Tuesday, March 8, 2016

MALAIKA WALIO FANYA DHAMBI

1. Je, Shetani aliumbwa kma Shetani au alikuwa na jina lingine?
2. Je, Majini yaliumbwa kama Majini au yalikuwa na majina mengine?
Ndugu msomaji,
Katika somo hili, tutajifunze kuhusu Malaika walio tenda dhambi, na matokea yao baada ya kufanya hivyo.
Biblia inafundisha kwamba Mungu ni Roho na kwamba viumbe wake wa kwanza walikuwa roho. (Yohana 4:24; Waebrania 1:13, 14) Isitoshe, Biblia pia inataja kwamba kuna roho waovu. (1 Wakorintho 10:20, 21; Yakobo 2:19) Lakini haifundishi kwamba Mungu ndiye aliyewaumba roho waovu. Basi wao ni nani, na walitokea jinsi gani?
Katika Biblia tunasoma kuwa, kuna Malaika walitenda dhambi na kufukuzwa Mbiguni. Mungu mwenye upendo, alipowaumba viumbe wa roho, viumbe hawa, aliwaumba wakiwa na uhuru wa kuchagua ikiwa watatende mema au mabaya.
Roho wa kwanza kuasi na mwenye sifa mbaya zaidi alikuwa Lucifer ambaye anajulikana sasa kwa jina la Shetani.
Ni nini kilichomchochea Shetani kumwasi Mungu?
Shetani alianza kutamani ibada ambayo ilikuwa hasa ya Muumba-Mungu, kisha akajikweza kutokana na tamaa hiyo na kujifanya kuwa mungu. Isaya 14: 11 Fahari yako yote imeshushwa mpaka kuzimu, pamoja na kelele ya vinubi vyako, mafunza yametanda chini yako na minyoo imekufunika. 12 Tazama jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya asubuhi, mwana wa mapambazuko! Umetupwa chini duniani, wewe uliyepata kuangusha mataifa! 1 3 Ulisema moyoni mwako, “Nitapanda juu hadi mbinguni, nitakiinua kiti changu cha enzi juu ya nyota za Mungu, ataketi nimetawazwa juu ya mlima wa kusanyiko, kwenye vimo vya juu sana vya mlima Mtakatifu.
Biblia inamfafanua Shetani kuwa kiumbe halisi ambaye yuko katika makao ya roho. (Ayubu 1:6) Inatueleza kuhusu sifa zake za ukatili kutia ndani matendo yake ya uovu. (Ayubu 1:13-19; 2:7, 8; 2 Timotheo 2:26) Pia inasimulia mazungumzo kati ya Shetani na Mungu na pia kati yake na Yesu.— Ayubu 1:7-12; Mathayo 4:1-11.
Kiumbe huyo mwovu alitoka wapi? Mungu aliumba viumbe “roho” wanaoitwa malaika. (Ayubu 38:4-7) Wote walikuwa wakamilifu na waadilifu. Hata hivyo, mmoja kati ya malaika hao akaja kuwa Shetani.
Malaika huyo hakuitwa Shetani alipoumbwa kama nilivyo sema hapo mwanzo na/au hakuumbwa akiwa Shetani, kama imani zingine zinavyo sema, bali alikuwa Malaika muadilifu mbele za Mungu. Jina hilo Shetani ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu.
Kiumbe huyo wa roho akaanza kukuza hisia za kiburi na za kushindana na Mungu. Alitaka wengine wamwabudu yeye. Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu alipokuwa hapa duniani, Shetani alimtaka Yesu ‘amfanyie tendo la ibada.’— Mathayo 4:9.
Katika Bustani ya Edeni, Shetani amdanganya Hawa:
Shetani “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alidai kwamba Mungu alikuwa mwongo, ilhali kwa kweli, yeye ndiye alikuwa mwongo. Alimwambia Hawa kwamba angekuwa kama Mungu, lakini ni yeye hasa aliyetaka kuwa kama Mungu. Na kupitia mbinu zake za ujanja, alitosheleza tamaa yake yenye ubinafsi. Alimfanya Hawa amwone kuwa mkuu kuliko Mungu. Kwa kumtii Shetani, Hawa alimkubali kuwa mungu wake.—Mwanzo 3:1-7.
Kwa kuchochea uasi, malaika huyo ambaye awali alikuwa mwenye kuaminika akawa Shetani, yaani, mpinzani na adui ya Mungu na wanadamu. Neno “Ibilisi,” linalomaanisha “Mchongezi,” likawa pia jina la malaika huyo mwovu. Malaika huyo ambaye aliongoza katika kutenda dhambi mwishowe aliwachochea malaika wengine wakose kumtii Mungu na wamwasi kama yeye. (Mwanzo 6:1, 2; 1 Petro 3:19, 20) Kwa kufanya hivyo malaika hao waliwaongezea wanadamu shida. Kwa sababu ya kuiga njia za Shetani zenye ubinafsi, “dunia ikajaa jeuri. Na uovu”—Mwanzo 6:11; Mathayo 12:24.
Ingawa ni wazi kwamba roho waovu wamezuiwa wasijigeuze kuwa wanadamu, bado wana nguvu na uvutano mwingi juu ya akili na maisha ya watu. Kwa kweli, Shetani, na roho wake waovu, ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (Ufunuo 12:9; 16:14) Kwa njia gani? Hasa kupitia “mafundisho ya roho waovu.” (1 Timotheo 4:1) Mafundisho hayo ya uwongo, ambayo mengi ni ya kidini, yamepofusha akili za mamilioni ya watu wasitambue ukweli kumhusu Mungu. (2 Wakorintho 4:4) Fikiria mifano kadhaa.
Unaweza kujilinda jinsi gani dhidi ya roho waovu?
Biblia inajibu hivi: “Jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.” (Yakobo 4:7) Tunatii agizo hilo tunapoishi kupatana na mafundisho yaliyo katika Biblia, kitabu pekee kitakatifu ambacho kinamfichua Shetani, roho waovu, na “hila” zao. (Waefeso 6:11; 2 Wakorintho 2:11) Pia, Biblia inatuambia kwamba roho waovu pamoja na wote wanaompinga Mungu, hawatakuwapo milele. (Waroma 16:20) “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake,” inasema Methali 2:21.
Jinsi shetani anavyotenda kazi:

Mark. 4:15 Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja shetani, akaliondoa lile neno lililopadwa mioyoni mwao.
Iwapo shetani alimjaribu na kumshawishi na kujaribu kumdanganya Yesu Kristo pale mlimani (Mk. 1:13). Je hatuwezi kufikiria ya kwamba atafanya hayo hayo ya udanganyifu na kutujaribu sisi pia?. Je hafanyi hayo hayo kwetu sisi kwa wakati huu?. Shetani anataka tuwaze na kufiri kunyume na mapenzi ya Mungu, na haya yakitokea hatutakuwa karibu na Mungu. Kufikiri kunyume na mapenzi ya Mungu ni kujitenga na Mungu. Shetani anatumia hila nyingi sana kutufanya tuwe na mawazo tofauti na Mungu. Shetani anaharibu mawasiliano ya mwanadamu na Mungu. Mchonganishaji wa mwanadamu na Mungu. yeye alikuwa muaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa uongo.
2 Wathesalonike 2:9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo.
Anatufanya tuamini pepo, uchawi, mageuzi yenye kuendelea kutokea, kwa utaratibu wa wanadamu (evolution) na miujiza, mambo ambayo hayatokani wala hayatoki kwa Mungu, anatulazimisha kuamini chochote kile ili kutuchanganya akili zetu.
2 Wakoritho 11:14 Wala si ajabu. Maana shetani mwenyewe hijigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki,ambao mwisho wake utakuwa sawa sawa na kazi zao.
Shetani ana udanganyifu wa hali ya juu sana, akifanya mazuri kuwa mabaya. Kuna makanisa mengi yanayohubiri imani ambazo wanaziona kuwa ni nzuri, lakini swali la kujiuliza, je hayo ndiyo mapenzi ya Mungu? Mungu anasema ya kwamba “Na uzima wa milele ndiyo huu, wakujue wewe Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Na kuonyesha ya kwamba tunampenda ni lazima tushike na kutunza amri zake. Kanisa linaloshika na kutenda amri za Mungu ndilo kanisa linalopaswa kufuatwa. Wengine wanashika na kutunza amri sita za mwisho na wakati huo huo wanafundisha mpende jirani yako, lakini amri za kwanza nne zinazotueleza tumpende Bwana Mungu wetu na ndizo zinazoshuhudia upendo wa Mungu ambazo hawaziangalii. Shetani amechanganya ulimwengu kwa udanganyifu wa hali ya juu sana, kiasi kwamba ni vigumu kupata wenye imani wanaoamini juu ya mambo haya.
Usijione kama umepotea au kuogopa kama vile majeshi, au jeshi la malaika ambalo ni waaminifu na ni wakiroho wanapotulinda tunapowahitaji. Malaika ni wajumbe wa Mungu, kwa hiyo ni kwa ye yote anayetuletea ujumbe kutoka kwa Mungu, kama vile mtu maalumu wa posta anayetuletea barua kutoka kwa Mungu. Kirsto alikuwa ni Malaika Maalumu, Mwana Maalumu wa Mungu aliyeleta ujumbe maalumu sana. Heshima aliyopewa ni kuu kuliko heshima aliyopewa malaika yeyote kwa sababu kuna tofauti na shetani, Kristo aliamini hukumu ya Mungu. Kwa sababu hiyo ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba na jeshi lote la mbinguni wanamtii na kumpa heshima.
Ufunuo 5:12 kwa sababu hii sasa ameketi katika mkono wa kuume wa Mungu akiwamilki malaika pamoja na sisi sote ni milki yake sote kwa pamoja tunampa heshima na utukufu na baraka.
Tunapofikiria juu ya shetani, Je tunakuwa tunafikiria juu ya kitu gani au shetani ni nini? Au ni nani? Je alikuja kutokea wapi? Madhumuni na makusudi yake ni nini? Je, Anatuathiri kwa namna gani? Na ni kwa nini shetani yupo? Je Ana mahusiano gani na Mungu?
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2013. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW