Sunday, September 10, 2017

JE UNAIJUA HOJA KUBWA NA PEKEE YA WASABATO "SDA" KUHUSU KUSHIKA SABATO? SEHEMU YA PILI

Image may contain: people standing, text and outdoor
2. KILA KAZI AIFANYAYO MUNGU ITADUMU MILELE.
Hii nayo ni hoja nyingine, wanasema eti Sabato ni kazi ya Mungu kwa hiyo inapaswa idumu milele wakinukuu andiko linalotoka katika (Muhubiri 3:14) linalosema “Kazi ya Mungu itadumu milele” kwa hiyo Sabato ni kazi ya Mungu inapaswa idumu milele. Biblia inatuonya kwamba tunapaswa kutumia neno la Mungu kwa halali: Maana yake inawezekana kutumia neno la Mungu isivyo halali (2Timotheo 2:15.).
Andiko la (Muhubiri 3:14) halizungumzii Sabato kabisa, kinachosemwa hapo ni kazi ya Mungu, maana ya neno kazi ni kitu cha kufanya kwa mfano; mtu akiwa anapika hiyo inaitwa kazi, mtu akijenga nyumba hiyo inaitwa kazi, mtu akibeba godoro hiyo ni kazi n.k.
Kazi ni lazima itumike nguvu – Swali lakujiuliza je Sabato ni kazi?
Jibu ni hapana. Sabato sio kazi, Sabato ni kutokufanya kazi. Sasa ni nini kilichozungumziwa katika Muhubiri 3:14?
Kinachozungumziwa hapa ni uumbaji wa Mungu ambao ndio kazi ya Mungu. Mungu alifanya kazi ya kuiumba dunia. Mungu alifanya kazi ya kuwaumba wanyama. Mungu alifanya kazi ya kumuumba mwanadamu na hata leo Mungu akifanya kazi yoyote ya kuinua mtumishi ili akahubiri injili. Mungu anafanya kazi kwanza ya kumtafuta ili aokoke, halafu aanze kumfundisha mambo mengi hatimaye anakuwa kiasi cha kuongoza wengine.
Shughuli yote ya kumtafuta mtu dhambini na kumfundisha hiyo inaitwa kazi. Sasa tazama kwa makini maandiko yanayo zungumzia kazi (Mwanzo 2:1-2) unaona Mungu, kuumba anakuita kazi, lakini alipo pumzika hajaita kupumzika kuwa ni kazi, hivyo tunajua Sabato sio kazi. Kuhubiri injili kunaitwa kazi (Marko 16:19-20) Bwana alikuwa anatenda kazi pamoja nao yaani kazi ya kuokoa, kuponya n.k (Matendo 5:34-39) Kuhubiri injili hapo kunaitwa kazi.
USIKOSE SEHEMU YA TATU
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW