Sunday, December 31, 2017

WAISLAM NI WAPI YESU ALISUJUDU?

Image may contain: one or more people and indoor
Makafiri Waislam wamekuwa wakipotosha watu kila siku, kwamba YESU ni muislam kisa ALISUJUDU, hii ndio imekuwa hoja yao kubwa kwenye mitandao ya kijamii na katika mihadhara wanayofanya mitaani, na kweli kupitia njia hii, wamejipatia makundi ya waumini kwa hila, kuna watu wengi wameacha Ukristo na kusilimu, baada tu ya kuambiwa YESU ALISUJUDU, hivyo YESU ni muislam!
😨😨😨
Inasikitisha sana, "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa"
HOSEA 4:6
Hii yote inachangiwa na uzembe wa Wakristo wengi kutopenda kusoma Biblia wao wenyewe, na wengine hawana Biblia kabisaa! Sasa mtu wa hivyo akikujia muislam na hila zake, lazima akupate, maana huna ujanja, Biblia yenyewe hujui, unafikri utamshinda? Sio rahisi! 😎😎
Tuendelee na mada!
Sasa waislam wanasema YESU ni Muislam, kisa tu,ALISUJUDU!
(Yaani kwa Waislam, mtu akifanya jambo lolote ambalo nao wanalifanya, tayari mtu huyo ni Muislam, hata kama haujui msikiti wala Allah! 😂😂😂😂
Mfano YESU alipofuga ndevu na akavaa kanzu, pia wanasema alikuwa muislam!
Ina maana uislam ni Kanzu, uislam ni Ndevu, yeyote anaefanya hayo hata kama haendi msikitini nae ni muislam)
Na wanapokuja kukulaghai wanaanza,
"Oooh, unajua YESU ALISUJUDU, je akina nani wanasujudu?" Ukijichanganya tu ukajibu 👉"WAISLAM", Wanakwambia "umeona sasa, YESU alikuwa muislam, kwa sababu Waislam ndo wanasujudu, Wakristo hamsujudu!" 😵😵😵
Kisha, wanakuongeza na swali juu, YESU ALISUJUDU, nyie wakristo KUPIGA MAGOTI mmetoa wapi?
Teh teh! Hoja dhaifu kabisa hii
😂😂😂😂😂😂😂
Sasa Cha ajabu in kuwa ukiwaomba andiko linalosema YESU ALISUJUDU, (hawana), eti wanakimbilia Mathayo 26:39.
Imeandikwa, 
"Akaendelea mbele kidogo, AKAANGUKA KIFULIFULI akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe."

Hapo sasa ndo wanatumia kulaghai watu, eti YESU alikuwa muislam. 😂😂
Zingatia, hiyo aya haisemi YESU ALISUJUDU, ila inasema ."ALIANGUKA KIFULIFULI", Kuna tofauti ya KUSUJUDU na KUANGUKA KIFULIFULI {KIFUDIFUDI},
(kama picha hapo chini inavyoonekana).
Unaposujudu, kwanza unakunja magoti yanagusa chini, viganja vya mikono vinagusa chini, vidole vya miguu vinagusa chini, hali kadhalika Uso na pua vinagusa chini ambapo unasujudia. Ila tumbo, kifua havigusi chini, na Makalio yanainuka juu! (Kama unavyoona picha hapo chini ya muislam akisujudu)!
Lakini KUANGUKA KIFULIFULI, INA MAANA UNALALA CHINI KABISA, UNAKUWA FLAT, UNANYOOKA WIMA! Kuanzia uso, kifua, tumbo, mapaja mpaka miguuni, vyote vinagusa chini kabisa, kiufupi KUANGUKA KIFULIFULI Ni kulala chini, hapa makalio hayainuki juu kama wakati wa kusujudu!
(Tazama picha hapo chini Askofu alivyolala chini, amenyooka barabara, huko ndo kuanguka KIFULIFULI AU KIFUDIFUDI kama YESU alivyofanya).
Sijaona andiko linalosema YESU ALISUJUDU, kama lipo waislam leteni andiko lililopo linasema YESU alianguka KIFUDIFUDI, NA KUANGUKA KIFUDIFUDI SIO KUSUJUDU, au je ninyi Waislam mnaanguka KIFUDIFUDI kama YESU alivyofanya?
Hivyo YESU SIO MUISLAM, na YESU Hawezi kuwa muislam hata kama ANGESUJUDU, watu hawawi waislam kwa kusujudu, je mimi nikisujudu leo ntakuwa Muislam? Vitu vinavyosujudu ni vingi, je vyote hivyo ina maana ni Viislam? Hata Mbwa, Nguruwe, majini na viumbe wengine wanasujudu, je nao ni waislam?
Rejea Quran 16:49 inasema kila kitu
kinamsujudia Allah. 😂😂😂
"Na vyote viliomo katika mbingu na katika ardhi, tangu wanyama mpaka Malaika, vinamsujudia Mwenyezi Mungu, na wala havitakabari."
Ongezea na Quran 13:15 "Na viliomo mbinguni na katika ardhi vinamsujudia Mwenyezi Mungu tu vikitaka visitake. Na pia vivuli vyao asubuhi na jioni."
  👆👆
Ooh! Ina maana hata Mbwa, Nguruwe, kobe, kenge, Mijusi, n.k ni Waislam, kwa kuwa nao pia wanasujudu! Na kwa mujibu wa waislam kila anaesujudu ni Muislam
😂😂😀😀
Waislam tuko pamoja?
Yesu alipoanguka KIFUDIFUDI mkasema ni muislam, ila pia kuna majini, nayo
yalianguka KIFUDIFUDI, 😀😀😀
Rejea Marko 3:11 
"Na pepo wachafu, kila walipomwona (YESU) WALIANGUKA MBELE YAKE, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.", swali, pepo wachafu nao ni waislam?
Au huyu mwingine hapa, ambaye alimsujudia YESU, je nae ni muislam?
Marko 5:2-3,6
"2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;
3 makao yake yalikuwa pale makaburini...
6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, AKAMSUJUDIA."
Sasa ikiwa uislam ni KUSUJUDU, basi vitu vyote hapo juu, ambavyo tumeona vikisujudu NI VIISLAM! 😀😀😀
Ndio maana nikasema, YESU SIO MUISLAM, YESU HAKUSUJUDU, NA HATA KAMA ANGESUJUDU, HIYO HAIMFANYI AWE MUISLAM, MAANA WATU HAWAWI WAISLAM KWA KUSUJUDU!
Na lile swali, eti Wakristo KUPIGA MAGOTI MMETOA WAPI, WAKATI YESU ALISUJUDU?
Swali hili halina mashiko kabisa, KWANZA YESU HAKUSUJUDU!
Pili, Hakuna aya ambapo MUNGU amewabana watu kumwabudu kwa aina fulani moja tu (ya kusujudu n.k)
Ni wewe tu utakavyopenda, ama upige magoti, usimame, uanguke KIFUDIFUDI, au USUJUDU kama waislam, yote sawa tu! Wakristo tunafanya yote hayo, ila waislam wameshupalia moja tu, la KUSUJUDU! Kwao kupiga magoti ni kama dhambi!
Wakati hata wafalme, manabii na mitume WALIPIGA MAGOTI KUOMBA,
Mfalme Sulemani aliomba amepiga magoti, soma 1Wafalme 8:54
"Hata ikawa, Sulemani alipokwisha kumwomba Bwana maombi hayo, na dua hiyo yote, akasimama na kuondoka hapo mbele ya madhabahu ya Bwana, hapo alipokuwa AMEPIGA MAGOTI, na kuikunjua mikono yake kuelekea mbinguni."
Mfalme Daudi anasema,
"Njoni, tuabudu, tusujudu, TUPIGE MAGOTI mbele za Bwana aliyetuumba."
Zaburi 95:6 Hapo una ruhusa ya kuchagua kimoja, kusujudu au kupiga magoti!
Nabii Danieli alipiga magoti,
"Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) AKAPIGA MAGOTI mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo." Danieli 6:10
Stefano pia alipiga magoti,
"Wakampiga kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu.
AKAPIGA MAGOTI, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona vema kwa kuuawa kwake."
Matendo 7:59-60
Mwisho kabisa, hata YESU, Kiongozi wetu naye ALIOMBA AMEPIGA MAGOTI,
akatuachia mfano bora. 👇👇
"Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe AKAPIGA MAGOTI akaomba" LUKA 22:41 👏👏 (Andiko hili LA YESU KUPIGA MAGOTI ,Waislam huwa wanajidai HAWALIONI), Na sisi basi tuseme YESU NI MKRISTO, kwa kuwa alipiga magoti! Haleluya! 😂😂😂
Wale mnaouliza Wakristo kupiga magoti tumetoa, wapi? Jibu ni kuwa, tunamfuata YESU, manabii na mitume wake. 
Kwanza MUNGU hana shida na Aina au namna ya kuabudu, ILA TU IWE YA HESHIMA, NIDHAMU, KICHO NA ADABU! Usikae ovyo ovyo kama uko baa! MUNGU si mtani wako.
Waislam wasikudanganye, YESU SIO MUISLAM NA HAITATOKEA YESU KUWA MUISLAM! Mwenye swali unakaribishwa!
MUNGU awabariki nyote! Ni mimi Zacharia Maseke, mtumwa wa Kristo YESU!
Zechariah Maseke

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW