Friday, December 7, 2018

JE, MUHAMMAD NI MTUME NA NABII WA UONGO AU WA KWELI?

Image may contain: 1 person, text


Ndugu msomaji,
Mara nyingi Waislam wamekuwa wakisema kuwa, eti, Yesu alitabiri kuja kwa Muhammad, pale alipo sema kuhusu Roho wa Kweli, la hasha.
Nabii ni mtu gani?
Nabii ni mtu aliyeteuliwa rasmi kwa vigezo vya Kiungu ili kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu, kwa maneno mengine nabii ni msemaji wa siri za Mungu.
Nabii: Ni mtu ambaye ni msemaji wa Mungu (a mouthpiece of God) .Husimama kati ya Mungu na binadamu, mwenye jukumu la kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu. Nabii anapokuwa msemaji wa Mungu, huvuviwa na Roho wa Mungu, bila ujumbe wake kuwa na makosa. Nabii hujizuia kabisa utashi wake, nafsi yake, na mawazo yake, anapokuwa anatoa ujumbe wa Kinabii toka kwa Mungu. Wakati mwingine Mungu mwenyewe hutia maneno yake vinywani mwao (Kum 18:18, Yer 1:9). Nabii ni mtumishi wa Mungu (Zekaria 1:6) na mjumbe wa Mungu 2 Nyak 36:15).
Ni kweli kuwa Yesu alitabiri kuja kwa manabii, lakini kamwe hakusema lolote kuhusu utume wa Muhammad zaidi ya kukiri kuwa watu wenye sifa kama za Muhammad ni Mitume na Manabii wa Uongo.
Miongoni mwa wanadamu wanaoitwa nabii na mtume, ni mtu aitwaye Muhammad s.a.w ibn Abdullah, ibn Abdu Mutallib, ambaye ni mtume na nabii katika dini ya Kiislamu.
Pengine wewe msomaji wa somo hili unaweza kushangaa ni kwa vipi sisi ambao si Waislamu bali Wakristo tuanze kuhoji habari za Muhammad s.a.w mtume wa Waislamu? Jibu lake ni kwamba kitabu cha Qur’an kinachotumiwa na Waislamu kimetutaja sisi Wakristo mara 62 kikitutaka kuupokea, kuuamini na hatimaye kuufuata ujumbe wa Muhammad s.a.w kwa madai ya kuwa yeye ni nabii na mtume wa mwisho hata kwetu Wakristo, aliyetumwa na Mungu.
YESU ATABIRI KUHUSU MTUME WA UONGO AMBAYE NI MUHAMMAD
Tahadhari ya Bwana Yesu: Bwana Yesu alipokuwa hapa duniani alituonya kuhusu kuwatambua manabii na mitume wa uongo kabla Muhammad hajazaliwa (amezaliwa 570 B.K), wala kabla Uislamu haujaanzishwa na Muhammad mwaka 610 B.K, wala kabla ya kuwepo kitabu kinachoitwa Qur’an. Tunayasoma maonyo hayo ya Bwana Yesu katika
Mathayo 7:15-16 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali, mtawatambua kwa matunda yao”.
Mathayo 24:11-13 “Na manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi na kwasababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho, ndiye atakayeokoka”.
Yesu katika Ufunuo alisema kuwa watakuja Manabii na Mitume wa Uongo.
Ufunuo 2:2 Nayajua matendo yako na taabu yako, subira yako, na kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume nao sio, ukawaona kuwa waongo.
Je, Muhammad ni nabii wa Mungu?
Je, Muhammad anasifa za nabii wa Mungu?
Hebu endelea na somo hapa chini:
JINSI YA KUMFAHAMU NABII WA UONGO:
Kwa hivyo Muhammad ni miongoni mwa hao Mitume ambao ni waongo, ambao sisi kama Wakristo yatupasa kuutambua uwepo wao hapa Duniani, kwani tumeshapewa angalizo la kuwatambua hawa wanaojiita Mitume na Manabii, hali ya kuwa ni waongo
1 Yohana 4:1-3
1 Wapenzi msiamni kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu: kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea duniani. 2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; KILA ROHO IKIRIYO KWAMBA YESU KRISTO AMEKUJA KATIKA MWILI, YATOKANA NA MUNGU, 3 Na Kila roho isiyomkiri Yesu, haitokani na Mungu. Na HII NDIO ROHO YA MPINGA KRISTO ambayo mliskia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
Vigezo hivi tulivyopewa na Biblia Takatifu kuwajua manabii na mitume wa uongo ni muhimu sana tukavichunguza katika maisha ya wale wanaoitwa nabii au mtume
Kila nabii na mtume ambaye yeye hakubali kuwa Kristo alikuja katika mwili, kwa maana kuwa Mungu alidhihirishwa katika mwili, hiyo roho yaani huyo nabii si ambaye anatokana na Mungu, huyo ni Nabii anaetokana na shetani, kwa mujibu ya maandiko Matakatifu, Kristo alidhirishwa katika mwili.
1 Timotheo 3:16 Na Bila shaka siri ya utauwa ni kuu, Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulikana kuwa na haki katika roho,
Akaonekana na Malaika, akahubiriwa katika mataifa. akaaminiwa katika ulimwengu, akachukuliwa juu katika utukufu,
SASA KAMA MNATAKA KUAMINI KUWA KWELI Muhammad ni nabii na mtume wa uongo, waulizeni wafuasi wake,
SWALI LA KUPIMA UNABII WA MUHAMMAD:
Je! Kwa mujibu wa uislamu, Wanakubali kuwa Mungu alikuja kwa njia ya mwili wa kibinadamu na kuonekana?
Wakikubali, basi tambueni kuwa Muhammad ni mtume wa kweli, na wakikataa basi mjue kuwa Muhammad ni nabii na mtume wa Uongo.
SIFA ZA NABII WA KWELI:
Nabii wa kweli hupata ufunuo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu:- 2Petro 1:20-21.” Mkijua neno hili kwanza,ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu;bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu,wakiongozwa na Roho Mtakatifu”.
LAKINI MUHAMMAD YEYE ALIPATA UNABII KWA NJIA HII, SOMA
Katika kitabu kiitwacho “ Wakeze Mtume Wakubwa Na Wanawe” kilichoandikwa na Sheikh Abdullah Saleh Al Farsy uk.12 tunasoma maneno haya
“Basi Mtume akafanya hofu akarejea kwa mkewe akamhadithia; na pale pale homa kubwa kabisa ikampanda akataka afunikwe maguo. Mara akawa anatetemeka kwa nderema na anaweweseka na kusema “Najikhofia nafsi yangu kuchezewa na shetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga”. Bibi Khadija palepale alimdakiza akamwambia; “ Wacha hayo; Siyo yatakayokuwa hayo. Wewe huwezi kuchezewa na mashetani. Shetani hawezi kumchezea mtu mwenye sifa zako. Wewe unatazama vyema jamaa zako, unachukuwa mizigo ya hata watu wasiokuwa wako, unawadhihirishia watu sifa zako nzuri ambazo hakuna mwenye nazo. Unafanya hivi na unafanya hivi. Furahi ndugu yangu. Tua moyo wako, Wallahi! Mimi naona umekwishakuwa mtume”.
Je, wapi katika Injili au Taurat au Zaburi tunasoma kuwa Manabii na Mitume katika Biblia walipata kwa njia ya homa na kukiri kuchezewa na mashetani kama Muhammad wa kwenye Quran?
1 Petro1:10-11 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta tafuta na kuchunguza chunguza ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi. Wakatafuta ni wakati upi na wakati wa namna gani ulioonywa NA ROHO WA KRISTO ALIYEKUWA NDANI YAO ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaokuwako baada ya hayo…..” (maneno ya msisitizo kwa herufi kubwa ni ya mwandishi)
Ufunuo 19:10 “Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndiyo roho ya unabii”
Biblia Takatifu imetuonya kuwachunguza mitume na manabii. Katika kitabu cha Ufunuo 2:1-2 “ Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao siyo ukawaona kuwa waongo”
Kwa mujibu wa aya hizi Muhammad s.a.w hastahili kuitwa nabii na mtume wa Mungu wa Kweli, bali anaangukia katika kundi la manabii na mitume wa uongo.
Mungu awabarikisana, na tuendelee kujifunza kweli, na kweli itatuweka huru.
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13
For Max Shimba Ministries Org.

MUHAMMAD ALIVUNJA AMRI KUMI ZA MUNGU (SEHEMU YA SITA)

Image may contain: 4 people
Katika somo letu la leo, tutaingalia amri ya Sita inayo sema "USIUE". Kitabu cha Kutoka 20:13. Usiue.
Hebu kwanza tumsome Bwana wetu Yesu Kristo anasema nini kuhusu amri kuu:
Luka 4:16 Yesu alipoulizwa, Nifanye nini ili niurithi uzima wa Milele, Yesu alizitaja Amri kumi kama kanuni kuu za Ufalme wa Mungu. Biblia yasema hivi: “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
MUHAMMAD ALIVUNJA AMRI YA SITA KWA KUFANYA MAUWAJI MABAYA SANA.
Hivi kwanini Allah aliruhusu kuuwawa kwa Vikongwe? Hivi kwanini Muhammad alifanya hiyo kazi ya Allah na kuwauwa Vikongwe na ajuza?
Mohammad na kikosi chake kiliuwa wazee wa makamo; Umm Qirfa Fatima, Abu Afak na mzee aliyekataa kusujudia Al-Kaaba.
Baada ya kuuteka mji wa Kaaba Mohammad alimtuma mfuasi wake, Zayd Ibn Haritha kuenda kuuteka kabila ambalo liliukana Uislamu. Zayd bin Haritha alifanikiwa kuuteka huo mji pamoja na kuuwa wazee wakongwe na kuwateka wanawake na watoto walitojaribu kutoroka.
“…na tuliwashambulia kutoka pande zote hadi tukafika karibu na visima vyao ambapo tulipigana vita vikali. Tuliwauwa Aadui zetu wengine huku wengine wakichukuliwa kama mateka wa vita. Niliona kwa mbali kundi la watu lililojumuisha wanawake na watoto wakitoroka. Niliogopa, wasije wakafike mlimani kabla yangu, hivyo nikalenga mshale kati yao na ukaangukia kwa mbele kati yao na mlima. Nikawarudisha nikiwakimbiza kama mifugo walikotoka. (Sahin Muslim 4345)
Umm Qirfa ni miongoni mwa wanawake walitekwa vitani
Alikuwa ajuza (bi kizee), mke wa Malik. Binti yake (na wenzake) walitekwa pia. Zayd Ibn Haritha akaamuru Qays kuuwa Umm Qirfa na akamuuwa kinyama kwa kumfunga kwa kamba kila mguu kwa ngamia mbili na kuwaamuru hao ngamia kuenda pande tofauti. Umm Qirfa alichanika katikati, akatokwa na damu akapasuka mishipa, mifupa na kufa ghafla! (Ibn Ishaq/Hisham 980)
Binti yake ajuza, Umm Qirfa Fatima, aliletwa Makka pamoja na mateka wengine ambapo alipewa kama jizya (zawadi). (Hii ilikuwa kabla ya Mohammad kumtambua)
Niliwatembeza hadi nikawaleta kwa Abu Bakr ambaye alinitunukiza huyu binti kama zawadi. Hivyo tukafika Medina. Sikuwa nimemvua buibui wakati mtume wa Allah (s.a.w) alipokutana nami njiani na kusema; “nipe huyu binti awe mke wangu.” (Sahih Muslim 4345)
Mohammad aliamuru kuuliwa kwa mkongwe aitwaye Abu Afak. Hii ilitendeka miaka miwili baada ya Mohammad kuingia Medina. Abu Afak akikuwa na umri wa miaka 120. ‘kosa’ lake likiwa kuandika mashairi ya kukashifu vitendo vya mtume wa Uislamu-Mohammad vya kuchinja na kuteka wanawake vitani.
Mohammad akasema, “Ni nani ataniadhibia huyu mtwana?” Hivyo mfuasi wake Mohammad akainuka na kumuua Abu Afak. (Ibn Ishaq/Hisham 995).
Alipokuwa anamuua Abu Afak, inasemekana muuaji alimkejeli na kuingiza kisu tumboni mwake na kusema, “chukua hicho Abu Afak, licha ya umri wako.” (Ibn Ishaq/Hisham 995)
Baadaye, Mohammad aliuwa mwanamke aliyekuwa na watoto watano kwa kupinga mauaji ya Abu Afak. Mtume bandia wa Allah aliuwa kila ambaye alipinga mambo yake, badala ya kukumbana na wapinzani wake kwa mjadala wa maantiki.
Vilevile, mkongwe mwingine aliuliwa kutokana na amri ya Mohammad ya kuuwa mtu yeyote kule Mekka ambaye sio mwislamu kufuatia utekaji wa mji huo mwaka 630. (Sehemu ya kuran ya sura ya 9 inaamuru kuchinja). Kifo cha huyu mtu kimenukuliwa kwenye kitabu cha Bukhari:
Mtume alisoma Suratan-Najm (103) akiwa Makka huku akiwa amelala chali na waliokuwa pamoja naye walifanya vivo hivyo isipokuwa mkongwe mmoja aliyechukua funda la mchanga na kuiweka kichwani kisha kusema; “hii yanitosha.” Baadaye, nikaona anauliwa kama kafir. (Bukhari 19:173)
**ni kawaida ya waislamu kulalamika kuwa dini yao inakashifiwa na allah wao kutukanwa. Nataka kuwataarifu kuwa hizo NUKUU sio zangu bali zimenukuliwa kutoka kwa vitabu vya Kiislamu. Mimi ni mjumbe tu.**
Ndugu msomaji, leo umejifunza kwa kutumia vitabu vyao kuwa Allah alimruhusu Muhammad kuuwa vikongwe na ajuza. Hakika hakuna dhambi mbaya kama ya kuuwa vikongwe na ajuza pamoja na watoto kama alivyo fanya Muhammad nabii wa Allah.
MUHAMAMD ALIVUNJA AMRI KUU YA SITA KWA KUFANYA HAYO MAUWAJI.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu. Toto 2:13
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

UNAYAFAHAMU MAJINA YA MUNGU AMBAYO HAYAPO KWENYE UISLAM?






Majina gani tofauti ya Mungu na yanamaanisha nini?
Kila majina mengi ya Mungu huelezea kipengele tofauti cha tabia Yake nyingi. Hapa ni baadhi ya majina ya Mungu inayojulikana zaidi katika Biblia:
EL, ELOAH: Mungu "mwenye ezi, mwenye nguvu, maarufu" (Mwanzo 7: 1; Isaya 9: 6) — kietimolojia, El inaonekana kumaanisha "nguvu," kama "nina uwezo wa kukudhuru" (Mwanzo 31:29). El inahusishwa na sifa zingine, kama uaminifu (Hesabu 23:19), wivu (Kumbukumbu la Torati 5: 9), na huruma (Nehemia 9:31), lakini wazo la mizizi la nguvu linabaki.
ELOHIM: Mungu "Muumba, Mwenye ezi na Nguvu" (Mwanzo 17: 7; Yeremia 31:33) — aina ya wingi ya Eloah, ambayo inashughulikia mafundisho ya Utatu. Kutoka kwa sentensi ya kwanza ya Biblia, asili ya juu ya nguvu za Mungu inaonekana kama Mungu (Elohim) inaongea ulimwengu kuwapo (Mwanzo 1: 1).
EL SHADDAI: "Mungu Mwenye Nguvu," "Mwenye Nguvu wa ya Yakobo" (Mwanzo 49:24; Zaburi 132: 2,5) — huzungumzia nguvu ya Mwenyezi Mungu juu ya yote.
ADONAI: "Bwana" (Mwanzo 15: 2; Waamuzi 6:15) — kutumika katika nafasi ya YHWH, ambayo ilikuwa inachukuliwa na Wayahudi kuwa takatifu sana ili kutamukwa na wanadamu wenye dhambi. Katika Agano la Kale, YHWH hutumiwa mara nyingi katika matendo ya Mungu na watu wake, wakati Adonai inatumiwa zaidi wakati anavyofanya na Mataifa.
YHWH / YAHWEH / YEHOVA: "BWANA" (Kumbukumbu la Torati 6: 4; Danieli 9:14) — kwa kusema, jina pekee la Mungu. Ilitafsiriwa katika maandiko ya Kiingereza "BWANA" (miji yote) ili kuitenganisha kutoka Adonai, "Bwana." Ufunuo wa jina hulitolewa kwanza kwa Musa "MIMI NIKO AMBAYE NIKO" (Kutoka 3:14). Jina hili linafafanua haraka, uwepo. Yahweh yupo, anaweza kupatikana, karibu na wale wanaomwita kwa ajili ya ukombozi (Zaburi 107: 13), msamaha (Zaburi 25:11) na mwongozo (Zaburi 31: 3).
YAHWEH-JIREH: "Bwana Atatoa" (Mwanzo 22:14) — jina lililokumbukwa na Ibrahimu wakati Mungu alipomtoa kondoo awe dhabihu badala ya Isaka.
YAHWEH-RAPHA: "Bwana anayeponya" (Kutoka 15:26) — "Mimi ni Yehova anayekuponya" kwote katika mwili na nafsi. Katika mwili, kwa kuhifadhi na kuponya magonjwa, na katika roho, kwa kusamehe uovu.
YAHWEH-NISSI: "Bwana Bendera yetu" (Kutoka 17:15), ambapo bendera inaeleweka kuwa mahali pa kupatanisha. Jina hili linakumbuka ushindi wa jangwa juu ya Waamaleki katika Kutoka 17.
AHWEH-M'KADDESHY: "Bwana atakayetakasa, hufanya Mtakatifu" (Mambo ya Walawi 20: 8; Ezekieli 37:28) — Mungu anaweka dhahiri kwamba Yeye pekee, sio sheria, anaweza kuwasafisha watu wake na kuwafanya watakatifu.
YAHWEH-SHALOM: "Bwana Wa Amani Yetu" (Waamuzi 6:24) — jina ambalo Gidioni alipewa kwenye madhabahu aliyoijenga baada ya malaika wa Bwana kumhakikishia kwamba hatakufa kwa kumwona.
YAHWEH-ELOHIM: "BWANA Mungu" (Mwanzo 2: 4; Zaburi 59: 5) — Mchanganyiko wa jina la Mungu la kipekee YHWH na "Bwana" wa kawaida, akiashiria kwamba Yeye ni Bwana wa Mabwana.
YAHWEH-TSIDKENU: "Bwana Wa Haki Yetu" (Yeremia 33:16) — Kama ilivyo na YHWH-M'Kaddesh, ni Mungu peke yake ambaye hutoa haki kwa mwanadamu, hatimaye katika mwanadamu wa Mwanawe, Yesu Kristo, aliyekuwa mwenye dhambi kwa ajili yetu "ili tuweze kuwa waadilifu wa Mungu ndani yake" (2 Wakorintho 5:21).
YAHWEH-ROHI: "Bwana Mchungaji Wetu" (Zaburi 23: 1) — Baada ya Daudi kutafakari uhusiano wake kama mchungaji kwa kondoo wake, aligundua kwamba ilikuwa ni uhusiano wa kweli na Mungu, na hivyo anasema, "Yahweh-Rohi Ni Mchungaji wangu. Sitataka "(Zaburi 23: 1).
YAHWEH-SHAMMAH: "Bwana yupo" (Ezekieli 48:35) — jina ambalo limeandikwa kwa Yerusalemu na Hekalu pale, kuonyesha kwamba utukufu wa Bwana uliopita mara moja (Ezekieli 8-11) ulirudi (Ezekieli 44: 1) -4).
YAHWEH-SABAOTH: "Bwana wa Wenyeji" (Isaya 1:24; Zaburi 46: 7) — Mwenyiji inamaanisha "vikundi," vyote vya malaika na wanadamu. Yeye ndiye Mwenyeji wa mbinguni na wanaoishi duniani, Wayahudi na mataifa, yenye matajiri na maskini, bwana na mtumwa. Jina hilo linaelezea ukuu, nguvu, na mamlaka ya Mungu na inaonyesha kwamba anaweza kukamilisha kile anachoamua kufanya.
EL ELYON: "Wa Juu Zaidi" (Kumbukumbu la Torati 26:19) — linatokana na mizizi ya Kiebrania kwa "kwenda juu" au "kupaa," hivyo maana ni ya kile kilicho juu zaidi.El Elyon inaashiria kuinua na kusema juu ya haki kabisa Kwa utawala.
EL ROI: "Mungu wa Kuona" (Mwanzo 16:13) — jina la Mungu lililowekwa na Hagari, pekee na kukata tamaa jangwani baada ya kufukuzwa na Sara (Mwanzo 16: 1-14). Wakati Hagari alipokutana na Malaika wa Bwana, aligundua kuwa amemwona Mungu Mwenyewe katika theophany. Pia alitambua kwamba El Roi alimwona katika dhiki yake na akashuhudia kwamba Yeye ni Mungu anayeishi na kuona yote.
EL-OLAM: "Mungu wa Milele" (Zaburi 90: 1-3) — Hali ya Mungu haina mwanzo au mwisho, bila vikwazo vyote vya wakati, na Yeye ana ndani yake mwenyewe sababu ya wakati yenyewe. "Kutoka milele hata milele, Wewe ni Mungu."
EL-GIBHOR: "Mungu Mwenye Nguvu" (Isaya 9: 6) — jina linaloelea Masiha, Yesu Kristo, katika sehemu hii ya unabii wa Isaya. Kama mwenye ngumu na mpiganaji mkuu, Masiha, Mungu mwenye nguvu, anaweza kutimiza uharibivu wa madui wa Mungu na kuongoza na chuma ya shaba. (Ufunuo 19:15)
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

UNAMJUA KAFIRI WA KWANZA DUNIANI?

Image may contain: one or more people and text
Je, Makafiri ni akina nani?
Je, unawafahamu makafiri wa kwanza ni akina nani?
Neno kafiri ni neno ambalo lipondani ya Biblia Takatifu, kabla hata ya Muhammad mtume wa waislamu kuzaliwa na wala uislamu haujakuwepo nawala Muhammad wala Quran haijaandikwa nawale Waarabu wa 4. Neno hilo kafiri lipo kwenye biblia kwa maana nyepesi neno hilo waislamu wamekuta likitumiwa na waliokuwa wanatumia Biblia Takatifu.
Katika Quran sijaona Wakristo wakiitwa MAKAFIRI, bali Quran nzima inawaita WAKRISTO wamchao Mungu tena wasomi, SURATUL AL-MAIDAH 5:82.
Kwa kuthibitisha kuwa neno KAFIRI limo ndani ya BIBLIA hebu tuziangalie aya chache ndani ya Biblia.
EZEKIEL 34: 28-31
Mistari hiyo ni Mungu mwenyewe anawahakikishia wana wa Israel kuwa hawatakuwa mateka wa MAKAFIRI, hivyo neno hilo hapo limetumika kabla hata uislamu haujakuwepo.
NEHEMIA 5: 8-9
NEHEMIA 5:17
NEHEMIA 6:16
MAOMBOLEZO 1:3
MAOMBOLEZO 1:10
MAOMBOLEZO 5:2
1TIMOTHEO 1:8-11
YUDA 1:4
1YOHANA 4:1-6
Maneno hayo yalisemwa kabla ya Muhammad hajazaliwa wa Quran haijaandikwa nawale waarabu wa 4 yaani Saydina Abubakar, Omar, Athumani na Ali na uislamu ulikuwa haupo.
TUANGALIE NENO KAFIRI LINAVYOTUMIKA
_________________________
Neno KAFIRI ni neno la Kiarabu lenye maana ya Mpingaji kwa kiswahili.
Yaani anaepinga maneno ya Mwenyezi Mungu neno hili lilikuwepo kwenye Biblia kama tulivyoona kwenye baadhi ya mistari ya Biblia hapo juu.
Ilikuwepo neno mpingaji KAFIRI nilazma kuwepo na kauli tangulizi iliyotangulia kusema kwahiyo kauli itakayofuata ya kupinga inaitwa kauli ya mpingaji kwa kiarabu KAFIRI.
Waislamu mara zote hukosi kuwasikia wakisema hawa MAKAFIRI wanatupa tabu au tuwakomeshe au wapigwe hawa MAKAFIRI kauli zao hizo zikitulenga sisi WAKRISTO.
SWALI LA UFAHAMU
Kati ya WAKRISTO au WAISLAMU nani MAKAFIRI?
2) Kati ya Imani ya KIKRISTO na dini ya KIISLAMU ni nani ilitangulia kuwepo duniani?
3) Kati ya YESU na Muhammad ni nani aliyepinga kauli ya mwenzake iliyotangulia?
HISTORIA FUPI KATI YA YESU NA MUHAMMAD.
Bwana Yesu ndiye mwanzilishi wa Imani ya Kikristo.
Waebrania 12:2
Huu ni mwaka 2015 tangu bwana Yesu alipopaa kurudi mbinguni na ni mwaka wa 1436 kwa mwaka wa kiislamu niandiko somo hili la KAFIRI kwani Muhammad alizaliwa mwaka wa 570 nandiye mwanzilishi wa dini ya kiislamu baada ya Yesu.
Hii inathibitisha kuwa Yesu alitangulia kuwepo duniani kabla ya Muhammad hakuna anaepinga hilo.
Kwamaana hiyo kauli za Yesu zitakuwa tangulizi na kauli za IMANI ya Kikristo zitakuwa kauli tangulizi.
Na kauli za Muhammad na Waislamu zitakuwa kauli za kupinga tangulizi.
Yohana 9:35-38
Kauli ya kusema yeye ni Mwana wa Mungu alijisema yeye mwenyewe Yesu aliitumia mwenyewe katika mistari ya sura ya hapo juu.
Hiyo ni kauli tangulizi ikipatikana kauli inasema Yesu sio Mwana wa Mungu hiyo ni kauli inayopinga maanayake ni KAFIRI?
JE NI NANI ALIEANZA KUSEMA YESU NI MWANA WA MUNGU?
LUKA 1:26-35
Hivyo kwa kauli ya mistari ya hapojuu hakuna mwanadamu alieanza kutamka kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu bali ni Mungu mwenyewe kupitia malaika gabriel alietumwa ndie aliyesema Yesu ni Mwana wa Mungu.
MATHAYO 3:13-17
MATHAYO 17:1-15
Hii ni kauli tangulizi iliyotoka kwa Mungu mwenyewe inasema YESU ni mwanae kabla ya Muhammad kuzaliwa wala Quran haijaandikwa nawala uislamu haujaanzishwa kwani uislamu umeanza mwaka 610.
Hii ni kauli tangulizi inatoka kwa Mungu na ikapatikana kauli toka kwa nduguzetu waislamu Yesu sio Mwana wa Mungu huyo atakuwa ni mpingaji kwa kiarabu ni KAFIRI.
JE KAFIRI WA KWANZA NI NANI?
Mungu alipoumba vitu vyoote kisha akamuumba mwanadamu na kumpa maagizo.
MWANZO 2:16-17
Hii kauli tangulizi ya Mwenyezi Mungu kauli itakatopinga kauli hii ni ya mpingaji ambae ni KAFIRI.
Tuangalie kauli iliyopinga kauli ya Mwenyezi Mungu tangulizi ni ya nani?
MWANZO 3:1-4
MUNGU amesema ukila matunda utakufa hakika, anakuja nyoka Shetan Ibilisi anasema HAKIKA HAMTAKUFA. hii ni kauli ya kupinga huyu ni KAFIRI.
Hivyo ukimsikia mtu anasema Yesu sio Mwana wa Mungu huyo ni KAFIRI.
QURAN INASEMAJE?
Surat an- Anaam 6:101 Yeye ndie muumba wa mbingu na ardhi inamkinikaje awe na mwana hali ana mke?
Kauli hii ya Quran ni ya ajabu inamaana Quran nikuwa Mungu awe na mke ndio awe na mtoto? Mawazo yao yakimwili ya kibinaadamu basi Quran inapinga kauli ya kwanza inayosema sisi ni wana wa Mungu si kimwili wala kidamu bali wote waliompokea walifanywa kuwa wana wa Mungu.
Lakini NENO la Mungu linasema.
YOHANA 3:10 KATIKA HILI WATOTO WA MUNGU NI DHAHIRI, NA WATOTO WA IBILISI NAO.
Mstari ukowazi kwamba wewe ukikataa kuwa si Mwana wa Mungu. Basi unae baba yako kwani ibilisi nae ana watoto.
Katika kitabu cha hadithi sahihi Muslim Vol 4. Wake wa Muhammad khadija, zainabu na salama wote hao wanaitwa "Ummul muuminun" yaani MAMA WA WAISLAMU. Inamaana waislamu wote wanawajibu wa kuwaita wa za Muhammad mama zao?
SWALI LA UFAHAMU?
Je Waislamu kwa kuwaita wake za Muhammad mama zao inamaana ndio waliowazaa Waislamu wote?
___________________________
Ukristo ulitangulia kuwepo duniani kabla ya uislamu kwa maana hiyo kauli za uislamu ni kupinga kauli tangulizi za Ukristo yaani wapingaji kwa kiarabu ni KAFIRI.
KUMBE BASI WAISLAM, ALLAH, MUHAMMAD NA JIBRIL NI MAKAFIRI.
Tafakari chukua hatua.
Barikiwa sana
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

YESU NI MUNGU MWENYE KUHIDIMIWA MILELE

Image may contain: text
Warumi Mlango 9:5 ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina. 

Neno la Mungu linatuambia yafuatayo:
1. Yesu yupo Juu ya mambo yote.
2. Yesu ni Mungu.
3. Yesu ni mwenye kuhidimiwa milele.

Tunapo sema Yesu ni Mungu huwa hatubahatishi.

Shalom,

Max Shimba Mtumwa wa Yesu kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

JE, YESU KRISTO NI MUNGU?

No automatic alt text available.

Mungu maana yake nini?
Mungu siyo jina bali ni sifa na hakuna mtu anayeitwa jina (Mungu). Nisawa sawa na kusema "Raisi". Hili neno Raisi sio jina bali ni wasifa wa mtu. Yeye ndiye Chanzo cha habari njema inayopatikana katika Biblia. (1 Timotheo 1:11) Kwa kuwa Mungu ndiye aliyetuumba, tunapaswa kumwabudu yeye peke yake.​—Soma Ufunuo 4:11.
Mungu ni Mmoja, lakini Yeye yupo katika nafsi tatu-Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu (Mathayo 3: 16-17). Mungu hana mwisho (1 Timotheo 1:17), hawezi kulinganishwa (2 Samweli 7:22), na hawezi kubadilika (Malaki 3: 6). Mungu yupo kila mahali (Zaburi 139: 7-12), anajua kila kitu (Mathayo 11:21), na ana nguvu zote na mamlaka (Waefeso 1; Ufunuo 19: 6).
Je , Yesu anazo hizo sifa za kipekee za Mungu?
Mungu akawa mwili (Yohana 1:14). Mwana wa Mungu akawa Mwana wa Mtu na hivyo ni "daraja" kati ya Mungu na mwanadamu (Yohana 14: 6, 1 Timotheo 2: 5). Kwa njia ya Mwana tu tunaweza kuwa na msamaha wa dhambi (Waefeso 1: 7), upatanisho na Mungu (Yohana 15:15, Warumi 5:10), na wokovu wa milele (2 Timotheo 2:10). Katika Yesu Kristo "ukamilifu wote wa Uungu huishi katika hali ya mwili" (Wakolosai 2: 9). Hivyo, kwa kweli kujua Mungu ni nani, tunapaswa kufanya ni kuangalia Yesu.
Mungu wetu tunayemwabudu jina lake ni YEHOVA, yeye ni Mungu wa Biblia Takatifu.
Kutoka 6:2, 3
Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.
Mwana tunayemwamini ni Yesu ambaye ni Kristo.
Yohana 3:36
Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.
Roho tunayoiamini ni Roho ya Kristo ambayo ni nguvu za utendaji kazi ya Mungu.
Isaya 1:25; 40:10, Ezekieli 3:14.
Pia Yesu akiri akisema hivi katika injili yake kama alivyoandika mtume Luka:
Luka 11:20
Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia
KWANINI TUNASEMA YESU NI MUNGU?
Matamshi ya Yesu mwenyewe na mitume wake kuhusu Uungu wake.
Tuanze kuangalia uthibitsho wa aya za Biblia zinazomtaja Yesu kuwa Mungu:
Mathayo 1:23-25
“Tazama; bikra atachukua mimba; naye atazaa mwana; nao watamwita jina lake Emanueli; yaani Mungu pamoja nasi”.
Tabia ya Yesu inaonyesha kuwa kama mwanadamu, kuzaliwa kwake kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Hapa tunaona jinsi alivyo na uwezo tofauti na wanadamu akiwa anafahamu mambo mengi kabla yatokee, hiyo ni sifana uwezo kama wa Mungu..
Mathayo 18:20
“Kwa kuwa walipo wawili watatu, wamekusanyika kwa jina langu, mimi nipo papo hapo katikati yao”.
Mwenye uwezo wa kukaa mahali pote ni Mungu.
1 Yohana. 5:20
“Nasi twajua kuwa Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli., yaani ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye MUNGU WA KWELI NAUZIMA WA MILELE”.
Yohana 20:26-29
“basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu na milango ilikuwa imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu. Kisha akamwambia Tomaso lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu; wala usiwe asiyeamini; bali aaminiye. Tomaso akajibu akamwambia, BWANA WANGU NA MUNGU WANGU.
Tito 2:13
Tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu Mkuu na Mwokozi wetu
Warumi 9:5
“Na katika hao alitoka KRISTO KWA NJIA YA MWILI, NDIYE ALIYE JUU YA MAMBO YOTE, MUNGU, MWENYE KUHIMIDIWA MILELE.AMINA.
Yesu Kristo ni mtawala juu ya vyote, hii ni moja kati ya sifa za Uungu Wake.
Yohana 3:30
“Yeye ajaye kutoka juu, huyo yu juu ya vyote. Yeye aliye wa dunia asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani,yeye ajaye kutoka mbinguni yuu juu ya yote” (Yohana 13:13) “Ninyi mwaniita , Mwalimu, na Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo“. ( WARUMI 14:9 ) “Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii,awamiliki waliokufa na walio hai pia”. Neno kumiliki ni kutawala sifa ya kutawala ni sifa ya Mungu.
Yesu Kristo ni zaidi ya mtu awayeyote, manabii au mitume wote.
(Waebrania 3:1-7)“Mustari 3 unasema, Kwa maana huyo amehesabiwa kuwa amestahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile yeye atengenezaye nyumba alivyo na heshima zaidi ya hiyo nyumba”.. Anayezungumziwa hapa ni Yesu Kristo Mungu muumbaji. YESU, ameketi mkono wa kuume wa ukuu huko mbinguni (Waebrania 1 :3-4).
Matamshi ya Yesu mwenyewe na mitume wake kuhusu Uungu wake.
Yohana 10:30-33
“Yesu akawajibu, kazi njema nyingi niwewaonyesha zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe? Wayahudi wakamjibu, kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru,na kwasababu wewe uliye. mwanadamu wajifanya kuwa Mungu.
Wafilipi 2:5-6
“Ambaye yeye mwanzo alikuwan yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho, bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu”.
Yesu anaitwa Neno la Mungu Yohana 1:1, Ufunuo 19:13 “Kwahiyo Neno ni Mungu” .. na huyo ndiye aliyevifanya kuwako vitu vyote.Aliyeshuka kutoka juu na kufanyika mwili ni Yesu pekee aliyezaliwa na bikira Mariamu bila mbegu ya kiume kama inavyotokea kwa wanadamu wengine..Katika yeye vtu vyote viliumbwa (Wakolosai 1:13-16) vinavyoonekana na visivyoonekana; vya mbinguni na vya duniani. Maandiko yako wazi kabisa kwa mtu mwenye Roho wa Mungu anaelewa kwa urahisi.
Hapa ni baadhi ya sifa za Yesu Mungu Mkuu kama ilivyofunuliwa katika Biblia:
Mungu ni wa haki (Matendo 17:31), mwwenye upendo (Waefeso 2: 4-5), mwenye kweli (Yohana 14: 6), na mtakatifu (1 Yohana 1: 5). Mungu anaonyesha huruma (2 Wakorintho 1: 3), huruma (Warumi 9:15), na neema (Warumi 5:17). Mungu anahukumu dhambi (Zaburi 5: 5) lakini pia hutoa msamaha (Zaburi 130: 4).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

YEHOVA NI NANI?

Image may contain: night
Katika Biblia Takatifu, Mungu anasema: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.” (Isaya 42:8) Ingawa ana majina mengi ya cheo kama vile “Mungu Mweza-Yote,” “Bwana Mwenye Enzi Kuu,” na “Muumba,” anawaheshimu waabudu wake kwa kuwaalika wamwite kwa jina lake la kibinafsi.—Mwanzo 17:1; Matendo 4:24; 1 Petro 4:19.
Biblia inamtaja Yehova kuwa Mungu wa Kweli, Muumba wa kila kitu. (Ufunuo 4:11) Manabii kama Abrahamu na Musa walimtumikia. (Mwanzo 24:27; Kutoka 15:1, 2; Yohana 20:17) Yeye si Mungu wa watu fulani pekee, bali wa “dunia yote.”—Zaburi 47:2.
YHWH / YAHWEH / YEHOVA: "BWANA" (Kumbukumbu la Torati 6: 4; Danieli 9:14) — kwa kusema, jina pekee la Mungu. Ilitafsiriwa katika maandiko ya Kiingereza "BWANA" (miji yote) ili kuitenganisha kutoka Adonai, "Bwana." Ufunuo wa jina hulitolewa kwanza kwa Musa "MIMI NIKO AMBAYE NIKO" (Kutoka 3:14). Jina hili linafafanua haraka, uwepo. Yahweh yupo, anaweza kupatikana, karibu na wale wanaomwita kwa ajili ya ukombozi (Zaburi 107: 13), msamaha (Zaburi 25:11) na mwongozo (Zaburi 31: 3).
Kama inavyoonyeshwa katika Biblia, Yehova ni jina la pekee la Mungu. (Kutoka 3:15; Zaburi 83:18) Linatokana na kitenzi cha Kiebrania kinachomaanisha “kuwa,” na wasomi wengi wanaona kwamba jina hilo linamaanisha “Husababisha Iwe.” Maana hii inapatana kabisa na cheo chake akiwa Muumba na Mtimizaji wa makusudi. (Isaya 55:10, 11) Biblia inatusaidia pia kuelewa utu wa Yehova, hasa sifa yake kuu ya upendo.—Kutoka 34:5-7; Luka 6:35; 1 Yohana 4:8.
Jina Yehova limetafsiriwa kutoka kwa jina la Mungu katika lugha ya Kiebrania lenye herufi nne za Tetragramatoni יהוה (YHWH).
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

KWA NINI TUNASHEREKEA EID YA KRISMASI?

Image may contain: text
Shalom Wapendwa,
Krismasi maana yake nini?
“Krismasi,” kinasema kitabu cha Encyclopedia of Religion, inamaanisha “‘Misa ya Kristo,’ yaani, misa ya kusherehekea kuzaliwa kwa Kristo.”
Tunasherekea sikukuu (IDI) ya Kristmasi kwa kukumbuka kuzaliwa Mwokozi, Masihi wetu yaani Yesu Kristo wa Nazareti. Zaidi ya hapo, sikukuu ya kuzaliwa husherekewa mtu anapo kuwa hai, kumbe basi tunasherekea Yesu Kristo aliye hai milele yote.
Hivyo basi naweza kusema kuwa tunasherekea kukumbuka ujio wa Wokovu kwa Mwanadamu. Sote twafahamu kwamba mwanadamu alipotea baada ya lile anguko la dhambi ya Adamu na Hawa pale bustani ya Eden.
Mwanadamu alikuwa amehesabiwa kutokuwa na maisha ya raha ya umilele. Lakini kwa kuwa Mungu aliupenda ulimwengu, yaani Bwana Mungu alikupenda wewe na mimi ndipo akamtuma mwanaye wa pekee Yesu Kristo ili kila amuaminie awe na uzima wa milele, tele (Yohana 3:16). Kwa lugha nyepesi ni kwamba tunasherekea siku hii kukumbuka WOKOVU aliouleta Bwana Yesu Mungu Mkuu na Mwokozi wetu; Soma Tito 2:13, maana ndani yake ndimo kuna maisha halisi ya umilele.
Nabii isaya alitabili kuzaliwa kwa Yesu (takribani miaka 700 kabla ya kuzaliwa kwake Bwana Yesu Kristo) akisema;
"...bikira atachukua mimba,atazaa mtoto mwanamume,naye atamwita jina lake Imanueli." Isaya 7:14
Tabiri hii ya Nabii Isaya ni hakika na kweli. Zipo tabiri nyingi zilizowahi kutolewa, lakini tabiri ya Nabii Isaya imekamilika maana hakika Bwana amezaliwa. Kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni muujiza ambao haukuwai kutokea wala haitegemewi kutokea, sababu kuzaliwa kwake kulitokana na uweza wa Roho Mtakatifu. Tena angali Bwana Yesu amezaliwa alikuwa tayari amekwisha vikwa uwezo, uweza na nguvu ndani yake.
Sasa waweza kufikiria kwamba ni mtoto gani anayezaliwa akiwa na utiisho wa ki-Mungu kama huo, kwa sababu Biblia inaanza kumuelezea kwamba alipozaliwa tu aliitwa mtoto MWANAMUME, yaani si mtoto wa kiume bali ni mwanamume ikionesha tayari alikuwa na nguvu za kipekee tena Yeye ni Imanueli Mungu pamoja nasi, soma Mathayo 1:23.
Biblia inasema;
"Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana." Wagalatia 4:4-5
Kumbe kabla ya ujio na kumpokea Bwana Yesu Kristo sisi tulikuwa chini ya sheria. Tukiitumikia miungu ya baba zetu, tulikuwa watu tusiokuwa na Mungu duniani. Hivyo basi hatukuweza kufanyika wana wa Mungu, bali ingawa tulikuwa ni watu wa Mungu tu.
Tunasherekea sikukuu hii kwa kukumbuka ujio wa injili duniani.
Yesu mwenyewe ndio injili.
Yeye alipozaliwa, Injili ndio ilizaliwa kwa mara ya kwanza chini ya jua.
Maana Yeye ni Neno, Injili ni habari njema ziletazo wokovu, hivyo ni neno la Mungu liletalo wokovu. Biblia imeeleza vizuri sana jambo hili, inasema;
" Malaika akawaambia, msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;" Luka 2:10
Malaika wa Bwana anatambulisha kuwa ujio wa Yesu Kristo duniani ni ujio wa habari njema ya furaha. Yaani ni ujio wa injili, maana injili ina furaha ndani yake, hivyo siku ya leo tunaposherekea sikukuu hii, tunakumbuka ujio wa habari njema chini ya jua.
Kumbe basi, hakuna kosa lolote lile kusherekea na kukumbuka ujio wa WOKOVU NA HABARI NJEMA.
Je, upo tayari kusherekea na kufurai kuwa Wokovu na Habari njema umekuja kwa ajili yako?
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13
Shalom Wapendwa,
Krismasi maana yake nini?
“Krismasi,” kinasema kitabu cha Encyclopedia of Religion, inamaanisha “‘Misa ya Kristo,’ yaani, misa ya kusherehekea kuzaliwa kwa Kristo.”
Tunasherekea sikukuu (IDI) ya Kristmasi kwa kukumbuka kuzaliwa Mwokozi, Masihi wetu yaani Yesu Kristo wa Nazareti. Zaidi ya hapo, sikukuu ya kuzaliwa husherekewa mtu anapo kuwa hai, kumbe basi tunasherekea Yesu Kristo aliye hai milele yote.
Hivyo basi naweza kusema kuwa tunasherekea kukumbuka ujio wa Wokovu kwa Mwanadamu. Sote twafahamu kwamba mwanadamu alipotea baada ya lile anguko la dhambi ya Adamu na Hawa pale bustani ya Eden.
Mwanadamu alikuwa amehesabiwa kutokuwa na maisha ya raha ya umilele. Lakini kwa kuwa Mungu aliupenda ulimwengu, yaani Bwana Mungu alikupenda wewe na mimi ndipo akamtuma mwanaye wa pekee Yesu Kristo ili kila amuaminie awe na uzima wa milele, tele (Yohana 3:16). Kwa lugha nyepesi ni kwamba tunasherekea siku hii kukumbuka WOKOVU aliouleta Bwana Yesu Mungu Mkuu na Mwokozi wetu; Soma Tito 2:13, maana ndani yake ndimo kuna maisha halisi ya umilele.
Nabii isaya alitabili kuzaliwa kwa Yesu (takribani miaka 700 kabla ya kuzaliwa kwake Bwana Yesu Kristo) akisema;
"...bikira atachukua mimba,atazaa mtoto mwanamume,naye atamwita jina lake Imanueli." Isaya 7:14
Tabiri hii ya Nabii Isaya ni hakika na kweli. Zipo tabiri nyingi zilizowahi kutolewa, lakini tabiri ya Nabii Isaya imekamilika maana hakika Bwana amezaliwa. Kuzaliwa kwa Bwana Yesu ni muujiza ambao haukuwai kutokea wala haitegemewi kutokea, sababu kuzaliwa kwake kulitokana na uweza wa Roho Mtakatifu. Tena angali Bwana Yesu amezaliwa alikuwa tayari amekwisha vikwa uwezo, uweza na nguvu ndani yake.
Sasa waweza kufikiria kwamba ni mtoto gani anayezaliwa akiwa na utiisho wa ki-Mungu kama huo, kwa sababu Biblia inaanza kumuelezea kwamba alipozaliwa tu aliitwa mtoto MWANAMUME, yaani si mtoto wa kiume bali ni mwanamume ikionesha tayari alikuwa na nguvu za kipekee tena Yeye ni Imanueli Mungu pamoja nasi, soma Mathayo 1:23.
Biblia inasema;
"Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana." Wagalatia 4:4-5
Kumbe kabla ya ujio na kumpokea Bwana Yesu Kristo sisi tulikuwa chini ya sheria. Tukiitumikia miungu ya baba zetu, tulikuwa watu tusiokuwa na Mungu duniani. Hivyo basi hatukuweza kufanyika wana wa Mungu, bali ingawa tulikuwa ni watu wa Mungu tu.
Tunasherekea sikukuu hii kwa kukumbuka ujio wa injili duniani.
Yesu mwenyewe ndio injili.
Yeye alipozaliwa, Injili ndio ilizaliwa kwa mara ya kwanza chini ya jua.
Maana Yeye ni Neno, Injili ni habari njema ziletazo wokovu, hivyo ni neno la Mungu liletalo wokovu. Biblia imeeleza vizuri sana jambo hili, inasema;
" Malaika akawaambia, msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;" Luka 2:10
Malaika wa Bwana anatambulisha kuwa ujio wa Yesu Kristo duniani ni ujio wa habari njema ya furaha. Yaani ni ujio wa injili, maana injili ina furaha ndani yake, hivyo siku ya leo tunaposherekea sikukuu hii, tunakumbuka ujio wa habari njema chini ya jua.
Kumbe basi, hakuna kosa lolote lile kusherekea na kukumbuka ujio wa WOKOVU NA HABARI NJEMA.
Je, upo tayari kusherekea na kufurai kuwa Wokovu na Habari njema umekuja kwa ajili yako?
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

NENO IDI MAANA YAKE NINI?

Image may contain: 4 peopleWAISLAM WENGI HAWAJUI MAANA YA NENO IDI.
NENO IDI MAANA YAKE NINI?
“Wakristo wengi husilimishwa kwa sababu ya kutojua lugha ya kiarabu”
Najua pengine unaweza usinielewe, Ila huo ndiyo ukweli, na mimi mwenyewe kabla sijaachana na Uislamu, nilishawahi kushuhudia, mke wa mchungaji wa Kanisa la BAPTISTI, akisilimishwa katika viwanja vya Mkanyenye Mwanza, kwa sababu ya kukuta neno Eid (عيد) Ndani ya BIBLIA, katika Tafsiri ya kiswahili cha zamani, ambacho katika Kumbukumbu la torati, 16:14 Kiliandika Idi.
Kumbukumbu 16: 14 nawe utafurahi katika Idi yako, wewe, na mwanao, na binti yako, na mtumwa wako, na mjakazi wako, na Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako.
👉Aliposomewa andiko hilo, akaulizwa kwamba, “Wanaosherehekea Sikukuu ya Idi ni watu wa dini gani?” akajibu “Waislamu” akaambiwa, Biblia inautambua Uislamu, akasilimu!
👉Siyo huyo tu Kuna mwingine, pia, alisilimishwa, kwa sababu ya neno Shehe ndani ya Biblia.
Nehemia 5:17 Pamoja na hayo wakawako mezani pangu, katika Wayahudi na mashehe, watu mia na hamsini, zaidi ya wale waliotujia kutoka kwa makafiri waliotuzunguka.
Mtu anaulizwa, Masheikh ni watu wa dini gani? Akijibu kwamba ni waislamu, basi hutakiwa kusilimu, ili aungane na Masheikh katika Uislamu.
👉Leo nataka nikifundishe, ili kukutoa kwenye huo utata! Ili hata kama watakakuja kukudanganya, basi uwaumbue, kwa sababu utakuwa umeshaelewa. nikianza na neno Idd.
👉Neno Iddi, ni neno la Lugha ya Kiarabu, kiswahili, kimechukua maneno mengi ya lugha ya Kiarabu, wakati wa kutafsiri, waliliweka kama lilivyo, yaani Iddi.
Katika kiswahili, Idi ni sikukuu, iliposemwa utafurahi katika Idi yako, maana yake utafurahi katika sikukuu yako.
Ukisoma katika Biblia ya Kiarabu, kila palipotajwa sikukuu kumeandikwa Iddi. Mfano Yohana 14:6
انجيل يو حنا
6: 4 وَكَانَ الْفِصْحُ عِيدُ الْيَهُودِ قَرِيباً.
Hapo nimenukuu Injili ya Yohana katika Lugha ya kiarabu, inasema:-
وَكَانَ الْفِصْحُ (Wakaana Al’fisuhu)
Nayo Pasaka 👆
عيد اليهود
Sikukuu ya Wayahudi (Eid al’yahuud)
قريبا
ilikuwa Karibu. (Qariiban)
Katika Kiarabu limetumika neno عيد (Idi) Likimaanisha sikukuu, kama katikaTafsiri ya kiswahili lingewekwa kama lilivyo, ingesomeka “Nayo Pasaka Iddi ya Wayahudi, Ilikuwa karibu,
Sikukuu yo yote kiarabu ni Idi, Sikukuu ya Muungano, ni Idi ya muungano, Unaweza kusema:-
👉Iddi ya Muungano
👉Iddi ya wapendao
👉Iddi ya Uhuru
👉Iddi ya Krismasi
Kwa sababu Neno Idi lina maana ya sikuu, na ndani ya Quran hakuna sehemu kumeandikwa, Sherehekeni Sikukuu ya Iddi, maana ni sawa na kusema, Sherehekeeni Sikukuu ya Sikukuu, hapo inakuwa haijakaa sawa, maana ni neno moja. Kwa hivyo usiyumbishwe, hakuna sikukuu ya Idmdi bali Idi ndo sikukuu.
Hata Waislamu wenyewe, Iddi (Sikukuu) Wamezipa majina yao.
👉Eid El fitry (Sikukuu baada ya mfungo wa mwezi ramadhani)
👉Eid El hajj (sikukuu ya kuchinja)
Tuje kwenye Neno Sheikh (Shehe) Neno hilo pia halina mahusiano kabisa na Dini, maana neno Sheikh, ni neno la Kiarabu, likiwa na maana ya mzee (شيخ)
Kwani hata ndani ya Quran neno hilo Sheikh (شيخ) Limetamkwa mara moja tu, na tena mtamkaji akiwa ni mwanamke, Sara akimsemea mumewe, katika.
Quran 11 SURATUL HUUD
ﻗَﺎﻟَﺖْ ﻳَﺎ ﻭَﻳْﻠَﺘَﻰ
ﺃَﺃَﻟِﺪُ ﻭَﺃَﻧَﺎْ ﻋَﺠُﻮﺯٌ ﻭَﻫَـﺬَﺍ
ﺑَﻌْﻠِﻲ ﺷَﻴْﺨًﺎ ﺇِﻥَّ ﻫَـﺬَﺍ
ﻟَﺸَﻲْﺀٌ ﻋَﺠِﻴﺐٌ
72. (Mkewe Ibrahim)
akasema; Ee mimi we! Je,
nitazaa na hali mimi ni
mkongwe na huyu rnume wangu
ni mzee sana hakika hili ni
jambo la ajabu.
Sara katika kiarabu amesema:-
ﻭَﻫَـﺬَﺍ
ﺑَﻌْﻠِﻲ ﺷَﻴْﺨًﺎ
Na Mume wangu ni mzee, neno Hilo mzee kiarabu limetamkwa ﺷَﻴْﺨًﺎ yaani Sheikh
Ndilo neno pekee la Sheikh ambalo linapatikana ndani ya Quran, likiwa na maana ya mzee na siyo kiongozi wa Msikiti, au Kiongozi wa Dini, Kwani hata katika Biblia, kila palipotajwa mzee, Kiarabu ni ﺷَﻴْﺨًﺎ (Sheikh) Ushahidi huu hapa:- 👇
Walawi 19:32 Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana.
Katika kiswahili limetumika neno mzee, Kiarabu 👇🏻
19: 32 من امام الاشيب تقوم و تحترم وجه الشيخ و تخشى الهك انا الرب
Hapo kumetajwa, وجه الشيخ Uso wa Sheikh (mzee) Sheikh inatafsiri ya Mzee, na pia katika ushahidi mwingine, ni kwa Nikodemo.👇
Yohana 3:4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
Katika Kiswahili, Kumetajwa neno mzee, katika Kiarabu kumeandikwa hivi.👇
3: 4 قال له نيقوديموس كيف يمكن الانسان ان يولد و هو شيخ العله يقدر ان يدخل بطن امه ثانية و يولد
Hapo kumetajwa و هو شيخ Nae ni mzee yaani Sheikh, yaani Sheikh anawezaje kuingia tumboni kisha akazaliwa mara pili? Sheikh hiyo haina maana ya kiongozi wa dini, bali Sheikh kwa umri mkubwa. Mtu mzima asiweze kuingia tumboni.
Pia hata Wazee wa Kanisa, nao pia katika Kiarabu ni Masheikh.
Yakobo 5:14 Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
👆Hapo ni Kiswahili wametajwa wazee wa kanisa, Kiarabu 👇
5: 14 امريض احد بينكم فليدع شيوخ الكنيسة فيصلوا عليه و يدهنوه بزيت باسم الرب
Hapo kumesemwa, شيوخ الكنيسة
Masheikh wa Kanisa, Kumetumika uwingi, شيو خ Masheikh المكنسة wa makanisa.
Kwa hivyo usiyumbishwe na Lugha, kwa kusikia au kusoma neno liliotaja Neno Sheikh au shehe, ukadhani ni kiongozi wa kiislamu, hapana, bali limetumika kwa maana ya mzee. Nehemia kukaa na mashehe, inamaana ya Wazee, na siyo Waislamu.
BY USTADH MHUBIRI WA INJILI, ABEL SULEIMAN SHILIWA
Shalom

