Sunday, September 10, 2017

BRASS BALLS: Egypt’s President el-Sisi Closes 27,000 Mosques to Fight Terrorism

strippenzieher-in-kairo-general-abdel-fattah-al-sisi-keystone
The Egyptian Ministry of Religious Endowment shuttered 27,000 local mosques under the pretext of fighting terrorism.
Al-Monitor reported:
The Egyptian Ministry of Religious Endowment has shuttered 27,000 local places of worship under the pretext of fighting terrorism, while awarding 400 preaching permits to Salafists.
An Egyptian administrative court on Feb. 18 upheld the Ministry of Religious Endowments’ decision issued in September 2013 to close down neighborhood places of worship of less than 80 square meters (861 square feet), a move intended to protect young people from the militancy and extremism that can prevail in such places, which lack the legal standing to hold Friday prayers.
This move sets a precedent that raises many questions about the fate of mosques in many Egyptian villages, the grounds of which are usually less than 80 square meters. In reply, opponents of the decision such as the Salafist Nour Party claimed that closing down places of worship without providing a larger alternative serves to further bolster extremist ideology, considering that the larger existing mosques cannot accommodate Friday worshippers who line surrounding streets to pray. On the opposite end of the spectrum, supporters of the decision such as intellectuals and scholars say that those mosques are time bombs that threaten national security, as they fall outside the purview of the Ministry of Religious Endowments and are used to spread subversive ideologies.
FOR THE ENTIRE ARTICLE CLICK LINK

KUMBE TORATI NA SABATO ILIKUWA NI KIVULI CHA MEMA YAJAYO?

Image may contain: sky, cloud, text, nature and outdoor
YESU KRISTO NI KUHANI MKUU:
Basi hata agano la kwanza lilikuwa na kawaida za ibada, na patakatifu pake, pa “kidunia.” (Waebrania9:1). Lakini “ile sharia haikukamilisha neno” (Waebrania 7:19). Kwa hiyo Mwana wa Mungu alikuja naye “kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa” (Waebrania 10:14). Basi, Kristo Yesu ni kuhani mkuu wetu sasa, na kwa hiyo, “ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.” (Waebrania 7:19).
Kumbe basi, ndio maana Mweyezi Mungu alifanya Agano Jipya kwa kupitia Mwane Yesu Kristo, “Kwa kule kusema Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka” (Waebrania 8:13). Agano la Kale lilijionyesha kuwa kuukuu Mungu amefanya Agano Jipya!
Kumbe basi lile agano na Musa ni Kukuu na ndio maana Mafarisayo na Masadukayo na Makuhani walio kuwa Yesu anavunja Torati. Sasa tunafahamu kuwa habari zote ndani ya gano la kale ni “KIVULI, Je, unaweza kula na au tegemea KIVULI? Je, unaweza kunywa kivuli? Je, unaweza kushika kivuli?
KUMBE SADAKA WAKATI WA AGANO LA KALE NI KAMA KIVULI?
“…wako watoao sadaka kama iagizavyo sheria; watumikiao mfano na KIVULI cha mambo ya Mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema…” (Waebrania 8:4,5)
Umesha ona hapo kuwa, kumbe sadaka zote ambazo za ndani ya hema zilikuwa ni mifano ya kivuli tu cha mambo ya Mbinguni. Sasa unapata faida gani kutoa sadaka kivuli?
Kumbe basi mambo ya kiroho ni mambo ya Yesu Kristo. Kumbe basi mambo ya uzima wa milele ni mambo ya Kristo! Sasa kwanini unashika kivuli “SABATO” na kuachana na Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa Sabato?
KUMBE TORATI ILIKUWA NI KIVULI CHA MEMA YAJAYO?
Hebu tusome Waebrania Mlango wa 10 aya ya 1 mapka ya 10 “Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha memo yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wowote kuwakamilisha wakaribiao…Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi… Mungu aliondoa agano la kwanza ili alilete au alisimamishe agano la pili kwa kupitia Mwanae Yesu Kristo. Katika mapenzi hayo mmepata utakaso kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.”
Kumbe basi Sabato wanayo itunza ni jambo la kivuli tu, sasa kwanini utunze kivuli wakati teyari tumesha mpata Bwana wa Sabato “Yesu Kristo”? Yesu alikuja na kutukomboa kutoka maisha ya kivuli ambayo ni pamoja na utunzaji wa Sabato. “Maana katika yeye “Yesu” unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili. Na ninyi mmetimilika katika yeye…” (Wakolosai 2:16-18).
Kumbe basi, mambo yote ya Sheria za Agano la Kale yalikuja ili kututayarisha kumjua Masia ambaye alikuja kukamilisha au rekebisha kosa tulilo lifanya pale kwenye Bustani ya Edeni.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

KWANINI ALLAH ANAOMBA MSAADA KWA MAKAFIRI?

Image may contain: one or more people, fire and text
Sura Al-Ankabut 29:6
Quran inasema:
Allah hahitaji kusaidiwa na viumbe wake. (bila shaka ni katika kutekeleza makusudi na mipango yake).
LAKINI QURAN HIYO HIYO INAWAAMBIA WAISLAMU:
Sura Muhammad 47:7
Kama mkimsaidia Allah, yeye naye atawasaidia na kuwafanya kuwa imara.
Maswali:
1. Umesema huhitaji msaada, kisha unasema tena unahitaji msaada! Je, Mungu anaweza kufanya jambo kama hilo?
2. Aya hizi zinafanana au zinapingana?
3. Je, hii si ishara kuwa aya hizi zilisemwa tu ili kukidhi mahitaji ya wakati fulani, lakini msemaji alipoona anahitaji kuwafanya watu watende kinyume chake, akajikuta amesema tofauti na alivyosema siku za nyuma?
Na tena quran inasema katika sura Al-Baqara 2:244
Fanyeni vita kwa ajili ya Allah na mkumbuke kwamba anaona yote na anajua yote.
Maswali:
1. Kama kweli Allah hahitaji msaada wa viumbe wake; na kama kweli aliumba ulimwengu wote kwa NENO TU, iweje NENO hilo hilo lisiweze kuwabadilisha wanadamu hadi alazimike kuliingiza ndani yao kwa nguvu, kwa vitisho na kwa ukali namna hiyo?
(Ukristo unashinda na kufanikiwa kwa NENO tu. Maana sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu wetu. Yeye aliumba kwa Neno; na sisi watoto wake, tunaumba kwa Neno hilo hilo. Tunahubiri tu na watu wanaokolewa, wanaponywa, wanalindwa na kusimama na Mungu wa kweli. Huoni kwamba hii hasa ndiyo maana ya nguvu ya Mungu? Hatuhitaji kuchinja au kupiga watu ili wampende Mungu!! Unawezaje, hata tu wewe mwenyewe, kumfanya mwanao au mkeo akupende kwa njia ya vipigo na kulazimisha? yaani, ukitaka mwanao au mkeo akupende utamshikia rungu au panga au bunduki? Je, hiyo si ishara kwamba wewe huna nguvu ndiyo maana unalazimisha? je, huko si kujikanganya maana umetuambia kuwa wewe ni Mungu unayeweza yote?)
2. Je, Allah anapotaka wanadamu wanaomwamini wafanye vita ili kuwalazimisha wasioamini wamwamini, huko si kutaka msaada kwa viumbe wake?
Ndio maana watu wenye kujitambua wanaukimbia Uislam.
Shalom
Max Shimba Ministries

KWANINI WASABATO WANAISUJUDU SIKU NA KUIFANYA SABATO NI BWANA ZAIDI YA YESU MUNGU MKUU?

Image may contain: sky, text and outdoor
Nitaanza na kuwalezea maana ya Mafarisayo.
Je, Mafarisayo ni akina nani hasa?
Mafarisayo waliunda madhehebu mojawapo ya Uyahudi ambayo wakati wa Yesu Kristo liliweza kufikia 5% ya Wayahudi wote, lakini lilikuwa na athari kubwa katika jamii yao, kutokana na sifa ya kuwa wanadini hasa. Jina lenyewe lina maana ya waliojitenga (na wakosefu) ili kushika kiaminifu masharti yote ya Torati ya Musa.
Mafarisayo wanajulikana hasa kutokana na Injili ambazo zinawataja kwa kawaida kama wapinzani wa Yesu, ingawa yeye alikuwa anakubaliana nao katika mafundisho mengi ya imani tofauti na yale ya Masadukayo, madhehebu nyingine kubwa iliyokuwa na wafuasi hasa kati ya makuhani.
Mafarisayo walianza mwishoni mwa karne ya 2 K.K. na kuendelea kustawi hadi mwaka 70 B.K. , ambapo Yerusalemu iliteketezwa na Warumi. Maangamizi ya hekalu yalivunja nguvu ya Masadukayo na kuwaachia Mafarisayo uongozi wa dini yao.
Mafarisayo ambao walikuwa WADINI au naweza kusema wenye siasa kali katika dini [utunzaji wa torati ya Musa], walimshitaki Yesu Kristo kwa Makuhani kwa kuwahusu wanafunzi wake wavunje sheria ya Musa ikiwa ni pamoja na kuvunja sabato (Marko 2:23-28). Ikimaanisha kuwa, mbele ya macho ya hawa Mafarisayo, Bwana Yesu na Wanafuzi wake walikuwa wanavunja Torati/Sabato. Je, Bwana Yesu aliwajibuje mashtaka ya hawa Mafarisayo? Hebu angali jinsi Yesu anavyo jibu kwa kutumia hekima! Bwana Yesu anawakumbusha Mafarisayo jinsi Mfalme Daudi alivyo vunja ya sheria.
Moja: Torati ya Musa inasema kuwa ni Makuhani pekee ndio walitakiwa kula mikate lakini tunamsoma Daudi akiingia ndani ya Hema na kuila Mikate, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Musa! Je, kwanini Yesu alifanya na au toa huu mfano wa Daudi kula Mikake? Katika mfano huu, tunajifunza kuwa Yesu anamtetea Daudi alipo kula Mkate ingawa alicho fanya Daudi kilivunja aya katika Hesabu 24: 5 mpaka 9.
Mbele ya Macho ya BWANA, uhai wa Mfalme Daudi alikuwa ni bora Zaidi kuliko kuto kula Mkate, ndio maana Yesu alisema, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, wala si mwanadamu kwa ajili ya sabato.” Kwa maneno hayo Bwana Yesu anaweka wazi kabisa kwamba sabato iliwekwa kwa ajili ya KUMTUMIKIA MWANADAMU na siyo iwe ‘bwana’ juu yake!
Hebu tumsome kwanza Yesu: Yesu alipomponya mtu ambaye alikuwa hawezi kwa muda wa miaka 38, alimwambia ‘jitwike godoro lako, uende.’ (Yohana 58). Hii ilikuwa ni siku ya sabato.
Lakini tunaona kwamba Wayahudi walipomwona mtu huyo walimwambia, Leo ni sabato, wala si halali kwako kujitwika godoro. (Yohana 5:10). Bila shaka walisema hivi kwa kuwa walifahamu fika jinsi sabato inavyotakiwa kutunzwa.
Hii ni kusema kwamba, kwa kadiri ya kanuni za utekelezaji wa sabato, hili lilikuwa ni kosa. Sasa, swali ni kwamba, kwa nini Yesu alivunja sabato kwa kumruhusu yule mtu abebe godoro?
Wayahudi walipomkasirikia Yesu kwa sababu ya kumruhusu yule mtu kubeba godoro siku ya sabato, Bwana Yesu aliwajibu kwamba: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. (Yohana 5:17). Haya ni maneno ya ajabu sana. Wewe uliye Mungu ulituambia kwamba siku ya sabato tusifanye kazi bali tupumzike; tumemwona mtu anafanya kazi ya kubeba godoro, tumekuja kwako, lakini wewe si tu kwamba hukumkemea, bali unasema tena kwamba na wewe unafanya kazi hata sasa (siku ya sabato)!
Kama sabato hasa ni kuacha kufanya kazi, iweje tena Yesu atamke jambo ambalo ni wazi kabisa linavunja sheria aliyoiweka mwenyewe ya kutofanya kazi; yaani aseme kuwa hata sasa yeye anafanya kazi?
Siku moja Yesu aliingia kwenye sinagogi ambamo mlikuwamo mwanamke mwenye pepo wa udhaifu. Yesu alimponya mama yule.
Hata hivyo, Biblia inasema: Basi mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu amemponya mtu siku ya sabato, akajibu, akawaambia mkutano, Kuna siku sita zifaazo kufanya kazi, basi njoni mponywe katika siku hizo, wala si katika siku ya sabato. (Luka. 13:14).
Maneno haya ya mkuu wa sinagogi yanatuonyesha kwamba, jambo alilofanya Yesu lilikuwa ni kuvunja sabato. Swali ni lilelile, kwa nini Yesu alivunja sabato?
Umeona jinsi ambayo hata Mkuu wa Sinagogi anakasirika alipo mwona Yesu akimponya yule Mwanamke, sembuse Mafarisayo. Unapo msoma Yesu, ndio utapata msingi wa Injili ambayo Bwana wetu Yesu alikuja kutuonyesha au fanya. Hebu msome hapa: “Mwanawa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.” Hiyo sentesi inamaana gani? Hapo Yesu anatuonyesha kuwa mwenye mamlaka ya kuvunja Torati ni yule yule aliye ileta Torati. Mungu aliyetoa sharia kwa Musa kwa kupitia Torati yeye Mungu huyo huyo ndioa anaivunja na au mwenye uwezo wa kuivunja Torati – Yeye ndiye Bwana wa sabato! Na hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu alivyofanya kupitia Yesu Kristo Mwanawe wa pekee. Ningependa uelewe kuwa, wakati wa Torati kulikuwa hakuna wokovu ambao tulio nao leo hii, hii inamaanisha kuwa TORATI HAINA UWEZO AU HAINA MAMLAKA YA KUOKOA. Torati ilitolewa kwa mkono wa Musa bali neema, kweli na wokovu zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.
Sasa basi, tunapo zungumzia Sabato na tunapo ona watu leo hii wanapigania kuitunza Sabato, hawa watu au dini au Imani inafanya kosa lilelile ambalo Mafarisayo walifanya katika karne ya kwanza, yaani, wanafanya sabato kuwa ‘BWANA WAO’ na kwa njia hiyo hawamheshimu wala hawamjali Bwana Yesu ambaye ni ‘Bwana wa wote na Bwana wa Sabato’. Biblia inasema kuwa Yesu ni Bwana wa Mabwana. 1Timotheo 6:15 na Ufunuo 19:16.
Je, wewe unaye itunza Sabato, unaona ni haki kumkana Bwana wa Mabwana na kuisujudu siku na/au Kuifanya SABATO ni Bwana zaidi ya Yesu?
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo na Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

JE UNAIJUA HOJA KUBWA NA PEKEE YA WASABATO “SDA” KUHUSU KUSHIKA SABATO? SEHEMU YA KWANZA

Image may contain: text
Iko hoja kwamba Sabato ni amri ya muhimu sana kwa sababu ilitoka moja kwa moja kinywani mwa Mungu tofauti na amri zingine ambazo zililetwa kupitia manabii au mitume.
Katika Agano la Kale Mungu alisema, “Ikumbuke siku ya Sabato uitakase…Kwa siku sita, BWANA aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo ndani yake, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo BWANA akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.” (Kutoka 20:8,11)
Hoja hii haina uzito kwa sababu kuu mbili:
Biblia kwa ujumla wake ni Neno la Mungu ambalo limetoka kinywani mwake lote. Na maandiko yako wazi kwamba: Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa, apate kutenda kila tendo jema. (2 Tim. 3:16-17).
Na kimsingi maandiko haya, ukisoma kwenye Biblia ya Kiingereza, hayasemi “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu”. Badala yake yanasema: All Scripture is God-breathed (NIV); au All scripture is given by inspiration of God (KJV). Hii ina maana kwamba: Maandiko yote yametokana na pumzi ya Mungu.
Kwa hiyo, hakuna mantiki kusema kwamba andiko hili lina maana zaidi kuliko lile kwa kuwa hili alitamka Mungu mwenyewe. Yote yana nguvu ileile; yote yametoka kwa Mungu yuleyule.
HOJA ZINAZOTUMIWA NA WASABATO KUISHIKILIA SABATO YA MWILINI
1. WANASEMA MUNGU SI KIGEUGEU
Yaani Mungu hawezi kusema alafu akaghairi (Malaki3:6) (Zaburi89:34) (Yakobo1:17)
Ni muhimu kujua Biblia inaposema Mungu hana kigeugeu lazima tujue hana kigeugeu anamaanisha nini?
Mungu hana kigeugeu au habadiliki katika ahadi, yaani Mungu akikuhaidi atakubariki na ukakaa katika njia zake, kubarikiwa ni lazima na hata hivyo akikuhadi kukubariki halafu ukaenda kinyume na mapenzi yake hugeuka na kutokutimiza aliyoyaahidi kwako (1Samweli 2:30).
Tukiyachunguza maandiko yote yanayoelezea kuwa Mungu si kigeugeu utaona chanzo cha maandiko haya ni ahadi (Malaki 3:5-6) Mungu anasema “Nita” maana yake anaahidi mambo kadhaa katika mstari wa 5, na katika mstari wa 6 anaeleza kuwa yeye si kigeugeu katika yale aliyoyaahidi katika mstari wa 5.
USIKOSE SEHEMU YA PILI
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

China Makes Major Moves To Ban Islam

ChinaIslam-1024x535

Apparently, China realizes what the West doesn’t. – Bet you never thought you’d read that here – Namely, that Islam is very dangerous. It’s kind of ironic that the oppressive nation sees what free nations don’t: Islam will turn nasty. It always does. Everywhere the religion/political ideology have been given an inch, they’ve taken a mile. Like a rabid dog, once it gets strong enough, it will bite us.
So what is China doing? It’s declaring an all-out war to make sure Islam doesn’t take over, and never gains the strength to attack them. So let me simplify it:
– Female head-coverings are banned. Period.
– Men are discouraged from growing long beards (often poorly grown ones, might I add)
– Even Islamic restaurants are forced sell cigarettes and drinks. And …
– They must display them prominently. Any business owner who does not follow this order…will lose their business. Gone.
They’re not tolerating Islam at all. That simple. China sees what’s happening to the West. It sees what happened in France, throughout the European world, in Boston and even in Texas. And that’s just the tip of the iceberg! They see it, and they’ve decided to stop any kind of political Islamic plague before it grows out of control.
In other words: China learns. Unlike our inept government, it realizes, ‘Hey, Islam wants destroy us.’ It realizes that Islam is political in nature, not just religious. Don’t get me wrong, communism is terrible, but it’s also what absolves China from the shackling burdens of political correctness. They’d rather survive than be politically correct.

TUMUOMBEE UPONYAJI TUNDU LISU

Image may contain: 1 person
Weka itikadi au udini pembeni na mwombee Mh Tundu Lisu uponyaji.
Baba katika jina la Yesu, neno lako liniasema katika Isaya 41:10-12 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.
Tunaomba uponyaji kwa Mhe Tundu Lisu katika Jina la Yesu.
Amen.

MAOMBI YA VITA YA KUTUMIA ALAMA ZA MUNGU

Image may contain: one or more people and text
Adui anakuja kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari kupambana na maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mungu. Ni lazima kujifunza neno la Mungu na kulitumia katika maisha yetu ya kila siku.
Baba neno lako katika Yer 23:29 linasema “Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? ”Nasimama sawa sawa na neno lako, na kuvunja vipande vipande kila mipango ya kishetani, miradi na kazi mbaya za adui, katika pepo nne za dunia, katika jina la Yesu.
Baba neno katika Waebrania 4:12 "linasema “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili. Nachukua mamlaka ya neno lako ambalo ni upanga na kugawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani ya kila nguvu za uchawi, kila enzi, falme, mamlaka, wakuu wa giza, mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho, mishale ya moto ya adui, maadui wa siri, maadui wanaojulikana, mapepo ya utambuzi, maadui wa ndani, na mamlaka zingine zote za adui, kwa kuwafunga na kuwatupa katika shimo milele, katika jina la Yesu, Amina.
Baba neno lako katika Yer 23:29 linasema “Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? ”. Natumia moto wa Mungu Mwenyezi, kuchoma kila kazi ya adui kama majivu. Chochote ambacho kilitumwa kwangu, kinachonifuata, kilichohamishiwa kwangu, au kwenye kitu chochote ambacho ni changu. Nazifunga, na kuzitupa katika lile ziwa la moto, sasa na hata milele, katika jina la Yesu.
Baba neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu Zaburi 119: 105. Nasimama sawa sawa na neno lako, na kutumia mwanga wako kuangaza kila mahali penye giza ambapo jua haliangazi. Naweka wazi kila matendo mabaya yanayotendeka kwenye maisha yangu, familia, watoto, fedha za nyumbani, kazi, huduma, ndoa, na yote ambayo ni yetu. Bwana nakushukuru kwa kufanya kazi za uovu wao kuwa dhaifu, zife, zifungwe na kufutwa, katika jina la Yesu.
Baba neno lako katika Yakobo 1:22-25 "linasema kwamba neno lako ni kama kioo" Natumia mamlaka ya neno lako, na kubamiza, kuangamiza vipande vipande vioo vyote vya mapepo, ambavyo adui hutumia kufuatilia maendeleo yetu, mafanikio, baraka, na yote yaliyo yetu. Naamrisha maadui, kuona shughuli zao mbaya, kushindwa, na anguko katika vioo vyao vya kipepo, katika jina la Yesu.
Baba neno lako ni kama maji ambayo yatusafisha dhambi zote na uovu. Waefeso 5:26-27. Natumia maji ya Bwana Mungu mwenyezi kuwazamisha maadui, mafarao wote, mayezebeli, goliati na maadui wengine wote wa maendeleo yetu katika bahari Shamu, sawa sawa na Kutoka sura ya 15
Baba neno lako linaniambia katika Zaburi 107:20 "Kwamba neno ni kama dawa" Nasimama sawa sawa na neno lako ambalo ni kama dawa, na kuponya mioyo yetu na machungu yote, uponyaji wa kimwili, kiakili, kihisia, na kiroho. Naomba neno lako liturejeshee mara mia moja, kila kitu tulichopoteza, katika jina la Yesu
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

MAHAKAMA YA KADHI HAIPO KWENYE QURAN

Image may contain: 3 people
Ndugu wasomaji.
Leo ningependa kusema kuwa, dai la Waislam wa Tanzania la Mahakama ya Kadhi halina msingi wala usaidizi wa Quran.
Kwa wanao ifahamu Quran, watakubaliana na mimi kuwa HAKUNA AYA HATA MOJA ambayo Allah alisema na au Waamrisha Waislam waende kwenye Mahakama ya Kadhi. Narudia tena hakuna aya.
SASA NDUGU WAISLAM:
1. Who appoints Chief Kadhi and Kadhis?
--Nani na au mnamteuaje Kadhi Mkuu na Kadhi? Leteni aya.
2. What are the qualification for appointment to the office of a Kadhi (including a Chief Kadhi)?
-- Je, mnatumia qualification/elimu zipi kuchagua/kufanya utezi wa Ofisi ya Kadhi na Kadhi mkuu/ Leteni aya.
3. Since the Kadhis are not trained lawyers who understand the Evidence Act and the Civil Procedure Act, how and/or what will they use to administer their Courts?
-- Inafahamika kuwa Kadhi sio Mawakili walio somea ambao wanaelewa ushahid wa keshi ambazo si za jinai na jinai, SASA hawa Kadhi watatumia nini katika kusimamia Mahakama ya Kadhi?
4. Muslims are mainly of two sects in Tanzania - the Sunni and Shia. Majority of the Muslims in Tanzania are Sunni Muslims but there is a significant population of Shia Muslims too and consideration ought to be given to the appointment of Kadhis of the Shia Sect to cater the interest of the Shia Muslims. Will they have two different Courts? For Sunni and Shia?
--- Waislam wapo katika makundi mawili makubwa, Sunni na Shia. Wengi wa Waislam wa Tanzania ni Sunni, ingawa kuna Shia wengi vile vile. JE, Hii Mahakama ya Kadhi itatumia Kadhi wa dhehebu lipi katia ya hayo mawili? Je, watakuwa na Mahakama mbili tofauti za Sunni na Shia?
5. How will Muslim Women be protected since: Muslim law regards women as less than men in matters of both marriage and divorce, as well as devolution of property: Holy Quran Surah 2:228-232, and Surah 65:1-7 (only a man may divorce his wife even if he is required to provide for her); a man may beat his wife, even if lightly, the evidence of two women, is equal to evidence of one man (Surah 2:282). The application of such beliefs of faith are contrary to the Constitution.
---Kivipi Wanawake wa Kiislamu watatetewa kwenye hizi mahakama? Inafahamika kuwa Sheria za Kiislam zinakiri kuwa Mwanamke ni nusu ya Mwanaume, au yupo chini sana ya Mwanaume. Je, katika kesi ya kutoa talaka na mirathi, hii mahakama itawezaje kumtetea Mwanamke ambaye yupo nusu ya Mwaume? Sura 2: 228-232 na Sura 65:1-7 ( zinasema mwenye haki ya kutoa talaka ni Mwaume tu) Mume anahaki ya kumpiga mkewe, Ushahidi wa wanawake wawili ni sawa na ushahid wa mwanaume mmoja, (Sura 2:282). Huu utamaduni wa Kiislam, ni kinyume na sheria za nchi.
Je, Mwanamke atatetewa vipi kwenye hizi Mahakama?
Islamic "Kadhi" courtsis illegal and discriminatory.
Kwanini mnamsaidia Allah kwa kuanzisha Mahakama ya Kadhi?
Waislam, nileteeni aya ambayo Allah anasema kuwa muende kwenye Mahakama ya Kadhi.
Mkiniletea aya kutoka Quran inayo waamrisha kwenda kwenye Mahakama za Kadhi, leo hii nitasilimu na kuwa Muislam.
Haya nasubiri ajibu ya aya na sio matusi.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.
For Max Shimba Ministries Org.

JE UNAIJUA HOJA KUBWA NA PEKEE YA WASABATO "SDA" KUHUSU KUSHIKA SABATO? SEHEMU YA PILI

Image may contain: people standing, text and outdoor
2. KILA KAZI AIFANYAYO MUNGU ITADUMU MILELE.
Hii nayo ni hoja nyingine, wanasema eti Sabato ni kazi ya Mungu kwa hiyo inapaswa idumu milele wakinukuu andiko linalotoka katika (Muhubiri 3:14) linalosema “Kazi ya Mungu itadumu milele” kwa hiyo Sabato ni kazi ya Mungu inapaswa idumu milele. Biblia inatuonya kwamba tunapaswa kutumia neno la Mungu kwa halali: Maana yake inawezekana kutumia neno la Mungu isivyo halali (2Timotheo 2:15.).
Andiko la (Muhubiri 3:14) halizungumzii Sabato kabisa, kinachosemwa hapo ni kazi ya Mungu, maana ya neno kazi ni kitu cha kufanya kwa mfano; mtu akiwa anapika hiyo inaitwa kazi, mtu akijenga nyumba hiyo inaitwa kazi, mtu akibeba godoro hiyo ni kazi n.k.
Kazi ni lazima itumike nguvu – Swali lakujiuliza je Sabato ni kazi?
Jibu ni hapana. Sabato sio kazi, Sabato ni kutokufanya kazi. Sasa ni nini kilichozungumziwa katika Muhubiri 3:14?
Kinachozungumziwa hapa ni uumbaji wa Mungu ambao ndio kazi ya Mungu. Mungu alifanya kazi ya kuiumba dunia. Mungu alifanya kazi ya kuwaumba wanyama. Mungu alifanya kazi ya kumuumba mwanadamu na hata leo Mungu akifanya kazi yoyote ya kuinua mtumishi ili akahubiri injili. Mungu anafanya kazi kwanza ya kumtafuta ili aokoke, halafu aanze kumfundisha mambo mengi hatimaye anakuwa kiasi cha kuongoza wengine.
Shughuli yote ya kumtafuta mtu dhambini na kumfundisha hiyo inaitwa kazi. Sasa tazama kwa makini maandiko yanayo zungumzia kazi (Mwanzo 2:1-2) unaona Mungu, kuumba anakuita kazi, lakini alipo pumzika hajaita kupumzika kuwa ni kazi, hivyo tunajua Sabato sio kazi. Kuhubiri injili kunaitwa kazi (Marko 16:19-20) Bwana alikuwa anatenda kazi pamoja nao yaani kazi ya kuokoa, kuponya n.k (Matendo 5:34-39) Kuhubiri injili hapo kunaitwa kazi.
USIKOSE SEHEMU YA TATU
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

The Prophethood of Muhammad

  The Prophethood of Muhammad: A Critical Theological Evaluation By Dr. Maxwell Shimba, Shimba Theological Institute, New York, NY The cla...

TRENDING NOW