Tuesday, August 22, 2017

UNAYAJUA MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA UTUPU "PONOGRAFIA"? (SEHEMU YA TATU)


UASHERATI NI NINI?
“Uasherati” ni nini, na ni kwa njia gani wale walio na mazoea ya kufanya uasherati huvuna kile wanachopanda?
Katika Biblia, neno “uasherati” (Kigiriki, por·neiʹa) linahusu mahusiano haramu ya ngono nje ya ndoa ya Kimaandiko. Linatia ndani uzinzi, ukahaba, ngono kati ya watu ambao hawajaoana, ngono ya kinywa, ufiraji au ulawiti, na kusisimua kingono viungo vya uzazi vya mtu mwingine ambaye si mwenzi wako wa ndoa. Pia linatia ndani mazoea kama hayo kati ya watu wa jinsia moja au kati ya mtu na mnyama. *
Maandiko yanataja waziwazi: Walio na mazoea ya kufanya uasherati hawawezi kuendelea kuwa katika kutaniko la Kikristo na hawatapata uzima wa milele. (1 Wakorintho 6:9; Ufunuo 22:15) Pia, wanajiletea wenyewe madhara makubwa hata sasa. Wanakuwa watu wasiotumainika, wanajidharau, wanakuwa na mizozo katika ndoa zao, wanakuwa na dhamiri chafu, wanapata mimba zisizotakikana, magonjwa, na hata kifo. (Wagalatia 6:7, 8) Kwa nini uanze kutembea katika barabara hiyo yenye hatari nyingi? Inasikitisha kwamba wengi hawafikirii madhara yanayoweza kutokea kabla ya kuchukua hatua ya kwanza isiyofaa, ambayo mara nyingi hutia ndani ponografia.
MADHARA YA PONOGRAFIA—HATUA YA KWANZA
Je, ni kweli kwamba ponografia haina madhara yoyote kama wengine wanavyodai?
Katika nchi nyingi, ponografia hupatikana katika magazeti, muziki, televisheni, na imejaa katika Intaneti. Je, ni kweli kwamba haina madhara yoyote kama wengine wanavyodai?
Sivyo hata kidogo! Mara nyingi wale wanaotazama ponografia husitawisha mazoea ya kupiga punyeto na kukuza “hamu za ngono yenye kufedhehesha,” mambo ambayo yanaweza kusababisha pupa ya ngono, tamaa potovu, matatizo mazito katika ndoa, na hata talaka. (Waroma 1:24-27; Waefeso 4:19) Mchunguzi fulani analinganisha pupa ya ngono na ugonjwa wa kansa. Anasema: “Hukua na kuenea daima. Uwezekano wa kupungua ni mdogo sana nayo haitibiki wala kupona kwa urahisi.”
Fikiria maneno haya yaliyo katika andiko la Yakobo 1:14, 15: “Kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi; nayo dhambi, wakati imetimizwa, huleta kifo.” Kwa hiyo tamaa mbaya ikiingia akilini mwako, iondolee mbali mara moja! Kwa mfano, ukiona bila kukusudia picha zenye kuamsha hamu ya ngono, angalia kando haraka, au uzime kompyuta, au ubadili stesheni ya televisheni. Fanya yote unayoweza ili kuepuka kulemewa na tamaa zilizopotoka kabla hazijaenea sana na kupita mipaka!—Mathayo 5:29, 30.
USIKOSE SEHEMU YA NNE
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW