
JINSI MUHAMMAD (S.A.W) ALIVYOPATA UTUME NA WAHYI (UFUNUO) WAKE
Ufunuo aliokuja nao Muhammad s.a.w , mtume wa Waislamu, ni tofauti sana na mitume wote walioishi kabla yake wanaotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Tofauti yake ni kwamba manabii na mitume wote waliotajwa ndani ya Biblia Takatifu, wameandika watu mbalimbali wapatao 40 kwa miaka mingi sana inayokaribia 1500, lakini ufunuo wao ni wa aina moja (it has comformity). Ule unabii wa Agano la Kale umetimizwa katika Agano Jipya. Hii ni kwa sababu chanzo cha ufunuo huo ni kimoja, Roho Mtakatifu.
Lakini kwa upande wa Muhammad s.a.w , mtume wa Waislamu yeye chanzo cha ufunuo na hatimaye utume wake ni masuala yenye utata sana ambao hata wafuasi wa dini hiyo na wao hawajui kwa hakika ukweli ni upi.
Hebu tuangalie kwa ufupi utata huo.
Muhammad s.a.w alipotimiza umri wa miaka 38 alihama toka nyumbani kwake, akahamia katika mapango yaliyokuwa hapo karibu na mji wa Makka. Alipofikisha umri wa miaka 40 siku moja alitokewa na kiumbe ambacho Waislamu leo wanakiita Malaika Jibril.
Wahyi (ufunuo) uliokuja kwa Muhammad alisikia makengele,uso kuwa mwekundu,jasho kumtoka. Katika Bukhar, Hadithi na 2, Juzuu na 1,Al-Lu’lu Kitabu cha 3.Uk. Na.874 Hadithi na 1505 “Hadithi ya Aisha r.a mama wa waumini amesema, kuwa Al Harith ibn Hisham r.a alimuuliza mtume wa Allah s.a.w ‘ Ewe mtume wa Allah hivi wahyi (ufunuo) hukujia vipi?’ mtume wa Allah s.a.w akajibu, “ Wakati mwingine hunijia kama mlio wa kengele, na aina hiyo ndiyo ngumu zaidi kwangu, inaondolewa hali hiyo kwangu wakati tayari nimeshapata wahyi. Na nyakati nyengine malaika anakuja kwangu akiwa katika mfano wa mtu, kwa hiyo ananieleza na ninayazingatia aliyoyasema.” Aisha r.a alisema , Na hakika nilimwona unamshukia wahyi siku ya baridi kali na ilipomuondoka hali hiyo, paji lake la uso lilichuruzika jasho.”
Qurani 53:2 – 6 Suratul Najm (Nyota) “Kwamba mtu wenu huyu Nabii Muhamad (hakupotea kwa ujinga) na wala hakukosa (Na hali ya kuwa anajua). Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake). Hayakuwa haya (anayosema) ila ni wahyi (ufunuo) uliofunuliwa (kwake). Amemfundisha (malaika) mwenye nguvu sana. Mwenye uweza na yeye (huyu Jibril) akalingana sawa sawa.
Huyu malaika Jibril ndiye Waislamu wanasema alimtokea Muhammad kule pangoni na kwamba yeye huyo malaika Jibril ndiye Roho Mtakatifu. Tunaposoma ufafanuzi wa aya ya 2:87 ya Suratul Baqarah, uliyomo ndani ya Qur’an unasema “Kwa Waislamu Roho Mtakatifu ni Malaika Jibril si yule wanaodai Wakristo kuwa ni mmoja wa asili ya utatu (Trinity)”.
Jambo ninalopenda ulijue ni kwamba Waislamu wote hawakubahatika kupewa elimu ya Roho. Hii ni kuanzia mtume na nabii wao Muhammad . Tunasoma hayo katika Qur’an 3:7 “Yeye ndiye aliyekuteremshia kitabu (hiki Qur’an) ndani yake zimo aya Muhkam (nyepesi kufahamika) ambazo ndizo msingi (asili) wa kitabu (hiki) na ziko nyingine Mutashabihat (zinababaisha kama habari za akhera,za peponi na motoni na mengine ambayo yamekhusika na Roho).Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazo babaisha kwa kutaka kuwaharibu watu na kutaka kujua hakika yake vipi; na hakuna ajuaye hakika yake vipi ila Mwenyezi Mungu. Na wale waliozama katika ilimu husema:”Tumeziamini,zote zimetoka kwa Mola wetu.”Na hawakumbuki isipokuwa wenye akili.”
Qur’an 17:85 Suratul Ban Israil (Wana wa Israeli). “Na wanakuuliza habari ya roho.Sema roho ni jambo lililohusika na Mola wangu (Mwenyezi Mungu),Nanyi hamkupewa katika ilimu (ujuzi) ila kidogo kabisa.(Nayo ni ilimu ya vitu visivyokhusika na roho”).
Hivyo katika Uislamu elimu ya Roho hawana kwa mujibu wa Qur’an. Hii ndiyo sababu mara nyingi wao hushughulikia sana mambo ya nje (externalistics) zaidi kuliko ya Rohoni k.m kutawadha na kupandisha maji puani wakiamini wamemtoa Shetani aliyekuwa ndani ya pua. Katika kitabu kiitwacho Al-Lu’lu’ wal-Marjan, Juzuu 1. Hadithi na 183 uk. 96 inasomeka hivi “Amesimulia Abu Huraira (r.a), Mtume (s.a.w) alisema, “Mmoja wenu anapoamka kutoka usingizini, basi atawadhe na apandishe maji puani na apenge mara tatu, kwa sababu Shetani alilala ndani ya tundu za pua yake”. (Bukhari, Hadithi, Na.516 Juzuu 4)







