Friday, July 14, 2017

MUHAMMAD ALIKUWA MTUME WA WAARABU PEKE YAO




KUMBE UISLAM NI DINI YA WAARABU.
HUU NI MSIBA MKUBWA SANA.
Katika hii mada ninawaletea ushaidi kuwa Uislam ni dini ya Waarabu peke yao na Muhammad ni Mtume wao.
Waislamu bila kuchoka wamekuwa wakidai kuwa Uislamu utatawala dunia nzima. Katika kufanya hivyo, wao watakuwa wamekwenda kinyume na maneno ya Allah kama yalivyo teremshwa kwenye Qur'an. Kwa hiyo, ni haki kwa kusema wao ni Makafiri.
Quran 10: 47. Na kila umma una Mtume. Alipo wajia Mtume wao walihukumiwa baina yao kwa uadilifu, wala hawa kudhulumiwa.
Angalia hii aya pia:
Quran 14: 4. Na hatukumtuma Mtume ila kwa ulimi wa kaumu yake ili apate kuwabainishia. Basi Allah humuacha akapotea amtakaye, na akamwongoa amtakaye. Naye ni Mtukufu Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Kama aya hizi ni kweli, basi Uislamu si kwa mashirika/ mataifa /ummah yasiyo ya Waarabu. Quran inasema kwamba kila watu wamepokea ujumbe wao kutoka kwa Mungu katika lugha yao wenyewe ili waweze kuelewa na Qur'ani akaishuka kwa Waarabu ili Waarabu waweze kulewa nini Allah anasema.
Dhana hii ya Allah kushusha Kitabu kwa kila lugha ni muhimu sana kwasababu imejirudia mara nyingi na ndio msingi wa hili somo.
Quran 16: 36. Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani. Basi kati yao wapo alio waongoa MwenyeziMungu. Na kati yao wapo ambao ulio wathibitikia upotovu. Basi tembeeni katika ardhi, muangalie ulikuwaje mwisho wa wanao kanusha.
Quran 5: 48. Na tumekuteremshia wewe, kwa haki, Kitabu hichi kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake katika Vitabu na kuyalinda. Basi hukumu baina yao kwa aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao ukaacha Haki iliyo kujia. Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka ange kufanyeni nyote umma mmoja, lakini ni kukujaribuni kwa aliyo kupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo yenu nyote, na atakuja kuwaambieni yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.
Quran 36: 5. Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. 6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
Hizi aya zimekamilka na kueleza kiuwazi kuhusu kuja kwake kwa Waarabu pekee. Allah katika Koran anasema kwamba kila watu wamekuwa na Mtume wao wenyewe ambao aliwaonya katika lugha zao wenyewe, na kwamba amemtuma Muhammad kwa wale ambao bado hawajaanza mwongozo wowote, na ambao baba zao hawakuonywa, yaani Waarabu. Kwa njia hii watakuwa hawana udhuru wowote na hawezi kusema, lakini hatukuwai kupokea ujumbe wowote.
Endelea kusoma Koran hapa chini:
Quran 6: 156. Msije mkasema: Hakika mataifa mawili kabla yetu yameteremshiwa Kitabu; na sisi tulikuwa hatuna khabari ya waliyo kuwa wakiyasoma. 157. Au mkasema: Lau kuwa tumeteremshiwa sisi Kitabu tungeli kuwa waongofu zaidi kuliko wao. Basi imekufikieni bayana kutoka kwa Mola wenu Mlezi, na uwongofu, na rehema. Basi nani aliye dhaalimu mkubwa zaidi kuliko yule anaye kanusha Ishara za Mwenyezi Mungu, na akajitenga nazo? Tutawalipa wanao jitenga na Ishara zetu adhabu kali kabisa kwa sababu ya kujitenga kwao.
Quran ni wazi ilitumwa kwa Waarabu. Wale ambao si Waarabu hawawezi kuielewa Koran, hayo ni maneno ya Allah. Waislamu wanasisitiza kuwa hakuna tafsiri ya Qur'ani inaweza kuwa sahihi. Hivyo, haiwezi kamwe kuwa wazi kwa mashirika yasiyo ya Waarabu na haikutumwa kwa mashirika/ummah yasiyo ya Waarabu.
Uthibitisho mwingine kuwa Qur'ani ilitumwa tu kwa ajili ya Waarabu ni katika mistari ifuatayo hapo chini:
Quran 26: 198. Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu, 199. Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
Kama ambavyo Waarabu wana haki ya kuto amini kitabu chechote kile kilichotumwa kwa lugha ambayo si yakwao, ikimaanisha Kiarabu, vivyo hivyo, mashirika yasiyo ya Waarabu nao wana haki ya kuto iamini Koran, kitabu kilichoandikwa kwa lugha ya Kiarabu. Ndio kwasababu Koran inasema Allah atatuma mjumbe kwa kila lugha ili wao wenyewe kwa wenyewe waweze kuelewa.
Kuhakikisha hakuta kuwa na kutokuelewana, Allah anashusha hii aya 05:19 Quran: Enyi Watu wa Kitabu! Bila ya shaka amekujilieni Mtume wetu akikubainishieni katika wakati usio kuwa na Mitume, msije mkasema: Hakufika kwetu mbashiri wala mwonyaji. Basi amekujieni mbashiri na mwonyaji. Na Mwenyezi Mungu anao uweza wa kila kitu.
Kwa mujibu wa Qur'an watu wote wamepokea ufunuo. Aya ya hapo juu inasema Qur'ani ni kwa wale ambao kamwe hawakupokea ufunuo, iliwasije kusema, `kuwa sisi hatuja wai kutumiwa mbashiri na hakuna mjuonyaji aliye tumwa kwetu'.
Jambo hili ni wazi, lakini Allah anataka liwe wazi hata na kwa asiye na ufahamu wowote ule aelewe kuwa Koran ilitumwa kwa Waarabu pekee kwa kuzitaja sehemu halisi za kijiografia ambazo Muhammad alitumwa kama Mtume wa Allah.
Leo, tumejifunza kuwa, Koran ilitumwa kwa Waarabu pekee na si kwa Mataifa yote. Sasa, nina uhakika baadhi ya Waislamu wanaweza kuleta aya nyingine zinazosema kwamba Uislamu ni kwa wanadamu wote. Kama Waislam watafanya hivyo, basi waelekuwa kwa kufanya hivyo ni kuthibitisha kwamba aya hapo juu ni za uongo.
Ama Quran ni pakiti ya uongo na utata au ni tu kwa Waarabu wa Makkah na jirani yake kama alivyo sema Allah ambaye ni mungu wa Waislamu.
Katika huduma yake,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Copyright © Max Shimba Ministries 2013

UCHAWI NDANI YA UISLAM

No automatic alt text available.


Uislam umekuwaa na imani Iliyojidhihirisha katikaa kuamini ushirikinaa,mizimu na majini/mapepo.siku Moja nilipoangalia Tv nilishangaa kuona maalim Hassan akifundishaa uchawi dhahiri,akifundishaa namna ya kuyatumia majini kufanya kazi unayotaka,kiukweli niligadhibishwaa kuonaa uchawi huu ukifundishwà wazi bilaa wasiwasi wowote!
Naomba nimnukuu maalim Hassan katika fundisho lake moja"VITU VINAVYOHITAJIKA WAKATI WA KUWAITA MAJINI:
MAANDALIZI.
Kwa mwenye kutaka kumuita Jini na kumtumia ahakikishe anazingatia mambo ya muhimu katika kutayarisha na kutafuta vifaa muhimu kwa ajili ya shughuli za kumuita jini.
Unatakiwa uwe na vifaa vifuatavyo
1. Fimbo maalum
2. Unyoya wa kwenye Bawa la kulia la Bata Mzinga
3. Kitambaa safi cha hariri
4. Mafusho
5. Njiwa (damu ya njiawa"
Je huu si uchawi uliopo ndani uislamu,je kuna utofauti gani kati uislam na uchawi?
Katika moja ya mambo yenye kutushangaza sana sisi Wakristo hatuchangamani kabisa na majini au Mashetani wala hatuna uhusiano nayo, Kinyume na hilo Waislamu wana uhusiano mkubwa na wakaribu na majini na mashetani na kwa ujumla Masheikh na Maalimu wanaotumia quran kutibu au kulaani watu (al-Badir) hutumia nguvu za majini ambazo ni nguvu za giza, Muhamad pia alitumia nguvu hizo za giza, Kuna wakati ambapo wakristo kutoka Narjan kusini mwa Arabia walimtembelea Muhamad kujadili mambo ya dini kwa siku kadhaa baada ya kuwa wakristo wamekataa kusilimu, Muhamad akasema “njooni hadharani tukusanyike pamoja wana wetu na wana wenu,wanawake zetu na wanawake zenu,sisi na ninyi kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana kwa Mungu iwashukie waongo! (surat al Imran 3:61).Muhamad alitaka kuwalaani wakristo kwa jina la allah na wakristo walaani kwa jina la Yesu kuona nani wenye nguvu,Wakristo walikataa kwani hawakuitwa kulaani bali kubariki tu.
JE SHETANI ANAHUSIANO GANI NA MAJINI?
Allaah Anasema:
"Basi wakamsujudia isipokuwa Iblisi; yeye alikuwa miongoni mwa majini.
shetani/Allah alikuwa miongoni mwa majini(al-kahf 18;50) hivyo shetani ni jinni na jinni ni shetani,quran inafundisha kuwa viumbe hawa waliumbwa kwa ndimi za moto(al-Hijir 15;26-27,ar –Rahman 55:14-15) woote wanaofanana na shetani woote wamezaliwa na shetani woote kazi zao zinafanana,Hivyo majini yana nafasi kubwa sana katika uislamu kujaribu kuwatenga majini na mashetani ni kiini macho tu kwani majini yalisilimu (surat 72;1-14)ingawa kuna kundi lingine halikuslimu,Hata hivyo Allah aliwatumia woote katika kazi mbalimbali mfano kumsaidia Sulemani katika kazi zake mbalimbali za ujenzi,kumletea johari na vito vya thamani toka baharini,kumjengea nk.Soma (Surat al anbiyaa 21;81-82)Allah alikuwa mlinzi yaani msimamizi,Allah pia huwatumia majini kufarikisha watu aliwatumia huko Babeli na kufundisha watu uchawi hawa mashetani huitwa Haruta na Maruta soma (al-Baqara 2;102) aidha katika namna ya kushangaza Allah alimletea kila nabii maadui aliowatuma mwenyewe yaani majini na Mashetani (surat al anam 6;112 na al-Hajj 22;52).
Baadhi ya Madhehebu kama ahmadiyya walipogundua kuwa majini ni mashetani na mashetani ni majini walianza kukataa dhana hii na shehk Farsiy anawakanusha vikali katika ufafanuzi chini,Waislamu wanatambua kuwa majini ni ndugu zao na ndio maana moja ya mashart ya swala katika kumalizia kikao cha mwisho kiitwacho (atahiyat) lazima kwa kila Muislamu asalimie pande zoote mbili yaani kwa kugeukia kushoto na kulia,kushoto ni kusalimia muislamu mwenzako na kulia ni kusalimia kundi kubwa la majini ambao hujumuika na waislamu katika swala (arshad-alMuslim) hii ni lazima hata kama mwislamu atakuwa pekeyake wakati wa swala kwani majini hujumuika nae.Aidha muhamad anasema kila muislamu anapozaliwa anapata ulinzi toka kwa majini na mashetani (soma al-muslim,Miskat),
Majini yana ufahamu mkubwa sana wa quran na uislamu, yameslimu Muhamad alipokwenda kwa majini na kuanza kuwauliza mambo ya uislamu majini yalijibu vizuri kuliko wanadamu soma (surat al ahqaf 46;29-30) soma pia ufafanuzi wa aya hiyo chini katika quran ya Farsiy.
KWANINI MAJINA YA KISLAMU HUFANANA NA MAJINA YA MAJINI?
Nilitafakari jambo kwa makini kwanini majina ya kislamu hufanana na majina ya majini,kama maimuna shwaibu, Hassan, Fatuma, Muhammed, Athuman, Sharif, Farid, nk.
Kwa ujumla hutakutana na jinni ambalo lina jina la kikristo majini yoote yana majina ya kiislamu anaeleza Desmon Mkumbo mmoja ya wataalamu wa huduma ya biblia ni jibu Tanzania.Majini au mapepo pia huhubiri Uislamu kwa nguvu na huhusika kusilimisha watu ukiwa na ugonjwa au pepo limekupagaa ukipelekwa kwa sheikh au maalim akusomee duwa utapewa masharti ya kubadili dini,jina, kusilimu au kuswali haya ni maagizo ya majini Mwenye masikio na asikie!.
Mtume Muhammad alikuwaa anatumia Uchawi?
Muhamad alikwenda Yerusalem akafika pale lilipokuwa Hekalu la wayahudi wenyewe waislamu hupaita Baittil maqdis kwa usiku mmoja kwa kutumia mnyama aitwae “Buraq” Mnyama huyu ni jinni lenye sura ya mwanamke mzuri na mwili wa Farasi (Soma kitabu Maisha ya nabii muhamad uk 28 kifungu cha mwisho) jambo hili lilimfanya akataliwe zaidi na watu wa makka wakisema ni MCHAWI MKUBWA na hawako tayari kumuamini mchawi,Hizi ni khadithi chache tu ambazo zinatudhihirishia kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya Uislamu na Majini, Mashetani na mambo ya uchawi au ushirikina katika uislamu tutachambua mtazamo wa quran kuhusu viumbe hao ikiwa ni pamoja na mashetani,malaika na majini. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) ametufundisha dua ya kusoma kabla ya mtu kuigia chooni, akasema:
Ukweli ni kwamba uislamu unajua vinzuri majini vinzuri na namna ya kuwatumia katika shghuli mbalimbali za kiuchawi...
Mtume anasema "
Mmoja wenu anapoingia chooni basi aseme;
"Allaahumma inniy audhu bika minal khubuthi wal khabaaith."
Muhammad anafundisha namna ya kujikinga na wachawi unapoingia Chooni.....lakini jambo linaloshangaza
muislamu ameoneka kumtii shetani anapoingia chooni kwa kuomba msamaha kwa mapepo ya kike na kiume maana baadhi ya mapepo huishi chooni!!!
Je uislamu siyo dini ya shetani????Tafakari.
Katika Biblia tunaona kipindi Yesu alipotwaa mwili na kuja duniani, hao majini, au mashetani au Ibilisi au Mapepo wachafu yalimfahamu na yalianza kulalamika mbele zake.
Math 8:28-31 “ Naye alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo (Majini) walikutana naye, wanatoka makaburuni wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama wakapiga kelele wakisema tuna nini nawe mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya muhula wetu………………. (MK 5:1-9).
Majini hayo yanafahamu kuwa Yesu ndiye atakayewahukumu ila yalichoshangaa ni kwamba mbona amewahi kabla ya kipindi chenyewe cha yeye Yesu kuyahukumu kwenda Jehanamu ya Moto?
Yesu alikuja duniani ili kumwokoa mwanadamu kutokana na mateso ya hayo majini au mashetani kwa sabahu katika Uf. 12:12 Malaika Mikael alipokuwa anawafukuza hao malaika waasi yaani hao majini au mashetani alisema OLE WA NCHI NA BAHARI ndiyo maana Yesu ilibidi aje duniani kupambana na huyo shetani, Joka, Ibilisi kwa niaba yetu maana sisi tusingeweza na wale, majini walisema kumuambia Yesu ukitutoa tuache tukawaingie nguruwe na ngurume wale wapatao 2000 waliona bora kufa baharini kuliko kuishi na viumbe hivi majini au mashetani miilini mwao na hivyo kutimiza ujumbe wa malaika Mikaeli “ Ole wa nchi na bahari”. Baharini ni sehemu mojawapo ambapo majini huishi.
Je Nguruwe ni Bora kuliko mwislamu?
Itaendelea sehemu ya pili.
Tafakari
Hoji mamboo
Chukua Hatua.
Yesu anakupenda
Na Shèikh Mstaafu Èden Hazard

KWANINI TUNAKULA NGURUWE? (SEHEMU YA KWANZA)

Image may contain: one or more people and text


Kwa taarifa yako Allah ameruhusu kula Nguruwe.
* Mafundisho ya Quran Kuhusu Nyama ya Nguruwe;
Pamoja na kuwa waislamu wanatushutumu sana wakristo kuwa tunakula Nguruwe Quran inajikanganya sana katika swala zima la kuliwa ama kutokuliwa kwa mnyama huyu ni muhimu kuangalia, kwa ufupi hakuna aya maalumu katika Quran inayoharimisha na kukataza kula Nguruwe.
Quran inasemaje kuhusu nyama ya nguruwe;-
Quran inaeleza wazi kuwa Mungu aliharimisha Vitu vizuri (akiwemo Nguruwe) kwa Wayahudi kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, yaani Mwenyezi Mungu aliwakataza kula nyama hii kama sehemu ya kuwahukumu Wayahudi na si vinginevyo soma (Surat an-nisaa 4;160).
Quran inasema hivi katika aya hiyo “Basi kwa dhulma yao hao Mayahudi tuliwaharimisha vitu vizuri walivyohalalishiwa na vilevile kwa sababu ya kuzuiliwa kwao watu wengi na njia ya mwenyezi Mungu”
ni aya iliyo wazi kuwa wayahudi walizuiliwa vitu vizuri kwaajili ya dhuluma Mungu alitaka kuwahukumu kwa kuwanyima baadhi ya vitu vizuri Quran inakiri wazi kuwa Nguruwe ni kitu kizuri Umeona?
Quran inafundisha kuwa Yesu alikuja kuhalalisha yale yaliyo harimishwa (Surat al-Imran 3;50).
Quran inasema haya katika aya hii “ Na nitakuwa Msadikishaji way ale yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati na nimekuja ili NIKUHALALISHIENI yale MLIYOHARIMISHWA na nimekujieni na hoja Kutoka kwa Mola wenu kwa hiyo mcheni mwenyezi Mungu na NITIINI”
Hayo ni meneno ya Yesu Ndani ya Quran ikionyesha wazi kuwa Yesu alikuja kuhalalisha yale yaliyoharimishwa katika Tourati na anatuamuru kumtii, ni wazi kuwa Yesu ameruhusu kula Nguruwe na Quran pia
Quran imehalalisha kula vilivyo vizuri walavyo waliopewa kitabu (Al-maida 5;3-5).
Sura hii almaida maana yake maswala ya meza inasema hivi “……..Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. Na chakula cha wale waliopewa Kitabu ni Halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao…”
Hii ni aya iliyo wazi inayoruhusu kila muislamu kula vyakula vya wakristo na wayahudi na sisi kula vyao umeona!
Quran ina kigugumizi kwa vile hakuna katazo la moja kwa moja kuhusu kutokula Nguruwe yaani inakataza kula Nguruwe na wakati huohuo inaruhusu endapo utashurutishwa na njaa (Al-baqara 2;173) au kama una dharula waweza kula hapa ndipo quran inapojikanganya ni muhimu kujiuliza imekataza au imeruhusu? Na dharula hii ni ipi? Quran inajibu kuwa dharula hii ni njaa (Al-an nam 6;145)Quran inasema kula bila kupita kiasi hili ni jema kwani Biblia inafundisha kuwa hata kama una njaa kiasi gani kula kupita kiasi hata kama si nguruwe chakula chochote ni ulafi ni dhambi (Galatia5;21)
Quran inafundisha kuwa Mungu hakuharimisha chochote ila wazee wa kiyahudi waliharimisha kwa mapokeo yao tu (Al-an nam 146).
Quran inatahadharisha kuwa makini kumzulia Mungu uongo kuwa ameharimisha kitu kumbe hakuharimisha chochote (An Nahl 16;116).
Quran inaamuru uletwe Ushahidi kuwa ni wapi Mungu ameharimisha wanyama? Soma (Al an- am 6;150).
Hivyo ukisoma kwa makini Quran utaona hakuna kilicho haramu ndugu zangu waislamu kula nguruwe ni ruksa ila kiasi tu usizidishe ndivyo Quran inavyofundisha kama husadiki pale uwanja wa sabsaba Tanga kwa Minchi waislamu wenzenu hujumuika kula kiti moto kila iitwapo leo kwani wameelimika na wamegundua siri hii. Mimi sikushawishi ila nina kuweka huru kama mwalimu wa kweli ya Mungu “….. Mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru.
Mafundisho ya Agano jipya kuhusu vyakula (Nguruwe).
Biblia inasema mafundisho yoyote yanayokataza mtu kula vitu Fulani ni mafundisho ya Mashetani (1Timoth 4;1-5). Ndio maana waganga wa kienyeji mtu anapokwenda kuaguliwa hukatazwa kula baadhi ya vitu Mungu sio Mganga wa kienyeji. Na wanaomwamini hawana sheria ya kuwazuia nini cha kula au kutokula.
Biblia inasema hakuna kitu najisi kwa mtu asiye najisi lakini kitu Fulani ni najisi kwake yeye aliye najisi (Rumi14;14)Biblia inafundisha kuwa kula au kutokula hakuongezi utakatifu wala hakuzuii tamaa za mwili (Kolosai 2;16-23) hivyo hatupaswi kujitia katika mambo ya kutunga tu ya mtu,au akilizake na maono ya wanao abudu malaika kumuabudu Mungu hakuji kwa kula au kutokula aina fulani ya vyakula bali katika moyo safi (Math 5;8).
Biblia inafundisha kuwa unajisi wa mtu hautoki nje bali ndani ya mtu pia Yesu alitakasa vyakula vyoote (Marko 7;14-16,17-19)
Paulo mtume alifundisha kuwa chakula ni kwa tumbo tu na si mambo ya rohoni.
(1Koritho 6;13). Hoja ya Pepo waliotolewa na Yesu kuwaingia nguruwe je ina maana gani?
USIKOSE SEHEMU YA PILI........
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Shalom.