MUHAMMAD ALIVUNJA AMRI KUMI ZA MUNGU (SEHEMU YA TANO)

Image may contain: 5 people, people standing and text
Bibilia katika kitabu cha Kutoka 20: “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi uewayo na BWANA Mungu wako.” Amri hii kila mara inaamrisha kuwafanyia wazazi vyema kila wakati kwa heshima na nidhamu.
Ndugu msomaji,
Muhammad aliye kuwa bila ya Wazazi wake, ALIWALAANI WAZAZI WAKE NA KUWAITA MAKAFIRI.
KUMBE MAMA YAKE NABII MUHAMMAD ALIKUFA KAFIRI
Bi Amina mamake na Muhammad kafa kafiri. tunasoma
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((اسْتَأْذَنْتُ رَبِّي أَنْ أَسْتَغْفِرَ لأُمِّي فَلَمْ يَأْذَنْ لِي ، وَاسْتَأْذَنْتُهُ أَنْ أَزُورَ قَبْرَهَا فَأَذِنَ لِي )) مسلم
Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Niliomba ruhusa kutoka kwa Allaah kumuombea msamaha mamangu, lakini Hakunipa ruhusa. Nikamuomba idhini nilizuru kaburi lake (mamangu), Naye Akanipatia ruhusa)) [Muslim]
Inaelezwa katika Kitabu cha ‘Awn al-Ma’abuud:
“Kauli yake (Muhammad) ((lakini Hakunipa ruhusa)) ina maana kuwa (mama yake) alikuwa kafiri na hairuhusiwi kumuombea maghfirah kafiri.”
Huu ni msiba mwengine kwa Waislam. Wazazi wake Muhammad wote wamekufa na dhambi kubwa kubwa na huku wakiwa MAKAFIRI.
Hivi huyu Allah mbona aliwachukiwa sana wazazi wa Muhammad?
Je, unafahamu kuwa baba yake Muhammad na yeye alikufa akiwa KAFIRI na yupoe Jehannam?
Hakika kuna mambo ya ajabu ajabu kwenye uislamu.
LAKINI HATUSOMI KUWA MAMA YAKE YESU ALIKUFA NA DHAMBI.
MUHAMMAD AKIRI KUWA BABA YAKE YUPO JEHANNAM
Huu ni MSIBA MKUBWA sana kwa Waislam. Muhammad ambaye baba yake anaitwa Abdullah ikimaanisha "mtumwa wa Allah" imethibitshwa kuwa yupo Jehannam/motoni akichomeka.
Haya si maneno yangu na wala mimi simsingizii baba ya Muhammad, bali haya ni maneno ya Muhammad.
Soma uthibitisho hapa.
Imeripotiwa na Anas: Hakika, mtu mmoja alisema: Mjumbe wa Allah, baba yangu yuko wapi? Akasema: Yuko motoni. Alipogeuka kuondoka, akamwita na kusema: Hakika baba yangu na baba yako wako Motoni. (Sahih Muslim, Kitabu 001, Namba 0398).
Na swali ambalo tungependa wajiulize Waislam ni kuwa, kwa nini baba yake Muhammad, ambaye alikuwa mpagani aliitwa ‘Abdullah’?
Na kwa kuwa ‘Abdullah’ maana yake ni ‘mtumwa wa Allah’, hii ni ishara ya wazi kwamba wapagani wa kipindi cha jahiliyah walikuwa wakimwabudu Allah hadi kufikia kuwapa watoto wao majina kwa heshima ya Allah – kama ambavyo Wayahudi nao walikuwa wakiwapa watoto wao majina kwa heshima ya Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
Kwa mfano:
Yoshua – Yahwe ni wokovu;
Yothamu – Yahwe ni mkamilifu;
Yehoahazi – Yahwe ameshikilia;
Hezekia – Yahwe ametia nguvu;
Elisha – Mungu ni wokovu, n.k.
Jibu liko wazi. Allah alikuwa ni mungu wa kipagani aliyeabudiwa kabla ya Uislamu kuja. Na mungu huyu alikuwa ni ‘mungu mwezi’, yaani ‘al-ilah’. Jina lake jingine aliitwa ‘hubal.’ Mungu huyu wa kipagani aliabudiwa kote mashariki ya kati; wala si kwa Waarabu peke yake.
ZAIDI YA HAPO,
1. Kwanini Muhammad anakiri kuwa baba yake yupo Motoni?
2. Je, huyu Abdullah/abdallah alipata wapi hili jina lenye Allah ndani yake?
3. Je, inamaanisha kuwa Allah ambaye ni mungu wa kipagani alikuwepo kabla ya Muhammad?
Na ndiyo maana baba yake Muhammad, yaani Abdullah, alikoswakoswa kuchinjwa na babu wa Muhammad, yaani Abdul Muttalib. Abdul Muttalib alitaka kumchinja mwanawe huyo kama sadaka kwa Allah. Lakini mjomba wake Abdullah akamwokoa na hatimaye walichinjwa ngamia 100 badala yake.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo Mungu Mkuu. Tito 2:13

BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds

  BREAKING VIDEO: IDF pounding Hezbollah training compounds. The targets included a Radwan Force training facility used for weapons drills ...

TRENDING NOW