Friday, January 21, 2022

MUHAMMAD ALITABIRI KUWA, ATAKAPO KUFA, MASWAHABA WAKE WATAUKANA UISLAM NA KURUDIA UKRISTO

 





MANENO YA MTUME (SAWW) YA KUWAAMBIA MASWAHABA.

Bukhari katika Juzuu ya 8 Mlango wa Kauli ya Mtume (saww) katika kitabu chake ameandika: Mtume (saww) Aliwaambia maswahaba wake: Mutafuata Mwenendo wa Watu Waliopita Kabla Yenu!

Imepokelewa kutoka kwa Ataa ibn Yassar kutoka kwa Abu Said Al Khudri naye kutoka kwa Mtume Muhammad (saww) Aliposema: Mutafuata Mwenendo wa Waliopita Kabla yenu hatua baada ya hatua na dhiraa baada ya dhiraa hata wakiingia kwenye shimo la Kenge na Nanyi mutawafuata!

Maswahaba wakauliza, Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, Hao waliopita ni nani hao, Mayahudi na Wakristo?

Mtume (saww) Akawajibu, Ni akina nani basi kama sio hao?
Rejea: Sahih Bukhari juz 8, uk 151.

Kauli hiyo ya Mtume (saww) Inaambatana na Aya ya Qur'aan 3:144 Isemayo Je Mtume Akiuliwa au Akifa basi mutarudi kinyume nyume kwa visigino vyenu?

Kauli ya Mwenyezi Mungu na ya Mtukufu Mtume zilianza kuthibitika mara tu Mtume (saww) Alipofariki, Haikuchukua hata dakika moja tu na chizi mmoja akatoka nje ya nyumba ya Mtume na kuutoa Upanga wake na kuwaambia Watu Waliokuwa wamekusanyika kumjulia hali Mtume (saww) ambaye Alikuwa Anaumwa na Yupo kwenye Kitanda cha Mauti: Nisisikie hata mtu mmoja akisema kuwa Muhammad Amekufa! Huyo Chizi alikuwa ni Umar Khattab!

Kwanini alizuia watu wasiseme kuwa Mtume (saww) Amefariki?
Kwa sababu nia ilishamuingia Arudi Kinyume nyume kwa Kisigino!
Kisha Umar akatuma mtu akamuite shoga wake Abubakar ambaye alikuwa kwa mkewe nje ya Madina.

Alipofika Abubakar akaingia ndani ya Nyumba ya Mtume (saww) Kisha akatoka nje na kuwaambia: Na Hakuwa Muhammad ni Mtume aliyepitiwa na Mitume kabla yake, sasa huyo Muhammad Ameshafariki.

Baada ya kueleza hayo Abubakar na swahibu wake Umar wakaenda mbio mbio kule Saqifa kugombea ukhalifa bila ya kuishughulikia Maiti ya Mtume (saww)!

Hiyo ilikuwa ni kurudi kinyumenyume kwa visigino kwa hao mabwana wawili.

Huko Saqifa baada ya mvutano baina ya Ansaar na Muhajirin, Abubakar akachaguliwa Ukhalifa baada ya watu kutishiwa maisha yao na wengine baada ya kuhongwa mapesa!

Hiyo ilikuwa ni kurudi kinyumenyume kwa visigino kwa hao mabwana wawili.

Baada ya hapo mambo machafu waliyoyafanya hao wawili wakishirikiana na watu wao waliowanunua ikawa ni sawa na yale Aliyoyasema Mtume (saww) kuwa: Mutafuata Mwenendo wa Waliopita Kabla yenu hatua baada ya hatua na dhiraa baada ya dhiraa hata wakiingia kwenye shimo la Kenge na Nanyi mutawafuata!

Leo tunashuhudia Watu wengi wanaojifanya kuwa ni Waislamu Safi Kabisa Wakiwafuata hao Abubakar na Umar ambao wameingia kwenye shimo la kenge na wao pia wanaingia!
Kila kukicha utasikia hii Bid'aa eti Mtume Hakufanya hivi na hakufanya vile.

Wengine wanasema eti kuwafuata hao mabwana na kuwatakia Radhi ni Faradhi na ni sawa kama ilivyo Sala, Funga!

Wengine wanafikia hata kuzusha machafu juu ya Mtume (saww), kwasababu eti Umar alisema Mtume Anaweweseka! 

No comments:

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW