Wednesday, August 16, 2017

KULIA NA KUSAGA MENO MILELE YOTE

Image may contain: text
Je, jina lako lipo ndani ya kitabu cha uzima?
Siku za mwisho zimekaribia, wenye dhambi tubuni, na watakatifu jiandaeni kunyakuliwa na Bwana, maana atakuja muda wowote sasa, tutanyakuliwa na tutaenda mbinguni, wenye dhambi wote, watatupwa kwenye ziwa la moto.
Luka 13:28 Ndipo kutakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo na manabii wote wapo katika ufalme wa Mungu, lakini nyinyi wenyewe mmetupwa nje!
(Luka 8:31, Ufunuo wa Yohana 9:1), na ziwa la moto, liwakalo na kiberiti ambapo watakao kuwemo watateswa usiku na mchana milele na milele (Ufunuo 20:10).
Huko kutakuwa na kulia na kusaga meno, ikiashiria machungu makali na hasira (Mathayo 13:42). Hapa ni mahali ambapo mdudu hatakufa wala makaa kuzimika (Marko 9:48). Mungu hafurahishwi na kufa kwa mtu muovu, lakini hutaka wazighairi njia zao mbaya ili waishi (Ezekiel 33:11). Lakini hatatulazimisha kumkubali; tukiamua kumkataa yeye. Hana budi kutupatia tulilolichagua – kuishi mbali naye.
Mpendwa, ni hatari kama nini ukikosekana kwenye Ufalme wa Mungu, hakuta kuwa na nafasi nyingine ya kutubu. Ndio maana tupo hapa kila siku kukumbushana kuwa, tuwe tayari na tuendelee kumfuata Yesu aliye kufa kwa ajili ya dhambi zetu.
HAKIKISHA JINA LAKO LIMEANDIKWA KWENYE KITABU CHA UZIMA.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW