Friday, February 19, 2016

MAHAKAMA YA KADHI HAIPO KWENYE QURAN

Ndugu wasomaji.
Leo ningependa kusema kuwa, dai la Waislam wa Tanzania la Mahakama ya Kadhi halina msingi wala usaidizi wa Quran.
Kwa wanao ifahamu Quran, watakubaliana na mimi kuwa HAKUNA AYA HATA MOJA ambayo Allah alisema na au Waamrisha Waislam waende kwenye Mahakama ya Kadhi. Narudia tena hakuna aya.
SASA NDUGU WAISLAM:
1. Who appoints Chief Kadhi and Kadhis?
--Nani na au mnamteuaje Kadhi Mkuu na Kadhi? Leteni aya.
2. What are the qualification for appointment to the office of a Kadhi (including a Chief Kadhi)?
-- Je, mnatumia qualification/elimu zipi kuchagua/kufanya utezi wa Ofisi ya Kadhi na Kadhi mkuu/ Leteni aya.
3. Since the Kadhis are not trained lawyers who understand the Evidence Act and the Civil Procedure Act, how and/or what will they use to administer their Courts?
-- Inafahamika kuwa Kadhi sio Mawakili walio somea ambao wanaelewa ushahid wa keshi ambazo si za jinai na jinai, SASA hawa Kadhi watatumia nini katika kusimamia Mahakama ya Kadhi?
4. Muslims are mainly of two sects in Tanzania - the Sunni and Shia. Majority of the Muslims in Tanzania are Sunni Muslims but there is a significant population of Shia Muslims too and consideration ought to be given to the appointment of Kadhis of the Shia Sect to cater the interest of the Shia Muslims. Will they have two different Courts? For Sunni and Shia?
--- Waislam wapo katika makundi mawili makubwa, Sunni na Shia. Wengi wa Waislam wa Tanzania ni Sunni, ingawa kuna Shia wengi vile vile. JE, Hii Mahakama ya Kadhi itatumia Kadhi wa dhehebu lipi katia ya hayo mawili? Je, watakuwa na Mahakama mbili tofauti za Sunni na Shia?
5. How will Muslim Women be protected since: Muslim law regards women as less than men in matters of both marriage and divorce, as well as devolution of property: Holy Quran Surah 2:228-232, and Surah 65:1-7 (only a man may divorce his wife even if he is required to provide for her); a man may beat his wife, even if lightly, the evidence of two women, is equal to evidence of one man (Surah 2:282). The application of such beliefs of faith are contrary to the Constitution.
---Kivipi Wanawake wa Kiislamu watatetewa kwenye hizi mahakama? Inafahamika kuwa Sheria za Kiislam zinakiri kuwa Mwanamke ni nusu ya Mwanaume, au yupo chini sana ya Mwanaume. Je, katika kesi ya kutoa talaka na mirathi, hii mahakama itawezaje kumtetea Mwanamke ambaye yupo nusu ya Mwaume? Sura 2: 228-232 na Sura 65:1-7 ( zinasema mwenye haki ya kutoa talaka ni Mwaume tu) Mume anahaki ya kumpiga mkewe, Ushahidi wa wanawake wawili ni sawa na ushahid wa mwanaume mmoja, (Sura 2:282). Huu utamaduni wa Kiislam, ni kinyume na sheria za nchi.
Je, Mwanamke atatetewa vipi kwenye hizi Mahakama?
Islamic "Kadhi" courtsis illegal and discriminatory.
Kwanini mnamsaidia Allah kwa kuanzisha Mahakama ya Kadhi?
Waislam, nileteeni aya ambayo Allah anasema kuwa muende kwenye Mahakama ya Kadhi.
Mkiniletea aya kutoka Quran inayo waamrisha kwenda kwenye Mahakama za Kadhi, leo hii nitasilimu na kuwa Muislam.
Haya nasubiri ajibu ya aya na sio matusi.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org.

MAHAKAMA YA KADHI NI HATUA YA AWALI KATIKA KUIFANYA TANZANIA KUWA TAIFA LA KIISLAM

na Max Shimba Ministries
Mahakama ya Kadhi ni nini?
Mahakama ya kadhi ni chombo cha kiislam kwa ajili ya kufanya mashauri ya ndoa , mirathi na mambo ya kidini kwa kutumia Sharia.
Sharia ni nini?
Sharia ni mkusanyiko wa sheria za dini ya kiislam ambazo zinatokana na kitabu cha quran na tamaduni za kiislam kwa kufuata mafundisho na hadithi za Mtume Muhammad.
Mambo ya kidini yanayo hukumiwa na mahakama ya kadhi ni yapi?
Ni mambo yote yanayokwenda kinyume na tamaduni za kiislamu. Mfano Kula hadharani wakati wa mwezi, wa ramadhani, kuchinja kwa mtu ambaye siyo muislamu, kufanya biashara ya vileo, biashara ya nyumba za kulala wageni, biashara ya nguruwe, mavazi yasiyoendana na tamaduni za kiislam kwa maana hiyo ili uwe salama kwa swala la mavazi sharti uvae hijabu kwa wanawake, kanzu na kibaragashia kwa wanaume, msuri na visuruari vizivyogusa viatu.
Kwa nini waislam wanataka Mahakama ya kadhi iingizwe kwenye katiba ya nchi?
Waislam wanataka mahakama ya kadhi iingizwe kwenye katiba ya nchi ili itambulike kisheria na iwe na nguvu kama mahakama za kawaida za makosa ya jinai na hiyo iwe na mamlaka ya kuhukumu watu wote waislam, wakristu na hata wapagani limradi tu hawaishi kwa kufuata tamaduni za kiislam. Mfano mtu atakaye kutwa anakula hadharani wakati wa mwezi wa ramadhani sharia itachukuwa mkondo wake na hukumu iliyotawala kwenye sharia kwa mtu anayeishi kinyume na tamaduni za kiislam ni kuuwawa kwa kuchinywa na jukumu hilo liko kwa Makadhi.
Hivyo basi mahakama ya kadhi ikiingizwa kwenye katiba itakuwa na nguvu za kuhukumu mambo ya siasa, kijamii na makosa ya jinai kwa ujumla kwa raia wote na si kwa waislam peke.
Muundo wa mahakama ya kadhi
Mahakama ya kazi inafuata muundo wa mahakama za kawaida hivyo zinaanzia ngazi ya chini kabisa kwenye wilaya na hadi ngazi ya kitaifa na mahakimu wa mahakama za kadhi ni makadhi amboa wote ni waislam
Kazi za Makadhi
1.Kusikiliza mashauri na kuhukumu kwa kufuata sharia
2.Kuhakikisha anatokomeza ukristu katika eneo lake na uislam unatawala
3.Kuhakikisha hakuna kanisa linajengwa katika eneo lake na wala kanisa linapo bomoka halitaruhusiwa kukarabatiwa wala kujengwa tena. Kujenga kanisa ni kinyume na tamaduni za kiislam ndiyo maana utaona wameanza kuchoma makanisa huko Zanzibar na sehemu zingine za Afrika kama Nigeria.
Madhara ya Mahakama ya Kadhi
1.Kuvunjika kwa umoja wa kitaifa uliopo kati ya waislam, wakristu na wapagani
2.Ugomvi wa kimasrahi kati ya wakristu, wapagani na waislam. Endapo Mahakama ya kadhi itaingizwa kwenye katiba ya nchi ni wazi itagharamikiwa na serikali na hivyo viongozi wa dini ya kiislam ambao ndiyo watakuwa makadhi watatumia fedha za walipa kodi wa Tanzania ambao ni waislam, wakristu na wapangani kujinufaisha wenyewe kwa kujitengenezea ajira. Vipi kuhusu viongozi wa dini za wakristu Maaskofu, Mapadri, Wachungaji na Viongozi wa dini za Jadi nao watakuwa wanalipwa na Serikali?
3.Kutoweka kwa wakristu kutokana na utawala wa sharia, sababu hukumu iliyo tawala kwenye sharia ni kifo hivyo wakristu
watauwawa kwa kuwa hawatakubali kuishi tamaduni za kiislam
4.Kuporomoka kwa uchumi wa nchi na kuongezeka kwa tatizo la ajira kwa mfano mashule ya wakristu au taasisi za kikristu zitachomwa kama ambavyo unaona yanatokea nchini Nigeria.
Viwanda vyote vya vileo vitafungwa, makumbi ya starehe yote yatafungwa. Ukiangalia uchumi wa Tanzania unategemea sana viwanda vya bia, Sigara nk. Sector hiyo ndiyo imeajiri watu wengi sana, anzia kwenye viwanda vyenyewe njoo kwenye mabaa, grosary na makumbi ya starehe
MAHAKAMA YA KADHI NI HARAM=TANZANIA
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

JE, WAKRISTO WANASTAHILI KUITUNZA SIKU YA SABATO? (SEHEMU YA KWANZA)

Ndugu msomaji,
Leo tutajikumbusha kwa mara nyingine tena kama tunatakiwa kuitunza Sabato.
Sabato ilipeanwa kwa Waisraeli, si kanisa. Sabato bado ingali siku ya Jumamosi si Jumapili na haijawai badilishwa. Bali sabato ni sehemu ya sheria ya Agano La Kale na Wakristo wako huru kutoka kwa mkono wa sheria (Wagalatia 4:1-26; Warumi 6:14). Wakristo hawitakiwi kuitunza sabato hata kama iko siku ya Jumamosi au Jumapili. Siku ya kwanza ya juma, siku ya Bwana (Ufunuo 1:10) za sherekea kiumbe kipya Kristo aliyefufuka akiwa kiongozi wetu. Hatujaamrishwa kiufuata sheria ya Musa ya sabato ya kustarehe, bali tuko huru kumfuata Kristo aliyefufuka. Mtume Paulo alisema kwamba kila mkristo amue mweneyewe kama ataifuata sabato, “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku; mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe” (Warumi 14:5). Twastahili kumwabudu Mungu kila siku, si Jumamosi pekee or Jumapili pekee.
Lengo la Mungu kupeana sabato kwa Waisraeli haikuwa kukumbuka uumbaji, bali waukumbuke utumwa wa Wamisri na kule kuokolewa na Bwana. Kumbuka yanayohitajika kwa kuitunza sabato: mtu aliyewekwa chini ya hiyo sheria hangeweza kutoka kwa boma yake (Kutoka 16:29), hangewakisha moto (Kutoka 35:3), angeruhusu mtu yeyote kufanya kazi (Kumbukumbu La Torati 5:14). Mtu mwenye angivunja shreria ya sabato angeuwawa (Kutoka 31:15; Hesabu 15:32-35).
Uchunganusi wa ukurasa wa Agano Jipya watuonyesha mambo mane muimu: 1) Popote Kristo alionekena baada ya kufufuka kwake na siku zimetajwa, kila wakati ni siku ya kwanza ya Juma (Mathayo 28:1,9, 10; Mariko 16:9; Luka 24:1,13,15; Yohana 20:19, 26). 2) Wakati pekee sabato imetajwa kutoka kwa kitabu cha Matendo ya Mitume hadi ufunuo ni kwa sababu ya lengo la uinjilisti kwa Wayahudi kwenye Masinagogi (Matendo Ya Mitume 13-18). Paulo aliandika, “Nilikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi” (1 Wakorintho 9:20). Paulo hakuenda kaitka Masinagogi kuwa na ushirika na kuwajenga waumini, bali alienda ili awathibitishie injili na kuwaokoa walikuwa wamepotea. 3) Mara moja Paulo anasema, “tangu sasa nitakwenda kwa watu wa Mataifa” (Matendo Ya Mitume 18:6), sabato tena haitajwi kamwe. Na 4) Badala ya kupendekeza kuwa waitunze siku ya sabato, sehemu nyingine ya Agano Jipya iliyobaki yasema kinyume ( ikijumulisha sehemu ya tatu ilioachwa nche hapo juu, inapatika katika Wakolosai 2:16).
Kwa kuingalia hoja ya nne kwa makini, tutafumbua kwamba, hakuna jukumu lolote la kuitunza sabato kwa waumini wa Agano Jipya. Pia tutaonyesha kuwa dhana ya Jumapili “Sabato ya Wakristo” si ya kibibilia. Vile imejadiliwa hapo juu, hakuna wakati sabato imetajwa baada ya Paulo kuanza kuangazia Mataifa, “Basi mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo” (Wakolosai 2:16-17). Sabato ya Kiyahudi ilifutiliwa msalabani hamali ambapo Kristo “Akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki” (Wakolosai 2:14).
Wazo hili limerudiwa zaidi ya mara moja katika Agano Jipya: “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku; mwinginie aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku huiadhimisha kwa Bwana” (Warumi 14:5-6a). “Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? Mnashika siku, na miezi, na nyaktati, na miaka” (Wagalatia 4:9-10).
Ni siku gani ya sabato, Jumamosi au Jumapili? Wakristo wastahili kuitunza hii siku?
Twastahili kumwabudu Mungu kila siku, si Jumamosi pekee or Jumapili pekee.
Mungu awabariki sana,

JE, WAKRISTO WANASTAHILI KUITUNZA SIKU YA SABATO? (SEHEMU YA PILI)


Ndugu msomaji,

Kwa kuwa Kristo alitimiza Sheria, je, Wakristo wana wajibu au daraka la kushika Sabato ya kila juma?

Akiongozwa na Roho wa Mungu, mtume Paulo anajibu hivi: “Kwa hiyo mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula na kunywa au kuhusu sherehe au kuhusu kushika mwezi mpya au sabato; kwa maana mambo hayo ni kivuli cha mambo yanayokuja, bali uhalisi ni wa Kristo.”—Wakolosai 2:16, 17.


Maneno hayo yaliyoongozwa na Roho wa Mungu yanaonyesha kwamba matakwa ambayo Mungu aliwapa watumishi wake yalibadilika sana. Kwa nini yalibadilika? Kwa sababu Wakristo wako chini ya sheria mpya, “sheria ya Kristo.” (Wagalatia 6:2) Agano la zamani la Sheria ambalo Mungu aliwapa Waisraeli kupitia Musa lilifikia mwisho wake wakati kifo cha Yesu kilipotimiza agano hilo. (Waroma 10:4; Waefeso 2:15)


Je, amri ya kushika Sabato ilifikia mwisho pia?
Ndiyo. Baada ya kusema kwamba “tumefunguliwa kutoka katika Sheria,” Paulo alitaja amri moja kati ya zile Amri Kumi. (Waroma 7:6, 7) Kwa hiyo, zile Amri Kumi, kutia ndani sheria ya Sabato, ni sehemu ya ile Sheria ambayo ilifikia mwisho. Kwa hiyo, waabudu wa Mungu, hawako chini ya takwa la kushika Sabato ya kila juma.


Mfano unaofuata unaweza kutusaidia kuelewa badiliko kutoka katika ibada ya Waisraeli kuingia katika ibada ya Kikristo: Nchi inaweza kubadili katiba yake. Baada ya katiba mpya kukubaliwa kisheria, watu hawatakiwi tena kufuata katiba ya zamani. Hata ingawa huenda sheria fulani katika katiba hiyo mpya zikafanana na sheria fulani za katiba ya zamani, sheria nyingine zinaweza kuwa tofauti. Kwa hiyo, mtu angehitaji kujifunza katiba mpya kwa uangalifu ili aone sheria ambazo zinatumika sasa. Kwa kuongezea, raia mshikamanifu angependa kujua katiba hiyo mpya ilianza kutumika wakati gani.


Vivyo hivyo, Mungu aliwapa Waisraeli sheria zaidi ya 600, pamoja na zile amri 10 za msingi. Sheria hizo zilitia ndani sheria kuhusu maadili, dhabihu, mambo ya kiafya, na kushika Sabato. Hata hivyo, Yesu alisema kwamba wafuasi wake watiwa-mafuta wangekuwa “taifa” jipya. (Mathayo 21:43) Kuanzia mwaka wa 33 W.K. na kuendelea, taifa hilo limekuwa na “katiba” mpya ambayo inategemea sheria mbili za msingi, yaani, kumpenda Mungu na kumpenda jirani. (Mathayo 22:36-40) Ingawa “sheria ya Kristo” inatia ndani maagizo mengi ambayo yanalingana na sheria ambazo Waisraeli walipewa, hata hivyo, Sheria fulani ni tofauti kabisa na sheria nyingine hazihitajiwi tena. Sheria ya kushika Sabato ya kila juma ni moja kati ya sheria ambazo hazitumiki tena.


Je, Mungu Amebadili Viwango Vyake?

Je, badiliko hilo la kuacha Sheria ya Musa na kufuata sheria ya Kristo linamaanisha kwamba Mungu amebadili viwango vyake?
Hapana. Yehova amebadili sheria ambazo watu wake wanapaswa kutii kama vile tu mzazi anavyobadili sheria anazowawekea watoto wake ikitegemea umri na hali zao. Mtume Paulo anaeleza hivi jambo hilo: “Kabla ya ile imani kufika, tulikuwa tukilindwa chini ya sheria, tukiwekwa pamoja kifungoni, tukiitazamia imani iliyokusudiwa kufunuliwa. Kwa sababu hiyo Sheria imekuwa mtunzaji wetu kutuongoza kwa Kristo, ili tutangazwe kuwa waadilifu kutokana na imani. Lakini sasa kwa kuwa imani imefika, sisi hatuko tena chini ya mtunzaji.”—Wagalatia 3:23-25.


Hoja hizo za Paulo zinaihusu vipi Sabato?
Fikiria mfano huu: Mwanafunzi anaweza kuagizwa ajifunze somo fulani shuleni, kama vile useremala, siku fulani ya juma. Hata hivyo, anapoanza kufanya kazi, huenda akahitaji kutumia ustadi aliojifunza, kila siku ya juma badala ya kuutumia siku moja tu. Vivyo hivyo, Waisraeli walipokuwa chini ya Sheria walitakiwa watenge siku moja kila juma ya kupumzika na kuabudu. Hata hivyo, Wakristo wanatakiwa wamwabudu Mungu kila siku badala ya siku moja tu kwa juma.


Basi je, ni kosa kutenga siku moja kila juma ili kupumzika na kuabudu?
Hapana. Neno la Mungu linamruhusu kila mtu ajiamulie jambo hilo, linasema hivi: “Mtu mmoja anaamua kwamba siku moja ni takatifu kuliko nyingine. Mtu mwingine anaamua kwamba siku zote ni sawa. Ni lazima kila mtu afanye uamuzi wake mwenyewe.” (Waroma 14:5, tafsiri ya God’s Word) Ingawa huenda watu fulani wakaamua kuona siku moja kuwa takatifu kuliko siku nyingine, Biblia inaonyesha waziwazi kwamba Mungu hatarajii Wakristo washike Sabato ya kila juma.


“Sheria imekuwa mtunzaji wetu kutuongoza kwa Kristo, ili tutangazwe kuwa waadilifu kutokana na imani. Lakini sasa kwa kuwa imani imefika, sisi hatuko tena chini ya mtunzaji.”—WAGALATIA 3:24, 25

Ndugu msomaji, leo tumejikumbusha tena kuwa hatupo chini ya Sheria bali tuna haki ya kuzitunza siku zote za Juma na kumwabudu Mungu kila siku, na sio siku moja to ya Jumamosi.

Mungu awabariki sana,

Max Shimba



For Max Shimba Ministries

Wednesday, February 17, 2016

ASILIA MBILI YA YESU KRISTO “MUNGU NA BINADAMU”

Tokea Dunia ianze, hapajawai toke Mtu yeyote alieishi kama Yesu Kristo. Yesu ni mtu wa maana sana ambaye ni Mwokozi, Mungu katika Mwili “Emanueli” (Isaya 9:6). Yesu sio Nusu Mungu na Nusu Binadamu kama watu na au imani nyingi zinavyo sema. Yesu yeye ni Mungu na ni Binadamu kwa wakati mmoja. Kwa maneno mengine, Yesu alikuwa na asilia Mbili tofauti ambazo ni Mungu na Binadamu kwa wakati mmoja.

Biblia inasema kuwa, Yesu ni “Neno” ambaye ni Mungu na alikuwa kwa Mungu na akafanywa kuwa Mwili na kuishi nasi, soma Yohana 1:1 na 14. Hii inamaanisha kuwa, mtu huyu mmoja ambaye ni Yesu alikuwa ana asilia mbili za Mungu na Binadamu.

Hii asilia ya Mungu haikubadirika pale ambapo “NENO” lilipo kuwa Mwili (Yohana 1:1, 14). Badala yake, Neno liliunga ubinadamu (Wakolosai 2:9). Hivyo basi, Umungu wa Yesu Kristo haukuharibika na au badirika. Zaidi ya hapo, Yesu hakuwa mtu tu ambaye alikuwa na Mungu ndani yake au Mtu aliye fanya kazi ya Mungu pekee, la hasha, Yesu ni Mungu katika Mwili na ni sehemu ya Pili katika Utatu Mtakatifu. Biblia inatuambia katika Waebrania 1 aya ya 3kuwa: Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi Yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno Lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko mbinguni. Hivyo basi, asilia hizi mbili za Yesu Kristo haziwezi kuchanganywa (Eutychianism), vile vile haziwezi kuwa pamoja na kuwa Mungu-Mtu (Monophysitism). Hizi asili mbili ni tofauti na zinajitemea na wakati huohuo ni moja katika Yesu (person of Jesus). Huu muungano unaitwa Hypostatic Union.

Jedwari lifuatalo litakusaidia uone hizi asilia mbili za Yesu Kristo:
MUNGU
BINADAMU
Yesu anaabudiwa (Matayo. 2:2, 11; 14:33)
Yesu anamwabudu Mungu Baba (Yohana 17)
Yesu anaitwa Mungu (Yohana  20:28; Waebrania 1:8)
Yesu anaitwa Mtu/Binadamu (Marko 15:39; Yohana 19:5)
Yesu aliitwa Mwana wa Mungu (Marko 1:1)
Yesu aliitwa Mwana wa Adam (Yohana 9:35-37)
Anaombwa/prayed(Matendo ya Mitume7:59)
Anamwomba Mungu Baba (Yohona 17)
Yesu hana dhambi/sinless (1 Petro. 2:22; Waebrania 4:15)
Yesu alijaribiwa (Matayo. 4:1)
Yesu anafahamu kila kitu (Yohana 21:17)
Yesu alikuwa na Hekima (Luka 2:52)
Yesu anatoa uzima wa milele (Yohana 10:28)
Yesu Alikufa (Rom. 5:8)
Adhama zote za Mungu zipo ndani ya Yesu (Wakolosai 2:9)
Alikuwa na Mwili na Mifupa (Luka 24:39)

USHAHIDI ZAIDI WA ASILIA MBILI YA YESU

Mafundisho ya muungano wa Hypostatic ni ya “communication idiomatum” (Ni maneno ya Kilatini “Communication of properties”). Haya ni mafundisho ya adhama mbili za Yesu Kristo za Mungu na Binadamu zote zipo ndani ya Yesu Mtu “person of Jesus”. Hii inamaanisha kuwa, binadamu Yesu alikuwa na haki ya kusema kuwa “Alikuwa na utukufu na Baba Mungu kabla ya dunia kuumbwa soma Yohana 17:5), vile ile kudai kuwa  alitoka Mbinguni (Yohana 3:13), na kudai kuwa alikuwa kila mahalai “omnipresence (Matayo 28:20). Haya madai yote ya Yesu ni adhama za Mungu na kuwa yeye Yesu alikuwanayo.
Moja ya Makosa makubwa sana yanayo fanywa na wasio Wakristo ni kushindwa kwao kuelewa kuwa Yesu alikuwa na ASILIA MBILI. Kwa mfano, Mashahidi wa Yehova wao wanamwangali Yesu kama Binadamu na kupuuza adhama zake za Umungu. Mara zote wao hutumia zile aya ambazo zinakiri Ubinadamu wa Yesu na kuzipambanisha na aya ambazo zinasema kuwa Yesu ni Mungu. Kwa upande mwingine, Masayantisti wa Kikristo wao hufanya kinyume chake. Wao wana angalia zaidi upande wa Yesu ni Mungu na kusahau kuwa, Yesu alikuwa Binadamu vile vile.

Ili kumwelewa Yesu vyema, basi kila mafundisho ambayo yanamuhusisha Yesu, hayana budi kuzumgumzia Yesu kama Mungu na Yesu kama Binadamu. Hizo asilia Mbili ni zake. Kumbe ndio maana Yesu katika Luka 2:52 inasema: Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu. Na wakati huo huo alikuwa kila kitu “omniscient” Soma Yohana 21:17. Yesu ni Neno la Mungu aliye kuwa Mwili/Binadamu (Yohana 1:1, 14).
Zaidi ya hapo, Biblia inamhusu Yesu (Yohana 5:39. Mitume wote walimtabiri Yesu (Matendo ya Mitume 10:43). Mungu Baba anatoa ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 5:37; 8:18. Roho Mtakatifu naye anato Ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 15:26. Kazi zake Yesu nazo zinashuhudia kuhusu Yesu Soma Yohana 5:36; 10:25. Makundi ya watu nayo yanashuhudia kuhusu Yesu, Soma Yohana 12:17. NA YESU anajishuhudia mwenyewe Soma Yohana 14:6 ; 18:6.
Kuna aya nyingine nyingi ambazo zinamshuhudia Yesu kuwa ni Mungu nazo ni
Yohana 10:30-33; 20:28; Wakolosai. 2:9; Wafilipi. 2:5-8; Waebrania 1:6-8; na 2 Petro. 1:1.
1 Timoteo 2:5 inasema , " Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani, mwanadamu Kristo Yesu, 6. aliyejitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wanadamu wote, jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake "   Hivi sasa, kuna Mtu Mbinguni ambaye yupo katika kiti cha Enzi. Yeye ni Mpatanishi wetu kwa Mungu Baba (1 Yohana 2:1). Ni Mwokozi wetu (Tito 2:13). Ni Bwana wetu (Warumi 10:9-10) Huyo Mtu anaitwa YESU.
Hakika Yesu Ni Mungu.
Kwa Maswali zaidi wasiliana nasi katika maxshimbaministries@gmail.com
Imeletwa kwenu na Max Shimba
Kwa Max Shimba Ministries Org.

@2015, April.  

JIBU KWA WASABATO KUHUSU KUTUNZA SIKU YA SABATO KATIKA UFALME MPYA WA MUNGU - ISAYA 66 AYA YA 22 NA 23

Ndugu msomaji,

Leo nitajibu hii hoja kuitunza siku ya Sabato katika Ufalme Mpya wa Mungu. Hebu tusome kwanza aya wanazo zitumia kusaidia hoja ya Sabato katika Ufalme Mpya wa Mungu.
ISAYA 66: 22-24
22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 
23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. 
24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.

Wasabato-SDA wamekuwa wakitumia aya ya 22 na 23 ya Isaya Sura ya 66 kuwa Sabato ni ya milele. NUKUU “22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.” 

Hoja hapa inakuja kwasababu katika hizi aya pamezungumzia pia Mbingu Mpya na Dunia Mpya, ambazo zimetajwa vile vile na Yohana katika kitabu cha Ufunuo, kwamba tutakuwa tunatunza Sabato. Lakini ikumbukwe kuwa katika aya hizi hizi pamesemwa vile vile kuhusu “MWEZI MPYA” Sasa kifikra lazima tujiulize swali hili: Je, kwanini hatutunzi siku ya MWEZI MPYA? Je, tutakuwa tunatunza MWEZI MPYA katika Dunia Mpya na Mbingu Mpya?
Swali la Kwanza nimeliweka na limekuja kwababu ya wazo yakinifu la Mwezi Mpya kuwepo pamoja na Sabato katika aya ya 23.
Sababu ya Wasabato kutumia hizi aya “22-23” ni kulinda dai au hoja yao ya kuitunza Sabato sasa na baadae. Hili ni kosa, kwasababu Isaya 66: 22-23 haizungumzii kuitunza Sabato sasa, LASIVYO, inatubidi kuitunza na siku ya MWEZI MPYA, sasa. Je, Wasabato wanaitunza siku ya MWEZI MPYA?

Swali la pili ni la kushangaza kidogo, na kuna mambo kadhaa ya muhimu lazima tuyawekee umaanani. KWANZA: Neno ambalo ni tafsir ya “mwezi mpya” katika Kihebrania ni “CHODESH” likimaanisha MWEZI. Hili neno halikuwa na maana ya watu washerekee MWEZI MPYA. Kwa mara ya kwanza lilitumika katika Kitabu cha Mwanzo 7 aya ya 11. , likiwa na tafsir ya “Mwezi”, zamani zaidi kabla ya chodesh kuwa sikukuu ya Wayahudi katika taifa la Israel.
Zaidi ya hapo, neno “mbingu mpya” na dunia mpya” linatupa mwanga kuwa mpango wa Mungu ni kurejesha kila kitu kama ambavyo alitaka kiwe kabla ya dhambi kuingia duniani kama ilivyo semwa kwenye Sura mbili za kitabu cha Mwanzo.  Mfalme mwenye hekima anatuambia kuwa Mhubiri 3:  14 Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye. 

Na katika Sura ya kwanza ya Mhubiri 1: 4 inasema: 4 Kizazi huenda, kizazi huja; nayo dunia hudumu daima. 
Iwapo unaamini kuwa Dunia itakuwa milele au la, hapa jambo la muhimu ni hili” Mungu atarejesha kila kitu na kuwa sawa kama pale mwanzo kabla ya dhambi kuingia duniani”
Matendo ya Mitume 3: 20-21 inasema: 20 apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani; 
21 ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu. 
Kwa maneno mengine, kila kitu kitarudishwa na kuwa thabiti kama pale mwanzo. Ushahidi zaidi ni yale maono ya Yohana ya Mbingu Mpya na Dunia Mpya. UFUNUO 22. Utagundua hata Mti wa Uzima ambao wakati Fulani ulikuwa katika Bustani ya Edeni (Mwanzo 2:9), umetajwa hapo.

Ufunuo 22:2  katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa. 
Hapo mwanzo tumekutana na mambo mengi, moja wapo ikiwa ni Siku ya Saba Sabato (Mwanzo 2:1-3). Ndio maana hatushangai kuwa, Nabii alisema kuhusu Sabato bado ipo hata baada ya dhambi kuingia, kwa marejesho ya kila kitu ikajumlisha na mwanzo wa Siku ya Saba. Hata hivyo, tunasoma kuhusu jinsi dunia ya kwanza katika Mwanzo 1 na 2, na hatusomi kitu chechote kile kuhusu shereza za MWEZI MPYA. Haikutajwa hiyo sherehe kabisa, je, hii ni kwanini? Jibu lako utalipata katika Ufunuo 22: 2

Ufunuo 22: 2 inasema: katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa. 
Kumbuka kuwa neno la MWEZI MPYA linamaanisha “mwezi” na tunapo linganisha maneno ya Isaya na ya Yohana, tunajifunza kuwa maneno ya mwezi mpya kwa mwezi imaanisha ni mkusanyiko wa Watakatifu, mara moja kwa mwezi, kwasabu ya kula mti wa uzima.  Hivyo, jibu kwa swali letu kama Mwezi Mpya utakuwepo katika dunia mpya, jawabu ni NDIO.  Ingawa sababu ya kukutana katika mwezi mpya ni kula mti wa uzima. Hivyo, sababu ya kusherekea Sabato itabadilika na sio kusherekea kila wiki kama ilivyo semwa katika Kutoka 20:11,  Hapa tutasherekea kuumbwa kwa dunia mpya, ndio maana Isaya alisema kuhusu MBINGU MPYA  na DUNIA MPYA –AMBAYO NITAIFANYA Isaya 66:22.
Isaya aliona mwezi mpya katika maono yake kama marejesho ya kila kitu katika ukamilifu wake, hususan Yerusalemu, na tunajua kuwa kutakuwa na Yerusalemu mpya. Kuona kwake kwa mwezi mpya au mwezi, ni sambamba na Yohana alipo ona kurejeshwa kwa mji (Ufunuo 22:20) hii ndio maona ambayo Isaya aliyaona katika aya ya 22-23 ya Sabato ya uumbaji, pamoja na kukutana kwa watakatifu wote, mara moja kwa mwezi, kufurahi na Bwana na kula Mti wa Uzima.
 HOJA:
Sasa tuendelee na aya ya 24 ya Isaya 66 inasema 24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.
Hii aya inaweza kujibu zaidi hoja ya SDA, KATIKA AYA YA 15 ya Isaya 16, INATUAMBIA KUWA Bwana Mungu “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto. Na katika aya ya 16 anasema Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi. 
Wakristo wengi wanaamini kuwa hizi aya zinazungumzia kuja kwa Bwana kwa mara ya pili, au kuja kwa Bwana na watakatifu wakati wa Milenium.
Je, kwanini hatutunzi siku ya MWEZI MPYA?
Je, tutakuwa tunatunza MWEZI MPYA katika Dunia Mpya na Mbingu Mpya?
Je, Adam na Hawa walisherekea Sabato?

Hivyo basi, leo tumejifuza kidogo kuhusu Isaya 66 aya ya 22 na 23 na kijibu hoja ya Wasabato kuhusu umilele wa kuitunza Sabato.
Mungu awabariki sana.
Max Shimba

For Max Shimba Ministries Org.

Tuesday, February 16, 2016

ALLAH NA MUHAMMAD WANASEMA KUWA NYOTA NI SILAHA ZA KUWAPIGA MASHETANI



Ndugu msomaji,
Tunaendela na hadith za msemakweli za Muhammad. Katika hadithi ya leo, tutajifunza kuhusu silaha anazo tumia Allah anapo pigana na mashetani.
Nyota Zinapaswa Kuyapiga Mashetani?
"Uumbaji wa nyota ulikuwa na malengo matatu, yaani kuwa mapambo ya mawingu, kupiga mashetani, na ishara za kuongozea wasafiri. Kwa hiyo, mtu yoyote anapojaribu kutafuta tafsiri tofauti, amekosea na anapoteza nguvu zake..." Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 (Mwanzo wa Uumbaji) sura ya 3 maelezo ya mwenye kutafsiri kabla ya na. 421 uk.282.
Hebu tujifunze kwanza maana ya Nyota:
Kwa kutumia darubini na vifaa vya kisasayansi imegunduliwa ya kwamba ni magimba makubwa sana katika anga la nje yanayong'aa kwa sababu yanatoa mwanga, joto na aina mbalimbali za mnururisho kutokana na myeyungano ya kinyukilia ndani yao. Lakini ziko mbali sana na kwa hiyo tunaziona kama nukta ndogo za nuru. Kwa jumla nyota zinaonekana kwenye anga kwa mpangilio usiobadilika na kila nyota huwa na mahali pake pasipobadilika kati ya nyota nyingine hata kama nyota kwa jumla zinazunguka angani juu yetu kila siku.
Baada ya kusoma maana ya Nyota, mtu anaweza jiuliza, kivipi Allah anapigana na Mashetani kwa kutumia Nyota?
Mbona Allah hajawai tuletea aya ambayo inasema jinsi alivyo pigana na Mashetani kwa kutumia Nyota?
Ni vita zipi ambazo Allah anatumia Nyota kupigana na Mashetani?
Kama Allah ni AKBAR kama wanavyo dai, Waislam, kwanini anshindwa kutumia nguvu yake kuyapiga mshetani mpaka atumie Nyota?
JIFUNZE ZAIDI KUHUS NYOTA:
Fizikia na astronomia zimegundua ya kwamba nyota hazidumu milele bali zina mwanzo na pia mwisho. Kutokana na tabia hii wataalamu mara nyingi huongea juu ya "maisha", "kuzaliwa" na "kufa" kwa nyota ingawa si viumbehai.
Nyota zinaanzishwa katika nebula au katika mawingu makubwa ya gesi kwenye anga la ulimwengu. Kama wingu ambalo sehemu kuwa yake ni hidrojeni ni kubwa sana inaanza kujikaza kutokana na graviti yake. Katika muda wa miaka mioni 10-15 wingu linajikaza kuwa tufe kadhaa kubwa na ndani ya tufe hizi halijoto inazidi kupanda. Kadiri jinsi gesi inajikaza nguvu ya graviti ndani yake inaongezeka na atomi zake zinaanza kugusana. Halijoto inazidi hadi kufikia kiwango ambako mmenyuko mfululizo wa kinyuklia unaanza kutokea hadi kufikia mmeyungano nyuklia wa hidrojeni kugeukia heli.
Kipindi cha mmeyungano nyuklia wa hidrojeni kinaendelea kwa miaka mabilioni hadi sehemu kubwa ya hidrojeni imekwisha. Hapa sehemu za nje ya nyota hupoa na kupanuka; halii hii huitwa pandikizi nyekundu (red giant) kwa sababu ya ukubwa na rangi yake. Mapandikizi mekundu kadhaa huonekana kwa macho tu angani yaking'aa kwa nuru nyekundu. Kama masi ya nyota bado ni kubwa mmeyungano nyuklia unaendelea kuzaa elementi nzito zaidi kwa sababu sehemu ya heli inaendelea kujibadilisha kuwa elementi za juu zaidi. Inaaminmiwa ya kwamba elementi zote ulimwenguni zilianzishwa ndani ya nyota.
Mwishowe kama masi haitoshi tena kuendeleza mmeyungano masi inaweza kujikaza; kutegemeana na ukubwa wa masi nyota inaweza kupasuka. Mabaki ya mlipuko huu yanakaa angani tu na mara nyingi huingia tena katika mwendo wa kuzaa nyota mpya; sehemu ndogo za masi hii huwa sayari.
Kama masi imejikaza sana shimo nyeusi (Kiing.: black hole) inatokea. Katika hali hii nguvu ya graviti ni kubwa mno inashika hata nuru yenyewe ambayo haiwezi kuoka nje tena.
Nategemea leo umesha gundua kuwa Allah hakuumba Nyota na wala Allah hazielewi Nyota.
Karibuni kwa Yesu Mungu Mkuu.
Mungu awabariki sana,
Max Shimba Ministries Org.

UTHIBITISHO WA MUHAMMAD KUMILIKI WATUMWA WA KIAFRIKA

Ndugu msomaji,
Leo nitwawapa uthibisho zaidi kuwa Muhammad alimiliki watumwa wa Kiafrika.
SOMA:
Mahusiano ya Kimbari (Race Relations) na Muhammud Kumiliki Watumwa Waafrika
"Anas alisimulia: Mtume alisema, ‘Msikilize na kumtii (chifu wako) hata kama ni Muethiopia ambaye kichwa chake ni kama zabibu kavu akifanywa kuwa chifu wako." Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 11 (Kitabu cha Wito wa Maombi) sura ya 54 na.662 uk.375 (pia Ibn-i-Majah juzuu ya 4 kitabu cha 24 (Kitabu cha Jihad) sura ya 39 na. 2860 uk.196) Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 11 (Kitabu cha Wito wa Maombi) sura ya 55 na.664 uk.376 husema vivyo hivyo.
Kama ilivyosemwa mwanzoni, Muhammad alikuwa mmiliki wa watumwa aliyekuwa na mtumwa Mwafrika angalau mmoja. (Bukhari juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 316 na.435 uk.407, juzuu ya 9 kitabu cha 91 (Kitabu cha Habari Zilizotolewa na Mtu Mkweli) sura ya 3 na.368 uk.275) Muhammad aliuza watumwa wake Waafriaka wawili ili aweze kumwacha huru mtumwa mwingine ambaye alibadilika kuwa Muislam Ibn-i-Majah juzuu ya 4 kitabu cha 24 (Kitabu cha Jihad) sura ya 41 na.2869 uk.202. Zifuatazo ni dondoo.
"Kisha nilivaa nguo zangu na kwenda nyumbani kwa Mtume wa Mungu, na tazama, alikuwa anakaa kwenye chumba chake cha juu ambako mtumwa wake Mwafrika alikuwa (anakaa) kwenye kituo cha kwanza." (Bukhari juzuu ya 6 kitabu cha 60 sura ya 316 na.435 uk.407)
"Umar alisimulia, "Nilikuja na tazama, Mtume wa Allah alikuwa anaishi kwenye Mashroba (chumba cha barazani) na mtumwa Mwafrika wa Mtume wa Allah alikuwa juu ya ngazi zake." (Bukhari juzuu ya 9 kitabu cha 91 sura ya 3 na.368 uk.275)
Jambo hili linafurahisha kwani Muhammad alimnunua mtumwa ambaye alikuwa amebadilika kuwa Muislam (labda kwa lengo la kumfanya kuwa huru.) Badala ya kumlipa mwenye kummiliki hela taslimu, Muhammad aliwauza watumwa wake wawili Waafrika. Mbari ya mtumwa wa kwanza haijaelezwa ila kwa sababu moja au nyingine ilionekana kuwa muhimu kuandika kuwa watumwa wawili ambao Muhammad aliwauza walikuwa Waafrika, na ilibidi wawe wawili ili aweze kumnunua mtumwa mmoja.
"Jabir (Allah apendezwe naye) aliripotiwa kusema kwamba kuna mtumwa aliyekuja na kutoa kiapo cha utii kwa Nabii Mtakatifu (amani na baraka za Mungu ziwe naye) kwani uhamaji (Hijra) na Nabii Mtakatifu (amani na baraka za Mungu ziwe juu yake) hakujua kwamba alikuwa mtumwa. Kisha mmiliki wake alikuja kumtafuta na Nabii Mtakatifu (amani na baraka za Mungu ziwe juu yake) alisema, ‘Muuze kwangu.’ Hivyo alimbadilisha na watumwa wawili Waafrika. Kisha Muhammad hakupokea kiapo cha utiifu toka kwa mtu yoyote baada ya hapo, mpaka hapo mtu atakapomuuliza: Je huyu ni mtumwa?" (Ibn-i-Majah juzuu ya 4 kitabu cha 24 (Kitabu cha Jihad) sura ya 41 na.2869 uk.202)
Hadithi za Bukhari zinapatikana kwenye mtandao wa kumpyuta katika tovuti:
Hii dini ya Uislam si ya Waafrika maana hata mtume wao alimiki Watumwa wa Kiafrika. Zaidi ya hapo ALIWATA MAJINA MABAYA WAFRIKA, eti wana PUA NENE, ETI WANA MACHOGO. Hakika hizi chuki kubwa kubwa hazipo kwenye Mitume wote wa Biblia bali kwa Mtume wa Allah aitwaye Muhammad.
Je, Muafrika ana haki ya kuwa Musialm?
Je, Allah anapenda Waafrika?
Kama kunauthibitisho wa Allah kusema anapenda Waafrika nileteeni hapa, leo hii nitasilimu na kuwa Muislam.
Kwa mara nyingie tena tunajifunza kuwa Allah na Muhammad hakuwapendi Waafrika na hakuna aya hata moja kwenye Quran ambayo Allah anasema kuwa anawapenda Waafrika.
Karibuni kwa Yesu Mungu Mkuu.
Max Shimba
For Max Shimba Ministries Org.

Monday, February 15, 2016

UTHIBITISHO WA MISTARI ILIYO FUTWA KWENYE QURAN

Ndugu msomaji,
Kama Quran imekamilika kama jinsi Waislam wanavyo dai, kwanini Muhammad alifuta mistari kwenye kitabu cha Allah?
Kama Quran ni maneno ya Allah, je, nani alimpa mamlaka Muhammad kufuta aya za Allah?
Je, hii Quran imekamilka au haijtakamiliak, maana sasa tunafahamu kuwa kuna aya zilifutwa na Muhammad bila ya ruhusa ya Allah.
Huu ni Msiba. Soma ushahid hapa chini.
"Baada ya hapo, Mungu alitufunulia mstari uliokuwa miongoni mwa ile iliyofutwa baadaye." Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 59 (Kitabu cha Safari za Kijeshi) sura ya 27 na.416 uk.288.
"Anas bin Malik alisimulia: ... Walifunuliwa wale waliouawa Bi’r-Ma’una, mstari wa Kurani tuliozoea kuukariri, lakini badaye ulifutwa. Mstari wenyewe ulikuwa: ‘Wafahamishe watu wetu kuwa tumekutana na Bwana wetu. Amefurahishwa nasi na ametufurahisha.’" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 52 (Kitabu cha Jihad) sura ya 19 na.69 uk.53. Tazama pia Historia ya al-Tabari juzuu ya 7 uk.156.
Kumbukumbu nyingine za mistari iliyofutwa ni Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 52 (Kitabu cha Jihad) sura ya 8 na.57 uk.45, Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 52 (Kitabu cha Jihad) sura ya 184 na.299 uk.191, na Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 59 (Kitabu cha Safari za Kijeshi) sura ya 27 na.421 uk.293 zote zinarudia kitu hicho hicho kuhusu mstari huo huo.
Wakati fulani Muhammad aliafikiana na kusema kuwa kuhusiana na mabinti wa Allah kwenye Sura 53:19 "sala ya ya kuombea ilipaswa kutumainiwa." Muhammad alisema tunapaswa kutegemea msaada wa sanamu hizi tatu.
Wafuasi wa Muhammad walishangazwa kuwa amesema hivi. Baadaye, Muhammad alibadilisha msimamo wake na kusema kuwa Shetani alimdanganya. Mistari hii ilibatilishwa au kutolewa. Wanazuoni wa Kiislam wanaiita mistari hii "aya za Shetani." Inafurahisha kusoma maelezo ya Waislam kuhusu namna ambayo nabii wa kweli angeweza kusema hivi.
MASWALI:
1. Kwanini Allah aliruhusu Shetani kumdanganya Nabii wake?
2. Kama Muhammad aliweza kudanganywa na Shetani, je, tutaiamini vipi Quran ambayo imejaa shaka?
3. Je, kuna aya ngapi ambazo ni za Shetani kwenye Quruan, ikiwa sasa tunafahamu kuwa, Shetani na yeye alikuwa anateremsha aya zake kwa kupitia Jibril huyo huyo?
4. Kwanini Waislam wanakataa ukweli wa Mabinti wa Allah ambao Muhammad aliuukubali?
5. Kwanini Muhammad alishindwa kutofautisha maneno ya Allah na Shetani na kudhani ni mtu huyo huyo anasema?
MABINTI WA ALLAH
Uarabuni kabla ya Muhammad, kabila la Muhammad, Quaraysh, lilimwamini Mungu aitwaye Allah (au Al’Ilah) aliyekuwa na mabinti watatu walioitwa Al-Lat, Al-Uzza, na Manat.
" ‘Urwa alisema, ... kuhusiana na Ansar aliyezoea kumdhania Ihram kuwa anaabudu sanamu anayeitwa ‘Manat’ ambaye walizoea kumwabudu kwenye sehemu iliyoitwa Al-Mushallal..." Bukhari juzuu ya 2 kitabu cha 26 (Hija) sura ya 78 na.706 uk.413.
"Mstari huu ulifunuliwa kwa kuhusiana na Ansar aliyekuwa anamdhania Ihram kuwa sanamu Manat ambaye aliwekwa karibu na sehemu iliyoitwa Qudaid..."Bukhari juzuu ya 3 kitabu cha 27 (‘Hija ya Umra) sura ya 10 na.18 uk.11. Al-Lat, Al-Uzza wameelezewa Bukhari juzuu ya 8 kitabu cha 74 (Kitabu cha Kuomba Ruhusa ya Kuingia) sura ya 52 na.314 uk.209; juzuu ya 5 na.375 uk.259
Hakika Quran sio kitabu cha Mungu na kimejaa shaka kubwa kubwa.
Leo tumejifunza tena kuwa Quran sio kitabu cha Mungu, na zaidi ya hapo, Allah alikuwa na Mabainti watatu.
Mungu awabariki sana,
Max Shimba
For Max Shimba Ministries

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW