Sunday, September 10, 2017

KUMBE SHETANI ANAISHI MAKKA




Ndugu zanguni huu ni Msiba mwingine kwa ndugu zetu. Amini usi amini habari ndio hii na ukweli leo unaanikiwa hapa.
Inapo fika siku ya 10 ya Zhu Al-Hijjah , wana Hijaa huondoka kutoka Muzdalifah, huku wakiokota Mawe wakiwa njiani. Kufuatana na Sunna, katika siku hii ya kwanza (10), wanaruhusiwa kuokoka Mawe Saba tu. NAJUA UNASHANGAA, HAYA MAWE NI YA NINI NA WAISLAM WANAELEKEA WAPI. Endele kusoma huu mkasa.

Nyakati za kupiga mawe Shetani:
Siku ya An-Nahr – Sikukuu mosi, usipige mawe mpaka jua lichomoze:
((Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alipokuwa Muzdalifah aliwatanguliza Minaa watu dhaifu na wazee na wanawake, akawaambia: “Musirushe mawe mpaka jua litoke”)) [Imepokewa na At-Tirmidhiy]
Mwenye udhuru anaweza kuchelewesha mpaka kabla ya Magharibi, lakini ni vizuri kupiga mawe baada ya kutoka jua na kabla haijaingia Magharibi kwa asiyekuwa na udhuru. (Baadhi ya Maulamaa wanajuzisha kupiga mawe baada ya Magharibi kwa udhuru, lakini bora ujaribu kupiga kabla jua kuzama).
Wakati wa kurusha mawe kwa siku mbili zilizobaki au siku tatu kwa wale wasiotaka kuharakisha, ni baada ya Zawal (wakati wa adhuhuri pale jua linaposogea kidogo baada ya kuwa katikati).

WANAPO FIKA "MINA", NDIO KAZI YA KUMPIGA MAWE SHETANI INAANZA.
1. Mahujjaj, hutupa mawe 7 'Jamrat Al-Aqabah'. Mahujjaj humtupia mawe Shatani huko Urabuni "MIRA" AKA MAKKA. Ndugu wasomaji, kumbe Shetani yupo Makka. Kumbe Shetani ni jamaa yao na wanampiga mawe.
Huu ni Msiba mkubwa sna kwa Waislam wanao enda Hijja ili wampige Mawe Shetani.
2. Mahujaj hurudi tena Mina na kuanza kumpiga Mawe Shetani na kuka usiku huko katika siku ya 11 na siku ya 12.
Hivi, Shetani ana Mwili mpaka wampige Mawe? Hivi Allah hawezi kummaliza Shetani mapka atumie watu kumpiga Mawe? Hakika kuna Shaka sana kwenye hii dini ya Allah.

Mahujaj hufanya hii kazi ya kumpiga Mawe Shetani katika siku ya 11, 12, na 13, na hufanya hii kazi wakati w Usiku na sio Mchana. Hapo sasa ndio utafahamu kuwa Shetani ni sehemu ya hii dini.
Kuomba Du’aaNi vizuri kuelekea Qiblah na kuomba du’aa baada ya kumaliza kupiga kila Jamaraat isipokuwa Jamaraat la mwisho. Hadiyth iliyosimuliwa na Al-Bukhaariy na Imam Ahmad inasema:
((Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alikuwa akeshapiga kila Jamaraat kwa mawe saba akisimama na kuelekea Qiblah na kuomba du’aa, isipokuwa baada ya kulipiga Jamaraat la mwisho hakusimama.)) [Imepokewa na Al-Bukhaariy na Imam Ahmad]

Siku Ya Kuharakisha
Ikiwa unataka kubaki hapo kwa mda wa siku mbili tu, basi siku ya tarehe Kumi na mbili Dhul Hajj ambayo hujulikana kama ni "Yawmul isti’ijaal" - Siku ya Kuharakisha – unapiga mawe na kuondoka Minaa kabla ya jua kuzama, na ikiwa utakawia kuondoka ukawepo hapo baada ya juwa kuzama itakubidi ubaki hapo siku moja zaidi. Ni vizuri kubaki usiku wa tatu ikiwa huna cha kukushughulisha.

Twawaaful Wida’a
Unapotaka kurudi nchini kwako baada ya kumaliza shughuli za Hajj, unatufu Twawaaful wida’a, (Twawaafu ya kuaga) nayo ni kama ifuatavyo:
Unatufu Al-Ka’abah mara saba na kufanya kama ulivyofanya katika Twawaafu za mwanzo, lakini mara hii bila ya kufanya Sa’ay baina ya Swafaa na Marwah.
NDUGU ZANGUNI,
Hii dini si ya Mungu wala hakuna sehemu kwenye Taurat au Injir au Zaburi ambayo Mungu anawaamrisha Waisrael wamtupie Mawe Shetani. Ndio maana huwa nasema kila siku kuwa, Allah hawezi kuwa Mungu wa Ada, Mungu wa Musa, Mungu wa Ibrahim, nk. Allah anaonyesha sifa tofauti kabisa na za Mungu wa Biblia.
Hivi Mtu na akili zako unaokota Mawe na kuanza kumpiga Shetani? Hakika hawa wamepotea wanao Mpiga Mawe Shetani.
HEBU SOMA TENA HIVI VIOJA NA UCHAWI WA KIISLAMUkishamaliza Twawaafu ya Ifaadhwah unarudi Minaa na unabaki hapo usiku wa tarehe 11, 12 na 13 kwa wasiokuwa na haraka. Hizo zinaitwa siku za Tashriyq. Inatosha kama utabaki hapo usiku wa tarehe 11 na wa 12 tu. Katika siku 2 au 3 hizo unapiga mawe Jamaraat zote tatu kila siku kwa mpangilio ufuatao.
Anza kupiga Jamaraat la mbali na Makkah, (Jamaraat dogo) kisha la kati, kisha Kubwa (Jamarat al Aqaba). Kila moja piga kwa mawe saba huku ukisema: "Allaahu Akbar", kila unaporusha jiwe. Hii ni kwa siku tatu zilizobaki.
Jamani. Nawasihi Wakristo wote duniani kuwaombea hawa Waislam wanao panda ndege na kwenda Makka kumpiga Mawe Shetani. Hawa ni vipofu na viziwi. Wnaihitaji upendo wa Yesu.
WAISLAM:
1. Hivi kumpiga Mawe Shetani kunawasaidia nini?
2. Wapi tunasoma kuwa Abrham alimpiga Mawe shetani?
3. Mbona huu utamaduni wa kupiga Mawe Shetani upo kwenye Quran peke yake?
Nawakaribisha kwa Yesu Mungu Mkuu.

Max Shimba Ministries Org.

KWANINI YESU ALIINGIA KWENYE SINAGOGI SIKU YA JUMAMOSI “SABATO”?



Kabla sijaanza kuelezea kwanini Yesu aliingia Sinagogi, ni vyema tukafahamu angalau kiufupi maana ya Sinagogi.

Sinagogi ni nyumba ya dini na ya jamii ya Wayahudi inayotumika hasa kusali. Jina hili Sinagogi linatokana na neno la Kigiriki συναγωγή sinagoge, likimaanisha "mkutano"; ni tafsiri ya neno la Kiebrania בית כנסת beit knesset, yaani "nyumba ya mkutano".

Wayahudi hutumia pia neno la Kiyiddish "shul" (=shule) kutajia sinagogi.
Sasa basi, baada ya kulewa maana ya Sinagogi, huto shangaa kuwa Wayahudi ndio watumiaji wa hayo Masinagogi na waliingia siku ya Saba “Sabato” kusali au kusoma “Shule” kama ambavyo neno hili hutamkwa katika Kiyiddish.

Hivyo, basi, haikuwa jambo la ajabu au kustaabisha tunapo soma kuwa Bwana Yesu aliingia ndani ya Masinagogi ili awafundishe Wayahudi kuhusu Ufalme wa Mbinguni. "Luka 4:16. alipokwenda Hapo Alipozaliwa Nazaret alipozaliwa na Siku ya Sabato(jumamosi) alikwenda katk#Sinagogi kama Ilivyokuwa Desturi Yake. Akasimama ili asome 17. akapewa kitabu cha nabii isaya akafunua mahali palipo andikwa "#Roho_wa_Bwana yuu Juu Yangu. Amenipaka mafuta Kuhubiriia maskini Habari njema "

Basi Wasabato wanapo soma hiyo aya teyari wanasema kuwa Yesu aliitunza Sabato kwasababu aliingia Sinagogi siku ya Saba ya Juma = Jumamosi. Haya madai hayana nguvu yeyote ile bali ni madai dhaifu. Kuingia Sinagogi siku ya Jumamosi hakukufanyi na au hakumfanyi mtu kuwa Msabato.

HILI DAI LA KUINGIA SINAGOGI naweza kulifananisha na dai la Waislam kuwa, eti, Yesu aliingia Sinagogi na hivyo Yesu ni Muislam. Waislam wao wana hoja ya kuwa Sinagogi ni Msikiti, basi ukiingia kwenye Sinagogi basi wewe ni Muislam HUKU WASABATO wana hoja ya kuwa Yesu kaingia SINAGOGI SIKU YA JUMAMOSI, basi Yesu ni Msabato. HOJA ZOTE MBILI ZA WAISLAM NA WASABATO NI DHAIFU.
Wakristo wa mwanzo hawakutumia Sinagogi katika ibada zao ndio maana Bwana wetu Yesu Kristo alisema hivi: Kwa mfano, baada ya kumtakasa mtu yule aliyejaa ukoma, Yesu alimwambia, “Asimwambie mtu, ila, Nenda ukajionyeshe kwa kuhani; ukatoe kwa ajili ya kutakasika kwako kama Musa alivyoamuru, iwe ushuhuda kwao.” (Luka 5:14). Haya maneno yanaashiria kuwa Yesu alipo fanya huu muujiza hakuwa kwenye Sinagogi na ndio maana alimwambia Nenda ukajionyeshe kwa kuhani; ukatoe kwa ajili ya kutakasika kwako kama Musa alivyoamuru, iwe ushuhuda kwao.” (Luka 5:14).

Hiki ni kipindi ambacho ni cha kiimani zaidi. Kimsingi hiki ni kipindi ambacho kinaendelea hadi sasa. Huu ni wakati wa kupumzika kazi za mwili za uovu, yaani kuacha dhambi na kuishi kwa kumtegemea Kristo. Ni maisha ya imani.

Imeandikwa: Njoni kwangu ninyi nyote wenye kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha. (Matayo 11.28), yaani, nitawapa ‘sabato’. Pia ndiyo maana ya andiko lisemalo: Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato. (Matayo 12:8). Sabato iko kwake, si kwenye siku.

Ni maisha ya kujiachia mikononi mwa Mungu ambaye yeye ndiye anayeshughulikia kila kitu katika maisha yetu. Kazi yetu ni kuamini tu kuwa atafanya; naye hakika anafanya. Hilo ndilo pumziko! Hiyo ndiyo raha! Hiyo ndiyo starehe! Hiyo ndiyo Sabato!

Shalom
Dr. Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na mwokozi wetu.

ROHO MTAKATIFU HUTUOMBEA

Image may contain: cloud, sky, text, outdoor and nature
Warumi 8:26-27 Bibilia Takatifu (SNT)=12pt26 Hali kadhalika Roho hutusaidia katika udhaifu wetu. Kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioelezeka kwa maneno. 27 Na Mungu ambaye ana chunguza mioyo yetu anafahamu mawazo ya Roho kwa maana Roho huwaombea watakatifu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
Katika aya hapo juu, tumesoma kuwa, Roho Mtakatifu anatuombea na kutusaidia katika udhaifu wetu. Hii sifa ya upendo usio na kipimo ni ya Mungu peke yake. Zaidi ya hapo, tunasoma kuwa, Mungu anachunguza mioyo yetu kwa kupitia Roho Mtakatifu. Kumbe basi, Roho Mtakatifu anafahamu mapenzi ya Mungu kwako.
Hii sifa ya Roho Mtakatifu kuwa na uwezo wa kufahamu nini Mungu anawaza inamfanya Roho Mtakatifu na yeye awe Mungu. Hakuna mwenye uwezo wa kufahamu mawazo ya Mungu, isipokuwa Mungu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

NAKALA ZA QURANI ZATUPWA KATIKA MTARO WA MAJI TAKA

Image may contain: outdoor
Nakala takribani 500 za kitabu kitukufu cha Qurani القرآن الكريم zimegunduliwa katika mtaro wa maji taka katika mji wa Taif, nchini Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa Afisa wa kamati ya kukuza na kufadhili mambo ya Qurani alisema tukio hilo liliripotiwa na mwanafunzi ambaye aliona msahafu katika mtaro wakati anaelekea nyumbani kwao maeneo ya Al-salama ambayo ni moja ya wilaya ya mkoa wa Taif.
Kampuni ya kuhudumia mifereji ya maji ilifungua na kukuta nakala zipatazo 500 za Qurani. Hii si mara ya kwanza kwa Quran Mtakatifu kukutwa imeharibiwa katika Saudi Arabia.
Mapema mwaka huu, Afisa wa gerezani la mkoa wa Al-Haer alitusi Qurani kiasi cha kupelekea maandamano katika sehemu mbalimbali za Saudi Arabia.
Kunajisiwa kwa Quran katika nchi ya Saudi Arabia ambayo ni jicho la Uislamu kumeibua hisia hasi katika ulimwengu wa Kiislamu.

MUHAMMAD ANAKIRI KUWA YEYE NI MTUME BANDIA NA HAKUFANYA MIUJIZA

Image may contain: 1 person, text
QURAN INASEMA KUWA, NABII LAZIMA AFANYE MIUJIZA;
MUHAMMAD ANAKIRI KUWA YEYE NI MTUME BANDIA NA HAKUFANYA MIUJIZA
Qur’an nayo inathibitisha kuwa manabii na mitume ni lazima wafanye miujiza.
Qurani 40:78 Suratul Al-Muumini [Waumini] inasomeka “Na kwa yakini tumewatuma mitume kabla yako wengime katika wao tumekusimulia (majina yao na habari zao) na wengine hatukukusimulia na haikuwa kwa mtume yoyote kuleta muujiza wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu”
Muhammad hakuwai fanya muujiza wowote ule ili kuthibitisha madai ya unabii na utume wake.
Qur’an 29:50 Suratul Al-Ankabuut (Buibui). “Na walisema “Mbona hakuteremshiwa miujiza kutoka kwa Mola wake? Sema miujiza iko kwa Mwenyezi Mungu tu (akitaka atakuteremshieni na kama hataki basi),nami hakika ni mwonyaji mbainishaji (dhahiri tu).” (Taz. Qur,an 6:35-37 13:7,)
Muhammad anakiri kuwa yeye hakuwai fanya miujiza. Hivyo Kutokana na Quran yao wenyewe Muhammad ni mtume bandia.
Zaidi ya hapo Muhammad hakuwai fanya unabii wowote ule. Sasa Nabii bila ya unabii inawezekanaje?
Sifa mojawapo ya Nabii ni kutoa unabii. Muhammad hakuwai toa unabii wowote ule.
KUROGWA KWAKE MUHAMMAD
Zaidi ya hayo tunaona Muhammad alirogwa. Kurogwa ni hali ya mtu kuathirika na nguvu za giza yaani uchawi. Je nabii au mtume wa Mwenyezi Mungu wa Kweli anaweza kurogwa?
Amesema Mwanaisha Mkewe Mtume kuwa "Yahudi Mmoja aitwaye Labiid bin Al'answan alimroga Mtume Muhammad, ikawa Mtume baadhi ya Nyakati huchanganyikiwa na kuanza kuita Ovyo ovyo na kupiga makelele. (Sahih Muslim J. 4 uk. 38-39)
Huu ni uthibitisho mwingine mzito unaoonesha kuwa utume wa Muhammad una utata.
MASWALI:
(a) Hivi, kuna Mtume au Nabii yeyote yule ambaye alikiri kurogwa kama Muhammad?
(b) Hivi Allah alikuwa wapi wakati Muhammad anarogwa? [Ingawa Quran inakiri kuwa aliye teremsha uchawi/urogi ni Allah]
(c) Wapi tunasoma kuwa Muhammad aliombewa na kutoa huo uchawi/urogi aliofanyiwa na Labiid bin Al'answan?
YAANI INA MAANA MUNGU ALIKOSA MTU WA KUTUMA MPAKA ATUME MTU ALIYECHEZEWA NA MASHETANI KAMA HUYU?
Ndugu msomaji,
Muhammad hakuwa Mtume wa Mungu na wala hana sifa za KITUME.
1. Muhammad hakuwai ongea na Allah aliye mtuma.
2. Muhammad alikuwa na Shetani tokea kuzaliwa kwake.
3. Muhammad alikiri kuchezewa na Shetani wakati wa kusimikwa utume wake Pangoni.
4. Muhammad alikiri kuwa Shetani amechezea akili na nafsi yake.
5. Muhammad alikiri kuwa alirogwa na Labiid bin Al'answan.
SASA WAISLAM, NIONYESHENI, wapi kwenye Taurat, au Zaburi au Injili kama kuna Mtume aliye na sifa za ajabu kama za Muhammad.
Karibuni kwa Yesu ambaye ndie Njia Pekee ya Kwenda Mbinguni.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na mwokozi wetu.
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

ROHO MTAKATIFU HUFANYA MAAMUZI YAKE

Image may contain: one or more people and text


Roho mtakatifu hufanya maamuzi kutokana na mapenzi yake mwenyewe (Wakorintho wa kwanza 12:7-11). 1 Wakorintho 12:7-11 Neno: Bibilia Takatifu (SNT) Roho Mtakatifu hudhi hirishwa kwa kila mtu kwa faida ya wote. 8 Maana mtu mmoja hupewa neno la hekima na huyo Roho, na mwingine hupewa neno la ufahamu kutoka kwa Roho huyo huyo. 9 Mtu mwingine hupewa imani na huyo Roho na mwingine karama za kuponya. 10 Huyo huyo Roho humpa mwingine uwezo wa kufanya miujiza, mwin gine unabii, mwingine uwezo wa kutofautisha kati ya roho mbalim bali, mwingine aina za lugha na mwingine uwezo wa kutafsiri lugha. 11 Lakini ni Roho huyo huyo mmoja anayefanya haya yote, naye hugawa karama kwa kila mtu, kama yeye mwenyewe apendavyo.
Katika Wakorintho wa kwanza hapo juu, tumesoma kuwa, Roho Mtakatifu ndie anaye toa zawadi/karama ya hekima, ufahamu, imani, kuponya, miujiza, unabii, nk. Hii sifa ya kutoa hizi Karama ni ya Mungu, lakini hapa kwenye Wakorintho tumesoma na kugundua kuwa, Kumbe Roho Mtakatifu ndie anaye toa hizi karama za Mungu. Hivyo basi, kwa kuwa Roho Mtakatifu ndie anaye toa hizi karama za Mungu, hufanya hivyo kwa kuwa yeye ni Mungu na hizo karama ni zake.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

ANGOLA YAPIGA MARUFUKU UISLAMU NA KUVUNJA MISIKITI

Image may contain: sky and outdoor
Angola imekuwa nchi ya kwanza duniani kupiga marufuku Uislamu na Waislamu, na kuchukua hatua za kwanza kwa kuvunja misikiti katika nchi hiyo.
"Mchakato wa kuhalalisha Uislamu haijawahi kupitishwa na Wizara ya Sheria na Haki za Binadamu , misikiti yao itafungwa hadi taarifa zaidi zitakapotolewa, alinukuliwa Waziri wa Utamaduni wa Angola Rosa Cruz e Silva, na 
Agence Ecofin.
Alisema kuwa uamuzi huo ni mfululizo wa jitihada za kupiga marufuku madhehebu 'haramu' ya dini ya kiislamu. Kwa mujibu wa Waziri, hatua hiyo ilikuwa ni muhimu kwa kupambana bila kuchoka dhidi ya kuibuka kwa misikiti na ni kinyume na desturi za utamaduni wa Angola.
"Madhehebu yote ambayo orodha yao imechapishwa na Wizara ya Sheria na Haki za Binadamu katika gazeti Angola la 'Jornal de Angola' ni marufuku kufanya ibada, hivyo wanapaswa kufunga milango ya majengo yao", alisema.
Gavana wa mkoa wa Luanda, Bento Bento, amesema Kwamba, "Waislamu wenye msimamo mkali si kuwakaribisha katika Angola na serikali ya Angola haipo tayari kuhalalisha kuwepo misikiti".
Mwaka jana Mwezi Oktoba, waislamu wa manispaa ya mjini ya Viana, Luanda, walishuhudia kuvunjwa kwa msikiti wao katika kuondoa athari zozote za kuwepo uislamu nchini humo.
Idadi ya waislamu nchini Angola inatajwa kufikia 90,000 na masikiti 80 ambayo yote itavunjwa.

WASABATO WANAPINGA AGIZO LA MUNGU LA KUFANYA IBADA SIKU YA JUMAPILI

No automatic alt text available.
Katika agizo la kukusanyika kwa wana wa Israeli, Mungu alitoa siku mbili yaani Jumapili na Jumamosi, ingawa wasabato karibu wote hawalijui jambo hili, maana hao wamekaririshwa siku ya sabato tu yaani Jumamosi.
UTHIBITISHO:
Tunaweza kuthibitisha ukweli huu katika kitabu cha Kutoka 12:16 Biblia inasema, “SIKU YA KWANZA kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na SIKU YA SABA kutakuwa na kusanyiko takatifu, haitafanywa kazi yoyote katika SIKU HIZO, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.”
Mungu aliwaamuru wana wa Israeli wakusanyike siku ya kwanza ya juma yaani Jumapili na siku ya saba yaani Jumamosi kwa kalenda ya kwetu. Pia Mungu hakuwaagiza kukusanyika tu, bali aliwaagiza wasifanye kazi pia. Lakini wanaojiita wasabato nyakati za leo, wanapinga kukusanyika Jumapili sawasawa na maagizo ya torati wanayodai kuifuata.
1. Swali ni kwamba, mafundisho yao ya kukusanyika siku ya sabato yametoka wapi?
2. Kama ni kwenye Biblia mbona siku moja hii wameiacha?
3. Je aliyetoa agizo la siku ya sabato ni Mungu mwingine na aliyetoa agizo katika kitabu cha Kutoka 12:16 (yaani kukusanyka siku ya Jumapili) ni Mungu mwingine?
Mtume Paulo anafundisha kuwa ni jambo la udanganyifu kuwafundisha watu washike siku ya Sabato. Kwa sababu ya wokovu wetu ndani ya Kristo (Wakolosai 2:11-15) Paulo anasema, “Basi, MTU ASIWAHUKUMU ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.” (mstari wa 16).
Kwa hiyo agizo la kukusanyika lilikuwa ni siku mbili, imetajwa ya kwanza ni Jumapili (siku ya kwanza ya juma) na ya pili ni Jumamosi (siku ya saba) kwa kalenda yetu, kama tulivyoona katika kitabu cha Kutoka 12:16. Sasa tukija kwenye agizo la kushika sabato halikuwa ni siku ya kukusanayika, bali ni pumziko la kazi tu na kustarehe kama tunavyoweza kuona katika kitabu cha Kutoka 31:14-15, “Basi mtaishika hiyo sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana, kila mtu atakayefanya kazi yoyote katika siku ya sabato, hakika yake atauawa.”
Mungu hapa anasema kila mtu atakayefanya kazi siku hiyo atauawa, hajasema kila mtu atakaye kosa kwenda kwenye kusanyiko atauawa. Na ndiyo maana kwenye Biblia, inapotaja neno sabato ina maana ya kupumzika kazi na siyo kufanya kusanyiko la kuabudu kama wafanyavyo wanaojiita wasabato wa leo.
Pia Kutoka 35:2 Biblia inasema, “Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni sabato ya kustarehe kabisa kwa Bwana; mtu awaye yote atakayefanya kazi yoyote katika siku hiyo atauawa.”
Tunaona tena hapa, Mungu anasisitiza kwamba, atakayeuawa, ni yule atakayefanya kazi siku ya sabato, na hakusema atakayekosa kwenda kukusanyika kwa ajili ya ibada, kwani agizo hili lilihusiana na kupumzika kufanya tu. Kimsingi unaposema sabato, siyo dhehebu, wala siyo siku ya kuabudu, bali ni pumziko la kazi. Nyakati za leo, wanaojiita wasabato, wanachanganya siku ya kusanyiko na siku ya pumziko la kazi.
Paulo alihuzunishwa sana, kwa sababu anasema wazi hivi “…..sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini KUYAREJEA TENA MAFUNDISHO YA KWANZA yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? MNASHIKA SIKU, na miezi, na nyakati, na miaka.”(Wagalatia 4:9,10).
“Maana yale YASIYOWEZEKANA kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa DHAIFU kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma “YESU KRISTO” Mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili; ILI HAKI YA TORATI YATIMIZWE NDANI YETU sisi, tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali mambo ya roho.” (Warumi 8:3,4).
Kwa hiyo, mtume Paulo anasisitiza, “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO.”
Tukiangalia tena maandiko katika kitabu cha Kumbukumbu la torati 5:14 kwenye ile amri ya nne ya kushika sabato, Biblia inasema, “Lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng’ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako yeyote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile vile kama wewe.”
Kadhalika na hapa Mungu anaifafanua kwa uzuri kabisa, maana ya sabato na lengo lake. Lengo lilikuwa watu wapumzike, wanyama wapumzike, wafanyakazi wapumzike na kustarehe, kwa sababu hiyo, sabato iliwagusa mpaka wanyama. Kama ingekuwa kwamba sabato ilimaanisha siku ya kuabudu basi wanyama wasingetajwa kupumzika.
Mtu aliyepigwa mawe hata kufa nyakati za Musa jangwani, hakuuawa kwa sababu hakwenda kuabudu siku ya sabato, bali aliuawa kwa sababu alifanya kazi (Hesabu 15:32-36). Hii inathibitisha kwamba agizo la kushika sabato lililenga pumziko la kazi tu na si agizo la kukusanyika kama wanavyodai wasabato wa leo. Wana wa Israeli walikusanyika siku ya saba (Jumamosi) na siku ya kwanza ya juma (Jumapili) kwa agizo la Mungu mwenyewe katika Kutoka 12:16, kama tulivyokwisha kuona hapo nyuma. Kimsingi ni kwamba, katika amri kumi (Kumbukumbu 5:12-15), amri ya nne inazungumzia kupumzika kazi tu. Na Kutoka 12:16 Mungu anatoa mwongozo wa siku za kukusanyika kwa ibada. Swali ni kwamba, wasabato wa leo wanakusanyika Jumamosi kwa msingi wa andiko lipi kati ya hayo? Kama kwa msingi wa amri ya nne ya kushika sabato (Kumbukumbu 5:12-15), basi watakuwa wamepotea, maana pale haikuzungumziwa siku ya kukusanyika kwa ajili ya ibada, bali ni pumziko la kazi tu. Lakini kama wana kusanyika Jumamosi, kwa msingi wa andiko la Kutoka 12:16, kadhalika watakuwa wamepotea, maana, katika siku za kukusanyika, katika andiko hili, Mungu ametoa siku mbili yaani siku ya kwanza ya juma (Jumapili) na siku ya saba ya juma (Jumamosi), sasa mbona siku ya kwanza ya Juma (Jumapili) wanaipinga? Ni wazi kabisa wanampinga Mungu.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na mwokozi wetu.

ROHO MTAKATIFU ANAFAHAMU MAMBO YOTE

Image may contain: one or more people, cloud, sky, text and outdoor


Kama ambavyo Mungu anafahamu mambo yote na anaweza yote, vivyohivyo Roho mtakatifu ni Mungu na anauwezo wa huohuo wa kufahamu yote. Kama Mungu, Roho mtakatifu anaweza kufanya kazi ya msaidizi na mshauri kama vile Yesu Kristo aliyevyoahidi kuwa atakuja kufanya (Yohana 14:16,26; 15:26). Yohana 14:26 Neno: Bibilia Takatifu (SNT) 26 Lakini yule Msaidizi, yaani Roho Mtakatifu, ambaye Baba yangu atamtuma kwenu kwa jina langu, atawafundisha mambo yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Katika Yohana hapo juu, tunajifunza kuwa, Roho Mtakatifu yupo nasi kila siku na anaishi ndani yetu. Huu uwezo wa kuishi ndani yetu na kuwa kila mahali, na kufahamu yote ambayo Yesu aliyo tuambia na kutukumbusha, huu uwezo ni wa Mungu na unamfanya Roho Mtakatifu kuwa Mungu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

UONGO WA MTUME MUHAMMAD NA QURAN KUHUSU KUPASUKA KWA MWEZI NA KUTEMBEA KWA JUA

Image may contain: sky, text, nature and outdoor
1. Mtume Muhammad adai kuwa alipasua Mwezi
2. Hakuna Ushahid wa wapi vilipo vipande hivyo vya Mwezi
3. Muhammad adai kuwa Jua linatembea.
Ndugu wasomaji, leo naanza kwa kusema, hakika Msingi wa Uislam ni uongo na shaka ambazo hazina Ushahid.
Ungana nami moja kwa moja na tuone huo uongo upo wapi katika dini hii ya Jibril ibn Allah.
KUPASUKA KWA MWEZI:
"Hitaji la wapagani kwa Nabii kuwa awaonyeshe miujiza. Nabii aliwaonyesha kupasuka kwa mwezi. ‘Abdullah bin Massud alisimulia: Wakati wa maisha ya Nabii mwezi ulipasuliwa vipande viwili na Nabii alisema kuhusiana na hilo, ‘Shuhudia (jambo hili).’" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 sura ya 26 na juzuu ya 4 kitabu cha 56 sura ya 26 na.830, uk.533.
"Anas alisimulia kwamba watu wa Makka walimwomba Mtume wa Allah awaonyeshe muujiza, na kwa ajili hiyo aliwaonyesha mwezi unaopasuka." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 sura ya 26 na.831, uk.533.
"Ibn ‘Abbas alisimulia: Mwezi ulipasuliwa vipande viwili wakti wa uhai wa Nabii." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 sura ya 26 na.832, uk.534.
Mwezi unaopasuka. Bukhari juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 225 na.290, uk.273 na rejeo la 1 chini ya uk.273; juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 287 na.387-391, uk.365-366; juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 261 na.345, 349, uk.331; Bukhari juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 265 na.368-370, uk.331, 336.
Kuupasua mwezi Sahih Muslim juzuu ya 4 kitabu cha 37 na.6721, 6724-6730, uk.1467-1468.
Sura 54:1 inasema, "Saa (ya hukumu) imekaribia, na mwezi ulipasuliwa vipande viwili. (toleo lililorekebishwa la Yusuf ‘Ali).
Tambua kuwa kupasuliwa vipande viwili kunamaanisha kuwa mwezi uligawanywa nusu kwa nusu, na kitenzi kilichotumika hapa ni cha wakati uliopita. Hatuna kumbukumbu za watu wengine wowote ulimwenguni, ikiwa ni pamoja na jirani zao wa Misri, Syria, au Uajemi ambao waliuona mwezi uliopasuliwa vipande viwili. Kurani na hadithi hazisemi ni jinsi gani mwezi uliweza kurudi kuwa kitu kimoja tena.
Vile vile Imaam Ahmad amerekodi kuwa Jubayr bin Mutw'im alisema: "Mwezi ulipasuka vipande viwili wakati wa Mjumbe wa Allah na sehemu ya mwezi ulikuwa juu ya mlima na sehemu nyingine kwenye mlima mwingine. Wakasema (makafiri) "Muhammad ametufanyia uchawi". Kisha wakasema: "Angeliweza kututeka kwa uchawi asingeliweza kufanya kwa watu wote" [Imaam Ahmad]
Usimulizi wa 'Abdullaah bin 'Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma):
Ibn 'Abbaas alisema: "Mwezi ulipasuka wakati wa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Ibn Jariyr alirekodi kwamba Ibn 'Abbaas alisema kuhusu kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
((اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَر))ُ (( وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ ))
((Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!))
((Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea)) [Al-Qamar:1-2]
MASWALI:
1. Vipo wapi hivyo vipande viwili vya Mwezi ambao Waislam wanadai Muhammad aliupasua?
2. Upo wapi ushahid wa Kihistoria au Kisayansi ambao unasaidia madai ya kupasuliwa kwa Mwezi na Muhammad?
Hatuna kumbukumbu za watu wengine wowote ulimwenguni, ikiwa ni pamoja na jirani zao wa Misri, Syria, au Uajemi ambao waliuona mwezi uliopasuliwa vipande viwili. Kurani na hadithi hazisemi ni jinsi gani mwezi uliweza kurudi kuwa kitu kimoja tena.
MUHAMMADA ANADAI KUWA JUA LINATEMBEA NA LINASUJUDI KWA KITI CHA ENZI CHA ALLAH
"Abu Dhar alisimulia: Nabii aliniuliza wakati wa machweo ya jua, ‘Unafahamu mahali ambako jua linakwenda (wakati wa kuchwa)?’ Nilijibu, ‘Allah na Mtume wake wanafahamu vizuri zaidi.’ Alisema, ‘Linakwenda (yaani linasafiri) hadi linasujudu chini ya kiti cha enzi, na linapata kibali cha kusimama tena, na linaruhusiwa na kisha (muda utakuja ambapo) litakuwa linakaribia kusujudu lakini kusujudu kwake hakutakubaliwa …’" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 4 na.441 uk.283.
al-Tabari juzuu ya 1 uk.231 inasema, "Nilimuuliza Mjumbe wa Mungu [Muhammad] ‘[Jua] linazama wapi?’ Alinijibu: ‘Linazama mbinguni na kisha linachomoza kutoka mbingu kwenda mbingu nyingine hadi linachomoza kwenye mbingu ya juu zaidi, mbingu ya saba. Hatimaye, linapokuwa chini ya kiti cha enzi, linaanguka chini na kusujudu, na malaika wanaolisimamia wanasujudu pamoja nalo. Kisha jua linasema, Bwana wangu, ni wapi unakoniamuru nichomozee, ni upande ule nilikozamia au nilikochomozea?’ Aliendelea. Jambo hili ndilo (linalokusudiwa na) neno la Mungu: ‘Na jua: Hukimbilia mahali linapotakiwa kuwepo (usiku)’ linaposhikiliwa chini ya kiti cha enzi – ‘Jambo hilo limeamriwa na Yeye Mwenye Nguvu na Mwenye Kujua’ Bwana kwa mamlaka yake ya kifalme, Bwana ambaye ‘anavijua’ viumbe vyake. Aliendelea, Gabriel alileta kwenye jua vazi lenye kung’aa tokana na mwanga utokao kwenye kiti cha enzi, kwa kufuata vipimo vya saa na siku. Ni refu zaidi wakati wa majira ya joto na fupi zaidi wakati wa majira ya baridi, na lenye urefu wa wastani wakati wa majira ya kupukutisha majani na wakati wa majira ya kuchipua majani. [Mitindo ya majira ya kuchipua majani, kupukutisha majani na majira ya baridi!] Aliendelea. Jua huvaa vazi hio, kama mmoja wenu anavyovaa zavi lake. Kisha, huwa huru kuzunguka kwenye anga la mbinguni mpaka linapochomoza kutokea upande linaochomozea. … Njia hiyo hiyo hufuatwa na mwezi wakati wa kuchomoza kwake … Lakini Gabriel huuletea vazi kutoka kwenye mwanga wa miguunil. Hivi ndivyo neno la Mungu (linavyomaanisha) ‘Amelifanya jua kuwa angavu na mwezi kuwa mwanga.’"
HUYU MUHAMMAD wanaye dai kuwa alipasua Mwezi, anaendelea kusema uongo kuwa eti Jua linazunguka na kufika kwa Allah ili kusujudu?
MASWALI:
1. Kama Muhammad alishindwa kujua historia rahisi ya Jua, kwanini tumwanini kuwa alipasua Mwezi?
2. Kama Muhammad anadai kuwa Jua n Mwezi vinatembea, kwanini tumwanini kuwa alipasua Mwezi?
MUHAMMAD ANAENDELEA KUSEMA UONGO NA KUZIDISHA SHAKA KWENYE QURAN
SASA MUHAMMAD ANASEMA KUWA JUA LINAZAMA KWENYE CHEMCHEM YA MATOPE
Dhu al-Qarnaiyn [Zul Qarnain] "alishuhudia kuzama kwa jua kwenye sehemu yake ya kupumzikia kwenye bwawa lenye ute mweusi na wenye harufu mbaya sana." al-Tabari juzuu ya 5 uk.173-174 (Tazama Sura 18:82-97).
al-Tabari juzuu ya 1 uk.234 pia inasema kuwa jua huzama kwenye chemchemi yenye matope. Msemo "yenye matope" ni hami’ah, unaomaanisha udongo mweusi wa mfinyanzi, lakini hamiyah ni neno lenye kufanana nalo linaloweza kumaanisha kitu cha moto. (Tazama rejeo la 442 chini ya uk.234).
Ndugu zanguni, hii dini ni Msiba ambao hauta isha mpaka kihama.
Sasa Muhammad aliye dai kuwa alipasua MWEZI na kushindwa tuonyesha wapi vilipo vipande vya Mwezi alio upasua, anasema kuwa ETI Jua linazama kwenye tope. Huu kama si msiba ni nini?
MUHAMMAD ANAENDELEA KUWEZA SHAKA KATIKA IMANI YAKE:
MUHAMMAD ANASEMA KUWA ETI JUA LINAPOROMOKA TOKA KITI CHA ENZI MPAKA KWENYE BAHARI.
" [Muhammad] Aliendelea. Wakati jua linachomoza, linainuka juu ya kibandawazi (kinachokokotwa na farasi) toka kwenye moja ya chemchemi hizo likiwa pamoja na malaika 360 …. Wakati Mungu anataka kuvijaribu jua na mwezi, ili kuwaonyesha watumishi wake ishara na kwa njia hiyo kuwataka waache kutokumtii Yeye na kuanza kutii, jua huporomoka ghafla toka kwenye kibandawazi na kuanguka kwenye kina cha bahari, ambacho ni cha mduara. Wakati Mungu anataka kuongeza umuhimu wa ishara kuwatisha zaidi watumishi wake, jua lote hunguka, na hapawi na sehemu yake yoyote inayobaki kwenye kibandawazi. Huko ndiko kupatwa kukamilifu kwa jua, wakati ambapo mchana hujiwa na giza na nyota hutokeza." al-Tabari juzuu ya1 uk.236.
JAMANI, hivi hawa ndugu zetu, wanafanya nini Shule? Mbona madai ya Muhammad na Allah wao yamejaa shaka na ni DHAIF DHAIF DHAIF? Hakika Uislam ni uongo na ni didi ya warongo.
MUHAMMAD NA ALLAH SASA WADAI KUWA:
1. NYOTA ni Makombora ya kumpiga Shetani
2. VIMONDO ni silaha za kuwapiga Mashetani
"Mbingu za chini kabisa zina taa [nyota], na ‘Tumeziumba (taa) hizi kama makombora ya kuwafukuzia waovu, na tumetayarisha Adhabu ya Moto Uwakao kwa ajili yao.’" Sura 67:5.
"Kuumbwa kwa nyota hizi kuna madhumuni matatu, yaani, kulipamba anga, makombora ya kuyapiga mashetani,na alama za kuwaongoza wasafiri. Kwa hiyo kama mtu yoyote anajaribu kupata tafsiri nyingine amekosea na anapoteza nguvu zake tu..." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 3 kabla na.421, uk.282.
Wakati mwingine vimondo hurushwa kwa mashetani ambao wanajaribu kusikiliza siri za mbinguni. Sahih Muslim juzuu ya 1 kitabu cha 4 na.902 na rejeo la 674 chini ya uk.243.
Vimondo vinapaswa kuwapiga malaika [wabaya] kabla hawajaeneza mambo walyoyasikia. Wakati mwingine malaika wabaya huwaambia watabiri kabla ya kuwapiga. Ibn-i-Majah juzuu ya 1 kitabu cha 1 na.194, uk.110.
Vimondo huyashambulia majini (genies) Sahih Muslim juzuu ya 4 kitabu cha 24 na.5538, uk.1210.
Nyota hulinda dhidi ya shetani. al-Tabari juzuu ya 1, uk.223.
Ndugu wasoamji leo nimeonelea kuwa, ni vyma tuendelee kumuumbua Allah na Muhammad maana wao wamejama shana na uongo kwenye dini yao.
Mungu awabariki sana.
Katika Huduma yake,
Max Shimba Mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na mwokozi wetu.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

TRENDING NOW