
Ndugu msomaji,
Tunaendelea kujifunza kuhusu Uungu wa Yesu. Quran, Allah, Muhammad na Jibril kwa mara nyingine tena wanakiri kuwa Yesu ni Mungu.
Hii ni sifa nyingine ya Mungu pekee na wala si ya mwanadamu.
Quran 40:2-3 Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye kujua. Anaye SAMEHE DHAMBI na anaye pokea toba, Mkali wa kuadhibu, Mwenye ukarimu, hakuna mungu ila Yeye; marejeo ni kwake.
Quran 40:2-3 Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye kujua. Anaye SAMEHE DHAMBI na anaye pokea toba, Mkali wa kuadhibu, Mwenye ukarimu, hakuna mungu ila Yeye; marejeo ni kwake.
Je, Bwana Yesu alikuwa na sifa hii ya kusamehe dhambi?
Katika tukio moja ambalo Yesu alionesha mamlaka yake ya Uungu kwa kusamehe dhambi na wakuu wa dini walioina hiyo kama kufuru kwani mwenye uwezo wa kusamehe dhambi ni Mungu pekee kwa vile hata wao hawakufahamu mamlaka ya Yesu ni Mungu
Katika tukio moja ambalo Yesu alionesha mamlaka yake ya Uungu kwa kusamehe dhambi na wakuu wa dini walioina hiyo kama kufuru kwani mwenye uwezo wa kusamehe dhambi ni Mungu pekee kwa vile hata wao hawakufahamu mamlaka ya Yesu ni Mungu
Marko.2:5-11 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao, Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu? Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu? Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza), Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.
Hili ni mojawapo ya matendo ya Yesu ***kusamehe dhambi*** aliyotenda kuonesha Uungu wake na mamlaka yake.
Sura ya 4
Ubinadamu wa Yesu na sababu ya kuitwa Mwana wa Mungu toka mamlaka ya Uungu.
Ubinadamu wa Yesu na sababu ya kuitwa Mwana wa Mungu toka mamlaka ya Uungu.
Ndugu mpendwa msomaji tutakubaliana kuwa hilo ni moja kati ya maswali nyeti yanayoulizwa na watu wengi wanao hoji na kutafiti mamlaka haswa ya Bwana Yesu.






