Monday, March 28, 2016

KWANINI ALLAH NA MUHAMMAD (S.A.W) WALIRUHUSU KUUWAWA KWA WAKONGWE NA AJUZA?


Ndugu msomaji,
Leo tutaangalia tabia mbaya ya Allah na Mtume wake Muhammad. Hivi kwanini Allah aliruhusu kuuwawa kwa Vikongwe? Hivi kwanini Muhammad alifanya hiyo kazi ya Allah na kuwauwa Vikongwe na ajuza?
Mohammad na kikosi chake kiliuwa wazee wa makamo; Umm Qirfa Fatima, Abu Afak na mzee aliyekataa kusujudia Al-Kaaba.
Baada ya kuuteka mji wa Kaaba Mohammad alimtuma mfuasi wake, Zayd Ibn Haritha kuenda kuuteka kabila ambalo liliukana Uislamu. Zayd bin Haritha alifanikiwa kuuteka huo mji pamoja na kuuwa wazee wakongwe na kuwateka wanawake na watoto walitojaribu kutoroka.
“…na tuliwashambulia kutoka pande zote hadi tukafika karibu na visima vyao ambapo tulipigana vita vikali. Tuliwauwa Aadui zetu wengine huku wengine wakichukuliwa kama mateka wa vita. Niliona kwa mbali kundi la watu lililojumuisha wanawake na watoto wakitoroka. Niliogopa, wasije wakafike mlimani kabla yangu, hivyo nikalenga mshale kati yao na ukaangukia kwa mbele kati yao na mlima. Nikawarudisha nikiwakimbiza kama mifugo walikotoka. (Sahin Muslim 4345)
Umm Qirfa ni miongoni mwa wanawake walitekwa vitani
Alikuwa ajuza (bi kizee), mke wa Malik. Binti yake (na wenzake) walitekwa pia. Zayd Ibn Haritha akaamuru Qays kuuwa Umm Qirfa na akamuuwa kinyama kwa kumfunga kwa kamba kila mguu kwa ngamia mbili na kuwaamuru hao ngamia kuenda pande tofauti. Umm Qirfa alichanika katikati, akatokwa na damu akapasuka mishipa, mifupa na kufa ghafla! (Ibn Ishaq/Hisham 980)
Binti yake ajuza, Umm Qirfa Fatima, aliletwa Makka pamoja na mateka wengine ambapo alipewa kama jizya (zawadi). (Hii ilikuwa kabla ya Mohammad kumtambua)
Niliwatembeza hadi nikawaleta kwa Abu Bakr ambaye alinitunukiza huyu binti kama zawadi. Hivyo tukafika Medina. Sikuwa nimemvua buibui wakati mtume wa Allah (s.a.w) alipokutana nami njiani na kusema; “nipe huyu binti awe mke wangu.” (Sahih Muslim 4345)
Mohammad aliamuru kuuliwa kwa mkongwe aitwaye Abu Afak. Hii ilitendeka miaka miwili baada ya Mohammad kuingia Medina. Abu Afak akikuwa na umri wa miaka 120. ‘kosa’ lake likiwa kuandika mashairi ya kukashifu vitendo vya mtume wa Uislamu-Mohammad vya kuchinja na kuteka wanawake vitani.
Mohammad akasema, “Ni nani ataniadhibia huyu mtwana?” Hivyo mfuasi wake Mohammad akainuka na kumuua Abu Afak. (Ibn Ishaq/Hisham 995).

Alipokuwa anamuua Abu Afak, inasemekana muuaji alimkejeli na kuingiza kisu tumboni mwake na kusema, “chukua hicho Abu Afak, licha ya umri wako.” (Ibn Ishaq/Hisham 995)
Baadaye, Mohammad aliuwa mwanamke aliyekuwa na watoto watano kwa kupinga mauaji ya Abu Afak. Mtume bandia wa Allah aliuwa kila ambaye alipinga mambo yake, badala ya kukumbana na wapinzani wake kwa mjadala wa maantiki.
Vilevile, mkongwe mwingine aliuliwa kutokana na amri ya Mohammad ya kuuwa mtu yeyote kule Mekka ambaye sio mwislamu kufuatia utekaji wa mji huo mwaka 630. (Sehemu ya kuran ya sura ya 9 inaamuru kuchinja). Kifo cha huyu mtu kimenukuliwa kwenye kitabu cha Bukhari:
Mtume alisoma Suratan-Najm (103) akiwa Makka huku akiwa amelala chali na waliokuwa pamoja naye walifanya vivo hivyo isipokuwa mkongwe mmoja aliyechukua funda la mchanga na kuiweka kichwani kisha kusema; “hii yanitosha.” Baadaye, nikaona anauliwa kama kafir. (Bukhari 19:173)
**ni kawaida ya waislamu kulalamika kuwa dini yao inakashifiwa na allah wao kutukanwa. Nataka kuwataarifu kuwa hizo aya sio zangu bali zimenukuliwa kutoka kwa vitabu vya Kiislamu. Mimi ni mjumbe tu.**
Ndugu msomaji, leo umejifunza kwa kutumia vitabu vayo kuwa Allah alimruhusu Muhamamd kuuwa vikongwe na ajuza. Hakika hakuna dhmabi mbaya kama ya kuuwa vikongwe na ajuza pamoja na watoto kama alivyo fanya Muhammad nabii wa Allah.
Biblia inasema kuwa
Katika Mathayo 5:21-28 Yesu anasawazisha kutenda uzinzi na kuwa na tamaa katika moyo wako, kuua na kuwa na chuki kwa moyo wako. Ingawa, hii haimanishi kuwa dhambi zote ni sawa. Chenye Yesu alijaribu kuleta karibu na Mafarisayo ni kwamba dhambi bado ni dhambi hata kama ulinuia kufanya tendo bila, hata bila kulitenda. Viongozi wa dini wa wakati wa Yesu walifunza kuwa ilikuwa sawa kufikiria juu ya kitu cho chote ulitaka, bora tu usifanye tendo juu ya hizo thamanio. Yesu anawalazimisha kugundua kwamba Mungu anahukumu mawazo ya mtu vilevile na matendo. Yesu alitangaza kuwa matendo yetu ni matokeo ya yale yaliyo katika mioyo yetu (Mathayo 12:34).
Kwa hivyo ingawa Yesu alisema kwamba tamaa na uzinzi zote ni dhambi, hiyo haimanishi kuwa ziko sawa. Itakuwa mbaya sana ukiua mtu kuliko kuchukia mtu, hata kama zote ni dhambi mbele za Mungu. Kuna viwango vya kusini. Dhambi zingine ni mbaya zaidi ya zingine. Kwa wakati huo huo kuambatana na madhara yote ya milele na wokovu, dhambi zote ni sawa. Kila dhambi itaelekeza kwenye hukumu ya milele (Warumi 6:23). Dhambi zote, haijalishi jinsi ilivyo “ndogo” ni kinyume na Mungu asiye na mwisho na wa milele na kwa hivyo anastahili hukumu isiyo na mwisho na ya milele. Zaidi, hakuna dhambi “kubwa” sana ambayo Mungu hawezi samehe. Yesu alikufa ili alipe hukumu ya dhambi (1 Yohana 2:2). Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu zote (2 Wakorintho 5:21). Je! Dhambi zote ni sawa? Naam na La. Kwa ukali? La. Kwa adhabu? Naam. Kwa msamaha? Naam.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 28, 2016

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW