Friday, December 8, 2017

HUYU NI BINTI MDOGO SANA KAZALIWASHWA KWA KUFUATA SHERIA ZA ALLAH


SOMA:

1. Sahih al-Bukhari 810-870 BK, 256 BH

1a. "Alisimulia baba wa Hisham: Khadija alkufa miaka mitatu kabla ya Nabii kuondoka Madina. Alikaa huko miaka miwili au zaidi kisha akamuoa 'Aisha alipokuwa msichana mwenye umri wa miaka sita, na Muhammad aliikamilisha ndoa yao kwa tendo la unyumba wakati 'Aisha alipokuwa na umri wa miaka tisa." Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.236, uk.153.
1b. Habari hizo zipo pia kwenye Bukhari juzuu ya 5 kitabu cha 58 sura ya 43 na.234, uk.152.
1c. "Alisimulia 'Urwa: Nabii aliandika (mkataba wa ndoa) na 'Aisha wakati msichana alipokuwa na umri wa miaka sita na aliikamilisha ndoa yake nay eye kwa tendo la unyumba wakati akiwa na miaka tisa na 'Aisha aliendelea kuwa naye kwa miaka tisa (yaani mpaka kifo cha Nabii). Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 62 sura ya 60 na.88, uk.65.
1d. Alisimulia 'Aisha: Nabii alikuwa akinisitiri kwa Rida (vazi lenye kukinga sehemu ya juu ya mwili) yake nilipokuwa nawaangalia Waethiopia waliokuwa wanacheza kwenye ua wa nyuma wa msikiti. (Niliendelea kuangalia) hadi nilipotosheka. Hivyo unaweza kuelewa ni jinsi gani binti mdogo (ambaye hajafikia umri wa kuvunja ungo) ambaye ana hamu ya kufurahia burudani alivyofanyiwa mambo ya namna hii. Bukhari juzuu ya7 kitabu cha 62 sura ya 115 na.163, uk.119.
2. Ibn-i-Majah 824-886/887 BK, 273 BH

2a. A'isha aliolewa alipokuwa na miaka sita, na tisa alipokwenda kwenye nyumba ya Muhammad. Ibn-i-Majah juzuu ya 3 kitabu cha 9 sura ya 13 na.1876, uk.133.
2b. A'isha aliolewa akiwa na miaka saba, alikwenda kwenye nyumba ya Muhammad akiwa na miaka tisa, na alikuwa na miaka 18 wakati Muhammad alipokufa. Kwa mujibu wa al-Zawa'id, isnad zake ni sahihi kwa mujibu wa Bukhari. Hata hivyo Abu 'Ubaida hakusikia kwa baba yake, kwa hiyo ni munqata (ina pengo) Ibn-i-Majah juzuu ya 3 kitabu 9 sura ya 13 na.1877, uk.134.

3. Mwana Historia ibn Ishaq - aliyefariki mwaka 767/773 BK, 145/151 BH

3a. "Yahya b. Abbad b. Abdullah b. al-Zubayr kutoka kwa baba yake aliniambia kuwa alimsikia Aisha akisema: "Mtume alifia kifuani pangu wakati wa zamu yangu: Sijamkosea mtu yoyote yule kuhusiana naye. Ilikuwa ni kwa sababu ya kutokujua kwangu na udogo uliozidi kiasi hata Mtume akanifia mikononi mwangu."

(Guillaume, A., The Life of Muhammad, tafsiri ya Ibn Ishaq's Sirat Rasul Allah, Oxford University Press, Karachi, Pakistan, uk. 682). A'isha alisema kuwa alikuwa kijana sana wakati Muhammad anakufa.
Njooni kwa Yesu kwenye uzima wa milele.

Shalom,

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW