Sunday, November 20, 2016

ZANZIBAR INAONGOZA KWA KUWA NA IDADI KUBWA YA MASHOGA WENYE UKIMWI


Na Nora Damian
KISIWA cha Unguja, kinaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya mashoga wanaoishi na virusi vya ukimwi.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam na Dk Subilaga Kasesela-Kaganda wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids), alipokuwa akizungumza katika kongamano kuhusu maambukizi ya ukimwi kwa wafanyabiashara ya ngono, mashoga na watumia dawa za kulevya.
Alisema Zanzibar ndio eneo lenye mambo ya ushoga hapa nchini na kwamba asilimia 12 ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi katika Kisiwa cga Unguja ni wale wanaojishughulisha na mambo hayo.
Alisema baadhi ya sababu zinazochangia kukua kwa tatizo hilo ni vishawishi, wazazi kuwa mbali na watoto wao, yatima wanaokosa malezi mazuri, watoto wa kiume kulelewa na mama kwa kipindi kirefu na mtoto wa kiume kupenda kuvaa mavazi ya kike.
Alisema sababu nyingine zinazochangia tatizo hilo ni mazingira ya shule za bweni, ambazo baadhi yake zina wanafunzi wa kiume pekee, mwanaume kuwa na homoni nyingi za kike na wanaume wengi kukaa sehemu moja kama jeshini na magerezani.
�Na wanawake wanaopenda kufanya ngono ya haja kubwa wanapaswa nao kujua kuwa ina hatari zaidi, kwa maana ya kupata maambukizo kuliko njia ya uke,�alisema Dk Kaganda.
Alisema utafiti uliofanywa umeonyesha kuwa asilimia sita ya Watanzania wanaishi na virusi vya ukimwi, wanawake wakiwa ndio waathirika wakubwa wa tatizo hilo.
Dk Kaganda alisema tatizo hilo liko zaidi katika maeneo ya mijini na ligawagusa mno watu wazima na wanawake wenye uwezo wa kufanya ngono na watoto wadogo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la TAWIF lililoandaa kongamano hilo, Fransisca Matao alisema jamii inachangia kwa kiasi kikubwa watoto wengi kuwa mashoga kufuatia kuwanyanyapaa na kuwatenga.

Thursday, November 17, 2016

YESU NI MWEMA


YESU NI MUNGU
Leo nitajibu HOJA ya Waislam ya Mungu Ndiye Mwema.
Waumini wa dini ya Kiislam katika Mihadhara mbalimbali ya kidni wamekuwa na tabia ya kutumia aya 18-19 iliyopo katika Luka Sura ya 18, inayo sema Mungu Ndiye Mwema. Waislam wanadai kuwa, katika aya hii, Yesu amekana kuwa yeye si "MWEMA" na kuwa Mungu Pekee ni Mwema, hivyobasi, kukana kwa Yesu kuwa yeye si Mwema kunapinga Madai ya Wakristo kuwa Yesu ni Mungu.
Kwa hivyo utaona kuwa wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu hufundisha jamii kwa kutumia Qurani na Biblia na kusema kuwa eti Yesu amekana kuwa yeye si MWEMA. Fundisho hili la "MUNGU PEKEE NDIYE MWEMA" wanalieneza kwa kupitia Mitandao mbalimbali kama ya Radio, Vijarida, Mihadhara, vitabu na Kanda (cassettes) za Video na Audio. Na hivyo kuwafanya baadhi ya Wakristo kuacha Imani yao na kuingia katika Dini ya Uislamu. Na baadhi ya Wakristo wengine ingawa hawajabadili dini wanaamini hivyo. Swali la muhimu la kujiuliza kwa kila Mkristo, je, ni kweli Yesu alikana kuwa yeye si MWEMA? Nakusihi fuatilia somo hili kwa makini ili kujua Ukweli wa aya hii:
Luka 18.18-19 "Tena mtu mkubwa mmoja alimuuliza Yesu, akisema, Mwalimu Mwema, nifanye nini ili kuuruthi uzima wa milele? Yesu akamwambia mbona unaniita Mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, Naye ndiye Mungu".
Ukitazama kwa haraka haraka namna wahadhiri hao wa Dini ya Uislamu wanavyoifunda hii aya ya Biblia unaweza ukashawishika kuamini hicho wanachokifundisha, lakini ni vyema tukajifundisha kwa undani kadiri majibu ya Yesu kuwa "Mungu Pekee Ndiye Mwema" kisha tuone kama kuna ukweli juu ya hayo mafundisho yao, ya kusema kuwa Yesu kakataa kuwa yeye si Mwema na hivyo kunamfanya kuwa yeye si Mungu.
Haya tuanze utafiti wetu.
Katika hii aya hapo juu, je, Yesu katoa jibu au kauliza swali? Hapa tunaona aya zinatufundisha waziwazi kuwa Yesu aliuliza swali na si kukana kuwa yeye si Mwema.
NUKUU: Yesu akamwambia Mbona waniita Mwema? Hapa Yesu kamuuliza swali, Yule mtu aliye muita “MWALIMU MWEMA” na si kukana kuwa yeye si “MWEMA" kama wanavyo fundisha Wahadhiri wa dini ya Kiislam katika Mihadhara yao ya kidini.
Baada ya Yule mtu kushindwa kujibu kwanini alimwita Yesu "Mwalimu Mwema". Yesu akasema yafuatayo:
Hakuna aliye Mwema ila mmoja, Naye ni Mungu. Je, Yesu alipo sema haya maneno alikana kuwa yeye si Mungu?
WAISLAM WANAKUBALI KUWA ALIYE MWEMA NI MUNGU TU.
Je, kuna sehemu yeyote ile katika Biblia ambayo Yesu anajiita yeye Mwema. Sasa tumsome Yesu katika Injili ya Yohana 10:14
Yesu anasema yafuatayo:
"14 Mimi ni Mchungaji MWEMA: ninawafahamu Kondoo wangu nao wananifahamu"
KATIKA YOHANA YESU ANAJIITA MWEMA.
Sasa basi, kufuatana na Waislam kukubali kwao kuwa "MUNGU PEKEE NDIE MWEMA" na Yesu kujiita Mwema katika Injili ya Yohana 10:14. Leo hii Yesu amewajibu Wahadhiri wa dini ya Kiislamu kuwa yeye ni Mwema na hivyo hii adhama ya Mwema inamfaya kuwa yeye ni Mungu, kutokana na Luka 18: 18-19. "Mungu Pekee ni Mwema".
Ni matumaini yangu kuwa leo hii umeweza kujua kwa undani maana ya "Mungu Pekee Ndiye Mwema" na Yesu alipo sema hayo alikuwa anamfahamisha yule kijana kuwa yeye ni Mungu na yule kijana hakukosea alipo muita MWALIMU MWEMA.
Sasa wapi aya Allah anasema yeye ni Mwema?
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

UKIMWI "HIV/AIDS" WASHAMIRI ZANZIBAR


Utafiti uliofanywa na "AIDS CONTROL PROGRAM ZANZIBAR" unaonyesha kuwa asilimia 56.2 ya watu wanao ishi Unguja wameathirika na ugonjwa huu wa Ukimwi "HIV POSITIVE".
Zanzibar ni kisiwa chenye asilimia 100 Waislam na kinaongoza kwa wagonjwa na au kuwa na watu walio athirika na UKIMWI.
Bwana Hamad Haji alisema kuwa, takwimu zao zinaonyesha kuwa katika kila watu SITA waishio ZANZIBAR mmoja wao ameathirika na UKIMWI.
Utafiti zaidi unaonyesha kuwa, tabia ya watu hawa wa visiwani wa kuwa na wake wengi na kuwa na nyumba ndogo, ndio sababu kubwa inayo usambaza huu ugonjwa.
Kwa takwimu kamili na habri kamili ingia hapa: http://www.zac.or.tz/
Zanzibar is a gateway to the African continent and is also situated along a major corridor for drug trafficking. Around one in six PWID in Zanzibar is infected with HIV according to estimates, but some believe this figure may be higher.14 15 The tendency to have multiple partners, share needles, engage in 'flash-blood' practices and have unprotected sex, place drug users in Zanzibar at high risk of HIV infection.
Statistics on HIV/AIDS in Zanzibar indicate that increase of the deadly diseases is at alarming rate. The manager of AIDS control program in Zanzibar, Mr. Hamad Haji says that a survey conducted by his centre revealed that 56.2 percent of people living in Unguja urban district were HIV positive.

