Wednesday, August 16, 2017

MUISLAM ABADILI DINI NA KUWA MKRISTO BAADA YA KUSOMA AYA HII YA BIBLIA


WAISLAM WANAULIZA, WAPI YESU KASEMA "MIMI NI MUNGU"?
Kuna aya nyingi sana Yesu kasema yeye ni Mungu. Tatizo ni kuelewa unacho kisoma.
Hebu rejea hapa:
Ufunuo 1: 17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.
Nilipo itoa aya hii kwa Muislam kama uthibitisho, MUISLAM akaniuliza nani msemaji wa hiyo aya, Nikamjibu kwa maksudi ni- Mungu.
Muislam, akacheka kwa kebehi sasa wapi kwenye hiyo aya Yesu anasema yeye ni Mungu?
Kwanza tukubaliane yafuatayo:
1. Waislam wanakiri kuwa Mungu ni Mwanzo na Mwisho "Alpha na Omega"
2. Kwenye hiyo aya inatuambia kuwa Mungu ni Alpha na Omega, au sio?
3. Tukubali kuwa msemaji wa hiyo aya ni Mungu.
SASA:
Turudi tena kwenye aya ya 18: MSEMAJI ANASEMA KUWA, "NAMI NALIKUWA NIMEKUFA" Je, Mungu tokea lini anakufa?
Muislam akabakia kimya na kuanza kujitafakari, baada ya Muda akasema kuwa Kama Alpha na Omega alikufa, basi huyo lazima awe ni Yesu.
Nikamwambia haswaa,
Bwana Abdullah akaendelea kusema, INAMAANA KUWA MUNGU ALIKUFA, maana kwenye aya ya 18 inasema "NIMI NALIKUWA NIMEKUFA". Nikamjibu tena, haswaa.
Baadae, ndugu yetu Abdullah akasema basi Yesu ni Mungu. Nikamuuliza, unakubali kuwa Mungu alijidhihirisha katika mwili? Ndugu yetu alikubali na nikamuongoza swala ya toba, papo hapo.
Leo hii, Abdullah si Muislam tena bali ni MFUASI YESU, MUNGU MKUU,
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW