Sunday, April 1, 2018

JE, MUNGU ANAKUBALI NDOA YA WAKE WENGI?

Image may contain: 3 people
Jibu rahisi na la haraka ni hili: Hapana hakubali; Mungu alipoanzisha ndoa ya kwanza katika Edeni aliweka kiwango cha kuoa mke mmoja. Baadaye Yesu Kristo alithibitisha kwamba wafuasi wake walipaswa kufuata kiwango hicho.—Mwanzo 2:18-24; Mathayo 19:4-6.
Lakini je, si ni kweli kwamba wanaume walioishi kabla ya nyakati za Ukristo kama vile Abrahamu, Yakobo, Daudi, na Sulemani walikuwa na wake wengi? Ndiyo, lakini Biblia inaonyesha nini kuhusu mpango huo? Inafunua vurugu na ugomvi ambao ulikuwa katika familia ya Abrahamu na ya Yakobo kwa sababu ya zoea hilo. (Mwanzo 16:1-4; 29:18–30:24) Baadaye, Sheria ya Mungu ilitia ndani amri hii iliyotolewa kwa kila mfalme: “Asizidishe wake kwa ajili yake, ili moyo wake usigeuke kando.” (Kumbukumbu la Torati 17:15, 17) Sulemani alipuuza amri hiyo kwa kuoa wake zaidi ya 700! Inasikitisha kwamba moyo wa Sulemani ulikengeushwa kikweli kutoka kwa Yehova kwa sababu ya uvutano mbaya wa wake zake wengi. (1 Wafalme 11:1-4) Kwa wazi, Biblia inaonyesha matokeo mabaya ya kuoa wake wengi.
Je, Yesu Mungu Mkuu anasemaje kuhusu ndoa ya wake wengi?
Mungu alimwagiza Yesu Kristo akazie mpango aliokuwa ameanzisha awali wa mwanamume kuwa na mke mmoja. (Yohana 8:28) Yesu alipoulizwa kuhusu ndoa, alisema hivi: “Yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamke na kusema, ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”—Mathayo 19:4, 5.
Je, Wakristo wa kwanza walisemaje kuhusu ndoa ya wake wengi?
Baadaye, mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu aliongozwa na roho ya Mungu kuandika hivi: “Kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 7:2)
Biblia inasemaje kuhusu ndoa ya wake wengi?
Pia, Biblia inasema kwamba katika kutaniko la Kikristo ni lazima mwanamume aliyefunga ndoa na ambaye ana majukumu ya pekee awe “mume wa mke mmoja.”—1 Timotheo 3:2, 12.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu. Tito 2:13

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW