Sunday, September 10, 2017

KUMBE TORATI NA SABATO ILIKUWA NI KIVULI CHA MEMA YAJAYO?

Image may contain: sky, cloud, text, nature and outdoor
YESU KRISTO NI KUHANI MKUU:
Basi hata agano la kwanza lilikuwa na kawaida za ibada, na patakatifu pake, pa “kidunia.” (Waebrania9:1). Lakini “ile sharia haikukamilisha neno” (Waebrania 7:19). Kwa hiyo Mwana wa Mungu alikuja naye “kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa” (Waebrania 10:14). Basi, Kristo Yesu ni kuhani mkuu wetu sasa, na kwa hiyo, “ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.” (Waebrania 7:19).
Kumbe basi, ndio maana Mweyezi Mungu alifanya Agano Jipya kwa kupitia Mwane Yesu Kristo, “Kwa kule kusema Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka” (Waebrania 8:13). Agano la Kale lilijionyesha kuwa kuukuu Mungu amefanya Agano Jipya!
Kumbe basi lile agano na Musa ni Kukuu na ndio maana Mafarisayo na Masadukayo na Makuhani walio kuwa Yesu anavunja Torati. Sasa tunafahamu kuwa habari zote ndani ya gano la kale ni “KIVULI, Je, unaweza kula na au tegemea KIVULI? Je, unaweza kunywa kivuli? Je, unaweza kushika kivuli?
KUMBE SADAKA WAKATI WA AGANO LA KALE NI KAMA KIVULI?
“…wako watoao sadaka kama iagizavyo sheria; watumikiao mfano na KIVULI cha mambo ya Mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema…” (Waebrania 8:4,5)
Umesha ona hapo kuwa, kumbe sadaka zote ambazo za ndani ya hema zilikuwa ni mifano ya kivuli tu cha mambo ya Mbinguni. Sasa unapata faida gani kutoa sadaka kivuli?
Kumbe basi mambo ya kiroho ni mambo ya Yesu Kristo. Kumbe basi mambo ya uzima wa milele ni mambo ya Kristo! Sasa kwanini unashika kivuli “SABATO” na kuachana na Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa Sabato?
KUMBE TORATI ILIKUWA NI KIVULI CHA MEMA YAJAYO?
Hebu tusome Waebrania Mlango wa 10 aya ya 1 mapka ya 10 “Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha memo yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wowote kuwakamilisha wakaribiao…Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi… Mungu aliondoa agano la kwanza ili alilete au alisimamishe agano la pili kwa kupitia Mwanae Yesu Kristo. Katika mapenzi hayo mmepata utakaso kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.”
Kumbe basi Sabato wanayo itunza ni jambo la kivuli tu, sasa kwanini utunze kivuli wakati teyari tumesha mpata Bwana wa Sabato “Yesu Kristo”? Yesu alikuja na kutukomboa kutoka maisha ya kivuli ambayo ni pamoja na utunzaji wa Sabato. “Maana katika yeye “Yesu” unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili. Na ninyi mmetimilika katika yeye…” (Wakolosai 2:16-18).
Kumbe basi, mambo yote ya Sheria za Agano la Kale yalikuja ili kututayarisha kumjua Masia ambaye alikuja kukamilisha au rekebisha kosa tulilo lifanya pale kwenye Bustani ya Edeni.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu na Mwokozi wetu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW