Thursday, March 11, 2021

JE, MAJINI, MASHETANI, MAPEPO NA YOTE YAMEUMBWA NA ALLAH?


1. Kwanini Allah alimuumba Shetani?

2. Kwanini Allah aliumba Majini machafu?

3. Kwanini Allah aliumba Mapepo?

4. Kwanini Allah aliumba Mahayawani?


MAJIBU YA MASWALI HAYO MANNE HAPO JUU UTAYAPATA KWENYE KAZI ZA MAJINI.


MTUME MUHAMMAD AKUTANA NA MAJINI USKU


Allah S.W.T. ametuhakikishia wazi kuwa ujumbe aliopewa Mtume S.A.W. ulikuwa kwa Wanadamu na Majini na Mashetani pia. Na katika Qurani na Hadithi za Mtume S.A.W. kuna dalili zilizo wazi zinazoyakinisha kuwa Mtume S.A.W. alikuwa akikutana nao na kuwafundisha dini. Na hata wakati mwingine Majini walikuwa wakitoa majibu mazuri zaidi kuliko Binadamu kwenye masuala ya dini. Na mfano ni wakati waliposomewa Suratir Rahmaan. Hadithi iliyopokelewa na Jaabir bin Abdallah R.A.A. na iliyotolewa na Ttirmidhi kasema, “Wakati ambapo Mtume S.A.W. alipowasomea Majini Suratir Rahmaan, “


ﻟَﻘَﺪْ ﻗَﺮَﺃْﺗُﻬَﺎ ‘‘ ﻳﻌﻨﻲ ﺳُﻮﺭَﺓَ ﺍﻟﺮَّﺣْﻤَﻦِ ’’ ﻋَﻠَﻰ ﺍﻟْﺠِﻦِّ … ، ﻓَﻜَﺎﻧُﻮﺍ ﺃَﺣْﺴَﻦَ ﻣَﺮْﺩُﻭﺩًﺍ ﻣِﻨْﻜُﻢْ ، ﻛُﻨْﺖُ ﻛُﻠَّﻤَﺎ ﺃَﺗَﻴْﺖُ ﻋَﻠَﻰ ﻗَﻮْﻟِﻪِ ‏] ﻓَﺒِﺄَﻱِّ ﺁﻻﺀِ ﺭَﺑِّﻜُﻤَﺎ ﺗُﻜَﺬِّﺑَﺎﻥِ ‏[ ﻗَﺎﻟُﻮﺍ : ﻻ ﺑِﺸَﻲْﺀٍ ﻣِﻦْ ﻧِﻌَﻤِﻚَ ﺭَﺑَّﻨَﺎ ﻧُﻜَﺬِّﺏُ ، ﻓَﻠَﻚَ ﺍﻟﺤﻤﺪ

Maana yake, “Hakika nimewasomea Majini (yaani Suratir Rahmaan)…wamejibu vizuri zaidi kuliko nyinyi. Kila nilipofikia kauli Yake (Mwenyezi Mungu S.W.T.) “Fabiayyi A-alaai Rabikumaa Tukadhibaan.) Maana yake, “Basi ipi katika neema za Mola wenu ambayo mnayoikanusha kuwa si kweli?” (Basi Majini) walijibu “Laa bishaay Min Niamika Rabbana Nukadhibu, Falakal Hamdu.”

Maana yake, “Hakuna neema yoyote katika neema Zako Mola wetu tunayoikadhibisha, bali tunashukuru.” Na Mtume S.A.W. alipowasomea Wanadamu hawakujibu chochote, akawaambia, “Ndugu zenu wa Ki-Jini wamejibu jawabu nzuri waliposikia haya.” Na dalili nyingine kuwa Mtume S.AW. pia alikuwa ametumwa kwao ni kisa cha baadhi ya Majini ambao baada ya kuisikiliza Qurani waliiamini na wakarejea kwao na kuanza kuwaita wenzao kwenye dini ya Kiislamu.


KUTOKANA NA BIBLIA

Majini au Mapepo au Mashetani (Malaika walio asi) ni viumbe ambavyo havionekani kwa macho, ni viumbe kama Malaika isipokuwa Majini na Mapepo yalifukuzwa Mbinguni pamoja na Shetani baada ya kuasi, na yalitupwa duniani yakisubiri siku ya mwisho ya hukumu. Hivyo Majini, Mashetani, Mapepo ni tokeo la kuasi kwa malaika. Ni sawa na kusema JAMBAZI ni tokeo au sifa ya mtu mwizi wa kutumia nguvu.

Biblia haisemi kuwa Mungu aliumba MAJINI, MASHETANI AU MAPEPO, maana Mungu wa Biblia hakuumba dhambi au ubaya au chuki au Ushetani au aina yeyote ile ya dhambi.

Shetani na Majini, wanajua kabisa kuwa Jehanum ya moto ipo kwa ajili yao, ndiyo maana wanafanya kila mbinu wasiingie peke yao huko Jehanum, Shetani ni mwongo, laghai anawatumia sana wachawi, waganga wa kienyeji, wasoma nyota kupandikiza majini, kuiba nyota yako ya mafanikio, kuchukua watu misukule nk.


KUNA AINA NYINGI ZA MAJINI, BAADHI YAO NA KAZI ZAO NI HIZI HAPA:-


1) Murafari – hili ni jini linalozuia mafanikio ya kupata fedha, mafanikio ya elimu nk.

2) Latifu – hili jini linaloleta ufukara, mateso, hata ukipata pesa matumizi yake yanakuwa ni hovyo

3) Jahari – Jini anayetumiwa kuiba mali na kuzuia biashara kustawi

4) Hasinani – jini hili ni la fujo, ulevi wa pombe, bangi na dawa za kulevya

5) Jube – jini hili linasababisha utasa

6) Subiani – jini la ajali, linasababisha wanawake kutokupata siku zao, na kunyonya damu za akina mama siku zao za hedhi ambapo wanapata maumivu makali sana.

7) Sumil – jini hili huangamiza mimba changa

8) Waidadat – jini hili husababisha wanaume kuvaa hereni kusuka nywele na kutoga masikio.

9) Alibadiri – jini la kifo, likikupata kifo hutokea wakati wowote.

10) Anzura – Linawazuia vijana wa kike na kiume kuolewa/kuoa

11) Maimuna – linawakamata wanaume wenye ndoa zao hadi ndoa inavunjika

12) Makata – linasababisha vifo vya mfululizo kwenye familia

13) Faziur – jini la maandishi. Unaletewa barua ukiisoma tayari umelikwaa

14)Subha – jini hili linasababisha mtu kuwa na kiburi sana na kujiinua.

15) Maulan – jini linalofanya watu kuwa kichaa, au mtu ananuka wakati wowote

16) Al-maul – jini hili linamfanya mtu kuwa ombaomba

17) Zuhura au Zohari – Jini la fujo

18) Araba – Jini hili linafanya mtu apende sana ubani

19) Farkh – jini hili linatumwa hasa kwa wakristo kuangalia kama ana kinga (Wokovu)

20) Baradi – jini hili likikupata basi ndoa yako ni lazima itavunjika.

21) Shamsu – jini hili huvaa umbile la binadamu kwa sura yoyote.(sasa hivi mitaani majini haya yapo mengi sana)

22) Abuni – jini wa hasira

23) Kaimu – jini la kutambua nyota za watu

24) Tajuruni – jini la utajiri wa kichawi – ni lazima utoe kafara ya mwanao, mkeo au kufanya tendo la ndoa na mama yako mzazi

25) Al-taliki – jini hili linapoteza watu katika mazingira ya kutatanisha

26) Naluju – linasimamia lugha

27) Janatusi – linatumwa alfajiri kabla ya adhana kuleta usingizi kwa Wakristo wasifanye sala

28) Riyaron – jini hili linamfanya mtu afanye kila kazi peke yake

29) Zaitun – Jini hili linasababisha wasichana kuwa na maringo

30) Ruyati – jini linalosimamia ndoto mbaya

31) Al-rahabu – jini linalosababisha hitilafu ya umeme

32) Hadharaji – jini hili linafanya kazi ya kukata kichwa cha mtu ili wapate damu

33) Anazihaji – jini hili ndilo linachukua roho yako ukifa kwenye dhambi

34) Nghruk – linasababisha maafa

35)Munkara – jini la makaburini

36) Takadhuru – jini linaloleta mali za masharti.

37) Rabindi – jini la Waislamu pekee yao ili wafanye fujo.

38) Balishebe – jini la magonjwa yasiyopona

39) Sajiduri – jini linalokusaidia kupata pesa, kisha zinapotea kwa haraka

40) Rumiran – linasimamia uwongo

41) Lairlihabi – linasimamia hofu, kutojiamini na kukata tamaa

42) Rohani – jini la mateso na fujo

43) Betrah – jini hili linasimamia mapambo, kwa mwanamke huwa anajipamba isivyo kawaida, halikadhalika mwanaume

44)Hanshari – linatumiwa sana na waarabu kulinda maduka yao

45) Walihuni – linazunguka nyumba likilinda biashara

46) Kurasih – jini la kupoteza fahamu

47) Tarik – huondoa amani nyumbani, kazini. Linafanya watu wasielewane

48) Atha – mungu wa kiarabu wa kuabudu sanamu

49) Munakir – linapoteza watu kimiujiza

50) Malik – jini la kumiliki biashara

51) Ghatabu – jini la kulainisha macho wa wanawake. Wanakuwa wanarembua

52) Khatuh – jini la uchawi wa kuchukua kucha, nywele na nguo za ndani

53) Fanken – jini hili linasimamia mtu kuzunguza kiswahili cha pwani

54) Zamzam – jini la marashi na kusimamia mikataba ya imani. Mkristo anaposilimishwa basi hutupiwa jini hili kupofushwa akili yake.

55) Mukitala – linatumwa kuangalia kinga za watu

56) Laufili – jini la uvivu

57) Al-khah – linakula damu iliyoganda

58 Abasaa – jini la hasira wivu na jeuri

59) Aherumi – jini la homa za mara kwa mara

60) Muba – jini la maradhi ya kuambikiza

61) Kamariram – jini hili linatoa kinga kwa majambazi

62) Zubiran – jini la uongo na uzushi

63) Abadi – Jini la wizi, umalaya na ujambazi

64) Muzamili- jini la matambiko ya kiarabu

65) Ruhadi – jini la wizi, umalaya na umasikini

66 Usuran – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini

67)Tubuyali – jini hili linamfanya mtu kuiba vitu vya ndani ya nyumba. Haibi nje ya nyumba

68) Zirach – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini

69) Ashuran – jini la utasa na maradhi ya akina mama

Kinga ya majini haya ni nyepesi ni KUOKOKA na kusimama katika neno la Mungu. Kama unayo dalili yoyote iliyosababishwa na Majini hayo hapo juu na umeokoka, taja jina la hilo jini, ni lazima litaitika, kisha liwashie moto wa Roho Mtakatifu. Tumia Damu na Jina la Yesu kuyavunja vunja

Marko 16:17-18 inasema, "ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina Langu watatoa pepo...." Kila Mkristo anao uwezo wa kuwatoa pepo! Sio swala la kwamba "una nguvu" kiasi gani au jinsi gani upo "kiroho" ; cha muhimu ni kuwa Yesu Amekupa mamlaka Yake; unatembea katika jina Lake.


Kama hujaokoka usiyarushie mawe au moto yatakuumiza. Muone kiongozi yeyote wa Kanisa akuongoze sala ya toba, kisha anza kuwasha moto, hakika yatakimbia na kuacha biashara, kazi, ndoa, na watoto wako huru.


Leo basi, tumejifunza aina za Majini na jinsi ya kuyaharibu kwa Jina la Yesu alie hai.


Max Shimba Ministries

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW