Sunday, March 26, 2017
CANADA: At Peel School Board meeting, outraged parents tear up quran, demand end to Islamic prayer in public schools
Board calls on security to throw out parents and press.
Saturday, March 25, 2017
USIOGOPE KWA MAANA MIMI NI PAMOJA NAWE, ASEMA BWANA WA MAJESHI

Isaya 41:10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Kumbuka kuwa Mungu yu pamoja nawe na atakusaidia katika kila shida zako. Usikate tamaa na Mtegemee yeye.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
MAPEPO NI NINI? [SEHEMU YA TANO]

Somo: MAPEPO
Mada Ndogo: Njia 8 za kuyashinda mapepo.
Bwana Yesu asifiwe sana,
Ndugu mpendwa, katika sehemu Nne zilizotangulia, tumejifunza maana,asili/ chanzo cha mapepo na dalili kuu za mtu alievamiwa na mapepo. Natumai umebarikiwa sana. Haleluya! Ndugu mpendwa, napenda kukukaribisha katika mwendelezo wa mafundisho yetu juu ya mapepo,ambapo kwasasa tutaangalia kwa kina mbinu/njia za kumshinda pepo.
Ndugu yangu mpendwa, kanisa la leo, liko katika mapambano makubwa sana. Upinzani mkubwa unatoka kwa ibilisi alie shetani, mwenye sifa kuu ya uharibifu.
Hata hivyo, Mungu ameliweka kanisa kwa wakati huu wa mashambulizi kwaajili ya kuukomboa ulimwengu. Amelifanya kanisa kama asikari wa mwamvuli ambaye hushushwa katikati ya eneo ambalo bado liko mikononi mwa adui, ila ikikusudiwa kupambana na hata kushinda. Kwa mantiki hiyo, si hoja tena juu ya kushinda kwa kanisa, bali daima linashinda na litaendelea kushinda.
Katika mwendelezo wa somo letu, leo tutaziangalia njia/uwezo wa kuyashinda mapepo.
Kwanza; Yesu alitoa mamlaka kwa kanisa juu ya mapepo (Marko 16:17). Uweza huu wa ajabu, Mungu ameutoa kwa watu wote wanaomwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wao (Yohana 17:20-23). Ujue, watu wengine wanateseka kwa kuwa hawajui, yule aliye ndani yao. Biblia inasema, aliyeko ndani ya aliyeokoka ni mkubwa mno, maana yake ni kuwa, anayashinda mapepo. Usikubali kuteswa na mapepo, kemea kwa jina la Yesu, lililo jina kuu kupita majina Yote, nawe utakuwa huru.
Pili; Mapepo huamriwa kwa jina la Yesu tu (Marko 16:17). Jina maagano na ahadi ni jina la Yesu tu. Usitumie jina lingine lolote lililo nje ya jina la Yesu. Ni jina la Yesu pekee huweza kuponya,kuokoa na kuhuisha, hata mapepo yanajua hivyo.
Kutumia majina mengine ni sawa na kukosea anwani wakati wa kutuma barua, ni kweli barua itaenda ila usitegemee kupokea majibu uliyotarajia kwa kuwa barua haitaenda kwa mlengwa.
Tatu; Yafukuize kwa kutumia mamlaka uliyonayo kama ilivyoelezwa katika hoja ya kwanza. Usiyabembeleze. Tumia amri. Watu wengine hutumia majadiliano, huyafanyia sherehe, huyafukizia uvumba,udi na hata kuyachezea muziki wa asili. Ndugu yangu, waswahili wanasema” ukifanya urafiki na mkia wa fisi,utakufirisi” usikubali kukaa meza moja na mapepo, shetani habembelezwi, yatimue kwa mamlaka ya Jina la Yesu (Mathayo 12:28,Luka 11:20).
Kutumia majina mengine ni sawa na kukosea anwani wakati wa kutuma barua, ni kweli barua itaenda ila usitegemee kupokea majibu uliyotarajia kwa kuwa barua haitaenda kwa mlengwa.
Tatu; Yafukuize kwa kutumia mamlaka uliyonayo kama ilivyoelezwa katika hoja ya kwanza. Usiyabembeleze. Tumia amri. Watu wengine hutumia majadiliano, huyafanyia sherehe, huyafukizia uvumba,udi na hata kuyachezea muziki wa asili. Ndugu yangu, waswahili wanasema” ukifanya urafiki na mkia wa fisi,utakufirisi” usikubali kukaa meza moja na mapepo, shetani habembelezwi, yatimue kwa mamlaka ya Jina la Yesu (Mathayo 12:28,Luka 11:20).
Nne; Usiyaruhusu kujieleza. Mpiganaji mzuri, hamuulizi adui ametoka wapi, yeye hushambulia hata kikosi kizimahukimaliza, kwa kuwa ni jasili na anajiamani, hababaishwi. Usikubalia kuhojiana na pepo, pepo ni waongo, watakudanganya kwa kutoa habari za uongo ili kulibomoa kanisa (mwili wa kristo) ili kuwatenganisha. Wataibua uadui kati yenu. We yaaamuru yaondoke, hata Yesu mwenyewe aliyaamuru tu yakaondoka (Luka 4:41,Marko 1:34).
Tano; Kwa kufunga na kuomba (Marko 9:29). Ndugu yangu mpendwa, kila mara, adui hushinwa kwa sala na kusoma neno. Jaama mamlaka ya mbinguni ili kumshinda ibilisi. Mtu asiye na maombi ni sawa na bunduki isiyo na risasi, na mtu asiyeomba anafanana na mlinzi anaetegea kazi yake, hutoa mwanya kwa mwizi kuvamia na kupora. Usikubali kuwa mlango wa ulegevu, daima jitahidi kuwekeza neno kwa wingi ili ujipatie maarifa zaidi.
Sita; Kuwa na Imani thabiti (Mathayo 17:19-20). Maombi pasipo imani, ni sawa na dhihaka. Ni bora ya majaribio, kuliko kudhihaki. Daima, kuwa jasili na umwamini Mungu na neno lake, ndipo litatimia kwako. Mtu asiyeamini, maombi yake hupeperushwa na mawimbi,hivyo hata majibu ya maombi yake hupeperushwa tu,kwakuwa hayana nguvu yoyote ndani yake.
Sita; Kuwa na Imani thabiti (Mathayo 17:19-20). Maombi pasipo imani, ni sawa na dhihaka. Ni bora ya majaribio, kuliko kudhihaki. Daima, kuwa jasili na umwamini Mungu na neno lake, ndipo litatimia kwako. Mtu asiyeamini, maombi yake hupeperushwa na mawimbi,hivyo hata majibu ya maombi yake hupeperushwa tu,kwakuwa hayana nguvu yoyote ndani yake.
Saba; Kwa Kumwamini Mungu (Marko 6:5&6), ukimwamini utamtegemea kwa kila jambo(Marko 9:23&24). Ukiwa na imani kwake, utakuwa na ujasili. Mwamini Mungu,ili athibitishe ujasili wako.
Nane; Kwa Muujiza. Mungu, ni Mungu wa maajabu, hufanya mambo yaliyojuu ya fahamu za mwanadamu. Hufanya mambo ya kushangaza, kuweza kufanya miujiza mikubwa mno,amabayo hata uwezo wa wasomi,hufikia kikomo. (Matendo 19:11&12), tunaonao nguo za Paulo zikifanya maajabu, ni muujiza wa nguo kutoa pepo. Ni kwa kuwa kuna upako unaokuwa sambamba na wamchao Bwana. Tegemea Miujiza kama uko kwenye uwepo muda wote. Kumbuka, imani wakati mwingine haionekani (Matendo 16:16-19), hivyo miujiza huithibitisha imani.
Swali la kujiuliza ni je, kila mtu anaweza kumtoa pepo?Jibu ni Hapana, si kila atakaye tumia jina la Yesu anaweza kutoa pepo, tena anaweza hata kujikuta yuko kwenye wakati mgumu zaidi kwa kuwa jina la Yesu lina uwezo wa ajabu, hivyo mtu anapaswa kulitumia kama silaha huku akihakikisha amejilinda vizuri mahali alipo (Matendo 16:13-16), mtu asiyejulikana katika ufalme wa Mungu, anapoliita jina la Yesu, huwa kama mtoto anaemlilia mama asiye wake, hata akimuonea huruma vipi, hawezi kuwa mama yake kabisa. Hii ni kwasababu, hawana utambulisho kwa Yesu, japo wanatumia jina lake(Luka 7:22&23).
Ifahamike kuwa, mtu ambaye hajamwamini Yesu,pengine ni mpagani kabisa, akiombewa, pepo hutii amri ya mwombaji na kuondoka, lakini kwa kuwa anayeombewa hajaamini, yule pepo huweza kurudi na kufanya makao tena ndani yake. Ni sawa na mpiganaji vitani anaevamia, na kupamabana na kuondoka bila kuacha walinzi. Adui, anakuwa na uwezo wa kurudi tena na kujimilikisha na hata akaweka ulinzi wake ulio imara zaidi kuliko ule wa awali (Mathayo 12:44&45).
Ndugu mpendwa, naimani unaendelea kubarikiwa kwa mafundisho yetu. Huu ndiyo utakuwa mwisho wa mada yetu. Usikose mada zijazo. Mungu akubariki.
UBATIZO NI NINI?

I. Ubatizo ni nini?
Ni ishara ya nje inayoonyesha kuwa mtu ameacha njia zake za zamani na ameanza kumfuata Yesu Kristo.
-Ni ishara ya kufa kuzikwa na kufufuka na Kristo.
Warumi 6:4
Wakolosai 2:12
-Ni ishara ya kufa kuzikwa na kufufuka na Kristo.
Warumi 6:4
Wakolosai 2:12
Maana ya neno “BATIZA”. Neno batiza limetokana na neno la Kiyunani,”BAPTIDZO” lenye maana zamisha au zika kabisa. Hivyo neno batiza maana yake ni zamisha, au zika kabisa.
II. Nani abatizwe?
A. Ni yule aliyeokoka
Matendo 2:38; 8:37; Marko 16:16; Mathayo 28:19
B. Ni mtu mzima
Mathayo 3:13
Matendo 8:36
A. Ni yule aliyeokoka
Matendo 2:38; 8:37; Marko 16:16; Mathayo 28:19
B. Ni mtu mzima
Mathayo 3:13
Matendo 8:36
III. Tubatizwe ubatizo gani?
Ubatizo wa maji mengi.
Mathayo 3:16
Matendo 8:38
Yohana 3:23
Ubatizo wa maji mengi.
Mathayo 3:16
Matendo 8:38
Yohana 3:23
IV. Tubatizweje?
A. Kwa kuzamishwa kwenye maji tele.
Matendo 8:38
Marko 1:10
Yohana 3:23
B. Kuingia majini wawili-Mbatizaji na mbatizwaji.
Matendo 8:38
A. Kwa kuzamishwa kwenye maji tele.
Matendo 8:38
Marko 1:10
Yohana 3:23
B. Kuingia majini wawili-Mbatizaji na mbatizwaji.
Matendo 8:38
V. Je kama kabla ya kuokoka nilishabatizwa, nikiokoka nibatizwe tena?
Kumbuka Ubatizo wa kweli alioagiza Yesu ni mmoja tu wa maji mengi, tena kwa mtu aliyeokoka na awe mtu mzima kama tulivyoona hapo juu. Hivyo hata kama umeambiwa ulibatizwa huko nyuma, ni lazima baada ya kuokoka ubatizwe sasa ubatizo halali Kibiblia maana ule wa mwanzo ulikuwa batili.
Matendo 19:1-7
Matendo 19:1-7
VI. Kwa nini tubatizwe?
A. Ni agizo kutoka kwa Yesu mwenyewe.
Mathayo 28:19
B. Ili kutimiza haki yote.
Mathayo 3:15
C. Ili kuzika mwili wa kale uliokufa.
Warumi 6:4
Wakolosai 2:12
D. Ili kuutangazi ulimwengu kuwa tumeacha mambo ya kale na tumeanza kumfuata Yesu.
A. Ni agizo kutoka kwa Yesu mwenyewe.
Mathayo 28:19
B. Ili kutimiza haki yote.
Mathayo 3:15
C. Ili kuzika mwili wa kale uliokufa.
Warumi 6:4
Wakolosai 2:12
D. Ili kuutangazi ulimwengu kuwa tumeacha mambo ya kale na tumeanza kumfuata Yesu.
2 Wakorintho 5:17
VII. Tubatizwe kwa Jina la nani?
Kwa Jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu
Mathayo 28:19
Kwa Jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu
Mathayo 28:19
VIII. Hitaji la ubatizo.
Maji tele, Mbatizaji na Mbatizwaji.
Yohana 3:23; Mdo 8:38-39; Marko 1:10
IX. Yesu anataka tubatizwe ubatizo aliobatizwa yeye.
- Marko 10:38,39
Maji tele, Mbatizaji na Mbatizwaji.
Yohana 3:23; Mdo 8:38-39; Marko 1:10
IX. Yesu anataka tubatizwe ubatizo aliobatizwa yeye.
- Marko 10:38,39
Tukitaka tuwe marafiki waYesu ni lazima tushike amri zake zote (maagizo yake yote) Yohana 14:14,15
-Raha ya wokovu ni pale tunapotenda yote aliyoagiza Yesu.
-Raha ya wokovu ni pale tunapotenda yote aliyoagiza Yesu.
Ubatizo unaeleza kitambulisho cha waumini kwa kifo cha Kristo, kuzikwa, na kufufuka kwake.
Warumi 6:3-4 inasema, "Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Krisot alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima." Hatua ya kuzamishwa katika maji inadhihirisha kufa na kuzikwa pamoja na Kristo. Hatua ya kutoka nje ya maji yaashiria picha ya ufufuo wa Kristo.
Katika 1 Petro 3:21, Petro alifundisha wazi kwamba ubatizo haukuwa tendo la sherehe ya utakaso wa kimwili, bali ni ahadi kwa dhamiri njema mbele ya Mungu. Ubatizo ni ishara ya kile tayari kimetokea katika moyo na maisha ya mtu ambaye amemwamini Kristo kama mwokozi (Warumi 6:3-5, Wagalatia 3:27, Wakolosai 2:12). Ubatizo ni hatua muhimu ya utii ambayo kila Mkristo anatakiwa kuchukua.
Shalom,
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Thursday, March 23, 2017
UNAWAFAHAMU MALAIKA WAKUU SABA WA MUNGU "ARCHANGELS OF GOD? (SEHEMU YA PILI)

MALAIKA MKUU JEGUDIEL "YEHUDIEL"
Neno la Kiebrania, mjumbe (messenger) katika Agano la Kale ni Malaika na linatafsiriwa kama Malaika (angel) katika Biblia za Kingereza. Neno linatumika katika kuonyesha wajumbe wa Kiroho waliotumiwa na Mungu. (Mwanzo 32:1-2) na pia lilitumika kwa wajumbe wanadamu waliotumwa na Yakobo (Mwanzo 32:3).
YEHUDIEL:
Kwa Kiebrania יהודיאל au Yehudiel ikimaanisha au "Mungu wa Wayahudi" ni mmoja wa Malaika Saba Wakuu.
Kwa Kiebrania יהודיאל au Yehudiel ikimaanisha au "Mungu wa Wayahudi" ni mmoja wa Malaika Saba Wakuu.
Jina Jegudiel au Yehudiel ni muungano wa majina mawili ya "YEHUDI" na "EL".
YEHUDI:
Kwa Kiebrania neno Yehudi ndani ya Biblia inamaanisha "Kutoka katika Kabila la Yuda na au "Wayahudi". Kwa wingi ni Yehudim (plural of יהודי, Yehudi).
Kwa Kiebrania neno Yehudi ndani ya Biblia inamaanisha "Kutoka katika Kabila la Yuda na au "Wayahudi". Kwa wingi ni Yehudim (plural of יהודי, Yehudi).
EL:
Mungu kwa Kiebrania ni EL. Neno EL linamaana ya "MAMLAKA" au "NGUVU" kwa Kiingereza Omnipotent, mighty, strength or power.
http://www.hebrew4christians.com/Names_of_G-d/El/el.html
Mungu kwa Kiebrania ni EL. Neno EL linamaana ya "MAMLAKA" au "NGUVU" kwa Kiingereza Omnipotent, mighty, strength or power.
http://www.hebrew4christians.com/Names_of_G-d/El/el.html
Mfano:
1. El Echad inamaana ya Mungu mmoja, Malaki 2:10.
2. El Hanneeman ina maana ya "MUNGU MWAMINIFU" Soma Torati 7:9.
3. El Emet ina maana ya Mungu ni Kweli, soma Zaburi 31:5
1. El Echad inamaana ya Mungu mmoja, Malaki 2:10.
2. El Hanneeman ina maana ya "MUNGU MWAMINIFU" Soma Torati 7:9.
3. El Emet ina maana ya Mungu ni Kweli, soma Zaburi 31:5
Sasa umeona katika kila jina la Malaika Wakuu kuna sehemu ya Jina la Mungu la "EL".
Ngoja nikukumbushe. Yehudi"EL", Gabri"EL", Micha"EL", Yuri”EL” n.k. Kuna sababu kubwa sana ya Mungu kuweka sehemu ya jina lake kwa kila hawa Malaika Wakuu. LAKINI HUONI sehemu ya jina lake kwa LUSIFA. Hili somo la Lusifa ni lingine na nitalifundisha.
Yehudiel inamaana ya Mungu wa Wayahudi au kwa Kiingereza ni God of the Jews.
Elah Yisrael, Mungu wa Waisrael, soma (Ezra 5:1)
Elah Yerushelem, Mungu wa Jerusalem (Ezra 7:19)
Elah Yerushelem, Mungu wa Jerusalem (Ezra 7:19)
Vivyo hivyo, Mungu alimtenga na au muumba Malaika Yehudiel kuwa Malaika atakae ilinda Taifa la Israel.
Kama mawakili wa Mungu walitumwa duniani kutoka mbinguni, kuchukua au kuleta maamuzi ya Mungu, juu ya wanadamu katika kutimiza adhabu ya Mungu kwa wanadamu, na katika kuwafundisha wanadamu (Kutoka 12:23; Zaburi 104:4; 2 Samuel 24:16; 2 Falme 19:35; 1 Nyakati 21:16; Matendo 12:23; Ebrania 11:28; 1 Kor. 10:10).
Ukiangalia matatizo kati ya Israel na Mataifa yanao izunguka, utagundua kuwa, hata itokee nini, hayo mataifa ya Kiarabu kamwe hayata weza ipiga Israel. Hebu jiulize, nchi hizi za Jordan, Syria, Lebanon, Misri, Ukanda wa Gaza na Golan Heights. Sababu ni hii, Mungu aliumba Maialka hususan kwa kuilinda Israel.
Tafsiri nyingine ya Malaika Wakuu saba ni kuwa wao ni Roho Saba za Mungu zinazosimama mbele za Mungu, na zilizotajwa katika kitabu cha Ufunuo 1:4; 3:1; 4:5; 5:6;
Malaika Wakuu Saba wanasemekana ni walinzi wa mataifa na nchi, na wanahusika, na masuala, na matukio yanayozizunguka, ikiwa ni pamoja na siasa, masuala ya kijeshi, na biashara, na uchumi. (Yoshua 5:13-15).
Vyeo mbalimbali vya Jeshi la Mbinguni
Malaika wana vyeo, uwezo na nguvu zinazotofautiana katika utendaji wa kazi mbalimbali. (Zekiel 1:7-11; Daniel 10:13; 12:1; 1Thesalonike 4:16; Yuda 1:9; Efeso 1:22; Kolosai 1:16).
MALAIKA WATUMISHI WATUMIKAO
"Malaika, angels" au malakhim, yaani, "malaika wa kawaida "plain" angels"(angeloi, wingi wa angelos, i.e. mjumbe (messenger) au wakili wa balozi, ubalozi (envoy), ni daraja la chini sana la malaika, na ndilo linalofahamika sana kwa watu wengi. Wanahusiana sana na mambo ya viumbe hai. Katika aina hii ya malaika, wapo wa namna nyingi tofauti tofauti, wakiwa na kazi mbali mbali. Hutumwa kama wajumbe kwa wanadamu. Malaika hawa ni wa karibu sana kwa ulimwengu wa vitu na wanadamu. Wana peleka maombi kwa Mungu na Majibu ya Mungu na ujumbe mwingine toka kwa Mungu kwa wanadamu. Malaika wanao uwezo wa kuwakaribia malaika wengine wa ngazi yoyote ile na kwa wakati wotote ule. Ni wanaojishughulisha sana na jamii kuwasaidia wale wanaoomba msaada katika mazingira magumu ya kimwili; mfano, katika ajali, vizuizi au vikwazo vya kutoka mahali kwenda mahali pengine (gerezani).
Usikose SEHEMU YA TATU itakayo zungumzia MALAIKA MKUU GABRIEL na kazi zake.
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Wednesday, March 22, 2017
The Lebanese and Syrian Muslim refugees converting to Christianity 'to find safety'
Ibrahim Ali remembers his first church service well. The smell of the candles, the cheap plywood pews, and the hymn singing that sounded so foreign to him at the time.
The 57-year-old Muslim Syrian never imagined that when he fled to neighbouring Lebanon to seek refuge from the war that he would end up converting to Christianity.
But Mr Ali is not alone. Hundreds of Muslim refugees living in Lebanon have been baptised in the past year alone.
Tuesday, March 21, 2017
Eleven Hindu families in remote village accept Christ—then denied access to local water by other villagers
“For the last three or four days I have been calling our Elijah Challenge Pastor Junul Putry to get the latest field reports, but he was out of range. Today I spoke to him and received the following report.
Junul Purty is one of our dedicated pastors, and he works in the very difficult, hardened region where Australian missionary Dr. Graham Staines and his two young sons were martyred in 1999.
This month he went to a remote Hindu village in a jungle area where he preached the gospel and ministered to the sick. Wonderfully, eleven families from a tribe called “HO” accepted the Christ. After a few days the other villagers started persecuting our new believers, not allowing them to withdraw water from the village well or a nearby stream. So our new believers are now suffering because of this. They must walk 3 kilometers to get water, and it is very difficult on them.
Imam of Mosque in Africa and Followers Risk All to Accept Jesus as Lord
(Ghana)—Members of a ministry based in Ghana are fighting more than poverty, illiteracy and illness. A spiritual battle against discouragement rose to a new level when evangelistic success brought threats of persecution.
“It has been tough and discouraging these days, but we are still dependent on Him,” the director of the ministry said.
Along with health, water, education and micro-enterprise development programs, the ministry has been showing “The Jesus Film” in villages, and not without opposition. The organization complements the screenings and other evangelistic efforts with broadcasts from its radio station. It reaches 2 million listeners with a wide range of community service programming, such as agricultural advice, besides its Christian programming.
Imam Stood Up from Washing Table Before Burial and Witnessing Jesus
Munaf Ali (name is not real), 45 years old, was an Imam of a Mosque as well as a scholar and preacher of Islam in a Middle East Kingdom.
One day Pastor Paul and the gospel team of Bibles for Mideast (http://bibles4mideast.com) met Munaf and had a discussion about Jesus Christ and the Bible. He denied the divinity of Jesus Christ and the credibility of the Bible.
Pastor gave him a sample gospel but he refused to receive. And also he cursed Pastor and his team.
At the same night a mob of fanatics under Munaf came to attack the gospel team shouting with “Allahu Akbar”. But the gospel team moved their shelter by God’s guidance and escaped from there before the attackers arrived.
After few days, one Friday afternoon, Munaf was going back home after the Juma Namaz. On the way he felt giddiness, became unconscious and falling on the ground. He knew he was dying. At that time, he saw demons coming to him to take his soul. Munaf said to them, “get lost, you cursed demons of Allah. You have no right to take my soul”.
An Egyptian Islamic Imam Professor Rejects Islam And Says Jesus Is Lord
The Story of M A Gabriel and his Indian connection
The former professor of Islamic history at Al-Azhar University, Cairo, Egypt
Disillusioned at Al-Azhar
Fifteen years ago I was the imam of a mosque in the city of Giza, Egypt, which is where the famous Egyptian pyramids are located. (Imam of a mosque is a position similar to pastor of a Christian church.) I preached the message of the week on Fridays from 12 to 1 in the afternoon, as well as performed other duties.
One Friday the topic of my message was jihad. I told the two hundred fifty people seated on the ground before me: Jihad in Islam is defending the Islamic nation and Islam against the attacks of the enemies. Islam is a religion of peace and only will fight against one who fights it. These infidels, heathens, perverts, Christians and Allah’s grievers, the Jews, out of envy of peaceful Islam and its prophet—they spread the myth that Islam is promulgated by the sword and violence. These infidels, the accusers of Islam, do not acknowledge Allah’s words. At this point I quoted from the Quran: And do not kill anyone whose killing Allah has forbidden, except for a just cause. —Surah 17:33, The Noble Quran When I spoke these words, I was just freshly graduated from Al-Azhar University in Cairo, Egypt —the oldest and most prestigious Islamic university in the world. It serves as the spiritual authority for Islam worldwide. I was teaching at the university, and I was an imam on the weekend at this mosque.
I preached my sermon on jihad that day according to the philosophy of the Egyptian government. Al-Azhar University focused us on the politically correct Islam and purposely overlooked areas of teaching that conflicted with the authority of Egypt . I was preaching what they taught me, but inside I was confused about the truth of Islam. But if I wanted to keep my job and my status at Al-Azhar, I needed to keep my thoughts to myself. After all, I knew what happened to people who differed from Al-Azhar’s agenda. They would be fired and would not be accepted to teach at any other university in the nation.
Subscribe to:
Comments (Atom)
TRENDING NOW
-
Baba umenipa funguo muhimu katika Mathayo 16:19 za kufunga na kufungua. Ninatumia funguo hizo kufunga na kufungua, kuvunja na kubamiza kil...
-
Kuna watu wanapitia mateso mengi sana, wengine wamefungwa katika vifungo bila wao kujijuwa basi chukua muongozo huu utakusaidia au itasaid...
-
Adui anakuja kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari kupambana na maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mun...
-
Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu. Twazidi pia kukushukuru kwa ajili ...