ISIS WALIPUA MSIKITI WA KIHISTORIA NCHINI IRAQ.

No automatic alt text available.


Jeshi nchini Iraq limethibitisha kwamba wanamgambo wa dola ya kiislam Islamic State wameulipua msikiti mkuu wa Al-Nuri ulioko mjini Mosul .
Msikiti huo unaaminika ndimo kiongozi wa wanamgambo wa ISIS Abu Bakr al-Baghdadi alitoa hotuba yake miaka mitatu iliyopita wakati alipokuwa akitangaza "ukhalifa" mpya.
Wakati hayo yakijiri, wanamgambo hao wa ISIS wao wanadai kwamba ndege za jeshi la Marekani ndiyo zilizo zilizousambaratisha msikiti huo.
Mapema leo, Kamanda wa majeshi ya Iraq aliiambia BBC kwamba walikuwa mita kadhaa kutoka msikitini hapo, walipokuwa katika harakati zao za kusonga mbele kwenye mapambano lengo likiwa ni kuteka ngome kuu ya wanamgambo hao wa kiislam wa Is nchini Iraq.
Source: BBC Swahili.

VIRGIN MARY MASJID

Image may contain: outdoor


KUMBE BIKIRA MARIA YUPO JUU KULIKO WANAWAKE WOTE WA KIISLAM. Quran 3 aya 42.
Ndio maana kwenye Quran hakuna majina ya wake wa Muhammad wala jina la mama yake Muhammad.
Halafu utakuta Muislam anasema Yesu sio Mungu. Thubutu.

MSIKITI MPYA WAFUNGULIWA UJERUMANI IMAM NI MWANAMKE

Image may contain: one or more people and people standing


Labda kwa yule ambae hana khabari, huu ni msikiti uitwao Ibn Rushd-Goethe huko Berlin Ujerumani.
Ni msikiti mpya unaojumuisha wanawake na wanaume pamoja.
Juzi ijumaa ndo umefunguliwa rasmi na ibada zitakuwa zinaendelea kwa mtindo huohuo.
Imam wa msikiti huu ni mwanamke kwa jina anaitwa Ani Zonneveld,
Wakati wa ufunguzi wamealikwa baadhi ya viongozi wa kidini wa kiyahudi na kinasara ili kushuhudia rasmi ufunguzi huo.
Aliskika imaam huyo mwanamama akitoa hutbah....
Haya ni masikitiko kwa hakika

KWANINI TUNAKULA NGURUWE? (SEHEMU YA PILI)

Image may contain: one or more people and outdoor


Kiti moto mdudu mwenye mjadala mkali duniani.
Biblia inasema hivi katika Wakolosai 2 : 16 ‘Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;’ Kwa tafasiri nyepesi biblia inasema usimuache mtu yeyote akuhukumu ‘do not let anyone judge you’ kwa habari ya nunakula nini unakunywa nini, au kama huandami mwezi au kushika sabato mtu asikuhukumu, maana yake ni kuwa mafundisho yoyote duniani ya imani yoyote yanayokataza ule nini usile nini ni mafundisho ya Mashetani, sisi wakristo hatuna miiko, ukienda kwa wapunga pepo wanganga watakupangia ule nini usile nini haya ni mafundisho ya mashetani ona 1Timotheo 4 1-5 Biblia inasema :-
1. Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2. kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 3. wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli. 4. Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani; 5. kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.’
Ndugu zangu unaweza kuona maandiko haya yako wazi kabisa kwamba kumzuia mtu ajiepushe na chakula fulani ni mafundisho ya roho zidanganyazo yaani mapepo na mashetani biblia iko wazi kuwa kila kiumbe kilichoumbwa na Mungu ni kizuri kama ukikipkea kwa shukurani kwa vile vimeatakaswa na neno la Mungu !
Wakati najenga Msingi huu napenda pia nikufahamishe vema somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo :-
Ufahamu kuhusu Nyakati saba za Maongozi ya Mungu.
Mafundisho ya Quran kuhusu Nyama ya Nguruwe.
Mafundisho ya Agano jipya kuhusu kula Nguruwe.
Ufahamu kuhusu nyakati saba za maongozi ya Mungu.
Moja ya sababu zinazopelekeabaadhi ya watu kupinga aina Fulani ya vyakula ikiwemo nyama ya nguruwe ni kuto kuyajua maandiko na kutofahamu juu ya nyakati saba za Maongozi ya Mungu ambapo Mungu aliongoza kwa Sheria tofauti tofauti, ikumbukwe kuwa Mungu ndie mtunga sheria na huweza kupanga au kupangua sheria “Amendments” kulingana na nyakati Yeye mwenyewe, kama apendavyo, Kama bunge linavyoweza kupitisha sheria na hatimaye kuibadili wakati Fulani kama wapendavyo ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu, Mungu ameiongoza Dunia hii kwa nyakati tofauti tofauti zipatazo saba, maeneo sita kati yake yametimizwa na eneo la saba litakuwa ni wakati ujao
Nyakati za Maongozi ya Mungu kibiblia Zimegawanyika katika Maeneo makuu saba yafuatayo
Innocence Period-Hiki ni kipindi cha uumbaji mpaka anguko la Adamu(mwanadamu)
Concience Period-Hiki ni kipindi cha dhamiri mpaka gharika
Human Government Period-Hiki ni kipindi cha kujitawala mpaka wakati wa Ibrahimu
Promise au Patriach Period-Hiki ni kipindi cha mababa mpaka wakati wa Musa.
Dispensation of Law- hiki ni kipindi cha sheria ya Musa.
Dispensation of Grace-Hiki ni kipindi cha neema au wakati wa Mataifa.
Escatological times-Kipindi cha mambo yajayo (Dhiki kuu, hukumu ya mataifa, utawala wa miaka 1000,vita ya gogu na magogu, ziwa la moto, Mbingu mpya na nchi mpya.)
Katika vipindi hivi vyoote Mungu aliweka sheria mbalimbali za kuongoza vipindi hivyo,Mtu asipofahamu vizuri anaweza kuchanganya mambo katika vipindi hivyo Mungu aliweka au kubadili sheria zake kulingana na nyakati hizo na makusudi yake aliyoyakusudia kwa wakati huo.
Mfano sheria kuhusu Vyakula;-
Kipindi cha uumbaji mpaka anguko la Adamu (Innocence Period).
Sheria ilikuwa moja tu wasile tunda la ujuzi wa mema na mabaya tu wakati huu mwanadamu hakula nyama (Mwanzo 2;16-17,1;28-30) Mungu aliweka sheria hii moja kwa sababu Adamu na Eva walikuwa Peke yao na Mungu aliwapa vitu vyote hebu jaribu kuwaza kama Mungu angesema Usizini, usiibe hizo sheria pale Bustanini zingemuhusu nani wakati Adam yuko peke yake na mkewe
Kipindi cha dhamiri Anguko mpaka wakati wa gharika Gharika (Concience period.)
Wakati huu Mungu aliamuru wale vitu vyoote isipokuwa Damu tu (Mwanzo 9;1-4).Baada ya gharika Mungu alimruhusu Nabii Nuhu na wanawe kula kila kitu yaani vitu vyote isipokuwa Damu tu yaani lazima damu ya mnyama imwagike unapotaka kumla, soma biblia yako Mwanzo 9: 1-4 waliruhusiwa kula kila kitu yaani vyote akiwemo Yule mdudu Nguruwe!
Wakati wa sheria ya Musa (Mungu aliamuru wale baadhi ya vitu na baadhi vilikatazwa).
hii ilikuwa ni kwa sababu za kiafya na kutafuta utii wa Israel, baadhi ya vitu vilivyokatazwa ni pamoja na Ngamia, Sungura, Nguruwe, Kambale, Taa, Pweza, Ngisi, n.k. Mungu aliwakataza WAYAHUDI peke yao wasile baadhi ya wanyama na samaki wote wasio na Magamba na wanyama wasio na kwato zilizopasuliwa kati, au wenye kwato zilizopasuliwa kati lakini hawacheui soma (Walawi 11;1-47).
Wakati wa Neema,
Wakati huu Mungu aliamuru kuliwa kwa vitu vyoote isipokuwa damu ambayo kibiblia imekatazwa milele. ( Luka 17;10,1Koritho 10;25-27,Kolosai 2;16,1Timotheo 4;1-5). Wakati wa neema ndio wakati huu wa agano jipya wakati huu tunaruhusiwa kula kila kitu bila kujali wala kuulizauliza soma maandiko yale juu.
Tatizo kubwa la waislamu ni kutokujua nyakati hizi za maongozi ya Mungu na Sheria alizoweka, wanachanganya mambo.
Aidha katika namna ya kushangaza waislamu wanaona Nguruwe tu kuwa ni haramu, huku wamesahau kuwa Mungu alikataza hata ngamia ambao mara nyingi huchinjwa na waislamu wakati wa iddi alhaji. wavuvi wengi wa pwani ni waislamu mara nyingi huvua taa, pweza na ngisi, Mtu anayeamua kuishika sheria na ashike yoote na asiyedumu katika yoote amelaaniwa (Galatia 3;10). Wanyama wengi miongoni mwa waliokatazwa wanahitilafu za kiafya kama wasipoandaliwa vema mfano Nguruwe ana tegu wengi katika nyama yake pia huharibika kwa Haraka nyama yake inapokaa zaidi ya wakati hivyo kutokana na mazingira ya jangwani walikokuwa wanasafiri Israel isingelikuwa vema kuruhusiwa kutumia aina hizi za nyama. Mungu aliwapa sheria hii Wayahudi peke yao wakiwa chini ya nabii Musa. Baada ya kuyaelewa haya sasa hebu tuangalie Mafundisho ya Quran kuhusu Nguruwe!
=====> USIKOSE SEHEMU YA TATU..........
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

