye umba kiume na kike?
Je, ni nani huyu aliye umba Kiume na Kike ambaye Allah wa Islam anaapa kwake? Endelea kusoma...kutoka Biblia Takatifu….
Yeremia 27: 5 Mimi nimeiumba dunia hii, wanadamu na wanyama walio juu ya uso wa nchi, kwa uweza wangu mkuu, na kwa mkono wangu ulionyoshwa; nami nawapa watu kama inipendezavyo.
Sasa tunamsoma Yehovah ambaye ni Mungu wa Biblia kuwa yeye ndie aliye umba kila kitu, pamoja na Kiume na Kike ambacho Allah wa Islam anaapa kwake. Kwahiyo, Jehovah aliumba kiume na kike, na Allah wa Islam anaapa kwake, sasa jaza mwenyewe nani ni Mungu?
Je, Mungu anaweza kuapa kwa Mwengine? Endelea kupata elimu …
Waebrania 6:13 Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa.
Jehova anasema hakuna Mkubwa wangu wa kuapa kwake, lakini Allah katika Kuran anasema kuwa yeye anaapa kwa aliye umba kiume na kike.
Hivyo basi leo tunafahamu kuwa aliye umba ni Jehona na Allah anaapa kwa Jehovah Mungu wa Biblia na Wakristo.
Mungu awabairiki sana
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa yesu Kristo
Copyright © Max Shimba Ministries 2016

MUHAMMAD ANAAPA KWA YESU NA KUKIRI KUWA YESU ATAHUKUMU KWA UADILIFU

Soma Sahih hadith kutoka Al Bukhar:
Muhammad aseme haya katika (Bukhari hadithi na 425, juzuu 3) hadithi ya Abu Huraira amesema mtume wa Allah s.a.w):
Amesema Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko ipo mkononi mwake karibu atateremka kati yenu Mwana wa Mariam atahukumu kwa uadilifu.
Kama Muhammad anaapa kwa Yesu na kukiri kuwa Yesu ndio atakaye hukumu, kwanini nimfuate Allah ambaye sio Yehova?
Kwanini Muhammad hakua-apa kwa Allah?
SASA KAMA KUAPA LAZIMA KUWE KWA MWENYEZI MUNGU, KWANINI MUHAMMAD ALIAPA KWA YESU?
KUMBE YESU NI MWENYEZI MUNGU.
katika Hadithi iliyopokelewe na Abdallah bin `Umar R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “
"إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أو فَلْيَصْمُتْ"
Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kuapa kwa baba zenu, atakaeapa aape kwa Mwenyezi Mungu au anyamaze
SASA MSOME NABII MUHAMAMD ANAPAAPA KWA YESU:
(Bukhari hadithi na 425, juzuu 3) hadithi ya Abu Huraira amesema mtume wa Allah s.a.w):
Amesema naapa kwa ambaye nafsi yangu iko ipo mkononi mwake karibu atateremka kati yenu Mwana wa Mariam atahukumu kwa uadilifu.
KUMBE MUHAMMAD ANAJUA KUWA YESU NI MWENYEZI MUNGU.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW