Saturday, July 2, 2016

KWANINI ALLAH ANAAPA KWA YEHOVA "YAHUH" ALIYE UMBA KILA KITU?


1. Kumbe Allah sio Yahuh-Yehova.
2. Kumbe Allah hakuumba.
3. Kumbe Yesu ni Mungu.
Ndugu msomaji,
Kwanza tujifunze maana ya kuapa ili tuweze elewa kwanini Allah aliapa kwa Yehova.
Nini maana ya kuapa?
Kuapa, au Kula kiapo, au Kula Yamini, kunamaanisha kumthibitishia, kwa kutumia Jina la Mwenyezi Mungu, kwamba jambo fulani linaloapiwa – na ambalo halina ushahidi wazi wazi- ni kweli na sahihi kama linavyodaiwa na mwenye kula kiapo hicho na hivyo basi ni budi kusadikiwa madai hayo kwani Mdhamini Mkuu ni Mwenyezi Mungu, Mjuzi Pekee wa ukweli au uwongo wa mambo yaliyofichika nyoyoni!
katika Hadithi iliyopokelewe na Abdallah bin `Umar R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “
"إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أو فَلْيَصْمُتْ"
Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kuapa kwa baba zenu, atakaeapa aape kwa Mwenyezi Mungu au anyamaze
Sasa tumsome Allah ambaye sio Yehova "Yahuh", je yeye anaapa kwa nani?
SURAT ASH-SHAMS 1-3
1. Naapa kwa usiku ufunikapo, 2 kwa mchana uingiapo, 3. na kwa aliye umba kiume na kike..
Hivi mtu anaye apa kwa mwengine anakuwa Mungu au binadamu? Je, nani kaumba hapo. Maana Allah anaapa katika aliye umba, na kuumba ni sifa ya Mungu. Kumbe Allah ambaye sie Yehova hakuumba.
Zaidi ya hapo, Allah anaapa kwa usiku. Kumbe usiku una mamlaka zaidi ya Allah. Allah anaapa kwa mchana, kumbe mchana una mamlaka zaidi ya Allah.
Mbona katika SURAT ASH-SHAMS Allah anaapa kwa (1) Usiku (2) Mchana (3) kwa aliye umba kiume na kike?
Je, ni nani huyu aliye umba Kiume na Kike ambaye Allah wa Islam anaapa kwake? Endelea kusoma...kutoka Biblia Takatifu….
Yeremia 27: 5 Mimi nimeiumba dunia hii, wanadamu na wanyama walio juu ya uso wa nchi, kwa uweza wangu mkuu, na kwa mkono wangu ulionyoshwa; nami nawapa watu kama inipendezavyo.
Sasa tunamsoma Yehovah ambaye ni Mungu wa Biblia kuwa yeye ndie aliye umba kila kitu, pamoja na Kiume na Kike ambacho Allah wa Islam anaapa kwake. Kwahiyo, Jehovah aliumba kiume na kike, na Allah wa Islam anaapa kwake, sasa jaza mwenyewe nani ni Mungu?
Je, Mungu anaweza kuapa kwa Mwengine? Endelea kupata elimu …
Waebrania 6:13 Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa.
Jehova anasema hakuna Mkubwa wangu wa kuapa kwake, lakini Allah katika Kuran anasema kuwa yeye anaapa kwa aliye umba kiume na kike.
Hivyo basi leo tunafahamu kuwa aliye umba ni Jehona na Allah anaapa kwa Jehovah Mungu wa Biblia na Wakristo.
Mungu awabairiki sana
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa yesu Kristo
Copyright © Max Shimba Ministries 2016

WAISLAM WA NCHINI SUDAN WAKIWA WAMELALA MSIKITINI BAADA YA KUZIDIWA NA NJAA WAKATI WA MFUNGO WA RAMADHAM.


Allah ambaye sio Yehova kupitia Quran anasema hivi:
“Hapana kulazimisha katika Dini.” (02:256)
WAKATI HUO HUO ANASEMA TENA HIVI:
WAISLAM WAMELAZIMISHWA KUFUNGA SWAUMU
Quran 2:183 Enyi mlioamini mmelazimishwa kufunga saumu kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha mungu.
SASA TUFUATE LIPI?

KUMBE ALLAH ANAYE MSAIDIZI


1. Je, Allah anaye Msaidizi, mbona anatumia wingi katika kujieleza?
2. Kama Allah hana msaidizi, je Waislam mna Ma-Allah wangapi?
Hebu rejea kwenye Kuran kwanza:
Suratul Anbiyaa 91. Na mwanamke aliye linda uke wake, na TUKAmpulizia katika roho YETU, na TUKAmfanya yeye na mwanawe kuwa ni Ishara kwa walimwengu.
Ndugu zanguni, Allah ameanza vituko vyake hapa. Katika Koran Allah anadai kuwa hana msaidizi Suratul Baqarah: aya 106 ― 107 Lakini katika aya tuliyo isoma hapo mwanzoni - Suratul Anbiyaa 91 tumeona kuwa Allah anatumia wingi alipo kuwa akielezea jinsi alivyo mpa ujauzito Maryam na au labda wenzetu wana MA-ALLAH WENGI.
Waislam, nyie mna Ma-Allah wangapi?
ALLAH ANAMUUMBA ISA BIN MARYAM KWA KUTUMIA WINGI
Kuran imejaa utata, hebu soma hapa Suratul Attahriim 12. Na Mariamu binti wa Imrani, aliye linda ubikira wake, na TUKAmpulizia humo kutoka ROHO YETU, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa wat'iifu.
HAPA: Allah anasema kwa undani zaidi TUKAmpulizia ROHO YETU. Hivi huyu Allah ni kweli alikuwa Mungu au ni madai ya Muhammad na rafiki yake Jibril? Mbona alisema kuwa yeye hana msaidizi wala Mwana? Kivipi Allah anatumia wingi katika kumuumba Isa Bin Maryam? Kumbe Waislam mna Ma-Allah wengi.
Aya zaidi kuhusu Maryam na kupata ujauzito za Isa: Suratul Anbiyaa 91.
Endelea hapa tena:
ALLAH ANAMUUMBA BINADAMU KWA KUTUMIA WINGI:
Suratul Hijr 26. Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
HAPA tumesoma kuwa Allah anamuumba Binadamu kwa kutumia wingi" Nukuu: Na TULIMUUMBA MTU"
Endele hapa tena
ALLAH ANAUMBA MAJINI KWA KUTUMIA WINGI:
Suratul Hijr 27. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
Allah anaendelea kutumia wingi katika uumbaji. Sasa anasema kuwa "TULIWAUMBA MAJINI" Allah anaendelea kutumia wingi katika uumbaji.
Je, unafikiri kuwa labda Allah alijisahau au fanya makosa pale alipo sema kuwa yeye hama msaidizi. Kumbe Waislam wana Ma-Allah wengi.
Wadhalimu wa dini ya Kiislam wamekuwa mstari wa mbele kusema kuwa, eti Wakristu wana miungu mingi na wao wana Mungu Mmoja tu naye ni Allah. Leo tumejifunza kuwa, Allah hayupo peke yake maana sasa anatumia wingi katika kazi zake ikiwa pamoja na ya uumbaji wa Binadamu na Majini.
Nukuu zingine ambazo ALLAH anatumia wingi: S. 3:44, S. 3:145, S. 17:1, S. 6:114, S. 19:40-42, 50-53, 56-74 Arberry, S. 2:252-253 , S. 3:108 Y. Ali; cf. S. 45:6, S. 37:161-166 Pickthall, S. 37:170-182 Y. Ali, S. 23:12-14 Arberry, S. 19:16-2, S. 66:12 Pickthall, S. 15:26-29 Pickthall.
Ndugu zanguni nimeweka ushaidi wa kutosha kutoka Quran yao kuhusu wingi ambao Allah amekuwa anautumia kila mara kwenye Quran yake.
1. Waislam, nyie mna MA-ALLAH WANGAPI?
2. Je, Allah anaye Msaidizi?
3. Je, Allah anaye Mwana ambaye na yeye ana wadhifa wa Ki Allah?
4. Kwanini Allah anatumia wingi huku tukifahamu kuwa Allah hafananishwi wala hana msaidizi?
Hakika kuna shaka kubwa kubwa kwenye Quran ya Allah ambayo sasa inasema kwa kutumia wingi.
Biblia inasema kuwa Mungu anaye Mwana na anaitwa Yesu, zaidi ya hapo Biblia inatuambia kuwa kuna Mungu Roho Mtakatifu na hao wote ni WAMOJA katika Roho.
Karibuni kwa Mungu wa Biblia ambaye amesema kiuwazi kuwa yeye ni Baba na ana Mwana ambaye na yeye ni Mungu. Kumbuka hawa ni wamoja kwa kupitia Mungu Roho Mtakatifu.
Katika Huduma yake.
Max Shimba Ministries Org.
1633 Broadway, 30th Floor, New York, NY 10019

MTUME MUHAMMAD ALITUMIA NDUMBA



1. Mtume Muhammad alitumia Ndumba
2. Mtume Muhammad adai eti Nywele zake zinatibu jicho ovu.
3. Wapi katika Biblia tunasoma kuwa Manabii na Mitume wa Biblia walitumia Ndumba?
Ndugu Msomaji,
Leo ningependa tusome kuhusu Muhammad na Utumiaji wa NDUMBA katika Uislam,
MTUME MUHAMMAD ANATUMIA NDUMBA
Muhammad alitumia ndumba [nguvu za kimazingaombwe] dhidi ya jicho ovu na wanyama jamii ya mjusi wenye sumu Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3525 uk.48.
Hivi wapi tunasoma katika Taurat au Zaburi au Injir kuwa Mitume na Manabii wa kwenye Biblia walitumia NDUMBA?
Hivi Allah hana uwezo wa kutibu jicho ovu au Sumu mpaka atumie NDUMBA?
MUHAMMAD SASA AMPA MKE WAKE AISHA NDUMBA
Muhammad alimpa ‘Aisha ndumba ili kutibu jicho ovu. Sahih Muslim juzuu ya 3 kitabu cha 24 na. 5445,5447-5450 uk.1196.
Hivi Ndumba ina tofauti gani na UCHAWI? Sasa hapo juu tumesoma kuwa Muhammad ametoa NDUMBA kwa mke wake kipenzi.
Wapi tunasoma kuwa Manabii wa Biblia walitumia NDUMBA?
Muhammad aliamini katika jicho ovu, na kulikuwa na hirizi dhidi yake al-Tabari juzuu ya 39 uk.134.
Sura mbili za mwisho (113 and 114) ziliandika juu ya ubaya wa jicho ovu kufuatana na Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3517 uk.41.
Hata hivyo, sura za 113 na 114 hazimo katika toleo la Ibin Mas’ud katika Korani (The Fihrist uk.57). Kuondolewa huko hakukuwa kwa bahati mbaya. Ilitaarifiwa kuwa Ibn Mas’ud alisema, "Hirizi mbili-Sura za [113, 114] si Kitabu cha Mungu."
Ibn Mas’ud alikuwa katibu muhtasi wa Muhammad. Muhammad aliwaambia watu wengine wajifunze kutoka kwa Ibn Mas’ud na wengine watatu. (Bukhari juzuu ys 6 kitabu cha 60 sehemu ya 8 na.521 uk.486-487).
MUHAMMAD ASEMA NDUMBA NANGAE HUTIBU JICHO OVU
Ndumba hutibu jicho ovu. Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3510, 3511 uk.41; juzuu ya 5 na.3512 uk.42.
ALBADIRI NI NDUMBA
Albadiri inaruhusiwa dhidi ya jicho ovu na inge Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3513-3518 uk. 42-44.
Jicho ovu ni hali halisi. Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 sehemu ya 36 na.636 uk.427, juzuu ya 7 kitabu cha 71 sehemu ya 86 na.827 uk.538. Soma pia Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 55 sehemu ya 9 na.590 uk.386.
Jicho ovu ni kweli. Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3506, 3507 uk.39.
"…Ushawishi wa jicho ovu ni hali halisi." Sahih Muslim juzuu ya 3 kitabu cha 24 na.5426 uk.1192. Soma pia Sahih Muslim juzuu ya 3 kitabu cha 24 na.5424-5427 uk.1192.
Amir bin Rabia alisemekana kuwa alitoa jicho ovu kwa mtu fulani. Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3508 uk.40.
Hata hivyo nywele za Muhammadi zilikuwa tiba ya jicho ovu. Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 72 sehemu ya 65 na.784 uk.518.
Wakati Muhammadi aliponyolewa nywele zake, wafuasi wake walitaka kudaka kila kipande cha unywele wake kwa ajili ya kukitunza. Muhammadi kwa ukarimu alisambaza nywele zake kwa watu. Sahih Muslim juzuu ya 2 kitabu cha 7 na.2991-2994 uk.656-657.
ETI MKIJUMUIKA TAREHE 17, 19, 21 YA KILA MWEZI NI TIBA. HII NAYO NI NDUMBA YA AINA YAKE
Muhammad alisema pia kuwa ikiwa watu watajiumika tarehe ya 17, 19 au 21 ya mwezi itakuwa ni tiba kwa kila ugonjwa. Abu Dawud juzuu ya 3 na.3852 uk.1084.
Kama Muhammad alikuwa Mtume wa Mungu, kwanini alifanya NDUMBA?
Kama Allah ni Mungu, kwanini anaruhusu kufanya NDUMBA?
Kama Uislam unatoka kwa Mungu, kwanini unaruhusu NDUMBA nangae?
Karibu kwa Yesu aliye hai na Mungu Mkuu,
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

WACHAWI WOTE WATAKWENDA MOTONI

ALLAH ATEREMSHA UCHAWI NA KUWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA
Huu ni Msiba Mkubwa sana katika taifa la Mtume Muhammad. Mara nyingi Wakristo wamekuwa wanajiuliza, hivi, uchawi ulitokea wapi na mwanzo wake ni nani?
Wote wanaologa, wanaopiga bao, wanaosoma nyota, wanaotumia utambuzi, wote wanaochanja chale, wanaotumia hirizi, wanaopiga bao, wanaosoma alama za mikono, na wote wanaowaendea wenye pepo na waganga, watu hao wote hawatakwenda mbinguni. Kama wewe ni mtu anayekwenda kwa waganga kwa ajili ya kutaka mafanikio kielimu na utajiri nawe pia ni mchawi. Yule aliyekupa uchawi na wewe uliyepokea wote ni kitu kimoja.
SURAT TAHA: 73. Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi.
Kwenye Surat Taha ayat 73 kama ilivyo teremshwa makka kwa Muhammad na kutafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani inasema kuwa ALLAH ANAWALAZIMISHA WAISLAM KUUFANYA UCHAWI. Huu ni msiba ndugu zangu. Swali la kujiuliza, hivi, tokea lini Mungu akawa mchawi? Hivi huu uchawi ulio teremshwa na Allah unafaida gani kwa Wislamu?
Hebu tuangalie tafsir ya pili ya Surat Taha aya 73 kama ilivyo tafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin inasema: 73. Kwani hakika sisi ni wenye kusimama juu ya Imani kumuamini Mola wetu Mlezi wa Haki, ili atufutie madhambi yetu yaliyo pita, na atusamehe huku kushughulikia uchawi ulio tulazimisha tujifunze na tuufanye! Na Mola wetu Mlezi ni Mbora wa malipo kuliko wewe, akit'iiwa; na ufalme wake na uwezo wake kulipa unadumu zaidi kuliko wako.
1. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kujifunza Uchawi
2. Inasema kuwa Waislam wanalazimishwa kuufanya Uchawi.
Ndugu msomaji, leo sina mengi ya kusema maana umesoma wenyewe kutoka Quran kuwa Allah aliteremsha uchawi na kawalazimisha Waislam wajifunze na kuufanya uchawi.
Nawashauri Wakristo wenye marafiki wa Kiislam wawe makini, maana huyo rafiki yako anaweza kuwa ndiye anaye-kuroga kwasababu kalazimishwa na Allah kufanya hivyo.
MTUME MUHAMMAD ANATUMIA NDUMBA
Muhammad alitumia ndumba [nguvu za kimazingaombwe] dhidi ya jicho ovu na wanyama jamii ya mjusi wenye sumu Ibn-i-Majah juzuu ya 5 na.3525 uk.48.
Hivi wapi tunasoma katika Taurat au Zaburi au Injir kuwa Mitume na Manabii wa kwenye Biblia walitumia NDUMBA?
Hivi Allah hana uwezo wa kutibu jicho ovu au Sumu mpaka atumie NDUMBA?
Mungu awarehemu na kuwasamehe ndugu zetu wote wanao fanya Uchawi. Maana Biblia inasema kuwa WACHAWI WOTE WATAINGIA JEHANNAM. 1 Samweli 15 : 23 .......... dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.
Ndugu msomaji, mpokee Yesu aliye hai na upate uzima wa milele. Dini haita kusaidia kitu, maana sasa unaelewa kuwa, ni dini ambayo inakufanya uwe mchawi na kuachana na upendo wa Mungu.
Katika huduma yake,
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2015

WAISLAM THIBITISHENI UWEPO WA ISA BIN MARYAM KWA VITABU VILIVYOKUWEPO KABLA YA QURAN




1. Mimi naomba mtuletee ushahidi unao weza
kuthibitishika wa uwepo wa "Isa na jina la Isa bin Maryam" kwa kutumia hivyo vitabu vilivyo kuwepo kabla ya Quran.
2. Sina muda na aya za Quran. Maana Waislam mnakiri kuwa Injil iliteremshwa na Allah, hivyo basi Injil mnaweza itumia na iwe na jina la Isa.
3. Quran iliyokuja baada ya Injil siitaki. Hadith zilizo kuja baada ya Injil sizitaki. Mimi nataka mtumie vitabu vilivyo kuwepo kabla ya Quran na Muhammad.
Sasa basi. Thibitisheni uwepo wa Isa kwa kutumia vitabu vilivyo kuwepo kabla ya (1) Quran (2) kabla ya Muhammad kuzaliwa (3) kabla ya Sahih Hadith za Muhammad.
Mkinipa huo uthibitisho basi leo nitasilimu na kuwa Muislam.

UTHIBITISHO 10 KUWA YESU NI MUNGU



“Wahubiri wa injili” wa Kiislamu huwa wanapinga kuwa Yesu ni Mungu na unapowakatalia wanakwambia, “Lete andiko.” Maandiko yapo mengi sana ndani ya Biblia juu ya ukweli kwamba Yesu ni Mungu. Ni mengi mno!
Ukishawapa andiko, wanabadilika na kusema, “Nataka maneno aliyoongea Yesu mwenyewe.” Kwa madai haya hata kwenye Qurana hawawezi thibitisha kuwa Allah Allah ni mungu, zaidi ya hapo, hata Utume wa Muhammad unakuwa kwenye njia panda, maana hakuna aya kwenye Quran Muhammad anasema mimi Muhammad ni mtume wa Mungu.
Hiki ni kigezo POTOFU na si cha kibiblia hata kidogo. Ukweli ni kwamba, Biblia YOTE ni Neno la Mungu. Haijalishi amezungumza Musa, Isaya, Yohana, Petro au Yesu mwenyewe. Imeandikwa:
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2Petro 1:21).
Hivyo, kudai kwao eti, “Nataka maneno aliyosema Yesu mwenyewe,” ni kigezo batili na kisicho na mantiki hata kidogo.
1. YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUZALIWA
Ufuatao ni ushahidi wa kibiblia kwamba YESU KRISTO ni Mungu.
Yohana 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.
NIKO ni jina la Mungu peke yake. Tunakutana na jina hilo pale Musa alipoongea na Mungu na kutumwa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka Misri. Imeandikwa:
Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO (Kutoka 3:13-14).
Mwanadamu yuko kwa sababu Mungu alisababisha awepo. Gari liko kwa sababu injinia au mbunifu alisababisha liwepo. Nyumba ipo kwa sababu fundi alisababisha iwepo. Lakini Mungu YEYE YUKO TU!! Hayupo kwa kusababishwa na yeyote! Ndiyo maana akasema MIMI NIKO AMBAYE NIKO! Yesu ni NIKO. Kwa hiyo, Yeye ni Mungu.
2. YESU NA BABA NI WAMOJA
Yohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.
Waislamu wana msemo wao kwamba eti, Yesu na Mungu ni wamoja katika malengo, si katika asili yao. Basi huwa nawauliza swali kuhusu aya ifuatayo ya Isaya, nao wanazimika na kukosa jibu:
Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu MTOTO amezaliwa, Tumepewa MTOTO MWANAMUME; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, Mfalme wa amani.
Aya hii iko wazi kabisa. anayetajwa ni Yesu kwamba Yeye ni Mungu mwenye nguvu.
Yohana 14:9
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Maneno haya Yesu aliyasema baada ya kuulizwa swali lililo wazi kabisa, ambalo lilikuwa na lengo la kumjua MUNGU BABA! Imeandikwa: Filipo akamwambia, Bwana, UTUONYESHE BABA, yatutosha. Ndipo Yesu akajibu waziwazi: ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA. Maana yake ni kuwa, “Mimi ndio Baba mwenyewe.”
3. YESU NI MWANZO NA MWISHO
Ufunuo 1:17 na Ufunuo 22:13
Mimi ni wa kwanza na wa mwisho
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Ni Mungu TU ndiye mwenye uwezo wa kuwa wa kwanza na wa mwisho; Yesu ni Alfa na Omega. Kwa hiyo Yeye ni Mungu.
4. YESU NI NENO
Yohana 1:1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye NENO ALIKUWA MUNGU.
Andiko hili Waislamu hawalipendi kabisa. ni kwa sababu liko wazi mno. Yesu ni Neno; na Neno ni Mungu; hivyo, Yesu ni Mungu!
5. THOMASO AKIRI KUWA YESU NI MUNGU, NA YESU HAKUKATAA KUITWA MUNGU
Yohana 20:28
Tomaso akajibu, akamwambia, BWANA WANGU NA MUNGU WANGU!
Tomaso aliposema hivi, Bwana Yesu hakukanusha na kusema, “Mimi sio Mungu.” Badala yake: Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. (Yoh 20:29).
Kama Thomaso alikuwa muongo, kwanini Yesu hakukataa kuitwa Mungu. Imani zote zinakiri kuwa Yesu hakufanya dhambi na hakuwa na dhambi.
6. DAMU YA YESU INAMAMLAKA
Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake MUNGU, ALILOLINUNUA KWA DAMU YAKE MWENYEWE.
Ni Mungu gani mwenye damu huyu? Jibu liko wazi. Huyu ni Yesu Kristo. Huyu ndiye aliyetoa uhai wake na kumwaga damu yake msalabani; na hapo ndipo alipoanzisha Kanisa.
7. KATIKA YESU, KILA KITU KILIUMBWA
Wakolosai 1:16
Kwa kuwa KATIKA YEYE VITU VYOTE VILIUMBWA, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
Katika Yeye Yesu vitu vyote viliumbwa. Ina maana kuwa vitu vyote vilitokana na Yesu; maana Yesu ni Neno la Mungu. Na tunajua kuwa Muumba wa vitu vyote ni Mungu; hivyo, Yesu ni Muumba – Yeye ni Mungu!!
8. KATIKA YESU, UNAKAA UTIMILIFU WA MUNGU
Wakolosai 2:9
Maana KATIKA YEYE UNAKAA UTIMILIFU WOTE WA MUNGU, kwa jinsi ya kimwili.
Sisi sote ni watu wasio wakamilifu. Tunaanguka tena na tena kwenye dhambi. Kwa hiyo, hakuna mwanadamu wa kawaida ambaye anaweza kujigamba kwamba yeye ametimia kama alivyo Mungu. Lakini katika Yesu “utimilifu WOTE wa Mungu unakaa.” Kwa nini? Kwa sababu Yeye ndiye Mungu huyohuyo.
9. YESU NI MUNGU PAMOJA NASI "EMMANUEL"
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
10. YESU NI MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii: Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yer 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua!

POSA SABA (7) ZA MUHAMMAD ZILIZO KATALIWA



1. Kwanini baadhi ya wanawake walikataa posa za Muhammad?
2. Kwanini muhammad aliendelea kuomba/toa posa na huku zikikataliwa?
Ndugu msomaji,
Leo nitakupa ushahid kadhaa kuonyesha jinsi Muhammad alivyo penda wanawake lakini wengine walikataa posa zake na kuto jali utume wake alio pewa na Mkewe.
Muhammad alimwomba amuoe Ghaziyyah kwa sababu ya uzuri wake, lakini alikataliwa. Tabari anadai kuwa [Ghaziyyah] hakuwa mwaminifu lakini hatoi ushahidi. al-Tabari juzuu ya 9 uk.136. Hakuna ushahidi kuwa [Ghaziyyah] hakuwa mwaminifu na kwamba Muhammad hakuwa makini kwa kutokumwadhibu, au kwamba hakuwa mwaminifu na Muhammad alimwadhibu.
Layla aligusa bega la Muhammad tokea nyuma na kumuomba amuoe. Muhammad alikubali. Ndugu za Layla walisema, "Ni jambo baya kiasi gani ulilolifanya! Wewe u mwanamke anayejiheshimu, lakini Nabii ni mpenda wanawake. Tafuta kujitengua toka kwake." Layla alikwenda kwa Nabii na kumuomba aikane ndoa hiyo na aliafikianana na hilo [ombi]." al-Tabari juzuu ya 9 uk.139.
Kutoka al-Tabari juzuu ya 9 uk.140-141, Muhammad alimposa lakini aliishia kutokumuoa:
1) Umm Hani’ bin Abi Talib [Hind] kwa sababu alikuwa na mtoto.
2) Duba’ah binti ‘Amir lakini alikuwa mzee sana.
3) Inaripotiwa kuwa alimposa Saffiyah binti Bashshamah, mateka. Alitakiwa achague mmoja kati ya Muhammad na mume wake, na alimchagua mume wake.
4) Umm Habib bint al-‘Abbas lakini kwa kuwa al-‘Abbas alikuwa kaka wa kulelewa pamoja naye kwa hiyo isingeruhusiwa kisheria kwa hiyo Muhammad aliamua kujiondoa.
5) Jamrah binti Al-Harith. Baba yake alida isivyo sahihi kuwa alikuwa anasumbuliwa na kitu Fulani. Aliporudi, alikuta ameisha kumbwa na ukoma.
Haielezwi kwa kauli moja endapo Umm Hani’ alikuwa muislam kabla au baada ya Muhammad kumwomba amuoe. al-Tabari juzuu ya 39 uk.197 na rejeo chini ya ukurasa 857 uk.197.
Ndugu msomaji ambaye ni mfuasi wa dini ya Uislam, je, unaweza tumabia kwanini posa 7 za Muhammad zilikataliwa?
Max Shimba Ministries

YESU ANAKIRI KWA MDOMO WAKE KUWA YEYE NI MUNGU


Ndugu zanguni, leo YESU anawajibu Waislam kwa mara nyingine tena kuwa yeye ni Mungu, "YESU NI MUNGU".
Hii aya hapa chini katika kitabu cha Ufunuo ni ya Yesu mwenyewee akiongea na Yohana. Yesu anakiri kuwa yeye ni Mungu. Hebu tuisome kwanza:
Ufunuo 21: 6 Yesu Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yo yote. 7 Yeye atakayeshinda atayarithi haya yote, NAMI NITAKUWA MUNGU WAKE, naye atakuwa mwanangu.
Mara nyingi kumekuwa na mtanashi kutoka Waislam kuwa eti Yesu hakuwai sema yeye ni Mungu. Mara zote wamekuwa wakidai kuwa, tuwaletee aya ambayo Yesu anasema yeye ni Mungu. Ingawa, Biblia imewajibu kuwa Yesu ni Mungu kutoka sehemu mbalimbali, lakini wamekuwa wabishi na kung'ang'ania waletewe aya, ili wabatizwe na kuwa Wakristo. Kwasababu Biblia imekamilika na haina shaka ndani yake. Leo Biblia inawajibu tena kuwa Yesu ni Mungu.
Aya ya 7 inasema kuwa, NUKUU: [Yeye atakayeshinda atayarithi haya yote, NAMI NITAKUWA MUNGU WAKE, naye atakuwa mwanangu.]
Yesu amekiri kuwa mtu yeyote yule atakaye urithi ufalme wake, basi ifahamike kuwa.
Moja: Yesu atakuwa Mungu wake
Pili: Wewe utakuwa Mwana wake.
Huu ni ushaidi mwingine kuwa Yesu ni Mungu. Waislam, ningependa mfahamu kuwa, Yesu ni Mungu kama ilivyo andikwa kwenye Ufunuo Sura 21 na aya ya 7.
Je, Upo tayari kumfuata Yesu ambaye ni Mungu? Kumbukeni kuwa, Yesu ndie Njia pekee ya kwenda Mbinguni. Dini haita wapeleka popote pale, lakini Yesu Kristo aliye hai ambaye sasa tunasoma kukiri kwake kuwa yeye ni Mungu, ndie njia pekee ya Uzima wa Milele.
Mpokee Yesu leo ili upate uzima wa milele.
Katika Huduma yake,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Kwa Max Shimba Ministries Org 2014

ROHO, NAFSI NA MWILI


Ndugu msomaji,
Je, mwanadamu ni nani?
Kwa kifupi ninaweza kusema kuwa Mwanadamu ni Roho, ina Nafsi na inakaa ndani ya Mwili.
Ukisoma 1 Wathesalonike 5:23 Inatusaidia Kuona maeneo yote matatu ya mwanadam/mtu;
"Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU na ROHO ZENU na MIILI YENU Mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo"
Hapa unaona Nafsi, Roho na Mwili vimetajwa kwenye hiyo aya.
ROHO NI NINI?
Roho ambayo inahusisha mambo ya Mungu.
Ni ile sehemu ya mtu yenye ufahamu wa Mungu, ambayo hufanywa hai na hutiwa nguvu na Roho wa Mungu wakati wa Wokovu. Kabla ya mtu Kuokoka, sehemu hii, haifanyi kazi kwa utimilifu kabisa kwa sababu ya dhambi. Dhambi huifanya kuondolewa nguvu ya kutenda kazi sawa sawa, kwa Amani na Roho ya Mungu. Lakini kupitia Ubatizo wa Roho Mtakatifu, mwanadamu hupokea nguvu ya kiroho, inayomwezesha kuishi maisha ya Kristo.
Roho inahusika na:-
i) Maombi na Ibada na Mungu,
ii) Ushirika na Mungu,
iii) Mapokezi ya karama za Roho,
iv) Vita vya kiroho,
v) Kuunda Mawazo na Ndoto,
vi) Dhamira, Kupambanua,
vii) Udadisi, Kuuliza,
viii) Ufahamu, Kutafsiri,
ix) Shuhuda kwa Wanadamu
NAFSI NI NINI?
Nafsi inahusika na mambo ya mtu.
Ni ile sehemu ambayo ina ufahamu wamtu mwenyewe au kiini cha ubinafsi wa mtu. Kazi yake ni:-
i) Kufikiri – Kutafakari, kuona
ii) Hisia – Kujisikia kuwa na tamaa na Upendo
iii) Utashi – Nia, Kuamua
MWILI NI NINI?
Mwili unahusika na mambo ya Ulimwengu.
Ni ile sehemu ya mwanadamu ambayo inafahamu na kukubaliana na ulimwengu wa nje. Inafanya yafuatayo:-
i) Utambuzi wa Ulimwengu, - yaani ile hali ya mwili kupokea habari kutoka Ulimwenguni kwa njia ya Ufahamu.
ii) Urejeshi – yaani ile hali ya Mwitikio wa kutenda kutokana na kutendewa kitu, kupitia utaratibu wa Maneno na Matendo.
iii) Udhihirisho – yaani ile hali ya Mwili ya kutoa habari za Ulimwengu kwa Mawazo, Kujisikia na Maamuzi ya Nafsi.''
Hivyo basi, Mtu ni Roho.
1) Mungu alimuumba mwanadamu kwanza kama roho ( Mwanzo 1:26) hapo bila mwili ndiyo maana Biblia inasema Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake kwa sababu Mungu ni Roho.
Mtu ambaye Mwanzo 1:26 inamuongelea, Biblia yenyewe inathibisha kuwa ni roho lakini yenye mwili wa rohoni (1 Korintho 15:44) ikiwa kuna mwili wa asili basi kuna mwili wa rohoni pia.
2) Mungu aliumba roho ya Mwanadamu kwanza ndio akaumba mwili wa nyama na nafsi baadae.
(Mwnzo 2:7) Mungu akauumba mwili wa Adamu kwa udongo akaichukua ile roho (kumbuka ina mwili wa kiroho) akaiweka/ingiza katika mwili kwa kuipulizia ndani ya ule udongo alio uumba, na mtu akawa nafsi hai.
Hivyo basi;
Mwanadamu amegawnyika mara tatu
1) Roho yenye ufahamu wa mambo ya Mungu. Chakula cha Roho ni neno la Mungu.
2) Nafsi ni shemu yenye ufahamu ambapo vitu vya kujifunza au elimu au kumbukumbu vinakaa. Roho huitia nafsi nguvu au kuwa mahiri kwenye eneo fulani ambalo rohoni umebarikiwa ili hicho kitu kithiirike kwenye ulimwengu wa mwili.
3) Mwili ni sehemu ya mwanadamu inayo onekana na imebeba roho na nafsi.
Bonus question.
KUFA NI NINI?
Kufa ni kitendo cha roho kuachana na mwili, kama huyo mtu(roho) alipokuwa ndani ya mwili aliishi maisha matakatifu roho yake itakwenda kwa Mungu na kama aliishi maisha yasiyompendeza Mungu huyo mtu(roho) atakwenda kuzimu.
Hivyo basi itunze sana Roho yako maana wewe ni Roho una nafsi na unaishi kwenye mwili.
Mungu awabariki sana.
Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo

TRENDING NOW