MUHAMMAD AKIRI KUWA BABA YAKE YUPO JEHANNAM

Ndugu msomaji,
Huu ni MSIBA MKUBWA sana kwa Waislam. Muhammad ambaye baba yake anaitwa Abdullah ikimaanisha "mtumwa wa Allah" imethibitshwa kuwa yupo Jehanna/motoni akichomeka.
Haya si maneno yangu na wala mimi simsingizii baba ya Muhammad, bali haya ni maneno ya Muhammad.
Soma uthibitisho hapa.
Imeripotiwa na Anas: Hakika, mtu mmoja alisema: Mjumbe wa Allah, baba yangu yuko wapi? Akasema: Yuko motoni. Alipogeuka kuondoka, akamwita na kusema: Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni. (Sahih Muslim, Kitabu 001, Namba 0398).
Na swali ambalo tungependa wajiulize Waislam ni kuwa, kwa nini baba yake Muhammad, ambaye alikuwa mpagani aliitwa ‘Abdullah’?
Na kwa kuwa ‘Abdullah’ maana yake ni ‘mtumwa wa Allah’, hii ni ishara ya wazi kwamba wapagani wa kipindi cha jahiliyah walikuwa wakimwabudu Allah hadi kufikia kuwapa watoto wao majina kwa heshima ya Allah – kama ambavyo Wayahudi nao walikuwa wakiwapa watoto wao majina kwa heshima ya Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
Kwa mfano:
Yoshua – Yahwe ni wokovu;
Yothamu – Yahwe ni mkamilifu;
Yehoahazi – Yahwe ameshikilia;
Hezekia – Yahwe ametia nguvu;
Elisha – Mungu ni wokovu, n.k.
Jibu liko wazi. Allah alikuwa ni mungu wa kipagani aliyeabudiwa kabla ya Uislamu kuja. Na mungu huyu alikuwa ni ‘mungu mwezi’, yaani ‘al-ilah’. Jina lake jingine aliitwa ‘hubal.’ Mungu huyu wa kipagani aliabudiwa kote mashariki ya kati; wala si kwa Waarabu peke yake.
ZAIDI YA HAPO,
1. Kwanini Muhammad anakiri kuwa baba yake yupo Motoni?
2. Je, huyu Abdullah/abdallah alipata wapi hili jina lenye Allah ndani yake?
3. Je, inamaanisha kuwa Allah ambaye ni mungu wa kipagani alikuwepo kabla ya Muhammad?
Na ndiyo maana baba yake Muhammad, yaani Abdullah, alikoswakoswa kuchinjwa na babu wa Muhammad, yaani Abdul Muttalib. Abdul Muttalib alitaka kumchinja mwanawe huyo kama sadaka kwa Allah. Lakini mjomba wake Abdullah akamwokoa na hatimaye walichinjwa ngamia 100 badala yake. Na ifahamike kwamba machinjo hayo yalifanyikia kwenye kaaba (hili tutaliangalia huko mbeleni).
Tunaambiwa kwamba:
Mshale ulionyesha kwamba Abdullah ndiye aliyetakiwa kutolewa kafara. Kwa hiyo, Abdul Muttalib alimchukua yule kijana hadi kwenye Al-Kaaba pamoja na wembe kwa ajili ya kumchinja. Quraish, mjomba wake kutoka kabila la Makhzum na kaka yake Abu Talib, hata hivyo, walijaribu kugeuza mawazo yake.
Walipendekeza kwamba amwite mwaguzi wa kike. Huyo aliagiza mishale ya uaguzi ichorwe baina ya Abdullah na ngamia kumi … hatimaye idadi ya ngamia ikafikia mia moja. (Ibn Hisham 1/151-155; Rahmat-ul-lil'alameen 2/89, 90).
Ndiyo maana Mungu wa Biblia alikuwa akiwaonya sana wana wa Israeli juu ya tabia za kipagani za jamii zilizowazunguka kuhusiana na masuala ya kuabudu familia ya nyota au jeshi la mbinguni. Kwa mfano, anasema:
….. tena usije ukainua macho yako hata mbinguni, na ulionapo jua, na mwezi, na nyota, jeshi la mbinguni lote pia, ukashawishiwa na kuviabudu, na kuvitumikia, ambavyo Bwana, Mungu wako amewagawanyia watu wote chini ya mbingu zote. (Kumbukumbu la Torati 4:19).
Ikiwa ameonekana katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, upewayo na Bwana, Mungu wako, mtu mume au mke afanyaye yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wako, kwa kuvunja maagano yake, ….. naye amekwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu, au jua, au mwezi, au vilivyo katika jeshi la mbinguni vyo vyote, nisivyoagiza mimi (Kumbukumbu la Torati 17:2-3).
Kwa maana akapajenga tena mahali pa juu alipopaharibu Hezekia baba yake; akamjengea Baali madhabahu, akafanya Ashera kama alivyofanya Ahabu mfalme wa Israeli. Akajiinama mbele ya jeshi lote la mbinguni na kulitumikia. (2 Wafalme 21:3).
Akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Bwana. (2 Wafalme 21:5).
Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. (2 Wafalme 23:5).
… nao wataitawanya mbele ya jua, na mwezi, na jeshi lote la mbinguni, walivyovipenda, na kuvitumikia, na kuandamana navyo, na kuvitafuta, na kuviabudu haitakusanywa pamoja tena, wala kuzikwa; itakuwa ni samadi juu ya uso wa nchi. (Yeremia 8:2).
…. na nyumba za Yerusalemu, na nyumba za wafalme wa Yuda, zilizotiwa unajisi, zitakuwa kama mahali pa Tofethi; naam, nyumba zote ambazo juu ya dari zake wamelifukizia uvumba jeshi lote la mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kunywewa. (Yeremia 19:13).
…. na wale walisujudiao jeshi la mbinguni juu ya dari za nyumba; na hao waabuduo, waapao kwa Bwana na kuapa pia kwa Malkamu (Zefania 1:5).
Katika mwaka 570 BK, mwaka uleule ambao Muhammad alizaliwa, alikuwapo mtawala mmoja wa dola ya Aksum ya Ethiopia ambaye alikaa Yemen. Huyu aliitwa Abrahah al- Ashram. Inaelezwa kwamba alikuwa na wivu na mji wa Makka kwa jinsi ambavyo watu wengi walikuwa wakienda kuhiji (yaani hija ya kipagani), hivyo na yeye naye akajenga kanisa kubwa kule Sanaa, Yemen akitarajia kuvuta watu wengi, jambo ambalo halikutokea.
Matokeo yake, aliamua kwenda kuvamia Makka kwa lengo la kuiharibu kaaba. Alisafiri na watu wake wengi juu ya kundi kubwa la tembo - ndiyo maana hata mwaka ule ukajulikana kama mwaka wa tembo.
Koo za Kiquresh ziliungana ili kujaribu kuikoa kaaba. Abdul Mutaleb (babu yake Muhammad) aliwaambia watu wakimbilie kujificha milimani wakati yeye na baadhi ya watu walibakia karibu na kaaba.
Lakini kwa sababu ya ukubwa na nguvu ya jeshi la yule Abrahah, Abdul Mutaleb alisema:
Mmiliki wa nyumba hii ndiye atakayekuwa Mlinzi wake, na nina uhakika ataiponya dhidi ya kushambuliwa na maadui na hawatawafedhehesha watumishi wa nyumba yake."
Mapokeo yanasema kwamba wakati Abrahah anasonga mbele kuiendea kaaba, lilitokea kundi kubwa la ndege ambao walianza kumdondoshea mawe kama mvua hadi wakamjeruhi. Hivyo, azma yake ya kuiharibu kaaba haikufanikiwa, badala yake akarudi kwake akiwa ameumizwa.
Sasa, swali ni kuwa, kama wakati ule Muhammad alikuwa bado kichanga, na hivyo Uislamu ulikuwa haujaanza; na pale kwenye kaaba inajulikana kwamba kulikuwa na mamia ya miungu ya kipagani; je, Mmiliki wa Nyumba anayetajwa na Abdul Mutaleb ni nani?
Ni wazi kwamba huyu ni mungu wa kipagani, yaani allah aliyekuwa akiabudiwa na kutumikiwa na Abdul Mutaleb, yaani mungu mwezi.
Na swali kubwa zaidi ni kuwa, Quran inasema katika sura Al-Fil (au Tembo) 105:1-5:
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Swali ni kuwa:
Mambo haya yalitokea wakati Uislamu haupo, bali ulikuwa ni wakati wa upagani. Mtumishi wa mungu wa kipagani Abdul Mutaleb alisema kwamba Mmiliki wa Nyumba ile (kaaba) angeitetea.
Je, Mmiliki wa nyumba aliyetajwa na Abdul Mutaleb alikuwa yupi na Mola wako anayetajwa na Quran kwenye sura hii ni yupi? Au tuseme kulikuwa na miungu miwili iliyoshirikiana kumpiga mawe Abrahah na tembo wake?
Abdul Mutaleb hakumjua Allah wa Muhammad, kwa hiyo kwa namna yoyote ile hangeweza kumtaja huyo (kama kweli Allah wa Muhammad ni tofauti na wa Abdul Mutaleb).
Mazingira yote yanaonyesha kwamba mungu mwezi, aliyeabudiwa na Abdul Mutaleb ndiye aliyeilinda kaaba dhidi ya tembo wa Abrahah. Kwa hiyo, aya hii ya Quran haina uwezo wa kujinadi kwamba inamtaja mungu tofauti na huyo!!
Kumbe basi Kaaba ni nyumba ya kipagani.
Kumbe basi baba yake Muhammad yupo Motoni.
Kumbe basi Waislam wote wanao enda kuhiji wataingia motoni.
Kumbe basi Allah ni mungu wa kipagani.
Hakika Uislam ni dini ya wapagani ndio maana Muhamamd alikiri kuwa baba yake yupo motoni.
Nawakaribisha kwa Mungu Mkuu aliye hai, YESU MWOKOZI WETU.
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 17, 2016

KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?


Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri ya Mungu ya kwenye Kumb 17:17?
Jibu: Kumbukumbu 17:17 inasema mfalme asiwe na wake wengi, na kwa kitendo hicho, Suleiman alifanya dhambi. Kuoa wake ilikuwa ni njia ya kuimarisha ushirikiano na falme nyingine, lakini pia ilikuwa ni makosa kutokumtii Mungu. 1 Fal 11:1-4 inasema kuwa Suleiman alifanya dhambi kwa kuoa hawa wake wageni, na kuugeuzia moyo wake kuwa mbali na Mungu.
Hard Sayings of the Bible uk.229 inalitumia jambo hili kwa njia ya kupendeza sana. Ingawa Suleiman angeweza kuweka viwango vya juu kama mfano, alianza kujiona kama hana haja ya kuzuiliwa na Mungu kwa njia hii. Leo hii kama kiongozi wa kikristo anajiona kuwa hayumo kwenye mipaka ambayo Mungu ameiweka kwa Wakristo wa kawaida, kiongozi huyu atakuwa kwenye shida kubwa sana ya kiroho. Kwenye Kurani, hakuna mwanaume anayeruhusiwa kuwa na zaidi ya wake wanne, isipokuwa Muhammad tu, ambaye alitokea kuwa na wake karibu 24 baada ya Khadija, na Masuria kumi na wawili.
Zaidi ya hayo, Muhammad na Waislam wengine walikuwa na wasichana mateka na watumwa, na Kurani inawaruhusu Waislam kufanya tendo la ndoa na wanawake ambao wanawamiliki kwa nguvu ya mikono yao. (Sura 4:24; 23:5-6; 70:29-30; 33:50,52 Abu Dawud juzuu ya 2 na.2150 uk.577)
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom

JE, UNAWEZA KUOKOKA BILA YA KUPITIA YESU?


Je naweza kuingia mbinguni bila kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu?
Jibu: Hapana, huwezi kwenda mbinguni kama unakataa kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Mambo manne ya kuzingatia kwenye jibu hili.
Haki: Mungu ni mwema, Mtakatifu, mwenye haki kwa watu wote (Waebrania 6:10). Mungu huwahukumu watu kwa kuzingatia ufahamu walio nao (Warumi 4:15; 5:13). Abraham hakujua jina la Yesu, lakini alimfuata Mungu na bado aliokolewa kupitia Yesu. (Yohana 8:56, Waebrania 9)
Njia moja tu: Hatuwezi kwenda mbinguni kwa kutegemea haki yetu wenyewe; tunahitaji rehema na neema za Mungu kupitia kwa Yesu. Yesu siyo tu njia ya kwendea kwa Mungu bali pia ni njia pekee ya kwendea kwa Mungu. (Yoh 14:6; 15:5; Matendo 4:12). Njia pekee ya kuifikia mbingu ya Mungu ni kupitia njia ya Mungu.
Ukimkataa Yesu kama Mwana wa Mungu utakuwa umeikataa mbingu: Hata kwa mtu anayeshika dini sana, Farisayo wa kiyahudi, Yesu alisema kuwa kama ukinikataa utakufa kwenye dhambi zako. (Yohana 8:24)
Mungu hutafuta: Mungu hapendi mtu yoyote aangamie (2 Petro 3:9), lakini kama Yeremia alivyowalilia watu wake (Yeremia 13:17; 14:17) na kama Yesu alivyoililia Yerusalem (Luka 19:41-44) na kama Petro alivyowasihi watu waliokuwa wanamsikiliza (Matendo 2:40), Mungu, huwatafuta watu wake kwa haja hiyo hiyo.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.

KITABU CHA DANIEL (SEHEMU YA KWANZA)


Kwenye hili somo tutajifunza kuhusu Kitabu cha Daniel kwa kutumia maswali na majibu. Tutazipitia aya zote na sura zote katika Daniel. Sasa tulia na tuanze kujifunza Neno la Mungu.
SWALI:
Kwenye Danieli, kitabu hiki kiliandikwa nini?
Kitabu cha Danieli kinaelekea kuandikwa muda mfupi baada ya matukio kutokea, kwenye karne ya 6KK, kwa mujibu wa The Bible Knowledge Commentary: Old Testament, uk.1324. Vijana wengi wa Kiyahudi walipelekwa uhamishoni Babeli mwaka 605 KK, na wafafanuzi wengine wa vitabu vya Biblia wanakadiria kuwa Danieli alikuwa na miaka kama 16 hivi. Makadirio haya yanamfanya Danieli awe na umri wa miaka 85 wakati Waajemi walipoiteka Babeli.
Kitabu chenye kutia shaka kiitwacho Asimov’s Guide to the Bible, uk.596 kinadai kuwa Danieli inaweza kuwa iliandikwa mwishoni mwa mwaka 165 KK. Hata hivyo, mwana historia wa Kiyahudi Josephus kwenye Antiquities of the Jews 11.8.5 (karibu mwaka 93-94 BK) anarekodi kuwa wakati Alexanda Mkuu alipoikaribia Yerusalemu (karibu mwaka 333 KK), Kuhani Mkuu Jaddua alikutana naye na alimwonyesha sehemu ya kitabu cha Danieli isemayo kuwa Wagiriki watawashinda Waajemi. Alexanda anaelekea kuwa alipendezwa na maneno haya, na aliachana na Wayahudi.
Origen (mwaka 225-254 BK) alisema kuwa wakati Alexanda wa Macedon alipokwenda Yerusalemu, kuhani mkuu wa Kiyahudi, alikutana naye akiwa amevaa joho lake takatifu. Alexanda aliinama mbele zake, akisema kuwa alimwona mtu mwenye joho kama hilo kwenye ndoto aliyoota, akimfahamisha kuwa anapaswa kuishinda Asia yote. Origen Against Celsus, kitabu cha 4, sura ya 50, uk.565.
SWALI:
Je Kitabu cha Danieli kiliandikwa kwenye karne ya pili (baada ya ushindi wa Alexanda), kwa sababu ya maneno ya Kigiriki yaliyopo kwenye Danieli?
Hapana. Ingawa kitabu cha mwenye kushuku kiitwacho Asimov’s Guide to the Bible, uk.597 kinadai, "sehemu nyingine za lugha zisizoeleweka kwa urahisi zilizotumiwa zinaonyesha kipindi cha Kigiriki tofauti na kile cha uhamisho wa Babeli", kuna maneno matatu tu ya Kigiriki kwenye Kitabu cha Daniel, ambayo ni kidogo kuliko maneno saba ya Kiajemi yaliyomo. Yafuatazo ni maelezo zaidi ya mambo haya mawili.
Maneno matatu tu ya Kigiriki yapo kwenye Kitabu cha Danieli (Dan 3:5, 10, 15), na yote hayo matatu ni majina ya vifaa vya muziki. Hata hivyo, jambo hili halionyeshi kuwa kitabu hiki kiliandikwa kwenye karne ya pili (2 KK), kama maandishi ya Kiashuri yanavyosema kuwa mateka wa Kigiriki walikuwa Mesopotamia kwenye karne ya 8 KK. Isitoshe, kwenye karne ya 7 KK, mshairi wa Kigiriki, Alcaeus wa Lebos, anasema kuwa kaka yake alikuwa kwenye jeshi la Babeli. Vivyo hivyo, The Expositor’s Bible Commentary, juzuu ya 1, uk.247 pia inasema, "Hakuna shaka kuwa majina ya vifaa (vya muziki) kwenye Kitabu cha Danieli yalikuwa na sifa za Kiajemi, na yalifanya na Wagiriki kuwa sehemu ya utamaduni wao na kufanyiwa mabadiliko machache ya kitahajia (herufi). Kwa hiyo, hoja hii ni ya muhimu tena katika kutathmini uandishi wa Danieli."
Maneno sita na nusu ya Kiajemi yaliyomo kwenye Kitabu cha Danieli yanaongelea utawala (Dan 6:1-4, 6-7), na yaliacha kutumika karne moja baada ya Himaya ya Kiajemi kuchukuliwa na Alexanda Mkuu. Kama 735 Baffling Bible Questions Answered, uk.193 inavyosema, ". . . Utumiaji sahihi wa Danieli wa maneno haya hauwezi kuelezwa endapo mwandishi alikuwa hafahamiki kwenye karne ya pili na hakufahamu undani wa serikali ya Kiajemi miaka mia tatu kabla ya muda alioishi." (Neno satrap [maliwali] linahesabiwa kuwa nusu, kwa sababu lilikuwa neno la Kimidiani, ambalo baadaye lilichukuliwa na Waajemi pia.
SWALI:
Je Kitabu cha Danieli kiliandikwa baada ya Kitabu cha Sirach, kwani Sirach 47-49 ina orodha ndefu kiasi ya Agano la Kale, isipokuwa Danieli, kama Asimov’s Guide to the Bible, uk.623 inavyosema?
Utawala wa Wamakabia haukuanza hadi mwaka 165 KK. Hata hivyo, kuna mambo manne yenye kutoa ushahidi unaotofautiana na nadharia hii ya karne ya pili.
1. Kwenye Apokrifa (vitabu vya kubuniwa vya dini ya Kiyahudi), 1 Maccabees 2:49-60 inawataja Danieli na vijana wengine watatu kwa namna ambayo inaashiria kuwa Kitabu cha Danieli kilikuwa tayari kimeishaandikwa. Vinginevyo, wasomaji wa 1 Maccabees wangewezaje kumwelewa Danieli na vijana wengine watatu?
2. Wataalamu wa elimukale wamekadiria muda hati ya kale yenye maandiko ya Kitabu cha Danieli ilipoandikwa kuwa ni mwaka 120 KK. Wycliffe Bible Dictionary, uk.436-438 inalitaja jambo hili, ikisema kuwa "linaibua swali kuhusu muda unaodaiwa kitabu cha Maccabean kuandikwa."
3. Uchimbuaji ulifanyika Babeli unaonyesha kuwa maelezo ya Danieli ni sahihi. M. Lenormant anasema, "Kwa kadri maandishi ya kikabari yanavyozidi kufahamika ndivyo haja ya kurekebisha shutuma zilizofanywa kwa haraka na shule ya ufafanuzi wa maandiko ya Ujerumani dhidi ya Kitabu cha Danieli inavyoongezeka" (La Magie, uk.14; nukuu ya 1001 Bible Questions Answered, uk.367).
4. Pia marejeo ya Josephus yaliyokwishatolewa kwenye swali lililotangulia.
USIKOSE SEHEMU YA PILI "Kwenye Kitabu cha Danieli, kuna vitu gani vinavyofanana na sehemu nyingine za Biblia?"
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Shalom

MAANA YA KANISA


Kwanza kabisa neno Kanisa linamaanisha "mkusanyiko wa waamini" kama ule wa Waisraeli chini ya Musa kwenye mlima Sinai walipopewa Amri za Mungu.
Neno hilohilo lilitumiwa na Wakristo wa kwanza kwa ajili yao wenyewe kusema wameshika nafasi ya Israeli kama taifa la Mungu hata wasipokuwa Wayahudi bali watu wa mataifa mengine.
Watu wengi siku hizi wanaelewa kanisa kumaanisha jengo. Huku si kuelewa kibibilia maan ya kanisa.
Neno “kanisa” maana ya asili yatoka kwa neno la Kiyunani ekklesia lili lo na maana ya “kusanyiko” au “walioitwa.” Maana ya asili ya “kanisa” sio ile ya jingo, bali ni watu. Ni kinaya kwamba unapowauliza watu ni kanisa gani wanashiriki, mara nyingi huwa wanajihushisha na jingo. Warumi 6:5, yasema, “…salimia kanisa linalokutana kwa nyumba.” Paulo anaashiria kanisa lilo katika nyumba yao- si jengo la kanisa bali mwili wa washiriki.
Wakristo walipoanza kujenga mahali pa ibada, pakaja kuitwa vilevile "kanisa" kwa sababu ndani yake lilikusanyika Kanisa hai.
Hivyo mara nyingi neno hilo linatumika kwa maana ya jengo, ambalo ni mfano mwingine uliotumiwa na Paulo kuhusu umoja wa Wakristo, ukiwa na Yesu kama jiwe kuu la msingi.
Majengo hayo ya ibada yanaweza kuwa na ubora tofauti hata upande wa sanaa; baadhi yake yanatembelewa na watalii na kuhifadhiwa kwa bidii kwa sababu hiyo.
Kwa namna ya pekee ni muhimu Kanisa kuu la kila jimbo (dayosisi), halafu Basilika na Patakatifu.
Jina hilo lilitumika kwa jumuia mama ya Yerusalemu, kwa kila mojawapo ya jumuia za Kikristo zilizotokana na umisionari wa wafuasi wa Yesu Kristo, na kwa umoja wao wa kimataifa uliotazamwa na Mtume Paulo kuwa Mwili wa Kristo, ukiwa na Yesu kama kichwa chake.
Kanisa ni mwili wa Kristo, ambapo ye ndie kichwa. Waefeso 1:22-23 yasema, “Akivitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.” Mwili wa Kristo umejengwa na wanaoamini katika Yesu Kristo toka siku ya Pentekosti (Matendo Ya Mitume 2) hadi Kristo arudi. Mwili wa Kristo uko na sehemu mbili:
1) Kanisa lote kwa ujumula ambalo ni wale wote wako na uhusiano na Kristo. “Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni Upendo” (1 Wakorintho 12:13). Aya hii inasema yeyote atakaye amini in sehemu ya mwili wa Kristo na ameupokea Roho wa Kristo ni ushaidi. Kanisa la jumla la Mungu ni wale wote ambao wamepokea wokovu kwa imani katika Yesu

WAISLAM WENYE KUIMBA/KUSIKILIZA MUZIKI WATAGEUZWA KUWA NYANI NA NGURUWE.


HUU NI MSIBA MKUBWA SANA KWA WAISLAM WOTE DUNIANI WANAO SIKILIZA MUZIKI AU IMBA MUZIKI.
Muziki ni haraam kutokana na dalili dhahiri tulizopewa katika Qur-aan na Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
وقال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((ليكونن من أمتي أقوام يستحلون الحر و الحرير و الخمر و المعازف، و لينزلن أقوام إلى جنب علم، يروح عليهم بسارحة لهم، يأتيهم لحاجة، فيقولون: ارجع إلينا غدا، فيبيتهم الله، ويضع العلم، ويمسخ آخرين قردة وخنازير إلى يوم القيامة ((رواه البخاري
Na akasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watakuweko watu katika Ummah wangu watakaojaribu kuhalilisha zinaa, uvaaji wa hariri, pombe na MUZIKI. Baadhi ya watu watakuwa pembeni mwa mlima na mchungaji wao atawajia jioni na kuwaomba haja [fulani]. Watasema: “Rudi kesho”. Allaah Atawaangamiza usiku, Atawaangushia milima kisha Atawabadilisha waliobakia wawe nyani na nguruwe na watabakia hivyo hadi siku ya Qiyaamah))[Al-Bukhaariy]
Imaam Abu Haniyfah amesema: “Kuimba (nyimbo, ngoma) ni katika madhambi makubwa ambayo inatakiwa Muislamu kujiepusha nayo haraka”
Khofu zaidi imuingie Muislamu kuwa anaweza kupata adhabu ya kugeuzwa nyani au nguruwe kwa maasi haya kama tulivyoonywa katika Hadiyth ifuatayo:
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watu katika Ummah wangu watakunywa pombe wakiipa jina jengine lisilokuwa hilo, MIZIKI itapigwa kwa ajili yao na watakuweko waimbaji wanawake. Allaah Atawadidimiza ardhini na Atawageuza wawe nyani na nguruwe)) [Ibn Maajah na Shaykh Al-Albaaniy ameipa daraja ya Sahiyh]
GHADHABU ZA ALLAH KUWAANGAMIZA WAFANYAO MAASI HAYA
Vile vile ghadhabu za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ni kali mno za kuangamizwa pindi maasi haya yatakapodhihirika.
عن عمر بن حصيل عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((يكون فى امتى قذف ومسخ وخسف)): قيل يارسول الله ومتى ذلك قال: ((اذا ظهرت المعازف… )) اخرجه الترمذى وصححه العلامه الالبانى
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Kutatokea katika Ummah huu maafa ya kuteremshiwa mawe kutoka mbinguni, kugeuzwa maumbile ya binaadamu [kugeuzwa kufanywa nyani na nguruwe] na mididimizo [ya ardhi]. Ikaulizwa: Ewe Mjumbe wa Allaah, lini yatatokea hayo? Akasema: ((Itakapodhihirika muziki … )) [At-Trimidhy na ameipa daraja ya Sahiyh Shaykh Al-Albaaniy]
SAUTI ZA NYIMBO ZIMELAANIWA DUNIANI NA AKHERA
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((صوتان ملعونان فى الدنيا والاخره مزمار عند نعمه ورنه عند مصيبه ((البزار و صححه العلامه الالبانى
Na kasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Sauti mbili maluuni [zilizolaaniwa] duniani na Akhera; mizumari katika furaha na kuombeleza katika misiba)) [Al-Baazaar – na Shaykh Al-Albaaniy kaipa daraja ya Sahiyh]
Hivyo tumeona kuna umuhimu mkubwa wa kuwakumbusha ndugu zetu waepukane na haramu hii ili wajiokoe na ghadabu za Mola Mtukufu, ghadhabu kali ambazo zinafika kumgeuza mtu awe nyani au nguruwe kama tutakavyosoma katika hizi dalili za wazi wazi zenye uhakika.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
((وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا أُولَئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ))
((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi, ili wawapoteze watu na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha)) [Luqmaan: 6]
Ibn Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema kuhusu Aayah hii “Naapa kwa Allaah hii inamaanisha ni kuimba” [At-Twabariy 20:127]
وعن ابن عباس قال عن آية: ((ومن الناس من يشتري لهو الحديث))، قال :الغناء وأشباهه إسناده صحيح – المحدث: الألباني
Na Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma) pia amesema kuhusu Aayah: ((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi)) “Ni nyimbo na maneno ya yanayofanana (ya upuuzi)” [Isnaad Sahiyh kutoka kwa Shaykh Al-Albaaniy]
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anamwambia Ibliys:
((وَاسْتَفْزِزْ مَنِ اسْتَطَعْتَ مِنْهُمْ بِصَوْتِكَ وَأَجْلِبْ عَلَيْهِم بِخَيْلِكَ وَرَجِلِكَ وَشَارِكْهُمْ فِي الأَمْوَالِ وَالأَوْلادِ وَعِدْهُمْ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلاَّ غُرُورًا))
((Na wachochee uwawezao katika wao kwa sauti yako, na wakusanyie jeshi lako la wapandao farasi na waendao kwa miguu. Na shirikiana nao katika mali na wana, na waahidi. Na shaytwaan hawapi ahadi ila ya udanganyifu)) [Al-Israa: 64]
Hii inamaanisha ni nyimbo kama ilivyo rai ya Mujaahid katika Tafsiyr ya Ibn Kathiyr]
Vile vile Hadiyth zifuatazo zimedhihirisha uharamu wa nyimbo, ngoma na kila aina ya muziki:
عبدالله بن عمرو بن العاص عن رسول الله صلى الله عليه وسلم انه قال: ((إن الله حرم الخمر والميسر والكوبه وكل مسكر حرام ((إسناده صحيح
و في رواية أحمد قال سفيان: قلت لعلي بن بذيمة: “ما الكوبة؟” قال: “الطبل”
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru ibnul ‘Aasw kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Ameharamisha pombe na kamari na kuubah na kila kilinacholewesha ni haram)) [Isnaad yake ni Sahiyh]

Wednesday, November 16, 2016

MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KULA NYAMA ZA FISI NA MIJUSI KAFIRI

Waislam wapo mstari wa mbele na wanasema kuwa eti Nguruwe ni Haran, lakini wamesahau kuwa Torati inakataza kula Ngamia, Fisi, nk.
MUHAMMAD AWARUHUSU WAISLAM KULA NYAMA YA FISI:
Sayyidina Ibn Ammar (RA) alisema kuwa, siku moja alimuuliza Jabir Jbn Abdullah (RA) kuhusu uwindaji wa FISI. Alinijibu na kusema, inaruhusiwa kuwinda Fisi. Nilimuuliza, Je, tunaruhusiwa kula, na akanijibu kuwa Kula Fisi ni Halal (Inaruhusiwa kula Fisi).
Nikamuuliza tena, Je, Nabii wa Allah(SAW) aliruhusu kula Fisi? Jabir r alinijibu na kusema. NDIO, Nabii wa Allah aliruhusu kula Fisi.
[Abu Dawud 3801, T 1798, Ibn e Majah 3085, Ahmedl4456]
9- Kitabu cha HAJJ.
MTUME MUHAMMAD ASEMA KULA NYAMA YA MIJUSI/KENGE NI HALAL.
Sahih Muslim Kitabu 21, 4788 Idadi :
Ibn 'Umar taarifa kwamba kulikuwa na baadhi ya watu na Mtume wa Allah (amani iwe juu yake) miongoni mwa maswahaba wake alikuwepo Sad. Basi ililetwa nyama ya Mjusi na mwanamke miongoni mwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani iwe juu yake) alisema: Ni nyama ya mjusi. Hapo Nabii Muhammad alisema: Kuleni hiyo nyama ya Mjusi kwa kuwa ni halali…
Eti kula Nguruwe ni haram lakini wanakula Fisi na Mijusi
Karibu kwa Yesu aliye hai na Mungu Mkuu,
Mungu awabariki sana,
Katika Huduma Yake,
Max Shimba Ministries Org.
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2015. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

TRENDING NOW