LIWATI NA USHOGA ULIVYOSHAMIRI VISIWANI ZANZIBAR

Image may contain: text


Utafiti uliofanyika huko Zanzibar kuhusu Hali ya Liwati na Ushoga imeelezwa kuwa asilimia 25 ya wanawake wanafanya mapenzi kinyume cha maumbile ama na waume zao au na wanaume wengine kama njia ya kukimbia kupata ujauzito na mambo mengine.
Takwimu hizo zilitolewa na Katibu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar kutoka wilaya ya magharibi, Sheikh Nassor Hamad Omar, wakati akiwasilisha ripoti ya awali ya utafiti wa kamati ya kupambana na vitendo vya liwati katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Tunguu, kwenye kongamano la vijana kuhusu udhalilishaji wa kijinsia na mimba za mapema.
Alisema takwimu hizo zimekusanywa kutokana na utafiti uliofanywa na Jumuiya ya Maimamu (JUMAZA) katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.
Na sababu ya kufanya hivyo, ama wanawake hao wanaogopa kupata ujauzito hasa wale ambao bado hawajaolewa lakini wako kwenye mahusiano yasio rasmi (Ndoa) na hata wale walioko kwenye ndoa.
Aidha utafiti huo umegundua watoto wengi wenye umri wa kuanzia miaka 9 hadi 20, wanaingizwa katika vitendo viovu ikiwemo liwati na usagaji.
Leo tangia ripoti hiyo itolewe adharani, japokuwa swala ili limekuwa likijulikana sana na kila mtu akiulizwa anajuwa kuwa miji ya Zanzibar maswala ya Liwati yapo, japo yanafungiwa macho.
Kama ilivyo kawaida ya Wazanzibar wengi, hata ili laweza kuwa limeletwa na Wabara, maana Zanzibar kila ovu limekuwa ni jambo ambalo asili yake ni Bara. Wizi umetoka Bara, Ulevi umetoka Bara, Ushoga na Usagaji janga ili nalo asili yake itakuwa bara tu!
Hii tabia ya kurembea kila ovu kuwa asili yake Bara, imekuwa ni jambo la kawaida sana, siku ukisikia askari amepiga mtu au nyumba fulani imeingiliwa na mapolisi basi utasikia maneno tu... "Mijitu ya Bara hiyo".
Zanzibar si Pepo kiasi kusiwe na mambo yote hayo, ulevi, umalaya, wizi, ushoga na maovu mengine yote yalikuwepo tangia zama za Sultani na yanaendelea mpaka leo.
Hii tabia ya kukana na kuona kuwa mabinti, vijana na wazee wa Kizanzibar ni Malaika hawawezi kujiingiza kwenye maovu, matokeo yake ndio haya, kwa sababu wazazi wameshindwa wenyewe kuwalea watoto wao kwenye maadili mema kwa visingizo tulivyo vitaja, na matokeo yake ndio haya...!
Zanzibar imepoteza mwelekeo wake baada ya kukumbatia siasa tena si kukumbatia tu, kiasi wameibeba siasa kiasi cha kusahau udugu baina yao, leo utawasikia huyu Mpemba na huyu Muunguja, nayo sijui yameletwa na Wabara, wanajisahau kuwa hakuna kisiwa kimeumbwa kikawa na watu ndani, wote asili yao ni nje ya Zanzibar, sasa hii tabia ya kurembea kila kitu kuwa kimekuwa import kutoka Bara, haita wafikisha popote.
Kwa kweli wananchi na viongozi wa SMZ inabidi wabadirike sasa kwani itakapofika adhabu ya MwenyeziMungu Basi wajue kiama chao kitaanzia hapa hapa duniani, Ahera zitaenda hesabu tu...
Zanzibar ilikuwa ni chemchem ya dini. Kama ilivyokuwa miji iliyokuwa na Waislamu wengi na dini kuwa na nguvu zaidi, kama Zanzibar, Waislamu wakafikia hatua ya kufuata sharia chache katika Uislamu, zinazohusu ndoa na mirathi na watawala wakiwateua makadhi kushughulikia hayo. Unguja Makadhi wa Kisunni ndio waliokuwa wengi na Pemba Makadhi wa Kiibadhi ndio waliokuwa wengi.
Walimu wa dini walikuja kutoka nchi za Kiarabu, hasa Masheikh wa Kisunni kutoka nchi za kusini ya Bara Arabu, baadhi yao wakiwa ni wafanyabiashara.
Maarufu katika hao ni Sheikh Muhammad Abdulwahab (1703 – 1792 AD). Kadhalika huu ulikuwa wakati wa kuanza kwa biashara na nchi za Ulaya ambayo baadaye mfalme Said bin Sultan aliiendeleza.
Karne ya 19 AD elimu za maarifa ya Uislamu ziliendelea. Watawala wa kifalme kutoka Oman ambao walikuwa wa madhehebu ya Ibadhi walishughulikia dola na biashara hawakuingilia itikadi za Kisunni na Masunni hawakuingilia watu walioitakidi Ushia.
Zanzibar ilikuwa sana kiuchumi na kisiasa ilidhibiti karibu mwambao wote na kufanywa kituo kikuu cha biashara yote ya nje hasa mali kutoka bara.
Wanazuoni wa miji ya Mwambao walitembeleana kubadilishana elimu na kufanya biashara, walitunga vitabu na kufungua madrasa kubwa kubwa za kufundisha elimu ya dini, wengine walikwenda nje kusomesha kama vile Uganda na kwingineko.

BIBLIA INAWAAMBIA HAWA WATOTO, ELIMU NI UZIMA WAO

Image may contain: 3 people, text


Hebu tusome kwanza Biblia.
Mithali 4: 13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako.
Neno la Mungu halikusema kuwa hawa Mabinti waache Shule kisa sasa wanaitwa wazazi la hasha. Neno la Mungu limetia mkazo kuwa TUIKAMATE ELIMU, maana ni UZIMA WETU.
Kuwanyima ELIMU WAZAZI hawa ni kuwanyima UZIMA na kwenda kinyume na Neno la Mungu.
Mithali 4: 1 Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.
Hayo ndio mausia kutoka Biblia Takatifu.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

YEYE ASIYE NA DHAMBI NA AWE WA KWANZA KUKUTUPIA JIWE


Image may contain: 1 person, sitting and text

“Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati. ”
Bwana Yesu asifiwe…( Yohana 8:7 )
Kwa lugha nyingine Bwana Yesu anawaambia ikiwa kama watu hao hawana dhambi basi wawe wa kwanza kumuhukumu huyo mwanamke. Anawaambia watesi wako siku ya leo kwamba ikiwa kama hawana makosa basi wawe wa kwanza kukuhukumu wewe.
Ndiposa nikajifunza jambo moja kubwa hapo, kwamba;
Hata wenye kukuhukumu wewe,kumbe wao pia wanadhambi za kuhukumiwa, hivyo hawastahili kukuhukumu,pia nikajua kwamba; Usalama wako haupo kwa wanadamu bali usalama wako upo magotini pa Yesu.
TUACHE KUHUKUMU KAMA VILE SISI NI MALAIKA HUKU TUKIFAHAMU KUWA WOTE SISI NI WATENDA DHAMBI NA TUNASTAHILI JEHANNAM.
Waacheni hao Watoto wenye watoto WAENDE SHULE.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

Ancient Jewish Wedding Ceremony: “No man knows the day or hour, only the Father”

  The Ancient Jewish Marriage Rite: A Detailed Exposition of Betrothal, Preparation, and Consummation Dr. Maxwell Shimba Shimba Theological ...

TRENDING NOW