Sunday, September 10, 2017

KWANINI WASABATO WANAISUJUDU SIKU NA KUIFANYA SABATO NI BWANA ZAIDI YA YESU MUNGU MKUU?

Image may contain: sky, text and outdoor
Nitaanza na kuwalezea maana ya Mafarisayo.
Je, Mafarisayo ni akina nani hasa?
Mafarisayo waliunda madhehebu mojawapo ya Uyahudi ambayo wakati wa Yesu Kristo liliweza kufikia 5% ya Wayahudi wote, lakini lilikuwa na athari kubwa katika jamii yao, kutokana na sifa ya kuwa wanadini hasa. Jina lenyewe lina maana ya waliojitenga (na wakosefu) ili kushika kiaminifu masharti yote ya Torati ya Musa.
Mafarisayo wanajulikana hasa kutokana na Injili ambazo zinawataja kwa kawaida kama wapinzani wa Yesu, ingawa yeye alikuwa anakubaliana nao katika mafundisho mengi ya imani tofauti na yale ya Masadukayo, madhehebu nyingine kubwa iliyokuwa na wafuasi hasa kati ya makuhani.
Mafarisayo walianza mwishoni mwa karne ya 2 K.K. na kuendelea kustawi hadi mwaka 70 B.K. , ambapo Yerusalemu iliteketezwa na Warumi. Maangamizi ya hekalu yalivunja nguvu ya Masadukayo na kuwaachia Mafarisayo uongozi wa dini yao.
Mafarisayo ambao walikuwa WADINI au naweza kusema wenye siasa kali katika dini [utunzaji wa torati ya Musa], walimshitaki Yesu Kristo kwa Makuhani kwa kuwahusu wanafunzi wake wavunje sheria ya Musa ikiwa ni pamoja na kuvunja sabato (Marko 2:23-28). Ikimaanisha kuwa, mbele ya macho ya hawa Mafarisayo, Bwana Yesu na Wanafuzi wake walikuwa wanavunja Torati/Sabato. Je, Bwana Yesu aliwajibuje mashtaka ya hawa Mafarisayo? Hebu angali jinsi Yesu anavyo jibu kwa kutumia hekima! Bwana Yesu anawakumbusha Mafarisayo jinsi Mfalme Daudi alivyo vunja ya sheria.
Moja: Torati ya Musa inasema kuwa ni Makuhani pekee ndio walitakiwa kula mikate lakini tunamsoma Daudi akiingia ndani ya Hema na kuila Mikate, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Musa! Je, kwanini Yesu alifanya na au toa huu mfano wa Daudi kula Mikake? Katika mfano huu, tunajifunza kuwa Yesu anamtetea Daudi alipo kula Mkate ingawa alicho fanya Daudi kilivunja aya katika Hesabu 24: 5 mpaka 9.
Mbele ya Macho ya BWANA, uhai wa Mfalme Daudi alikuwa ni bora Zaidi kuliko kuto kula Mkate, ndio maana Yesu alisema, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, wala si mwanadamu kwa ajili ya sabato.” Kwa maneno hayo Bwana Yesu anaweka wazi kabisa kwamba sabato iliwekwa kwa ajili ya KUMTUMIKIA MWANADAMU na siyo iwe ‘bwana’ juu yake!
Hebu tumsome kwanza Yesu: Yesu alipomponya mtu ambaye alikuwa hawezi kwa muda wa miaka 38, alimwambia ‘jitwike godoro lako, uende.’ (Yohana 58). Hii ilikuwa ni siku ya sabato.
Lakini tunaona kwamba Wayahudi walipomwona mtu huyo walimwambia, Leo ni sabato, wala si halali kwako kujitwika godoro. (Yohana 5:10). Bila shaka walisema hivi kwa kuwa walifahamu fika jinsi sabato inavyotakiwa kutunzwa.
Hii ni kusema kwamba, kwa kadiri ya kanuni za utekelezaji wa sabato, hili lilikuwa ni kosa. Sasa, swali ni kwamba, kwa nini Yesu alivunja sabato kwa kumruhusu yule mtu abebe godoro?
Wayahudi walipomkasirikia Yesu kwa sababu ya kumruhusu yule mtu kubeba godoro siku ya sabato, Bwana Yesu aliwajibu kwamba: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. (Yohana 5:17). Haya ni maneno ya ajabu sana. Wewe uliye Mungu ulituambia kwamba siku ya sabato tusifanye kazi bali tupumzike; tumemwona mtu anafanya kazi ya kubeba godoro, tumekuja kwako, lakini wewe si tu kwamba hukumkemea, bali unasema tena kwamba na wewe unafanya kazi hata sasa (siku ya sabato)!
Kama sabato hasa ni kuacha kufanya kazi, iweje tena Yesu atamke jambo ambalo ni wazi kabisa linavunja sheria aliyoiweka mwenyewe ya kutofanya kazi; yaani aseme kuwa hata sasa yeye anafanya kazi?
Siku moja Yesu aliingia kwenye sinagogi ambamo mlikuwamo mwanamke mwenye pepo wa udhaifu. Yesu alimponya mama yule.
Hata hivyo, Biblia inasema: Basi mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu amemponya mtu siku ya sabato, akajibu, akawaambia mkutano, Kuna siku sita zifaazo kufanya kazi, basi njoni mponywe katika siku hizo, wala si katika siku ya sabato. (Luka. 13:14).
Maneno haya ya mkuu wa sinagogi yanatuonyesha kwamba, jambo alilofanya Yesu lilikuwa ni kuvunja sabato. Swali ni lilelile, kwa nini Yesu alivunja sabato?
Umeona jinsi ambayo hata Mkuu wa Sinagogi anakasirika alipo mwona Yesu akimponya yule Mwanamke, sembuse Mafarisayo. Unapo msoma Yesu, ndio utapata msingi wa Injili ambayo Bwana wetu Yesu alikuja kutuonyesha au fanya. Hebu msome hapa: “Mwanawa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.” Hiyo sentesi inamaana gani? Hapo Yesu anatuonyesha kuwa mwenye mamlaka ya kuvunja Torati ni yule yule aliye ileta Torati. Mungu aliyetoa sharia kwa Musa kwa kupitia Torati yeye Mungu huyo huyo ndioa anaivunja na au mwenye uwezo wa kuivunja Torati – Yeye ndiye Bwana wa sabato! Na hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu alivyofanya kupitia Yesu Kristo Mwanawe wa pekee. Ningependa uelewe kuwa, wakati wa Torati kulikuwa hakuna wokovu ambao tulio nao leo hii, hii inamaanisha kuwa TORATI HAINA UWEZO AU HAINA MAMLAKA YA KUOKOA. Torati ilitolewa kwa mkono wa Musa bali neema, kweli na wokovu zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.
Sasa basi, tunapo zungumzia Sabato na tunapo ona watu leo hii wanapigania kuitunza Sabato, hawa watu au dini au Imani inafanya kosa lilelile ambalo Mafarisayo walifanya katika karne ya kwanza, yaani, wanafanya sabato kuwa ‘BWANA WAO’ na kwa njia hiyo hawamheshimu wala hawamjali Bwana Yesu ambaye ni ‘Bwana wa wote na Bwana wa Sabato’. Biblia inasema kuwa Yesu ni Bwana wa Mabwana. 1Timotheo 6:15 na Ufunuo 19:16.
Je, wewe unaye itunza Sabato, unaona ni haki kumkana Bwana wa Mabwana na kuisujudu siku na/au Kuifanya SABATO ni Bwana zaidi ya Yesu?
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo na Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW