Tuesday, August 22, 2017

JE, MUNGU ANATAKA NINI KUTOKA KWAKO? SEHEMU YA PILI

Image may contain: 2 people, child and outdoor
DUMISHA VIWANGO VYA JUU VYA MAADILI
Umejionea mambo gani kuhusiana na maadili ya ulimwengu leo?
Maadili ya Kikristo muhtasari wake umetolewa na Wakolosai 3:1-6 : "Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkon wa kuum wa Mungu.
Roho Mtakatifu hukaa ndani ya kila muumini, na sehemu ya majukumu yake ni kufundisha jinsi ya kuishi: "Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia,"(Yohana 14:26). "Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yankaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama matufa yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake"(1 Yohana 2:27). Hivyo, wakati tunaomba kwa maandiko, Roho atatuongoza na kutufundisha. Atawaonyesha sisi kanuni tunahitaji ili kusimama katika hali yoyote.
Mungu anatuagiza tuwe safi kiadili licha ya uovu ulio katika ulimwengu kwa sababu anataka tuwe na hali nzuri ya kiroho na kimwili. (Malaki 2:15) Ulimwengu umejaa habari nyingi sana za ngono. Watu wengi wana maoni ya kwamba kutazama picha na sinema za ngono, kusoma vichapo vyenye mambo machafu ya ngono, na kusikiliza muziki unaoamsha ashiki ni mambo ya kawaida ya maisha. Isitoshe, kuna watu wasiowaheshimu wanawake, wanawaona kuwa vyombo vya ngono tu. Au huenda vijana shuleni wakafanya mizaha michafu na kusema mambo machafu kuhusu ngono. Utashindaje mikazo hiyo yenye kuchafua?
Wengi walikosaje kudumisha viwango vya Mungu wakati wa wale manabii 12?
Wale manabii 12 tunaozungumzia wanatoa mashauri mazuri sana. Waliishi kabla ya kubuniwa kwa majumba ya sinema na maduka ya video. Hata hivyo, wakati huo kulikuwa na ishara za viungo vya uzazi, kulikuwa na ule ulioitwa ukahaba mtakatifu, na matendo mapotovu sana ya ngono. (1 Wafalme 14:24; Isaya 57:3, 4; Habakuki 2:15) Mambo ambayo manabii waliandika yanathibitisha hivyo: “Kwa habari ya wanaume, hujiendea zao wenyewe pamoja na makahaba, nao hutoa dhabihu pamoja na wanawake makahaba wa hekaluni.” “Mwanamume na baba yake wamemwendea msichana yuleyule, kwa kusudi la kulitia unajisi jina langu takatifu.” Baadhi yao walitoa kwa ukawaida “malipo ya kahaba” katika sherehe za uzazi.* Uzinzi ulienea kotekote, huku wake na waume wasio waaminifu ‘wakiwafuata wale wanaowapenda kwa tamaa nyingi.’—Hosea 2:13; 4:2, 13, 14; Amosi 2:7; Mika 1:7.
(a) Mwenendo mpotovu husababishwa na nini hasa?
(b) Watu wa kale wa Mungu walitumbukiaje katika uasherati wa kiroho?
Huenda unajua kwamba upotovu wa maadili unahusiana na mtazamo na nia ya mtu. (Marko 7:20-22) Kuhusu watu wake wenye maadili mapotovu, Mungu wetu alisema kwamba “roho ya uasherati [“tamaa ya ngono,” Contemporary English Version] imewafanya watange-tange” na kwamba “wameendeleza mwenendo mpotovu.” (Hosea 4:12; 6:9) Zakaria alitaja “roho ya uchafu.” (Zakaria 13:2) Watu walikuwa na mtazamo wa kutojali, walipuuza au hata kudharau viwango vya Mungu na mamlaka yake. Kwa hiyo, mtu yeyote mwenye mwelekeo huo anapaswa kubadili kabisa fikira zake na hali yake ya moyoni ili arekebishe nia yake. Wakristo wanapojua hivyo wanapaswa kuthamini hata zaidi jitihada zinazofanywa ili kuwasaidia waepuke ukosefu wa maadili na madhara yake.
USIKOSE SEHEMU YA TATU
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo, Mungu Mkuu na Mwokozi Wetu

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW