Monday, July 11, 2016

ALLAH NA MUHAMMAD WARUHUSU NDOA YA MUT’AH. HII NI NDOA YA MASAA, UNAOA MKE KWA MASAA KWA AJILI YA NGONO HALAFU UNAMPA TALAKA


Somo la leo ni la Umalaya kama lilivyo pewa kipaumbele na mungu wa Uislam ajulikanaye kwa jina la Allah. Uislam unaruhusu Umalaya kwa kutumia sheria ya Mut'ah.
Mut'ah ni ndoa AMBAYO inaweza kudumu kwa muda mfupi sana. Ndoa Hii haihitaji mashahidi, na haina kipindi cha 'iddah. Fidia ya kima cha chini ambayo inaweza kulipwa kwa mwanamke kwa ajili ya mahusiano ya kingono ni dirham moja (yaani, chini ya dola senti 25) ". 29 (Dr Ahmad 'Abdullah Salamah, Mashia Dhana ya Ndoa Muda (Mut'ah)
Katika Mut'ah, HAKUNA TALAKA ; Pale utakapo mlipa huyo hawara kiasi cha fedha na utakapo maliza shida zako za kingono, unakuwa huru na hakuna wajibu, hakuna sheria ya urithi, au mchakato wa talaka. Sheria inayo bakia ni moja tu ambayo inambana mwanamke kwa siku 45 kabla ya kuingia kwenye ndoa nyingine ya Mut’ah, wakati huohuo Mwanaume yeye anaweza kuingia Ndoa nyingine ya Mutah mara moja, hata ikiwa bado ameoa katika Mut'a nyingine. Cha kushangaza, Waislam wanashabikia hii Ndoa ya kimalaya huku Allah akiwaambia kuwa, kabla ya kuingia Ndoa nyingine ya Mut’ah lazima watoe talaka, wao wamejipa haki ya kuendelea kutekeleza matakwa yao ya kingono. Katika Surah 2 aya 228 Allah anasema, Wanawake wangoje peke yao kwa vipindi vitatu kila mwezi na si halali kwao kuficha kile ambacho Allah aliviumba katika matumbo yao . Katika Mut'a, mwanamke anaweza kuwa mjamzito na mtoto wa mume wake wa kwanza wa Mut'a na kuolewa na mume wake wa pili wa Mut'a au kuingia ndoa ya kudumu.
Ndugu wasomaji, leo tumejifunza kuhusu umalaya ndani ya dini ya Kiislam. Uislam umeruhusu Ndoa hii ili kukidhi matakwa ya Wanaume wa Kiislam na kuendelea kuwashusha hadhi Wanawake wa kiislam ambao katika Uislam wao ni nusu ya Mtu.
Quran 4:11. Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili. Na ikiwa wanawake zaidi ya wawili, basi watapata thuluthi mbili za alicho kiacha maiti. Lakini akiwa mtoto mwanamke ni mmoja, basi fungu lake ni nusu. Na wazazi wake wawili, kila mmoja wao apate sudusi ya alicho kiacha, ikiwa anaye mtoto. Akiwa hana mtoto, na wazazi wake wawili wamekuwa ndio warithi wake, basi mama yake atapata thuluthi moja. Na akiwa anao ndugu, basi mama yake atapata sudusi. Haya ni baada ya kutolewa alicho usia au kulipa deni. Baba zenu na watoto wenu, nyinyi hamjui ni nani baina yao aliye karibia zaidi kwenu kwa manufaa. Hiyo ni Sharia iliyo toka kwa Mwenyezi Mungu. Bila ya shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mwenye hikima.
Katika Uislam, Mwanamke hana thamani yeyote ile, ndio maana Allah alitoa ahadi ya Wake 72 kwa Wanaume wa Kiislam na kutotoa ahadi yeyote ile kwa Wanawake wa Kiislam.
Quran 2:228. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao. Na Allah ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima
Allah anaendelea kusema kuwa Mwanaume wa Kiislam ni wathamani zaidi ya Mwanamke wa Kiislam. Hapo ndipo tunaelewa kuwa, hata hii Sheria ya ndoa ya MUT’AH iliwekwa ili kuwakidhi Wanaume ambao wapo juu ya Wanawake.
Ndugu wasomaji.
Mungu wa Biblia anakataza umalaya wa aina yeyote ile.
Katika Injili kutokana na Mathayo Sura ya 5 aya ya 28 inasema kuwa: lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Neno la Mungu linatuonya kwamba, hata kumwangalia Mwanamke kwa matamanio ni kutenda dhambi, lakini katika Uislam, unayo ruhusa ya kumtamani Mwanamke na kuingia kwenye ndoa ya Mut’ah ili kukidhi shida zako za kimwili. Hii ni tofauti ya Yehovah wa Biblia na Allah wa Koran ambaye anaruhusu umalaya kupitia Mut’ah wakati Yehovah anasema kufanya hivyo ni kutenda dhambi.
Mungu atusaidia ili tuifahamu kweli iliyo katika Kristo Yesu.
Katika Huduma yake
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

YESU NI MUNGU


Kama kawaida Waislam wanazidi kushikiria na kupinga kuwa Yesu ni Mungu! na Kinacho nishangaza wakipewa maandiko kuhusu u Mungu wa Yesu, wanachofanya ni kubadilisha maada!
Utasikiaaa "Oooh!!! Paulo sio Mtume wa Mungu. Mara ooooh Yesu hakufa!! Ooooh Wakristo mnakula Mashonde"na wanakuletea hoja nyingi ili kupoteza mada husika na Wakristo wanapowajibu kwa kutumia maandiko na kutaka kuendelea na maada husika wanabaki kuchanganyikiwa na kukimbia maada!
HUKO NI KUJIDANGANYA WENYEWE NDUGU ZANGU WAISLAM!!!! SISI Wakristo kazi yetu kuelimisha!! Maana Bwana Yesu alituagiza KUHUBIRI INJILI
"*************"
Marko 16:15-16(Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. ).
LAKINI HOJA YAO KUU NI IPI???
Leo mwislam mmoja alikuja inbox kwangu na hii hoja tena kwa ujasili wote akasema haya leta Biblia yako unijibu hoja hii
AYUBU 36 aya 26
Tazama, Mungu ni Mkuu Nasi hatumjui. Hesabu yake haitafutiki
Haya sasa umeona hapo Juu! Hesabu ya Miaka ya Mungu hakuna aijuaye..tangu kuwepo kwake Yesu miaka yake inaesabika!! Itakuwaje Yesu awe Mungu?
Ebu soma hii
Luka 3:23
Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusuph, wa Eli!
Haya kwa mujibu wa maandiko niliyokupa hapo juu niambie JE YESU ANASIFA YA MUNGU?
Mwislam akacheka kwa kebehi
hahaahaahaaaha ni jibu bhana! Usinikimbie.
Ukiangalia hoja kama ya huyo hapo ndugu!amejitahidi kuisema kwa ujasiri wote lakini amesahau kwamba nasisi tunaijua Biblia vizuri sana na inamajibu yote.
Kwa kuangalia hoja ya huyo ndugu hapo juu, na mjibu kama ifuatavyo:
Kamata Biblia yako twende sawa hapa!
Imeandikwa:
Wafilipi 2:5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Ukiangalia maandiko hapo juu, unaona Yesu alikuwa namna ya Mungu lakini kwa upendo wake mkuu aliamua kuja ulimwengu kutuokoa (Yohana3 aya 16)
Alijifanya kuwa hana utukufu akatwaa namna ya mtumwa akawa anamfano wa Mwanadamu.
Imeandikwa kwamba: Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima; umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (Zaburi 8:4-6).
Mtunga Zaburi anasema mtu ni kitu gani paka umuangalie.
Hapo kuwa Yesu alitupenda paka akatoka kwenye kiti chake cha enzi ili aje kutuokoa toka dhambini.
Imeandikwa: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (Yohana 3:16).
JE WEWE USIYEMWAMINI YESU una uzima wa milele? (tafakari) Ukisoma Yohana 8:56 Yesu anawaambia Wayahudi. Ibrahim, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu: naye akaiona akafurahi 57 Basi Wayahudi wakamwambia, wewe hujapata bado miaka Hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? 58 Yesu akawaambia amin, Amin, nawaambia YEYE IBRAHIM ASIJAKUAKO,MIMI NIKO.
Yesu ni Mungu alikuwepo kabla ya kuumbwa kwa dunia. YEYE NI ALFA NA OMEGA.
Imeandikwa
Hapo mwanzo kulikuwako Neno naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu (Yohana1:1)
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu: nasi tukauona utukufu wake.utukufu kama wa mwana atokaye kwa Baba: Amejaa neema na kweli. (Yohana1:14)
Nadhani hadi hapo Waislam wanaanza kuelewa somo!!
Ilibidi Yesu Mungu Mkuu kufanyika mwili ili kufidia dhambi zetu mimi na wewe! (Warumi5:8)
Imeandikwa
Yeye asiyejua dhambi alimfanya dhambi kwa ajili yetu ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye.
Kuna baadhi ya Waislam wanasema "kwahiyo nyinyi Wakristo mna Mungu watatu"
Jibu ni kwamba! Mungu wetu ni mmoja tu!
Mungu Baba
Mungu Mwana
Mungu Roho Mtakatifu
=Mungu mmoja!!
Ila amegawanyika katika Utatu. (Kumb 6;4)
Maana ya Nafsi Tatu angalia mwenyewe
Mwanzo1:1, 1:26, 3:22
Isaya 6:8
Mathayo 3:16-17
Soma Yohana 10:30
Imeandikwa
1Timotheo2:5
Kwasababu Mungu ni mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja mwanadamu kristo Yesu 6 ambaye alijitoa mwenyewe kwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.
Ukiangalia kwenye andiko hilo unaona kazi ya kila nafsi!
Mungu Baba katika uumbaji
Mungu Mwana katika ukombozi
Mungu Roho Mtakatifu katika ualimu!
Majukumu
Baba-Mwana-Roho Mtakatifu!!
Wakorintho 8:6
Lakini kwetu sisi Mungu ni Mmoja tu aliye Baba ambaye vitu vyote vimetoka kwake: Yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo ambaye kwake vitu vyote vimekuwako na sisi kwa yeye huyo!
Ukiangalia andiko hilo utagundua Yesu ana sifa zote za ki Mungu!
-Yeye ni muumbaji
-Mkombozi
1Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu.
MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, akaonekana na Malaika, akahubiriwa katika mataifa,
Akaaminiwa katika ulimwengu, akachukuliwa juu katika utukufu.
Ni Mungu gani aliyedhihirishwa katika mwili? Jibu liko wazi. Ni Yesu Kristo peke yake.
Tito 2:13
….tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa KRISTO YESU, MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU
Yesu Kristo ni Mungu Mkuu!!
Shida KUU ya Waislamu ni hii:
Wanampima Mungu kwa vigezo vya kibinadamu. Mungu anasema: Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza? (Yeremia 32:27)
Jibu liko wazo. HAKUNA!
Lakini utakuta Waislamu wanauliza maswali ya ajabu sana. Eti, kama Yesu ni Mungu, wakati amekufa, nani alikuwa anaangalia dunia?
Hili ni swali linalofaa kuulizwa juu ya kiumbe. Kama tungesema kuwa mwanadamu fulani alikuwa amekufa, ndipo kuna mantiki kuuliza kwamba, wakati amekufa nani alikuwa anatunza familia yake? Maana hili ni swali linalohusu tabia za kibinadamu kwa kuwa mwanadamu hawezi kuwa mahali kuwili au zaidi kwa pamoja. MUNGU SI MWANADAMU! ANAWEZA YOTE – NA HASA MUNGU WA IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO!
YESU NI MUNGU MILELE NA MILELE!!
HALELUYA!!
HITIMISHO
Yohana 8:31 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini. NINYI MKIKAA KATIKA NENO LANGU Mmekuwa wanafunzi wangu kwelikweli 32 tena mtaifahamu kweli nayo hiyo ITAWAWEKA HURU.
Ndugu zangu Waislam njooni kwa Yesu mpate kujua kweli na hiyo kweli itawaweka huru!
-itawaweka huru na dhambi
-itawaweka huru na vifungo vya Shetani
Ndugu yangu kwanini un'gan'gani kubaki kwenye vifungo vya Shetani wakati Yesu anakuita kwa sauti ya upole!!
Mimi ndimi njia ya kweli na uzima HAKUNA AJAYE KWA BABA ILA KUPITIA MIMI (Yohana 14:6)
Sasa basi unategemea kwenda mbingu ipi kama unamkataa Yesu?
Tafakari
Hoji mambo
Chukua hatua
IJUE KWELI NAYO ITAKUWEKA HURU!!

POLISI NCHINI RWANDA IMEUNGA MKONO KUPIGWA MARUFUKU KWA UVAAJI WA NIQABU "GUBIGUBI" NCHINI HUMO........


Kitengo cha Polisi nchini Rwanda kimeunga mkono maamuzi yaliyofavywa na Baraza Kuu ya Waislamu nchini Rwanda la kupiga marufuku uvaaji wa NIQAB "GUBIGUBI". Hijabu ni vazi ambalo huvaliwa na wanawake wa Kiislamu kufunika uso mzima na Kubakiza macho tu. Huu ni utamaduni wa Kiislam na nchi za Kiarabu.
Kamishna Msaidizi wa Polisi wa Rwanda Bwana Celestin Twahirwa amesema kuwa POLISI RWANDA imepokea Uwamuzi huo wa Baraza kuu kwa mikono Miwili na Kusema ni Uamuzi Mzuri katika kuimarisha Usalama na Ulinzi wa Nchi na sio wa Kidini.
Kwa habari zaidi soma hapa:
RNP supports decision on Niqab by High Council of Muslims in Rwanda
Assistant Commissioner of Police (ACP) Celestin Twahirwa, Rwanda National Police spokesperson.
Following a decision by the High Council of Muslims in Rwanda banning Niqab, a veil worn by Muslim women covering the whole face apart from eyes, Rwanda National Police (RNP) has welcomed and supported the decision adding that it is a measure for safety and security.
The decision to ban Niqab, cloth that covers the face as a part of sartorial Hijab, was reached during the meeting of High Council of Muslims in Rwanda also known as Fatuwa held on May 14, 2016.
This also followed a report by the Muslim community in Rwanda that raised security concerns the Niqab is likely to cause in the face of the emerging security threats, which are cross-border and transnational in nature.
“Rwanda National Police supports any decision by any institution, religious denominations and other civil society organization that aims at complementing existing policies and initiatives to ensure maximum security,” said RNP spokesperson, Assistant Commissioner of Police (ACP) Celestin Twahirwa.
“Religious institutions and the Muslim community in particular are among RNP active partners in policing and if they find and decide that some of their traditions and beliefs pose security risks it is a healthy decision to do away with them for the general good and we will continue to work together to ensure public order,” he added.
Chanzo: RNP supports decision on Niqab by High Council of Muslims in Rwanda
http://www.police.gov.rw/news-detail/…

WAISLAM WAPAGAWA BAADA YA KUONA SHEHE MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM KUINGIA KANISANI



Baada ya kuona picha hapa chini, baadhi ya Waislam wenye msimamo mkali na wafia dIni wamepinga vikali kitendo cha Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam kuingia Kanisani na kuamua kumuita Kafiri.
Waislam hawa wameshindwa kuvumiLIa na kuonyesha hisia zao kubwa zilizoo jaa chuki kuhusu kitendo cha Shehe wa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam kuingia kanisani.
Waislamu msihukumu kwa kutazama picha, bali fuatilieni mjue hapo ni Kanisani kweli? na kama ni Kanisani kweli, Je! ameenda kufanya nini? kuliko tu kuanza kutoa shutuma kwa kutazama picha.
Maana hata sisi Wakristo, tungeweza kutoa shutuma kwa Pope alipo ingia Msikitini kule Uarabuni, lakini tunajua aliingia kwa sababu zipi na ndio maana Wakristo wenye akili hawakuanza kumshutumu Pope kama ambavyo Waislam wanafanya kwa Shehe wa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaama alipo ingia Kanisani.
Swali kwa Waislam: Kwanini Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam alingia Kanisani?
Usijibu kwa jazba.
SURATUL MAIDDAH-51
Enyi mlio amini msiwafanye mayahudi na wakristo kuwa ni marafiki
Wao ni marafiki wao kwa wao na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki basi huyo ni katika wao hakika mwenyezI mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu.
JE, SHEHE MKUU NI MMOJA WAO?

KUMBE FIRAUNI A.K.A FARAO ALINYENYEKEA NA KUWA MUISLAMU



Ndugu msomaji,
Kutokana na ushahid wa Surat Yunus aya ya 90-92, iliyo teremka Makka na kufanyiwa turjuma na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani inakiri kuwa Farao aka Firauni alisilimu na kuwa Muislam.
Surat Yunus 90. Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!
91. Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!
92. Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu
Aya hizo hapo juu kama zilivyo kwenye Surat Yunus zinatufahamisha kuwa Farao aka Firauni alisilimu na kuwa Muislam, lakini nilipo endelea kuisoma Quran kwa makini, nikakutana na shaka kubwa sana ndani ya Quran. Hebu soma kwanza ......aya kutoka Surat An Nisaai amabazo zinapinga aya kutoka Surat Yunus hapo juu.
Surat An Nisaai 17. Hakika toba inayo kubaliwa na Mwenyezi Mungu ni ya wale wafanyao uovu kwa ujinga, kisha wakatubia kwa haraka. Hao ndio Mwenyezi Mungu huwakubalia toba yao, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na ni Mwenye hikima.
18. Wala hawana toba wale wafanyao maovu mpaka yakamfikia mmoja wao mauti, kisha hapo akasema: Hakika mimi sasa nimetubia. Wala wale wanao kufa na hali wao ni makafiri. Hao tumewaandalia adhabu chungu.
Allah kupitia Surat An Nisaai analeta shaka na utata kwa kusema kuwa, toba inayo kubaliwa ni ile uliyo fanya dhambi kwa ujinga, lakini wote tunafahamu kuwa Farao yeye alikuwa anajua nini anafanya, hivyo hawezi kuingizwa kwenye kundi la wajinga.
ENDELEA KUSOMA UTATA NDANI YA QURAN
Surat Ghaafir 83. Walipo wajia Mitume wao kwa dalili zilizo wazi walijitapa kwa ilimu waliyo kuwa nayo. Basi yakawazunguka waliyo kuwa wakiyafanyia maskhara.
84. Walipo iona adhabu yetu walisema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu kuwa ni wa pekee, na tunaikataa miungu tuliyo kuwa tukiishirikisha naye.
85. Lakini imani yao haikuwa yenye kuwafaa kitu wakati ambao wamekwisha iona adhabu yetu. Huu ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu ulio kuwa kwa waja wake. Na hapo walio kufuru walikhasiri
Allah anaendelea kupinga ya zake mwenye kwa kusisitiza kuwa, yeye huwa hasamehi watu ambao wamekwisha ionja adhabu, lakini cha kushangaza, WAISLAM HAWA HAWA, huwa wanaombea Maiti msamaha wa dhambi, sasa Allah atawasamehe vipi maana teyari wamesha ionja adhabu ya kifo?
Kufuatana na wasomi wa dini ya Uislam, wengi wao nakubali kuwa Allah alimuokoa Farao na kumsamehe dhambi zake na kuwa Muislam. (Muhammad Asad, The Message of the Qur'an [Dar al-Andalus Limited, 3 Library Ramp, Gibraltar 1993], p. 306, fn. 112)
Ndugu zanguni, kila ninapo isoma Quran, huwa napata na kukutana na utata mkubwa sana kiasi cha kujiuliza, hivi ni kweli Allah aliumba na yeye ni mjuzi wa yote? Mbona Quran yake imejaa shaka na utata mkubwa?
Nawasihi Waislam wote duniani, mje kwa Yesu ambaye yeye hana utata wala hana shaka ndani yake. Maana Yesu ni JIBU, NJIA NA YEYE NI MWOKOZI WETU NA MUNGU MKUU.
Je! Unataka kumpa Yesu maisha yako sasa hivi ili akuokoe na kukupatia uzima wa milele? Je! Unajua maana ya kumpokea Yesu maishani mwako?
Kumpokea Yesu maana yake ni KUKIRI kwamba Yesu ni MWOKOZI, na pia hakuna mwingine awezaye kuokoa isipokuwa Yesu pakee. Biblia Takatifu inatuambia kwamba:
“Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (Matendo 4:12)
Kama unataka kuokoka sasa hivi; Tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa kutamka kwa kinywa chako sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)
“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu yote. Ninatubu kwa dhati ya kweli kutoka rohoni mwangu. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho Wako – Uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Nakuomba unifanye niwe vile utakavyo mimi niwe. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina."
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zote zimesamehewa kabisa. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka
Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
(a) Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7).
(b) Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11).
(c) Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17).
(d) Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6).
(e) Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25).
(f) Ikemee dhambi na ujitenge nayo. Ukiamini, kwa jina la Yesu unaweza kuishi maisha matakatifu (Yakobo 4:7-8).
(g) Jidhihirishe wazi kwa watu kwamba wewe umeokoka na pia shuhudia kwa watu injili (Mathayo 10:32-33; Warumi 1:16).
Hongera kwa kuokoka, tangu sasa umekuwa kiumbe kipya. Nakutakia baraka tele katika jina la Yesu Kristo, amina.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 20, 2016

NA UZIMA WA MILELE NDIO HUU, WAKUJUE WEWE ULIYE MUNGU WA PEKEE, WA KWELI NA YESU KRISTO ULIYE MTUMA

Ndugu wasomaji,
Leo nitaielezea aya ya Yohana 17: 3 ambayo Waislam wamekuwa wakiitumia mara nyingi sana kudai kuwa eti, Yesu amekana kuwa yeye ni Mungu. Waislam kwa kupitia mihadhara ya kidini na kwa kutumia vijarida mbali mbali wanatishia Umma wa Wakristo kuwa, Yesu ameukana Uungu. Je, hayo madai ya Waislam ni kweli? Je, hiyo aya ina la zaidi la kujifunza?
Ili uielewe Biblia vizuri, nilazima usome aya kadhaa ili upate kuelewa nini hasa Mungu anasema kupitia Neno lake. Hivyo basi, nimeweka aya ya 4 na ya 5 ili kufafanua nini hasa Yesu alikuwa anasema katika Yohana 17.
Ngoja niziweke aya zote hapa:
Yohana 17: 3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue Wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma.4 Nimekutukuza Wewe duniani kwa kuitimizaile kazi uliyonipa niifanye. 5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele Zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na Wewe kabla ulimwengu haujakuwako.
Yesu katika aya ya 5 [Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele Zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na Wewe kabla ulimwengu haujakuwako] ==> YESU anasema kuwa
1. Yeye aliishi kabla ya Ulimwengu kuwepo! Hapo panaanza kukupa mwanga halisi, wa nini Yesu alikuwa anasema na Yesu ni nani. Imani zote zinakiri kuwa aliye kuwepo kabla ya vitu vyote ni Mungu. Lakini katika aya ya 5, Yesu nae anadai kuwepo kabla ya uumbaji.
2. Yesu anaendelea kusema katika aya hiyo hiyo kuwa, yeye alikuwa na adhama ya Mungu -"UTUKUFU". Yesu anamwambia Mungu Baba kuwa, AMTUKUZE YESU KWA UTUKUFU ALIOKUWA NAO KABLA YA ULIMWENGU HAUJAKUWAKO. Sasa, kama Yesu, sio Mungu na alikuwa Binadamu wa kawaida, kwanini basi amwambie BABA YAKE AMTUKUZE? Yesu anatumia mamlaka gani hayo kudai Utukufu ambao sio wake bali ni wa Mungu pekee?
3. Kama Yesu sio Mungu. Je, alipo dai atukuzwe na Mungu Baba, huoni kuwa alikuwa anakufuru? Lakini Hatusomi kuwa YESU aliwai tenda dhambi yeyote ile. Hata dini ya Waislam, inakiri kuwa, Katika Binadamu wote ambao waliishi Duniani, ni Yesu pekee aliweza kuishi bila ya kutenda dhambi na kuwa na dhambi.
Ndugu wasomaji, madai ya Waislam kuwa Yohana 17:3 INAPINGA UUNGU WA YESU ni Batili kabisa, maana, leo tumejifunza katika Yohana hiyo hiyo kuwa Yesu aliishi kabla ya Ulimwengu kuwepo na Yesu anautukufu wa Mungu.
Aya ya 5 NUKUU: Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele Zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na Wewe kabla ulimwengu haujakuwako.
HOJA:
1. Yesu anadai kuwa aliishi kabla ya ulimwengu kuumbwa.
2. Yesu anadai kuwa anautukufu kama wa Baba yake.
SASA BASI:
1. Yesu ni nani mpaka adai utukufu kama wa Mungu tena kutoka kwa Mungu Baba?
2. Yesu ni nani mpaka aseme kuwa aliishi hata kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu, tena namwambia Mungu Baba?
Ndugu zanguni,
Mada imekamilika na kujibu maswali ya Waislam kuwa Yesu aliukana uungu wake katika aya 3 ya Yohana 17.
Nawakaribisha wote Kwa Yesu Kristo aliye hai. Yeye ndie njia kweli na uziama. Njooni kwake ili mpate maisha ya milele na yenye uzima tele.
Katika Huduma yake,
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu.
Kwa Max Shimba Ministries Org.
April 28, 2015 @Max Shimba Ministries.

JINA LA ISA MAANA YAKE NINI?


Ndugu msomaji,
Mwezi huu nitaweka mada kadhaa zitakazo fundisha kuwa, Isa wa Quran na Yesu wa Biblia ni wawili na tofauti:
MAANA YA JINA ISA
Ni jambo la kawaida sana jina au majina kuwa na maana. Mfano majina haya ya kiarabu yana maana hizi: Muhammad, linamaanisha mwenye kushukuriwa, Abdalla ni Mtumwa wa Allah; Abu-Bakar maana yake ni Baba wa bikira; Abu Huraira ni baba wa Mapaka. Aidha majina ya Kiebrania nayo pie yana maana. Malaki ni mtumishi au Mjumbe wa Yehova, Isaya ni Wokovu wa Yehova; Ezekiel inamaanisha Mungu hutia nguvu, Daniel – Mungu ni hakimu wangu.
JINA LA ISA MAANA YAKE NINI?
Katika Qurani yenye jumla ya juzuu 30; Surah 114; aya 6236; maneno yenye kutamkia 76,440; herufi 322,373; jina Isa linatamkwa lisa au Aysi limetajwa mara 25. Isa pia ameitwa masihi mara 93. Lakini tunaposoma Qurani iliofarsiriwa/tafsiriwa na Imam Baidawi Vol 1 Ukurasa 160 ameeleza kuwa Isa jina la Kiarabu maana yake ni Wekundu unaozidiana na weupe "ZERUZERU". Hii ndio maana ya Jina la Isa wa Quran. Je, Yesu wa Biblia maana yake nini?
JINA LA YESU MAANA YAKE NINI?
JINA Yesu linatokana na lugha ya Kiebrania ‘Yehoshua’ katika lugha ya Kigiriki wanasema ‘lesous’ inatamka ‘Yesous’ yaani Yesu. Katika lugha ya Kiarabu wanasema ‘Yasu’, kwa kiingereza ni “Jesus” maana yake ‘Bwana anaokoa au Bwana ni Mwokozi’ Isaya 43:6, 10-11.
Katika Biblia ambayo ina jumla ya Sura 1189; aya 31,102; vitabu 66 – Agano la kale vitabu 39 na agano Jipya vitabu 27; Neno Mwokozi kwa Kiingereza wanasema ‘Saviour’ limetajwa mara 55. Ikumbukwe kwamba katika agano jiypa jina Yesu au Yehoshua (kwa Kiebrania) limetajwa mara 1275 katika aya zipatazo 1226.
Zingatia pia kuwa agano jipya lina jumla ya aya 7930 na Sura 260 hivyo hapa tunaona jina Yesu maana yake ni Mwokozi na jina Isa ni wekundu uliozidiana na weupe. Kwa kuwa maana ya haya majina tofauti bila shaka Isa sio Bwana Yesu.
Leo tumejifunza kwa kifupi tu kuwa, Jina la ISA lenye maana ya Wekundu unao zidiana na weupe ni TOFAUTI KABISA NA Jina la Yesu lenye maana ya MWOKOZI katika Biblia. Zaidi ya hapo, tafsir ya Jina la Yesu kwa Kiarabu ni Yasu na sio Isa kama ambavyo Waislam wanadai katika vitabu vyao.
Mungu awabariki sana na tuendele kujifunza Neno lake bila ya kuchoka.
Katika huduma Yake,
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 7, 2016

KWANINI ALLAH HAKUITAJA PALESTINA KWENYE QURAN?



1. Allah asema Israel ndio taifa la Mungu
2. Palestina yakatwa na haipo kwenye Quran
Ndugu wasomaji,
Huu ni Msiba kwa Waislam wanao pigia debe Wapalestina. Hivi kwanini Allah hakuitaja Palestina kwenye Quran yake? Lakini ameitaja Israel na Waisraeli?
ALLAH ANASEMA KWA WAYAHUDI:
Allah (s.w.t.) amesema: Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi iliyotakaswa ambayo Allah amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika.(5:21)
Katika aya hapo juu, Allah anawaita Waisrael kupitia Musa "WATU WANGU" zaidi ya hapo anawaambia kuwa Waende Israel kwenye ARDHI ILIYOTAKASWA. Ndugu msomaji, kwanini Allah anaiita ardhi ya Israel kuwa imetakaswa lakini hakuwai sema hivyo kwa Saudi Arabia/Makka?
Ardhi hii imebarikiwa kiroho na kirutba. Ni jambo hili ndilo lililowafanya watu na staarabu tofauti kuigombania. Agano la Kale inatuhadithia ya kuwa ardhi hii ilibubujika asali na maziwa.(Hesabu, 13:27) Na katika kitabu cha Hesabu Sura ya 13 inatueleza kuwa WAISRAEL walipo kuwa wakitoka Misri walipata humo matunda ya makudhumani, tini na zaituni ambayo yalikuwa makubwa na kila tunda kubebwa na watu wawili.
Swali lamsingi: KWANINI ALLAH HAKUITAJA PALESTINA KWENYE QURAN YAKE?
Waislam, Allah kasema kwa Waisrael kuwa, WAINGIE KATIKA ARDHI ILIYOTAKASWA, sasa, kwanini nyie mnataka Wapalestina ambao hata Allah hawajui, wavamie ardhi ya Israeli?
Waislam wana wivu mkubwa sana kwa Israel kwasababu Allah amesema kuwa Israel ni ardhi iliyotakasika na hakusema kuwa Uarabuni kumetakasika. Huu ni MSIBA kwa Waislam.
ALLAH ANASEMA:
SURAT AL BAQARA 40. Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyo kuneemesheni, na timizeni ahadi yangu, na Mimi nitatimiza ahadi yenu, na niogopeni Mimi tu.
Allah anaendelea kusema kuwa Israel wana neema ya Mwenyezi Mungu, lakini hatusomi Palestina ikitajwa hata sekunde moja.
ALLAH ANASEMA KUWA ISRAEL NI ZAIDI YA WAARABU WOTE
Surat Al Baqara 47. Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni zile neema zangu nilizo kuneemesheni, na nikakuteuweni kuliko wote wengineo.
Kama ulivyo soma hapo juu, Israel ina neema na ni zaidi ya wengine wote, pamoja na Palestina na Waarabu wote. Kumbe ndio maana Waarabu hawana ubavu kwa Israel.
Leo ningependa muelewe kuwa, Israel ni nchi iliyo barikiwa na hata Waarabu wafanye nini hawata weza kitu, hata Allah wao amekiri kuwa Waarabu wataendelea kufuata mkia kwa Israel mpaka Kiyama.
ALLAH KAWAPA ISRAEL KITABU, HUKUMU NA UNABII
Surat Al Jaathiya 16. Na hakika tuliwapa Wana wa Israili Kitabu na hukumu na Unabii, na tukawaruzuku vitu vizuri vizuri, na tukawafadhilisha kuliko walimwengu wote.
Kumbe Israel wamepewa Unabii, Kitabu na Hukumu. Hii ndio sababu Waraabu wanaendelea kusaliti amri kwa Israel.
Kwanini Allah hakuitaja Palestina kwenye Quran?
Mungu awabariki sana,
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Max Shimba Ministries

YESU KWA KIARABU NI YASU "YASUA" NA SIO ISA.



Ndugu msomaji
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika Kiarabu. Je, Isa ni jina la Yesu wa Biblia?
Jibu sahihi la kihistoria na la wataalam wa kutafsiri litatupa ukweli halisi wa Jina la Yesu na kwanini alipewa Jina hilo katika " sherehe ya kumtaja " (Luka 2:21). Jina ambalo aliitwa na Mama yake, Baba yake wa Kambo, Ndugu zake na jamaa wengine, majirani zake , marafiki zake na wanafunzi wake wakati wa maisha yake duniani. Hakuna kutokuelewana kuhusu ukweli kwamba jina la Yeshua halikuwa la Kiarabu bali la Kiyahudi na Yesu/Yeshua mwenyewe aliishi katika Israeli, na alizaliwa katika familia ya Wayahudi wacha Mungu.
Jina la Yesu bila ya shaka yeyote ile ni la Kiyahudi. (Maana yake ni “kweli”). Tafsir ya jina la Yeshua Kiebrania katika Kiingereza itakuwa ni Jesus. Jina la Yesu halikuchaguliwa kiholela na wazazi wake, lakini yeye alipata jina lake moja kwa moja kutoka kwa Mungu (Mathayo 1:21 , Luka 1:31) kwa sababu ya maana ya jina lake na nani alilileta, basi leo hii tunaelewa madhumuni ya Yesu kuzaliwa na kuja hapa duniani (Mathayo 1:21 ).
Katika utamaduni na jadi ya Kiarabu. Jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislam. Na hata leo, jina la Yasu linatumiwa na zaidi ya 99.99% ya Wakristo wote wa Kiarabu. Tembea katika kanisa lolote la Kiarabu huto sikia wanatumia jina la Isa, Sikiliza matangazo ya Wakristo wa Kiarabu katika Radio na Televisheni (za Kiarabu) huto sikiwa Mkristo anatumia jina la Isa, bali wanatumia jina la Yasu. Matangazo yote ya Kikristo katika Uarabu wanatumia jina la Yasu. Kamwe huto ona jina la Isa kama lilivyo kwenye Koran ya Waislamu.
Katika jadi ya Kiarabu na utoaji wa tafsiri wa jina, jina sahihi la Kiebrania (Yeshua) ni Yasu katika Kiarabu. Kila uchaguzi wa tafsiri ya jina la kigeni katika lugha tofauti ni uvumbuzi wa binadamu.
Kiisimu ipo wazi jinsi jina la Yeshua Kiebrania lilivyo tafsiriwa na kuwa Yesu Kiswahili na Jesus Kiingereza:
Yeshua '(Kiebrania) -> Ιησους (Kiyunani) -> Yesu (Kilatini) -> Jesus (Kiingereza) -> Yesu (Kiswahili).
Mpito muhimu ni kutoka Kiyahudi kwenda Kigiriki. Hatua hii ilifanyika miaka 200 kabla ya Yesu kuzaliwa. Watafsiri wa Septuaginta (LXX), classical Kigiriki tafsiri ya maandiko ya Kiyahudi, kutokaa Yeshua Kiebrania jina kama Ιησους katika Kigiriki. Injili ziliandikwa katika lugha ya Kigiriki ilitumia utamaduni huu wa kutafsir kwa muda mrefu.
Kwasababu Kiyahudi na Kiarabu ni lugha mbili za Kisemiti, na zina uhusiano wa karibu, kuna baadhi ya sheria maalumu ambayo sauti/maneno/maandishi ya Kiebrania yanahusiana na ambayo sauti/maneno katika Kiarabu. Hasa, Neno la Kiebrania Shin mara kwa mara linatumika kama Dhambi katika Kiarabu, kwa mfano neno la Kiyahudi la amani, shalom ni sambamba na neno “salam” la Kiarabu. Kulingana na sheria za lugha na mahusiano kati ya Kiyahudi na Kiarabu, Yasu 'ni sahihi kwa Kiarabu na kwa Kiebrania ni Yeshua:
Yeshua '= Yod + + Shin Waw +' Ain
Yasu '= + Ya + Sin Waw +' Ain
Tena, katika lugha sahihi, jina la Yasu ni Kiarabu sawa na Yeshua Kiebrania. Hivyo, katika utamaduni na jadi ya Kiarabu jina la Yasu ndilo sahihi na pekee kutokana na kiisimu. Mpito kutoka Yeshua kwa Yasu inafuata sheria ya kawaida ya mabadiliko fonetiki kutoka Kiyahudi na Kiarabu. Yasu ni jina la Kiarabu la Yesu. Kinyume chake, Yasu ndio jina lenye asili ya Yeshua.
Early Hebrew (long form): Yehoshua' = Yod + He + Shin + Waw + 'Ain
Later Hebrew (short form): Yeshua' = Yod + Shin + Waw + 'Ain
Arabic (Christian): Yasu' = Ya + Sin + Waw + 'Ain
Arabic (Muslim): 'Isa = 'Ain + Ya + Sin + Ya
“Ya” na “Waw” ni maneno dhaifu, katika lugha ya Kiarabu, hufundisha kwamba mtu anaweza kurejea katika maneno mengine kama kuchukua juu ya aina mbalimbali (declension, inflection). Hivyo, mtu anaweza kuona kwamba fomula ya Kiislamu 'Isa kimsingi ni ya bandia/kutungwa na binadamu (inversion) (pamoja na mabadiliko ya Waw ili Ya) kwa Mkristo wa Kiarabu jina la Yesu ni Yasu na si Isa kama ilivyo andikwa kwenye Koran ya Kiislamu.
Nategemea leo umejifunza tofauti iliyopo kati ya Jina la Yesu-Kiswahili, Yasu-Kiarabu na Yeshua-Kiebrani.
Jina la Yesu Libarikiwe Sana
Katika Huduma yake
Max Shimba
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

WAISLAM WENYE SIASA KALI WA BOKO HARAMU WAKAMATWA NDANI YA KANISA.



WATU sita kati ya 100 wanaoaminika kuwa ni memba wa kundi la kigaidi la Boko Haram waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Ulinzi la Nigeria wamekamatwa wakiwa wamejificha Kanisani huko Festac Jijini Lagos.
Zoezi hilo lilifanikiwa jana kutokana na ushirikiano wa raia wema wa maeneo ya karibu kutoa taarifa kwa jeshi hilo kuhusu kuwepo kwa watu waliyowatilia shaka wakiingia kwenye Kanisa hilo lililopo mjini Festac kwa lengo la kujificha ilihali muonekanao wao sio wa kusali.
Washukiwa hao waliripotiwa kutafutwa na jeshi hilo tangu wiki iliyopita baada ya kufanya shambulizi na kutokomea huko mjini Maiduguri Borno.
Watuhumiwa waliokamatwa jana wametamnbulika kwa majina ya Ali Ibrahim, Ahmed Abubakar, Kamsalem Goigoi, Adams Ibrahim, Mohammed Ibrahim na Ali Blam Babagana waliokuwa wakitoroka kutoka Borno walikotekeleza shambulio.

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration

The Angelic Guardianship in Psalm 91:11: A Scholarly and Inspirational Exploration By Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological Institute A...

TRENDING NOW